14-Oktoba-1999: Ulikuwa wapi?

14-Oktoba-1999: Ulikuwa wapi?

Nilikua nna miaka sita nikisoma darasa la kwanza B tukuyu mbeya huko. Nakumbuka sana ilikua alihamis maana siku hyo shuleni kwetu by that time ilikua ni ya ukaguzi wa sare za shule na viatu kuwa safi. Wakati narud nyumbani majira ya saa sita hivi, niliona wafanyakazi wa TTCL wakiwa wanasikiliza radio kwa makundi alafu wanasikitika. Baadaye ndo nikajua walipata taarifa za msiba wa Nyerere. Nilipata shida sana kujua huyo Nyerere alikua na umuhimu gani? Kwanini watu weng wahuzunike? Tumetoka mbali! Sikua najua
 
Majira ya saa nne asubuhi au niseme saa tano kasoro hivi nikiwa katika viunga vya mabweni ya Shule ya Sekondari Iyunga baada ya purukushani za kupata chai kwa maandazi ya mafuta ya mawese, taarifa ya kifo cha Muasisi wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zilikuwa dhahiri.

Je wewe ulikuwa wapi ukifanya nini?


Kumbuka.
Nilikuwa nafanya tempo Mwadui mining baada ya kumaliza form six Musoma secondary
 
Back
Top Bottom