666-NYAYO ZA KUZIMU-15-
Ilichukua kama dakika kumi yule mzee akiitizama na kuipekua ile miili huku wanakijiji wakiwa wamemzingira,aliinua macho yake na kutoa amri ya ile miili kuingizwa ndani,wale vijana wa baba Madhifa walitekeleza hilo jambo haraka,waliingiza ile miili ya
mzee Otongo na mama Kadogo ndani ya kale kajumba kadogo cha udongo cha yule mzee alieonekana kuheshimiwa na kusikilizwa na wanakijiji,bila ya kujivunga yule mzee nae aliingia ndani na kuwaacha nje wanakijiji waliokua na shauku kubwa ya kutaka jua kinachoendelea,baadhi yao walianza onekana wakijiondoa kwenye lile eneo taratibu na kwenda kuendelea na
shughuli zao zingine huku bado midomo yao ikiteta lile tukio lililoonekana kuchota hisia zao kwa kiasi kikubwa,wakati hayo yote yanachukua nafasi kuna baadhi ya wanakijiji walikua hawana habari kabisa kuhusu lile tukio!!...labda kutokana na kubanwa na
hali husika,umbali wa nyumba kumi na tano toka pale pa yule mzee kulikua na nyumba moja tulivu ya udongo iliyopakwa chokaa iliyofanya ionekane ni ya kipekee kidogo tofauti na nyumba zingine,madirisha yake makubwa yapitishayo hewa na sauti bado
hayakutosha kuwajuza watu walio ndani juu ya kinachoendelea kwa nje,nyuso zao zilijawa na tabasamu na huku wakionekana
kutowaza kabisa yanayojiri ulimwengu mwingine,
"enhe..sasa nimpe jina gani?"
lilikua swali alilouliza mdada mmoja aliemshika mtoto akijulikana kama Julina huku akitabasamu
"mmh mie mwenyewe sijui,we si ndo mama bwana! Mie kazi yangu ya ukunga nshaimaliza"
alijibu mama Halima,mmama mwenye rangi ya maji ya kunde,mkunga maarufu kijijini aliebakia baada ya kifo cha mama Ramla miaka miwili iliyopita,
"au tumsubirie baba yake?"
"utakavyoona wewe ni sahihi..."
"ujue nini mama,mimi ni kama mwanao,sina utofauti na mwanao Halima,sijui hata nikushukuru vipi kwa kweli,namsubiria tu mume wangu arudi ndipo tutakapojua cha kufanya"
"wala usihofu mwanangu,ujue hii kazi ya ukunga ni kama karama kwangu,si ajira!! Kwahiyo naifanya kwa ajili tu ya kuwasaidia
wanizungukao kwani baada ya mwanangu Halima kufariki,kila mtoto nizalishae ni kama mtoto wangu"
"pole sana mama,kifo cha Halima kiliniachia pia pengo kubwa,kama unavyojua,alikua ni rafiki yangu mkubwa! Yeye ndo kwa kiasi kikubwa alinishawishi niole na Kitanzi"
"tuachane na hayo mwanangu nisije nikatonesha donda lililoanza kupona,ila mumeo Kitanzi yupo wapi saa hizi?"
"mmmh...hata sifahamu kwa kweli,aliahidi kuwa atakuwepo hapa usiku wa jana,lakini mpaka saa hizi sijamtia kwenye zangu mboni"
nyuso zao zilificha matabasamu yalionawiri hapo kabla,mawazo yakaonekana kuwashika hatamu,Julina alianza kupata hofu,mama Halima akaligundua hilo..
"sikiliza mwanangu,ujue sisi binadamu tunapanga na mungu pia anapanga,hivyo huwezi jua,tuombe tu uzima!"
"mmh kweli mama.."
kidogo maongezi yaliingiliwa na kilio cha mtoto,mtoto alieonekana hana muda mrefu ulimwenguni,haraka Julina alitoa titi lake la kushoto na kumyamazisha nalo,uso wa Mama Halima ulionekana unaficha jambo,na hata macho yake yalikua yanasadifu ya kwamba ana kitu ndani ya mtima chamsumbua..
"mama vipi??..mbona hivyo tena!"
"mmh,kuna kitu kinanitatiza kusema kweli,jana usiku wakati tupo katija zile shughuli za kufungulishana nilisikia kelele!!"
"kelele??...si kelele zangu hizo ama?"
"hapana!...mara ya kwanza ilikua ni kelele ya kike,na mara ya pili ilikua ya kiume!!!"
"wee!..mie mbona sikuzisikia??"
"usingeweza kuzisikia,uchungu uliokua nao usingekuruhusu ufanye hilo.."
"mama una uhakika na hilo jambo??"
aliuliza Julina kwa umakini huku akimtikisatikisa mwanae kitaratibu,
"asilimia zote!...na ubaya ni kwamba kila ninapotulizana,zile sauti hunirudia masikioni!!!!!"
kwa msisitizo alinena Mama Halima huku akiyatoa macho,hofu ikaanza kumrudi Julina tena!!...huyo atakua sio mume wangu kweli?? Alijiuliza moyoni,kabla hajapata majibu,hodi ikaskika!
"ngo!-ngo!-ngo!"
"nani??"
aliuliza mama Halima,
"wageni!!"
sauti ilijibu toka nje,
"wakina nani?"
"wageni!!"
ilirudia tena!
Ilimbidi mama Halima ainuke na kwenda kuchungulia dirishani kabla ya kufungua,he!! Alishuhudi mabibi wawili wageni machoni wakiwa mlangoni!!..aligeuza shingo yake na kumtizama Julina kwa tahadhari,
"unawajua hawa watu?"
aliuliza,
"wakina nani?"
"njoo uwaone!"
alielekeza kwa sauti ya chini iliyokamatwa na kauoga,
Julina aliwatazama wale mabibi kupitia pale dirishani kisha akamjibu mama Halima kwa kunong'oneza,
"mmh mh,siwajui!!!"
* * * *
je hao watu ni wa kina nan? Wana uhusiano wowote na jeshi! Jeshi la 666?
Vipi kuhusu mume wa Julina,kitanzi?
Mzee Otongo na Mama Kadogo wanaendeleaje? Na lengo la kumuokoa mtoto litafanikiwa?
Jeshi la 666 lipo wapi?
USIKOSE SIMULIZI HII YA KUSISIMUA SEHEMU 16 IJAYOO.........