Uanza na matangazo mengi ya biashara karibia robo saa nzima wanatangaza filamu zilizotengenezwa na studio husika.
Jamaa anasema yupo nyumbani kwake lakini kiunoni amefunga taulo imeandikwa "Bondeni Guest House"
Mwanamke yupo kitandani amelala usiku wa manane na mumewe lakini amevaa kitop na jeans, mdomoni lip stick,machoni wanja vimeshaini! Mume ana pensi na Tshit mkononi ana saa kali!
Wachezaji hawatumii taswira zao halisi ikiwemo sauti za kubana pua, mavazi ya kukodisha au kuazima nk.
Msanii anapiga picha akiwa amesimama kwenye mkoko (usafiri) mkali ambao kwenye tamthilia au filamu nzima humuoni akiendesha..
Jamaa ana act yeye ni mkuu wa kituo cha polisi lakini anamwita "afande" askari aliye chini yake ("yupo wapi afande Jack aje nimtume eneo la tukio)
Binti ana act "u secretary" lakini haonekani akitumia hata mara moja kompyuta iliyo mbele yake.
Mtu ana act yupo ofisini ni Boss lakini pembeni yake unaona Kabati la Nguo