666-nyayo za kuzimü

666-nyayo za kuzimü

666-NYAYO ZA KUZIMU--31-

"nitume mimi!"
mzee Rama alirudia kauli yake huku akimtamzama mzee Patili machoni,macho yao yaliyokua yanatazamana yalihakisi hali ya shari,tabasamu alilokua nalo mzee Rama halikua la wema,lilificha uadui mkubwa wa wivu ndani yake na pia malengo makubwa ya kimapinduzi.

Mzee Patili aliwageukia wanakijiji huku akiwa na sura ya kufikiri akasema...

"ameamua kujitolea,siwezi nikamzuia,maombi yetu yawe nae aweze fanikisha kile tulichodhamiria."
baada ya kusema hayo maneno aliingia ndani na kuchukua fimbo fulani akamkabidhi mzee Rama kwenye mkono wa kuume kisha akamshika bega na kumpa maelekezo madogo juu ya ile fimbo,jinsi gani atakavyoitumia kumlinda,pia akamtakia safari njema.Mzee

Rama baada ya hayo maelekezo alimuaga mkewe na wanae huku akiwahaidi ya kwamba atarudi,akamfuata kijana mmoja aitwae Sadiki ambae ndie wa kwanza kumrubuni juu ya mzee Patili kisha akamuambia waende pamoja,alikubali na safari ikaanza.

Mzee Rama aliamini ya kwamba ile ni moja ya fursa adimu aliyokua anaitafuta kwa muda mrefu,japokua ni ya hatari lakini hakujali hilo,aliweka maisha yake rehani,eidha afe au afanikiwe kumpindua mzee Patili.

Safari ilitawaliwa na ukimya wa hali ya juu kutokana na kila mmoja wao kutoruhusu mdomo wake ufunguke,mwanga mwanana wa mwezi uliokuwepo uliwafanya waone wakanyagapo hivyo kutokua na hitaji la koroboi,mioyo yao ilikua inasema na mungu wao lakini ilikua ni zaidi ya hivyo kwa mzee Rama aliekua anasema na akili yake hasa juu ya nini atakachofanya afanikishe lengo.

Huku safari ikiendelea wingu zito taratibu lilianza kufunika mwezi uliokua unatoa nuru,giza totoro likaanza kuingia na kuwapa wakati mgumu wakina mzee Rama kwa kutoona walipokua wanaelekea! Sadiki aliekua ameshikwa na uoga maradufu alivunja ukimya

"..sasa mzee tutaendaje na hili giza??...si bora turudi tu!"

mzee Rama alitulia kwa muda bila kujibu,kisha kwa sauti ya msisitizo akasema...
"hatuwezi kurudi hilo sahau kabisa,tumeamua kujitolea na hii ndio maana ya kujitolea,wingu lipitalo lisikufanye ukageuza wako moyo,baada ya muda hali itarudi mahali pake"

baada ya mzee Rama kutoa hilo jibu ukimya ukarudi tena,hakuna alieongea zaidi,miguu yao ilizidi kusogea mbele taratibu kwa kukisia njia huku wakiyatoa macho yao ili yapambane na hali ile ya kiza iliyotawala,bado sadiki alikua na kinyongo moyoni lakini lile jibu alilopewa lilimfunga mdomo wake,hakua na jinsi,ilimbidi afuate kile atakachoelekezwa na ilikua ni robo saa sasa tangu waanze safari,walishakiacha kijiji chao kwa umbali wa kutosha japokua umbali wa maana bado ulikua mbele yao,walipiga konde.


Wingu jeusi taratibu lilianza kuacha mwezi uchomoze hivyo kuruhusu mwanga urejee na kuamsha matumamini ya wakina mzee Rama,waliongeza kasi sasa baada ya uhakika wa njia huku bado vinywa vyao vikiwa vimefungwa na macho yakitizama wanapoelekea,ghafla walisikia sauti za watu tokea nyuma zikiwaita!!! Mioyo yao ililipuka kwa uoga puh!! Kusikia majina katika hali kama ile ni kitu kilichowashangaza mno!! Mzunguko wa damu ukaanza kwenda kama mbio za marathoni! Shingo zao zilizowageuza nyuma hazikuwashuhudisha chochote,hawakuona kitu ila walisikia sauti!!..Miili ilitetemeka!!


"kimbiaaa Sadiikii!!" kauli hiyo ya mzee Rama ilikua kama kipenga kilichoruhusu mbio zianze,kila mmoja alikimbia kadiri ya uwezo wake huku akitizamatizama nyuma kuangalia kama wanafuatwa,umri wa mzee Rama ulikua ni kikwazo kikubwa kwani ulimfanya asiweze kukimbia kwa kasi kama Sadiki aliekua mbele yake,kila alipojitahidi kuvuta makasia ya mbio alihisi miguu inauma japokua alijitahidi kujizuia asisimame,mioyo yao ilikua inagonga kwa nguvu mno na jasho lilianza kutotesha nguo zao huku wakihema kama mbwa!! Fikra za kujutia uamuzi alioufanya zilianza kumtawala Sadiki mloe,atafanya nini sasa katikati ya ile safari?? Hakua na jinsi zaidi ya kuifungua miguu yake iokoe maisha yake.


Upepo mkali wa baridi ulimpita ghafla mzee Rama na kumfanya mwili mzima uite kwa msisimko wa ajabu!! Cha kustaajabisha ule upepo ulipomfikia Sadiki ulimbeba na kutokomea nae maporini!! Sauti yake nzito ya kuomba msaada ilifika vema kwenye masikio ya mzee Rama aliekua hana cha kufanya zaidi ya kutoa macho kwa kutoamini anachokiona,kama mchezo wa kuigiza Sadiki alipotelea kabisa..sauti yake nayo pia ikatokomea huko!!!


Mzigo wa hofu lawama na majuto ukatuama ndani ya moyo wa mzee Rama,alisimama huku mikono ikiwa kichwani,macho yakimtoka na jasho likimchuruza,alijiuliza mara mbilimbili kwanini ule upepo haukumbeba yeye akakosa jibu kabisa,hakujua ya kwamba ile fimbo iliyomkononi ndio iliyomuokoa,mkojo taratibu ulianza kutiririka katikati ya mapaja yake na kufanya nguo aliyoivaa iloe chepechepe,haraka wazo la kutaka kurudi kijijini likamjia kichwani,kwa macho ya uoga alitizama alipotokea na kuona kiza kimetawala,alipotizama na anapoelekea aliona hali ileile!! Harufu ya kifo ikaanza kugonga puani kwake,makelele ya umauti yakaanza kuita masikioni mwake!!

Je atapona na kufanikisha lengo lake???


USIKOSE SEHEMU 32 IJAYO.
 
Mh! Kazi kweli kweli MziziMkavu endelea big up!!!,hiki kitufe cha like kwanini hakipo kwenye simu?
 
Last edited by a moderator:
666-NYAYO ZA KUZIMU--32-

Harufu ya umauti ilianza kugonga puani,makelele ya kifo yalianza kugonga masikioni!! Alitembea kama hatua tano kurudi nyuma alipotokea akahisi moyo wake unamsuta,alikumbatia kile kifimbo alichokua nacho kisha akageuka tena na kuendelea na safari kama kawaida,tumbo likichemka na mwili ukitetemeka huku nguo ikiwa imelowa ndembendembe.


Nyuma ya mzee Rama hatua kama ishirini walikuwepo watu wawili wanasogea taratibu huku macho ya mmoja wao yakiwa yanang'aa mithili ya paka,mungu wangu!! Walikua ni wale mapatna wauaji,lile jibaba na yule mdada mwenye roho ya paka! Walionekana wanajadiliana jambo fulani lililoonekana kuwateka hisia,baada ya muda kidogo walinyamaza na kuendeleza zoezi lao la kumfuata mzee Rama taratibu bila

mwenyewe kusikia,masikini mzee Rama aliekua mwenyewe alikua hana hili wala lile,alikua hatambui ya kwamba bado anafuatwa na wale watu waliowaita,alikua hatambui ya kwamba nae anaundiwa mipango kabambe ya kumalizwa.

Dakika kama kumi na tano tu zilibakia ili mzee Rama aweze kuufikia mto Inguvai,miti ya midigidigi aliyotumwa ilikua inapatikana tu kwenye kingo za mto huo na si pengine popote,masikio yake yalianza kusikia sauti za maporomoko ya maji na sauti hiyo ilizidi kufika masikioni

mwake kila alipozidi kujongea,alishukuru mungu anakaribia lakini kichwa kilikua bado kizito kuchambua ya kwamba atafanikiwa kurudi kijijini au la! Hicho kitendawili alishindwa kabisa kukitegua.


Penye nia pana njia wahenga hawakukosea hata chembe kusema hivyo,nia ya mzee Rama kufanikisha lengo lake ilianza kuchomoza pale alipofanikiwa kuupata mdigidigi alioagizwa,hakutaka kuvunga muda,haraka alinyofoa matawi kadhaa,alipoona yanatosha hakuondoka kama ilivyotakiwa afanye,alianza shughuli za kutafuta mti mwingine aina ya Mtiriri tena kwa juhudi kubwa! Na hata alivyoupata aliunyofoa matawi

mengi ukilinganisha na aliyoyatoa kwenye mti wa mdigidigi,si kwa sababu miti ile ya mitiriri ni mifupi na rahisi kupatikana,hapana! Alikua ana malengo binafsi,matumaini yake ya kishenzi yalilala kwenye ule mti ambao ni sumu kubwa na mti hatari zaidi,alikua na lengo gani nao?? Je malengo yake ni kuua wanakijiji?? Hayo yote yalikua moyoni mwake binafsi,safari iliyotawaliwa na hofu ya kurudi alipotokea ikaanza rasmi taratibu huku kichwani kwake akijenga picha ya kufanikiwa.


Mzeee Ramaaaaaaa!!!! Sauti ya kike yenye nguvu ilisikika toka nyuma ikimuita! Mama yangu!! Mzee Rama alichanganyikiwa kabisa! Mara ya kwanza alipoisikia ile sauti Sadiki alibebwa,je sasa hivi kuna mwingine zaidi yake?? Hapana! Alikua ni yeye tu! Hakua na mkojo tena wa kutoka,moyo wake ulianza kudunda kwa pupa na miguu yake ya kizee ilianza kuchanganyia mbio!! Mkono wa kulia akishikilia fimbo na

matawi aliyoyakunjakunja ya mdigidigi na huku wa kushoto akibebelea majani ya mtiriri,magoti yake ya kizee yalianza kumvuta kwa maumivu,alijitahidi mno asisimame ili auokoe uhai wake lakini mwisho alishindwa,maumivu yalizidi mno na hata pumzi haikua nae tena!! Alisimama akihema kwa pupa huku sura yake ikitawaliwa vilivyo na uoga,alikodoa kutizama nyuma hakuona kitu kama kawaida!! Nafsi yake

ikamtonya kifo kimewadia,alipogeuza macho yake mbele aelekeapo uso kwa uso alikutana na yule mdada!!! Mzee Rama alifanya kosa kubwa kumtizama machoni kwani ndipo nguvu kubwa ya lile jini ilipo,alipoteza nguvu kabisa na kudondoka chini kama zigo..Fimbo kule!!


Lile jini lilimsogelea mzee Rama aliedondoka,macho yake mithili ya paka yaking'aa kama mwezi,masikio yake marefu yakichezacheza na ngozi yake ya kijivu ikitoa jasho,kiremba chekundu kilichokuwepo kichwani kilificha mapembe yake na kupunguza kidogo ubaya wake wa kutisha.Alipiga makofi mawili kwa mtindo wa mkono wa kushoto kuufuata wa kulia,ghafla mwili wa mzee Rama uliokua chini ukainuka

kimaajabu huku uso wake ukionyesha ya kua hajui kinachoendelea,yani hana fahamu,lile jini likapiga tena makofi ila ya sasa hivi yalikua ya haraka na pia kiganja cha kulia kilifuata cha kushoto,ghafla akapotelea na kua kama upepo! Kisha kwa madaha likamvaa mzee Rama!! Macho yaliyokua yamefumba yakafunguka! Mwili uliokua umelegea na kunyong'onyea ukapata nguvu ya ajabu!! Majani ya mtiriri na matawi

ya mdigidigi yaliyotawanyika chini yakaokotwa na kutiwa mkononi kisha tabasamu mwanana lililoakisi furaha ya yule jini alie ndani likajaza uso wa mzee Rama,taratibu kwa maringo yote likaanza kujongea kukitafuta kijiji cha Utowele alipo adui wao mkubwa waitajie kumtokomeza,ili kuifanya safari yake iwe ya kuvutia na kufurahisha alikua anaimba njia nzima huku akiuchezesha mwili ule wa kizee,lile jibaba linyongaji nalo ghafla likatokea na kumpa kampani mwenzie.

Je wanakijiji watapona?? Au ndio watapukutika kama mwanzoni?? Awamu hii mzee Patili ataeleweka?? Na vipi kuhusu mzee Rama na malengo binafsi??


USIKOSE SEHEMU 33 IJAYO UPATE JUA KILICHOJIRI.
 
Ila na tupate tumain mana tumain hata kiuhakisia tumain lipo kuna wingi wanafungua macho wengine kwenye ngiza so iwe ndio strng asiuwawe
 
Ayaaaaa amekata loh ila ni kweli wachungaji wanamitego mingi sana naanza kudhani huyu mch Joshua ni mtoto wa Juliana anyway fanya fanya mkuu roho zinapwita hapa

BACK TANGANYIKA
 
MziziMkavu, umemiksi mambo, hebu ianze upya sehemu ya 32, kuna mambo umeruka kutoka sehemu ya 3 ambayo yanafanya mtiririko wa hadithi usiewe mzuri
 
Last edited by a moderator:
666-NYAYO ZA KUZIMU--33

Safari ilikua kabambe mno,walicheza na kuimba bila woga wowote kwani walishafahamu ya kwamba muda si mrefu watakamilisha kile walichoagizwa,kazi ilikua kwa wanakijiji waliokua wanasubiria dawa ingali wanaletewa kifo!! 'ya nini uepuke chumvi ingali jirani ni bahari?' huo msemo ni dhahiri ulikua unaendana na tukio halisi kwani wanakijiji walionekana wakisumbuka

kweli kukwepa kifo bila kufahamu kwamba kilikua pembeni (jirani).Zilibakia dakika chache tu kuingiza miguu kwenye kijiji cha Utowele,lile jibaba linyongaji lilipotelea kusikoju likana na kumuacha yule bimdada aliekua ndani ya mwili wa mzee Rama aendelee na safari,mkono wake wa kushoto alioshikilia baadhi ya majani ya mtiriri sumu aliusogeza karibu na macho

yake,alichezesha kope zake kwa muda tu na ghafla yale majani yalibadilika na kua ya mdigidigi!! Kwa madaha aliyachanganya na yale ya mdigidigi halisi yaliyokuwepo mkono wa kuume,kama kawaida tabasamu likachomoza usoni mwake na kwa maringo akamalizia kaumbali kalikobaki.


Wanakijiji waliokua wamejikunyata kwa hofu na ukimya ukiwa miongoni mwao walilipuka kwa furaha baada ya kumuona mzee Rama,ilikua ngumu mno kuamini macho yao hasa familia yake!! Kusema ukweli ni asilimia ndogo iliyokuwepo mioyoni mwao iliyokua ikishuhudia kufanikiwa kwake,walimlaki kwa furaha huku wakimbeba na kumrusharusha mithili ya mtoto! Nyimbo za

kishujaa zikipamba tukio na wakisahau kabisa kuuliza yu wapi alieenda nae(sadiki).Mzee Patili,mama kadogo na mzee Otongo walikuwepo ndani wakifanya shughuli ya upakaji dawa,walitoka nje baada ya kusikia makelele ya wanakijiji,ilikua ngumu pia kwao kuamini macho yao pale yalipomshuhudia mzee Rama aliekua anarushwa na wanakijiji,muda mfupi tu baada ya wakina mzee Patili kutoka ndani wanakijiji walimshusha mzee Rama ili apate fursa ya kuwasilisha kile alichoagizwa,mzee Rama nae

hakufanya ajizi,taratibu alianza kujongea huku akishikilia yale majani akielekea walipo wakina mzee Patili,mzee Patili aligundua jambo la tofauti haraka akauliza..

"sadiki yupo wapi??"
"ameuwawa!!"
kifupi alijibu jini lile lililojivika mwili wa mzee Rama na kuwashtua wanakijiji,bado mzee Patili alitia wasi,akauliza tena
"fimbo niliyokukabidhi ipo wapi??"

lile jini lilijing'atang'ata kutoa maelezo yaliyonyooka hali iliyoanza kumpa mashaka mzee Patili na hata pia wakina mama Kadogo,mzee Patili hakutaka kuuliza swali lingine,alimshukuru mzee Rama kwa niaba ya wanakijiji na kumtakia baraka toka kwa mungu kisha aliingia na yale majani ndani na kumuacha mzee Rama akiwa amesimama pale nje karibia na mlango.


Udhaifu mkubwa wa yule jini kwenye mioyo ya binadamu ulianza kujionyesha,harufu ya binadamu iliyokua inagusa pua yake ilianza kumpa hamu kubwa na kuruhusu mate kuchuruza!! Mama Kadogo aliekua pembeni hofu ilianza kumteka akamshtua mzee Otongo ashuhudie lile jambo,si mate tu! Hata macho yake yalianza kubadilika badilika!! Kutokana na kuwapa mgongo

wanakijiji hakuna alieshuhudia hayo zaidi ya mzee Otongo na mama Kadogo,tamaa ya kula mioyo ilizidi kumtawala kichwa kumpelekesha na kumsahaulisha kusubiria malengo yake yatimie,taratibu lilianza kusogeza miguu yake na kuelekea ndani alipo mzee Patili!!!

Mama Kadogo alishindwa kunyamazia hilo akapayuka kwa nguvu..
"mzee Patili huyo anaaakujaaaa!!!!"

huku akinyooshea kidole na macho yakimtoka,sauti ile kali ya tahadhari iliwastua mno wanakijiji ilihali na mtu lengwa ambae ni mzee Patili,haraka mzee Patili aliuvuta mkono wake uliokuwepo ndani ya mfuko fulani mweusi na kumrushia unga wa kahawia lile jini usoni!! Sauti kali mno ya kulalamika mithili ya paka ilisikika toka kwenye kinywa cha yule jini!! Alijibamiza huku na huko na

kuhangaika mno huku akifikicha fikicha macho yake yaliyopokea ile dawa!!! Ilikua ni kama ndoto kwa wanakijiji waliokua wanashuhudia lile jambo kwa macho na mioyo ya hofu,walishuhudia mwili wa mzee Rama ukipotea na kuwa wa lile jini halisi!! Kiremba chake kinachoficha mapembe yake kiliruka huko na kuruhusu pembe zake mbili mithili ya mbuzi na chapa yake ya 666

kuonekana!!! Liliangaika mno huku likilia kila aina ya mlio,macho yake yaliyoingia dawa yalianza kufuka moshi ulioashiria ya kwamba nguvu yake inateketea na taratibu lilidondoka chini na kutulizana!!!

Wanakijiji wakiwa bado wameshikwa na mshangao na wasijue la kufanya walisikia sauti nzito isiyoeleweka ilalalamikayo inasogelea lile eneo!!!.....loh!! Walipogeuza macho yao kushoto walimuona lile jibaba linyongaji likija kwa kasi ya ajabu na

kamba yake mkononi!!!

Macho yakimtoka na sura ikiakisi ghadhabu kubwa aliyokua nayo!! Kabla hata halijafanya chochote kwa nakijiji walioanza kukimbia huku na kule kuokoa maisha yao jua lilianza kuchomoza!!! Mwili wake mkubwa mithili ya tembo ulianza kufuka moshi kama sigara kali!!! Nalo likaanza kutapatapa kama samaki nchi kavu!

* *
USIKOSE SEHEMU IJAYO,NYAYO ZA KUZIMU jaribio la pili 'mwanga wa giza' sehemu ya 34.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom