666-nyayo za kuzimü

666-nyayo za kuzimü

666-NYAYO ZA KUZIMU--24-

akasogea karibu huku akinyata aweze kumuona vizuri,mara lile jitu likagonga hodi kwa mtindo ule ule alioutumia kwa Mama Matata! Nini hiki? Alijiuliza mzee Patili,kutokana na uoga wa watu waliokuwepo mule ndani tendo la kufungua mlango lilichukua muda,mama Kadogo na mzee Otongo hawakuweza kufungua

kutokana na miili yao yenye majeraha na maumivu kutowaruhusu,mama Halima na Julina walio wazima walikua na hofu hivyo kufanya lile zoezi lichukue muda kutendeka,lakini lile jibaba lililokuwepo mlangoni lilihisi kitu,lilipepesa macho yake huku likinusanusa na kugundua jambo,lilisikia harufu ya binadamu hivyo likafahamu ya kuwa haliko peke yake pale nje,haraka lilitoweka! Mzee Patili alijitahidi kufikicha zake mboni

lakini hakuona kitu! Alishangazwa mno na lile jambo,haraka alikimbia mpaka mlango ulipo na kuanza kubisha hodi huku akitamka kwamba yeye ni mzee Patili! Maswali na hofu yalijazana vichwani mwa waliokua ndani,mara ya kwanza walipoisikia hodi iliambatana na sauti ya kike ila sasa hivi wanaisikia sauti ya kiume tena ni ya mzee Patili! Walisita kufungua.

Tendo la busara lililofanywa na mama Halima la kuchungulia dirishani ndilo lililowashawishi kumfungulia mzee Patili baada ya kugundua ndie,aliingia ndani na kuwaeleza yote aliyoyashuhudia tokea alipotoka mpaka alipomuona lile jitu mlangoni,walishtuka sana na vilevile walishukuru hawakuifungulia hodi ile kwani ingekua

ni hadithi nyingine sasa hivi,mzee Patili alizidi kulielezea lile aliloliona..
"yule mtu alikua ameshikilia kamba nyekundu! Na hasa zinafanana na zile zilizotumika kuwanyongea wakina baba Tito! Hicho kitu kilinishangaza sana!"
"mungu wangu! Jamani tuhame hiki kijiji tutakwisha!"
kiuoga alinena Julina akiwa anamnyonyesha mwanae,
mama Kadogo akasema,
"sidhani kama hilo ni suluhisho,kila tutakapoenda watatufata mpaka pale watakapohakikisha ya kwamba lengo lao limefanikiwa!"
kauli ile iliwashtua mama Halima na Julina waliokua hawajui kiendeleacho,haraka wote wakauliza
"lengo! Lengo gani hilo??"
mama Kadogo akazidi kunyumbua,

"haya mambo yote yajiriyo ndani ya kijiji chenu yalitokea vilevile kijijini kwetu Igesambo,watu wetu wengi wa karibu wameuwawa na wengine wamejiunga kwenye jeshi la 666 lililo na itikadi moja tu ya kuusambaza utawala wa Ibilisi wao alieingizwa duniani,ilibidi tukimbie kuokoa maisha yetu kwasababu hatukutaka abadani kuungana na mashetani wale,lakini kuonyesha ya kwamba mungu yu upande wetu,alizaliwa mwana mwingine! Mwana ambaye ndie tumaini letu na vilevile anaweza akawa kifo chetu!"

"nani huyo??"
Julina aliuliza kwa papara huku akimtizamatizama mwanae,
mama Kadogo akaendelea,
"huyo mtoto ndie hasa lengo la hawa watutafutao na watuuwao,namaanisha jeshi la 666 kwani ni hatari kwao na huyo mtoto ndie hasa yatubidi tumlinde kwa hali zote kwani ndie tumaini na mwanga wetu,tukimruhusu afe,tumeruhusu utawala wa kiza!"
mzee Otongo nae akadakia

"mtoto huyo ana alama kwenye paja lake la kushoto kwa chini,alama ya nyota!"
mama Halima na Julina walishtushwa na ile kauli! Kwani mtoto yule alikua na hiyo alama! Macho ya Julina yakatoka kwa uoga! Huku akitetemeka akasema
"haiwezekani!! Ah-ah! Haiwezekani jamani,haiwezekani!!! Mtoto wangu! Hapana!"
* * * *

Bado wanakijiji walikua wamekusanyana mbele ya nyumba ya mama Kurwa na baba Matata,hakuna hata mmoja alieonekana na dalili wala hamu ya kurudi kwenye viota vyao na kulala,hali ilikua tete mno mioyoni mwao! Mada kubwa iliyokua inaongelewa ni juu ya ule ujumbe uliokutwa kwenye lile joho alilovishwa mama Matata baada ya kunyongwa uliosomeka BADO KIDOGO!! Hawakuelewa ulikua unamaanisha nini? Kila mtu alisema yake juu ya hilo.

Kutokana na hofu kulowanisha nafsi zao waliamua kukaa pale pale mpaka usiku utakapokwisha na kuiona adhuhuri,hawakua na lingine la kufanya zaidi ya hilo waliloona ya kwamba ni salama kwa maisha yao.Baba Matata na mwanae walikuwepo sebuleni,huzuni iliwafanya wakose cha kusema na kuwa kimya,ilikua ni

ngumu bado kuamini ya kwamba mtu waliekua nae muda si mrefu ni marehemu sasa hivi! Baba matata aliona mzigo wa majukumu waongezeka,Matata mwenye miaka tisa bado alikua anahitaji malezi ya mama yake na ukizingatia yeye si mkaaji nyumbani,kichwa kilivuruga.

Ghafla upepo mkali ulipiga lile eneo!! Upepo usio wa kawaida kabisa!! Vibatari vilivyokua vinatoa mwanga vyote vilizima na kufanya giza totoro kushika hatamu!! Wakina mama walipiga makelele ya uoga na kila mtu hofu iliita ndani yake! Miili ilitetemeka kwa uoga,mioyo ilizizima kwa hofu!!

Mchakato wa kuwasha vibatari ulipofanikiwa watu wawili hawakuonekana!! Hawakujulikana walielekea wapi...hawakujulikana walibebwa na nani!! Mtoto mmoja wa mzee Rama na mmama mmoja wa makamo walishabebwa!!!
Mungu wangu! Sauti zao zilisikika zikiishilia kama ilivyokua kwa mama Matata!!
Matumbo yalichemka,jasho liliteremka!! Wengine walizirai kwa uoga,na wengine walitamani kujimaliza!!!!


USIKOSE SEHEMU 25 IJAYO.
 
jamani hili jitu kaa! mtoto nyota walinde wanaokuhifadhi wasidhuruke. Aasante MziziMkavu
 
Last edited by a moderator:
666-NYAYO ZA KUZIMU--25-

Matumbo yalichemka,jasho liliteremka!! Wengine walizirai kwa uoga,na wengine walitamani kujimaliza!!
Vilio vya wamama na watoto vilimeza ukimya wote wa usiku,ile sehemu haikukalika kabisa! Wake waliwakimbilia waume zao ilihali na watoto vilevile!

Mzee Rama na mkewe waliumia sana kumpoteza wao mwana,japokua walikua saba lakini hawakuhitaji kumpoteza hata mmoja wao machoni pao,machozi vilio na mafua ya uoga na uchungu vilitawala,kila mtu akawa anatizamatizama nyuma kwa hofu ya usalama wake binafsi.

Wakati taharuki bado imeshika nafasi,miili ya watu waliobebwa koroboi zilipozima ilionekana tena ikining'inia kwenye ule ule mti wa muembe aliotundikwa mama Matata!! Mavazi yao waliyokua wamevaa

hayakuonekana wala kujulikana yalielekea wapi,walikua wamevishwa majoho mekundu kama alilovishwa mama Matata na yote yakiwa na ujumbe ule ule uliosomeka BADO KIDOGO!! Masikio yao na midomo ilikua inavuja damu na huku macho na ulimi vikiwa vimetoka nje!! Walitisha sana,hasa wakionekana wakibembea na kamba zao nyekundu shingoni! Idadi ya waliokufa na kamba kwa ile siku ikawa ni tano tayari.je mchezo

utaendelea vilevile?? Na sasa ni yupi alie kwenye zamu?? Maswali hayo yalijaza vichwa vya wanakijiji.
Ilibidi kifanyike kitu sasa,kukaa tu pale kwa kutegemea ni salama ilikua si sahihi,mzee Rama na mwalimu Baraka walijitolea kwenda kwa mzee Patili kwa lengo la kumpa taarifa ili awasaidie kwa lolote kunusuru maisha yao yaliyo mikononi,waliwaaga wanakijiji huku wakiwaomba wawaombee wafike salama kwani safari

iliyombele yao ni ya kutisha,hofu ilikuwemo mioyoni mwao lakini hakuna jinsi jambo lile ilibidi litendeke,mke wa mzee Rama na wanae sita waliobaki walikua hawana matumaini kama baba yao atarudi,walimuangalia kwa huzuni huku wakimpungia mkono wa kheri,mwalimu Baraka nae alikua anajilaumu nafsini kwanini alikubali kuja kufundisha kijiji kile,ndio serikali ilimpangia lakini aliona alifanya kosa kuja lile eneo,ni bora angekataa hata kama ingehatarisha kibarua chake,mambo yanayojiri yataka moyo.

Safari ilianza,taratibu mwalimu Baraka na mzee Rama wenye baraka za usalama kutoka kwa wanakijiji walikua wanajongea,hofu waliyonayo mioyoni iliwafanya washindwe kujizuia kugeukageuka nyuma na mioyo kwenda mbio,lakini nyuso zao zilificha hayo,kila mmoja alikua anataka kudhihirisha kwa mzenzie kwamba haogopi.

Wakiwa kwenye mwendo mwalimu Baraka aliitoa simu yake iliyofeli mtandao tokea majuzi kwa lengo la kujua wakti,alishtushwa sana na alichokiona,muda uliokua unaonyeshwa na simu yake haukumwingia kabisa akilini! Ni muda mrefu umepita tangu giza liingie lakini bado saa ilikua inasema ni saa MOJA NA NUSU

USIKU!! lile jambo lilimfanya mwalimu Baraka ahisi saa yake imepoteza majira lakini bado alipata maswali kichwani kwamba hii tabia ya kupoteza majira imeanza lini kwani alikua ameiseti saa yake hivyo hata likitokea jambo lolote bado majira huwa palepale,alipata hofu lakini hakutaka kumshirikisha mzee Rama,alinyamaza na safari ikaendelea,lakini ukweli ni kwamba muda ulikua hausogei,yani ulisimama palepale!
* * *
Julina baada ya kupewa somo zito na wenzake,aliituliza hofu yake,akatambua thamani ya mwanae na hakuwahi tarajia kwamba angekua mtu wa kumzaa mtoto ambaye angehitajika kwa ule muda,alijivunia hilo.Mzee Otongo hakutaka kumficha Julina,bayana alimjuza ya kuwa asipoteze muda kumsubiria mumewe kwani ni dhahiri atakua ameuwawa na Jeshi la 666 tangu yeye ni baba wa kiumbe hatarishi kwao,hii habari

ilimsikitisha sana Julina japokua nae alikua na hisia hizo hizo japo hakua na uhakika,chozi lilimdondoka,alimpenda sana mumewe Kitanzi na hata ndoa yao haikufikisha hata miaka miwili,bado alikua na hamu nae na ukizingatia hajamuona mtoto ambaye mkewe alimleta ulimwenguni,ilitia huruma.

Kila mtu alie mule ndani aliuona usiku ni mrefu,walitamani kuona mwanga wa jua ukipendezesha tena macho yao,waliona usiku ni hatari kwao hivyo mioyo yao ilishikwa na tamaa kubwa ya kuona tena miale ya jua itakayoamsha matumaini yao,sauti za wadudu ziendeleazo huko nje zilizidi kuwaogopesha,hasa Julina.
Ngo! Ngo! Ngo! Sauti toka mlangoni iliwasili masikioni na kuwashtua kidogo,kama kawaida mama Halima alikimbilia dirishani na kuchungulia ni wakina nani,kisha akawatonya wenzie "ni wakina Madhifa!"
"wafungulie!"
mzee Patili akasema,

wakina Madhifa waliingia ndani kwa haraka huku wakihema kwa nguvu hali iliyowatisha na macho yao yalikua yanamimina machozi,kwikwi ikiwabana na kuwazuia kusema walilodhamiria,ilibidi mzee Patili awatulize kwanza ili waweze shusha presha na kusema kilichowaleta,baada ya kutulia wakasema
"Mama Linda na mumewe wamenyongwa!!"

kauli hiyo iliwafanya wakina mzee Patili mioyo ipasuke kwa mshangazo na kuanza kwenda kasi!!! Ilikua ni kama tamthilia kwenye masikio ya mzee patili aliewaona hao watu muda si mrefu,wakiwa kwenye taharuki na butwaa wakasikia hodi tena!! Ya Mara hii ilikua ni ya wakina mzee Rama na mwenzie mwalimu Baraka! Je itakuaje?


USIKOSE SEHEMU YA 26 IJAYO....
 
Duh! Mungu saidia hiki kiama kisitukute,asante MziziMkavu hadithi nzuri sana tupe uhondo.
 
Last edited by a moderator:
666-NYAYO ZA KUZIMU--26-

Nao pia wakasema kilichowaleta,watu watatu ambao ni mama matata,mtoto wa mzee Rama na mmama mmoja wa makamo wamenyongwa katika mazingira ya kutatanisha na aliewanyonga hajulikani,kwa ujumla taarifa za vifo zilizomfikia mzee Patili zilikua tano!! Alishangazwa na hiyo

idadi,na si tu yeye hata wakina mzee Otongo na wakina Julina!! Hofu ziliwashika mpaka kwenye ukucha,puh! Julina akadondoka na kupoteza fahamu!! Mtoto aliekua amembeba aliwahiwa

haraka na mama Halima na ilikua rahisi kwake kwa kua walikaa karibu,shughuli za kumpepea kumrudisha kwenye fahamu zikaanza haraka!! Mzee Rama na mwalimu Baraka wakapata kibarua cha muda cha kupepea huku wakina Madhifa wakiwa tu pembeni wakishuhudia hayo,uadui bado uliwatenganisha.

Baada ya kamuda kadogo Julina alirudi kwenye fahamu zake.
Uhasama uliokuwepo baina ya makundi mawili yaliyokuwepo pale ulionekana dhahiri,wakina Madhifa walijitenga kabisa na wakina mzee Rama kwani ndio wanahousika na uchomaji wa

nyumba zao,vilevile mzee Rama hakujumuika nao kwa kudhani ku yote yajiriyo chanzo ni wao na alikua anawatizama wakina mzee Otongo kwa jicho baya kutokana na imani yao kua wale wageni pia huchangia kutokea kwa hali husika,mwalimu Baraka yeye hakua upande wowote kwani yeye si mwenyeji pale kijijini,mzee Patili aligundua huo mkanganyiko,kazi ya kuwatuliza wale watu wenye imani tofauti ziendeshazo mioyo yao ilibidi ifanyike,aliamini ya kua umoja utakaokuwepo

baina yao ndio utakaokua silaha kubwa ya kujilinda na kukabiliana na linalowasibu,elimu hasa juu ya kinachoendelea ilihitajika kwenye vichwa vyao na vya wanakijiji wote ili iwe kama chachu ya mabadiliko na mwanzo wa mapambano,alitumia busara,aliwauliza wakina mzee Otongo kama

wanaweza jongea wakajibu watajitahidi,akawapa ujumbe wakina Madhifa ya kwamba wakawaite wenzao yani jamii ya wawindaji na wakutane kwa mama Kurwa,walitii walichoambiwa,wakatokomea kwenda kuwasilisha,kisha akawaambia wakina Julina na wakina

mzee Otongo wainuke na safari ianze ya kuelekea huko walipotokea wakina mwalimu Baraka,yani kwa mama Kurwa ambapo ndipo wanakijiji walipokusanyika,akachukua vibuyu vyake viwili kisha safari taratibu ikaanza wakiwemo watu nane;mama Kadogo na mzee Otongo

waliokua wanachechemea,Julina na mama Halima aliembeba mtoto,mzee Patili mwalimu Baraka na mzee Rama.Japokua walikua wengi lakini bado kale kamchezo ka kuangaliangalia nyuma hakakukoma,kila kaupepo kalipopiga miili yao iliiteka misimko ya kioga hasa Julina

alieng'ang'ania awe katikati ya watu,ni sauti za miguu yao tu ndio ilyosikika walipokua wanapita,kote kulikua kimya ukiondoa vikelele vidogodogo vya vijidudu vya usiku,muda huo wote waliokua njiani mzee mzee Patili alikua anafanya kazi ya kuvitikisa vile vibuyu vilivyomkononi,haikujulikana kazi yake ni nini na hakuna mtu aliemuuliza,walimuacha afanye mambo yake kwa uhuru.

Hatimaye walifika walipokua wanaelekea,watu waliokua wamejikunyata kwa kukosa matumaini waliamka na kumlaki mzee Patili,aliwapa mwanga wa kufanikiwa,akikua mwema kwao kwa ule muda,walisahau kabisa walichokifanya huko nyuma,ila ujio wa wakina mama Kadogo na mzee Otongo uliwashtua wanakijiji,moja kwa moja minong'ono ikaanza kururuma....mzee Patili hakuvumilia hilo,aliufungua mdomo wake kwa ukali akasema

"acheni upumbavu wenu usio na msingi!! Huo ujinga ndio upelekeao hali kua mbaya zaidi na hautupi unafuu wowote! Nani asiemjua huyu mzee Otongo?? Si nawauliza nyie! Ni mara ngapi alikua anakuja hapa kijijini na kuwasaidia matatizo mbalimbali?? Iweje leo unaufungua mdomo wako na kumnyooshea kidole,mshausahau wema wote alioutenda kwenu? Mbona mnakua na vichwa vya panzi na mioyo y kutu!"

wanakijiji wote walitulia na kusikiliza kwa makini na roho zao zilianza kuwasuta,mzee Zptili akaendelea kunena..."umoja wetu ndio unaohitajika,kugawanyika kwetu ndiko kunapoipa mwanya kushindwa kwetu,nawaambia kama tusipokua pamoja,shingo zote zilizokuwepo hapa zitaonja kamba nyekundu kama waliopita!! Tutanyongwa kama kuku!!"

alizidi kusisitiza kwa sura ya mkazo,muda si muda wakina Madhifa wakaingizana,ukimya bado ukawa umetawala,masikio na macho yao alipewa mzee Patili aliesimama mbele.Baada ya mzee Patili kurudufisha imani za waliokua wanamsikiliza,aliwakaribisha wakina mzee Otongo na mama Kadogo kwa lengo la kutoa somo juu ya hali iliyojiri,waliwadadavulia na kuwanyumbulia wanakijiji kwa undani tangu walipotokea na nini kimewaleta hasa.


USIKOSE SEHEMU YA 27 IJAYO...
 
666-NYAYO ZA KUZIMU--27-

waliwadadavulia na kuwanyumbulia wanakijiji kwa undani tangu walipotokea na nini kimewaleta hasa.Maneno na maelezo yaliyotolewa na wakina mzee Otongo yalionekana kuwatisha zaidi wanakijiji,habari za jeshi la 666 zilikua ni za kuogofya na zenye kutaka ujasiri kuzisikia,hakukua

na jinsi ilibidi waambiane ili wapate pa kuanzia,elimu hasa iliyokua inatolewa juu ya kiendeleacho ndicho kilikua cha kwanza kisha hayo mengine yachukue nafasi,zoezi lilifanikiwa na kumalizika salama huku likianzisha ukurasa mpya wa maisha yao ambao walikua hawajautambua,nia na

nguvu yote ya wanakijiji ilielekezwa juu ya kumlinda yule mtoto aliezaliwa na mengine pia kama watakavyoelekezwa kufanya na viongozi wao waliowateua ambao ni Mzee Patili,mama Kadogo na mzee Otongo,hakukuwa na ubishani tena wala minong'ono isiyo na msingi,sasa kila tendo lililochukua nafasi lilikua ni maelekezo dhabiti toka kwa viongozi wao,hakuna alietia dosari.

Mzee Patili aliwataka wanakijiji wajipange mistari miwili ya kijinsia,bila kuchelewa wakajipanga,alivichukua vibuyu vyake na kimoja akamkabidhi mama Kadogo kisha akampa maelezo madogo tu yaliyofanikisha kumjuza kiendeleacho,zoezi la kuwapaka wanakijiji dawa

usoni na mikononi kwa lengo kuu la kudhoofisha nguvu za adui wao lilichukua nafasi,mzee Patili akiwa anapakaa mstari wa wanaume na wavulana huku mama Kadogo akiwa anashughulika kwenye mstari wa wanawake na wasichana,idadi ya wanakijiji iliyokuwepo haikuendana na kiasi

cha dawa husika hivyo ilipelea,watu kama ishirini hawakua wamepakwa dawa kitu kilichompa maswali mzee Patili juu ya nini hasa cha kufanya,baada ya kufikiria kidogo aliwachagua wanaume wawili (mrisho na tabwe) kisha akawaagiza waende nyumbani kwake kwa lengo la

kuchukua dawa ili apate malizia waliobaki,ujasiri waliopewa na dawa walizopakwa ziliwafanya wasijifikirie mara mbilimbili,haraka walijiondoa lile eneo na kueleke walipotumwa.
Wakati hayo yote yanachukua nafasi lile jibaba linyongaji lilikua likishuhudia,kwa mbali lilijificha

kwenye mapori ila macho yake mekundu makubwa yalimfanya aone vizuri kilichokua kinafanyika,hakua peke yake kwa sasa hivi kama ilivyokua,pembezoni yake alikuwepo mwanamke mmoja mwenye macho ya paka na ulimi mwekundu!!! Alijivika kaniki nyeusi na

kiremba chekundu kilichositiri mapembe yake vizuri,ngozi yake ilikua na rangi ya kijivu na masikio yake yalikua marefu ilihali na kucha za mkononi,sasa walikua wawili kwa idadi,jeshi la 666 liliongeza mashambulizi!!! Wanakijiji watahimili hili??

Lile pande la mtu jeusi na yule mwanamke mithili ya paka walitabasamu na kuruhusu meno yao ya kutisha kuonekana,walipeana ishara,wakashika njia na kuelekea kule wale wanaume walipotumwa,yani kwa mzee Patili kwa lengo la kuzuia zoezi la uletaji dawa,lile Pande la mtu mkononi lilishikilia kamba nyekundu kama ilivyokawaida yake na yule mdada mithili ya paka akiwa na kisu kirefu!!!

Matamanio yao ya kuua bila kuchelewa na kufanikisha lengo lao yaliwafanya wajione wanachelewa kwa kutembea,hivyo walianza kukimbia huku macho wakiwa wameyatupia mbele!!
* * * * * * *
mrisho na mwenzake walishafika eneo husika,walikua ndani ya kijumba cha mzee Patili wakifanya jitihada za kusaka dawa waliyotumwa,uwepo wa dawa nyingi mule ndani ulifanya zoezi liwe gumu kwani kila dawa waliyoipata walipoinusa waligundua sio yenyewe,ilichukua kama

muda wa dakika saba mpaka walipoitia mkononi iliyolengwa,waliangaliana kwa tabasamu kisha wakaelekea mlangoni,Mrisho aliunyoosha mkono wake na kuuvuta mlango,mlango ukagoma kufunguka!! Alizidi kutumia nguvu zaidi lakini bado matokeo yakawa yaleyale,mlango uligoma

kabisa kufunguka!!! Ikabidi amuachie Tabwe nae ajaribu lile zoezi,hakuna aliefanikiwa,bado hawakuweza kuufungua,hofu ilianza kuchochewa mioyoni mwao,wakaangaliana kwa uoga huku kajasho kakitirika,Tabwe huku akitetemeka akasema..

"Mrisho..tunakufa...!!"
Mrisho akameza mate,moyo ulikua unampwitampwita na macho yakimtoka,alipata wazo kichwani haraka akamwambia mwenzie
"Tabwe...tu..tu..tuvunje mlango!!!"

Tabwe alionekana kukubaliana na hilo wazo lililoonekana ni pekee kwa ukombozi wao,bila kuchelewa harakati za uvunjifu zikaanza kikamilifu kwa kutumia mateke,hawakua na habari ya kuwa lile jibaba linyongaji na yule mdada mithili ya paka walikua kwa nje wakiwasubiri kwa

hamu zote ili kuongeza idadi ya waliokwenda na maji na kusafisha njia ya kufanikisha lengo lao,puh!! Mlango ukatupwa kule na nguvu ya teke zito la wakina Mrisho!! wakatoka nje,he!!! hawakuamini walichokiona!! Kitendo cha kugonganisha macho na yule mdada mithili ya paka

lilikua ni kosa kubwa!!! Walinyong'onyea na kupoteza nguvu,wakadondoka chini kama mizigo tii!!! Lile Jibaba likasogea karibu yao huku likitengenezea vitanzi tayari kwa ajili ya

kuwanyonga,macho ya yule mdada yalishalainisha zoezi kwa kudhoofisha ile dawa waliyopakwa hivyo kuruhusu zoezi la unyongaji kuchukua nafasi kama kawaida!!!!

JE ITAKUAJE? MUUNGANIKO WA WANAKIJIJI UTAUKABILI MUUNGANIKO WA JESHI?


USIKOSE SEHEMU YA 28 IJAYO....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom