interlacustrineregion
JF-Expert Member
- Oct 28, 2018
- 7,134
- 7,409
14/10/1999 Nilikuwa najiandaa kumzika Baba Mzazi Marehemu nukifanyiwa uhamisho wa shule ya msingi Mazimbu A Morogoro kwenda kusoma Mara Tarime.Majira ya saa nne asubuhi au niseme saa tano kasoro hivi nikiwa katika viunga vya mabweni ya Shule ya Sekondari Iyunga baada ya purukushani za kupata chai kwa maandazi ya mafuta ya mawese, taarifa ya kifo cha Muasisi wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zilikuwa dhahiri.
Je wewe ulikuwa wapi ukifanya nini?
Kumbuka.
Bele 9(Abednego Nyamoga, Ramadhani, Nicholas na Maneno classmates wezangu nimewakumbuka sana enzi za utotoni daaah




