666-NYAYO ZA KUZIMU--34-
lile jibaba nalo likaanza kutapatapa kama samaki nchi kavu!! Macho ya wanakijiji waliokua wemejificha hayakuamini yalichokishuhudia,lile Jibaba ilikua kama mtoto kwa jinsi lilivyokua linajibaraguza na kurukaruka huku na kule kwa mitindo yote,ni dhahiri miale ya jua lililochomoza ilimuunguza kupita kiasi na alishindwa kabisa kuvumilia hilo,alitia huruma mno kwa jinsi alivyokua
akilalamika,waweza sahau mabaya yote aliyoyatenda kwa jinsi alivyokua anateseka,hatimaye mwili wake ulikua majivu kabisa na wa yule mdada pia,hakuna kilichobaki juu yao na huo ndio ukawa mwisho wao,chereko nderemo na vifijo zilitawala.
Je wanakijiji wataishi kwa amani sasa?? Ni swali lililohitaji ufumbuzi mzito.
* * * * * *
(Dar es salaam,Msasani)
mchungaji Josiah alikua amejipumzisha juu ya kitanda chake sita kwa sita akiitawanya miguu na mikono kwenye pande zote nne za kitanda,ni dhahiri huduma ya kiroho aliyoifanya jana usiku ilimchosha mno kwani japokua jua lilikua lishachomoza mwili wake bado ulionekana kutamani kitanda ambacho hakikushushiwa hata neti ya kumzuia na mbu,alijigeuza kivivu na kuendelea kuvuta makasia ya usingizi mpaka pale aliposhtushwa na mlio mkali wa simu yake ya kichina yenye muito wa nyimbo fulani ya injili ya muimbaji
maarufu nchini,macho yake yaliyotawaliwa na mang'amung'amu ya usingizi yalifunguka kwa mbali kuangalia ni nani anaepiga,alishtushwa kuona ni Askofu Emmanuel haraka aliiweka simu sikioni..
"shalom Askofu!"
"shalom Josiah...vipi unaendeleaje?"
"safi tu namshukuru mungu aisee.."
"ni kweli mungu aliejuu ashukuriwe,sasa Josiah..."
"naam Mtumishi!"
"embu fika hapa kanisani mara moja kuna kitu cha muhimu inabidi tujadiliane"
"haina shida mtumishi wa mungu,nitakuwepo hapo muda si mrefu!"
"sawa,bwana mungu awe nawe.."
"amina,awe nawe pia mtumishi.."
maongezi yakakata,mchungaji Josiah aliekua amechoka kama mbwa kutokana na shughuli pevu aliyofanya jana aliamka kwa kujivutavuta na kuelekea bafuni kupata maji,hakuweza kabisa kumbishia Askofu hivyo hakua na jinsi zaidi ya kutekeleza kile alichoambiwa na mkubwa wake ukizingatia yeye bado ni mchungaji mwanafunzi kwani si muda mrefu tangu aanze rasmi shughuli zile
za uchungaji.Ilichukua kama dakika thelathini na tano kwa mchungaji Josiah kumaliza kabisa zoezi la kujiandaa,alipanda daladala chapchap na kufika kanisani haraka tu kutokana na ukaribu uliokuwepo,alipoingia tu kanisani macho yake yaliweza kumuona
Askofu Emmanuel akiteta jambo na mtu fulani alievalia suti nyeusi,kabla hata ya yeye kufika walishamaliza maongezi yao na yule mtu akapanda gari na kuondoka,Askofu Emmanuel alimkaribisha mchungaji Josiah na moja kwa moja walielekea ofisini walipowakuta watu kama kumi wenye vialama vyeupe shingoni vilivyoashiria ya kwamba ni wachungaji,baada ya salamu za hapa na
pale majadiliano yalianza baada ya kufunguliwa na sala nzito toka kwa Askofu,kikao kile hasa kilikua kinahusu usambazwaji na uenezaji wa neno la bwana kama ilivyoagizwa,kilikua ni mahususi kwa ajili ya kujadili mikakati itakayowezesha injili kufika mahali ambapo hapajafikika,kanisa lilihitaji kufungua matawi yake zaidi ili iweze kuwafikia watu wengi zaidi waliohitaji huduma za kiroho
sehemu mbalimbali za nchi hasa vijijini,baada ya masaa mawili kikao kilikwisha kwa kumteua mchungaji Josiah asimamie shughuli ya kwenda kusambaza injili mkoani mbeya na kutia msingi wa kanisa,hakuamini kilichotokea kwani aliona ile ni kazi kubwa ambayo hakustahili apewe,haikua na jinsi,Askofu Emmanuel alimuamini na ukizingatia mchungaji mzoefu Isaya alikuwepo mkoani Arusha
kiroho,ilipangwa siku ya kufunga safari na idadi ya watu watakaokuwepo kisha mchungaji Josiah alirudi nyumbani kwake kwa ajili ya kuendelea na mapumziko.
Alipojirusha kitandani usingizi haukuja kama alivyotegemea,moja kwa moja akili yake ilianza kupitia kile alichoambiwa na kidogo kupata mawazo,ila katikati ya yale mawazo taratibu tabasamu lilichomoza usoni mwake na kuupendezesha uso wake mrefu wenye dimpoz,hakuna mwingine alieleta hilo tabasamu zaidi ya Rachel Mwakatwila mwanakwaya mahiri pale kanisani aliyewekwa kwenye
orodha ya wale waendao kutoa huduma,moyo ulilifurahia hilo,fursa adimu aliyokua anaisaka imekuja mikonomi mwake,nini nataka zaidi?? Kazi ni kwangu!! Alijiambia mchungaji Josiah.
* *
Jumatano alfajiri na mapema mchungaji Josiah,Rachel na watumishi wengine wawili walianza safari ya kuelekea mkoani mbeya kwa kutumia bus,kitendo cha mchungaji Josiah kupewa fursa ya kukata tiketi ilitumika vema kwani aliutumia ule mwanya kukata tiketi iliyomueka karibu na Rachel kitulizo chake cha moyo,safari nzima ilitawaliwa na vijistori vya hapa na pale na vicheko vya haja,Josiah alisahau kabisa cheo chake cha uchungaji mbele ya Rachel,stori zilinoga,ila mwishowe Rachel alibebwa na uchovu wa safari akamlalia mchungaji Josiah begani.
* * * * *
USIKOSE SEHEMU 35 IJAYO UPATE JUA KILICHOJIRI.