uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. Poppy Hatonn

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Kenya2022 Uchaguzi wa Kenya leo matatizo Ni prana. Raila amechoshwa sana na kampeni

    Prana ni neno la Kihindi,maana yake 'pumzi'. Raila amefanya kampeni kwa bidii na anechoka sana. Hatujawahi kumuona Raila anechoka namna Ile. Lakini sasa kampeni imekwisha nadhani he will get his breath back. Siyo rahisi kutabiri nani atashinda. Hata Wainjilisti wanaopenda kutabiri wameshindwa...
  2. Kisambusa

    JamiiForums Tanzania Mjumbe wa Kamati ya siasa ya CCM mkoa Kilimanjaro, Yasin Lema anaharibu uchaguzi wa CCM Jimbo la Hai

    Kwa masikitiko makubwa Tena Kwa huzuni kubwa Mzee Yasin Lema mkazi wa Hai Kilimanjaro na ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Kilimanjaro ameandaliwa/amejiandaa kuharibu majina ya wagombea uongozi ngazi ya wilaya kwenye kikao cha kupitisha majina mkoani kupitia kamati ya siasa ya...
  3. MWALLA

    JamiiForums Tanzania Tanzania tunajifunza nini kuhusu uchaguzi wa Kenya? Tubadilike

    Naona vyombo vya habari vingi vinajifanya kama havina habari kabisa kuhusu uchaguzi wa kenya yaani wanachukulia kama vile uchaguzi wa kumchagua mjumbe nyumba 10 10. Serikali y a CCM mnalo la kujifanza hapa msijifanye hampo na hamna habari, angalieni chaguzi ya Kenya inavyofanyika pamoja na...
  4. Mganguzi

    JamiiForums Tanzania Raha ya kuwa na tume huru ya uchaguzi hakuna mwenye uhakika wa kushinda watu wanamenyana kweli kweli

    Kuna wakati chakura ukila peke Yako hakinogi. Hata mji wenye watu wa kabila Moja Huwa Hauna maendeleo. Chama Cha siasa au nchi inayoogopa ushindani wa kweli, haiwezi kufikia mafanikio Kwa wakati, Kenya siasa imechangamka sana hakuna anayemuogopa mwenzake polisi hawaingilii siasa, wanawaaacha...
  5. Roving Journalist

    JamiiForums Tanzania Rais Mstaafu Kikwete, akiwa Kiongozi wa Timu ya Uangalizi ya Uchaguzi wa Kenya akutana na Wageni mbalimbali

    Mheshimiwa Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa Kiongozi wa Timu ya Uangalizi ya Uchaguzi wa Kenya, ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, amekutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Fred Matiang’i, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Kenya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Kenya tarehe 9 Agosti 2022...
  6. Lady Whistledown

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Kenya2022 Waziri wa Mambo ya Ndani akanusha Madai ya Ruto ya kuzima umeme na internet siku ya Uchaguzi

    Fred Matiang’i, Waziri wa Mambo ya Ndani na Uratibu wa Serikali ya Kitaifa nchini humo amesema madai ya Naibu Rais William Ruto ya Serikali kuzima Umeme na Mtandao ili kutekeleza wizi wa kura ni kejeli kwa kuwa wanaunga mkono Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kuendesha na kufanikisha...
  7. BARD AI

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Kenya2022 Zaidi ya Waangalizi 18,000 kufuatilia Uchaguzi Mkuu Kenya

    Zaidi ya waangalizi 18,000 na mamia ya waandishi wa habari wa kimataifa wamewasili Nchini Kenya kufuatilia Uchaguzi huo, idadi hiyo imetajwa kama kiashiria cha namna Uchaguzi huo unavyotazamwa Duniani kote - Uchaguzi huo una wagombea 16,098, wanne wakiwania kiti cha Urais na idadi inayobaki...
  8. Lady Whistledown

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Mahakama: Uamuzi wa Tume ya Uchaguzi wa Kutumia Usajili wa Kilektroniki Pekee katika uchaguzi wa Agosti 8 ni batili

    Mahakama ya Juu imebatilisha uamuzi wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) wa uandikishaji wa Wapiga kura kwa Kielektroniki pekee katika uchaguzi wa Agosti 9, na kusema kuwa sababu zilizotolewa na tume hiyo hazitoshi Tume hiyo ilisema kuwa Usajili wa Wapiga kura kwa Makaratasi unaweza...
  9. Tony254

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Kenya2022 US secretary of State Anthony Blinken aitakia Kenya uchaguzi wenye amani

    Huyu jamaa kumbe anajua Kenya ni nchi muhimu ukanda huu. Aitakia Kenya uchaguzi mwema.
  10. Stephano Mgendanyi

    JamiiForums Tanzania Victoria Mwanziva awapongeza vijana kwa kushiriki uchaguzi ndani ya Chama cha Mapinduzi

    VICTORIA MWANZIVA AWAPONGEZA VIJANA WENZAKE KWA KUSHIRIKI UCHAGUZI NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI Hongereni sana Vijana wenzangu wote ambao kwanza; mmeshiriki mchakato wa uchaguzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi. Nawapongeza kwa uthubutu wenu; Nawapongeza kwa utayari wenu wa kuhudumia Vijana wenzenu...
  11. I

    JamiiForums Tanzania Uchafuzi wa Sensa 2022

    Sisi wenye vigezo stahiki tumefanyiwa maagizo ya usaili hapa kata ya kivule wilaya ya Ilala na kufutiliwa mbali wakati namba 174. Yusuph Nyansika Getema (mtoto wa Diwani kata ya kivule) mwenye namba ya simu 0655 700 002 karani wa sensa ni miongoni wa wale watakaohudhuria sensa KESHO pale shule...
  12. Mlalamikaji daily

    JamiiForums Tanzania Ni wakati sasa Serikali iache kutumia walimu kwenye zoezi la Uchaguzi Mkuu

    Ni wakati muafaka Sasa walimu waachwe wapumzike na mazoezi haya kama ilivyo kwenye sensa, post code na mazoezi mengine ya kitaifa serikali itumie Hawa vijana wasio na ajira ili kuinua vipato vyao. Tuache kuwatumia walimu kwenye uchaguzi Tutumie Hawa vijana wasio na ajira. Mwisho.
  13. Abraham Lincolnn

    JamiiForums Tanzania Ushauri: Rais ajiuzulu, uchaguzi uitishwe

    Kwa mambo yanayoendelea hapa nchini kwa sasa, Ni wazi kwamba wananchi hawana tena imani chini ya uongozi wa awamu hii ya sita. Kila unapoenda ni lawama na hali ya kutoridhika na utendaji wa serikali. Mambo haya yamekuwa yakilalamikiwa sana. 1: Uchumi wa Tanzania Umeporomoka. Laiti kama uongozi...
  14. Lady Whistledown

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Kenya2022 Tume huru ya Uchaguzi yatoa wito wa Wakandarasi wa Teknolojia ya Uchaguzi kuachiliwa

    Tume Huru ya Uchaguzi nchini humo (IEBC) imesema kuwa Wakandarasi wa Smartmatic International BV wamekamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta walipowasili kutoka Venezuela licha ya mamlaka kuarifiwa kuwa waliingia nchini kihalali. Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati amesema...
  15. Lady Whistledown

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Kenya2022 Kenya: Facebook yafuta maelfu ya machapisho kwa kukiuka sera zake kuelekea Uchaguzi Mkuu

    Kampuni ya teknolojia ya Meta imeondoa maelfu ya machapisho yanayowalenga watumiaji wa Kenya kwenye mtandao wake wa kijamii wa Facebook kwa kukiuka sera zake. Facebook imesema kuwa imeondoa machapisho zaidi 37,000 yaliyohamasisha chuki na 42,000 kwa kukiuka sera yake ya ghasia katika muda wa...
  16. Lady Whistledown

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Kenya2022 Kenya: Baraza la Habari laagiza uchunguzi wa kushambuliwa kwa wanahabari kuelekea Uchaguzi Mkuu

    Baraza la Habari la Kenya (MCK), limewataka Polisi kuchunguza kwa haraka mashambulizi dhidi ya Wanahabari, kuelekea uchaguzi Mkuu wa Agosti 9, siku chache baada ya kushambuliwa kwa Mwanahabari wa Nation Media Group, Ian Byron Mwanahabari huyo mnamo Julai 10, anadaiwa kushambuliwa na watu...
  17. peno hasegawa

    JamiiForums Tanzania Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Hai punguza kupokea rushwa kipindi hiki cha uchaguzi wa chama

    Kwa masikikito makubwa na kwa kilio kikubwa tunakuomba uheshimu chama cha mapinduzi. Umekuwa ukipokea rushwa kwa wagombea wote wanaochukua na kurudisha fomu za jumuia ya wazazi wilaya ya Hai mkoa wa Kilimanjaro. Bila aibu tena kwa kujiamini. Umekatisha tamaa wanachama wa jumuia ya wazazi...
  18. B

    JamiiForums Tanzania Kwanini mwaka 2020 Hayati Magufuli aliamua kufanya uchafuzi badala ya uchaguzi?

    Swali hilo najiuliza hadi leo sipati jibu. Huenda alidhamiria kuua upinzani na kutawala milele? Lakini hata hivyo Mungu Mwenyezi alikuwa na yake. Halafu kama ni hivyo na baada ya CHADEMA kutotambua uchafuzi huo kwa kutangaza dunia nzima imekuaje tena Bunge hilo lisilotambuliwa na Chadema...
  19. Getrude Mollel

    JamiiForums Tanzania Katiba Mpya haiwezi kupatikana kabla ya 2025 na CHADEMA haitosusia Uchaguzi Mkuu

    Niliwahi kusema hapa vyama vyama vyote vya siasa vimetokana na CCM. Ni kama vile madhehebu mengine ya dini ya kikristo yalivyomeguka kutoka Katoliki. CCM ni chama kikubwa sana barani Afrika, hivyo hakuna chama hata kimoja Tanzania kinaweza kukitingisha. CCM ni kweli wamesema kwamba wanategemea...
  20. J

    JamiiForums Tanzania Hamad Rashid Mohammed: CCM haina uwezo wa kushinda uchaguzi ulio huru Zanzibar

    ..Msikilizeni ktk mahojiano haya.
Back
Top Bottom