14-Oktoba-1999: Ulikuwa wapi?

14-Oktoba-1999: Ulikuwa wapi?

Dah, siku hiyo nilikuwa Wilayani Mbinga tukinunua Kahawa. Tulitumia magari 109 landrover yakiwa na radio call. Ps wa ofisini alitupigia tuliopo field kwamba baba wa Taifa kafariki. Kimsingi REDIO call wote mnasikia fulan na fulan wanachoongea ila mnapotezea, but ile habari tukaifuatilia wote. Kimsingi SOTE tulijawa na HUZUNI sana. Ilisikitisha. Jioni kufikia Mjini tukawa tunajaa kwenye kumbi za starehe kuona habari kwenye ITV. Kikubwa msiba ule ulikuwa na msisismko ambao haujawahi tokea na sijui kama utatokea tena kwa sababu Viongozi wa sasa wana mahasimu wengi ambao TAARIFA ya KIFO kwa wengine hawajali kama vile huwa FURAHA. Lkn Mwl wananchi wote tulisikitika sana. Mara ya mwisho kumuona Ilikuwa 1995 akimfanyia kampeni Mzee Mkapa. Nilikuona live, jamaa alikuwa na confidence sana. Akanishawishi kupiga kura na nilimchagua Mema enzi hizo anarindima hatareeee!!
RIP Mwalimu!!
 
Tulikuwa Enschede, Uholanzi, tukisoma kozi ya Masters. Watanzania tulijiunga kwa pamoja kuomboleza kifo cha Baba wa Taifa. Baadhi ya wanafunzi wenzetu wa nchi nyingine za Kiafrika, walishindwa kutuelewa; maana sisi ni tuliozaliwa na kukulia awamu ya Nyerere na zilizofuata.

Pumzika Kwa Amani, Baba wa Taifa.
 
Mmh wewe mwongo [emoji1787][emoji1787][emoji1787] sasa ivyo vidudu ulikuwa unajua ata maombolezo kweli wakat ulikuwa unawaza pipi zile za shiling tano [emoji849][emoji849][emoji849][emoji12][emoji12][emoji12]
Nilikua Nursery/vidudu hata sikuelewa vizuri, nakumbuka tulikua tunaangalia maombolezo kwenye TV
 
Nilikuwa nina miaka miwili, miezi miwili na siku mbili hivyo sikumbuki nilikuwa wapi.
 
Huyu mzee Nyerere alipendwa sana na Taifa hili hatakama kuna mabaya aliyafanya ila hakutaka ubinafsi.

Kila Raia wa nchi hii alimlilia,Daaah mimi nakumbuka nilikuwa Yombo makangarawe kipindi hicho nyumbani kulikuwa na Redio mbao,yani kila stesheni ilikuwa inamtangaza

Yaani mtaa mzima ulipoa daah,Kweli Mwl hatosaulika
Makangarawe ipi mkuu? Utakua ulisoma Yombo Dovya wewe
 
Majira ya saa nne asubuhi au niseme saa tano kasoro hivi nikiwa katika viunga vya mabweni ya Shule ya Sekondari Iyunga baada ya purukushani za kupata chai kwa maandazi ya mafuta ya mawese, taarifa ya kifo cha Muasisi wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zilikuwa dhahiri.

Je wewe ulikuwa wapi ukifanya nini?


Kumbuka.
Naongeza mke wa pili tarehe hyo msata
 
Nilikua darasa la kwanza,najiandaa kwenda shule,Mara naskia wimbo wa taifa redion.Mama angu na wapangaji wote wakatulia kusikilizia nini kinajiri maana haikuwa kawaida.Baada ya taarifa ya kifo kutangazwa wakina mama wakaanza kusema ooh vita itatokea.
 
👀 nawazoom wazee wa humu ndani

👧nilikuwa mdogo sana kama mwaka na nusu
 
Nilikua nafanyakazi Makongo na Lugalo kulikua kunaonekana magari ya jeshi madogo yamewekewa mazuria mekundu, ndio yale ymetumika/yaliobeba mwili wa Mwalimu Nyerere.

M/Mungu ampe makazi ya milele peponi baba wa Taifa.
 
Back
Top Bottom