666-NYAYO ZA KUZIMU--16-
Cha kushangaza walivyorudisha tena nyuso zao dirishani kutizama nje...hawakuona kitu!!!!..Pah!!!..tik-tak!!! Tik-tak!!! Tik-tak!!! Tik-tak!!..mioyo yao ilianza kwenda kasi ya ajabu!!! Bumbuwazi lilikamata midomo yao bara-bara! Macho yaliwatoka mithili ya kwamba wamemshuhudia shetani akionja pepo!!!..walitupiana macho ya uogo wakiulizana wameenda wapi??? Swali lililopasua hisia zao mithili ya shoka kali lililotoka kiwandani kwenye gogo bua lililochoka!
Mungu wangu..watafanyaje sasa?? Hilo lilikua ni swali la pili rejea lililokita vichwani mwao kama hitimisho!!!
Hapakukalika tena!!..nyumba ilizidi kuwa ndogo kwao!
* + * + *
koh-koh! Sauti ya kikohozi cha maumivu kiligona sikioni mwa mzee Patili,aligeuka haraka na kuangalia kilipotokea akagundua ya kwamba chatoka kwa mzee Otongo aliekua amelala chini chali,alitabasamu kwa mbali,jitihada za dawa yake aliyompaka zilionekana kuvuta kheri,hakutaka kupumbazwa na hilo jambo,aligeuka na kuendelea na shughuli yake ya kumpaka dawa mama Kadogo taratibu akimalizia miguuni baada ya mikononi na usoni akijitahidi kuyaziba majeraha na dawa ile ya unga yenye rangi ya kahawia,mchanganyiko wa miti mbalimbali iliyosagwa.
Chumba kilitawaliwa na moshi kwa kiasi kikubwa,lakini hilo halikuonekana kumkwaza mzee Patili,kwani tangu na tangu,enzi na enzi amekua katika yale mazingira ambayo hasa huchangiwa na shughuli zake za upikaji dawa,mvi ziligoma kabisa kuja kichwani japokua umri uliruhusu hilo,uso wake ulio na makunyanzi ndio uliothibitisha ya kwamba kala chumvi,mzee Patili alikua ni zahanati tosha pale kijijini,akiheshimika na kusikilizwa kama marehemu baba yake aliemrithisha hizo kazi.Baada ya kumaliza ile shughuli ya upakaji dawa,alishusha pumzi ndefu kisha akajituliza kwenye kigoda chake chenye ufa kwa mbali uliodhihirisha ya kwamba ni cha muda mrefu,haraka akili yake ilimtumbukiza kwenye lindi la mawazo,lindi la mawazo mazito juu ya ndoto aliyoota usiku wa kuamkia hiyo alfajiri,ndoto ile ilionekana kumkosesha amani na hata raha vilevile na kila alipotaka kuitafutia ufumbuzi hakupata kitu!!!
Alitizama juu ya dari kimawazo huku kichwa kikiegemea mkono akijaribu kuitumikisha akili yake iliyojaa uzoefu wa maisha kumpa majibu,
ghafla!!!!
"mzee patili funguaaa!!!"
sauti za kile zilisikika toka nje,
"niniii???..nyie wakina nani!!!"
kwa tahamaki aliuliza,
"Julina na mama Halima!!!..tafadhali tufungulie haraka!!"
alijibiwa,alijinyanyua toka kwenye kile kigoda haraka na kuelekea mlangoni,akaufungua mlango na haraka kwa papara waliingizana wakina mama Halima!!
"nyie vipi???"
aliuliza mzee Patili,hakujibiwa,akauliza kwa mara ya pili kwa sauti ya msisitizo!
"nyie kuna nini?? We mama Halima vipi na huyu Mzazi tena!!!"
huku wakihema kwa pupa wakajibu,
"kuna wabibi wawili!!"
"wamefanya nini?"
"wa..wa..walikua wanagonga..mm..mlang..mlango.."
"halafu haraka wakapotea!!!"
Julina akamalizia sentensi huku akiwa kamkumbatia mwanae na mikono itetemekayo!,
"wakapotea!!! Wakaelekea wapi??"
"hatujuuii!!!!"
julina alidakia,
"he! Mzee Patili hawa waliolala hapa chini wakina nani???"
aliuliza mama Halima baada ya kuiona ile miili ya mama Kadogo na mzee Otongo pale chini,Julina pia mwenye damu iliyotawaliwa na uoga nae alistuka baada ya kuona hilo,akatahamaki
"mungu wangu!!!! Mzee Patili hawa wakina tena???"
"msijali kuhusu hao watu,waliletwa hapa na baba Madhifa,waliokotwa toka porini,embu punguzeni uoga na presha enh...tulieni embu,tulieni kisha mnielezee kilichojiri"
aliwatuliza mzee Patili.
Mzunguko wa damu wa Julina uliongeza kasi kutokana na uoga! Alikua anahema kwa kasi,mama Halima vilevile!
Mzee Patili ilimbidi anyamaze huku akiwashuhudia wale wakina mama kwa jicho la kutafakuri hali ile iliyowatokea,moshi uliokuwemo mule ndani ulianza kumuathiri mtoto,akaanza kupaliwa na kikohozi hali iliyomfanya mzee Patili kumshauri atoke nje,kiuoga alijibu
"nani?? Mie!! Ah-ah sitoki nje! Wale wabibi watanifata!!!"
mzee Patili aliamua kumaliza zogo,alimnyakua mtoto toka kwenye mikono ya mama yake Julina kisha akatoka nae nje,hali ya kushangaza Julina nae kwa uoga akatoka nje!!!!
* * * * *
JE ITAKUAJE? Usikose! SEHEMU 17 IJAYOO....