666-nyayo za kuzimü

666-nyayo za kuzimü

666-NYAYO ZA KUZIMU--10.

Kadogo alikua anahema juu juu na kwa nguvu hali iliyomfanya mzee Otongo amzibe mdomo,ubavu wa mzee yule uliegemeana na wa mama Kadogo aliyekua anatetemeka hivyo mtetemo wote ule uliokua unampitia mama Kadogo alikua anausikia,walitoa macho na kufumba kabisa midomo yao ili wasiskike,huku wakishuhudia watu wale walio idadi ya watu watano wakiwa wanapepesa macho yao kutafuta watu kwa ajili ya sadaka zaidi,mzee Otongo alinong'oneza..

"mama Kadogo tuondoke hapa si salama"
"mh tukiondoka si watatuskia?"
"hapo walipo wananusa harufu yetu na ndo mana unaona wamekazania hili eneo"
"kwahiyo?"
"tuondoke taratibu kabla hawajatugumia"
alizidi kutia msisitizo mzee Otongo,
baada ya muda si mrefu walinyanyuka taratibu toka kwenye kibanda kilichokongoroka walipokua wamejificha,walianza kunyata kama watu wanaohesabiwa hatua,pole pole huku macho ya tahadhari yakiwa yanawatizama wale watu mara kwa mara,mioyo yao ilikua inadunda kwa kasi hasa Kadogo ambaye ana matatizo,alitoka jasho mno ikiwa ni moja ya viashiria ya kuanza kuzidiwa,damu ilikua inazunguka kwa kasi mwilini na mama yake aliligundua hilo,alianza kuhisi mkono wa mwanae alioushika unapoteza nguvu na hakua na jinsi zaidi ya kumnyanyua na kumweka mgongoni,waliendeleza zoezi la kunyata kunyata na kunyata mpaka pale mzee Otongo alipotoa ishara,
"tukimbie mama Kadogo!"
na mbio zikaanza kama za farasi,mzee Otongo alitangulia sana mbele na kumuacha mama Kadogo nyuma hali iliyomfanya aamue kumsaidia mama Kadogo mtoto anaeonekana kumchosha ili wakimbie zaidi,mkono wa mama Kadogo ulishikwa na mzee Otongo kinguvu hasa ili usiponyoke,walijitahidi sana kukimbia huku wakipambana na hali ile ya baridi la usiku na visiki na mawe mbalimbali yaliyoonekana kuwaumiza miguu yao,hawakujali hilo ila walilenga tu kusogea mbele na kuokoa roho zao.Mgongo wa mzee Otongo ulionekana kuhimili mzigo wa mtoto Kadogo ila mama Kadogo ambaye alitoka kukimbia kabla ya kukutana na mzee Otongo alionekana hana nguvu tena ya kuendelea na zoezi lile,alisimama huku akishika kiuno,akasema..
"mzee....uuh!...uuh..siwezi tena!...nimechoka!"
"mama Kadogo jitahidi,hatujawaacha mbali sana wanaweza wakatufikia!"
"mzee Otongo....uuuh..uuh!..nimechoka sana aisee..!"
huku akiinama,
"mama Kadogo!!"
"abee...mzee Otongo"
kiuchovu aliitika
"embu angalia ile!!"
"nini tena??"
mama Kadogo aliuliza,
"ile angani! Ni nyota nyingine ama macho yangu!!?"
haraka mama Kadogo aliyarusha macho yake angani kutizama alichoelekezwa,
"ndio!! ...eh!..ndiooo jamani! Ni nyota nyingine mzee Otongo...ni nyota nyingine!!!"
"ha! Mama Kadogo kuna mmama ana uchungu wa kujifungua sasa hivi tunavyoongea!! Na ndie atazaa mtoto atakaetuokoa,mama Kadogo tumaini li hai!..huree!!"
"sasa huyo mmama yupo wapi??"
"kijiji cha pili toka ilipo Igesambo,na inabidi tumuwah kabla huyo mama hajadhuriwa na Jeshi la 666 kwani wakiiona tu ile nyota watamtafuta kwa udi na uvumba ili wamtokomeze!!...haraka inuka mama Kadogo,haraka tumuwahi mtoto anekuja!"
haraka mama Kadogo alieanza kupata nyuso yenye mwanga wa matumaini aliinuka na wakaanza kutembea harakaharaka kwa dhumuni la kukusanya nguvu ya kukimbia hapo mbele,kushoto kulia kushoto kulia miguu yao ilipiga maksai wakitafuta kijiji cha pili toka kilipo Igesambo,kijiji cha Utowele,kijiji cha wavuvi na wakulima kama imaanishavyo jina lake,kukifikia kijiji cha Utowele inabidi wavuke mto mkubwa Inguvai,wapite safu ya milima Iramba kisha ndipo watakapokanyaga ardhi ile ya mwanga,ardhi ya tabasamu,ardhi ya mapinduzi na ardhi ya ukombozi,baada ya safari yao kutimiza nusu saa walianza kusikia maporomoko ya maji yaliyowajulisha ya kwamba wapo karibu na mto,mto Inguvai usiopungukiwa na maji misimu yote ya mwaka kutokana na kutokea kwenye safu ya milima Iramba ipokeayo mvua za kutosha zipendeshazo msitu kwa umbijani,
ilihitaji uangalifu mkubwa sana kuvuka mto ule hasa muda ule wa usiku,maji yake yana nguvu mno na yanatosha kabisa kumpeleka mtu mzima hata mnyama yeyote endapo akitumbukizwa.
Walivyowasili kwenye kingo za ule mto mzee Otongo alimshusha chini kadogo,kisha aligeuza sura yake na kumtazama mama Kadogo akisema
"inatubidi tusali mama Kadogo,mungu awe nasi na atushike mkono,atuongoze kuuvuka mto huu,na pia atuongoze tuivuke milima ile...na hata kama mmoja asipofanikiwa isiwe mwisho wa mapambano.umenisikia mama kadogo?"

* * * * *
JE WATAFANIKIWA??
JESHI LA 666 NALO LIMEGUNDUA KUHUSU ILE NYOTA?
USIKOSE! SEHEMU 11 IJAYO...
 
666-NYAYO ZA KUZIMU--11-

"Inatubidi tusali mama Kadogo,mungu awe nasi na atushike mkono,atuongoze kuuvuka huu mto,na pia milima ile....na hata mmoja wetu asipofanikiwa isiwe mwisho wa mapambano yetu.umenisikia mama Kadogo?"
sura yenye msisitizo isiyotania ya mzee Otongo iliyatamka yale maneno.

"sawa mzee Otongo,inatubidi tupigane mpaka tone la mwisho la damu yetu,inabidi tufe tukijaribu"

alieleza mama Kadogo huku chozi likimlengalenga.
Aliyatupia macho ya huruma kwa mwanae,akachuchumaa akambusu kwenye paji la uso kisha aliinuka na kusema
"sasa tunaweza kuvuka.."

akamueka mwanae mgongoni,akaanza kusogelea maji ya mtoni taratibu huku akitanguliwa na mzee Otongo.

Mto Inguvai hauna daraja la kumuwezesha mtu kuvuka kwa urahisi,ni utashi wa mtu tu ndio unaotakiwa ili aweze kurukia mawe yaliyokuwepo pale kwa ajili ya kuikuta ng'ambo,ilimuwia vigumu sana mama Kadogo kurukia yale mawe kwani ukiachana na lile

giza la ule muda bado alikua na mtoto mgongoni,walisogea hatua mbili tatu huku moyo wa kila mtu ukidunda kwa uoga na tumbo la kila mtu likisokota kwa uoga pia,mawe waliyokua wanayakanyaga yalikua yameshika utelezi hivyo ilihitaji uangalifu mkubwa na bado miguu yao iliyo peku ilikua inapitiwapitiwa na maji kitu kilichoashiria ya kwamba maji ni mengi kiasi cha kukaribia

kufunika yale mawe yatumiwayo kama kivushio,hakukua na muda wa kutosha wa kuangalia nyuma,kila mtu aliyatoa macho kwa kiasi kikubwa ili yapambane hata kidogo na lile giza lililopo ili apaone pa kuutuliza mguu wake,walizidi kusogea na mwendo wao wa kinyonga na ilibakia kama mawe matano tu ili waweze kupita kile kizuizi,ghafla sauti kubwa ya mlio wa pembe la ng'ombe iliskika!!


Haraka kwa uoga mama Kadogo aligeuka nyuma kabla sauti ya mzee Otongo kufika masikioni mwake ya kwamba hatakiwi kugeuka!!


Mguu wake wa kulia ulio mbele uliteleza na kumfanya aifungue mikono yake kwa ajili ya tahadhari ya anapodondokea na kumuacha Kadogo aliekua kambeba mgongoni akidondoka kwa urahisi!!!


Mikono yake miwili ilishikilia mawe kwa nguvu na kumfanya abakie salama kwa kutopelekwa na maji ila mwanae Kadogo ambaye kamwili kake hakakutosha uzito kushindana na ile nguvu ya yale maji alibebwa kama kikaratasi akimuacha mamaye akilia kwa uchungu bila msaada wowote!!


Mzee Otongo ilimbidi arudi nyuma kitaratibu,alishika mikono ya mama Kadogo iliyoanza kuzidiwa nguvu na kuanza kumvuta kwa lengo la kumuondoa kwenye yale maji yenye kasi kubwa!!


"mama Kadogo jitaahiiidiiiiiiii!!!!.."

"mzee Otongo niache tu nife! Mwanangu jamani!!!!!"
"mama Kadogo hatuna muda wa kupotezaaa!!!!..
Tafadhali jitahidi utoke kwenye hayo maji nguvu inaniishiaaa!!!!!"
"mwanangu Kadogo jamaniii!!!"
"mama Kadogooo!!!...tafadhali nadhani unakumbuka nilivyokuambia kabla hatujavuka..tafadhali jitahidi utoke,tafadhali nguvu zinaniiiishaa!!!"
kwa nguvu aliropoka huku akikunja sura!
* * * *
upande wa pili wa shilingi jeshi la 666 lilikusanyika,ile mbiu ya pembe la ng'ombe iliyopigwa ilikua ni ishara ya kwamba wanaitwa,walisimama kwa utulivu na usikivu,na tahamaki ndani ya jeshi hilo mama Utopi alikuwepo!!..na si tu huyo hata mama

Marinda na Vero!!...walishapigwa chapa,hivyo walishakua chini ya utawala wa Chernobog!!

Mzee mmoja asie mfupi wala mrefu yani saizi ya kati alisimama mbele yao,mkononi alishika fimbo yenye alama ya nyota nyekundu na kimavazi alinawirishwa kwa rangi nyeusi na nyeupe,macho mekundu na lips zake pana ziliönyesha ana kabiliwa na jambo,bugudha na hasira zilionekana kumteka!!

Kabla ya kufungua mdomo na kunena jeshi la 666 liliinamisha vichwa na kudhihirisha ya kwamba alie mbele ni mkubwa wao,

"ni nyota ndio iliyotuita!
Ni kwasababu ya nyota tupo hapa!!
Nyota nyingine imechomoza angani,nyota itishiayo nyota ya CHERÖBOG!!!..nyota imaanishayo ya kwamba kuna mtoto anazaliwa,nyota imaanishayo hatari kwa utawala wa giza,nyota itakayoamsha tena Jua lililopotea,nyota itishiayo makazi ya KUZIMU duniani!!!

Hakikisheni huyo mtoto haponi! HAKIKISHENI MNAMTOKOMEZA KABLA JUA HALIJACHOZA TENA!!! HAKIKISHENI

MNAMMALIZA HARAKA IWEZEKANAVYO!!!"

"Ameen!!"

waliitikia na kutoweka haraka kwa kasi wakielekea kule mtoni walipo wa kina mama Kadogo na mzee Otongo!!

Watapona kweli kwa ile kasi? Na ni nani atakua wa kwanza kumchukua yule mtoto alie katika kijiji cha Utowele?
Vita kati ya giza na mwanga ndio inaanza??
UsIKOSE!!

USIKOSE! SEHEMU 12 IJAYO...
 
MziziMkavu hii sehemu hii!!
"nao ni utawala wa giiiiza!
Nao ni utawala wa kiiiiza!
Wasio amini kuwaumiza!
Na watakaoungama kuwahimiza!
Sita! Sita! Sita!
(sauti nyingine ikidakia)
kwenye paji la uso!
Sita! Sita! Sita!
Kwa maisha!
Sita! Sita! Sita!
Tunawasilisha!
Sita! Sita! Sita!
Tunawakilisha!!"
kisha sauti ikatulia kwa muda kidogo,sauti nyingine ya mtu mmoja ikaskika..
"kama wataka jiunga na ulimwengu,
kama wataka kuishi tangu na tangu,
toka nje upewe alama ya maisha!
Toka nje na yote yatakwisha!
Ila ukibaki humo ndani utakua ni wa sadaka!!"
* * * * * * *
 
Last edited by a moderator:
666-NYAYO ZA KUZIMU--12-

Walikimbia kwa kasi ya ajabu,hasira na dhamira ya kweli ikitawala vichwa vyao,kila mmoja kwenye paji lake la uso alikua na alama ya 666 ikiashiria na kuthibitisha ya kwamba anamilikiwa na utawala wa giza,utawala wa wapinga mwanga,utawala wa nyama na damu,utawala wa mungu mweusi,utawala wa CHERNOBOG,macho yao mekundu na pua inusayo harufu ya binadamu,miili yao ya baridi na yenye rangi ya kijivu bila kusahau masikio yao yaliyosimama yalikua ni sare zao mbali na nguo zao nyekundu na nyeupe,walitumwa wakamuangamize mtoto aliezaliwa,walitumwa wakamtokomeze haraka iwezekanavyo kabla ya jua kuchomoza kwani ni hatarishi kwa utawala wao na ni hatarishi kwa malengo yao,baada ya muda wa dakika arobaini na tano walishawasili kwenye kingo za mto Inguvai!!!
Je wakina mama Kadogo wako wapi?
Kwa mbaali juu ya safu ya milima Iramba mzee Otongo na mama Kadogo walionekana wakizidi kukwea,walizidi kupanda milima kwa lengo la kwenda upande wa pili kumuwahi mtoto aliezaliwa kabla ya kuchukuliwa au kuwahiwa na jeshi la 666,miili yao ilikua imechoka kutokana na zoezi lile gumu lakini hawakujiruhusu wapumzike kwani walifahamu ya kwamba jeshi la 666 li njiani na tayari watakua na taarifa juu ya uzao ule,wote walikua wanahema kama mbwa hasa mama Kadogo ambaye bado uchungu wa kupotelewa na mwanae ulikua umemtawala moyoni,alishindwa kuzuia machozi yasimtoke lakini pia hakutaka aruhusu miguu yake isimame,alimuita mzee Otongo alie mbele yake kisha akampa mkono wake wa kulia,akasema
"nahisi kichomi!"
..mzee Otongo akamvuta na kumkumbatia kwa nguvu kisha akamnong'oneza..
"imebakia umbali wa kama nusu saa kufika kijiji cha Utowele,imebakia huo umbali tu ili tulikute tumaini letu,imebakia tu umbali huo kwa ajili ya maisha yetu.hapa nilipo nina kiu na miguu inanivuta mno,lakini unanihitaji ili tuendelee,na mimi pia nakuhitaji ili niendelee,tafadhali jitahidi tukamilishe tulichokianzisha"
yale maneno yalimpa motisha kubwa mama Kadogo,alishusha pumzi ndefu kisha wakaanza tena kutembea kuelekea mbele kwa mbele.
Wafuasi wa jeshi la 666 bila kujiuliza mara mbilimbili walijitosa ndani ya mto Inguvai,mto wenye maji yenye kasi na nguvu ya hatari,lakini cha kushangaza walipiga mbizi mithili ya samaki na hakuna hata mmoja wao alieonekana kuzidiwa!!..hata mama Utopi mama Marinda na Vero waliopigwa chapa tayari walionekana kumudu yale maji!!
Mikono yao ilikua na nguvu ya ajabu na pia nyuso zao zilionekana kupambwa na alama ya moto ya tarakimu 666!
Baada ya kufika upande wa pili wa mto,pua zao zilianza kuvuta harufu ya binadamu na haraka bila kupoteza muda walianza kuifatilia kwa mwendo wa kasi,huku macho yao yalioakisi mwezi yakionekana kung'ara mithili ya paka!!
Umbali waliopo wao ulikua ni kama kilomita moja kamili tokea walipo wakina mama Kadogo,ila kwa ile kasi waliyokua nayo ilikua ni hatarishi na hivyo uwezekano wa kuwafikia ulikua ni mkubwa ukizingatia matatizo ya vichomi na miguu inavyowapa mtihani mama Kadogo na mzee Otongo.
Jeshi lile la 666 halikua na utofauti wowote na wanyama,hawakua na huruma hata kidogo kutokana na mioyo yao kubadilishwa na kua ya kishetani,maumbo yao pia hayakua ya binadamu wa kawaida,kuanzia kwenye vidole na kucha mpaka kwenye unywele,walikua na nguvu mno na ni kutokana na giza lililopo na ndio mana walipopewa maagizo waliambiwa wayatekeleze kabla ya jua kuchomoza kwani ndio utakua ukomo wa nguvu zao za ajabu!
Walizidi kujongea kwa kasi bila kuonyesha dalili yoyote ya kuchoka huku wakiwa wamepangana kimstari!...mara ghafla mwenzao alie mbele alisimama kisha akageuza shingo na kuwaambia wenzake
"nimeona watu kule juu!!!"
je hao watu ni wakina nani?
Na wataweza kutimiza walichoagizwa kabla ya jua kuzama?
Mama kadogo na mzee Otongo watafanikiwa kumuwahi mtoto kwa ile kasi na nguvu ya jeshi la 666?


USIKOSE! SEHEMU 13 IJAYO.....
 
Ohooo


||"Tomorrow will say its a memory and we have enjoyed our lives for a couple of days."||
 
Ingawa ni tungo tu lakini ni uhalisia wa kile kijacho. MWENYEZI MUNGU atunusuru giza lijalo. asante MziziMkavu
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom