PreGE2025 Ado Shaibu: CCM inashinda kwa mbeleko ya dola! Atoa msimamo wa ACT Wazalendo kushiriki Uchaguzi Oktoba 2025

PreGE2025 Ado Shaibu: CCM inashinda kwa mbeleko ya dola! Atoa msimamo wa ACT Wazalendo kushiriki Uchaguzi Oktoba 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo Ado Shaibu amesema CCM inashinda kwa mbeleko ya dola, akitoa msimamo wa ACT Wazalendo kuhusu Uchaguzi


Kuhusu G-55 na Wabunge 19

"Tutawapokea, umezungumza kuhusu Kundi la G-55, mtu yeyote anayetaka kujiunga na ACT Wazalendo kwa nia ya Kugombea, kwa nia ya kuleta mabadiliko tutampokea hatutasita hata mara moja. Uteuzi utafanywa na vikao vyenye dhamana kwa mujibu wa Katiba, kwahiyo tunawakaribisha sana milango iko wazi"

"Habari ya Wabunge 19, yoyote yule anayetaka kujiunga na Chama hiki tutampokea na hatutasita hata kidogo na ukiona mwanasiasa anasita kumpokea mwanachama mtazame, we pokea mwanacha akishaingia ndani ya Chama ataendeshwa kwa mujibu wa Katiba na taratibu za Chama"

Kuhusu Reforms na Uchaguzi

"Tunashiriki katika Uchaguzi huu ili kwenda kulinda dhamani ya KURA, tumejiridhisha uamuzi wa ACT Wazalendo kususia Uchaguzi huu utafurahiwa Chama cha Mapinduzi hatutaki kutoa nafasi hiyo kwa CCM na sababu ya tatu tumesema CCM imeshindwa kuendesha nchi, ni wakati muafaka ikae pembeni tutaishinda!"

"Uzoefu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019, Uchaguzi Mkuu 2020 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 umedhihirisha kwamba CCM hakiingii madarakani kwasababu ya kupata baraka za Wananchi kupitia mchakato wa Kura, ukweli ambao umejidhihirisha bayana CCM inaingia madarakani kwa msaada wa dola"

"Sasa kama CCM inatumia dola kubaki madarakani, sisi tumesema tunashiriki Uchaguzi huu kwenda kupigania thamani ya Kura, tunakwenda kupambana! Na tumewaambia CCM wakae wajue Uchaguzi huu hautaenda kuwa wa kawaida, tutajibu mapigo ya CCM itakavyokuja, tumejiandaa, tumejipanga tunakwenda kukikabili Chama cha Mapinduzi"

"Kupitia oparesheni yetu ya Linda Demokrasia tunakwenda kuwahamasisha Watanzania wasimame imara wapambane na CCM mpaka Haki yao ipatikane"

"Tumekusudia kujenga vuguvugu kubwa la umma la kuwaleta pamoja wadau wote wa Demkrasia pamoja na Wananchi kwa ujumla wao kupambana dhidi ya CCM, nawaambia CCM haijawahi kuwa tested [kujaribiwa] vya kutosha, wametibia 2019 na 2020 tume-react vipi?, 2024 mwitikio wetu ni upi? ACT Wazalendo tunasema hii ngoma haitoenda kuwa kama tulivyozoea inaenda kuwa Nginja nginja"

Fomu Urais, Ubunge muda waongezwa

''Kamati ya Uongozi Taifa ya ACT kwenye kikao chake cha April 15, 2025 ilitoa maelekezo kwa Ofisi ya Katibu Mkuu kuongeza muda wa Wanachama kuchukua na kurejesha fomu za kugombea nafasi za Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Urais wa Zanzibar, Ubunge, Ubunge wa Viti Maalum, Uwakilishi, Uwakilishi wa Viti Maalum, Udiwani na Udiwani wa Viti Maalum ili kutoa fursa ya kutosha kwa wanachama kugombea, ninayo furaha kuwajulisha Wanachzma wa ACT Wazalendo na Wananachi kwa ujumla kuwa muda wa kuchukua fomu za kugombea nafasi za Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Urais wa Zanzibar, Ubunge, Ubunge wa Viti Maalum, Uwakilishi, Uwakilishi wa Viti Maalum, Udiwani na Udiwani wa Viti Maalum umeongezwa''

''Katika utekelezaji wa agizo la kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Feb 23, 2025, Ofisi ya Katibu Mkuu ilitoa maelekezo ya kuruhusu wanachama kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali, licha ya maelekezo hayo kutolewa kabla ya tamko rasmi la Chama cha ACT Wazalendo kushiriki kwenye Uchaguzi Mkuu 2025, Wanachama wetu wengi wamejitokeza kugombea nafasi mbalimbali''

''Mathalani, kwa nafasi za Ubunge, jumla ya Wanachama 317 wamechukua fomu hadi sasa, kwa nafasi ya uwakilishi, jumla ya Wanachama 106 wamejitokeza kuchukua fomu, tunapenda kuchukua fursa hii kuwapongeza Wanachama wetu waliojitokeza kuchukua fomu, kuchukua kwao fomu kabla ya Chama kutangaza ushiriki kwenye uchaguzi ni ishara ya wazi ya utayari wao katika mapambano ya kulinda na kutetea thamani ya kura''
 
ACT ni kama wale jamaa wa stand wanaita wasafiri na kusema twende ,dereva washa chombo tuondoke halafu wao wanashuka wanaenda kwingine hawasafiri!!, ACT baada ya novemba tusisikie milio kuwa mmehujumiwa hatutawaelewa
 
Si walishatoa, sasa mkakati upi tena? Generali Ulimwengu amesema, CCM wangepata shida sana kama vyama vyote vingekataa kutia sahihi, na hiyo ni nafasi vyama vya siasa vimeshindwa kuiona na kuitumia
 
ACT wazalendo tatizo lao ni double standard, wanataka hawataki wanataka kushiriki uchaguzi mkuu ila hawana uhakika wa kushinda. Wanataka kuingia kwenye uchaguzi wakabahatishe ushindi. Hawa walitakiwa waungane na no reforms, no election ya CHADEMA iliyo chini ya Lissu. Hiyo linda demokrasia yao haina impact wala ccm haiiogopi
 
Siasa za ACT wazalendo zinaathiriwa na upande wa zanzibar. Wana ushirika na ccm kule zanzibar na hawawezi kuishinda ccm kamwe labda waachiwe wabunge na madiwani wachache ili tu ushirika wao uendelee. ACT wazalendo ni dhaifu, ipo ipo tu kukamalisha inkama ya vyama vya siasa nchini, si chama makini cha kukiamini wacha tu ccm iendelee kutawala kwa abrakadabra zake na itafika muda wake wa life span kijifie chenyewe zije zama zingine za siasa nchini
 
Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo Ado Shaibu amesema CCM inashinda kwa mbeleko ya dola, akitoa msimamo wa ACT Wazalendo kuhusu Uchaguzi


Kuhusu G-55 na Wabunge 19

"Tutawapokea, umezungumza kuhusu Kundi la G-55, mtu yeyote anayetaka kujiunga na ACT Wazalendo kwa nia ya Kugombea, kwa nia ya kuleta mabadiliko tutampokea hatutasita hata mara moja. Uteuzi utafanywa na vikao vyenye dhamana kwa mujibu wa Katiba, kwahiyo tunawakaribisha sana milango iko wazi"

"Habari ya Wabunge 19, yoyote yule anayetaka kujiunga na Chama hiki tutampokea na hatutasita hata kidogo na ukiona mwanasiasa anasita kumpokea mwanachama mtazame, we pokea mwanacha akishaingia ndani ya Chama ataendeshwa kwa mujibu wa Katiba na taratibu za Chama"

Mbona mnashiriki uchaguzi

Ova
 
Unaweza kwenda kushiriki uchaguzi ambao unajua kabisa sio huru na haki, Unasimama kabisa unasema mshindani wako anashinda kwa hila na bado unashiriki huo uchaguzi.

Thamani ya kura inatoka wapi wakati CCM wanashinda kwa nguvu ya dola?

Nafikiri ACT wanataka kushiriki uchaguzi ili kuhalalisha ujinga wa CCM tu hakuna lolote la maana hapo.

Thamani ya kura inakuwepo kama Ile mianya yote inayoweza kuifanya thamani ya kura isiwepo inazibwa.
 
Hawaleweki wanataka nn hawa
Kabisa mkuu, Wanaenda kwenye uchaguzi alafu bado wanakiri mapungufu!

Ni mda waendelee kujipanga na uchaguzi hakuna sababu ya kuanza kutoa kasoro zilizopo ili hali zinajulikana.

Kukubali tu wamekubaliana na kila kitu so wajiandae na uchaguzi
 
Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo Ado Shaibu amesema CCM inashinda kwa mbeleko ya dola, akitoa msimamo wa ACT Wazalendo kuhusu Uchaguzi


Kuhusu G-55 na Wabunge 19

"Tutawapokea, umezungumza kuhusu Kundi la G-55, mtu yeyote anayetaka kujiunga na ACT Wazalendo kwa nia ya Kugombea, kwa nia ya kuleta mabadiliko tutampokea hatutasita hata mara moja. Uteuzi utafanywa na vikao vyenye dhamana kwa mujibu wa Katiba, kwahiyo tunawakaribisha sana milango iko wazi"

"Habari ya Wabunge 19, yoyote yule anayetaka kujiunga na Chama hiki tutampokea na hatutasita hata kidogo na ukiona mwanasiasa anasita kumpokea mwanachama mtazame, we pokea mwanacha akishaingia ndani ya Chama ataendeshwa kwa mujibu wa Katiba na taratibu za Chama"

Kuhusu Reforms na Uchaguzi

"Tunashiriki katika Uchaguzi huu ili kwenda kulinda dhamani ya KURA, tumejiridhisha uamuzi wa ACT Wazalendo kususia Uchaguzi huu utafurahiwa Chama cha Mapinduzi hatutaki kutoa nafasi hiyo kwa CCM na sababu ya tatu tumesema CCM imeshindwa kuendesha nchi, ni wakati muafaka ikae pembeni tutaishinda!"

"Uzoefu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019, Uchaguzi Mkuu 2020 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 umedhihirisha kwamba CCM hakiingii madarakani kwasababu ya kupata baraka za Wananchi kupitia mchakato wa Kura, ukweli ambao umejidhihirisha bayana CCM inaingia madarakani kwa msaada wa dola"

"Sasa kama CCM inatumia dola kubaki madarakani, sisi tumesema tunashiriki Uchaguzi huu kwenda kupigania thamani ya Kura, tunakwenda kupambana! Na tumewaambia CCM wakae wajue Uchaguzi huu hautaenda kuwa wa kawaida, tutajibu mapigo ya CCM itakavyokuja, tumejiandaa, tumejipanga tunakwenda kukikabili Chama cha Mapinduzi"

"Kupitia oparesheni yetu ya Linda Demokrasia tunakwenda kuwahamasisha Watanzania wasimame imara wapambane na CCM mpaka Haki yao ipatikane"

"Tumekusudia kujenga vuguvugu kubwa la umma la kuwaleta pamoja wadau wote wa Demkrasia pamoja na Wananchi kwa ujumla wao kupambana dhidi ya CCM, nawaambia CCM haijawahi kuwa tested [kujaribiwa] vya kutosha, wametibia 2019 na 2020 tume-react vipi?, 2024 mwitikio wetu ni upi? ACT Wazalendo tunasema hii ngoma haitoenda kuwa kama tulivyozoea inaenda kuwa Nginja nginja"

Fomu Urais, Ubunge muda waongezwa

''Kamati ya Uongozi Taifa ya ACT kwenye kikao chake cha April 15, 2025 ilitoa maelekezo kwa Ofisi ya Katibu Mkuu kuongeza muda wa Wanachama kuchukua na kurejesha fomu za kugombea nafasi za Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Urais wa Zanzibar, Ubunge, Ubunge wa Viti Maalum, Uwakilishi, Uwakilishi wa Viti Maalum, Udiwani na Udiwani wa Viti Maalum ili kutoa fursa ya kutosha kwa wanachama kugombea, ninayo furaha kuwajulisha Wanachzma wa ACT Wazalendo na Wananachi kwa ujumla kuwa muda wa kuchukua fomu za kugombea nafasi za Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Urais wa Zanzibar, Ubunge, Ubunge wa Viti Maalum, Uwakilishi, Uwakilishi wa Viti Maalum, Udiwani na Udiwani wa Viti Maalum umeongezwa''

''Katika utekelezaji wa agizo la kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Feb 23, 2025, Ofisi ya Katibu Mkuu ilitoa maelekezo ya kuruhusu wanachama kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali, licha ya maelekezo hayo kutolewa kabla ya tamko rasmi la Chama cha ACT Wazalendo kushiriki kwenye Uchaguzi Mkuu 2025, Wanachama wetu wengi wamejitokeza kugombea nafasi mbalimbali''

''Mathalani, kwa nafasi za Ubunge, jumla ya Wanachama 317 wamechukua fomu hadi sasa, kwa nafasi ya uwakilishi, jumla ya Wanachama 106 wamejitokeza kuchukua fomu, tunapenda kuchukua fursa hii kuwapongeza Wanachama wetu waliojitokeza kuchukua fomu, kuchukua kwao fomu kabla ya Chama kutangaza ushiriki kwenye uchaguzi ni ishara ya wazi ya utayari wao katika mapambano ya kulinda na kutetea thamani ya kura''

Kwa hoja hizi, sheria ya uchaguzi ikiruhusu vyama kuungana ndiyo itakuwa mwarobaini wa kuindoa CCM, lakini kwa chama kimoja kimoja ni kazi sana!
 
Unaweza kwenda kushiriki uchaguzi ambao unajua kabisa sio huru na haki, Unasimama kabisa unasema mshindani wako anashinda kwa hila na bado unashiriki huo uchaguzi.

Thamani ya kura inatoka wapi wakati CCM wanashinda kwa nguvu ya dola?

Nafikiri ACT wanataka kushiriki uchaguzi ili kuhalalisha ujinga wa CCM tu hakuna lolote la maana hapo.

Thamani ya kura inakuwepo kama Ile mianya yote inayoweza kuifanya thamani ya kura isiwepo inazibwa.

Mara ngapi CHADEMA wameshiriki chaguzi hizo hizo?
 
ACT ni wajinga wajinga tu ambao hata hawajui wanataka nini kwenye siasa za nchi hii. Eti Kuna cheo pale cha kiongozi mstaafu wa chama ambaye naye ni mwamuzi wa Kila kinachoendelea kwenye chama. Yaani ACT ni ujinga mtupu.
 
Back
Top Bottom