1981 Israel Raid on the Reactor: Jeshi la anga la Misri linaweza kufanya shambulizi la ghafla (Blitzkrieg) kwenye bwawa la umeme huko Ethiopia?

Sawa mkuu...
Mkuu mi ni msomi kidoogo wa war tactics.
Hii blitzkrieg ni offensive tactic iliyotumiwa sana na Hitler akitumia vikosi vyake maalum, yeye akiviita Storm Troopers.
Storm Trooperswalikuwa hatari, wakisaidiwa na mizinga, Air raids na Panzer Division(vifaru).

Tatizo kubwa ya tactic hii ni yale mafanikio yake!
Logistics zinaanza kuwa shida!
Risasi na supply lines zinakuwa nyuma sana.

Chini ya Generali Paulus aliyekuwa anaogopewa sana, Wajerumani walishambulia kwa kasi ya ajabu hadi Urusi.
Vi nchi vidogo kama Poland, Chzeckoslovakia, Hungary, vilipitiwa kama mswaki hadi nchini Urusi.

Huko Urusi wakakuta ukuta unawasubiri Stalingrad.
Na hiyo tactic ya blitzkrieg ndiyo ikawa mwisho wake, baada ya ushindi wa maelfu ya kilometa.

Hapo walimkuta mbabe wa Kisoviet, Marshal Zhukov, ambaye si tu aliwazuia, bali alitayarisha mshambulizi makali yaliyoangamiza kabisa nguvu za wajerumani.

Marshal Zhukov hakupumzika mashambulizi hadi ameiteka ngome ya Hitler , huko Berlin.
 
Mkuu mi ni msomi kidoogo wa war tactics.
Hii blitzkrieg ni offensive tactic iliyotumiwa sana na Hitler akitumia vikosi vyake maalum, yeye akiviita Storm Troopers.
Storm Trooperswalikuwa hatari, wakisaidiwa na mizinga, Air raids na Panzer Division(vifaru).
Ufafanuzi safi sana huu mkuu...
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Eti ndugu zangu watanzania;

Jeshi la anga la Misri linaweza kufanya shambulizi la ghafla (Blitzkrieg) kwenye bwawa kubwa la kuzalishia umeme huko Ethiopia (Grand Ethiopian Renaissance Dam) kama ambavyo Israel Defense Force (IDF) walivyofanya "Raid on the Nuclear Reactor" huko Iraq mwaka 1981?

SOMA KWA UFUPI KISHA CHA ISRAEL NA UVAMIZI KATIKA KINU CHA NYUKLIA HUKO NCHINI IRAQ:

Mnamo mwaka 1976, Iraq ilinunua kinu cha nyuklia (nuclear reactor) kutoka Ufaransa. Wakati Iraq na Ufaransa walikuwa wakiiendelea na ujenzi wa kinu kile cha nyuklia, ambacho wafaransa wenyewe waliamua kukipa jina la OSIRAK, na kilikusudiwa kwa matumizi ya amani hususan katika utafiti wa kisayansi, Waisrael waliutazama mradi ule kwa jicho la mashaka sana, wakiamini ya kwamba ulilenga katika kutengeneza silaha za nyuklia.

View attachment 1527149

Mnamo tarehe 7 mwezi wa June Mwaka 1981, msafara wa midege ya kivita ya Israel aina ya F-16A ikisindikizwa na ndugu zake aina ya F-15As iliangusha makombora na mabomu mazito na kuharibu nyang'anyang'a kinu hicho cha OSIRAK. Israel wali iita operation ile kuwa ni ya kujilinda (pre-emptive attack) wakisema kwamba kinu kile kilikuwa kina si zaidi ya mwezi mmoja kabla ya kuanza kutumika (before it might have become critical).

View attachment 1527150

Askari kumi wa Iraq pamoja na engineer mmoja wa Ufaransa waliuawa. Shambulizi hilo lilifanywa wiki tatu kabla ya uchaguzi mkuu ndani ya bunge la Israel (Knesset).

Kwa wakati ule, shambulizi hili lilikutana na ukosoaji mkubwa sana kutoka jumuiya za kimataifa, ikiwemo Marekani, baraza la usalama pamoja na mkutano mkuu wa umoja wa mataifa katika matamko mawili tofauti.

Baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa vilifikia mpaka hatua ya kusema kuwa huu ulikuwa ni ugaidi wa kufadhiliwa na serikali (state-sponsored terrorism) na kwamba kitendo cha Israel kushambulia kinu hicho kwa kuvizia ni hatua ya ubabe na uchokozi usiosameheka.

View attachment 1527152

Uharibifu wa kinu cha Osirak umekuwa ukitizamwa na baadhi ya wataalam wa masuala ya usalama, siasa pamoja na sheria za kimataifa kama mfano moja wapo wa shambulizi za kuzuia hatari (preventive strike) ambao wanasema pia ya kwamba liliirudisha nyuma sana Iraq kutoka hatua chache za kuwa na uwezo wa nyuklia (it brought back Iraq from the brink of nuclear capability) na kuzima kabisa ndoto za Rais Saddam Hussein kuja kumiliki silaha za nyuklia hapo baadae.

MZOZO BAINA YA MISRI NA ETHIOPI JUU YA BWAWA KUBWA LA KUZALISHIA UMEME:

View attachment 1561801

Ethiopia Ni chanzo kikuu Cha maji ya mto Nile, pamoja na Uganda na Tanzania kwa kiasi fulani. Misri na Sudan Ni nchi ambazo zinategemea maji ya mto Nile kwa kunywa, matumizi ya nyumbani, kilimo, ufugaji na viwanda.

Vita kamili inanukia Kati ya Ethiopia na Misri kupigana kwaajili ya matuzi ya maji ya mto Nile, hasa baada ya Ethiopia kujenga bwawa (Gerd) kubwa la kufua umeme kwa kutoa maji ya mto Nile kujaza bwawa hilo litakalotumia mabilion ya ujazo ya maji ya Nile.

Ethiopia inataka kujaza bwawa la Grand Renaissance kwa miaka 6 lakini Misri imependekeza angalau mradi huo uchukue kipindi cha miaka 10 kwa kuhofia kwamba kuchukua kipindi kifupi kutaathiri mtiririko wa maji ya Mto Nile ambayo inategemea asilimia 90 ya maji ya mto huo.

View attachment 1561803

Misri kwa upande wake inahofia kuwa ujazo wa maji ya mto Nile yatakayofika Misri utapungua hivyo kuathiri maisha na uchumi wa Misri.

Ujenzi wa Bwawa la Grand Renaissance linalojengwa Ethiopia ukishamalizika, mradi huo unaogharimu kima cha bilioni 5 za Marekani, litakuwa ndio bwawa kubwa zaidi la uzalishaji umeme barani Afrika lenye uwezo wa 6,000MW.

(1) JE, AFRIKA ITAARAJIE KWA MARA YA KWANZA KUPOKEA "BREAKING NEWS" KAMA ZILE TULIZOZOEA KUZISIKIA KATIKA ARDHI YA MASHARIKI YA KATI?

(2) Njia ipi sahihi itumike katika matumizi ya maji ya mto Nile ili uhusiano miongoni mwa nchi za Africa uendelee kuwa mwema na imara??

WADAU KARIBUNI SANA KWA MICHANGO.

OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Asante Rais Magufuli kwa kutupeleka Tanzania katika uchumi wa kati, Mungu akupe afya uendelee kututumikia.
 
Mkuu, njia ipi sahihi itumike katika matumizi ya maji ya mto Nile ili uhusiano miongoni mwa nchi za Africa uendelee kuwa mwema na imara?
Kiufupi ni kwamba mkataba huu wa "kipumbavu" ulisainiwa kati ya Waingereza na Wafaransa kunako mwaka 1929 ambapo Waingereza (wakiwa watawala wa Kenya, Uganda na Tanzania kuliko na vyanzo vya mto) walitaka kuchepusha mto Nile na kuupeleka Uganda ili kuwakomoa Wafaransa ambao walikuwa na bifu nao wakati wa kugombea makoloni. Mkataba huu tata unaipa Misri haki kubwa ya matumizi ya maji ya mto Nile, na kuwaacha na bumbuwazi wale wanaotumia maji hayo upande wa juu (upstream Users) ambako ndiko maji yanakotoka. Kupitia taasisi iitwayo Nile Basin Initiative (NBI) utekelezaji wa masharti ya mkataba huu unaendelezwa. Watumiaji waliopo juu kwenye vyanzo ni :-
  1. Tanzania
  2. Rwanda
  3. Burundi
  4. Uganda
  5. Kenya
Watumiaji wengine ni Misri, Sudan zote mbili na Ethiopia ambako ni chanzo cha Nile ya bluu. Kwa miaka mingi mkataba hu umekuwa ukizipiga mkwara nchi hizo hapo juu pale zinapotaka kuendeleza miradi inayotumia maji ya mto Nile. Hata Tanzania tulipochota maji kutoka ziwa Victoria kupeleka Kahama na Nzega kulikuwa na mikwara sana, ila kwa kiburi tukachota maji hayo na kuwanyweshwa Watanzania wenye kiu. Hali kadhali ule mradi wa umeme wa Rusumo unaojengwa kwa uboa kati ya Rwanda na Tanzania unasimamiwa na taasisi tajwa hapo juu, ili kuhakikisha kwamba maji yanayochotwa hayaathiri watumiaji waliopo Sudan na Misri. Sasa Misri wanatumia mto Nile kama fimbo ya kuwachapia hawa walioko huku vyanzoni. Ila wanasahau kwamba tusipolinda mazingira sisi nchi 5 wao wanakufa.
Naamini kwenye huu mgogoro watamaliza salama kwa maelewano, kwa sababu vita haitakuwa na faida kwa yeyote kati yao. Kwa sababu Misri wakiamua kulivunja bwawa la Ethiopia Kibabe, Ethiopia wanaweza kutia sumu kwenye maji pale yanapoacha nchi yao kuelekea Misri ili kuwakomoa Wamisri. Naamini kila nchi imefanya calculated RISK ya vita hii kabla wajaliamsha dude.
Nawasilisha kile ninachofahamu
 
Kiufupi ni kwamba mkataba huu wa "kipumbavu" ulisainiwa kati ya Waingereza na Wafaransa kunako mwaka 1929 ambapo Waingereza (wakiwa watawala wa Kenya, Uganda na Tanzania kuliko na vyanzo vya mto) walitaka kuchepusha mto Nile na kuupeleka Uganda ili kuwakomoa Wafaransa ambao walikuwa na bifu nao wakati wa kugombea makoloni.
Safi sana mkuu...
 
Hilo bwawa wakilivunja kingo maafa yake si ni balaa!

Hayo maji yatatiririka kuelekea wapi na yasilete athari?

Wangelishambulia kabla halijaanza kujazwa maji.

Mikataba yote ya enzi za mkoloni inatakiwa ipitiwe upya na wadau wa pande zote ili iendane na mahitaji ya sasa.
 
Hilo bwawa wakilivunja kingo maafa yake si ni balaa!

Hayo maji yatatiririka kuelekea wapi na yasilete athari?

Wangelishambulia kabla halijaanza kujazwa maji.

Mikataba yote ya enzi za mkoloni inatakiwa ipitiwe upya na wadau wa pande zote ili iendane na mahitaji ya sasa.
Vp kuhusiana na mikataba inayohusu mipaka baina ya nchi moja na nyingine? Nayo pia inapaswa kupitiwa upya mkuu?
 
Mkuu mi ni msomi kidoogo wa war tactics.
Hii blitzkrieg ni offensive tactic iliyotumiwa sana na Hitler akitumia vikosi vyake maalum, yeye akiviita Storm Troopers.
Storm Trooperswalikuwa hatari, wakisaidiwa na mizinga, Air raids na Panzer Division(vifaru).

Tatizo kubwa ya tactic hii ni yale mafanikio yake!
Logistics zinaanza kuwa shida!
Risasi na supply lines zinakuwa nyuma sana.

Chini ya Generali Paulus aliyekuwa anaogopewa sana, Wajerumani walishambulia kwa kasi ya ajabu hadi Urusi.
Vi nchi vidogo kama Poland, Chzeckoslovakia, Hungary, vilipitiwa kama mswaki hadi nchini Urusi.

Huko Urusi wakakuta ukuta unawasubiri Stalingrad.
Na hiyo tactic ya blitzkrieg ndiyo ikawa mwisho wake, baada ya ushindi wa maelfu ya kilometa.

Hapo walimkuta mbabe wa Kisoviet, Marshal Zhukov, ambaye si tu aliwazuia, bali alitayarisha mshambulizi makali yaliyoangamiza kabisa nguvu za wajerumani.

Marshal Zhukov hakupumzika mashambulizi hadi ameiteka ngome ya Hitler , huko Berlin.
Bila shaka wewe ni afande
 
Back
Top Bottom