KARIA
JF-Expert Member
- Jan 15, 2011
- 717
- 473
666-NYAYO ZA KUZIMU--35-
kila mara Josiah alipomtizama Rachel alielalia begani kwake alijihisi amani,alitamani alalie na kwenye moyo wake vilevile,hakujua cha kufanya ili aweze muingiza Rachel kwenye system ukizingatia cheo chake cha uchungaji,kuhisiwa vibaya mbele ya jamii na kunyooshewa kidole vilimtia hofu pia hisia za kukataliwa zilizidi kumtisha,alisema tu na moyo wake mkavu unaoumia.
Mwendo wa kasi wa bus ulifanya baadhi ya abiria walipuke kwa maneno wakimshutumu na kumsema dereva,makelele na malalamiko yao yalimuamsha mchungaji Josiah toka kwenye usingizi mzito wa mawazo juu ya Rachel aliokua nao,hakuchangia chochote kwani hakuna alichoshuhudia ila aliona watumishi wenzake wawili David na Rio wakijibizana na baadhi ya abiria juu ya mwendokasi wa gari,alipomtizama Rachel alikua bado amelala hivyo nae hakujua lolote linalojiri.
Baada ya muda kidogo bus lilipaki kwa ajili ya kuruhusu abiria wapate cha kutia tumboni,mchungaji Josiah alimuamsha Rachel aliekua bado amelala kisha wakaenda kupata msosi na kurudi ndani ya gari,muda si mrefu gari nalo lilijiondoa lile eneo na kuendelea na safari ya kuelekea jijini mbeya,shibe na uchovu vilimlemea mchungaji Josiah na sasa ikawa ni zamu yake
kulala,usingizi mzito uliombeba ulimpeleka mpaka kwenye ardhi ya ndoto ya ajabu isiyopata kusemeka,alijiona yupo kwenye giza zito nene na hajui pa kuelekea,miguu yake iliyokanyaga chini ilihisi baridi kali na kufanya mwili wake uitike kwa mtetemeko,moshi mzito ulimzunguka na kumfanya akohoe huku akihangaika kuitafuta pumzi kwa hali na mali ilhali moyo na akili yake vikishika kasi ya uoga,alikohoa na kukohoa,alikohoa mno mpaka kifua kikaanza kuita kwa maumivu!! Alikohoa mpaka
macho yakaanza kububujika machozi na kuhisi kichomi!! bado kikohozi hakikukoma hata kidogo,aliendelea kukohoa tena zaidi na zaidi mwishowe akaanza kukohoa damu!!! Mapigo ya moyo yalienda sawa na mbio za farasi wa mashindano,mzunguko wa kasi wa damu ulifanya baridi alilokua nalo lipotelee,joto liingie na kuruhusu vijasho kuchuruza mpaka sehemu za siri,kila alipojitahidi kuzuia kile kikohozi ule moshi ulizidi ongezeka na kumpalia hivyo kutompa machaguzi,mishipa ya uso ilimsimama
na koo nalo likaanza kuuma!! Koh!-koh!-koh!-koh!-koh! Bado alizidi kukohoa!!....mchungaji Josiah alianza kushindwa kumudu mwili wake,mkojo ulianza kumchuruza na kufanya nguo yake ya ndani kuwa tepetepe,bado kikohozi hakikukoma wala kupungua kasi!! alitia huruma na imani mno kwa jinsi alivyokua anahangaika,alishindwa kabisa kusimama kwani miguu ilikwisha nguvu hivyo akapiga magoti na kuendelea na lile zoezi la kukohoa tena sasa akihisi mkono umemkaba shingo!!! alizidi kutoa damu na
kutapatapa mpaka pale alipoisikia sauti nzito isiyojulikana imetokea wapi ikimwambia RUDI ULIPOTOKA!!!! kisha kufuatiwa na kicheko kikali cha kishetani!! Ha!-ha!-ha!-ha!-ha!-ha!-ha!
Baada ya hayo maneno mchungaji Josiah alishtuka toka kwenye usingizi huo mzito kwa pupa na kuwastua abiria wengine waliokuwepo karibu ikiwemo Rachel alie jirani.Rachel kwa tahamaki alimuuliza mchungaji...
"vipi mtumishi,kuna nini???"
mchungaji Josiah alishindwa kujibu,alionekana akihema kwa pupa huku akipepesapepesa macho kushoto na kulia kuhakikisha mazingira aliyopo,baada ya kutulia kidogo ndipo alipoanza kumuhadithia Rachel kile alichokiona kwenye ndoto,Rachel alishtushwa pia na zile habari na kumtaka mchungaji Josiah wasali ili mungu atie mkono katika safari yao,walishindwa kuwashirikisha watumishi wenzao kwani walikua usingizini,wakiwa katikati ya sala walisikia sauti kali za abiria kisha ukafuata
mlio mkali Puh!!!! presha kali iliwasukumiza mpaka mbele na kujigonga kwa nguvu!! gari liligonga!!....muda si muda gari nalo likaanza kubiringita kwa nguvu!!! Vilio vya maumivu na uoga vilitawala ndani ya gari!! Baada ya dakika kama tano gari lilitulia huku bado vilio vya baadhi ya abiria vikiskika kwa nguvu vikiomba msaada,wengi wao walikua kimya huku miili yao ikivuja damu,wengine walionekana wakilia huku wakigusa sehemu waliyodhurika au kujeruhiwa,watoto wadogo wawili wenye miaka si
juu ya mitano walionekana wakiwa wamelaliwa na gari hivyo sehemu kubwa ya miili yao ikawa imesagika,haikuhiaji utaalamu wowote,walikua wamekufa,hamaki mmama mmoja mjamzito alionekana tumbo limepasuka!! Ilitia huruma na ilisisimua kwa kutisha!! Damu iliyomwagika ilifanya nyasi zote zilizokuwepo kuwa nyekundu,lile eneo lilikua kama machinjioni!!
Huku akijikokota taratibu kutokana na maumivu mazito aliyokua anapata mchungaji Josiah alipata kuita kwa taabu.."Reeecho!!" hakuna aliyeitika,nae muda si muda alipoteza fahamu!!
*
JE NINI KITATOKEA??? Like 10 zahtajika kufanya simulizi isogee.ONE LOVE.
Nimeipenda.