50 Greatest Tanzanians (minus politicians)

Marehem Mtemi Senge wa Singida.

Mzee aliyekuwa na kipaji kuhusu wanyama pori mpaka ikasemekana anajuwa lugha za wanyama, he is a legend, ni wangapi humu wanamuelewa?
Fafanua ueleweke hicho kipaji cha wanyama..
 
jamaa wapo weng sannaa,kwa wasaanii,

1. honorable mr 2 aka sugu....
2. mzee jongo
3.bishanga bashaija.

Waandishi ni wengi mno lakini wachahce ni
1. karugendo padri
2.mwanakijiji
3.ulimwengu
4.said kubenea
na weng mnoo

madractrari kwauchache,
1. dr Maro mtaharam wa moyo na former dr wa mkapa
2.Dr Rwakatare na wengine weng..

hahahaha huwezi amini kuwa huyo jamaa in red jamaa ni mnyakyusa ,maana alikuwa anaiga wahaya lol!!!
 
Duh!!!wote nimewasahau!!!!!!!
Maria Nyerere!!!!huyu alikuwa mwanamgambo mahiri aliyetumia mda wake kuwafundisha wananchi juu ya ukakamavu bila kujali wadhifa wake wa kuwa First Lady
 
Stephen Akhwari- Mtanzania aliyekwenda Olympic Mexico 1968. Aliumia baada ya kuanguka na aliendelea na mbio kwa taabu na maumivu makubwa akiingia uwanjani baada ya saa 2 mshindi wa kwanza kupatikana. Amepewa heshima kubwa sana Duniani hadi leo kwa akuli yake 'sikutumwa na nchi yangu kuja kuanza mashindano bali kumaliza'.

Filbert Bayi- Alivunja record ya dunia ya mita 1500 christ church Newzealand na akawika sana dunia kama 'symbol 'ya Tanzani katika vyombo vya habari duniani. Kwa msisimko wake ndio tukawapata akina Gidamas Shahanga, J.Ikangaa n.k.

Jela Mtagwa- Aliongoza kikosi cha Tanzania mashindano ya soka Lagos mwaka 1980. Hatujarudi tena hadi kesho. Alikua na akina Peter Tino, Tenga, Kajole(RIP), Mohamed Salum n.k

Fadhili William (Mtanzania? Mkenya?)- Kutoa kibao kisichochuja hadi leo Malaika.

Prof Shivji- Gwiji la kitaaluma nchini na ughaibuni, mwanaharakati na mtu anayeijali jamii sana.

Ananilea Nkya- Mama mwenye nguvu ya ushawishi wa hoja na inspiration kwa akina Dada.

Hemed bin Jumaa- Kiongozi wa dini aliyekuwa na busara na ushawishi mkubwa sana wa hoja. Aliheshimika sana nje ya nchi kwa uzamifu wake katika mambo ya dini( ulamaa). Aliheshimiwa sana hata na wapinzani wa hoja zake

Rugambwa- Mtanzania wa kwanza kuwa na shahada ya PhD katika mambo ya dini. Alikuwa na mtulivu mwenye busara,asiyependa kuonekana wala makuu. Ameacha mengi katika sekta hasa ya elimu

Mama Kam- Mwalimu aliyethibitishia umma kuwa wasichana hawana tofauti na wavulana kitaaluma kama kutakuwa na uwanja sawa wa kushindana.

Rwegarulila- Mwanataaluma aliyebuni miradi mingi ikiwa ni pamoja na chuo cha maji kilichopewa jina kwa heshima yake.

Prof Thom MMari- Alifungua uwanja wa mawazo huru chuo kikuu, kutoa fursa ya majadiliano bila kujali yanakinzana na maslahi yake au la.
Ndiye makamu mkuu wa chuo kikuu cha Dar aliyeweza kuingia Mkrumah katikati ya zogo la mgomo. Aliheshimiwa sana na wanafunzi. Aliweza kutoka nyumbani kwake kwenda kwenye vikao vya Kunji alipotakiwa bila ulinzi.

itaendelea
 
Stephen Akhwari- Mtanzania aliyekwenda Olympic Mexico 1968. Aliumia baada ya kuanguka na aliendelea na mbio kwa taabu na maumivu makubwa akiingia uwanjani baada ya saa 2 mshindi wa kwanza kupatikana. Amepewa heshima kubwa sana Duniani hadi leo kwa akuli yake 'sikutumwa na nchi yangu kuja kuanza mashindano bali kumaliza'.

Filbert Bayi- Alivunja record ya dunia ya mita 1500 christ church Newzealand na akawika sana dunia kama 'symbol 'ya Tanzani katika vyombo vya habari duniani. Kwa msisimko wake ndio tukawapata akina Gidamas Shahanga, J.Ikangaa n.k.

Jela Mtagwa- Aliongoza kikosi cha Tanzania mashindano ya soka Lagos mwaka 1980. Hatujarudi tena hadi kesho. Alikua na akina Peter Tino, Tenga, Kajole(RIP), Mohamed Salum n.k

Fadhili William (Mtanzania? Mkenya?)- Kutoa kibao kisichochuja hadi leo Malaika.

Prof Shivji- Gwiji la kitaaluma nchini na ughaibuni, mwanaharakati na mtu anayeijali jamii sana.

Ananilea Nkya- Mama mwenye nguvu ya ushawishi wa hoja na inspiration kwa akina Dada.

Hemed bin Jumaa- Kiongozi wa dini aliyekuwa na busara na ushawishi mkubwa sana wa hoja. Aliheshimika sana nje ya nchi kwa uzamifu wake katika mambo ya dini( ulamaa). Aliheshimiwa sana hata na wapinzani wa hoja zake

Rugambwa- Mtanzania wa kwanza kuwa na shahada ya PhD katika mambo ya dini. Alikuwa na mtulivu mwenye busara,asiyependa kuonekana wala makuu. Ameacha mengi katika sekta hasa ya elimu

Mama Kam- Mwalimu aliyethibitishia umma kuwa wasichana hawana tofauti na wavulana kitaaluma kama kutakuwa na uwanja sawa wa kushindana.

Rwegarulila- Mwanataaluma aliyebuni miradi mingi ikiwa ni pamoja na chuo cha maji kilichopewa jina kwa heshima yake.

Prof Thom MMari- Alifungua uwanja wa mawazo huru chuo kikuu, kutoa fursa ya majadiliano bila kujali yanakinzana na maslahi yake au la.
Ndiye makamu mkuu wa chuo kikuu cha Dar aliyeweza kuingia Mkrumah katikati ya zogo la mgomo. Aliheshimiwa sana na wanafunzi. Aliweza kutoka nyumbani kwake kwenda kwenye vikao vya Kunji alipotakiwa bila ulinzi.

itaendelea

JELA MTAGWA: LIcha ya kuwika kwenye hayo mashindano, Jela pamoja na Dilunga waliitwa kwenye timu ya Africa (All African Stars) na pia ni mwanamichezo ambaye picha yake iliwekwa kwenye stamp, nadhani mnajua umuhimu wa stamp wakati huo

LAURIEN LUGAMBWA: Huyo ndio alikuwa Kardinal wa kwanza Mwafrika (Mweusi?)
 
Kuna mtu kamuweka riziwani...Hugo ni mwanasiasa bora miraji..though wote bado..",bora uwaweke capt John na capt Andrew Nyerere(jet fighter pilots) ,walikuwa watoto wa kwanza wa sitting president kupigana mstari wa mbele Uganda....pamoja na mdogo wao capt .makongoro.

Kuna kina ,Dendego,Mzena wakuu wa mwanzo kabisa wa Tiss,..kuacha kinaa Lau Gama na Hassan Kitine...ambao wao baadaye waliingia..siasa..",
Tuna majemedari wa vita na jeshi letu kwa ujumla......wotte wastahili kuenziwa miaka 50 ya Uhuru.....
kuna kundi la wanamichezo waliotia fora nao ni mashujaaa...
Kuna wa iota ya mambo yaliyookoa maisha ya mamilioni Kama yule sajenti wa Kikosi cha zimamoto ..aliyejitoa muhanga kupita katikati ya moto kwenda kuzima tank lililokuwa linaungua kwenye katakana ya mafuta na gesi pale ubungo....Kama sio yeye matenti yenye mafuta na gesi kwa mamilioni ya ujazo yanelipuka....Mazda yangetokea ya ajabu nadhani kuanzia ubungo Hadith sinza yote Hadi relini mabibo Kungeenea moto.

Wapi wengi wengi ...na ni kazi inayotakiwa kufanywa kwa kuwashirikisha watu ma background ,na umri tofauti...otherwise unsung heroes watakuwa wengi.....waasisi wa Uhuru nao watafutwe ili wale mashujaaa wa Uhuru ambao hawakuenziwa nao wawepo
 
Filbert Bayi (born June 23, 1953) is a former middle-distance runner of the 1970s who set the world records for 1500 metres in 1974 and the mile in 1975. He is still the 1500 m Commonwealth Games record holder. The following writers have influenced us in one way or another. Godfrey Mwakikagile, Mohamed Said, Abdulrazak Gurnah, Julius Nyang'oro, Prof. Clement Ndulute, Prof. Frank Chiteji, Prof. Joseph Mbele, Prof. Issa Shivji, Jenerali Twaha Ulimwengu, Prof. Penina Mlama, Prof Chris Peter Maina, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (you can’t avoid this man, yuko kotekote), Adam Shafi, Dr. Malima M.P Bundala and Shaaban Robert.

But by greatest Tanzanian go to Suleiman Nyambui (born February 13, 1953). His remarkable history is inspiring. He won the silver medal in 5000 metres at the 1980 Summer Olympics. Nyambui had dropped out of school after primary education. He became a fisherman in Ukerewe District Mwanza Region where his potential as a good athlete was spotted by the Region's Athletic Organization.

In short, the organization helped in his training and afforded him facilities and guidance in making him a national and international athlete. This just shows that if talented people are offered facilities and guidance they can be the greatest not only nationally but also internationally. Nyambui also had joined the Tanzania National Service before he went to train as a teacher. He taught school at Bukumbi -twenty miles from Mwanza City - till he went to study in the United States for his Bachelor's and Master's degrees at UTEP.

Then, he took a contract to train Saudi Arabian athletes. After that he moved back to Tanzania. In between all these, he also did the followings:

  • He won a bronze medal at the 1978 All-Africa Games, and twice (1987 and 1988) triumphed at the Berlin Marathon.
  • Attended the University of Texas at El Paso (UTEP) from 1978 to 1982, where, as an older aged athlete (he was 29 when he graduated), he won four straight NCAA titles in the 10,000 meters — one of only five Division I men to ever accomplish such a feat.
  • He also won 3 straight NCAA titles in the 5,000 meters while at UTEP and was the 1980 NCAA Cross Country champion.
  • In a memorable Millrose Games race in New York in February 1981, Nyambui broke the world indoor 5,000 meter record with a 13:20.4, just ahead of Alberto Salazar who broke the American indoor 5,000 meter record.
 
Kwa upande wa sanaa kuna mtu aliyejulikana kama George Lilanga.

Huyu alikua na kipaji cha hali ya juu cha uchongaji vinyago, uchoraji na upakaji rangi.

Amekua akipeperusha vyema bendera ya Tanzania kila pembe ya dunia. Na amewahi kupata several
international accolades.

Kwa taarifa zaidi unaweza kucheki GeorgeLilanga.com
 
Sheikh mkuu mufti Hemed bin Jumaa Bin Hemed..almarhum ,nilikuwa nikipenda Sanaa kusikiliza mawaidha Yake...enzi hizo kuna RTD ...kipindi cha mawaidha ya kiislamu...mwandaa vipindi enzi hizo alikuwa sheikh Gorogosi(marehem)...Huyu pia alikuwa katibu wake...pamoja ya kuwa Mimi sio muislamu ,Nikiyapenda Sanaa mawaidha ya mufti hemmed ,na sio Mimi pee...wengi tulimpenda...
Naomba waalim wallop humu jamvini watueleze zaidi juu Yake!....
 
DNS na wengineo asanteni sana kwa hili somo. Mmetufungua macho,Mdharau kwao mtumwa.
 
Kwa upande wa sanaa kuna mtu aliyejulikana kama George Lilanga.

Huyu alikua na kipaji cha hali ya juu cha uchongaji vinyago, uchoraji na upakaji rangi.

Amekua akipeperusha vyema bendera ya Tanzania kila pembe ya dunia. Na amewahi kupata several
international accolades.
Kwa taarifa zaidi unaweza kucheki GeorgeLilanga.com

Au unamaanisha mzee Tinga Tinga?

Pia tinge kwenye usomi ...daktari wa kwanza mzalendo kina mwaisela....,profess wa kwanza,..etc etc...majaji...jaji wa kwanza mzalendo,jaji wa kwanza mwanamke....etc...engineer wa kwanza....
Mkuu wa kwanza wa mlimani ..dr www chagulla..etc..
 
marehemu askofu sebastian kolowa, wengine hamkawii kusema naingiza udini, lakini alikuwa ni mtu anaheshimika kwa kada zote na kwa dini zote, viongozi wa serikali pia walimtambua kwa busara zake za kutatua migogoro hasa ule mgogoro wa dayosisi ya meru, ameifanyia makubwa ya kukumbukwa taasisi ya warutheli tanzania.
 
dah! kweli bado wapo wengi, mbaraka mushehe, aisee huyu mzee sijawahi kumuona ila namhusudu sana,
 
chifu kimweri, ngoja nitakuja na taarifa zake za kutosha kuhusu huyu mtu.
 
marehemu askofu sebastian kolowa, wengine hamkawii kusema naingiza udini, lakini alikuwa ni mtu anaheshimika kwa kada zote na kwa dini zote, viongozi wa serikali pia walimtambua kwa busara zake za kutatua migogoro hasa ule mgogoro wa dayosisi ya meru, ameifanyia makubwa ya kukumbukwa taasisi ya warutheli tanzania.

Augustine Mrema mediated Meru..diocese conflict and earned himself unconstitutional post of Deputy Prime Minister.
 
Marehemu Stan Katabaro! Stan umelala, lakni you will always be remembered. Alikuwa mwandishi wa gazeti la Mfanyakazi enzi hizo za S.L.P, siyo dot.com!
 
Ruge wa clouds fm.

Kwa lipi? Kuwapigia magamba kampeni? Kwa kumwandalia jk happy bday? Kwa kuanzisha fiesta inayosambaza ukwimwi kwa vijana wetu? Nafikiri ukiwachambua clouse mengi yana negative effect to the public so guy stop jocking we are serious
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom