2020 akishindwa sijui atakubali kutoka?

2020 akishindwa sijui atakubali kutoka?

Mwaka 2020 kuna uchaguzi kijijini kwetu, mfalme anayetawala sasa ni katili, ashauriki na kila mtu anamuogopa, mpaka wasaidizi wake wa karibu kabisa.

Wananchi hawajui kesho yao hapa kijijini. Hali ya maisha imekuwa ngumu hamna mfano.

Bado tuna mashaka, kwa jinsi watu wanavyomuogopa hivi, 2020 iwapo atashindwa kwenye uchaguzi kuna atakayethubutu kumwambia kuwa umeshindwa?

Hata akiambiwa umeshindwa atakubali kutoka ampishe aliyeshinda kweli? Yani wenzenu tuna mawazo.!
Alisema hataki katiba mpya sababu anaogopa time guru ya uchaguzi itamzuia kuiba kama alivyofanya lubuva
 
Hizi thread ndiyo zinazoponza akina Melo kuhangaika na kesi. Sababu anaambiwa kuwafichua, anawaonea haya na kuogopa lawama! Hakuna wazo jipya kuweza kujadiliwa na wanaforum, isipokuwa ni utawala kwa kejeli?

Tulia wewe upakatwe.melo kaingiaje hapa.huyo kiongozi wenu keshafeli tunasubir wakati wa bwana ufike ila pumzi imekata kitambo sana
 
Hivi kuna watanzania mwenye akili timamu ambaye anawaza Magufili atashindwa uchagizi 2020 kweli? Atakuwa hana akili timamu. Tatizo watu mnajipa moyo kwa kusoma JF, facebook na kwenye mitandao ya kijamii ambao wanaopost ni wale wale walioliibia taifa hili kwa kiasi kikubwa, kwa hiyo sasa wanachofanya ni kulalamika vitu ambavyo havipo.

Sidhani kama mtu ambaye amefanikiwa kuleta mabadiliko makubwa kwenye idara za serikali na sasa watu wanafanya kazi na matokeo yanaonekana anaweza kutolewa kirahisi kama mnavyoandika hapa.

Asilimia kubwa ya wananchi wanaopiga kura wanafikiwa kwa kupelekewa huduma zao muhimu kama maji, afya, elimu za watoto, etc.

Watanzania hawahitaji demokrasia ya kupiga kelele mnazoziita kwenye 'demokrasia' wakiwa hawana maji, afya shida, watoto wa shule shida.

Watanzania wanahitaji maendeleo, sio kelele
Ni kweli kabisa na huduma zote zapatikana kwa uhakika sana..ila kule Arumeru waliandamana wanakosa maji DC akakasirikia na kumrundika 24hours. Matatizo hayatakiwi tushayamaliza na tunaendelea kutekeleza kuyakamilisha..hatutaki kukosolewa ni uchochezi
 
Tatizo ukawa wamekuwa wakala wa mafisadi hawafai tena kuwapa nchi
Pamoja na mapungufu ya aliyepo....bora tuendelee kukomaa naye hivyo hivyo
Kuna watu wanaongea kama hawanaga ubongo
 
kwenda zako wewe hata aibu huna. mumekaa kutumika na mtu anayeamini kazaliwa awe rais. uchaguzi juzi rais na serikali yake wanafanya kazi mumekaa kumkwamisha. 2020 ndio hampati kitu mtabakia kulialia zaidi.
Hivi mimi na wewe anayetumika ni nani hapo. Hapo ulipo maisha yamekuchapa, hata pesa ya kununulia vipande viwili vya mihogo unywe chai huna
 
Hivi mimi na wewe anayetumika ni nani hapo. Hapo ulipo maisha yamekuchapa, hata pesa ya kununulia vipande viwili vya mihogo unywe chai huna
Wacha bana yaani hata vipande vya mihogo nishindwe kununua! sawa bana wewe si mtumbuliwa umejaa minoti.
 
Mwaka 2020 kuna uchaguzi kijijini kwetu, mfalme anayetawala sasa ni katili, ashauriki na kila mtu anamuogopa, mpaka wasaidizi wake wa karibu kabisa.

Wananchi hawajui kesho yao hapa kijijini. Hali ya maisha imekuwa ngumu hamna mfano.

Bado tuna mashaka, kwa jinsi watu wanavyomuogopa hivi, 2020 iwapo atashindwa kwenye uchaguzi kuna atakayethubutu kumwambia kuwa umeshindwa?

Hata akiambiwa umeshindwa atakubali kutoka ampishe aliyeshinda kweli? Yani wenzenu tuna mawazo.!

Kwa kusema Jecha apewe medal kwa kufuta uchaguzi wa znz ..basi hata nyooote wa mukatae haondoki ngooo...kwanza uchaguzi wa 2020 hautokua wa kawaida...kina lema watakua wengi sana.....kwa ufupi hali si hali
 
Mkuu nilikuwa sijui kama tupo kijiji kimoja. Simpendi huyu mfalme mpk mwisho. Naamini ni asilimia kubwa tu hatumpendi
 
Kwa kusema Jecha apewe medal kwa kufuta uchaguzi wa znz ..basi hata nyooote wa mukatae haondoki ngooo...kwanza uchaguzi wa 2020 hautokua wa kawaida...kina lema watakua wengi sana.....kwa ufupi hali si hali

Mkuu inaelekea wewe hatupo kijiji kimoja but seems we are facing same problems.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom