666-nyayo za kuzimü

666-nyayo za kuzimü

Nasomaga sana hadithi za MziziMkavu lakin sijawah kumpa like wala kucoment chochote,leo nmeona nikupe big up sana mkuu kwa hadithi zako,ziko vizur kip it up,

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mzee Patili achanganye vibuyu vyake wayachome moto kabla menzao hajashituka.
 
666-NYAYO ZA KUZIMU--34-

lile jibaba nalo likaanza kutapatapa kama samaki nchi kavu!! Macho ya wanakijiji waliokua wemejificha hayakuamini yalichokishuhudia,lile Jibaba ilikua kama mtoto kwa jinsi lilivyokua linajibaraguza na kurukaruka huku na kule kwa mitindo yote,ni dhahiri miale ya jua lililochomoza ilimuunguza kupita kiasi na alishindwa kabisa kuvumilia hilo,alitia huruma mno kwa jinsi alivyokua

akilalamika,waweza sahau mabaya yote aliyoyatenda kwa jinsi alivyokua anateseka,hatimaye mwili wake ulikua majivu kabisa na wa yule mdada pia,hakuna kilichobaki juu yao na huo ndio ukawa mwisho wao,chereko nderemo na vifijo zilitawala.

Je wanakijiji wataishi kwa amani sasa?? Ni swali lililohitaji ufumbuzi mzito.
* * * * * *
(Dar es salaam,Msasani)
mchungaji Josiah alikua amejipumzisha juu ya kitanda chake sita kwa sita akiitawanya miguu na mikono kwenye pande zote nne za kitanda,ni dhahiri huduma ya kiroho aliyoifanya jana usiku ilimchosha mno kwani japokua jua lilikua lishachomoza mwili wake bado ulionekana kutamani kitanda ambacho hakikushushiwa hata neti ya kumzuia na mbu,alijigeuza kivivu na kuendelea kuvuta makasia ya usingizi mpaka pale aliposhtushwa na mlio mkali wa simu yake ya kichina yenye muito wa nyimbo fulani ya injili ya muimbaji

maarufu nchini,macho yake yaliyotawaliwa na mang'amung'amu ya usingizi yalifunguka kwa mbali kuangalia ni nani anaepiga,alishtushwa kuona ni Askofu Emmanuel haraka aliiweka simu sikioni..

"shalom Askofu!"
"shalom Josiah...vipi unaendeleaje?"
"safi tu namshukuru mungu aisee.."
"ni kweli mungu aliejuu ashukuriwe,sasa Josiah..."
"naam Mtumishi!"
"embu fika hapa kanisani mara moja kuna kitu cha muhimu inabidi tujadiliane"
"haina shida mtumishi wa mungu,nitakuwepo hapo muda si mrefu!"
"sawa,bwana mungu awe nawe.."
"amina,awe nawe pia mtumishi.."

maongezi yakakata,mchungaji Josiah aliekua amechoka kama mbwa kutokana na shughuli pevu aliyofanya jana aliamka kwa kujivutavuta na kuelekea bafuni kupata maji,hakuweza kabisa kumbishia Askofu hivyo hakua na jinsi zaidi ya kutekeleza kile alichoambiwa na mkubwa wake ukizingatia yeye bado ni mchungaji mwanafunzi kwani si muda mrefu tangu aanze rasmi shughuli zile

za uchungaji.Ilichukua kama dakika thelathini na tano kwa mchungaji Josiah kumaliza kabisa zoezi la kujiandaa,alipanda daladala chapchap na kufika kanisani haraka tu kutokana na ukaribu uliokuwepo,alipoingia tu kanisani macho yake yaliweza kumuona

Askofu Emmanuel akiteta jambo na mtu fulani alievalia suti nyeusi,kabla hata ya yeye kufika walishamaliza maongezi yao na yule mtu akapanda gari na kuondoka,Askofu Emmanuel alimkaribisha mchungaji Josiah na moja kwa moja walielekea ofisini walipowakuta watu kama kumi wenye vialama vyeupe shingoni vilivyoashiria ya kwamba ni wachungaji,baada ya salamu za hapa na

pale majadiliano yalianza baada ya kufunguliwa na sala nzito toka kwa Askofu,kikao kile hasa kilikua kinahusu usambazwaji na uenezaji wa neno la bwana kama ilivyoagizwa,kilikua ni mahususi kwa ajili ya kujadili mikakati itakayowezesha injili kufika mahali ambapo hapajafikika,kanisa lilihitaji kufungua matawi yake zaidi ili iweze kuwafikia watu wengi zaidi waliohitaji huduma za kiroho

sehemu mbalimbali za nchi hasa vijijini,baada ya masaa mawili kikao kilikwisha kwa kumteua mchungaji Josiah asimamie shughuli ya kwenda kusambaza injili mkoani mbeya na kutia msingi wa kanisa,hakuamini kilichotokea kwani aliona ile ni kazi kubwa ambayo hakustahili apewe,haikua na jinsi,Askofu Emmanuel alimuamini na ukizingatia mchungaji mzoefu Isaya alikuwepo mkoani Arusha

kiroho,ilipangwa siku ya kufunga safari na idadi ya watu watakaokuwepo kisha mchungaji Josiah alirudi nyumbani kwake kwa ajili ya kuendelea na mapumziko.


Alipojirusha kitandani usingizi haukuja kama alivyotegemea,moja kwa moja akili yake ilianza kupitia kile alichoambiwa na kidogo kupata mawazo,ila katikati ya yale mawazo taratibu tabasamu lilichomoza usoni mwake na kuupendezesha uso wake mrefu wenye dimpoz,hakuna mwingine alieleta hilo tabasamu zaidi ya Rachel Mwakatwila mwanakwaya mahiri pale kanisani aliyewekwa kwenye

orodha ya wale waendao kutoa huduma,moyo ulilifurahia hilo,fursa adimu aliyokua anaisaka imekuja mikonomi mwake,nini nataka zaidi?? Kazi ni kwangu!! Alijiambia mchungaji Josiah.

* *
Jumatano alfajiri na mapema mchungaji Josiah,Rachel na watumishi wengine wawili walianza safari ya kuelekea mkoani mbeya kwa kutumia bus,kitendo cha mchungaji Josiah kupewa fursa ya kukata tiketi ilitumika vema kwani aliutumia ule mwanya kukata tiketi iliyomueka karibu na Rachel kitulizo chake cha moyo,safari nzima ilitawaliwa na vijistori vya hapa na pale na vicheko vya haja,Josiah alisahau kabisa cheo chake cha uchungaji mbele ya Rachel,stori zilinoga,ila mwishowe Rachel alibebwa na uchovu wa safari akamlalia mchungaji Josiah begani.

* * * * *
USIKOSE SEHEMU 35 IJAYO UPATE JUA KILICHOJIRI.
 
666-NYAYO ZA KUZIMU--35-

kila mara Josiah alipomtizama Rachel alielalia begani kwake alijihisi amani,alitamani alalie na kwenye moyo wake vilevile,hakujua cha kufanya ili aweze muingiza Rachel kwenye system ukizingatia cheo chake cha uchungaji,kuhisiwa vibaya mbele ya jamii na kunyooshewa kidole vilimtia hofu pia hisia za kukataliwa zilizidi kumtisha,alisema tu na moyo wake mkavu unaoumia.

Mwendo wa kasi wa bus ulifanya baadhi ya abiria walipuke kwa maneno wakimshutumu na kumsema dereva,makelele na malalamiko yao yalimuamsha mchungaji Josiah toka kwenye usingizi mzito wa mawazo juu ya Rachel aliokua nao,hakuchangia chochote kwani hakuna alichoshuhudia ila aliona watumishi wenzake wawili David na Rio wakijibizana na baadhi ya abiria juu ya mwendokasi wa gari,alipomtizama Rachel alikua bado amelala hivyo nae hakujua lolote linalojiri.


Baada ya muda kidogo bus lilipaki kwa ajili ya kuruhusu abiria wapate cha kutia tumboni,mchungaji Josiah alimuamsha Rachel aliekua bado amelala kisha wakaenda kupata msosi na kurudi ndani ya gari,muda si mrefu gari nalo lilijiondoa lile eneo na kuendelea na safari ya kuelekea jijini mbeya,shibe na uchovu vilimlemea mchungaji Josiah na sasa ikawa ni zamu yake

kulala,usingizi mzito uliombeba ulimpeleka mpaka kwenye ardhi ya ndoto ya ajabu isiyopata kusemeka,alijiona yupo kwenye giza zito nene na hajui pa kuelekea,miguu yake iliyokanyaga chini ilihisi baridi kali na kufanya mwili wake uitike kwa mtetemeko,moshi mzito ulimzunguka na kumfanya akohoe huku akihangaika kuitafuta pumzi kwa hali na mali ilhali moyo na akili yake vikishika kasi ya uoga,alikohoa na kukohoa,alikohoa mno mpaka kifua kikaanza kuita kwa maumivu!! Alikohoa mpaka

macho yakaanza kububujika machozi na kuhisi kichomi!! bado kikohozi hakikukoma hata kidogo,aliendelea kukohoa tena zaidi na zaidi mwishowe akaanza kukohoa damu!!! Mapigo ya moyo yalienda sawa na mbio za farasi wa mashindano,mzunguko wa kasi wa damu ulifanya baridi alilokua nalo lipotelee,joto liingie na kuruhusu vijasho kuchuruza mpaka sehemu za siri,kila alipojitahidi kuzuia kile kikohozi ule moshi ulizidi ongezeka na kumpalia hivyo kutompa machaguzi,mishipa ya uso ilimsimama

na koo nalo likaanza kuuma!! Koh!-koh!-koh!-koh!-koh! Bado alizidi kukohoa!!....mchungaji Josiah alianza kushindwa kumudu mwili wake,mkojo ulianza kumchuruza na kufanya nguo yake ya ndani kuwa tepetepe,bado kikohozi hakikukoma wala kupungua kasi!! alitia huruma na imani mno kwa jinsi alivyokua anahangaika,alishindwa kabisa kusimama kwani miguu ilikwisha nguvu hivyo akapiga magoti na kuendelea na lile zoezi la kukohoa tena sasa akihisi mkono umemkaba shingo!!! alizidi kutoa damu na

kutapatapa mpaka pale alipoisikia sauti nzito isiyojulikana imetokea wapi ikimwambia RUDI ULIPOTOKA!!!! kisha kufuatiwa na kicheko kikali cha kishetani!! Ha!-ha!-ha!-ha!-ha!-ha!-ha!

Baada ya hayo maneno mchungaji Josiah alishtuka toka kwenye usingizi huo mzito kwa pupa na kuwastua abiria wengine waliokuwepo karibu ikiwemo Rachel alie jirani.Rachel kwa tahamaki alimuuliza mchungaji...
"vipi mtumishi,kuna nini???"

mchungaji Josiah alishindwa kujibu,alionekana akihema kwa pupa huku akipepesapepesa macho kushoto na kulia kuhakikisha mazingira aliyopo,baada ya kutulia kidogo ndipo alipoanza kumuhadithia Rachel kile alichokiona kwenye ndoto,Rachel alishtushwa pia na zile habari na kumtaka mchungaji Josiah wasali ili mungu atie mkono katika safari yao,walishindwa kuwashirikisha watumishi wenzao kwani walikua usingizini,wakiwa katikati ya sala walisikia sauti kali za abiria kisha ukafuata

mlio mkali Puh!!!! presha kali iliwasukumiza mpaka mbele na kujigonga kwa nguvu!! gari liligonga!!....muda si muda gari nalo likaanza kubiringita kwa nguvu!!! Vilio vya maumivu na uoga vilitawala ndani ya gari!! Baada ya dakika kama tano gari lilitulia huku bado vilio vya baadhi ya abiria vikiskika kwa nguvu vikiomba msaada,wengi wao walikua kimya huku miili yao ikivuja damu,wengine walionekana wakilia huku wakigusa sehemu waliyodhurika au kujeruhiwa,watoto wadogo wawili wenye miaka si

juu ya mitano walionekana wakiwa wamelaliwa na gari hivyo sehemu kubwa ya miili yao ikawa imesagika,haikuhiaji utaalamu wowote,walikua wamekufa,hamaki mmama mmoja mjamzito alionekana tumbo limepasuka!! Ilitia huruma na ilisisimua kwa kutisha!! Damu iliyomwagika ilifanya nyasi zote zilizokuwepo kuwa nyekundu,lile eneo lilikua kama machinjioni!!

Huku akijikokota taratibu kutokana na maumivu mazito aliyokua anapata mchungaji Josiah alipata kuita kwa taabu.."Reeecho!!" hakuna aliyeitika,nae muda si muda alipoteza fahamu!!

*
JE NINI KITATOKEA??? Like 10 zahtajika kufanya simulizi isogee.ONE LOVE.
 
Like! Like! Like! Like! Like! Like! Like! Like! Like! Like! Story nzuri sana,asante MziziMkavu endelea kutupa mambo.
 
Last edited by a moderator:
666-NYAYO ZA KUZIMU--36-

"Reeecho!!" hakuna alieitika,nae muda si muda akapoteza fahamu!! Watu waliokaribu walianza kusogelea eneo la tukio huku wakitoa macho kwa kutoamini,wengi wao walishika vichwa na sura zao zilionekana zenye huzuni na masikitiko makubwa,dhahiri lile tukio liliteka hisia zao mno kwani macho yao hayakuwahi kushuhudia ajali mbaya kama ile.Shughuli za uokoaji zilichukua

nafasi,wakazi wa yale maeneo walionekana kujitolea mno kutoa miili ya watu iliyokwama ndani ya gari ambayo mingi ilipoteza uhai na kuharibika vibaya,ilikua ngumu kuitambua kwa urahisi kutokana na kuchakazwa na ajali,palinuka damu lile eneo na pia vilio vya baadhi ya walionusurika kufa na washuhudiaji vilevile vilitawala,ilikua ni zaidi ya msiba.


Ilichukua kama dakika hamsini na tano kwa ambulance ya hospitali kuu ya Iringa kufika eneo la tukio,udogo wa ambulance hiyo ulifanya zoezi liwe gumu hivyo wengi wao waliozidiwa walipoteza maisha ukizingatia na umbali uliokuwepo mpaka hospitalini,zoezi lile lilidumu mpaka saa mbili ya usiku ambapo ndipo taarifa ziliposambaa na kwenye vyombo vya habari juu ya ajali hiyo mbaya

kuwahi kutokea,ilimshangaza kila alieshuhudia na pia kila alieisikia,hofu kubwa ilitanda mioyoni mwa watu waliohisi eidha ndugu jamaa na marafiki walipanda lile gari kwani taarifa zilionesha kuwa ni idadi ndogo ya watu iliyopona ukilinganisha na ya waliobakia majeruhi,miongoni mwa hao watu alikua ni Askofu Emmanuel aliezipata hizo habari kwenye breaking news ya Redio moja maarufu,alichanganyikiwa mno kwani alijua fika watumishi wake walipanda lile gari,aliwajulisha wenzie na mkakati wa kuelekea

hospitali kuu ya Iringa ulipangwa ufanyike haraka iwezekanavyo kesho yake asubuhi kwa kutumia gari la Dayosisi.

Mochwari ya hospitali kuu ya Iringa ilijaa hivyo baadhi ya maiti zilifunikwa tu na kuachwa mawodini,ilikua siku bize sana kwa wauguzi wachache waliokuwepo pale,hata pia madaktari wengine ambao hawakua na zamu na walio likizo waliitwa kazini wasaidie jahazi,bado walikua wachache mno kukidhi matakwa yote.

Mchungaji Josiah bado fahamu hazikumrudia,kichwa chake kilizungukwa na bandeji nzito iliyoshiba nyeupe huku sindano ya dripu ikipenyeza dawa mwilini mwake,uso wake ulionekana umejaa kutokana na kuvujia damu hata mikono yake vilevile ilivishwa P.O.P,alikua ndani ya wodi ya wanaume sanjari na David isipokua tu Rio alieaga dunia kutokana na kupasuka fuvu la kichwa,upande wa wodi ya wanawake bibie Rachel alikua hana hali nzuri pia,mashine ya kupumulia ilijaza uso wake kutokana na mfumo wa upumuaji kushindwa kufanya kazi baada ya uvunjikaji wa mbavu,vilevile mguu wake wa kushoto ulivunjika,alitia huruma.


Wakati mchungaji Josiah akiwa bado hajarudi katika hali yake ya ufahamu alipata kuota tena kwa mara ya pili,sasa hivi alijiona amekaa na Rachel pembeni wakiteta jambo,matabasamu yaliyopendezesha nyuso zao ziliashiria ya kwamba walichokua wanaongelea kiliwakonga nyoyo,kila mtu alifurahi na dhahiri stori zilikua zinasonga vema.Ghafla Josiah alihisi ameshikwa begani na

mtu tokea nyuma,alipogeuza shingo yake kutizama ni nani aliefanya hivyo hakuona kitu na hata uso wa Rachel ulionyesha hauna habari na lile tendo,aliamua kupotezea na stori kama kawaida zikaendelea,kale kamchezo bado hakakukoma! alihisi tena mkono umemgusa begani kwa mara ya pili na alipogeuka hakuona kitu tena!! alianza kupata hofu,alipomtonya Rachel juu ya hilo alipuuzia

na kumwambia ni stress tu hizo hivyo kufanya mchungaji Josiah atulie tena ila kwa imani ndogo na hofu ya kuonekana muoga mbele ya mwanamke,baada ya dakika mbili tatu ule mchezo uliendelea!!....mchungaji Josiah alihisi mkono umemgusa tena begani,alipogeuka haraka kuangalia hakushuhudia chochote!!...akili yake ikamtonya kwamba pale si pa salama,alimuambia tena Rachel juu ya hilo na sasa wakalichukulia jambo serious,waliinuka na kuanza kujiondoa lile eneo,wakiwa njiani walihisi watu

wanaongea na kucheka nyuma yao ila kila walipotizama hawakuona chochote!!..tendo hilo lilizidi kujirudia na kuwatia uoga maradufu,mbio zilianza huku wakiwa wameshikana mikono! Kila mara waligeuka geuka nyuma kutizama kama wanafuatwa,japokua hawakuona kitu ila bado sauti za watu zilifika masikioni mwao!! kitendo hicho cha kutizama tizama nyuma mara kwa mara kulifanya Rachel ajikwae na kumpa Josiah kazi ya kumdaka,cha kushangaza Rachel alipounyanyua uso wake

ulionekana si wa Rachel yule ajulikanae,macho yalikua makubwa na meno yalitokeza nje kama mamba!!! Uso wake wa maji ya kunde ulikua mweusi kama mkaa na masikio yake yakawa marefu kama punda!!! Mungu wangu! mchungaji Josiah aliyatoa macho kwa kushangaa,bila kujiuliza mara mbili mbili alianza kukimbia kwa kasi toka pale Rachel alipo,katika hali isiyo ya kawaida Rachel aliebadilika sura alikua anamkimbilia Josiah huku akilalamika kwanini anamkimbia kwa sauti yake ileile halisi!! Ghafla mchungaji Josiah alizinduka toka ndotoni huku akipiga makelele makubwa na kustua watu waliopo mule wodini!!!

*

Hizi ndoto zina maana gani? Like 5 ili stori isogee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom