Ugonjwa wa Pumu (Bronchial Asthma): Chanzo, dalili na tiba

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,012
Pumu Kwa Watu Wazima.jpg

Utangulizi
Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu zinazojulikana kitaalamu kama bronchioles. Mtu mwenye pumu huwa na mcharuko mwili sugu (chronic Inflammation) kwenye mirija yake ya

kupitishia hewa (bronchioles tubes) hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija hii, kujaa kwa ute mzito (mucus) na kupungua kwa njia ya kupitishia hewa, hali ambayo humfanya muathirika kushindwa kuvuta na kutoa hewa

nje na hivyo kupumua kwa shida sana. Hali hii inaweza kudumu kwa muda mfupi au mrefu kiasi cha kuhitaji tiba ili kumuwezesha mgonjwa kupata nafuu.
Kutokana na kuwepo kwa msuguano na uzuiaji wa kupitisha hewa wakati wa kupumua hwa nje, pumu hujulikana pia kama obstructive lung disease . Mtu aliye na pumu, huwa nayo kipindi chote cha maisha yake.

Makundi ya Pumu
Pumu inaweza kugawanywa katika makundi mawili;

  • Pumu ya ghafla (Acute asthma): Wagonjwa wanaopatwa na kundi hili la pumu huwa na hali ya kawaida katika njia zao za hewa isiyobadilika kati ya shambulizi moja na jingine.
  • Pumu sugu (Chronic Asthma): Kundi hili la pumu huwa na tabia ya kuwa na njia nyembamba za kupitisha hewa na kadiri jinsi mgonjwa anavyoendelea kupata matukio zaidi ya pumu, njia za hewa huzidi kuwa nyembamba zaidi.
Aina za ugonjwa wa pumu
Bila kujalisha mgonjwa anaingia katika kundi gani, ugonjwa wa pumu unaweza kugawanywa katika aina kuu nne, ambazo ni 1.Pumu inayobadilika (brittle asthma): Kulingana na tabia ya kujirudia rudia kwa matukio ta ugonjwa huu na madhara yake kwa mgonjwa, aina hii ya pumu inaweza kugawanywa zaidi katika aina nyingine mbili, ambazo ni

  • Aina ya kwanza ya pumu inayobadilika (type 1 brittle asthma) ni pumu yenye tabia ya kuwa na matukio na mashambulizi ya kubadilika kila mara japokuwa mgonjwa anaweza kuwa anapata matibabu kadhaa.
  • Aina ya pili ya pumu inayobadilika (type 2 brittle asthma) ni pumu ambayo mgonjwa anatokea kupata shambulizi la ghafla (asthmatic attack) wakati hapo awali ugonjwa wake uliweza kuthibitiwa kwa matibabu.
2.Pumu hatari isiyobadilika (status asthmaticus): Hii ni aina ya pumu iliyo hatari zaidi kwa mgonjwa. Pamoja na

matumizi ya dawa kadhaa,zikiwemo vitanua njia za hewa (bronchodilators) na vipoza mcharuko mwili (steroids), mgonjwa wa aina hii ya pumu anaweza asipate nafuu ya haraka, na anaweza kupoteza maisha.
3.Pumu

inayosababishwa na mazoezi (Exercise Induced Asthma): Hali hii husababishwa na ufanyaji wa kupitiliza wa mazoezi ya viungo. Kwa kawaida wakati wa kufanya mazoezi mtu hupumua kwa kutumia pua na kupitia mdomoni. Hata hivyo wakati

mwingine hutokea hewa aivutayo huingia ndani ikiwa haijapozwa vya kutosha puani na hivyo kusababisha ongezeko la mtiririko wa damu katika mishipa inayosambaza damu katika mirija ya kupitisha hewa. Hali hii husababisha kuvimba

kwa kuta za mirija hiyo na muhusika kupata shambulizi la pumu. Aina hii ya pumu yaweza kudhibitiwa na dawa. Inashauriwa sana kwa watu wenye matatizo kama haya kupasha moto misuli kwa mazoezi mepesi (warming up) kabla

ya kuanza mazoezi mazito na ya muda mrefu.
4. Pumu inayosababishwa na aina ya kazi afanyayo muhusika (Occupational Induced Asthma): Wakati fulani, mazingira ya kazi yanaweza kusababisha kutokea kwa pumu hata kwa baadhi ya wafanyakazi wasio na tatizo hili. Mara nyingi aina hii huweza kuwatokea watu wanaofanya kazi kwenye viwanda vya kutengeneza matairi, vigae, rangi, kemikali mbalimbali, mbolea, chuma, unga na mbao.

Pumu husababishwa na nini?
Kuna mambo kadhaa yanayoweza kusababisha kutokea kwa pumu au yanayohusishwa na shambulizi lake. Mambo hayo ni pamoja na

  1. Matatizo ya kinasaba: Matatizo ya kinasaba yamehusishwa na kutokea kwa karibu asilimia 90 ya ugonjwa wa pumu hususani kipindi cha utoto.
  2. Uvutaji wa sigara au tumbaku kipindi cha ujauzito pia unahusishwa na kusababisha pumu kwa mtoto atakayezaliwa.
  3. Maendeleo ya kiuchumi: Ugonjwa wa pumu umeonekana sana kwenye nchi zilizoendelea kiuchumi ikilinganishwa na nchi zenye maendeleo na hali duni ya kiuchumi.
  4. Magonjwa ya mapafu kama bronchitis
  5. Vyanzo vya mzio (allergens)kama vile vumbi, vinyesi vya wanyama na baadhi ya vyakula.
  6. Uchafuzi wa mazingira kama moshi na baadhi ya harufu kali.
  7. Baadhi ya kemikali kwenye maeneo ya kazi hasa kwenye viwanda kama vya rangi, chuma, sementi na vigae.
  8. Baadhi ya wagonjwa wanaotumia dawa za kushusha shinikizo la damu zilizo katika jamii ya beta-blockers kama vile propanolol wapo katika hatari ya kupata shambulio la ugonjwa wa pumu.
  9. Magonjwa kwenye mfumo wa kupumua yasabishwayo na baadhi ya virusi na bakteria kama vile rhinovirus, Chlamydia pneumonia au Bordetella pertusis.
  10. Matumizi ya mapema sana ya baadhi ya dawa hasa antibiotiki kwa watoto yanaweza kubadilisha mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa na hivyo kumfanya mtoto kuwa katika hatari ya kupata pumu.
  11. Ongezeko la msongo wa mawazo huweza kusababisha pumu na matatizo katika mfumo wa upumuaji
  12. Upasuaji wakati wa kujifungua (caesarian section): Tafiti kadhaa zimeonesha kuwa kujifungua kwa njia ya upasuaji huongeza uwezekano wa kupata pumu kwa vile njia hiyo yaweza kuathiri mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya maradhi.
Vihatarishi vya ugonjwa wa pumu
Uwezekano wa kupata ugonjwa wa pumu huongezeka iwapo mtu

  1. Atakuwa na magonjwa ya mzio kama vile magonjwa ya ngozi (eczema) au homa isababishwayo na aina fulani ya vumbi (hay fever)
  2. Atavuta chavu (pollen) kutoka kwenye maua au miti
  3. Atajihusisha na uvutaji sigara
  4. Ana historia ya ugonjwa wa pumu au mzio kwenye familia
  5. Utumiaji wa dawa aina ya aspirin
  6. Ana msongo wa mawazo
  7. Ana uambukizi wa magonjwa ya virusi kamarhinovirus
  8. Mazoezi
  9. Anaishi sehemu zenye baridi
  10. Ana matatizo katika njia yake ya chakula (Gastroesophageal reflux disease au GERD)

Dalili za ugonjwa wa pumu
Dalili za ugonjwa wa pumu ni pamoja na

  1. Kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida (shortness of breath)
  2. Kutoa sauti kama mtu anayepiga miluzi wakati wa kupumua (wheezing)
  3. Kukohoa sana (chronic cough) hasa nyakati za usiku au asubuhi. Aidha kikohozi huambatana na kutoa makohozi mazito, yasiyo na rangi au yenye rangi ya njano.
  4. Kubana kwa kifua.
  5. Kwa mtu aliyepata shambulizi kubwa la pumu (severe asthmatic attack) anaweza kushindwa kuzungumza na pia kuwa na hali kama ya kuchanganyikiwa.
Vipimo na Uchunguzi
Pamoja na daktari kutaka kufahamu historia ya mgonjwa, anaweza pia kuamua kufanya vipimo vifuatavyo ambavyo vitamsaidia kufahamu chanzo na madhara ya ugonjwa wa pumu kwa muathirika.

  1. Kipimo cha damu (complete blood count) msisitizo ukiwa kwenye wingi wa seli za damu aina ya eosinophils ambazo uhusika na kuwepo kwa shambulio la mzio.
  2. Kipimo cha kuchunguza uwezo wa mgonjwa kutoa hewa nje mara baada ya kuivuta (spirometery). Aina hii ya uchunguzi hufanyika kabla ya mgonjwa kupewa dawa kwa kutumia nebulizer.
  3. Kipimo cha kuchunguza kiwango cha hewa ya oksijeni kilichopo kwenye damu ya mgonjwa (oximetry).
  4. Kipimo cha kuchunguza uwezo wa mgonjwa kupumua hewa nje wakati wa shambulizi la pumu (Peak flow meter).
  5. X-ray ya kifua kwa ajili ya kutofautisha pumu na magonjwa mengine yenye dalili za kufanana kama vile ugonjwa wa moyo (congestive heart failure), magonjwa sugu ya kuziba kwa njia za hewa (COPD kama vile chronic bronchitis na emphysema) na magonjwa mengine ya kuzaliwa kama vile cystic fibrosis.
  6. Kipimo cha mzio cha ngozi (skin allergy test) kwa ajili ya kutambua aina ya mzio inayomsababishia mgonjwa shambulizi la pumu.

Matibabu ya Pumu
Kwa ujumla matibabu ya pumu hujumuisha kuepuka visababishi vya ugonjwa huu na matumizi ya madawa kwa walio na hali mbaya. Aidha, kwa wanaopata ugonjwa huu kwa sababu ya msongo wa mawazo hupewa ushauri nasaha kwa ajili ya

kusaidia kutatua matatizo yanayowakabili. Vilevile inashauriwa kwa wenye tatizo hili, kuwa na dawa karibu muda wote kwa ajili ya matumizi pindi shambulizi litakapotokea. Pia inashauriwa sana kuepuka mazingira na hali za baridi ambazo

huweza kuchochea kutokea kwa shambulio la ugonjwa huu. Matibabu ya kutumia dawa hujumuisha matumizi ya dawa za kusaidia kupunguza na kuondoa makohozi (expectorants), dawa zinazosaidia kutanua mirija ya hewa (bronchodilators), dawa za kuondoa mcharuko mwili kama vile cortisone ya drip (hasa wakati wa dharura) au nebulizer, na dawa za kuzuia

mzio (antihistamine drugs).
Hata hivyo, kuna matibabu ya ziada kulingana na hali ya mgonjwa pamoja na kundi na aina ya pumu inayomuathiri mgonjwa. Kwa wagonjwa wenye pumu ya ghafla na wenye hali mbaya (acute asthma) matibabu hujumuisha matumizi ya dawa za kutanua mirija ya hewa (bronchodilators) pamoja na kuongezewa hewa ya

oksijeni, dawa za kutuliza mcharuko mwili (steroids) pamoja na dawa za kutuliza kukakamaa kwa misuli ya mwili (intravenous muscle relaxants). Aidha kwa vile mara nyingi shambulizi hili laweza kuwa la hatari sana, mgonjwa hulazwa

hospitali na huongezewa hewa ya oksijeni, na kwa wagonjwa wasioweza kupumua kabisa, husaidiwa kufanya hivyo kwa kutumia mashine maalum iitwayo (mechanical ventilator).
Kwa wagonjwa wenye pumu sugu, jambo la muhimu ni

kuepuka visababishi vya pumu na kuendelea na matumizi ya dawa zinazosaidia katika kutanua mirija ya hewa. Kwa wagonjwa wanaopata mashambulzi ya mara kwa mara wanaweza kushauriwa na daktari kutumia dawa kadhaa zikiwemo zile zinazopunguza mcharuko mwili (mast cell inhibitors, inhaled steroids au oral steroids), pamoja na dawa za

kutuliza kukakamaa kwa misuli ya mwili (muscle relaxants). Aidha ni vema pia kutibiwa na kuthibiti kutokea kwa magonjwa yote yahusuyo mfumo wa hewa. Matumizi ya chanjo ya magonjwa kama influenza na pneumococcal pneumonia nayo husaidia sana katika uthibiti wa kutokea kwa pumu. Ni vema pia kuepuka matumizi ya dawa za jamii ya beta-blockers kwa wagonjwa wenye shinikizo la damu na ambao pia wana pumu.


Nini madhara ya pumu kwa mama wajawazito?
Tafiti kadhaa zimeonesha kuwa takribani theluthi moja ya wajawazito wenye pumu hupata nafuu kipindi cha ujauzito, theluthi nyingine hupata matatizo kipindi hiki na theluthi iliyobakia huwa na hali ya kawaida kama kabla ya ujauzito.

Kwa kawaida dalili za pumu hujirudia kama awali miezi mitatu baada ya kujifungua.
Dalili za pumu kwa mjamzito zinaweza kuwa mbaya zaidi kuanzia wiki ya 24-36 (mwezi wa sita mpaka wa nane). Ni mara chache sana mjamzito

anapata shambulizi la pumu wakati wa kujifungua. Inakisiwa kuwa, ni asilimia 10 tu ya wajawazito wenye pumu wanaopata shambulizi la pumu wakati wa kujifungua.
Baadhi ya dawa zinazotumika wakati wa ujauzito na baada ya

kujifungua huongeza madhara ya pumu, hivyo ni vizuri kumueleza daktari kwamba una pumu kabla ya kupewa dawa. Aidha na si vyema kunywa dawa kwa mazoea.
Wanawake wenye pumu isiyoweza kuthibitiwa kipindi cha ujauzito

hupata madhara ya kuzaa mtoto njiti (premature baby), kuzaa mtoto mwenye uzito mdogo, kifafa cha mimba, shinikizo la damu (Hypertension), na iwapo atapata shambulizi hatari wakati wa ujauzito mtoto anaweza kufa kwa kukosa hewa ya oksijeni.



UGONJWA WA PUMU (ASTHMA) KWA WATOTO

asthma-1_wide-2f768a58a50dce7303f873c7dde31c188555d08.jpg

Nini maana ya Pumu?
Pumu ni hali ambayo huathiri njia za hewa, njia hizi za hewa pia huitwa mirija ya kupumulia. Mirija hii huanzia kwenye njia ya hewa(trachea) hadi kwenye mapafu.

Mchakato wa kupumua kwa watoto walio wengi ni rahisi : Watoto huingiza hewa kupitia puani au mdomoni na hewa huingia kwenye njia ya hewa(trachea) na kuelekea kwenye mapafu. Lakini Kwa watoto wenye pumu, hupumua Kwa shida Kwa sababu njia ya hewa hushindwa kupitisha hewa kwa sababu ya njia yao kuwa imehathiriwa na hali ya pumu.

Shambulio la pumu (Asthma attack) ni nini?
Hii ni hali ambayo hutokea wakati njia ya hewa inapo vimba na kuwa nyembamba na inakuwa vigumu kwa hewa kuingia na kutoka kwenye mapafu. Wakati mwingine njia za hewa zinapokuwa zimevimba hutoa majimaji mfano wa makamasi, hali ambayo husababisha mchakato mzima wa mabadlishano ya hewa katika mapafu kuwa mgumu na hii hali ndo inapelekea tatizo zima la mtotoanapo patwa na pumu kushindwa kupumua vizuri.

Wakati ugonjwa huu unaanza, upumuaji kwa mtoto unaweza kuwa wa kawaida na kuonekana kama vile hakuna tatizo, Lakini kipindi ugonjwa unapoanza, unaweza kuhisi kwamba mtu anapumua kupitia kwenye mrija. Mtoto mwenye pumu anaweza kutoa mlio kama wa filimbi (anapopumua), kukohoa, na kusikia kifua kubana.

Wakati shambulio la ugonjwa wa pumu(asthma attack), hali inaweza kuwa mbaya zaidi kama mtoto hatatumia dawa sahii za pumu. Baada ya kutumia dawa na kupata matibau sahii wakati wa shambulio la ugonjwa wa pumu, njia ya hewa mara nyingi hurudia hali yake ya kawaida, ingawa inaweza kuchukua muda mrefu kidogo wakati mwingine.

Pumu huwapata watu gani?
Pumu ni ugonjwa ambao huwapata watu wengi zaidi ya unavyo weza kufikiri.Karibia watoto milioni sita nchini marekani wanaumwa ugonjwa wa pumu(Hatujui hapa kwetu Tanzania ni idadi gani?).Ugonjwa wa pumu humpata mtoto mmoja hadi wawili katika kila watoto 10 kwa marekani. Hii ina maana kwamba kama una watoto 20 darasani, watoto 2-4 kati yao wanaweza kuwa na ugonjwa wa pumu. Ugonjwa wa pumu unaweza kumshika mtu katika umri wowote- kuanzia mtoto mchanga hadi mtu mzima-lakini huwashika zaidi watoto wenye umri wa kwenda shule(kuanzia miaka sita na kuendelea)

Hakuna anayejua kwa uhakika kwa nini ugonjwa huu unampata mtu mmoja na kuacha mwingine, lakini tunajua kwamba ugonjwa wa pumu unatokea ndani ya familia zetu. Hii ina maana kwamba kama mtoto ana pumu, yeye pia anaweza kuwa na mzazi, ndugu, mjomba au jamaa mwingine mwenye pumu au alikuwa na ugonjwa huu wakati bado mtoto.

Ugonjwa wa pumu unapoanza,huonyesha kama vile ni mafua,ambayo huambatana na kikohozi chenye kutoa mlio wa filimbi,lakini ugonjwa wa pumu siyo wa kuambukizwa. Huwezi kuambukizwa Kama unavyopata mafua


Ni sababbu zipi zinazopelekea Kupata shambulio la ugonjwa wa pumu (Asthma attack)?
Visababishi hutofautiana kutoka mtoto mmoja hadi mwingine. Sababu zipo nyingi.Baadhi ya watoto huwa na mzio(allergy), kwa vile vitu ambavyo huathiri njia ya hewa. Mara nyingi vitu vinavyoleta mzio kwa watoto wenye pumu ni vijidudu vidogo jamii ya mchwa vinavyopatikana kwenye vumbi, harufu mbaya (kama ulikuwa karibu na dimbwi na kuvuta harufu hiyo), mbelewele(pollen) kutoka mitini, majani na kwenye magugu.

Watoto wengi hupata shambulio la pumu wanapokuwa karibu na wanyama wenye manyoya kama Paka na mbwa,baadhi watoto wanapovuta hewa iliyochanganyika na chembechembe za manyoya hawa wanaweza pata shambulio la pumu.

Visababishi vingine ni pamoja na marashi(perfumes), vumbi la chaki, na uvutaji wa sigara. Uvutaji wa sigara sio mzuri hasa kwa mtu mwenye pumu.

Wakati mwingine maambukizi mbalimbali yanaweza kusababisha kulipuka kwa ugonjwa wa pumu,maradhi kama mafua, Kwa baadhi ya watoto, hali ya hewa yenye baridi inaweza kusababisha kulipuka kwa ugonjwa huo,baadhi ya watoto hupatwa na matatizo ya pumu wanapokuwa wanafanya mazoezi,hii ni aina ya pumu inayosababishwa na mazoezi.

Jinsi gani unaweza kutibu ugonjwa wa pumu kwa watoto?
Watoto wenye ugonjwa wa pumu wanatakiwa kujaribu kuepuka visababishi vyote vinavyoweza kuwasababishia shambulio la hewa.Ingawa kuna baadhi ya visababishi kama vumbi la chaki ni vigumu kuviepuka katika mzaizngira yetu hasa shuleni,lakini mtoto,wazazi na walimu wajaribu kuwasaidia watoto wenye matatizo haya.

Sura ya ugonjwa wa pumu hutofautiana kutoka kwa mtoto mmoja hadi mwingine, hivyo kuna dawa mbalimbali za kutibu ugonjwa wa pumu,na matibabu haya hutofautiana kati ya mtoto mmoja na mwingine hii ni baada yake daktari kujaribu kufuatilia sababu zilizopelekea ugonjwa huo, ni kwa kasi gani ugonjwa umetokea, na kiwango cha madhara ya ugonjwa huo. Hapo ndipo ataamua tiba ipi itakuwa sahii na bora kwa mtoto.

Baadhi ya watoto wanatakiwa wameze dawa za pumu mara kwa mara punde wanapopata ugonjwa huu. Hii huitwa dawa ya dharura kwa sababu hufanya kazi ya kufungua njia ya hewa ili mtu aweze kupumua. Watoto wengine wanatakiwa kutumia dawa za kudhibiti ugonjwa wa pumu kila siku,Dawa hizi huzuia shambulio la ugonjwa(asthma attack) kutokea.Kwa hiyo matibabu ya Pumu yanatofautina kutoka mtoto mmoja na mwingine.

Kwa watoto walio wengi ugonjwa wa pumu hupona au hupata nafuu wanapokua wakubwa. Baadhi ya madaktari wanadai kwamba hii hutokea kwa sababu, njia ya hewa hupanuka kadri mtoto anavyokua mkubwa. Njia ya hewa inapopanuka, hewa huingia na kutoka kiurahisi

Baadhi ya watu wazima hupata ugonjwa wa pumu, lakini hii haiwasumbui.Wanariadha wengi katika mbio za olimpiki na magwiji wengine wa michezo wanaweza kuendelea na michezo hata wanapokuwa na ugonjwa wa pumu.

UJUMBE WA KUPELEKA NYUMBANI:
Mzazi au mlezi anayeona mtoto mwenye dalili za ugonjwa wa pumu kama nilivyouelezea hapo juu kitu cha kwanza cha kufanya ni kumwaisha Katika kituo chochote cha Afya au Hospitali iliyo karibu nae.

Na kwa wale watoto walikwisha gundulika tayari na ugonjwa huu wa Pumu ni kuhakikisha wanafuta masharti yote ya Matibabu ili kuzuia shambulio la ugonjwa huu.

Mtoto anayejua mapema kwamba kuna vitu vinamletea madhara katika njia ya hewa au sababu nyingine anaweza kutumia dawa mapema zitakazosaidia kufanya njia ya hewa iendelee kuwa wazi.Mtoto ambaye hupata pumu anapofanya mazoezi anaweza kutumia dawa kabla ya kufanya mazoezi ili waweze kumaliza mbio au michezo vizuri.

Kwa watoto walio wengi ugonjwa wa pumu hupona au hupata nafuu wanapokua wakubwa. Baadhi ya madaktari wanadai kwamba hii hutokea kwa sababu, njia ya hewa hupanuka kadri mtoto anavyokua mkubwa. Njia ya hewa inapopanuka, hewa huingia na kutoka kiurahisi

Baadhi ya watu wazima hupata ugonjwa wa pumu, lakini hii haiwasumbui.Wanariadha wengi katika mbio za olimpiki na magwiji wengine wa michezo wanaweza kuendelea na michezo hata wanapokuwa na ugonjwa wa pumu.



MICHANGO YA WADAU (BAADHI NI WAHANGA) WA UGONJWA HUU
MIMI NINA PUMU YA NGOZI, IMEPUNGUA KUTOKANA NA UMRI

Poleni sana. Pumu ya ngozi ipo.

Mie ninayo. Kawaida it's on and off inategemea na allergic reaction. I was advised to stop taking eggs and fish kwani zinaongeza sana joto mwilini. I was treated with Nerisone Cream, zipo tatu, cream, ointment na pommade. Ni tabu sana kupatikana kwake.

Nilikuwa natibiwa na Prof. Masawe wa MNH, he is a skin specialist. Nilishauriwa kuvaa cotton outfits, nioge kwa sabuni mbuni kwani perfumed soaps zinasababisha nawashwa sana ngozi na kupiga chafya sana.

I used to scratch myself a lot, nikoga kwa maji baridi hali inakuwa mbaya zaidi najikuna kupita kiasi. Nilifanyiwa allergy test na Dr. Mboneko naye wa MNH ila Saturdays anakuwa Luther house. Jaribu kuwaona hao kwa ushauri zaidi.

Once when I was young, a Chinese Dr. advised me to take at least 16 glasses of water everyday, sikuweza. Ila he said, as I grow older tatizo linapungua, ni kweli limepungua ila halijaisha. Siruhusiwi kutumia hair chemicals, perfumes, etc kwani muwasho huongezeka, lakini kusema kweli, I use perfumes making sure they don't touch my skin kwa sababu I have a sensitive skin. Jaribu kuwaona kwa ushauri zaidi.

Inabidi wazazi muwe waangalifu na perfumes zenu zisimpate mtoto or any other cosmetics zinazoweza kumuongezea reaction.

Ukweli ni kwamba natumia dawa hadi leo, ila nikiona nimevimba sana, i apply the ointment, ikiishia au kupungua,naacha kabisa,it's on and off and very tiring too. usafi inabidi uwe wa hali ya juu.

Poleni sana, please consult the above mentioned Dr.s.
SUALA LA NGUO NA PUMU

Nikisisitiza swala la nguo.

Hakikisha mashuka ya mtoto ni 100% cotton, kuna mashuka yasiyokuwa ya cotton, yanasababisha kuwashwa.

Ikibidi kuvaa sweater liwe la material inaitwa flunnel kwani wool inasababisha ngozi iwashe.
Blanket material haifai kwake, atumie something in cotton.

Hakikisha nguo yake yoyote ile iwe 100% cotton kwani itamgusa ngozi atawashwa tu. From my experience, taulo pia linaniwasha, unapojifuta it's like you are stimulating the itchy skin, so dry the baby using a cotton/flunnel material uwe kama unam-sponge sio kufuta, ukifuta the sensitive skin becomes itchy again.

Wakati wa kuoga, usitumie dodoki, it's too rough for the skin and the itchiness worsens! Vizuri don't scrub the child kabisa, make sure you apply the mbuni soap thoroughly ili atakate vizuri. Mpake Vaseline Blue Seal not perfumed lotions or body butter.

If the skin becomes too dry it cracks na kutoa damu. Pumu ya ngozi need to be handled with a lot of care and patience. If you need to know something niulize, i live with it for many years now!

Poleni sana.
NILISHAURIWA NIKAFANYA MAZOEZI, NI MUDA SASA HAIJANI-ATTACK

Ndugu inatibika,

I used to be asthmatic. Ilinitesa sana nilipokuwa mdogo, sindano za masaa, vidonge vile vya salbutamol, kukosa shule, afu baadae nilipokua kidogo zikaja hizi inhalers. Zilisadia wen i had an attack, lakini hazikuponyesha!

Siku moja rafiki yangu (tukiwa form 5 Majengo Sec. Moshi)akaniambia wewe na hizo dawa si utakuwa addict? Akanipa stori ya brother ake alikuwa na pumu na hakutumia dawa yeyote!

The only thing alifanya ni kwenda gym, mazoezi ya kufa mtu na sasa ivi u will neva believe, amepona. So, nikasema y nt giv it a try maana mi nlichoka enzi izo unapiga PCM afu unashindwa kwenda shule, inauma!

Nikaingia gym, palepale maeneo ya Majengo kila siku..mdgomdogo (samtymz unakata tamaa), weekends naenda kukimbia au kucheza mpira uwanja wa ushirika (now MUCCoBS)..na bado kifua kilikua kinabana. But hata sijui nisemeje, after sometime, nilijikuta tu kimeacha! since then..trust me..sijapatwa attack yoyote na sijaacha mazoezi!

Observation:
Watoto wengi wenye pumu wanakuwa reserved and antisocial..hali hiyo inawafanya wasiparticipate in sporting and other extracurricular activities. Little do they know that their chests need the exercise to expand. So, kwa ushauri tu, hakikisha wanao wanafanya mazoezi frequently..wasiogope kupata ataack because in the long itaisha.

Hakikisha hawawi addicted!!! please!!! Nilipata wanafunzi wawili nilipoenda chuoni, yani wao wakipanda ngazi floor moja tu wanapuliza kale kakitu..mpaka nikawaonea huruma. but wao walikuwa beyond help! don't let your kid reach that stage..It can be controlled.
One last thing, check on their diet..more fat means more attacks!
Thanks.

*Above all, hakikisha unawaombea sana kwa Mungu maana yeye anaweza yote!!!
LISHE YA MGONJWA WA PUMU (ASTHMA)

Baadhi ya vyakula vinavyoaminika kutoa ahueni na kuwa kama tiba kwa mgonjwa wa pumu ni pamoja na asali, juisi ya limau, mchanganyiko wa vitunguu swaumu na maziwa na mchangayiko wa abdalasini pamoja na asali. Vyakula hivyo vikiwa sehemu ya mlo wa mgonjwa kila siku, atapata ahueni ya ajabu. Pamoja na kuepuka ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, mgonjwa wa pumu anatakiwa pia kula kwa kiasi kidogo mlo wenye matunda, mboga za majani na vyakula vingine vitokanavyo na nafaka ambavyo hutoa ‘alikalaini'.

Aidha, wagonjwa wa pumu wanatakiwa kujiepusha na ulaji wa kiasi kikubwa cha wali, sukari, mtindi (yoghurt), unywaji mwingi wa chai, kahawa, pombe na vyakula vote vya kusindika au kwenye makopo. Mgonjwa anashauriwa pia kufanya mazoezi ya kuvuta hewa safi na kuishi katika hali ya hewa isiyo na baridi, kunywa maji mengi mara kwa mara, kufunga kula (fasting) japo mara moja kwa wiki. Kwa kufuata masharti hayo, mgonjwa anaweza kuishi na pumu bila kusumbuliwa wala kutumia dawa kali kwa maisha yake yote.

Pia unatakiwa kuepuka kufanya mazoezi kwenye baridi, epuka moshi wa sigara, dhibiti ugonjwa wa kucheua na kiungulia, epuka kukaa na wanyama na epuka kuishi katika mazingira yenye hewa yenye unyevunyevu.
ASTHMA HAIPONI MOJA KWA MOJA

Asthma haitibiki ukapona kabisaaa, ila huwa tunatibu zile attacks kuepusha kifo au madhara mengine makubwa ya njia ya hewa, kwa kutumia dawa ambazo zinaeffect ya kupanua njia za hewa (bronchodilators) - Dr. RIWA''. Hivyo ndivyo alivyoandika daktari wetu mpendwa dr.Riwa katika kuchangia thread hii.

Kwanini huwezi kupona kabisa pumu?, ni kwa sababu Mwili wa binadamu unapopungukiwa maji hutoa ishara (indicators), tumeziita ishara hizo kuwa ni magonjwa, hauumwi, una kiu, usiitibu kiu kwa madawa.

Siyo pumu pekee isiyotibika kabisa. Watu wengi wenye Mzio (allergy), shinikizo la damu (BP), kisukari (diabetis), Upungufu wa kinga mwilini (ukimwi) na magonjwa mengi wanabaki nayo katika safari yao ya kuishi. Dawa nyingi hospitali hupunguza maumivu na kuahirisha tatizo kidogo lakini mwili utaendelea kuleta ishara (magonjwa) za kupungukiwa maji moja baada ya nyingine mpaka hapo utakapoupa mwili kile unachokihitaji.

Ni dhana ya zamani kusubiri kiu ndipo unywe maji na huku unajuwa kuwa maji ni uhai. Kwa kutumia maji watu wengi wamepona kabisa pumu na kusahau kutumia inhalers. Tembelea maajabuyamaji2.artisteer.net ujifunze namna ya kunywa na kutumia maji ili kujitibu ugonjwa wowote.
IFAHAMU PUMU

Pumu ni hali ambayo huathiri njia za hewa, njia hizi za hewa pia huitwa mirija ya kupumulia. Mirija hii huanzia kwenye njia ya hewa(trachea) hadi kwenye mapafu.

Mchakato wa kupumua kwa watoto walio wengi ni rahisi : Watoto huingiza hewa kupitia puani au mdomoni na hewa huingia kwenye njia ya hewa(trachea) na kuelekea kwenye mapafu. Lakini Kwa watoto wenye pumu, hupumua Kwa shida Kwa sababu njia ya hewa hushindwa kupitisha hewa kwa sababu ya njia yao kuwa imehathiriwa na hali ya pumu.

Shambulio la pumu (Asthma attack) ni nini?
Hii ni hali ambayo hutokea wakati njia ya hewa inapo vimba na kuwa nyembamba na inakuwa vigumu kwa hewa kuingia na kutoka kwenye mapafu. Wakati mwingine njia za hewa zinapokuwa zimevimba hutoa majimaji mfano wa makamasi, hali ambayo husababisha mchakato mzima wa mabadlishano ya hewa katika mapafu kuwa mgumu na hii hali ndo inapelekea tatizo zima la mtotoanapo patwa na pumu kushindwa kupumua vizuri.

Wakati ugonjwa huu unaanza, upumuaji kwa mtoto unaweza kuwa wa kawaida na kuonekana kama vile hakuna tatizo, Lakini kipindi ugonjwa unapoanza, unaweza kuhisi kwamba mtu anapumua kupitia kwenye mrija. Mtoto mwenye pumu anaweza kutoa mlio kama wa filimbi (anapopumua), kukohoa, na kusikia kifua kubana.

Wakati shambulio la ugonjwa wa pumu(asthma attack), hali inaweza kuwa mbaya zaidi kama mtoto hatatumia dawa sahii za pumu. Baada ya kutumia dawa na kupata matibau sahii wakati wa shambulio la ugonjwa wa pumu, njia ya hewa mara nyingi hurudia hali yake ya kawaida, ingawa inaweza kuchukua muda mrefu kidogo wakati mwingine.

Pumu huwapata watu gani?
Pumu ni ugonjwa ambao huwapata watu wengi zaidi ya unavyo weza kufikiri.Karibia watoto milioni sita nchini marekani wanaumwa ugonjwa wa pumu(Hatujui hapa kwetu Tanzania ni idadi gani?).Ugonjwa wa pumu humpata mtoto mmoja hadi wawili katika kila watoto 10 kwa marekani. Hii ina maana kwamba kama una watoto 20 darasani, watoto 2-4 kati yao wanaweza kuwa na ugonjwa wa pumu. Ugonjwa wa pumu unaweza kumshika mtu katika umri wowote- kuanzia mtoto mchanga hadi mtu mzima-lakini huwashika zaidi watoto wenye umri wa kwenda shule(kuanzia miaka sita na kuendelea)

Hakuna anayejua kwa uhakika kwa nini ugonjwa huu unampata mtu mmoja na kuacha mwingine, lakini tunajua kwamba ugonjwa wa pumu unatokea ndani ya familia zetu. Hii ina maana kwamba kama mtoto ana pumu, yeye pia anaweza kuwa na mzazi, ndugu, mjomba au jamaa mwingine mwenye pumu au alikuwa na ugonjwa huu wakati bado mtoto.

Ugonjwa wa pumu unapoanza,huonyesha kama vile ni mafua,ambayo huambatana na kikohozi chenye kutoa mlio wa filimbi,lakini ugonjwa wa pumu siyo wa kuambukizwa. Huwezi kuambukizwa Kama unavyopata mafua

Ni sababbu zipi zinazopelekea Kupata shambulio la ugonjwa wa pumu (Asthma attack)?
Visababishi hutofautiana kutoka mtoto mmoja hadi mwingine. Sababu zipo nyingi.Baadhi ya watoto huwa na mzio(allergy), kwa vile vitu ambavyo huathiri njia ya hewa. Mara nyingi vitu vinavyoleta mzio kwa watoto wenye pumu ni vijidudu vidogo jamii ya mchwa vinavyopatikana kwenye vumbi, harufu mbaya (kama ulikuwa karibu na dimbwi na kuvuta harufu hiyo), mbelewele(pollen) kutoka mitini, majani na kwenye magugu.

Watoto wengi hupata shambulio la pumu wanapokuwa karibu na wanyama wenye manyoya kama Paka na mbwa,baadhi watoto wanapovuta hewa iliyochanganyika na chembechembe za manyoya hawa wanaweza pata shambulio la pumu.

Visababishi vingine ni pamoja na marashi(perfumes), vumbi la chaki, na uvutaji wa sigara. Uvutaji wa sigara sio mzuri hasa kwa mtu mwenye pumu.

Wakati mwingine maambukizi mbalimbali yanaweza kusababisha kulipuka kwa ugonjwa wa pumu,maradhi kama mafua, Kwa baadhi ya watoto, hali ya hewa yenye baridi inaweza kusababisha kulipuka kwa ugonjwa huo,baadhi ya watoto hupatwa na matatizo ya pumu wanapokuwa wanafanya mazoezi,hii ni aina ya pumu inayosababishwa na mazoezi.

Jinsi gani unaweza kutibu ugonjwa wa pumu kwa watoto?
Watoto wenye ugonjwa wa pumu wanatakiwa kujaribu kuepuka visababishi vyote vinavyoweza kuwasababishia shambulio la hewa.Ingawa kuna baadhi ya visababishi kama vumbi la chaki ni vigumu kuviepuka katika mzaizngira yetu hasa shuleni,lakini mtoto,wazazi na walimu wajaribu kuwasaidia watoto wenye matatizo haya.

Sura ya ugonjwa wa pumu hutofautiana kutoka kwa mtoto mmoja hadi mwingine, hivyo kuna dawa mbalimbali za kutibu ugonjwa wa pumu,na matibabu haya hutofautiana kati ya mtoto mmoja na mwingine hii ni baada yake daktari kujaribu kufuatilia sababu zilizopelekea ugonjwa huo, ni kwa kasi gani ugonjwa umetokea, na kiwango cha madhara ya ugonjwa huo. Hapo ndipo ataamua tiba ipi itakuwa sahii na bora kwa mtoto.

Baadhi ya watoto wanatakiwa wameze dawa za pumu mara kwa mara punde wanapopata ugonjwa huu. Hii huitwa dawa ya dharura kwa sababu hufanya kazi ya kufungua njia ya hewa ili mtu aweze kupumua. Watoto wengine wanatakiwa kutumia dawa za kudhibiti ugonjwa wa pumu kila siku,Dawa hizi huzuia shambulio la ugonjwa(asthma attack) kutokea.Kwa hiyo matibabu ya Pumu yanatofautina kutoka mtoto mmoja na mwingine.

Kwa watoto walio wengi ugonjwa wa pumu hupona au hupata nafuu wanapokua wakubwa. Baadhi ya madaktari wanadai kwamba hii hutokea kwa sababu, njia ya hewa hupanuka kadri mtoto anavyokua mkubwa. Njia ya hewa inapopanuka, hewa huingia na kutoka kiurahisi

Baadhi ya watu wazima hupata ugonjwa wa pumu, lakini hii haiwasumbui.Wanariadha wengi katika mbio za olimpiki na magwiji wengine wa michezo wanaweza kuendelea na michezo hata wanapokuwa na ugonjwa wa pumu.

UJUMBE WA KUPELEKA NYUMBANI:
Mzazi au mlezi anayeona mtoto mwenye dalili za ugonjwa wa pumu kama nilivyouelezea hapo juu kitu cha kwanza cha kufanya ni kumwaisha Katika kituo chochote cha Afya au Hospitali iliyo karibu nae.

Na kwa wale watoto walikwisha gundulika tayari na ugonjwa huu wa Pumu ni kuhakikisha wanafuta masharti yote ya Matibabu ili kuzuia shambulio la ugonjwa huu.

Mtoto anayejua mapema kwamba kuna vitu vinamletea madhara katika njia ya hewa au sababu nyingine anaweza kutumia dawa mapema zitakazosaidia kufanya njia ya hewa iendelee kuwa wazi.Mtoto ambaye hupata pumu anapofanya mazoezi anaweza kutumia dawa kabla ya kufanya mazoezi ili waweze kumaliza mbio au michezo vizuri.

Kwa watoto walio wengi ugonjwa wa pumu hupona au hupata nafuu wanapokua wakubwa. Baadhi ya madaktari wanadai kwamba hii hutokea kwa sababu, njia ya hewa hupanuka kadri mtoto anavyokua mkubwa. Njia ya hewa inapopanuka, hewa huingia na kutoka kiurahisi

Baadhi ya watu wazima hupata ugonjwa wa pumu, lakini hii haiwasumbui.Wanariadha wengi katika mbio za olimpiki na magwiji wengine wa michezo wanaweza kuendelea na michezo hata wanapokuwa na ugonjwa wa pumu.
NINA PUMU. NIMEPUNGUZA MAKALI KWA NJIA HII
Mimi nina miaka 23 nina pumu tangu siku ya kwanza nimezaliwa wazazi wangu walijitahidi sana hata kutumia miti shamba nimekunywa dawa za kila kabila hadi mafuta ya simba nimekula.

Matokeo inatulia kwa miezi hadi mwaka basi nimekuwa nikiangaika sana hadi ilifikia kipindi sindano siogopi kwa jinsi nilivyozizoea
Mwaka 2008 nilikutana na DR mmoja nikamwambia shida yangu mimi nilkuwa hadi natumia kipumulio kama ikinibana njiani ndio akanipa tiba ambayo ni hii.

Aliniambia kabla pumu haijakubana huo unapata dalili zipi? Nikamwambia hua nawashwa macho,pua, masikio, na koo kukereketa
Basi akaniambia unatakiwa nijisome ndani ya miezi mitatu nitajua dalili zote za kubanwa na pumu.

Akaniambia natakiwa nitumie cetrizen or dazit nyakati za kulala mfululizo miezi miwili alf baada ya hapo nikiwa napata reaction na hali ya hewa ndio niwe na meza au kama nataka kufanya kitu kwenye vumbi basi ninywe kwanza ndio niende ki ukweli tangu hapo mimi aminofilin nimezisahau tangu 2008 kipumulio situmii tena na nilikuwa kila mara na zimia kwa kubanwa na pumu lakini sasa sijabanwa japokuwa inakuja naiwahi natumia hizo dawa za allergy mda mwingine zinakataa mpaka nakohoa mpaka naandika hivi juzi ilinipata reaction ila nimeiwahi haijanibana.

Pumu haina tiba ila ni kujua dalil na kuziwahi mapema kwa mtoto hawezi kujisoma ila mzazi unatakiwa kuwa nae karibu pia unatakiwa usikose syrup ndani na pipi aina ya methodex.
UJUE UGONJWA WA PUMU (ASTHMA)

Utangulizi
Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa sugu ambao huathiri njia za hewa ambazo huingiza na kutoa hewa katika mapafu. Upatapo ugonjwa wa pumu, kuta za ndani za njia ya hewa hupata maumivu (inflammation) na kuvimba.

Maumivu katika njia za hewa huzifanya kujihami kwa kusinyaa na hivyo kupunguza kiasi cha hewa kinachopita kwenda kwenye mapafu. Hali hii husababisha muathirika kutoa mlio kama wa filimbi au mluzi wakati wa kupumua.

Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa sugu lakini unaotibika. Unaweza kudhibitiwa kama vile ugonjwa wa kisukari na moyo unavyoweza kudhibitiwa.

Aina za Pumu
Kuna aina kuu mbili za pumu. Aina ya kwanza ni ile inayoanza mapema (early onset asthma) na aina ya pili ni ile inayochelewa kuanza (late onset asthma).
Kwa kifupi tutaenda kuangalia tofauti chache kati ya aina hizi za pumu.

Pumu inayoanza mapema
Ni kawaida kwa aina hii ya pumu kuanza utotoni na kwa kawaida huwatokea waathirika ambao miili yao hutengeneza kingamwili (antibodies) za IgE.
Waathirika wa aina hii ya pumu hutambuliwa kwa vipimo maalum vya ngozi ambapo huonesha kuathirika kwa asilimia kubwa vipimo hivyo vinapofanywa.

Pia waathirika hawa huwa na matatizo mengine ya mzio (allergic disorders) kama mafua na ukurutu (eczema).

Pumu inayochelewa kuanza
Aina hii ya pumu tofauti na iliyopita huanza katika umri wowote na asilimia kubwa ya waathirika ni watu wazima. Hakuna ushahidi wowote unaohusianisha vizio (allergens) vinavyotokana na mazingira na uwezo wa kusababisha aina hii ya pumu.

Pumu husababishwa na nini?

Bila shaka mpenzi msomaji umekua ukijiuliza swali hili mara kwa mara. Haifahamiki haswa ni sababu zipi zinazopelekea njia za hewa kupata maumivu na hivyo kupelekea mtu kupata pumu.

Vyanzo mbali mbali vinaonyesha kuwa inatokana na mseto wa vitu kama tumbaku, maradhi na baadhi ya vizio.

Pia kuna vitu katika mazingira ambavyo vinaweza kusababisha mtu kushambuliwa na pumu. Vitu kama vile mazoezi, vizio, viwasho (irritants) na maradhi yatokanayo na virusi.

Baadhi ya vizio ni kama vifuatavyo:
-Vumbi
-Mende
-Chavua (pollen) kutoka kwenye miti na majani
-Magamba ya wanyama, manyoya n.k

Viwasho kama:
-Moshi wa sigara
-Uchafuzi wa hewa
-Harufu kali (kutoka kwenye rangi au chakula)
-Msongo wa mawazo

Vingine ni kama:
-Dawa kama Aspirin
-Ugonjwa wa kucheua
-Viwasho au vizio vitokanavyo na kemikali
-Magonjwa ya njia ya hewa n.k

Ieleweke kwamba orodha iliyotajwa hapo juu siyo kamilifu kwa maana kwamba haijasheheni vitu vyote vinavyoweza kuleta dalili za pumu na pia muathirika anaweza kuathirika na kimoja wapo au zaidi.

Vigezo hatarishi

Baadhi ya vigezo hatarishi vinavyoweza kuongeza uwezekano wa kusababisha ugonjwa wa pumu ni pamoja na:

-Kuishi katika miji mikubwa, haswa katikati ya mji ambapo huongeza uwezekano wa kukutana na vizio

-Kuvuta hewa iliyo na moshi

-Kemikali zitokanazo na kilimo, dawa za kutengeneza nywele, rangi, vyuma, plastiki au vifaa vya elektroniki

-Kuwa na mzazi mmoja au wawili wenye pumu
-Kuathirika na maradhi ya mfumo wa hewa kama kikohozi na mafua wakati wa utoto.

-Unene wa kupita kiasi (obesity)

-Ugonjwa wa kucheua na kiungulia (Gastro esophageal reflux disease)

Dalili za Pumu

Baadhi ya dalili za kawaida za ugonjwa wa pumu ni kama zifuatazo:

-Kikohozi: Mara nyingi kikohozi cha pumu huwa kikali nyakati za usiku au alfajiri na hivyo kumfanya mwathirika kutolala vizuri

-Kutoa sauti ya mfano wa mtu anayepiga mluzi au filimbi wakati wa kupumua

-Kifua kubana: Mgonjwa husikia kama kitu kinakandamiza kifuani au wakati mwingine husikia kama mtu amemkalia kifuani.

-Kukosa hewa: Baadhi hujisikia kama hawawezi kupumua na kukosa hewa ya kutosha inayoingia au kutoka kwenye mapafu.

-Kupumua haraka haraka

Ikumbukwe kwamba si watu wote huwa na dalili zilizokwisha tajwa hapo juu na dalili zaweza kutofautiana kati ya mtu na mtu.

Dalili pia zinatofautiana ukali. Wakati kwa mwingine dalili zinakuwa za wastani, wengine zinakuwa za kukera tu au mbaya kiasi cha kumzuia muathirika kufanya shughuli zake za kila siku.

Vile vile wapo wengine ambao dalili zinakuwa mbaya kiasi cha kuhatarisha maisha. Dalili pia zaweza kutofautiana kwa kipindi zinapotokea.

Wengine hupata dalili mara moja tu kwa mwezi, wengine kila wiki na wengine hupata dalili kila siku.

Hata hivyo iwapo muathirika atapata matibabu sahihi anaweza kuishi na dalili chache au bila dalili kabisa.

Uchunguzi

Kipimo cha muhimu katika uchunguzi iwapo mtu ameathirika na pumu ni kuangalia jinsi mapafu yanavyofanya kazi.

Kipimo hicho kijulikanacho kwa lugha ya kitaalamu kama spirometry hutathmini kiasi cha hewa mtu awezacho kukitoa baada ya kuvuta hewa kwa nguvu na kwa haraka kiasi gani.

Viwango huwa chini ya kawaida iwapo njia za hewa zina maumivu na zimesinyaa. Kipimo hicho cha spirometry pia hutumika kutathmini jinsi mgonjwa wa pumu anavyoendelea kupata nafuu au tatizo kuongezeka.

Hata hivyo kipimo hicho ni kwa ajili ya watoto wenye zaidi ya miaka mitano na watu wazima tu.

Baadhi ya vipimo vingine vinavyoweza kufanywa iwapo kipimo cha spirometry hakitaonesha tatizo ni:

Kipimo cha Kizio (Allergy test)

Husadia kugundua iwapo kuna vizio mbalimbali vinavyoathiri mwili wako.

Kipimo cha Mazoezi

Kugundua iwapo kuna mabadiliko yoyote katika njia ya hewa kutokana na mazoezi.

Kipimo cha Ugonjwa wa Kucheua na Kiungulia

Kipimo hiki ni muhimu pia kutokana na uhusiano uliopo kati ya kiungulia, kucheua na ugonjwa wa pumu.

Kipimo cha Picha ya Mapafu (X-ray)

Kipimo hiki pia hutumika kuona iwapo kuna kitu chochote kilichoziba njia ya hewa au kama kuna maradhi yoyote katika mapafu au moyo.

Kutokana na vipimo daktari wako atapata picha ya ukali wa pumu yako na kukuanzishia tiba muafaka.

Matibabu

Kuna aina mbili za matibabu ya pumu. Moja ni ile ya dharura ili kutoa msaada au nafuu ya haraka. Dawa hizi ni zile zinazosaidia kutanua njia za hewa ambazo zimesinyaa (bronchodilators) pia husaidia kuilainisha misuli ya njia za hewa iliyosinyaa ili iweze kutanuka na kuruhusu hewa ya kutosha kuingia.

Ni vizuri kutumia dawa za kuleta nafuu haraka punde uonapo dalili za pumu zilizoorodheshwa hapo juu.

Aina nyingine ya dawa ni zile za muda mrefu. Aina hizi za dawa hutumiwa mara kwa mara kwa kipindi kirefu kuzuia dalili za pumu na mashambulizi.

Watu wenye pumu isiyoisha wanahitaji matumizi ya dawa ya muda mrefu. Kotikosteroidi za kuvuta (inhaled corticosteroids) ni nzuri kwa aina hii ya pumu.

Matibabu ya pumu kwa watoto

Watoto wenye pumu kama ilivyo kwa watu wazima wanapaswa kumwona daktari kwa matibabu. Watoto walio na umri mdogo wanahitaji uangalizi wa wazazi/walezi ili kudhibiti pumu.

Watoto wenye umri mkubwa wanaweza kujifunza wenyewe jinsi ya kutumia dawa chini ya uangalizi mdogo kutoka kwa wazazi.

Matibabu ya pumu kwa watu wazima
Watu wazima wanaweza kutakiwa kupunguza au kuongeza matumizi ya dawa za pumu kutokana na maradhi mengine waliyonayo.

Dawa kama ya kutibu shinikizo la juu la damu, ugonjwa unaotanua mboni ya jicho na kutatiza kuona (glaucoma), aspirini na dawa za maumivu (non steroidal anti inflammatory drugs) huingiliana na utendaji wa dawa za pumu au zenyewe kusababisha pumu.

Matibabu wakati wa ujauzito

Ni muhimu kudhibiti vyema ugonjwa wa pumu wakati wa mimba kwani iwapo utasababisha kusinyaa kwa njia ya hewa basi waweza kupelekea upungufu wa hewa ya oksijeni kwa mtoto hali ambayo ni hatari kwa mtoto.

Dawa nyingi za pumu hazina madhara kwa kichanga hivyo ni muhimu kuendelea na matibabu wakati wa mimba kuliko kuacha.

Kinga

Njia pekee ya kujikinga na pumu ni kuepuka vizio vinavyoweza kusababisha kuanza kwa dalili za pumu. Waweza fanya hivyo kwa kusafisha nyumba kila wiki kupunguza vumbi.

Pia unatakiwa kuepuka kufanya mazoezi kwenye baridi, epuka moshi wa sigara, dhibiti ugonjwa wa kucheua na kiungulia, epuka kukaa na wanyama na epuka kuishi katika mazingira yenye hewa yenye unyevunyevu.

Ushauri

Jinsi ya kumsaidia mtoto mwenye pumu

-Mpeleke kwa daktari kwa uchunguzi wa mara kwa mara na matibabu.

-Mueleweshe kuhusu pumu na jinsi ya kuidhibiti.

-Mueleweshe ajue vitu vinavyoweza kusababisha yeye kupata dalili za pumu na jinsi ya kuepukana navyo.

-Muepushe na moshi wa sigara kwa kutovuta sigara na kutoruhusu watu kuvuta sigara nyumbani kwako.

-Tafuta jinsi ya kumpunguzia mtoto wako kukutana na vizio kama vumbi, chavua, mende n.k

-Hakikisha anatumia dawa kama inavyotakiwa

-Mhimize kufanya mazoezi ya viungo.
 
Pumu ya ngozi? Dah! Kwakweli ndio mara ya kwanza hata mimi kuusikia huo ugonjwa.

Hata hivyo, waweza jifunza zaidi hapa, kwani yaelekea hauna tiba, ila waweza tafuta sababu za kuzuia hiyo allergy inayomletea hizo rashes. Poleni sana jamani.

[edit] Prevention

Since there is no cure for atopic eczema, treatment should mainly involve discovering the triggers of allergic reactions and learning to avoid them.

Diet: Originally controversial, the association of food allergy with atopic dermatitis has now been clearly demonstrated. Many common food allergens can trigger an allergic reaction: such as milk, nuts, cheese, tomatoes, wheat, yeast, soy, and corn. Many of these allergens are common ingredients in grocery store products (especially corn syrup, which is a sugar substitute). Specialty health food stores often carry products that do not contain common allergens. If a child avoids these allergens early on, the frequency of reactions to these later in life is decreased significantly. Breastfeeding is the best way to avoid these problems, but if that is unavailable, then hydrolyzed formulas are preferred to cow's milk.[8]

Environment and Lifestyle: Since dust is a very common allergen and irritant, adults with atopic eczema should likely avoid smoking, as well as the inhalation of dust in general. The dander from the fur of dogs and cats may also trigger an inflammatory response. It is a common misconception that simply removing an animal from a room will prevent an allergic reaction from occurring. A room must be completely free of animal dander in order to prevent an allergic reaction. Anger, stress, and lack of sleep are also factors that are known to aggravate eczema. Excessive heat (especially with humidity) and coldness are known to provoke outbreaks, as well as sudden and extreme temperature swings.

The Scratch Test: An allergy skin-patch or "scratch" test, given by an allergist, can often pinpoint the triggers of allergic reactions. Once the causes of the allergic reactions are discovered, the allergens should be eliminated from the diet, lifestyle, and/or environment. If the eczema is severe, it may take some time (days to weeks depending on the severity) for the body's immune system to begin to settle down after the irritants are withdrawn.

source; Atopic dermatitis - Wikipedia, the free encyclopedia


=====================================================
Vyakula muhimu kwa ajili ya ugonjwa wa pumu
=====================================================

BEST ANTI-ASTHMA FOODS

There might not be a perfect cure for asthma, but we can find many superfoods with a nutrient profile that is particularly well suited for preventing and alleviating asthma symptoms such as shortness of breath, wheezing and chest tightness. Let's take a look at 12 such foods and their asthma fighting qualities.
1. AVOCADOS - is one of the prime source of Glutathione, which has been shown to protect cells against free radical damage and to detoxify foreign substances such as pollutants. Without glutathione, other antioxidants would not be able not function efficiently. Avocados are also a good source of vitamin E, particularly for people whose asthma is linked to a nut allergy (nuts are one of the most common sources of vitamin E). However, if you have been diagnosed with a latex allergy, you may want to be careful with avocados, particularly non-organically grown produce. Many suggests that people who are allergic to latex are often also allergic to avocados and other foods that may contain substances called chitinases. Organically grown avocados not treated with ethylene gas contain lower levels of chitinases.

2. BROCCOLI SPROUTS - are true nutritional treasure and a great addition to yourdiet if you suffer from asthma. A recent study found that the study participantswho ate broccoli sprouts for 3 days had an increase in antioxidant compounds that control the airway inflammation associated with bronchial asthma. The effect was most pronounced in those who ate the most broccoli sprouts. Available at many health food stores and grocery stores, broccoli sprouts makea great addition to salads, soups, salsa-topped dishes, and sandwiches.

3. APPLES - Studies show that apples possess some extraordinary properties that may provide protection against asthma. One study discovered that pregnant women who ate apples protected their child from developing asthma. Another study found that by drinking apple juice daily children could reduce their chance of suffering from wheezing by 50%. These beneficial effects of apples may be linked to their high concentration of bioflavonoids, such as quercetin. Quercetin is known to possess strong anti-histamine, antioxidant, and anti-inflammato ry properties. When buying apples, be sure topurchase organically grown fruit: together with peaches, conventionally grownapples top the list of fruits that contain the highest levels of pesticides and other harmful chemicals.

4. BANANAS - Including bananas in your diet may help you breathe easier. According to a British study, children who ate just one banana a day had a 34% lower chance of developing asthmatic symptoms such as wheezing. The resultswhere not surprising considering that bananas are one of the best sources of pyridoxine, commonly known as vitamin B6. Pyridoxine plays a critical role in the production of adenosine triphosphate (ATP) and cyclic adenosine monophosphate (cAMP), molecules that have been shown to help relax bronchial smooth muscle tissue.

5. GINGER - one of the oldest spices in the world, is well known for its cold treating powers, but it may also help alleviate asthma symptoms. Its asthma fighting properties are thought to be attributable to gingerols, strong anti-inflammato ry substances that also give ginger its distinctive flavor. Fresh ginger, which is said to be the most effective form of ginger, is available year round in the produce section of your local supermarket.

6. SPINACH - Popeye was right about one thing: you'd better eat your spinach! The nutritional profile of spinach makes it an excellent health food and an important functional food to be included in any anti-asthma diet. One study with 68,535 female participants found that women with a high intake of spinach had a lower prevalence of asthma. This is not surprising considering that spinach features a host of important asthma preventing nutrients, including beta-carotene (spinach is one of the best sources of beta-carotene there is), vitamin C, vitamin E, and magnesium. It also has a substantial potassium content in proportion to its calorie content: a 100 calorie serving provides about 40% of the reference daily intake for this important anti-asthma mineral.

7. ROSEMARY - It contains rosmarinic acid, that may help alleviate asthma symptoms due to its strong antioxidant and anti-inflammato ry properties. The antioxidant power of rosmarinic acid is believed to be even stronger than that of vitamin E. In addition, rosmarinic acid encourages cells to create prostacyclins, which help keep the air passages of the lungs open and thus promote easy breathing. Rosemary can be used to flavor fish, roast meats, and tomato sauces, but also fruits, especially oranges.

8. SUNFLOWER SEEDS - are brimming of anti-asthma nutrients, as these mild nutty tasting seeds are loaded with vitamin E, potassium, and magnesium. They are also a good source of selenium, with 1 cup providing more than 1/3 of the recommended daily intake for this important mineral. Furthermore, sunflower seeds are among the seeds and nuts that are least likely to cause allergic reactions in people. But, be careful while consuming them, as they are quite calorie-dense.

9. SWEET POTATOES - are one of the oldest vegetables known to man and one ofthe most nutritious too. Sweet potatoes are one of the foods that are least likely to cause allergic reactions, which is great news since asthma is often linked to allergies. What's more, sweet potatoes contain plenty of vitamin C and potassium as well as unique root proteins which, according to preliminary studies, may have significant antioxidant properties. The pink, orange, and yellow varieties are also one of the most concentrated food sources of beta-carotene (the more intense the color, the more beta-carotene).

10. KALE - This relatively unknown member of the cabbage family is a nutritional powerhouse packed with vitamins and other phytochemicals that have been shown to alleviate symptoms associated with asthma. Not only is kale a great source of vitamin C, it is also one of the most concentrated dietary sources of beta-carotene (kale contains 10 times the beta-carotene of broccoli). Kale can be eaten raw, for example as a substitute for iceberg lettucein salads. The beautiful green leaves of kale can also be transformed into a savory warm dish by sautéing the leaves and mixing them with chopped onions, crushed garlic and a drizzle of extra virgin olive oil.

11. TURMERIC - a spice that lends its yellow color to curries and many other foods, has long been used in traditional Asian medicine to treat asthma and many other conditions and diseases. In recent years, western medicine has started to pay greater attention to this extraordinary spice. Recent research suggests that turmeric possesses strong anti-inflammato ry properties. Although best known for its use in Indian style curries, turmeric can also be used to add flavor and color to fish, seafood, meat, rice, vegetable, and pasta dishes.


12. MUSTARD GREENS - Chock-full of antioxidants and nutrients, mustard greens can make an excellent addition to your diet if you are susceptible to asthma attacks. In addition to being one of the best sources of beta-carotene, they provide a good amount of vitamin C and vitamin E. The nutrients in mustard greens can remove free radicals that cause smooth muscle contraction and airway constriction in people with asthma. Moreover, they may aid in the breakdown of histamine. Mustard greens with their distinctly peppery flavor are available throughout the year and can be found in the produce section of your local supermarket.

Like said before, no food can actually "cure" asthma; but only provide relief for asthma symptoms, in a long run of consumption. So, if you are asthmatic, or prone to frequent attacks, don't forget these nutrient-rich foods that may help alleviate your asthma symptoms.
 
Hi JF Doctor/Members,

Nina shida na mwnangu mara ngingi anotokwa vipele vidogo vidogo na vingi sehemu za shingoni na kifuani. Initially we thaought ni some sort of alergic reactions but tulipofika kwa Dk. wa Agha Khan Hosp akatuambia ni pumu ya ngozi na ni ya kurithiwa. We did not understand well na ninaomba kama kuna mwenzangu kwenye hii jf anafhamu lolote kuhusu hili anishauri. Dawa nilizopewa so far sijaona kama zinamsaidia mwanangu.

Pumu ya ngozi

Pole sana.

Pumu ya ngozi (Eczema)

Pumu ya ngozi au kwa kitaalamu Eczema (atopic dermatitis au atopic eczema) ni maradhi ya ngozi ambayo yamefanyiwa utafiti muda mrefu sana na kusema ukweli andiko langu hili halitoweza hata kuandika robo ya yale yanayofahamika kitaalamu kuhusiana na pumu ya ngozi.

Maradhi haya kwa kifupi yamekuwa yakiathiri watoto wengi ulimwenguni na yamekuwa yakisumbua akili za wanasayansi na watabibu kote ulimwengu kwa muda mrefu.

Neno Eczema ambalo ndio jina la maradhi haya kwa kitaalamu ni neno la Kigiriki na linamaanisha kututumka sehemu ya nje ya ngozi, hali ambayo huonekana pale mtoto anapopata maradhi haya.

Maradhi haya ya ngozi yanachangia asilimia arobaini (40) ya maradhi yote ya ngozi yanayoripotiwa hospitalini.

Shambulizi lake

Maradhi haya hushambulia zaidi watoto na huweza kupitiliza mpaka ukubwani, pia lakini kwa wengi huwa yanapungua kadri mtoto anavyokua. Watafiti mbalimbali wanasema kuwa kumekuwa na ongezeko la maradhi haya katika kipindi cha miaka ya usoni hali inayoashiria kuwa maradhi haya ni ya kurithi (atopic eczema)

Karibu asilimia themanini (80) ya wagonjwa wa pumu ya ngozi huanza kuugua maradhi haya wakiwa chini ya umri wa miaka mitano (5). Wagonjwa wengi pia huonyesha dalili za maradhi haya wakiwa na umri chini ya mwaka mmoja.

Maradhi haya pia huweza kujitokeza ukubwani ingawa ni mara chache sana hali hii huonekana.

Maradhi haya huathiri watu wa jinsia zote kwa uwiano sawia yaani wanaume na wanawake.

Dalili zake

Maradhi haya ni ya muda mrefu nikimaanisha kuwa mtu huweza kukaa nayo kwa muda mrefu, ingawa si kuwa muda wote ngozi huonyesha dalili za maradhi. Watu wenye maradhi hupitia vipindi ambavyo ngozi hututumka na kuonyesha dalili za maradhi na vipindi ambavyo ngozi huonekana kama imepona ovyo kutoonyesha dalili yoyote ya maradhi.

Dalili za pumu ya ngozi ni kama zifuatazo:

-Sehemu ya ngozi iliyoathirika huwa inakuwa kavu (inaonekana kavu),

-Sehemu ya ngozi iliyoathirika huwa inatutumuka,

-Ngozi huwasha na kama ukikuna kwa muda mrefu basi hupasuka na kuweza kusababisha vidonda.

-Eneo la ngozi lililoathirika mara nyingine huuma.

-Ngozi huwa inakua na mipasuko inayoweza kuruhusu vimelea vya maradhi kushambulia sehemu za ndani za ngozi.

-Muwasho wa ngozi huwa mkali zaidi nyakati za usiku

-Maeneo yenye athari huwa yanavimba (au kututumka) na kuwa na joto.

-Maeneo ya ngozi yaliyoathirika huweza pia kuwa na malengelenge na hata kutoa majimaji.

Dalili za pumu ya ngozi ni kama zifuatazo:

-Zaidi ya eneo la ngozi kututumka vivimbe pia huweza kuonekana kwenye maeneo ya ngozi yaliyoathirika.

-Bila matibabu ya haraka ngozi inaweza fanya vidonda.

Ingawa maeneo yenye athari huweza kutokea sehemu yoyote ya mwili lakini pumu ya ngozi hupenda kushambulia sehemu zifuatazo

-Mikono hususan eneo baada ya kiwiko kwenda chini

-Miguu

-Viganja vya mikono

-Eneo la nyuma ya magoti (mkunjo wa mguu kwenye eneo la goti)

-Maungio ya mkono kwenye kiwiko

-Shingo

-Sehemu ya juu ya kifua

-Wagonjwa wengine hupata mashambulizi kwenye maeneo yanayozunguka macho na kama mgonjwa atafikisha macho basi maradhi husababisha madhara kwenye macho kutokana na hali ya mgonjwa kukuna macho yake kwa muda mrefu.

-Watoto wengi hupata pumu ya ngozi kwenye uso.

Kujitutumua kwa ngozi huweza kuonekana kwa muda wa siku chache mpaka miezi.

Wagonjwa wa pumu ya ngozi hutofautiana na kwa wengine hupata maradhi sehemu chache tu za mwili wakati wengine hupata sehemu kubwa zaidi za mwili.

Kwa wenye pumu ya ngozi mbaya kabisa sehemu kubwa zaidi ya mwili hututumka na vidonda hutokea pamoja na kutokwa na majimaji kwenye maeneo yenye vidonda.

Bahati mbaya kuhusu maradhi haya ni kuwa eneo la ngozi linapoanza kuonyesha dalili za maradhi haya huanza na umwasho ambao husababisha mgonjwa kujikuna hali ambayo husababisha mikwaruzo kwenye ngozi ambayo nayo husababisha vimelea vya maradhi kuweza kupenya na kusababisha vidonda vikubwa zaidi kutokea kwenye eneo hilo la ngozi. Vidonda vinapotokea husababisha mgonjwa kupata msongo ambao husababisha madhara mengine ya kisaikolojia hasa kama maradhi haya yametokea kwa mtoto mdogo.

Kama hali hii ikitokea kwa mtoto aliye shule basi hata mahudhurio yake shuleni huwa mabaya na hata uwezo wake darasani hupungua.

Sababu za mashambulizi zaidi

-Kuogea maji ya moto kwa muda mrefu

-Kuruhusu ngozi ya mwili kukaa ikiwa kavu kwa muda mrefu (bila kupaka mafuta)

-Kuwa na msongo wa mawazo

-Kubadili joto la mwili (kusafiri kutoka kwenye eneo lenye joto kwenda lenye baridi au kinyume chake)

-Kuvaa mavazi yasiyo ya pamba (cotton)

-Uvutaji wa sigara

-Kukaa kwenye vumbi

-Kukaa kwenye mchanga

-Matumizi ya mafuta ya mwili yanayosababisha mzio wa mwili

-Matumizi ya sabuni zinazosababisha mzio wa mwili

-Ulaji wa chakula kinachosababisha mzio wa mwili (mfano, wale wenye mzio wa vyakula vinavyopatikana kwenye maji/bahari)

Sababu za pumu ngozi

Wanasayansi wanasema kuwa mtu mwenye maradhi haya huzaliwa nayo na kuwa huwa yanarithiwa. Athari za maradhi haya huzidi kutokana na sababu nyingine za ndani au nje ya mwili.

Vitu kama manyoya ya wanyama au mbegu za mimea huweza kusababisha mzio ambao huweza kusababisha madhara makubwa zaidi kutokea kwenye ngozi.

Chanzo: Mwananchi

Pumu ya ngozi? Mie pia sina uhakika ni nini hiyo, lakini bado nadhani ni aina fulani ya allergy kwani allergy pia yarithiwa yakhe.

Na kama ndio hivyo, inategemeana na umri - sometimes jinsi age inavyoongezeka tatizo huisha lenyewe.

Na kuhusu dawa inabidi upate ushauri wa karibu wa wataalam (kwa kumuona mtoto live, sio kwa internet) kwani kumpa sana dawa zingine zaweza kumletea matatizo tena makubwa, hasa zile zenye steroids.

Ni hayo tu.
 
Kuna daktari bingwa wa mambo ya ngozi pale mitaa ya Sokoine Drive kama sikosei, ila jengo ni Luther House, Dar es Salaam.

Unaweza kwenda pale kwa kuweka mihadi ya kuonana naye ni daktari mzuri sana. Ila sina uhakika kama bado yupo ama lah.

Habari ndugu wapendwa WanaJF!

Bila shaka tupo katika msimu wa baridi karibu mikoa yote ya Nchi yetu. Yamkini umekuwa ukiteswa na ugonjwa wa pumu (asthma) kila mara kiasi cha kukata tamaa....
 
Ndugu yangu hiyo ni shida kubwa mimi naifaham kwa mtoto wa nduguwangu kabisa na inapona ikirudi na wataalaam wametuambia tujaribu kumuachisha baadhi ya vyakula, ilitubaini kipi kinamdhuru.na inapomzidia huwwa inamuwasha na kujikuna mpaka dam zinaanza kutoka.na huwa inaachia kwenye umri wa miaka 7 au 8 na saa ingine haiponi kabisa. Kwahiyo ndugu yangu yuko katika kusubiri kama itapona au lah lakini mtoto huwa anasumbuka sana.
 
Nashukuru sana kwa ushauri wenu na ni kweli kabisa huwa anapata shida sana wakati kunapokuwa na joto kali na Dar es salaam is always humidy. Kwa ushauri wenu nitamcheki huyu Dk. wa hapo Luther house and I hope kama tukiweza kujua ni vyakula gani au mazingira gani ya kuepuka then tutam-save mtoto but shida kubwa ni pale anaokuwa nje ya nyumbani especially in school. Ni vigumu sana ku-m-control kwenye mazingira hayo.
 
Hi JF Doctor/Members,

Nina shida na mwnangu mara ngingi anotokwa vipele vidogo vidogo na vingi sehemu za shingoni na kifuani. Initially we thaought ni some sort of alergic reactions but tulipofika kwa Dk. wa Agha Khan Hosp akatuambia ni pumu ya ngozi na ni ya kurithiwa. We did not understand well na ninaomba kama kuna mwenzangu kwenye hii jf anafhamu lolote kuhusu hili anishauri. Dawa nilizopewa so far sijaona kama zinamsaidia mwanangu.
Poleni sana.

Pumu ya ngozi ipo.
Mie ninayo. Kawaida it's on and off inategemea na allergic reaction.
I was advised to stop taking eggs and fish kwani zinaongeza sana joto mwilini.
I was treated with Nerisone Cream, zipo tatu, cream, ointment na pommade.
Ni tabu sana kupatikana kwake.

Nilikuwa natibiwa na Prof. Masawe wa MNH, he is a skin specialist.
Nilishauriwa kuvaa cotton outfits, nioge kwa sabuni mbuni kwani perfumed soaps zinasababisha nawashwa sana ngozi na kupiga chafya sana.

I used to scratch myself a lot, nikoga kwa maji baridi hali inakuwa mbaya zaidi najikuna kupita kiasi. Nilifanyiwa allergy test na Dr. Mboneko naye wa MNH ila Saturdays anakuwa Luther house.
Jaribu kuwaona hao kwa ushauri zaidi.

Once when I was young, a Chinese Dr. advised me to take at least 16 glasses of water everyday, sikuweza. Ila he said, as I grow older tatizo linapungua,ni kweli limepungua ila halijaisha. Siruhusiwi kutumia hair chemicals, perfumes,etc kwani muwasho huongezeka,lakini kusema kweli, I use perfumes making sure they don't touch my skin kwa sababu I have a sensitive skin. Jaribu kuwaona kwa ushauri zaidi.

Inabidi wazazi muwe waangalifu na perfumes zenu zisimpate mtoto or any other cosmetics zinazoweza kumuongezea reaction.

Ukweli ni kwamba natumia dawa hadi leo, ila nikiona nimevimba sana, i apply the ointment, ikiishia au kupungua,naacha kabisa,it's on and off and very tiring too. usafi inabidi uwe wa hali ya juu.

Poleni sana, please consult the above mentioned Dr.s.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Nikisisitiza swala la nguo.

Hakikisha mashuka ya mtoto ni 100% cotton, kuna mashuka yasiyokuwa ya cotton,yanasababisha kuwashwa.

Ikibidi kuvaa sweater liwe la material inaitwa flunnel kwani wool inasababisha ngozi iwashe.
Blanket material haifai kwake, atumie something in cotton.

Hakikisha nguo yake yoyote ile iwe 100% cotton kwani itamgusa ngozi atawashwa tu. From my experience, taulo pia linaniwasha,unapojifuta it's like you are stimulating the itchy skin, so dry the baby using a cotton/flunnel material uwe kama unam-sponge sio kufuta, ukifuta the sensitive skin becomes itchy again.

Wakati wa kuoga,usitumie dodoki,it's too rough for the skin and the itchiness worsens! Vizuri don't scrub the child kabisa,make sure you apply the mbuni soap thoroughly ili atakate vizuri. Mpake Vaseline Blue Seal not perfumed lotions or body butter.

If the skin becomes too dry it cracks na kutoa damu. Pumu ya ngozi need to be handled with a lot of care and patience. If you need to know something niulize, i live with it for many years now!

Poleni sana.
 
I have been athmatic since birth. Is there cure?

.......ndiyohiyo

Asthma not athma has no cure.

However, about 50% of children diagnosed of asthma have spontaneous recovery by adulthood. Spontaneous recovery in adult-onset asthma is unlikely.

Pole ila there are a lot you can do to live normally.

Nasikia Scholes ni Asthmatic!
 
Asthma not athma has no cure.

However, about 50% of children diagnosed of asthma have spontaneous recovery by adulthood. Spontaneous recovery in adult-onset asthma is unlikely.

Pole ila there are a lot you can do to live normally.

Nasikia Scholes ni Asthmatic!

Asante, I am 33 years old, still caught by it periodically. What can I do to live normally?
 
Asante, I am 33 years old, still caught by it periodically. What can I do to live normally?

.......ndiyohiyo

You will probably live with it, pole.

*Identify factors which exacerbate your asthma eg. house dust, strong scents, heavy exertion, etc. and avoid them.

*Compliance to step-by-step prescribed medications; sio leo aminophylline tabs, kesho salbutamol tabs, siku nyingine steroid inhaler, etc.

*Ukihisi dalili za attack pata dawa mapema usisubiri kifua kibane sana.

*Avoid smoking, hata mtu mwingine akivuta wewe inabidi usogee mbali.

*Live normally, meaning punguza hofu juu ya asthma yako kwani hata kwa kuwa na hofu tu waweza kupata attack.

Good luck.
 
Thanx Sunshine, nashukuru sana kwa ushauri wako na pole pia kwa kuishi nayo manake ni kweli kabisa inahitaji uangalifu na uvumilivu wa hali ya juu. Surely nitakutafuta kwa ushauri zaidi na tumeplan tuende kwa huyo Dk. hapo Luther house tuone what we can do to help this litle boy.
 
Asthma Home Remedy Using Garlic And Milk


Conditions Treated: Chronic Illness

Specific Conditions Treated: Asthma

Ingredients Used: Garlic, Milk

Description: Asthma is an ancient Greek word meaning 'panting' or 'short-drawn breath'. It is an allergic condition resulting from the reaction of the body to one or more allergens, and is the most troublesome of respiratory diseases.

An asthma patient gets frequent attacks of breathlessness, in between which he may even be completely normal.

Patients suffering from asthma appear to be gasping for breath, Actually, they have more difficulty in breathing out than breathing m, and this is caused by spasms or sudden involuntary muscular contractions of the smaller air passages in the lungs. The effect is to blow the lungs up because the patient cannot drive the air properly out of the lungs before he has to take another breath. Most asthmatics have more difficulty at night or early morning.

Asthma is caused by a variety of factors. It may be due to an allergy caused by weather conditions, food, drugs, perfumes, and other irritants. Allergies to dust are the must common. Foods which generally cause allergic reactions are wheat, eggs, milk, chocolates, beans, fish, and sea foods. The disease may also result from psychological factors. According to some studies, about twenty-five percent of young asthmatics have a deep-seated emotional insecurity and an intense need for parental love and protection. Heredity also plays an important role.

Modem medical system has not been able to find a cure for this crippling disease. Drugs and vaccines have only limited value in alleviating the symptoms. Most of these are habit forming and the dose has to be increased from time to time to give the same amount of relief. The frequent introduction of drugs in the system, while giving only temporary relief, tends to make asthma chronic and incurable. Allergy, which is the immediate cause of asthma, itself is an indication of lowered resistance and internal disharmony caused by faulty eating and bad habits. This is the root cause and the real cure lies in a return to nature
Directions For Use: Ten garlic cloves, boiled in 30 ml of milk, make an excellent medicine for the early stages of asthma.

This mixture should be taken once daily by the patient. Steaming ginger tea with two minced garlic cloves in it, can also help to keep the problem under control, and should be taken in the morning and evening.
Expected Results Within: 1 month
 
Napenda kuuliza dawa ya athma kwa mtoto wa miaka miwili ni ipi na naweza kupata wapi? Kimsingi nina mtoto wa ndugu yangu anapata sana shida na athma kiasi cha kumuonea huruma. Tusaidiane kama kuna mtu ana uelewa wa dawa za ugonjwa huu hasa zile zisizo umiza kama hujuavyo mtoto mdogo ni mvivu wa kula sasa akipa dawa kali inakuwa tatizo tena.

Asanteni
 
Umeenda hospital? maana dawa hupaswi kunywa tu bila ushauri wa kitabibu.

Nenda Morocco kwa hospital ya Dr. Massawe anashughulikia matatizo ya watoto, inahitaji uvumilivu tu kwenye kusubiri mana foleni ni kubwa ila mtoto wenu atapata kutibiwa na kupewa dawa kwa ushauri wa Doc.. Au kama uko mbali, pia tatufa Doc maeneo mlioko mtapata kumtibu mtoto pia.
 
Umeenda hospital? maana dawa hupaswi kunywa tu bila ushauri wa kitabibu.

Nenda Morocco kwa hospital ya Dr. Massawe anashughulikia matatizo ya watoto, inahitaji uvumilivu tu kwenye kusubiri mana foleni ni kubwa ila mtoto wenu atapata kutibiwa na kupewa dawa kwa ushauri wa Doc.. Au kama uko mbali, pia tatufa Doc maeneo mlioko mtapata kumtibu mtoto pia.

Ngoja nitoe hii habari kwa mhusika ili amcheki Dr. Massawe

Asante belinda
 
lakini inakuwaje mtoto anapoenda kwa daktari ananyimwa kula vitu vifuatavyo kwa ushauri kuwa vinamletea aleji
Maziwa
Nyama
Samaki
Juice
Soseji
Blueband
Jam

Sasa atumie vyakula gani mbadala?
 
Wadau naombeni mawazo yenu nina mtoto wa dada yangu anasumbuliwa sana na kifua, haipiti miezi miwili lazima atabanwa na kifua sana.
Baada ya uchunguzi ikaja gundulika baba yake anamatatizo ya pumu na kwakuwa ugojwa huu ni wa kurithi, basi amemuachia na mwanae.
Katika harakati za matibabu kuna nesi akamwambia sister pumu kwa hospitali haina dawa ila kuna mitishamba yaani dawa za kienyeji zinaponesha pumu na hasa akiwa bado mdogo.

Je kuna yeyote mwenye experiance na hili au amewahi sikia tufahamishane.
Nawasilisha.
 
Mimi ni mdau wa afya...kwa taaluma yangu nafahamu kuwa hakuna tiba ya Pumu (kwamba haitibiki ikakoma isitokee tena). Pumu inafanana na allergy jinsi inavyotokea, kunakuwa na kianzishi (allergen/trigger) halafu njia ya hewa ina'respond' kwa kubana haswa wakati wa kutoa hewa nje. Kikohozi na mafua ni moja ya vianzishi. Wakati mwingine Pumu inaweza ikaacha yenyewe (hasa inayoanzia utotoni) lakini sio mara zote.

Dawa zilizopo sasa na kupatikana hospitali au madukani husimamisha 'attack' inapotokea kwa kupanua njia za hewa ili mgonjwa apumue kawaida, hazitibu kuponyesha tatizo moja kwa moja.

Sijasikia bado dawa ya kienyeji iliyothibitishwa kuwa inapunguza kutokea kwa pumu au kutibu pumu kabisa. Kwa maelezo zaidi unaweza kwenda Muhimbili kitengo cha dawa asilia watakufahamisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom