14-Oktoba-1999: Ulikuwa wapi?

14-Oktoba-1999: Ulikuwa wapi?

Nilikuwa Tabora Shule Moja Maarufu Kidato Cha Sita Nakumbuka Nilirudi Home Dar Kwa Muda Maana Shule Hakuna Kilichokuwa Kikiendelea Baada Ya Kutangazwa Siku Kadhaa Za Maombolezo."
Heshima yako Mkuu, kama ulikuwa kidato cha sita, nakumbuka mm nilikuwa dalasa la saba, sikumbuki kama tulikuwa tumefanya mitahani ya kuhitimu au ilikuwa bado ila ilikuwa kwenye purukushani za kumaliza dalasa la saba, nakumbuka tukawa tunajazwa hofu ya kutokea vita kati ya TZ na Nchi Jirani! Dah long time sana Shule ya Msingi Mwenge Kasulu!
 
**** primary school Mtwara,tumeshapiga paper ya standard seven tunafanya mazoezi ya mahafali,mara paap kengele ya dharula inagonga muda huo mi nipo juu ya mnazi wa shule naangusha madafu,wahuni wenzangu wapo chini wanayafua hahahaa basi tukakusanyika fasta assembly shule nzima,mwalimu mkuu Mama Mwangata anatangaza kwamba nyerere kafariki,wanafunzi wa madarasa ya chini wanalia kwa sauti,walimu wanawatuliza kwamba hakutakua na vita tulieni,that was 14/10/1999...
Dah haaa haaa umenikimbusha mbali sn aise, nikiwa nimemaliza mitihani ya dalasa la 7 tulijazwa hofu ya vita
 
Daah nilikua darasa la pili pale Shule ya msingi Yombo Dovya, ninachokumbuka zaidi siku hii ni kwenye maombelezo , bibi yangu alilia sana na kipindi hicho home hakukua na tv hivyo alienda nyumba jirani kuangalia maombelezo....
Zamani chakula tulikua tunakula pamoja, nilienda kumsihi twende tukale akasema nitangulie, nilimaliza chakula chote bibi akalala njaa
Mola amrehemu huko aliko
Pole kwa bibi
 
Ndo nlikuwa natika kwenye kaptula ya baba kwenda tumboni kwa mama
Majira ya saa nne asubuhi au niseme saa tano kasoro hivi nikiwa katika viunga vya mabweni ya Shule ya Sekondari Iyunga baada ya purukushani za kupata chai kwa maandazi ya mafuta ya mawese, taarifa ya kifo cha Muasisi wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zilikuwa dhahiri.

Je wewe ulikuwa wapi ukifanya nini?


Kumbuka.
 
Huyu mzee Nyerere alipendwa sana na Taifa hili hatakama kuna mabaya aliyafanya ila hakutaka ubinafsi.
Kila Raia wa nchi hii alimlilia,Daaah mimi nakumbuka nilikuwa Yombo makangarawe kipindi hicho nyumbani kulikuwa na Redio mbao,yani kila stesheni ilikuwa inamtangaza
Yaani mtaa mzima ulipoa daah,Kweli Mwl hatosaulika
Pindi hilo kuelekea buza ni chaka hatari
 
Daaah! Nilikua Drs la 6 nakumbuka tumetoka skul kurud home namkuta bmkubwa analia KINOMA!! ITV nyimbo za komba "taifa lahuzunika" "kwaheri mwalimu" zinapigwa!
 
Aiseee
Nilikuwa shule ya msingi, hakuna wakati shule ilikuwa ngumu kwangu kama wakati ule...nilikuwa nachukia sana shule na kikitokea kitu chochote cha kunifanya nisiende shule nafurahi sana. Nasikitika kusema hata taarifa za kifo cha baba wa taifa zilikuwa za kufurahisha masikioni mwangu
 
Nilikuwa bado mdogo. Tulikuwa tunaishi maeneo ya Mwananyamala Maduka matatu. Kiukweli sikuelewa sana just nilifatisha namna wakubwa walivyokuwa wanahuzunika.
Jirani alikuwa na tv so ilikuwa nakaa mbele ya tv kwa siku nzima nikiangalia nyimbo za maombolezo za Marehem Mzee Komba.
Ile week yote toka anakufa mpaka anapokelewa uwanja wa ndege anapitishwa barabarani mpaka kuagwa uwanja wa Taifa nakadhalika yote niliyashuhudia. Msina kufika Butiama nk. Yaani ilikuwa ni kuamka kunywa chai kukaa kwenye tv mpaka saa saba baada ya kula ugali tv mpaka saa 2 usiku then kula ubwabwa, halafu kwenye tv mpaka saa tano alafu kulala. Kesho tena hivyohivyo.
Kama nakuona ulivyokuwa unawashangaa wakubwa zako wakihuzunika
 
Nilikua nauza duka manzese kwa mfuga m'mbwa,
Tukio nalokumbuka zaidi siku maiti yake imeletwa dar inapitishwa mtaani nilifunga duka nkaenda kushuhudia tukio, kurudi dukani km saa 10 jioni hivi ili nkafungue nkapata taarifa ya kifo cha boss wangu, ndio ilikua mwisho wa duka kufunguliwa hadi leo.
Dah pole sn
 
Back
Top Bottom