"A man should provide for his wife. PERIOD"

"A man should provide for his wife. PERIOD"


...mimi maswali yangu manne iwapo mwanaume anastahiki ku 'provide for his wife'

1. kwa kiwango gani?...kwa kila kitu? au kwa yaliyo makuu i.e Nyumba, Chakula, Mavazi, na Matibabu.
2. kwa muda gani? mume akiwa mzima au ugonjwa, mume akiwa kijana au mzee
3. mwanamke abakie (full-time) mama wa nyumbani? ...kwakuwa pesa yake haihitajiki, ruksa alee watoto tu?
4. kipato chake (mke) kitafsiriwe vipi?

...nachelea tafsiri ya maamuzi haya 'compared' na mila, desturi na tamaduni za makabila/utaifa.
Kwetu 'Mwambao' yanawezekana sana haya. Mke anashinda ndani kulea watoto, kujifukiza udi nk...
'Unyamwezini' mume na mke wote wanapiga matuta!...Sijui kule kwa 'Wakurya' kukoje...!


Mbu unaweza kuombwa hela ya kodi ya nyumba au ada ya watoto wakati unaumwa umelazwa hospital, na pengine umekuwa mlemvu kabisa huwezi kufanya kazi tena kisa eti wewe lazima uprovide
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Hahaaaaaaaaa lini utaacha vichekesho huwezi amini nshatengeneza mtu anafanana na wewe sijui uko ivo au nimekosea.


Mkuu unaweza badili hili jina lako?

Kila nikiwaza Katelero narekebisha Jiografia ya suruali yangu. Niombi tu......
 
Mbu unaweza kuombwa hela ya kodi ya nyumba au ada ya watoto wakati unaumwa umelazwa hospital, na pengine umekuwa mlemvu kabisa huwezi kufanya kazi tena kisa eti wewe lazima uprovide

...umeona ee? badala ya kumfariji mgonjwa kwa ibada na maombi, unamkuta Mke kawa mkali eti anataka kujua msimamo wa maisha yake na watoto! No wonder misiba ya kisasa ni full kugombea mirathi!


Kasignecha kamenistua....... kwanini ulimdanganya mwenzio?

Inauma sana aisee

...waonyesha ulishakula mahari ya watu wewe,...ha ha ha!


Hawa dawa yao tuwaanzishie Thread!
.................Mchungaji kwani sie wagonjwa hadi utupe dawa? Mie niko fit sijui Mbu pengine yu aumwa!!

...mtamaliza madawa, mbu hana tiba.
 
Umesema kweli shost saa ingine nasi tunachangia sana kwa hawa wababa kuwa hivi. Ninavyoamini mie huwa kuna mwanzo wa kila kitu...na inawezekana kabisa wakati wa mwanzo baba alikuwa anaprovide tena na vya ziada! Lakini baadhi yetu hufikia kuona kuwa ....nimemweka kiganjani.. tunabweteka miguu juu, hata kama unazo ukiambiwa mama chumvi imekwisha unajibu ..subiri baba enyu akirudi...huku unavaa kandambili zako mbio saluni!!

Kisha tena haya umeletewa, hata shukrani, neno aksante na sauti ya puani hakuna, ndio kwaaanza unamwangalia mume anaingia na kifurushi chake mpaka anakuletea hapo ulipokaa.na bado hunyooshi mkono ukapokea, unamnyooshea kidevu aweke juu ya meza. kisha wasubiriiii mpaka unagutuka ah nlisahau kumbe kuna kifurushi..haya tena ushakifungua umeona kilichomo hukukipenda waanza kitolea kasoro, ..oh ungeleta rangi ya samawati, kama ni dhahabu basi we unaropoka bora ungenunua kwa Kasmani ili mradi huonyeshi shukrani!..... wadhani kesho bwana atarudia kuleta?! Inaanza zawadi na mwisho matumizi .

Jamani dia.....kwa ukweli wa moyo wangu sidhani kama kuna mwanamke wa namna hiyo. Hapana pls........haiwezekani. Yaani sipati picha hali ikifikia hivyo nyumba inakuwaje? Yaani hata kumpokea mume alicholeta inakuwa ngumu? Siamini. Najua kuna tofauti kwenye maisha lakini wanandoa hawapaswi kuishi kwa kisirani kuanzia asubuhi mpaka jioni mpaka siku zinazofuata. Hapana.........kuna kitu hakiko sawa mahali.
 
Jamani dia.....kwa ukweli wa moyo wangu sidhani kama kuna mwanamke wa namna hiyo. Hapana pls........haiwezekani. Yaani sipati picha hali ikifikia hivyo nyumba inakuwaje? Yaani hata kumpokea mume alicholeta inakuwa ngumu? Siamini. Najua kuna tofauti kwenye maisha lakini wanandoa hawapaswi kuishi kwa kisirani kuanzia asubuhi mpaka jioni mpaka siku zinazofuata. Hapana.........kuna kitu hakiko sawa mahali.

Kbd......tembea uyaone mwanakwetu....haya mie nimeyajuaje? we acha tu kuna kina kaka mpaka unawaonea huruma.
 
Hahaaaaaaaaa lini utaacha vichekesho huwezi amini nshatengeneza mtu anafanana na wewe sijui uko ivo au nimekosea.

Nina aibu sana! Kwa kuwa niko nyuma ya PC naweza hata kukutokea....ukionana na mimi domo zege!
 
Hapa nimegundua Kila mtu ana njia tofauti kuendesha familia yake ukikosea tu ukabeba za Chauro umekwisha utashangaa kuniona nadunda wewe ushaunguza kibanda chako.


Mbu unaweza kuombwa hela ya kodi ya nyumba au ada ya watoto wakati unaumwa umelazwa hospital, na pengine umekuwa mlemvu kabisa huwezi kufanya kazi tena kisa eti wewe lazima uprovide
 
.........Hahahahah Babu ah haya bana mie Mtiifu sibishani na Babu!.

................Mchungaji kwani sie wagonjwa hadi utupe dawa? Mie niko fit sijui Mbu pengine yu aumwa!!

Tutakutana kama kamati kutengeneza thread!

A wife should provide for her Husband! Mumesoma muswada wa sheria za ndoa wa Kenya? Kwa wale ambao hamjauona ...inapendekezwa kama baba hana kazi basi anaweza tumia mshahara wa mkewe kutafutia mkopo.

Nanukuu (Kenya's Marriage Bill )

The Marriage Bill privileges heterosexual marriage as the ideal union that receives recognition and privileges within the law. For instance, Part IV, Matrimonial Rights, Liabilities and Status, notes,
Either spouse is presumed to have authority to pledge the other spouse's credit, or to borrow money in his or her name, or to use any of his or her money which is in his or her possession or under his or her control, or to convert his or her movable property into money, and use it, so far as that credit or money is required or used for the purchase of necessaries for himself or herself and any children of the marriage, and so far as is reasonable having regard to the other spouse's means and way of life.

 
Jamani dia.....kwa ukweli wa moyo wangu sidhani kama kuna mwanamke wa namna hiyo. Hapana pls........haiwezekani. Yaani sipati picha hali ikifikia hivyo nyumba inakuwaje? Yaani hata kumpokea mume alicholeta inakuwa ngumu? Siamini. Najua kuna tofauti kwenye maisha lakini wanandoa hawapaswi kuishi kwa kisirani kuanzia asubuhi mpaka jioni mpaka siku zinazofuata. Hapana.........kuna kitu hakiko sawa mahali.

Hahhhhhh???...

wapo, tena wengi sana!....kisirani tuuuuu,...yaani hasharifiki wala nini...
....yeye ni kukosoa mwanzo mwisho!
 
Mbu unaweza kuombwa hela ya kodi ya nyumba au ada ya watoto wakati unaumwa umelazwa hospital, na pengine umekuwa mlemvu kabisa huwezi kufanya kazi tena kisa eti wewe lazima uprovide


My dia Kate.....sidhani kama hayo ndo tunayoyazungumzia hapa. Huo sio ubinadamu kabisa na sidhani kama hiyo ndio mada inayojadiliwa.
 
Mkuu majibu ya maswali yako kwa sisi ambao tunatanguliza imani zetu kwanza ni haya:



...mimi maswali yangu manne iwapo mwanaume anastahiki ku 'provide for his wife'

1. kwa kiwango gani?...kwa kila kitu? au kwa yaliyo makuu i.e Nyumba, Chakula, Mavazi, na Matibabu.
Kwanza kabisa Mwanamme anawajibika kutoa mahari kumpa mwanamke wakati akioa ilhali mwanamke yeye hatoi mahari bali ndiye anayepatiwa mahari tena anayotaka yeye.

Pili, Mwanamme amelazimishwa kutoa mahitaji kwa mkewe kwa kila kitu, kuanzia Nyumba, Chakula, Mavazi, Matibabu, mapambo na kila ambalo linahitajika kwa mke wake.
Pia ni wajibu wa mume kuwaelimisha watoto, kuwatibu wenye kumtegemea na kuwatunza.


2. kwa muda gani? mume akiwa mzima au ugonjwa, mume akiwa kijana au mzee
Kwa muda wote wa maisha yake, ila ni pale tu mume atakapokuwa hana uwezo wa kutoa mahitaji ya mume na familia yake.


3. mwanamke abakie (full-time) mama wa nyumbani? ...kwakuwa pesa yake haihitajiki, ruksa alee watoto tu?
Hapa nasema hivi, si lazima mwanamke hawe mama wa nyumbani haya ni makubaliano ya mume na mke, kama watakubaliana kuwa mke akae nyumbani na alee watoto ni sawa, na wakikubaliana mke na mume wote watoke na kutafuta riziki ni juu yao.


4. kipato chake (mke) kitafsiriwe vipi?
Kipato cha mwanamke ni chake, na kila mali atakayo chuma itakuwa ni yake anaweza kuweka akiba, wala hatolazimika kutoa senti moja katika mali. Ni pale tu atakapoamua kufanya ihsani, na yeye mwenyewe kuona kuwa maisha ni magumu na msaada wake unaitajika, ila si lazima.... Na hata uko kupika, kufua, kufagia na kazi zote za ndani si lazima kuzifanya. Hizo zote ni kazi za Mume.

Kama mwanamke ataamua kuzifanya basi ihesabike kama anafanya ihsani tu na si kumshushia makofi na mateke pale atakapokuwa hakufanya moja ya kazi za nyumbani. Ila atakapozifanya basi ni kheri kwake na kunaongeza mapenzi ndani ya nyumba, kwani maisha ni kusaidiana.
 
Hapa nimegundua Kila mtu ana njia tofauti kuendesha familia yake ukikosea tu ukabeba za Chauro umekwisha utashangaa kuniona nadunda wewe ushaunguza kibanda chako.

Umemaliza kila kitu Chauro,...kuingiza u JF kwenye nyumba inaweza ku cost nyumba ya mtu. By the time anarudi JF kuulizia kulikoni, anakuta Mbu kesharuka...! Muhimu ni vile mtu awezavyo kuhimili kasi ya mabadiliko ndani ya nyumba yake.

...kila nyumba ina viwango na vigezo vyake vya kuzingatia.
 

Hahhhhhh???...

wapo, tena wengi sana!....kisirani tuuuuu,...yaani hasharifiki wala nini...

jfa1942l.jpg
....yeye ni kukosoa mwanzo mwisho!


Mbu pls jamani.........hii sio kawaida. Kama ni kweli basi hiyo ndoa haikutakiwa kuwepo toka siku ya kwanza. Mi nilidhani ndoa msingi wake ni mapenzi na hayo mengine ni ziada tu. Sasa tukianza kunyima raha na kisirani 24/7 hapo hatutafika. Utakuta hizi ndio zile za ahadi na maahadi kibao mwisho siku lazima igeuke. Mi naamini kama kuna mapenzi ya dhati lazima kuelewana kutakuwepo baada ya malumbano maana kuna mapenzi ya dhati yanayowaunganisha nyie wawili. Na ukimpenda mtu ni lazima utachukuliana naye tu........asikwambie mtu.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mkuu majibu ya maswali yako kwa sisi ambao tunatanguliza imani zetu kwanza ni haya:

Kwanza kabisa Mwanamme anawajibika kutoa mahari kumpa mwanamke wakati akioa ilhali mwanamke yeye hatoi mahari bali ndiye anayepatiwa mahari tena anayotaka yeye.

Pili, Mwanamme amelazimishwa kutoa mahitaji kwa mkewe kwa kila kitu, kuanzia Nyumba, Chakula, Mavazi, Matibabu, mapambo na kila ambalo linahitajika kwa mke wake.
Pia ni wajibu wa mume kuwaelimisha watoto, kuwatibu wenye kumtegemea na kuwatunza.


Kwa muda wote wa maisha yake, ila ni pale tu mume atakapokuwa hana uwezo wa kutoa mahitaji ya mume na familia yake.


Hapa nasema hivi, si lazima mwanamke hawe mama wa nyumbani haya ni makubaliano ya mume na mke, kama watakubaliana kuwa mke akae nyumbani na alee watoto ni sawa, na wakikubaliana mke na mume wote watoke na kutafuta riziki ni juu yao.


Kipato cha mwanamke ni chake, na kila mali atakayo chuma itakuwa ni yake anaweza kuweka akiba, wala hatolazimika kutoa senti moja katika mali. Ni pale tu atakapoamua kufanya ihsani, na yeye mwenyewe kuona kuwa maisha ni magumu na msaada wake unaitajika, ila si lazima.... Na hata uko kupika, kufua, kufagia na kazi zote za ndani si lazima kuzifanya. Hizo zote ni kazi za Mume.

Kama mwanamke ataamua kuzifanya basi ihesabike kama anafanya ihsani tu na si kumshushia makofi na mateke pale atakapokuwa hakufanya moja ya kazi za nyumbani. Ila atakapozifanya basi ni kheri kwake na kunaongeza mapenzi ndani ya nyumba, kwani maisha ni kusaidiana.

...aaahhh, kaka. Nakushukuru kwa kunikumbusha haya. Najua tafsiri hii inatokana msimamo wa Imani gani.
Tatizo linakuja je? kwenye maisha ya leo na mfumuko wa gharama za maisha hayo yote yanawezekana?

Chukulia Income ya Baba mwenye nyumba haizidi Tshs 125,000/= kwa mwezi kima cha chini (hapa Unguja)
 
....mnnnnnnnnnn?! taratibu kaka, wengine tupo lunch time tunakula bana.

tulia bwana! Kila siku wanawake wanaomba haki sawa! Sasa hapo hapo wanataka tuwape vitu. Sasa kazi yao ni nini hasa?
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
<br><br><font size="3">tulia bwana! Kila siku wanawake wanaomba haki sawa! Sasa hapo hapo wanataka tuwape vitu. Sasa kazi yao ni nini hasa?</font><br>

Chapakazi, naona kama unaandika kwa hasira!
Tunaomba utujengee hoja hapa tufafanulie ili nasi tufaidi!! Kuna hazina ya elimu hapa kwenye post yako lakini umeifunga sana mpendwa hebu funguka..................
 
Mkuu majibu ya maswali yako kwa sisi ambao tunatanguliza imani zetu kwanza ni haya:

Kwanza kabisa Mwanamme anawajibika kutoa mahari kumpa mwanamke wakati akioa ilhali mwanamke yeye hatoi mahari bali ndiye anayepatiwa mahari tena anayotaka yeye.

Pili, Mwanamme amelazimishwa kutoa mahitaji kwa mkewe kwa kila kitu, kuanzia Nyumba, Chakula, Mavazi, Matibabu, mapambo na kila ambalo linahitajika kwa mke wake.
Pia ni wajibu wa mume kuwaelimisha watoto, kuwatibu wenye kumtegemea na kuwatunza.


Kwa muda wote wa maisha yake, ila ni pale tu mume atakapokuwa hana uwezo wa kutoa mahitaji ya mume na familia yake.
Hapa nasema hivi, si lazima mwanamke hawe mama wa nyumbani haya ni makubaliano ya mume na mke, kama watakubaliana kuwa mke akae nyumbani na alee watoto ni sawa, na wakikubaliana mke na mume wote watoke na kutafuta riziki ni juu yao.
Kipato cha mwanamke ni chake, na kila mali atakayo chuma itakuwa ni yake anaweza kuweka akiba, wala hatolazimika kutoa senti moja katika mali. Ni pale tu atakapoamua kufanya ihsani, na yeye mwenyewe kuona kuwa maisha ni magumu na msaada wake unaitajika, ila si lazima.... Na hata uko kupika, kufua, kufagia na kazi zote za ndani si lazima kuzifanya. Hizo zote ni kazi za Mume.

Kama mwanamke ataamua kuzifanya basi ihesabike kama anafanya ihsani tu na si kumshushia makofi na mateke pale atakapokuwa hakufanya moja ya kazi za nyumbani. Ila atakapozifanya basi ni kheri kwake na kunaongeza mapenzi ndani ya nyumba, kwani maisha ni kusaidiana.

Kwanza karibu sana Kaka X-Paste......
Nashukuru sana umetuwekea na upande mwingine wa mtazamo ili utusaidia kuelewa vizuri hii mada....mtazamo ambao nafikiri ni muhimu sana kwa maisha ya kila mtu, kuangalia mila na desturi zake. Hapa sina mengi ila ningependa kuuliza swali moja tu.......
1. Mwanaume anayefuata/takiwa kufuata mtazamo huu ambaye HAYATIMIZI haya kama inavyotakiwa, either kwa kuwa mambo ya kiuchumi hayajakaa sawa, jamii hii inayofuata mtazamo huu inamchukuliaje?;
2. Yule je anayeDHARAU haya kwa KUSUDI kabisa naye anachukuliwaje?
 
Back
Top Bottom