666-nyayo za kuzimü

666-nyayo za kuzimü

666-NYAYO ZA KUZIMU-5-

"mnasema nini??"
"sisi ni mamajusi wa kishetani!..na tumekuja kumlaki mfalme wetu!!.."
"m..m..mfa..mfalme...yu..yu..yupi!"
aliuliza Vero huku akitetemeka,
"mfalme Chernobog,Mungu mweusi!"

Vero macho yalizidi kumtoka,hofu ilichochea ndani yake,alimuangalia yule mtoto aliembeba akamuona anatabasamu!...aliporudisha macho juu,aliona wale wazee watatu tayari washaingia,alisk

ia moyo umepasuka ghafla....hakuvuta tena pumzi,mwishowe akapoteza fahamu.Neno CHERNOBOG lina asili ya urusi,ni

mchanganyiko wa majina mawili,cherno ikimaanisha 'nyeusi' na bog imaanishayo 'mungu',kwahiyo kwa pamoja huza neno 'mungu mweusi' kama anavyoitwa mtoto yule na wale wazee.


Mtoto alichukuliwa kutoka kwenye mikono ya Vero aliepoteza fahamu,kila mzee alimbusu kwenye paji la uso na kuongea maneno fulani yaliyozid kulitunza tabasamu la yule mtoto.

Ghafla alifungua macho yake,hayakua ya binadamu wa kawaida na hata alipopanua mdomo wake,hakua na ulimi wa binadamu

wa kawaida,vyote vilikua ni viungo vya nyoka,tabasamu lenye afya lilichomoza kwenye kila sura ya wale wazee,kwa pamoja wakasema..

"baruch haba chernobog..
Ooh baruch haba"

lugha ya kiebrania(Hebrew) ikimaanisha 'karibu mungu mweusi,ooh karibu!'

..Vero bado fahamu hazikumrudia,hivyo hakupata kushuhudia kilichokua kinajiri,alijiona yu ndani ya giza nene akipepesa macho huku na kule kuutafuta mwanga,akiwa katika harakati hizo mara ghafla alihisi mkono umemgusa begani,haraka aligeuza yake shingo kwa hofu kuangalia ni nani,hakuona kitu,jasho likawa linamtiririka,mwili nao ukawa unatetemeka ilihali na nywele kichwani zikawa zinasisimka,
"wewe nanii???"

sauti iliyoshiba uoga ya Vero iliskika,hakuna sauti yoyote ya kimajibu iliyorudi masikioni mwake zaidi tu ya mwangwi uliomjuza ya kwamba yu ndani ya jengo.


Aliunyanyua mguu wake na kuanza kusogea mbele akiutafuta mlango huku akipata taarifa finyu kuhusu anapokanyaga kutokana na macho yake kushindwa kupambana na giza lile kali,kila alipozidi kusogea mbele alizidi kusisimka na kuhisi hatari zaidi,mguu wake wa kulia ulio mbele ulikanyaga kitu chenye ncha kali,alipiga yowe ya maumivu uliojibiwa na mwangwi mkali uliorudi masikion mwake,nafsi yake ilizidi kushiba hofu kwani alipoangalia kilichomchoma ni nini,hakupata kukiona!..bali tu alishuhudia mguu wake ukimimina damu,hapo ndipo alipoisikia sauti,nzito ya msisitizo na yenye kuogopesha!..

"tazama nao huo ndio utawala unaokuja!..
Utawala wa kiza!...kiza!..kiza na giza!!
Utawala wa nyama na damu!!

UTAWALA WA CHERNOBOG!!!...

Ha! Ha! Ha! Ha! Ha!........."

Vero alipiga makelele ya kiuoga na ghafla alijikuta ameamka toka kwenye usingizi ule mzito!....alipotazama pembeni hakuona kitu zaidi ya kusikia sauti za nyimbo zikitokea nje,alijinyanyua kwa tabu kutokana maumivu aliyokua bado anayo,alijisogeza mpaka mlangoni na kuanza kuchungulia,macho yake yalishuhudia wazee karibia ishirini wakiwa wamevaa mavazi meupe na mekundu wakicheza na kuimba huku wakimrusha rusha yule mtoto juu juu!!..


Baada ya dakika tano lile zoezi lilikoma,sauti ya mzee mmoja aliyekua ameshikilia fimbo yenye alama ya msalaba ikasema..


"wana wa utawala wa kiza huu ni wakati wetu!!"

"amen!"
wakaitikia wale wengine huku wakiinamisha vichwa vyao,
"na tupo hapa kumlaki mfalme atakaetuöngoza mpaka pale tutakapoikamata dunia!!"
"ameen!"
"na kuanzia leo jua halitochomoza,na ni ishara ya kutokua na mipaka kwenye maamuzi!"
"Ameen!"
"ila sadaka ya mtu mmoja haitoshi kabisa kumpokea mfalme wetu,hivyo basi inahtajika nyingine ya ziada!!.."
"ameen!"
"na nendeni mashariki na magharibi,kaskazini na kusini..MKAITWAE!!!!...."

Wale watu walitawanyika huku na huko kwenda kutafuta sadaka kwa ajili ya mapokezi ya mungu wao CHERNOBOG yani 'mungu mweusi',macho yao mekundu,miili yao ya kijivu iliyofunikwa na mavazi meupe na mekundu ilizidi kuchanja mbuga pande zote nane za dunia kwa ajili ya kuifanisha tafrija yao.


Baba Kadogo alizidi kutembea kuelekea mbele,alibakisha umbali usio mrefu sana kukamili

sha safari yake aliyodhamiria,ghafla panga lilimponyoka,akainama akaliokota akaendelea na safari,baada ya hatua mbili tatu panga likamponyoka tena!

Moyo ukaguma,akapata wasiwasi kuhusu ile hali,ila hakujali sana,aliinamisha tena mgongo wake akaliokota,mara ghafla akahisi upepo umempita kwa haraka!

Mwili wake wote ukasisimka!

Ujasiri wake ukaanza kupata mashaka,moyo wake nao taratibu ukaanza kuchanganyia mbio,alihisi joto limepanda,kijasho chembamba kilimshuka,alimeza mate kisha akaendelea kutembea,haukupita tena muda mrefu panga likamponyoka kwa mara ya tatu!


Milio ya hatari ikaanza kuita kichwani mwake,nafsi yake ikamtonya ya kwamba hayuko salama,bila kuuliza mara mbilimbili wala kupoteza muda wa ziada aliinama na kuliokota ganga kisha akaanza kukimbia!!


Hakuruhusu miguu yake isimame wala kupunguza kasi,alikimbia kadiri ya uwezo wake huku akihema juu juu kwa pupa kuitafuta oksjeni,tahamaki alisikia vishindo kwa nyuma vinakuja kwa kasi!

...Baba Kadogo alieanza kuloa uoga na kujuta kwanini hakusikia ile kauli ya mkewe alizidi kuongeza mwendo!

Alikimbia kupita uwezo wa miguu yake,mwishowe kama kiroba cha viazi alidondoka puh!!...panga kule!


Kabla ya kujikusanya na kuinuka,tayari alishazungukwa na watu watatu waliopendezeshwa na mavazi meupe na mekundu!!

Sauti kali ya maumivu ya baba Kadogo iliskika kwa nguvu kutoka msituni
"aaaaaahhh!!!!!!"
kisha tena kukawa kimya,
idadi ikawa ni watu wawili waliokwenda kwa ajili ya sadaka tayari!
* * * * * * * *

mama kadogo alihisi moyo wake umelipuka ghafla!

Alikosa amani,moja kwa moja alihisi kuna jambo baya limechukua nafasi,alitoka kwenye dirisha alipokua anachungulia na kumsubiria mumewe,kiuchovu na kimawazo akaelekea kwenye kiti alipo mama Utopi ambaye bado fahamu hazikumrudia,alikaa kihuzuni huku akishika tama,

"jamani mume wangu,sijui yupo salama huko?..mbona mapigo yangu ya moyo yanaenda mbio hivi?....eh mungu saidia!"

"koh!-koh!"
ghafla kikohozi cha mama Utopi kikaskika!
Haraka mama Kadogo aligeuza yake shingo na kumtazama,
"mama Utopi!"
"ab..bee!"
"vipi mama unajiskiaje?"

"......mmm,mikono inaniuma na miguu pia..inavuta sana!"

alisema mama Utopi huku sura yake ikiakisi maumivu aliyokua nayo,
"usihofu mama,itapoa tu kwani dawa iliyoekwa kwenye hizo bandeji ni kiboko.."
"ahsanteni jamani...ahsanteni sana"

alisema mama Utopi huku akikunja kunja sura kutokana na miale ya maumivu kumpitia,

"haina shida mama,ila samahani sana kwa wale mbwa wetu waliokujeruhi.."
"wala usihofu mwanangu.."
"hivi mama ilikuaje kwani?"
"mh...mama Kadogo,tumekwisha!!"
"tumekwisha? Kivipi yani...sijaelewa!"

"kile kizazi cha nyoka alichotuambia mzee Otongo yule mganga..kimewadia!!"

"eh? Umekionea wapi??"
"mtoto va Vero!..mtoto wa Vero ndie yule....
(kabla hajamalizia alikatishwa na hodi toka mlangoni)
"ngo! Ngo! Ngo!"
"nanii?"

aliuliza mama Kadogo huku macho yakiwatoka kwa uoga,

"mimi Baba Kadogo!"
sauti toka nje iliskika,

mama kadogo alifikiria kidogo,kisha akataka kuinuka ila mama Utopi alimzuia haraka!

Kisha akamuuliza,
"una uhakika huyo ni Baba Kadogo??"
swali lililomstua mama kadogo na kumfanya aanze kutia shaka,
* * * * * * *
je huyo mlangöni ni nani?


USIKOSE SEHEMU 6 IJAYO!
 
666-NYAYO ZA KUZIMU-6-

"mnasema nini??"
"sisi ni mamajusi wa kishetani!..na tumekuja kumlaki mfalme wetu!!.."
"m..m..mfa..mfalme...yu..yu..yupi!"
aliuliza Vero huku akitetemeka,
"mfalme Chernobog,Mungu mweusi!"
Vero macho yalizidi kumtoka,hofu ilichochea ndani yake,alimuangalia yule mtoto aliembeba akamuona anatabasamu!...aliporudisha macho juu,aliona wale wazee watatu tayari washaingia,aliskia moyo umepasuka ghafla....hakuvuta tena pumzi,mwishowe akapoteza fahamu.Neno CHERNOBOG lina asili ya urusi,ni mchanganyiko wa majina mawili,cherno ikimaanisha 'nyeusi' na bog imaanishayo 'mungu',kwahiyo kwa pamoja huza neno 'mungu mweusi' kama anavyoitwa mtoto yule na wale wazee.
Mtoto alichukuliwa kutoka kwenye mikono ya Vero aliepoteza fahamu,kila mzee alimbusu kwenye paji la uso na kuongea maneno fulani yaliyozid kulitunza tabasamu la yule mtoto.
Ghafla alifungua macho yake,hayakua ya binadamu wa kawaida na hata alipopanua mdomo wake,hakua na ulimi wa binadamu wa kawaida,vyote vilikua ni viungo vya nyoka,tabasamu lenye afya lilichomoza kwenye kila sura ya wale wazee,kwa pamoja wakasema..
"baruch haba chernobog..
Ooh baruch haba"
lugha ya kiebrania(Hebrew) ikimaanisha 'karibu mungu mweusi,ooh karibu!'
..Vero bado fahamu hazikumrudia,hivyo hakupata kushuhudia kilichokua kinajiri,alijiona yu ndani ya giza nene akipepesa macho huku na kule kuutafuta mwanga,akiwa katika harakati hizo mara ghafla alihisi mkono umemgusa begani,haraka aligeuza yake shingo kwa hofu kuangalia ni nani,hakuona kitu,jasho likawa linamtiririka,mwili nao ukawa unatetemeka ilihali na nywele kichwani zikawa zinasisimka,
"wewe nanii???"
sauti iliyoshiba uoga ya Vero iliskika,hakuna sauti yoyote ya kimajibu iliyorudi masikioni mwake zaidi tu ya mwangwi uliomjuza ya kwamba yu ndani ya jengo.
Aliunyanyua mguu wake na kuanza kusogea mbele akiutafuta mlango huku akipata taarifa finyu kuhusu anapokanyaga kutokana na macho yake kushindwa kupambana na giza lile kali,kila alipozidi kusogea mbele alizidi kusisimka na kuhisi hatari zaidi,mguu wake wa kulia ulio mbele ulikanyaga kitu chenye ncha kali,alipiga yowe ya maumivu uliojibiwa na mwangwi mkali uliorudi masikion mwake,nafsi yake ilizidi kushiba hofu kwani alipoangalia kilichomchoma ni nini,hakupata kukiona!..bali tu alishuhudia mguu wake ukimimina damu,hapo ndipo alipoisikia sauti,nzito ya msisitizo na yenye kuogopesha!..
"tazama nao huo ndio utawala unaokuja!..
Utawala wa kiza!...kiza!..kiza na giza!!
Utawala wa nyama na damu!!
UTAWALA WA CHERNOBOG!!!...
Ha! Ha! Ha! Ha! Ha!........."
Vero alipiga makelele ya kiuoga na ghafla alijikuta ameamka toka kwenye usingizi ule mzito!....alipotazama pembeni hakuona kitu zaidi ya kusikia sauti za nyimbo zikitokea nje,alijinyanyua kwa tabu kutokana maumivu aliyokua bado anayo,alijisogeza mpaka mlangoni na kuanza kuchungulia,macho yake yalishuhudia wazee karibia ishirini wakiwa wamevaa mavazi meupe na mekundu wakicheza na kuimba huku wakimrusha rusha yule mtoto juu juu!!..
Baada ya dakika tano lile zoezi lilikoma,sauti ya mzee mmoja aliyekua ameshikilia fimbo yenye alama ya msalaba ikasema..
"wana wa utawala wa kiza huu ni wakati wetu!!"
"amen!"
wakaitikia wale wengine huku wakiinamisha vichwa vyao,
"na tupo hapa kumlaki mfalme atakaetuöngoza mpaka pale tutakapoikamata dunia!!"
"ameen!"
"na kuanzia leo jua halitochomoza,na ni ishara ya kutokua na mipaka kwenye maamuzi!"
"Ameen!"
"ila sadaka ya mtu mmoja haitoshi kabisa kumpokea mfalme wetu,hivyo basi inahtajika nyingine ya ziada!!.."
"ameen!"
"na nendeni mashariki na magharibi,kaskazini na kusini..MKAITWAE!!!!...."
* * * * * * * *

USIKOSE SEHEMU 7 IJAYO!
 
MziziMkavu leo naona ni chipskande sijaelewa 5,6,& 7 mmmhhhhh! ila inaelekea kutisha.
 
Last edited by a moderator:
"666-NYAYO ZA KUZIMU--07.

Wale watu walitawanyika huku na huko kwenda kutafuta sadaka kwa ajili ya mapokezi ya mungu wao CHERNOBOG yani 'mungu mweusi',macho yao mekundu,miili yao ya kijivu iliyofunikwa na mavazi meupe na mekundu ilizidi kuchanja mbuga pande zote nane za dunia kwa ajili ya kuifanisha tafrija yao.

Baba Kadogo alizidi kutembea kuelekea mbele,alibakisha umbali usio mrefu sana kukamilisha safari yake aliyodhamiria,ghafla panga lilimponyoka,akainama akaliokota akaendelea na safari,baada ya hatua mbili tatu panga likamponyoka tena!
Moyo ukaguma,akapata wasiwasi kuhusu ile hali,ila hakujali sana,aliinamisha tena mgongo wake akaliokota,mara ghafla akahisi upepo umempita kwa haraka!
Mwili wake wote ukasisimka!
Ujasiri wake ukaanza kupata mashaka,moyo wake nao taratibu ukaanza kuchanganyia mbio,alihisi joto limepanda,kijasho chembamba kilimshuka,alimeza mate kisha akaendelea kutembea,haukupita tena muda mrefu panga likamponyoka kwa mara ya tatu!
Milio ya hatari ikaanza kuita kichwani mwake,nafsi yake ikamtonya ya kwamba hayuko salama,bila kuuliza mara mbilimbili wala kupoteza muda wa ziada aliinama na kuliokota ganga kisha akaanza kukimbia!!
Hakuruhusu miguu yake isimame wala kupunguza kasi,alikimbia kadiri ya uwezo wake huku akihema juu juu kwa pupa kuitafuta oksjeni,tahamaki alisikia vishindo kwa nyuma vinakuja kwa kasi!
...Baba Kadogo alieanza kuloa uoga na kujuta kwanini hakusikia ile kauli ya mkewe alizidi kuongeza mwendo!
Alikimbia kupita uwezo wa miguu yake,mwishowe kama kiroba cha viazi alidondoka puh!!...panga kule!
Kabla ya kujikusanya na kuinuka,tayari alishazungukwa na watu watatu waliopendezeshwa na mavazi meupe na mekundu!!
Sauti kali ya maumivu ya baba Kadogo iliskika kwa nguvu kutoka msituni
"aaaaaahhh!!!!!!"
kisha tena kukawa kimya,
idadi ikawa ni watu wawili waliokwenda kwa ajili ya sadaka tayari!
* * * * * * * *
mama kadogo alihisi moyo wake umelipuka ghafla!
Alikosa amani,moja kwa moja alihisi kuna jambo baya limechukua nafasi,alitoka kwenye dirisha alipokua anachungulia na kumsubiria mumewe,kiuchovu na kimawazo akaelekea kwenye kiti alipo mama Utopi ambaye bado fahamu hazikumrudia,alikaa kihuzuni huku akishika tama,
"jamani mume wangu,sijui yupo salama huko?..mbona mapigo yangu ya moyo yanaenda mbio hivi?....eh mungu saidia!"
"koh!-koh!"
ghafla kikohozi cha mama Utopi kikaskika!
Haraka mama Kadogo aligeuza yake shingo na kumtazama,
"mama Utopi!"
"ab..bee!"
"vipi mama unajiskiaje?"
"......mmm,mikono inaniuma na miguu pia..inavuta sana!"
alisema mama Utopi huku sura yake ikiakisi maumivu aliyokua nayo,
"usihofu mama,itapoa tu kwani dawa iliyoekwa kwenye hizo bandeji ni kiboko.."
"ahsanteni jamani...ahsanteni sana"
alisema mama Utopi huku akikunja kunja sura kutokana na miale ya maumivu kumpitia,
"haina shida mama,ila samahani sana kwa wale mbwa wetu waliokujeruhi.."
"wala usihofu mwanangu.."
"hivi mama ilikuaje kwani?"
"mh...mama Kadogo,tumekwisha!!"
"tumekwisha? Kivipi yani...sijaelewa!"
"kile kizazi cha nyoka alichotuambia mzee Otongo yule mganga..kimewadia!!"
"eh? Umekionea wapi??"
"mtoto va Vero!..mtoto wa Vero ndie yule....
(kabla hajamalizia alikatishwa na hodi toka mlangoni)
"ngo! Ngo! Ngo!"
"nanii?"
aliuliza mama Kadogo huku macho yakiwatoka kwa uoga,
"mimi Baba Kadogo!"
sauti toka nje iliskika,
mama kadogo alifikiria kidogo,kisha akataka kuinuka ila mama Utopi alimzuia haraka!
Kisha akamuuliza,
"una uhakika huyo ni Baba Kadogo??"
swali lililomstua mama kadogo na kumfanya aanze kutia shaka,
* * * * * * *
je huyo mlangöni ni nani?

USIKOSE SEHEMU 8 IJAYO!
 
"666-NYAYO ZA KUZIMU---08"

"mh..lakini ni sauti yake hiyo ninayoisikia?"

"haijalishi mama Kadogo...inabidi uwe makini,embu nenda kachungulie pale dirishani kuhakiki"
"nenda basi wewe"
"ah..ah si mume wako? Nenda wewe!"
walisakiziana kwa uoga,
"lakini mama utopi...mi...mi..naogopa! Au tumuamshe Kadogo aje atusaidie?"
"atusaidie nini? Kwani tunajifungua hapa?...
Jiamini mtoto wa kike,tupo wawili humu we nenda tu,mie ningeenda sema miguu inanivuta kweli!"
alitamka mama Utopi kwa ujasiri huku akifichama hisia zake za uoga,
mama Kadogo alinyanyuka na taratibu alianza kujongea kuelekea kwenye dirisha,alitizama tizama nyuma kila mara kumuangalia mama Utopi ambaye alikua anampa ishara za kujiamini na kuzidi kusogea,aliunyanyua mguu wake wa kulia kumalizia umbali uliobakia wa kulifikia dirisha,ghafla alishtushwa na hodi ya mara ya pili iliyotoa sauti kali na kuutikisa mlango!
"ngo!! Ngo!! Ngo!! Ngo!!"
aliyatoa macho na haraka aliyageuzia kwa mama Utopi alieonesha kwamba naye kashtushwa!
Alishindwa kuizuia miguu yake,alikimbia haraka kurudi alipotoka kuungana na mwenzie alieonekana naye kujawa na uoga uliomeza ule ujasiri wake wa kuigiza,
"umesikia hiyo??...mh,sasa hivi nenda wewe!"
"mimi?...kwa we ulifika?!"
"mie sijafika ndio ila nilikaribia karibia!"
"sasa kwani sie tulikubaliana kukaribia karibia ama kufika pale dirishani?"
aliuliza mama Utopi kwa sauti ya chini,
"ngo!!! Ngo!!! Ngo!!! Mama kadogo fungua!!!"
sauti tena ya kuamuru iliskika toka nje ikiambatana na mlio wa nguvu wa mlango,kwa mara hii sauti haikua tena ya Baba kadogo iliyokua mwanzoni,ilikua ni sauti nzito ya kutisha!
"mama Utopi hiyo si sauti ya mume wangu!!"
kwa mshangao uliojaa uoga alibwatuka mama Kadogo,
haraka waliinuka wakakimbilia chumbani na kuacha sebule tupu,waliingia chumba cha kwanza kabisa kilichokua karibu yao ambacho ni chumba cha Kadogo mtoto wa pekee wa mama Kadogo,hali ya kuingia kwa kukurupushana ilimfanya Kadogo astuke toka kwe usingizi,alipigwa na butwaa na kile kitendo cha kuona mama yake anajaribu kuingia chini ya uvungu wa kitanda chake,na alipogeuza shingo upande wa kushoto alishuhudia mama wa rafiki yake kipenzi mama Utopi akiwa anafanya jitihada za kuchungulia dirishani,
"mama kuna nini?"
aliuliza kadogo,hakuna aliyejibu swali lake kila mtu alionekana yu bize kufanya kile kilichoonekana kumleta lile eneo,mama Kadogo baada ya kushindwa kuingia uvunguni alikua amesimama akipepesa pepesa macho yake kushoto kulia juu na chini kuona ni wapi ambapo anaweza kujishkiza na kusahau kabisa ya kwamba mwanae bado anamuangalia kimshangao na anasubiri jibu la swali lake alilouliza,wakati hilo zoezi linachukua nafasi sauti ya mama Utopi aliekua anachungulia dirishani ilipata kuskika,
"mama kadogo,mbwa wako wote wamekufa!!"
"wamekufa? Nani kawaua?"
"sasa mie ntajuaje na wote tupo ndani?
Alafu nilivyochungulia upande wa mlangoni sijaona mtu!"
"we! Ujaona mtu?..sasa ile sauti iliyokua inabisha hodi ni ya nani?"
"hapo sasa!!..au kazunguka kwa nyuma?"
"mh mungu wangu!..mie hata sielewi,yani hapa haja zote zimenibana!"
"mie naona bora ya wewe,mwenzio hapa miguu inatetemeka na moyo unanienda mbio kweli!"
"mama kwani kuna nini??"
Kadogo alilirudia swali kwa msisitizo baada ya kuona maongezi yaliyokua pale hayaelewi,
Mama kadogo alitazamana na mama Utopi kwa muda kidogo,kisha akajibu
"lala tu baba wala usiogope.."
"mama silali mpaka uniambie kuna nini
mbona mnaonekana mnaogopa?"
"haina shida mwanangu,hakuna chochote baba eenh...wala usiogope we lala tu"
"kweli Kadogo wala usihofu hakuna kitu"
alidakia mama Utopi huku akililazimisha tabasamu kumjazisha Kadogo ujinga,
mama Kadogo alisita kumwambia ukweli mwanae kwa hofu kua unaweza kulirudisha tatizo ambalo huwa linamsumbua la mshtuko wa moyo,hivyo alijitahidi kuuzika ukweli kwa uso wa bandia na maelezo yasiyo sahihi ili aepushe jambo lingine kutokea,
wakiwa katika maongezi mafupi ya kuubadilisha ukweli katika macho na masikio ya Kadogo,ghafla walishtushwa na sauti toka nje zilizokua zinaimba!
"nao ni utawala wa giiiiza!
Nao ni utawala wa kiiiiza!
Wasio amini kuwaumiza!
Na watakaoungama kuwahimiza!
Sita! Sita! Sita!
(sauti nyingine ikidakia)
kwenye paji la uso!
Sita! Sita! Sita!
Kwa maisha!
Sita! Sita! Sita!
Tunawasilisha!
Sita! Sita! Sita!
Tunawakilisha!!"
kisha sauti ikatulia kwa muda kidogo,sauti nyingine ya mtu mmoja ikaskika..
"kama wataka jiunga na ulimwengu,
kama wataka kuishi tangu na tangu,
toka nje upewe alama ya maisha!
Toka nje na yote yatakwisha!
Ila ukibaki humo ndani utakua ni wa sadaka!!"
* * * * * * *

USIKOSE SEHEMU 09 IJAYO YA SIMULIZI HII YA KUSISIMUA!
 
"666-NYAYO ZA KUZIMU---09"

Mama Utopi baada ya kusikia hayo alidondoka chini kama mzigo,akapoteza fahamu!
Kazi ilibakia kwa mama Kadogo ambaye tayari aliishalowesha khanga yake kwa mkojo,masikini mwanae nae alikua anachungulia dirishani akiyatoa macho yake kwa kutoamini,watu waliokua pale nje na mavazi yao meupe na mekundu walioonekana hawana muda wa kupoteza,wapo serious na wanasubiri ujio wao,aligeuza macho yake kwa mama yake akauliza,
"mama hawa wakina nani?"
hakujibiwa kama alivyotarajia,mama yake alikua amezubaa na mdomo ulikua mzito kuufungua,macho yalikua yamemtoka na kichwani alikua anajaribu kujiuliza kwamba yupo ndotoni ama ni kweli?
Alishtuliwa na sauti ya mwanae Kadogo iliyouliza tena kwa mara ya pili ikiambatana na tendo la kumsukuma sukuma ili kumrudisha kwenye fahamu,
"mama hawa watu ni wakina nani?"
"njoo...njoo! Sogea haraka!!!"
alielekeza mama Kadogo,alimvuta mwanae baada ya kumkaribia kisha akamueka mgongoni,kabla ya kujitoa ndani ya chumba alimuangalia mama Utopi aliyezirai,kwa uchungu akasema
"inanibidi nifanye hivi,samahani sana"
kisha haraka alitoka ndani ya nyumba kwa kupitia mlango wa nyuma,
alikimbia sana kadiri ya uwezo unavyomruhusu kutokana na mzigo wa mtoto aliokua nao mgongoni,alikatiza mashambani kama hana akili nzuri,alikimbia na alikimbia maskini kuokoa maisha yake na ya mwanae mwenye umri wa miaka saba tu,kila alipokimbia bado aliona haitoshi hivyo alizidi kuendeleza zoezi,baada ya muda wa dakika arobaini na tano alichoka na alikua anahema kama mbwa,alimshusha mwanae na wakaanza kutembea haraka haraka wakielekea mbele wasikokufahamu kutokana na giza kali lililotawala machoni mwao,
"mama tunaelekea wapi?"
"sijui,ila twende tu"
"mama mi naogopa...ni giza sana!"
"nisikie mwanangu,hatuna la kufanya zaidi ya hili tulifanyalo sasa kama tungependa kuishi zaidi,tusogee tu mbele kwa mbele tutajua cha kufanya hukohuko"
"mama...kwani yupo wapi baba?"
"sijui yupo wapi!"
"hatujamuacha nyumbani?"
"hayupo nyumbani,aliondoka na hajarudi mpaka sasa hivi"
alijibu kiuchungu mama Kadogo,
"he! Mama ile nini?"
"wapi??"
kiuoga haraka aliuliza,
"kile kinachowaka!"
"mh nadhani ule ni moto,ila...ni nani atakua kauwasha?"
aliuliza mama Kadogo huku wakiwa wamesimama na mwanae kibutwaa,
baada ya muda kidogo walimuona mzee mmoja akitokea na kuni alizozishika mkononi kisha akazirushia kwenye ule moto,kumbukumbu za mama Kadogo zilimwambia kwamba yule ni mzee Otongo mganga wa jadi wa pale kijijini kwao na ndie yule aliyekua anawaonya juu ya ujio wa kizazi cha nyoka ambacho sasa hivi ndicho kinachoanza utawala,bila kupoteza muda alimshika mwanae mkono na kuanza kumswaga kuelekea lile eneo,
"mzee!.."
aliita mama Kadogo na kumfanya mzee Otongo ataharuki kwa kutokutegemea,
"we nani?"
"mie mama kadogo!"
"mama Kadogo? Umefikaje huku?"
"mzee tumekimbia nyumbani,lile jeshi la 666 lilituvamia!"
"yote mmeyataka nyie!!!"
"mzeee!"
"hakuna cha mzee,yote mmesababisha nyie wenyewe!...ni mara ngapi nilikua nawaambia kwamba Vero auwawe?"
"mzee sasa mimi ningewezaje?"
"unataka kuniambia kwamba kijiji chote cha Igesambo kingeshindwa kufanya hilo jambo?
Mume wako ni shujaa,na anajulikana kijiji kizima,kwanini hakufanya hivyo kuokoa maisha yetu??"
"lakini mzee wangu sidhani kama huu ni muda wa kuzozana na kulumbana,inabidi tutafute suluhisho la haya.."
"suluhisho gani unavyodhani? Kwanza una uhakika hata wa kuiona baadae hapo ulipo??!"
alifoka mzee Otongo huku mate yakirukaruka toka mdomoni,
"kwahiyo mzee Otongo tusubirie tufe tu hivihivi?"
"sina matumaini tena,mke wangu wameshambeba,watoto wangu pia watatu washachukuliwa,na Kilembo yule msaidizi wangu tayari ashapigwa chapa kwenye paji lake la uso,amekua mfuasi wao!"
"kwahiyo mzee wangu hakuna cha kufanya kabisa?"
aliuliza tena mama Kadogo kwa sura ya udadisi,
"sijui yani,sijui! Tegemeo letu lipo tu sehemu moja mama Kadogo,sehemu moja tu!"
"sehemu ipi hiyo tena mzee Otongo??.."
aliuliza,
Mzee Otongo alionekana anafikiria jambo,kisha alifungua kinywa chake kwa mjazo akasema
"kila saa naangalia angani,kila mara nanyanyua nyuso yangu kuielekeza juu kutizama na kuchunguza kama kuna tumaini lolote litakalochipukia,tumaini letu ni kuchomoza kwa nyota nyingine angani,nyota itakayoamsha matumaini yetu yaliyokufa,nyota itakayozima uoga wetu na kuangaza amani yetu.."
ghafla sauti ya kitu kilicho kwenye mwendo iligota kwenye masikio yao,walitoa macho kwa uoga,mapigo ya moyo yakaanza kuchochea kasi hasa ya Mtoto Kadogo mwenye matatizo ya moyo,walitizamana kwa macho ya viulizo na midomo iliyogoma kufunguka,joto likatotesha nguo zao,haraka wakainuka na kukimbia kwenda kujificha!
* * * * *

JE NINI KITAWAKUTA? NA HIYO SAUTI WALIOISIKIA NI YA NANI? NA HIYO NYOTA YA MATUMAINI ITACHOMOZA?
USIKOSE!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom