30 - 36 years old: An Official Thread

ila ukweli mchungu mzazi huwapenda watoto wake wote kwa usawa wakiwa wadogo wakishakuwa watu wazima, wanapendwa kulingana na kipato na msaada wanaotoa.hasa hawa wakina mama zetu .
 
ujinga tu . endelea na mipango yako achana na mambo ya umri
Point sana hii; Ila wengi hawatakuelewa; Umri is nothing zaidi ya mind ya Mtu; Ndio maana kuna mtu ana 50 years ila ana utoto/mambo ya kitoto halafu kuna mtu ana 20-25 ila mind yake ni utu uzima full,

Achaneni na mambo ya Umri as long as uko hai katika ulimwengu huu na unaendelea kuishi basi achana na mambo ya umri. Mzee wa KFC ametoboa akiwa on his 60's huko. Ishu ni kuwa determined bila kujali umri wako;
 
Noted , muhimu sana kuangalia maisha baada ya kifo maana starehe za dunia ni udanganyifu mtu unaweza kuwa na pesa lakini ukawa na stress za kuchapiwa na kukosa amani.

Kuna mwehu humu aliwahi kukomenti eti "Mwenyezi Mungu siku ya kiama awapunguzie adhabu ya motoni na kuwaonea huruma wale walioishi Tanzania maana ugumu wake ni sawaa na kuishi motoni"sasa just imagine umeishi Tz kea kupigika kisha ukaishi kama hautofufuliwa tena kisha hatima yako iwe motoni unakuwa umepigika kote kote bora kuweka na kwengine tupate kusalimia.
 
kuitafuta pepo.

Ndo nini hiki???
 
Ndo maana mnakufa kwa stress kwa kujilinganisha na fulani wewe Ni wewe na hakuna Kama wewe, we pambana tu age is just a number!
 
Kwenye maisha stress haziwezi kuisha ukimaliza kusoma unaaamin ukipata kazi utaridhika lakin ukipata kazi unawaza vyeo/mali, ukijipindua unawaza mtoto ukipata mtoto unawaza atasomaje vizuri, bahat mbaya hata kaz unaweza usipate na kila unachoshika kikanguk yan kwakifup kwanzia unazaliwa had unaondka dunia hii huwez kuridhika na mahali ulipo

Binadam tumekua tunataman kila kizuri ambacho hatuna na kwa bahat mbaya huwez kupata vyote, unaweza ukapata mali ukakosa afya njema pia huwez kuridhika
 
Inategemea
Kwa mazingira yetu ya nchi za Dunia ya Tatu ni wachache ambao kwa umri huo wanakua wamefanikiwa kwa vigezo ulivoweka
Binafsi nipo katika umri huo. Nipo katika ajira mwaka WA pili naenda WA Tatu Sasa lakini bado bila bila zaidi ya mke na mtoto.
Mzunguko wetu WA kusoma tangu shule ya msingi mpaka chuo inafanya iwe ngumu kufanikiwa kwa vigezo vya mtoa Mada katika umri huo, inawezekana pia.
 
Kuna watu humu wana act kama hazimo.

Uzi, hauoneshi kuwa ni lazima ufanikiwe b4 au katika 30s

Uzi haumanishi kukupa pressure kwa kuwa haujafanya chochote at 30s

In reality, 30 to 36, ni mid life ya mwanadamu, wengi sasa tunakufa 55 to 65yrs.

Uzi ni kupeana mitazamo na kushauriana
 
Hakuna formula ya Maisha! Acheni kutia watu pressure. Njia yako si njia ya mwingine, wakati wako siyo wakati wa kila mtu.

Vinginevyo mapacha wangekuwa wanalingana kwa viwango vya mafanikio. Watu wafanye yaliyo sawa tu.

Unajaribu kuwambia watu hapa kwamba usipofanya hayo ulisema katika umri huo huwezi tena kuyafanya?! Nonsense.

Kuna watu wametoka vyuoni at the age of 25yrs wakapata kazi yao ya kwanza wakiwa at the age of 40 years! Na wana life adorable.

Na wengi waliopata kazi at 25- 30, bado ni useless people.


Acheni kudhani mnajua maisha, acheni kuyageneralize. Life is too personal and unique to everyone of us.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…