666-nyayo za kuzimü

666-nyayo za kuzimü

watu wagumu kwa kutoa like!! kama watapungukiwa na kitu vile, kama vipi mzizimkavu usiendelee.
 
666-NYAYO ZA KUZIMU--40-

387955_520867291275780_80757636_n.jpg



(mwanga wa giza)


walianza na hospitali kuu ya Iringa!! Hatari ilioje?? Waliingizana taratibu huku wakinyata,kila kilichonenwa na kiongozi wao aliyekua ni mama Marinda ndicho kilichotekelezwa,macho yao yaliyoakisi mwang
a wa mwezi yaliwafanya waonekane mithili ya paka! Masikio yao marefu na mjazo wa tarakimu 666 kwenye mapaji ya uso ilizidi kuwafanya waonekane wanyama ukiachilia

mbali na miili yao yenye rangi ya kijivu.Geti la hospitali lililo kuu kuu hata halikuguswa hivyo hamna kelele iliyozalishwa.Miguu yao iliyo peku ilikanyaga chini kiustaarabu huku macho yao yakiangaza angaza huku na kule kiusalama zaidi.Mikono yao yenye kiu ya kutekeleza walichoagizwa ilianza kufanya kazi kwa mlinzi mzee waliemkuta fofofo kwa usingizi.Walimnyonga kama kuku bila

kumpa fursa hata ya kusema lolote,akajazilishia idadi.Macho yao yakaelekezwa kwenye wodi ya wanaume alipo mchungaji Josiah,taratibu wakaanza kujongea huku wakipangana mstari,mbele akiwa mama Marinda kiongozi,walikua wanatisha mno na vilevile walikua wananuka kifo! Hilo ndio jeshi la 666.Mkono wa mama Marinda wenye michirizi ya mishipa na kucha ndefu ulishika kitasa na kufungua taratibu kisha akachungulia,baada ya kurudisha kichwa chake alitoa amri iliyotekelezwa bila ya maswali,waliingia watu watatu,wanaume wawili na mwanamke mmoja wakanyooka mpaka kwenye kitanda cha kwanza

kabisa,walipogundua ya kwamba alielala pale ashafariki waliachana nae na kujongea kwenye cha pili,wakamkuta aliepale mzima ila usingizi mzito umembeba,haraka wakatawanyika na kukizunguka kile kitanda kutokana na idadi yao,wakafumba macho na vinywa vyao vikaanza kutetema maneno fulani ya lugha ya ajabu yenye maana ya kutanakabali kafara yao,mara ghafla yule mtu aliekua amelala pale akatapatapa kama anaenyongwa na baada ya muda kidogo akatulia tuli kumaanisha ashakufa! Mtindo ukawa ni

uleule,wakasogea kwenye kitanda kinachofuatia.Wakati hayo yote yanachukua nafasi mchungaji Josiah alikua hana habari,alikua akikoroma kutokana na usingizi mzito uliombeba na kitanda chake kilikua ni cha sita tokea walipo wale wauaji wa kafara.
Macho yakafumbwa tena na sala ya kuitanakabali kafari ikafanyika,mwingine wa kitanda kinachofuata nae akaenda na maji,wale

watu watatu wauaji wakasogelea kitanda kingine kifuatacho wakakuta aliepale kafariki hivyo wakakiruka na kwenda kingine,idadi ya vitanda vilivyobaki ili mchungaji Josiah akutwe vikawa ni vinne tu.Kama kawaida mchezo ukaendelea,mgonjwa aliyekuwepo pale nae akarusharusha miguu kisha akaenda na maji kwa ajili ya kafara.Idadi ya waliouwawa ikawa ni wanne akiwemo mlinzi

aliefungua dimba.Bado haikuwatosha,walisogelea tena kitanda kifuatacho alipo mzee mmoja asumbuliwaye na figo,kitambi chake kilikua kama kichuguu kwani alijifunika na shuka gubigubi akilala chali.Hawakutaka kupoteza muda,kama kawaida waliyafunga macho yao wote na kutetema maneno fulani kwa lengo la kuitanakabali kafara yao,yule mzee akarusharusha miguu yake kuitetea roho yake lakini mwishowe akatulia tuli na mapigo ya moyo yakazizima.Wakasogelea kitanda kingine!!!
* *
Ndani ya kanisa la Under the God Fontain sala nzito ilikua inaendelea ikiongozwa na askofu Emmanuel Mgaya,wachungaji watano pia walikuwepo kwenye mkesha ule wa dharura ulio maalum kwa ajili ya kumuomba mungu awaweke mikononi watumishi wake waliokumbwa na ajali wakiwa njiani kwenda kumtumikia.Kila aliyekua pale alisema na mungu kwa njia na uwezo wake.Sauti zao pekee ndizo zilizosikika kwa ule muda wa usiku totoro,wakiomba kwa nguvu huku sura na matendo yao vikiakisi ni kwa jinsi gani lile jambo lilivyo serious kwao na jinsi gani linavyowagusa.Miili yao iliyokua ikipata joto kutokana na sala hiyo nzito ilikua inapoozwa taratibu na feni aina ya SOLCE hivyo basi kuwafanya wazidi kudumu kwenye maombezi.
* * *
Wale watu watatu wauaji waliwadia rasmi kwenye kitanda cha mchungaji Josiah,walikizunguka kama kawaida na bila kupoteza muda walifunga macho yao na kuanza kutetema maneno kama walivyofanya kwenye vitanda vilivyopita.Baada ya muda wakafungua macho yao kutizama majibu,Josiah bado alikua anahema,waliangaliana kwa mshangao kisha wakarudia tena lile tendo kwa uhakiki zaidi.Walipofungua tena macho yao wakamkuta mtu bado mzima,walishangaa sana juu ya hilo huku wakijiuliza ni wapi wamekosea,wakiwa wamepigwa bumbuwazi walisikia sauti ya makofi tokea kule mlangoni iliyowaashiria ya kwamba wanaitwa,wakageuza na kuanza kukimbia kuelekea langoni na kisha kupotelea kabisa.Josiah alishtushwa na sauti na sauti za watu zilizokua zinaishia,alipotizama huku na kule hakuona kitu,muda si mrefu yule muuguzi akaingia mule ndani akiwa na sura iliyojaa uoga.
Je kuna nini??

Muendelezo wa hii simulizi upo kwenye kitabu,kwa wanaokihitaji twaweza wasiliana,na

-Stevie Byblove Fericious
-0718246094
 
Duh! MziziMkavu kusema kwamba ndo umeishia hapa?? Endelea mkuu..... Basi usiku wa kuamkia leo wacha niiote hii hadithi jaman niliteseka sana,nilipostuka ilikuwa ni saa 8 kasoro ilibidi niamke na kuanza kusali tu.
 
Last edited by a moderator:
Duh! MziziMkavu kusema kwamba ndo umeishia hapa?? Endelea mkuu..... Basi usiku wa kuamkia leo wacha niiote hii hadithi jaman niliteseka sana,nilipostuka ilikuwa ni saa 8 kasoro ilibidi niamke na kuanza kusali tu.

Kwa iyo ukaota hadith!!...bas tuendelezee mzizi mkavu apumzike...
 
Last edited by a moderator:
Mzizi sijakusoma, kwamba ndo umefika tamati? Maliza kabisa mkuu, hamkani si shwari tena!
 
MziziMkavu

Amekata stimu yote,

hatujui ilikuwaje lile Jeshi mwisho wake;

Naona sasa wameamua kuja na DENGUE kutumaliza wote. Na sisi tutajipaka dawa ya kupambana na hao Mbu tu.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Last edited by a moderator:
Mzizi mkav,,come ths way plx...dengue tayar dawa ishapatikana...
 
Kwa iyo ukaota hadith!!...bas tuendelezee mzizi mkavu apumzike...

Yaani siyo niliota kwa muendelezo kwamba nini kinafuata,ni kwamba yale mauzauza ya hii hadithi ndiyo niliyaota,nadhani hii ni kwasababu hii hadithi imenikuna sana nikajikuta hadi naota.
 
Yaani siyo niliota kwa muendelezo kwamba nini kinafuata,ni kwamba yale mauzauza ya hii hadithi ndiyo niliyaota,nadhani hii ni kwasababu hii hadithi imenikuna sana nikajikuta hadi naota.

Haha...m ikiwa ni uck i never read ata km ni muendelezo...hua nasoma asbh au mchana...maana ni balaa
 
Haha...m ikiwa ni uck i never read ata km ni muendelezo...hua nasoma asbh au mchana...maana ni balaa

Umeona ehhh??? mi nilijikanyaga siku hiyo nikasoma usiku,acha tu nilikuwa naota tu Pastor Josiah na 666,sijui kama sikuropoka hilo jina ni bahati!! maana ningeachika kabisa!! ila nakumbuka nilistuka kwa kupiga kelele Mungu nisaidieeeeee!!
 
Umeona ehhh??? mi nilijikanyaga siku hiyo nikasoma usiku,acha tu nilikuwa naota tu Pastor Josiah na 666,sijui kama sikuropoka hilo jina ni bahati!! maana ningeachika kabisa!! ila nakumbuka nilistuka kwa kupiga kelele Mungu nisaidieeeeee!!

Hahaha..unabahat!!!...ungeropoka jina sa iz ungekua unaomba ushaur wa uende kwenu au ugande umo umo..tehe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom