666-nyayo za kuzimü

666-nyayo za kuzimü

666-NYAYO ZA KUZIMU--35-

kila mara Josiah alipomtizama Rachel alielalia begani kwake alijihisi amani,alitamani alalie na kwenye moyo wake vilevile,hakujua cha kufanya ili aweze muingiza Rachel kwenye system ukizingatia cheo chake cha uchungaji,kuhisiwa vibaya mbele ya jamii na kunyooshewa kidole vilimtia hofu pia hisia za kukataliwa zilizidi kumtisha,alisema tu na moyo wake mkavu unaoumia.

Mwendo wa kasi wa bus ulifanya baadhi ya abiria walipuke kwa maneno wakimshutumu na kumsema dereva,makelele na malalamiko yao yalimuamsha mchungaji Josiah toka kwenye usingizi mzito wa mawazo juu ya Rachel aliokua nao,hakuchangia chochote kwani hakuna alichoshuhudia ila aliona watumishi wenzake wawili David na Rio wakijibizana na baadhi ya abiria juu ya mwendokasi wa gari,alipomtizama Rachel alikua bado amelala hivyo nae hakujua lolote linalojiri.


Baada ya muda kidogo bus lilipaki kwa ajili ya kuruhusu abiria wapate cha kutia tumboni,mchungaji Josiah alimuamsha Rachel aliekua bado amelala kisha wakaenda kupata msosi na kurudi ndani ya gari,muda si mrefu gari nalo lilijiondoa lile eneo na kuendelea na safari ya kuelekea jijini mbeya,shibe na uchovu vilimlemea mchungaji Josiah na sasa ikawa ni zamu yake

kulala,usingizi mzito uliombeba ulimpeleka mpaka kwenye ardhi ya ndoto ya ajabu isiyopata kusemeka,alijiona yupo kwenye giza zito nene na hajui pa kuelekea,miguu yake iliyokanyaga chini ilihisi baridi kali na kufanya mwili wake uitike kwa mtetemeko,moshi mzito ulimzunguka na kumfanya akohoe huku akihangaika kuitafuta pumzi kwa hali na mali ilhali moyo na akili yake vikishika kasi ya uoga,alikohoa na kukohoa,alikohoa mno mpaka kifua kikaanza kuita kwa maumivu!! Alikohoa mpaka

macho yakaanza kububujika machozi na kuhisi kichomi!! bado kikohozi hakikukoma hata kidogo,aliendelea kukohoa tena zaidi na zaidi mwishowe akaanza kukohoa damu!!! Mapigo ya moyo yalienda sawa na mbio za farasi wa mashindano,mzunguko wa kasi wa damu ulifanya baridi alilokua nalo lipotelee,joto liingie na kuruhusu vijasho kuchuruza mpaka sehemu za siri,kila alipojitahidi kuzuia kile kikohozi ule moshi ulizidi ongezeka na kumpalia hivyo kutompa machaguzi,mishipa ya uso ilimsimama

na koo nalo likaanza kuuma!! Koh!-koh!-koh!-koh!-koh! Bado alizidi kukohoa!!....mchungaji Josiah alianza kushindwa kumudu mwili wake,mkojo ulianza kumchuruza na kufanya nguo yake ya ndani kuwa tepetepe,bado kikohozi hakikukoma wala kupungua kasi!! alitia huruma na imani mno kwa jinsi alivyokua anahangaika,alishindwa kabisa kusimama kwani miguu ilikwisha nguvu hivyo akapiga magoti na kuendelea na lile zoezi la kukohoa tena sasa akihisi mkono umemkaba shingo!!! alizidi kutoa damu na

kutapatapa mpaka pale alipoisikia sauti nzito isiyojulikana imetokea wapi ikimwambia RUDI ULIPOTOKA!!!! kisha kufuatiwa na kicheko kikali cha kishetani!! Ha!-ha!-ha!-ha!-ha!-ha!-ha!

Baada ya hayo maneno mchungaji Josiah alishtuka toka kwenye usingizi huo mzito kwa pupa na kuwastua abiria wengine waliokuwepo karibu ikiwemo Rachel alie jirani.Rachel kwa tahamaki alimuuliza mchungaji...
"vipi mtumishi,kuna nini???"

mchungaji Josiah alishindwa kujibu,alionekana akihema kwa pupa huku akipepesapepesa macho kushoto na kulia kuhakikisha mazingira aliyopo,baada ya kutulia kidogo ndipo alipoanza kumuhadithia Rachel kile alichokiona kwenye ndoto,Rachel alishtushwa pia na zile habari na kumtaka mchungaji Josiah wasali ili mungu atie mkono katika safari yao,walishindwa kuwashirikisha watumishi wenzao kwani walikua usingizini,wakiwa katikati ya sala walisikia sauti kali za abiria kisha ukafuata

mlio mkali Puh!!!! presha kali iliwasukumiza mpaka mbele na kujigonga kwa nguvu!! gari liligonga!!....muda si muda gari nalo likaanza kubiringita kwa nguvu!!! Vilio vya maumivu na uoga vilitawala ndani ya gari!! Baada ya dakika kama tano gari lilitulia huku bado vilio vya baadhi ya abiria vikiskika kwa nguvu vikiomba msaada,wengi wao walikua kimya huku miili yao ikivuja damu,wengine walionekana wakilia huku wakigusa sehemu waliyodhurika au kujeruhiwa,watoto wadogo wawili wenye miaka si

juu ya mitano walionekana wakiwa wamelaliwa na gari hivyo sehemu kubwa ya miili yao ikawa imesagika,haikuhiaji utaalamu wowote,walikua wamekufa,hamaki mmama mmoja mjamzito alionekana tumbo limepasuka!! Ilitia huruma na ilisisimua kwa kutisha!! Damu iliyomwagika ilifanya nyasi zote zilizokuwepo kuwa nyekundu,lile eneo lilikua kama machinjioni!!

Huku akijikokota taratibu kutokana na maumivu mazito aliyokua anapata mchungaji Josiah alipata kuita kwa taabu.."Reeecho!!" hakuna aliyeitika,nae muda si muda alipoteza fahamu!!

*
JE NINI KITATOKEA??? Like 10 zahtajika kufanya simulizi isogee.ONE LOVE.

Nimeipenda.
 
Like! Like! Like! Like! Like! Hizo ni za kianologia,digitali sina,duh! Maskini Pastor Josiah!!!
 
666-NYAYO ZA KUZIMU--37-

ilibidi muuguzi aje haraka kumjulia hali,Josiah alionekana akigugumia kutokana na maumivu makali aliyokumbana nayo,kichwa chake kilichofungwa bandeji kililemewa na maumivu vilevile mkono uliofungwa P.O.P ulimvuta bila kusahau uti wa mgongo,alitulia kitandani kama alivyoelekezwa na muuguzi ya kwamba anahitaji mapumziko,ila

kabla ya muuguzi kuondoka Josiah aliomba jambo fulani lililodhihirisha ya kwamba fahamu zimerudi mahala pake,huku akivumilia maumivu aliyokua anayapata alimwambia yule muuguzi akamuangalizie mwenzie ambae ni

Rachel huku akiambatanisha na maelezo ya mtindo wake wa nywele alionao na nguo aliyovaa,bila kinyongo yule muuguzi alilipokea lile ombi,alimtaka Josiaha apumzike wakati yeye akienda kulitekeleza hilo,roho ya Josiah sasa ikawa imetulia huku ikisubiria taarifa kwa hamu kubwa isiyoelezeka.

* *
Mwanga uliochipukia baada ya wale viumbe wauwaji kufa iliwawezesha wanakijiji kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo ujenzi,nyumba za wakina Madhifa zilijengwa kwa ushirikiano mkubwa wa wanakijiji,nyumba ya mzee Patili vilevile.Ilikua ni saa tatu ya usiku hivyo mwanga ulishamezwa na giza,kila mwanakijiji alikuwemo ndani ya kiota

chake akiendelea na shughuli mbalimbali hivyo kufanya huko nje kua kimya! hakuna kilichoendelea huko nje zaidi ya upepo wa taratibu kutikisa matawi ya miti na kutengeneza sauti fulani,milio ya bundi nayo ilipamba tukio.

Julina alikua ndani kwake akimnyonyesha mwanae wa pekee aliebeba tumaini la watu huku akimchezeachezea

mashavu na kumfanya mtoto atoe tabasamu la kupendeza,furaha ya mtoto ni furaha ya mama hilo lilionekana kwani kila mwanae alipotabasamu nae alishindwa kulizuia la kwake,alisahau kabisa upweke aliokua nao kwa kutokuwepo mume wake,kila alipotizama sura ya mwanae mwenye afya alipata amani na furaha moyoni kwani ndicho kitu pekee alichokua nacho kwa sasa,furaha yake iliingia dosari pale tu masikio yake yalipoisikia hodi

tokea mlangoni,asili yake ya uoga ilimfanya achungulie dirishani kuhakiki ni nani,alipogundua ni mama Halima alimfungulia mlango hasa ukizingatia ujenzi uliofanyika mchana ulifanya nyumba yake iwe katikati ya nyumba za wanakijiji hivyo hofu kuwa adimu kwake,vijistori vya hapa na pale viliendelea kati ya Julina na mama yake wa hiari

mama Halima,baada ya muda kidogo Julina alimkabidhi mama Halima mtoto wake ili aweze mpakulia japo chakula atie sunna,ilikua ni kosa kubwa!! Mama Halima hakua mama Halima aliedhaniwa,mama Halima halisi alikua yu nyumbani kwake akipika chakula,baada tu ya mama Halima yule feki kupewa yule mtoto alijiinua taratibu

huku akizuga kumbembelezabembeleza na kumuimbia nyimbo za kikabila mtoto alieonekana kumkataa kabisa kwa kulia kwa sauti kubwa huku akirusharusha mikono,hali ile ilimshangaza kidogo Julina kwani mwanae hana tabia hiyo ukizingatia huwa anatulia tuli akibebwa na mama Halima,hakulichukulia kwa uzito hilo jambo hivyo

aliendelea kupakua wali kwa ajili ya mama Halima,alipomgeuzia mgongo tu yule mama Halima feki aliutumia ule mwanya kuufungua mlango taratibu huku akinyata na kutoka nje na mtoto!!! Julina alihisi sauti ya mtoto wake anaelia imefifia hivyo aligeuza haraka shingo yake kutizama,moyo wake ulikita puh!!! Hakumuona mwanae na masikio yake yalizidi kusikia sauti ya mwanae inazidi kufifia!! haraka alitoka nje huku akipiga makelele ya nguvu

yaliowashtua wanakijiji!! makelele yake na ya mwanae aliekua anakimbizwa na yule mmama yalitosha kabisa kuwatoa wanakijiji nje ya nyumba zao, haraka habari zilisambaa na haraka wanaume walianza kumkimbiza yule mama aliekua amemshikilia mtoto huku akiwa na sura ya mama Halima!! mikono yao ilishika silaha mbalimbali za

jadi tayari kwa ajili ya kupambana kumuokoa mtoto alie tegemeo kwao!! wanakijiji waliobakia walishikwa na simanzi kubwa,walimshirikisha mungu wao kwenye sala awasaidie lolote baya lisije likajiri kwani ni dhahiri walifahamu ya kua endapo yule mtoto akipotea basi hawana budi,watakua chini ya utawala wa CHERNOBOG,yani mungu mweusi! Nini kitakachojiri? Jasho jembamba la hofu lilitirika!

*
Baada ya mchungaji Josiah kurudishiwa majibu kwamba Rachel yu hai moyo wake ulijawa na furaha,alimuona pia David pembeni yake hivyo hofu yake ikawa ni kwa Rio ambae hakumtia machoni,saa nne usiku juu ya alama ikawadia.

Wodi ilikua kimya mno,macho ya mchungaji Josiah hayakua na usingizi hata kidogo kutokana na kulala mno ndani ya basi hivyo yalikua tu yakipepesapepesa vitanda mbalimbali vilivyopo,baada ya muda kidogo Josiah alitekwa na mawazo mazito,mawazo hasa juu ya ndotoa alizoziota ile siku,alitafakari sana lakini hakupata jibu la ndoto hata

moja hivyo akakosa amani.Huku bado akili yake ikiwa inabarizi ndani ya kisiwa cha mawazo alihisi mlango wa wodi unafunguliwa! Ukimya uliokuwepo ulifanya sauti ya mlango kufika vizuri masikioni mwake,haraka alirushia macho kwenye ule mlango!!

*
Je nini hiko?? Usikose sehemu ijayo,like 5 zitafanya simulizi isogee.ONE LOVE.
 
Naipenda sio tu kwakuwa ni nzuri..la hasha!! hili ni bonge la story lenye ujumbe mzito sana..tafakarini mara mbilimbili jamani...much respect mzizi mkavu
 
666-NYAYO ZA KUZIMU--37-

ilibidi muuguzi aje haraka kumjulia hali,Josiah alionekana akigugumia kutokana na maumivu makali aliyokumbana nayo,kichwa chake kilichofungwa bandeji kililemewa na maumivu vilevile mkono uliofungwa P.O.P ulimvuta bila kusahau uti wa mgongo,alitulia kitandani kama alivyoelekezwa na muuguzi ya kwamba anahitaji mapumziko,ila

kabla ya muuguzi kuondoka Josiah aliomba jambo fulani lililodhihirisha ya kwamba fahamu zimerudi mahala pake,huku akivumilia maumivu aliyokua anayapata alimwambia yule muuguzi akamuangalizie mwenzie ambae ni

Rachel huku akiambatanisha na maelezo ya mtindo wake wa nywele alionao na nguo aliyovaa,bila kinyongo yule muuguzi alilipokea lile ombi,alimtaka Josiaha apumzike wakati yeye akienda kulitekeleza hilo,roho ya Josiah sasa ikawa imetulia huku ikisubiria taarifa kwa hamu kubwa isiyoelezeka.

* *
Mwanga uliochipukia baada ya wale viumbe wauwaji kufa iliwawezesha wanakijiji kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo ujenzi,nyumba za wakina Madhifa zilijengwa kwa ushirikiano mkubwa wa wanakijiji,nyumba ya mzee Patili vilevile.Ilikua ni saa tatu ya usiku hivyo mwanga ulishamezwa na giza,kila mwanakijiji alikuwemo ndani ya kiota

chake akiendelea na shughuli mbalimbali hivyo kufanya huko nje kua kimya! hakuna kilichoendelea huko nje zaidi ya upepo wa taratibu kutikisa matawi ya miti na kutengeneza sauti fulani,milio ya bundi nayo ilipamba tukio.

Julina alikua ndani kwake akimnyonyesha mwanae wa pekee aliebeba tumaini la watu huku akimchezeachezea

mashavu na kumfanya mtoto atoe tabasamu la kupendeza,furaha ya mtoto ni furaha ya mama hilo lilionekana kwani kila mwanae alipotabasamu nae alishindwa kulizuia la kwake,alisahau kabisa upweke aliokua nao kwa kutokuwepo mume wake,kila alipotizama sura ya mwanae mwenye afya alipata amani na furaha moyoni kwani ndicho kitu pekee alichokua nacho kwa sasa,furaha yake iliingia dosari pale tu masikio yake yalipoisikia hodi

tokea mlangoni,asili yake ya uoga ilimfanya achungulie dirishani kuhakiki ni nani,alipogundua ni mama Halima alimfungulia mlango hasa ukizingatia ujenzi uliofanyika mchana ulifanya nyumba yake iwe katikati ya nyumba za wanakijiji hivyo hofu kuwa adimu kwake,vijistori vya hapa na pale viliendelea kati ya Julina na mama yake wa hiari

mama Halima,baada ya muda kidogo Julina alimkabidhi mama Halima mtoto wake ili aweze mpakulia japo chakula atie sunna,ilikua ni kosa kubwa!! Mama Halima hakua mama Halima aliedhaniwa,mama Halima halisi alikua yu nyumbani kwake akipika chakula,baada tu ya mama Halima yule feki kupewa yule mtoto alijiinua taratibu

huku akizuga kumbembelezabembeleza na kumuimbia nyimbo za kikabila mtoto alieonekana kumkataa kabisa kwa kulia kwa sauti kubwa huku akirusharusha mikono,hali ile ilimshangaza kidogo Julina kwani mwanae hana tabia hiyo ukizingatia huwa anatulia tuli akibebwa na mama Halima,hakulichukulia kwa uzito hilo jambo hivyo

aliendelea kupakua wali kwa ajili ya mama Halima,alipomgeuzia mgongo tu yule mama Halima feki aliutumia ule mwanya kuufungua mlango taratibu huku akinyata na kutoka nje na mtoto!!! Julina alihisi sauti ya mtoto wake anaelia imefifia hivyo aligeuza haraka shingo yake kutizama,moyo wake ulikita puh!!! Hakumuona mwanae na masikio yake yalizidi kusikia sauti ya mwanae inazidi kufifia!! haraka alitoka nje huku akipiga makelele ya nguvu

yaliowashtua wanakijiji!! makelele yake na ya mwanae aliekua anakimbizwa na yule mmama yalitosha kabisa kuwatoa wanakijiji nje ya nyumba zao, haraka habari zilisambaa na haraka wanaume walianza kumkimbiza yule mama aliekua amemshikilia mtoto huku akiwa na sura ya mama Halima!! mikono yao ilishika silaha mbalimbali za

jadi tayari kwa ajili ya kupambana kumuokoa mtoto alie tegemeo kwao!! wanakijiji waliobakia walishikwa na simanzi kubwa,walimshirikisha mungu wao kwenye sala awasaidie lolote baya lisije likajiri kwani ni dhahiri walifahamu ya kua endapo yule mtoto akipotea basi hawana budi,watakua chini ya utawala wa CHERNOBOG,yani mungu mweusi! Nini kitakachojiri? Jasho jembamba la hofu lilitirika!

*
Baada ya mchungaji Josiah kurudishiwa majibu kwamba Rachel yu hai moyo wake ulijawa na furaha,alimuona pia David pembeni yake hivyo hofu yake ikawa ni kwa Rio ambae hakumtia machoni,saa nne usiku juu ya alama ikawadia.

Wodi ilikua kimya mno,macho ya mchungaji Josiah hayakua na usingizi hata kidogo kutokana na kulala mno ndani ya basi hivyo yalikua tu yakipepesapepesa vitanda mbalimbali vilivyopo,baada ya muda kidogo Josiah alitekwa na mawazo mazito,mawazo hasa juu ya ndotoa alizoziota ile siku,alitafakari sana lakini hakupata jibu la ndoto hata

moja hivyo akakosa amani.Huku bado akili yake ikiwa inabarizi ndani ya kisiwa cha mawazo alihisi mlango wa wodi unafunguliwa! Ukimya uliokuwepo ulifanya sauti ya mlango kufika vizuri masikioni mwake,haraka alirushia macho kwenye ule mlango!!

*
Je nini hiko?? Usikose sehemu ijayo,like 5 zitafanya simulizi isogee.ONE LOVE.

Like like like like like like like ×283748836×5+719927366382816263723728628638273829273737×3672727272818
 
666-NYAYO ZA KUZIMU--38

Baada ya mlango ule kufunguliwa hakuna mtu aliyeingia,ulikua unaenda tu mbele na kurudi nyuma ukisindikizwa na sauti za malalamiko,moyo wa mchungaji Josiah ulitokota kama maji mafigani na alipotizama ni nani mwingine anashuhudia hakuona mtu! Wote walikua wamelala na wengine walikua washakufa,alimeza mate,sala fupi ya kuwa salama ilifuata kimoyonimoyoni.Kila alipojitahidi kupotezea lile swala alishindwa! Aliuona usiku ni mrefu,kuinuka na kwenda kuangalia pia alishindwa kutokana na majeraha aliyonayo hivyo alibakia tu na gubu moyoni.Ule mchezo wa mlango kufunga na kufunguka wenyewe ghafla

ulisimama,mchungaji Josiah akakazia macho kuangalia kunani,hakuna kitu kilichoendelea ila kwa mbali sauti ya nyimbo ilianza kusikika,nyimbo isiyoeleweka inanena lugha gani! Wala nyimbo isiyoeleweka ina maanisha nini! Mara ya kwanza mchungaji Josiah alidhani masikio yake yanamdanganya ila alivyozidi kuisikia ile sauti ndipo alipoamini ya kwamba asikiacho ni sahihi,haikutosha hiyo tu...sauti ya kugonga gonga ilisikika toka juu ya paa!! nini hiki?? Mchungaji Josiah alijiuliza,sauti ya nyimbo za ajabu na za kugongwa paa zilizidi kumchanganya na kumuogopesha,imani yake ilianza kuterereka.Baada ya muda kidogo zile sauti

zilikoma,hazikusikika tena hivyo kuruhusu ukimya utawale na mchungaji Josiah kupumua,kuisha kwa kioja kile ulikua ni mwanzo wa kingine,sauti za miguu ikitembetembea ndani ya wodi ilianza kufika vema katika masikio ya Josiah,mungu wangu!!...mwili ulianza kusisimka na moyo ukaanza kudunda kama kitenesi pale alipohisi ile sauti ya miguu itembeayo inakaribia kwake!!...mchungaji Josiah alijifunika na shuka gubigubi kwa uoga asione kitakachoendelea huku joto na hofu vikimmimina jasho vya kutosha,mkono ulimgusa mgongoni na sauti ya kike ikaskika..
"kaka! nini shida??"
* * *
Jitihada za wanakijiji kumkimbiza yule mmama zilianza kuzaa matunda,ni hatua chache tu zilisalia ili wafanikishe lengo la kumkamata aliemuiba mtoto,yule mmama baada ya kuona anazidi kukaribiwa na wale wanaume alianza kuhofia usalama wake hivyo alimrusha mtoto huko!! wanaume wanne waliokua wanamkimbiza walisitisha lile zoezi na kwenda haraka kumtizama mtoto na kumuachia upenyo yule mmama wa kupotelea maporini,walimuinua yule mtoto na kuanza safari ya kurudi kijijini kwao,kitendo cha kumuokoa yule mtoto kilikua ni cha faraja mno kwao na hata wanakijiji walilifurahia hilo kwa kiasi kikubwa! matumaini yao yaliyopotea

yalirudi mahala pake na hapo ndipo mtoto alipopewa jina,akaitwa RENZO ikimaanisha TUMAINI kwa kilugha chao.
Baada ya furaha ya muda juu ya lile jambo wanakijiji walirudi tena majumbani mwao,ulinzi wa yule mtoto haikua tu inamhusu Julina bali kila mwanakijiji hivyo walihamasishana juu ya hìlo,vikoroboi vilizimwa na vitanda vikalaliwa.
Upande wa pili wa kijiji cha Igesambo ambapo ndipo yaliyopokua makao ya jeshi la 666 mambo hayakua mambo!..kushindwa kwa jaribio la kwanza la muda usiosogea na la pili la kumuiba mtoto kulifanya kusilalike wala kusilike,ni dhahiri viongozi wao

walichukizwa mno na lile jambo na ilibidi mipango mizito iundwe,kikao kizito kiliitishwa,wazee watano waliovaa majoho mekundu na meupe walikusanyika na baada ya muda kidogo alikuja mwingine alievalia joho jeusi tii! sura yake ilikua nyeusi na macho yake yalikua meupe,wale wengine watano walisimama na kumuinamishia kichwa yule alieingia na kudhihirisha ya kwamba ni mkubwa kwao,baada ya kufanya hivyo wale wazee wote ikiwemo na yule mkubwa wao waliinama na kusujudu huku wakitaja jina la mungu wao CHERNOBOG,kisha kikao kizito kilichukua nafasi..

"ni kwanini hasa tunashindwa???"
aliuliza yule mzee aliekua ameketi kwenye kiti kikubwa akizungukwa na wengine watano,kwa jina Abbadon.
"majaribio yetu hayakua na nguvu Oh shalom Abbadon,hivyo yaliweza kupanguliwa kiurahisi na wale binadamu"
alijibu mzee wa kwanza kabisa toka kwenye mkono wa kushoto wa yule mkuu wao,
"mnashindwaje na binadamu?? mnashindwaje na damu na nyama?? mnataka niambia kwamba wamewazidi akili??"
aliuliza tena Abbadon,mzee wa pili tokea mkono wake wa kulia akajibu..

"hatukufanya udadisi wa kutosha ili tuweze fahamu wapi ni nguvu yao na wapi ni udhaifu wao hicho ndicho kilipelekea hasa kushindwa kwetu.."
"kipi hasa ni nguvu yao??"
"kuna mzee aitwae Patili alie kijijini kwao,ni kikwazo kikubwa kwetu kutokana na kuwa na utaalamu utupao mushkeli!!"
"kwahiyo mmeamua kufanya nini sasa??"
Abbadon kwa msisitizo aliuliza,mzee mmoja aliekua kimya tokea kikao kianze alinyanyuka taratibu na kusema..

"Oh Shalom Abbadon,mimi kama Alvah mratibu mipango ningependa kuchukua fursa hii kuomba radhi kwa kushindwa kufanikisha majaribio yangu ila ningependa nipewe nafasi ya mwisho na endapo nisipofanikisha lengo nitawajibika"
hiyo kauli ilionekana kuwastua wazee wengine na kumpenya Abbadon moyoni,akaendelea
"naomba nipewe jaribio la mwisho,jaribio litakalobeba imani yangu kwako Shalom Abbadon na kwa mungu wangu CHERNOBOG..!!!"

Ni jaribio lipi hilo? Lyk 5 ili story iendlee





 
666-NYAYO ZA KUZIMU--39-

Palikua kimya vya kutosha,kila mtu alie kwenye kile kikao alimpa masikio ya uelewa Alvah mratibu wa mipango kama alivyoapishwa mapema tu baada ya uzao wa mungu mweusi CHERNOBOG,huku akijiamini na akiyanyoosha maelezo yake ya msingi juu ya jaribio lingine lifuatalo baada ya yale mengine kugonga mwamba,jaribio lililozito na jeusi,jaribio lililobeba ushindi na

kushindwa,jaribio litakalotabiri yatakayojiri,jaribio lililoshika nyadhifa yake na mwanzo au ukomo wa Mungu wake,ilikua hatari mno na ni dhahiri vita ilitangazwa.Macho ya Alvah yaliakisi mno kile alichokinena,yalikua makali na ya msisitizo vilevile yaliendana na uzito wa lile jaribio alinenalo,huku akinyoosha kidole alipata sema

"kafara ya watu ishirini yahitajika upesi! tuliyoipata leo jioni ilikua ni thelathini tena kwa mkupuo baada ya kupindua basi liendalo jijini mbeya,idadi iliyopelea ni ishirini ili niweze fanikisha lengo,ili niweze fanya jaribio zito litakalotusafishia njia kufikia mafanikio yetu hakika!!"

Abbadon alipata yasikia hayo yote na kumpenya,alimuamini Alvah vya kutosha kwani ni mchapakazi na dhahiri alikua anastahili kile cheo alichokua nacho,japokua alishindwa kwenye majaribio ya mwanzoni bado imani ilikua upande wake,hakukua na mtu aliyeonyesha kutilia shaka alichokinena hivyo kufanya hitimisho lipatikane kwa urahisi na kikao kufungwa ili kuruhusu shughuli za upatikanaji wa kafara za kuongeza nguvu jaribio zifanyike,waliinama na kusujudu kama mwanzoni wakiongozwa na Abbadon huku wakitamka baadhi ya maneno kwa sauti nzito ya kutisha "Oooh...Shalom CHERNOBOG!..eeeehh!...Shalom CHERNOBOG! Ukapate kutwaa!!"
kisha kikao kikafungwa kwa kunyunyuzia damu ya mbuzi aliechinjwa muda huohuo.
* *
Sauti aliyoisikia mchungaji Josiah akiwa ndani ya shuka alilojitwika ilimstua zaidi kwani ilikua inafanana na ile ya muuguzi aliemjulia hali muda si mrefu,hakujibu chochote,mdomo ulikua mzito na alikua anatetemeka mno,moyo uliokua unaenda kasi mithili ya maporomoko ya mto Owen ulikua unaomba mkono wa mungu utanakabali huku akizidi kujikunja kama kifaranga cha kuku kilicholoana na kuachwa na *****,
"kaka vipi kwani???"

sauti tena ileile ya kike ilisikika huku ikiambatana na zoezi la kumgusagusa Josiah alieloa uoga ndembendembe.Bado Josiah hakujibu lolote hali iliyompa mashaka yule muuguzi aliekua anamsubiria atoe kauli,
"jamani we kaka kuna nini??"

muuguzi wa watu alievalia nguo ya rangi ya karoti aliuliza tena kiupole,bado Josiah hakujibu chochote ila aliruhusu macho yake yapenye na kuchungulia kupitia shuka lile jepesi na kuhakikisha aongeae,alimuona muuguzi yule mweupe saiz ya katikati akiwa na sare zake zilezile alizokua nazo muda ule,hofu kidogo ikapungua akalishusha shuka lile lililokua limemfunika mpaka kichwani na kumuangalia muuguzi yule kwa macho ya aibu,huku akitabasamu akasema

"za saa hizi dada??"
"safi tu kaka,vipi kwani mbona ulikua katika ile hali???"
"ah! Kawaida tu dada,ni maumivu tu yalikua yananisumbua kusema ukweli"
"maumivu???"
"ndio!"
"ehh!! wapi panakusumbua kaka yangu??"

"huu mkono mlionifunga hii P.O.P unaniuma sana,kichwa nacho kinanipasua!"
"pole sana,usihofu lakini utazidi kupata nafuu kadiri unavyozidi kusonga mbele,cha umuhimu upumzike vya kutosha na usiwe unajikunjakunja kama ulivyofanya kwani utajisababishia maumivu zaidi na hiyo sindano ya dripu yaweza kuchomoka!"
"sawa dada,haina shida!!....naa vipi kuhusu yule dada niliyekuagizia mchana,anaendeleaje??"
"usihofu yupo sawa tu,sasa hivi anapumzika.."

mchungaji Josiah alitamani yale maongezi yasiishe kwani alijihisi ana amani zaidi kutokana na ule uwepo wa yule mdada,ila yule muuguzi ilibidi aondoke ili akawajulie hali na wengine hivyo alimuaga mchungaji Josiah na kujiondoa lile eneo.
*
Sauti kali za mbwa na bundi zilipamba usiku ule wa saa saba,mwezi ulikua unang'aa mno kutokana na kutokuwepo kwa mawingu angani na pembeni yake kulikua na nyota mbili zing'aazo,nyota ya upande wa kushoto ilikua inang'aa kupita nyingine hivyo kuashiria ya kwamba kuna litakalojiri,upepo wa baridi nao ulipuliza taratibu na kufanya miti na majani viiname,haikua ya kawaida,nyota ile

ing'aayo zaidi ilizidi kung'aa na kufanya mwanga wake kuwa mkali mithili ya mwezi,hakuna aliyeligundua hilo kutokana na watu kuwa vitandani kwa muda huo na hata baadhi yao waliokua macho sehemu mbalimbali kama kwenye kumbi za starehe na kwenye magari ya masafa marefu hawakulitambua hilo,ulikua ni wakati wa jeshi la 666 kutawala!!!! ile hali yote iliyokuwepo ilikua ni

kionyeshi ya kua usiku ule ulikua ni wa kafara,watu walikua wanatafutwa kwa ajili ya kafara ya kuongezea nguvu jaribio la kumtokomeza RENZO,mtoto pekee alieye kikwazo kwao kuushika ulimwengu,idadi ya watu kama ishirini na tano ikiwa imevalia majoho yenye rangi nyeupe na nyekundu na huku nyuso zao zikiwa na chapa ya 666 walishika njia kuelekea mahospitali yalipo,walianza na hospitali kuu ya Iringa!! Mchungaji Josiah na wenzake waliopo huko watapona??


Bila like 5,naidrop hii simulizi.ONE LOVE.
 
666-NYAYO ZA KUZIMU--39-

Palikua kimya vya kutosha,kila mtu alie kwenye kile kikao alimpa masikio ya uelewa Alvah mratibu wa mipango kama alivyoapishwa mapema tu baada ya uzao wa mungu mweusi CHERNOBOG,huku akijiamini na akiyanyoosha maelezo yake ya msingi juu ya jaribio lingine lifuatalo baada ya yale mengine kugonga mwamba,jaribio lililozito na jeusi,jaribio lililobeba ushindi na

kushindwa,jaribio litakalotabiri yatakayojiri,jaribio lililoshika nyadhifa yake na mwanzo au ukomo wa Mungu wake,ilikua hatari mno na ni dhahiri vita ilitangazwa.Macho ya Alvah yaliakisi mno kile alichokinena,yalikua makali na ya msisitizo vilevile yaliendana na uzito wa lile jaribio alinenalo,huku akinyoosha kidole alipata sema

"kafara ya watu ishirini yahitajika upesi! tuliyoipata leo jioni ilikua ni thelathini tena kwa mkupuo baada ya kupindua basi liendalo jijini mbeya,idadi iliyopelea ni ishirini ili niweze fanikisha lengo,ili niweze fanya jaribio zito litakalotusafishia njia kufikia mafanikio yetu hakika!!"

Abbadon alipata yasikia hayo yote na kumpenya,alimuamini Alvah vya kutosha kwani ni mchapakazi na dhahiri alikua anastahili kile cheo alichokua nacho,japokua alishindwa kwenye majaribio ya mwanzoni bado imani ilikua upande wake,hakukua na mtu aliyeonyesha kutilia shaka alichokinena hivyo kufanya hitimisho lipatikane kwa urahisi na kikao kufungwa ili kuruhusu shughuli za upatikanaji wa kafara za kuongeza nguvu jaribio zifanyike,waliinama na kusujudu kama mwanzoni wakiongozwa na Abbadon huku wakitamka baadhi ya maneno kwa sauti nzito ya kutisha "Oooh...Shalom CHERNOBOG!..eeeehh!...Shalom CHERNOBOG! Ukapate kutwaa!!"
kisha kikao kikafungwa kwa kunyunyuzia damu ya mbuzi aliechinjwa muda huohuo.
* *
Sauti aliyoisikia mchungaji Josiah akiwa ndani ya shuka alilojitwika ilimstua zaidi kwani ilikua inafanana na ile ya muuguzi aliemjulia hali muda si mrefu,hakujibu chochote,mdomo ulikua mzito na alikua anatetemeka mno,moyo uliokua unaenda kasi mithili ya maporomoko ya mto Owen ulikua unaomba mkono wa mungu utanakabali huku akizidi kujikunja kama kifaranga cha kuku kilicholoana na kuachwa na *****,
"kaka vipi kwani???"

sauti tena ileile ya kike ilisikika huku ikiambatana na zoezi la kumgusagusa Josiah alieloa uoga ndembendembe.Bado Josiah hakujibu lolote hali iliyompa mashaka yule muuguzi aliekua anamsubiria atoe kauli,
"jamani we kaka kuna nini??"

muuguzi wa watu alievalia nguo ya rangi ya karoti aliuliza tena kiupole,bado Josiah hakujibu chochote ila aliruhusu macho yake yapenye na kuchungulia kupitia shuka lile jepesi na kuhakikisha aongeae,alimuona muuguzi yule mweupe saiz ya katikati akiwa na sare zake zilezile alizokua nazo muda ule,hofu kidogo ikapungua akalishusha shuka lile lililokua limemfunika mpaka kichwani na kumuangalia muuguzi yule kwa macho ya aibu,huku akitabasamu akasema

"za saa hizi dada??"
"safi tu kaka,vipi kwani mbona ulikua katika ile hali???"
"ah! Kawaida tu dada,ni maumivu tu yalikua yananisumbua kusema ukweli"
"maumivu???"
"ndio!"
"ehh!! wapi panakusumbua kaka yangu??"

"huu mkono mlionifunga hii P.O.P unaniuma sana,kichwa nacho kinanipasua!"
"pole sana,usihofu lakini utazidi kupata nafuu kadiri unavyozidi kusonga mbele,cha umuhimu upumzike vya kutosha na usiwe unajikunjakunja kama ulivyofanya kwani utajisababishia maumivu zaidi na hiyo sindano ya dripu yaweza kuchomoka!"
"sawa dada,haina shida!!....naa vipi kuhusu yule dada niliyekuagizia mchana,anaendeleaje??"
"usihofu yupo sawa tu,sasa hivi anapumzika.."

mchungaji Josiah alitamani yale maongezi yasiishe kwani alijihisi ana amani zaidi kutokana na ule uwepo wa yule mdada,ila yule muuguzi ilibidi aondoke ili akawajulie hali na wengine hivyo alimuaga mchungaji Josiah na kujiondoa lile eneo.
*
Sauti kali za mbwa na bundi zilipamba usiku ule wa saa saba,mwezi ulikua unang'aa mno kutokana na kutokuwepo kwa mawingu angani na pembeni yake kulikua na nyota mbili zing'aazo,nyota ya upande wa kushoto ilikua inang'aa kupita nyingine hivyo kuashiria ya kwamba kuna litakalojiri,upepo wa baridi nao ulipuliza taratibu na kufanya miti na majani viiname,haikua ya kawaida,nyota ile

ing'aayo zaidi ilizidi kung'aa na kufanya mwanga wake kuwa mkali mithili ya mwezi,hakuna aliyeligundua hilo kutokana na watu kuwa vitandani kwa muda huo na hata baadhi yao waliokua macho sehemu mbalimbali kama kwenye kumbi za starehe na kwenye magari ya masafa marefu hawakulitambua hilo,ulikua ni wakati wa jeshi la 666 kutawala!!!! ile hali yote iliyokuwepo ilikua ni

kionyeshi ya kua usiku ule ulikua ni wa kafara,watu walikua wanatafutwa kwa ajili ya kafara ya kuongezea nguvu jaribio la kumtokomeza RENZO,mtoto pekee alieye kikwazo kwao kuushika ulimwengu,idadi ya watu kama ishirini na tano ikiwa imevalia majoho yenye rangi nyeupe na nyekundu na huku nyuso zao zikiwa na chapa ya 666 walishika njia kuelekea mahospitali yalipo,walianza na hospitali kuu ya Iringa!! Mchungaji Josiah na wenzake waliopo huko watapona??


Bila like 5,naidrop hii simulizi.ONE LOVE.

Wacha maneno hayo....unanitesa mwenzio
 
Like! like! Like! Like! Like hii ya kianalogia,kidigitali itafuata,duh!! Pastor Josiah atapona kweli??
 
afu mzizi una utani na watu mi nina rafiki anaitwa Josia afu ni Pastor na huwa tunamwita pastor Josia , nimecheka sana nilipoona unatumia jina la pastor Josia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom