666-nyayo za kuzimü

666-nyayo za kuzimü

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,051
Reaction score
34,788
666-NYAYO ZA KUZIMU..

SEHEMU YA 1

387955_520867291275780_80757636_n.jpg



Upepo ulivuma mno,miti na majani ilionekana kuinama kutokana na kushndwa kupambana na pepo ile kali,giza lilikua kali sana kwa kuwa mwezi ulikua umefunikwa gubigubi na wingu zito jeusi lisiloonyesha hata

kama mvua itanyesha.utulivu wa hali ya juu ulitawala,hakuna kilichosikika zaidi ya milio ya kiuoga ya mbwa na vijidudu vidogo vidogo vya usiku,kila kibatari kilic
howashwa ilhali na moto ilizimika kutokana na kutokua

stahimilivu na hali iliyokuwepo,hakukuwa na mtu yeyote alieonekana yu nje akifanya jambo lolote,na ni kutokana na hali ya ajabu ya ghafla iliyotawala katika lile eneo.Kwa mbaali angani ilionekana nyota ndogo

ikichomoza,ghafla sauti ya kuamuru ilisikika kutoka kwenye kijumba cha msonge ikisema..

"sukuma,jitahidi Vero sukuma!...enhee..tena...tena!!..ewaaah!...umepata mtoto wa kiume Vero!"
sauti ya mama Marinda mkunga wa jadi Maarufu kijijini iliskika..iliyoambatana na tendo na kumsaidia bibie

Veronica kupata mtoto wake wa kwanza kabisa,upepo ulitulia ghafla,hali iliyomfanya Mama Utopi kupumzika na zoezi la kukikinga kibatari kisizimwe na upepo ili shughuli ile ya Ukunga iliyokua inafanyika ipate kuisha

salmini,alikiweka kile kibatari chini na kusogea karibu zaidi ili apate kumshuhudia mtoto aliyeingzwa

ulimwenguni..

"mbona hata halii?"

akauliza mama Utopi kwa shauku kubwa ya kufahamu,
"mie mwenyewe sijui,kwani miaka yangu yote ishirini ya ukunga sijawah kukutana na hili jambo la mtoto kutolia ingali anaonyesha yu mzima kwa kuchezesha mikono na miguu yake.....
Na isitoshe...ni wa baridi mno! Zaidi hata ya maji ya asubuhi ya mtoni!"

alisema kwa msisitizo mama Marinda huku akimtolea macho mama Utopi aliesimama,Vero hakuchangia chochote kwani hakuwah kukumbana na lile swala kokote pale,hivyo aliishia kuwatazama mama Utopi na

Mama marinda wakiwa wanajibizana.Mama marinda aliemshkilia mtoto alianza kuingiwa na hofu,alimtazama yule mtoto kwa macho yakinifu hakupata jibu,alionekana ni mtulivu mno,hakuonyesha dalili ya kucheka wala

kulia,Mama Marinda akaanza kuhisi mapigo yake ya moyo yanaenda mbio,jasho lililojaa uoga taratiibu lilishuka...
* * * * * *
USIKOSE SEHEMU YA PILI!
 
"666-NYAYO ZA KUZIMU" SEHEMU YA PILI

Mama Marinda alianza kuhisi mapigo ya moyo yanaenda mbio kuliko kawaida,mikono yake iliyomshka mtoto ilianza kutetemeka,alitoa macho kwa mshangao na ghafla aliropoka..

"mama Utopi embu mchukue huyu mtoto,haraka!!"
naye mama Utopi bila kujivunga aliinama na kumtwaa mtoto akiwa na kiulizo kichwani..
"kwani vipi jamani?"
aliuliza Vero baada ya kuiona ile hali linayoendelea pale,
Mama Marinda alikua kimya akionekana kubanwa na mawazo hali iliyompa nafasi mama Utopi kunena..
"mwanao ni wa tofauti Vero?"
"kivipi?"
"kwanza halii,pili ni wa baridi mno!"
"mmmh...haitokua ni kwasababu ya hali ya hewa?"
"sidhani,mana hata hali yenyewe imebadilika tu baada ya wewe kusikia uchungu,na sasa hivi umeshajifungua huoni kama hali imetulia?"
alisema Mama Utopi huku akimtazama Vero alieonekana anafikiria jambo kutokana na kauli aliyoambiwa,aliona Vero anapata shida kuongea na ni kutokana na kutoka kujifungua na hali ilikua inaonyesha dhahiri ya kwamba kachoka,hakutaka muongelesha tena na alimsihi apumzike kwa muda,mama Utopi alimtazama vizuri mtoto aliyembeba huku mikono yake ikistahimili baridi lililoonekana kuanza kumzidia,allivua khanga yake na kubakia na gauni tu lililochoka la rangi nyekundu lenye maua maua kisha ile khanga akamfunikia tena mtoto ili kujikinga na mikono yake vilevile na kumkinga mtoto na hali ya hewa.Mama Utopi,mmama mwembamba mwenye uweupe wa mbali na kichwani akiwa kasuka vibutu vibutu vilivyoonekana kufumuka fumuka alimgeuzia shingo mama Marinda,alimuona bado butwaa ya mawazo imemshika...na yupo tu pale kifikra,alimstua..
"we mama Marinda!"
"Abee!..."
kwa kukurupuka aliitika,
"vipi wewe?"
"mmmh...embu njoo nje tuongee kidogo"
alijibu Mama Marinda huku akitoka nje ya ile nyumba ya msonge akifuatiwa na Mama Utopi baada ya kumkabidh Vero mwanae,
walisogea kidogo mbali na ile nyumba hali iliyoashiria ya kwamba maongezi yao ni ya siri.
Mama Marinda aliangalia kushoto na kulia kama kuna mtu,akatengenezea khanga yake rangi ya kijani na manjano yenye nyota nyekundu,akakuna kichwa chake kilicho na mvi zilizotosha kujionyesha kisha kwa msisitizo akasema..
"hivi unayakumbuka maneno ya yule mganga?"...
* * * * *

USIKOSE SEHEMU YA TATU..
 
"666-NYAYO ZA KUZIMU" SEHEMU YA 3

"unayakumbuka maneno ya mganga?"
"maneno yapi tena?"
"si yale ya kizazi cha nyoka...
Hukumbuki?"
alizidi kusisitiza mama Marinda,
"aahaaa!..nishakumbuka,enhe?"
"sasa wewe huoni kama inahusiana na haya?"
"yapi?"
"nawe!..he! Si haya ya huyu mtoto!...
Hukumbuki mganga alituambia kwamba,kwanza siku akizaliwa hali ya hewa itabadilika na kua ya kutisha naa....."
"ndioo!..pia nakumbuka alituambia kwamba nyota ndogo itachomoza!"
(haraka wakanyanyua nyuso zao na kutazama angani)
"haa!...si unaiona!"
kwa tahamaki alisema mama Marinda huku akinyooshea kidole nyota ile,
"ndio mama Marinda,naiona!"
alijibu kwa mshangao mama Utopi,
"sasa tunafanyaje?"
sura yenye wasi wasi ya mama Marinda ilitamka,
"mmh...mi nadhani hapa si pa kukaa tena,mana yule mtoto ni hatari sana!...si unakumbuka alituambia kwamba akifungua macho yake wote wasio na imani thabiti juu yake watapata majanga..!!"
"ndio!...tuondoke haraka iwezekanavyo tumuache atajijua yeye na mumewe!!"
aling'aka mama Marinda,walishikana mikono na kuanza kukimbia haraka wakipita katikati ya msitu mzito ilipo njia nyembamba ya kuelekea kwao,milio ya mbwa na wadudu ilizidi kuwatisha na kuwafanya waangalie nyuma kila mara kwa hofu,mama Marinda alianza kuchoka kukimbia,uzee na mwili wake ulikua ni kikwazo tosha kwake kuendelea na safari,ilibidi wapumzike kidogo.....wakusanye nguvu kisha wamalizie safari yao iliyobakia kidogo kuikamilisha,walilaumu nafsi zao kwa tamaa ya pesa ya mzee Ndolanga mume wa Vero iliyowafanya waingie kwenye matatizo yote hayo,kwani kama wangelijua wasingejisumbua na kujihusisha na ile shughuli,katikati ya mapumziko yao mafupi walisikia sauti na vishindo vya watu vinakuja,haraka walijificha,punde si punde walishuhudia wazee watatu waliojifunika gubi gubi wanaotumia msaada wa fimbo kutembea,wakiwa wanajongea bila uoga huku wakionekana kufurahia jambo...
Ghafla wale wazee walisimama,mmoja wao akasema..
"nasikia harufu ya binadamu hapa.."
huku akipepesa pepesa macho yake mekundu,
mwingine akadakia..
"naisikia hata mimi pia!.."
macho ya wakina Mama Marinda yalitoka na mioyo ilipiga mbio mithili ya mkizi baharini,walishikana kwa uoga,waliwaona wale wazee wakiwa wanarudi kuelekea upande wao huku wakiwa wanatazama tazama wakitafuta kitu!
* * * *
"mama Marinda tukimbie!.."
alinong'oneza mama Utopi,
"mie siwezi tena,miguu inaniuma!"
"jitahidi jamani,huoni wanazidi kuja!..
Na wanasikia harufu yetu!!"
alizidi kusisitiza mama Utopi huku wakiwa bado wamejificha na wale wazee wapo hatua kumi tu toka walipo...
"tupige tu ukunga watu waje watusaidie"
"usiku wote mzito huu nani atajitoa nje ya nyumba yake?...
Twende mam
a Marinda...twendeee!!"
alimshka mkono na kuanza kukimbia,alikua mbele ya mwenzake na aliutumia mkono wa kushoto kumkokotea...
Wale wazee hawakuonekana wakikimbia,walisimama tuli huku macho yao yakiwa yanawatizama wakina mama Marinda wanaokimbia,hawakufika umbali mrefu,mkono wa mama Marinda ulimponyoka mama Utopi,kama gunia la ulezi alidondoka chini!!.
"mama Marinda...amka twendee!..amkaa!!...
"siwezi!...siwezi!!..miguu yangu imefungwa na majani mama Utopi!..siwezi kuitoa!!...
Mama Utopi nisaidieee navutwaa!"
mama Utopi alijitahidi kumpa mkono mama Marinda lakini hakufanikiwa,Mama Marinda alivutwa haraka kwa kasi ya ajabu,sauti yake ya kuomba msaada ilizidi kupotelea msituni,na mwishowe haikuskika kabisa.Mama Utopi hakua na cha kufanya,aligeuka na kuanza kukimbia kwa kasi zaidi....machozi yakimtoka na moyo ukidunda kwa nguvu kutokana na uoga na hofu nzito iliyomshika,aliona umbali wa kufika nyumbani umeongezeka,na kila akijitahidi kuongeza kasi ilikua kama ni kazi bure,mapafu yalimbana...na alihisi kama hapati pumzi,ilimbidi asimame kidogo apate kuhema,hakua na amani kabisa,alikua anatizama kila pande kuthibitisha usalama wake,machozi yalizidi kumtoka alipofikiria mwenzake aliekua nae muda si mrefu hayupo tena,ilikua ni kama mchezo wa kuigiza alipomshuhudia mwenzie akivutwa na majani na kupotelea kabisa,alitupia macho upande wa kulia,aliona mwanga wa taa umbali wa kama hatua ishirini na tano toka alipo,akili yake ilimuambia kwamba pale ni kwa mama kadogo,haraka bila kupoteza muda aliamza kukimbia akielekea upande huo.
Alifungua kwa pupa geti la makuti la ile nyumba,aliingia ndani na kuanza kupepesa pepesa macho aone wapi atapata msaada,ghafla alisikia sauti kali iliyompasua wake moyo..
"wow! Wow!..wow!"
alistuka mno kuona mbwa watatu wakimfuata,alianza kurudi nyuma kwa tahadhari huku akiwaangalia mbwa wanaomsogelea,kwa nguvu aliropoka kuomba msaada..
"mama Kadogoo!!..mama Kadogoo!"
sauti hiyo ilimstua mama Kadogo aliekua ndani amelala na mumewe,na zaidi aliogopeshwa na sauti kali za mbwa zilizofika vizuri masikioni mwake,alimuamsha haraka mumewe,ilikua kidogo kazi nzito kwani alikua ametekwa vilivyo na usingizh mzito,ila kwa bugudha za kutosha alizozifanya zilifanikisha kuondoa mang'amung'amu ya mumewe,
"nini mama Kadogo?"
"nimesikia sauti nje ya mwanamke inaniita..na huskii mbwa wanavyobweka kwa nguvu??"
aliuliza mama Kadogo,
bila kuchelewa baba Kadogo alichukua panga lake chini ya kitanda kisha akatoka nje kwa kasi,alipofika nje alishuhudia mbwa wake wakiwa wanamparua parua mmama ambaye alikua bado hajamfahamu ni nani,aliwaamrisha mbwa wake waache lile tendo na haraka walitii amri,alimsogelea yule mtu na kugundua ya kwamba ni mama Utopi,aliloa damu kutokana na majeraha makubwa aliyosabishiwa na wale wanyama,alikua anagugumia kwa maumivu na huku akitetemeka.

* * * * *
USIKOSE SEHEMU 4
 
666-NYAYO ZA KUZIMU-4-

"mama Marinda tukimbie!.."
alinong'oneza mama Utopi,
"mie siwezi tena,miguu inaniuma!"
"jitahidi jamani,huoni wanazidi kuja!..
Na wanasikia harufu yetu!!"

alizidi kusisitiza mama Utopi huku wakiwa bado wamejificha na wale wazee wapo hatua kumi tu toka walipo...

"tupige tu ukunga watu waje watusaidie"
"usiku wote mzito huu nani atajitoa nje ya nyumba yake?...
Twende mama Marinda...twendeee!!"

alimshka mkono na kuanza kukimbia,alikua mbele ya mwenzake na aliutumia mkono wa kushoto kumkokotea...

Wale wazee hawakuonekana wakikimbia,walisimama tuli huku macho yao yakiwa yanawatizama wakina mama Marinda wanaokimbia,hawakufika umbali mrefu,mkono wa mama Marinda ulimponyoka mama Utopi,kama gunia la ulezi alidondoka chini!!.
"mama Marinda...amka twendee!..amkaa!!...
"siwezi!...siwezi!!..miguu yangu imefungwa na majani mama Utopi!..siwezi kuitoa!!...
Mama Utopi nisaidieee navutwaa!"

mama Utopi alijitahidi kumpa mkono mama Marinda lakini hakufanikiwa,Mama Marinda alivutwa haraka kwa kasi ya ajabu,sauti yake ya kuomba msaada ilizidi kupotelea msituni,na mwishowe haikuskika kabisa.Mama Utopi hakua na cha kufanya,aligeuka

na kuanza kukimbia kwa kasi zaidi....machozi yakimtoka na moyo ukidunda kwa nguvu kutokana na uoga na hofu nzito iliyomshika,aliona umbali wa kufika nyumbani umeongezeka,na kila akijitahidi kuongeza kasi ilikua kama ni kazi bure,mapafu yalimbana...na alihisi kama hapati pumzi,ilimbidi asimame kidogo apate kuhema,hakua na amani kabisa,alikua anatizama kila

pande kuthibitisha usalama wake,machozi yalizidi kumtoka alipofikiria mwenzake aliekua nae muda si mrefu hayupo tena,ilikua ni kama mchezo wa kuigiza alipomshuhudia mwenzie akivutwa na majani na kupotelea kabisa,alitupia macho upande wa kulia,aliona mwanga wa taa umbali wa kama hatua ishirini na tano toka alipo,akili yake ilimuambia kwamba pale ni kwa mama kadogo,haraka bila kupoteza muda aliamza kukimbia akielekea upande huo.


Alifungua kwa pupa geti la makuti la ile nyumba,aliingia ndani na kuanza kupepesa pepesa macho aone wapi atapata msaada,ghafla alisikia sauti kali iliyompasua wake moyo..

"wow! Wow!..wow!"
alistuka mno kuona mbwa watatu wakimfuata,alianza kurudi nyuma kwa tahadhari huku akiwaangalia mbwa wanaomsogelea,kwa nguvu aliropoka kuomba msaada..
"mama Kadogoo!!..mama Kadogoo!"

sauti hiyo ilimstua mama Kadogo aliekua ndani amelala na mumewe,na zaidi aliogopeshwa na sauti kali za mbwa zilizofika vizuri masikioni mwake,alimuamsha haraka mumewe,ilikua kidogo kazi nzito kwani alikua ametekwa vilivyo na usingizh mzito,ila kwa bugudha za kutosha alizozifanya zilifanikisha kuondoa mang'amung'amu ya mumewe,

"nini mama Kadogo?"
"nimesikia sauti nje ya mwanamke inaniita..na huskii mbwa wanavyobweka kwa nguvu??"
aliuliza mama Kadogo,

bila kuchelewa baba Kadogo alichukua panga lake chini ya kitanda kisha akatoka nje kwa kasi,alipofika nje alishuhudia mbwa wake wakiwa wanamparua parua mmama ambaye alikua bado hajamfahamu ni nani,aliwaamrisha mbwa wake waache lile tendo na haraka walitii amri,alimsogelea yule mtu na kugundua ya kwamba ni mama Utopi,aliloa damu kutokana na majeraha makubwa aliyosabishiwa na wale wanyama,alikua anagugumia kwa maumivu na huku akitetemeka.

* * * * *

USIKOSE SEHEMU 5 INAYOFUATA.!
 
Nimetia hashuo la kusoma hii usiku hahahahaha leo ntaomba nisindikizwe kila pahala lol inatisha bhana

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
666-NYAYO ZA KUZIMU-4-

"mama Marinda tukimbie!.."
alinong'oneza mama Utopi,
"mie siwezi tena,miguu inaniuma!"
"jitahidi jamani,huoni wanazidi kuja!..
Na wanasikia harufu yetu!!"

alizidi kusisitiza mama Utopi huku wakiwa bado wamejificha na wale wazee wapo hatua kumi tu toka walipo...

"tupige tu ukunga watu waje watusaidie"
"usiku wote mzito huu nani atajitoa nje ya nyumba yake?...
Twende mama Marinda...twendeee!!"

alimshka mkono na kuanza kukimbia,alikua mbele ya mwenzake na aliutumia mkono wa kushoto kumkokotea...

Wale wazee hawakuonekana wakikimbia,walisimama tuli huku macho yao yakiwa yanawatizama wakina mama Marinda wanaokimbia,hawakufika umbali mrefu,mkono wa mama Marinda ulimponyoka mama Utopi,kama gunia la ulezi alidondoka chini!!.
"mama Marinda...amka twendee!..amkaa!!...
"siwezi!...siwezi!!..miguu yangu imefungwa na majani mama Utopi!..siwezi kuitoa!!...
Mama Utopi nisaidieee navutwaa!"

mama Utopi alijitahidi kumpa mkono mama Marinda lakini hakufanikiwa,Mama Marinda alivutwa haraka kwa kasi ya ajabu,sauti yake ya kuomba msaada ilizidi kupotelea msituni,na mwishowe haikuskika kabisa.Mama Utopi hakua na cha kufanya,aligeuka

na kuanza kukimbia kwa kasi zaidi....machozi yakimtoka na moyo ukidunda kwa nguvu kutokana na uoga na hofu nzito iliyomshika,aliona umbali wa kufika nyumbani umeongezeka,na kila akijitahidi kuongeza kasi ilikua kama ni kazi bure,mapafu yalimbana...na alihisi kama hapati pumzi,ilimbidi asimame kidogo apate kuhema,hakua na amani kabisa,alikua anatizama kila

pande kuthibitisha usalama wake,machozi yalizidi kumtoka alipofikiria mwenzake aliekua nae muda si mrefu hayupo tena,ilikua ni kama mchezo wa kuigiza alipomshuhudia mwenzie akivutwa na majani na kupotelea kabisa,alitupia macho upande wa kulia,aliona mwanga wa taa umbali wa kama hatua ishirini na tano toka alipo,akili yake ilimuambia kwamba pale ni kwa mama kadogo,haraka bila kupoteza muda aliamza kukimbia akielekea upande huo.


Alifungua kwa pupa geti la makuti la ile nyumba,aliingia ndani na kuanza kupepesa pepesa macho aone wapi atapata msaada,ghafla alisikia sauti kali iliyompasua wake moyo..

"wow! Wow!..wow!"
alistuka mno kuona mbwa watatu wakimfuata,alianza kurudi nyuma kwa tahadhari huku akiwaangalia mbwa wanaomsogelea,kwa nguvu aliropoka kuomba msaada..
"mama Kadogoo!!..mama Kadogoo!"

sauti hiyo ilimstua mama Kadogo aliekua ndani amelala na mumewe,na zaidi aliogopeshwa na sauti kali za mbwa zilizofika vizuri masikioni mwake,alimuamsha haraka mumewe,ilikua kidogo kazi nzito kwani alikua ametekwa vilivyo na usingizh mzito,ila kwa bugudha za kutosha alizozifanya zilifanikisha kuondoa mang'amung'amu ya mumewe,

"nini mama Kadogo?"
"nimesikia sauti nje ya mwanamke inaniita..na huskii mbwa wanavyobweka kwa nguvu??"
aliuliza mama Kadogo,

bila kuchelewa baba Kadogo alichukua panga lake chini ya kitanda kisha akatoka nje kwa kasi,alipofika nje alishuhudia mbwa wake wakiwa wanamparua parua mmama ambaye alikua bado hajamfahamu ni nani,aliwaamrisha mbwa wake waache lile tendo na haraka walitii amri,alimsogelea yule mtu na kugundua ya kwamba ni mama Utopi,aliloa damu kutokana na majeraha makubwa aliyosabishiwa na wale wanyama,alikua anagugumia kwa maumivu na huku akitetemeka.

* * * * *

USIKOSE SEHEMU 5 INAYOFUATA.!

Naomba niicopy then niipost kwenye account yangu ya fb
 
666-NYAYO ZA KUZIMU-4-

"mama Marinda tukimbie!.."
alinong'oneza mama Utopi,
"mie siwezi tena,miguu inaniuma!"
"jitahidi jamani,huoni wanazidi kuja!..
Na wanasikia harufu yetu!!"

alizidi kusisitiza mama Utopi huku wakiwa bado wamejificha na wale wazee wapo hatua kumi tu toka walipo...

"tupige tu ukunga watu waje watusaidie"
"usiku wote mzito huu nani atajitoa nje ya nyumba yake?...
Twende mama Marinda...twendeee!!"

alimshka mkono na kuanza kukimbia,alikua mbele ya mwenzake na aliutumia mkono wa kushoto kumkokotea...

Wale wazee hawakuonekana wakikimbia,walisimama tuli huku macho yao yakiwa yanawatizama wakina mama Marinda wanaokimbia,hawakufika umbali mrefu,mkono wa mama Marinda ulimponyoka mama Utopi,kama gunia la ulezi alidondoka chini!!.
"mama Marinda...amka twendee!..amkaa!!...
"siwezi!...siwezi!!..miguu yangu imefungwa na majani mama Utopi!..siwezi kuitoa!!...
Mama Utopi nisaidieee navutwaa!"

mama Utopi alijitahidi kumpa mkono mama Marinda lakini hakufanikiwa,Mama Marinda alivutwa haraka kwa kasi ya ajabu,sauti yake ya kuomba msaada ilizidi kupotelea msituni,na mwishowe haikuskika kabisa.Mama Utopi hakua na cha kufanya,aligeuka

na kuanza kukimbia kwa kasi zaidi....machozi yakimtoka na moyo ukidunda kwa nguvu kutokana na uoga na hofu nzito iliyomshika,aliona umbali wa kufika nyumbani umeongezeka,na kila akijitahidi kuongeza kasi ilikua kama ni kazi bure,mapafu yalimbana...na alihisi kama hapati pumzi,ilimbidi asimame kidogo apate kuhema,hakua na amani kabisa,alikua anatizama kila

pande kuthibitisha usalama wake,machozi yalizidi kumtoka alipofikiria mwenzake aliekua nae muda si mrefu hayupo tena,ilikua ni kama mchezo wa kuigiza alipomshuhudia mwenzie akivutwa na majani na kupotelea kabisa,alitupia macho upande wa kulia,aliona mwanga wa taa umbali wa kama hatua ishirini na tano toka alipo,akili yake ilimuambia kwamba pale ni kwa mama kadogo,haraka bila kupoteza muda aliamza kukimbia akielekea upande huo.


Alifungua kwa pupa geti la makuti la ile nyumba,aliingia ndani na kuanza kupepesa pepesa macho aone wapi atapata msaada,ghafla alisikia sauti kali iliyompasua wake moyo..

"wow! Wow!..wow!"
alistuka mno kuona mbwa watatu wakimfuata,alianza kurudi nyuma kwa tahadhari huku akiwaangalia mbwa wanaomsogelea,kwa nguvu aliropoka kuomba msaada..
"mama Kadogoo!!..mama Kadogoo!"

sauti hiyo ilimstua mama Kadogo aliekua ndani amelala na mumewe,na zaidi aliogopeshwa na sauti kali za mbwa zilizofika vizuri masikioni mwake,alimuamsha haraka mumewe,ilikua kidogo kazi nzito kwani alikua ametekwa vilivyo na usingizh mzito,ila kwa bugudha za kutosha alizozifanya zilifanikisha kuondoa mang'amung'amu ya mumewe,

"nini mama Kadogo?"
"nimesikia sauti nje ya mwanamke inaniita..na huskii mbwa wanavyobweka kwa nguvu??"
aliuliza mama Kadogo,

bila kuchelewa baba Kadogo alichukua panga lake chini ya kitanda kisha akatoka nje kwa kasi,alipofika nje alishuhudia mbwa wake wakiwa wanamparua parua mmama ambaye alikua bado hajamfahamu ni nani,aliwaamrisha mbwa wake waache lile tendo na haraka walitii amri,alimsogelea yule mtu na kugundua ya kwamba ni mama Utopi,aliloa damu kutokana na majeraha makubwa aliyosabishiwa na wale wanyama,alikua anagugumia kwa maumivu na huku akitetemeka.

* * * * *

USIKOSE SEHEMU 5 INAYOFUATA.!



Mzizimkavu tupe radha aiseee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom