666-NYAYO ZA KUZIMU--21-
"kwanini usiweze??...ushaanza!!"
kwa ukali kidogo mama Halima alitamka,
"sawa mama nitajitahidi kadri ya uwezo wangu"
Julina alimtia moyo,waliendelea na safari yao ya kuelekea majumbani taratibu huku wakiwa washaachwa nyuma na wenzao,stori ndogo ndogo zilitawala maongezi yao hasa juu ya tendo lile la uchomaji moto wa nyumba zakina Madhifa kitu walichoonekana kupinga kupinga kabisa japokua walikua hawana uwezo wa kuongea mbele ya umati wa wanakijiji,wangeonekana wasaliti.taratibu walitembea bila hofu walishasahau
kidogo mambo ya vifo kutokana na kupumbazwa na vijistori vidogo vidogo vya hapa na pale,ila ghafla Julina alisimama kisha akasema..
"mama Halima,nina hofu"
"nini tena Julina mwanangu? Mwanao si yupo kwa mzee Patili.."
alisema mama Halima huku akirudi nyuma kumfuata,
"sio juu ya mtoto wangu Mama,ni juu ya mume wangu Kitanzi!...ni muda sasa hajarudi,sijui nae atakua ashanyongwa??"
"mh-mh,usiseme hivyo bwana kwanza embu twende nyumbani ukapumzike mana tokea usiku ulipojifungua upo kwenye heka heka tu hata mtoto wako atakua anakuhitaji mno kwa sasa,tafadhali twende!"
kidiplomasia mama Halima alipooza jambo lililotaka kuzuka,alimshika mkono Julina na kumvuta waende.
Nyuma ya mama Halima na Julina alionekana mtu anakuja kwa kasi! Pande la mtu,pande la mbaba! Mweusi tii kwa rangi na kichwani alikua hana nywele kabisa,yani upara!!
Mikono yake miwili mikubwa iliyoshiba ilikua imeshikilia kamba nyekundu,macho yake makubwa mekundu yalisadifu hamu kubwa iliyo moyoni mwake,masikio yake yalizoea makelele ya kuomba msamaha ya watu mbalimbali na hata pia mikono yake ilizoea kunyofoa roho za watu,alikua ni mnyongaji!!!
Ghafla mama Halima alihisi kitu akageuka nyuma haraka,hakuona kitu!! Wasiwasi ulimteka moyo,akamwambia Julina
"nahisi kuna kitu!"
huku akigeuka geuka nyuma,
"nini tena hiko??"
Julina mama uoga haraka aliuliza,
"bado sijafahamu! Ila tuongeze mwendo Julina,twende!!"
haraka mbio zikaanza,maumivu bado yalikua na Julina kwani si muda mrefu toka atoke kujifungua lakini uoga wake ulimsaidia mno kumkimbiza,tayari moyo wake ulishawasha jenereta,ulikua mbio mno kuliko hata wa yule aliehisi kitu,yani mama Halima!! Joto lilipanda mwilini mwake,kajasho kauoga kalimteremka! Mungu wangu nisaidie!! Alijiambia moyoni.
Baada ya muda kidogo waliwafikia wenzao wakaungana nao,walishusha pumzi ndefu ya kutoamini kama wamefanikiwa huku mioyo yao ikianza kutulia taratibu,walijuta kwanini walibaki.
Lile jitu lilitokomea,halikuonekana tena,halikujulikana lilielekea wapi!! Lilichokipanga hakikufanikiwa,wakina
mama Halima waliponea chupuchupu watiwe kitanzini kama isingelikua hisia zao zilizowastua,hivyo nani anafuata?? Hiko kilikua ni kitendawili.
Upande wa pili wa shilingi nyumbani kwa mzee Patili maongezi madogo madogo yalichukua nafasi,fahamu
zilishamrudia mama Kadogo japokua majeraha bado mwilini yalimsumbua na pia vilevile kichwa kilikua kinamuuma,dawa alizopewa na yule mzee sio siri zilimsaidia vilevile mzee Otongo.
Maongezi yao yaliokua yanaendelea yalishindwa kufikia hitimisho kwani kila walipojadili kuhusu vilivyotokea huko nyuma bado hawakupata jibu kwamba vimeishia wapi,ni ngumu kuamini kama lile jeshi limewaacha tu
vilevile,walipata kidogo mashaka,walikua hawafahamu ya kuwa kuna mauaji yanaendelea kijijini,walikua hawajui kabisa juu ya hilo,walikua hawafahamu ya kwamba sasa jeshi la 666 limekuja kivingine!!
Muda ulianza kuruhusu jua lizame,taratibu giza likaanza kuingia,wanakijiji kutokea kwenye mazishi walianza
kuitia miguu yao ndani ya kijiji,mila zao na desturi haziruhusu kulaza maiti,hivyo mtu akifariki mapema tu anazikwa akapumzike kwa amani,kila mwanakijiji alielekea kwenye nyumba yake,tito aliekua yatima yeye alichukuliwa na mama Kurwa,mmama mmoja muongeaji sana mwembamba ambaye ni jirani yao,mama
Halima na Julina moja kwa moja walielekea kwenye nyumba ya mzee Patili,kumpasha habari na kumchukua mtoto waliemuacha hapo kwa muda.Habari zile ziliwashtua sana! Mauaji ya watu wawili ndani ya kijiji kwa kunyongwa kilionekana kuamsha hisia ya kwamba ujio wa jeshi la 666 umewadia!
Mama Kadogo na mzee Otongo pia walihisi vivyo hivyo!
Upande wa pili mzee patili na wakina mama Kadogo walijisikia vibaya juu ya taarifa ya kuchomwa kwa nyumba za wakina baba Madhifa na walijiona wakosefu mbele zao.
Ngo! Ngo! Ngo! Hodi iliita,mzee patili aliinuka na kwenda kufungua,alikua ni Khadhifa! Alikuja kumuita mzee patili akawasaidie kwani baba yao yupo kwenye hali mbaya!! Mzee Patili alishangazwa na zile habari na hasa alishangazwa zaidi baada ya kuambiwa hicho kitu kilijiri baada ya kuleta mwili wa mama yao waliokuta umenyongwa maeneo ya kisimani,haraka mzee Patili alichukua madawa fulani kisha mbio zikaanza kuelekea eneo la tukio!
Kutokana na kaumbali kalichopo walichelewa,walipokaribia walisikia sauti ya kilio waliyoitambua ni ya Madhifa! Hofu zikajazwa mioyoni mwao! Nini tena hiki jamani?? Walijiuliza huku wakiongeza kasi!!
USIKOSE SEHEMU 22 IJAYO!