Wakuu mvua ya leo kiboko, imeanza kunyesha kuanzisha jana usiku, tupo nayo mpaka sasa. Kama kawaida mvua kama hii ya mfululizo lazima iache madhara sehemu mbalimbali kama miundombinu kuharibika, foleni kuongezeka, watu kuchelewa kazini nk nk.
Vipi eneo ulililopo mvua haijaacha madhara? Tupia...
Wakuu tuseme tu ukweli hii nchi bado ni ya hovyo sana, hizi barabara kipindi cha mvua ni mtihani sana hasa ukiwa na gari ya chini!
Ukiwa unapita hizi barabara kuu unaweza ukasema mji si ndo huu! Sasa jana nilitoka Kimara nikaenda Tabata, mtaani kwetu kuna madimbwi ila sio ya kutisha kushindwa...
Nimechungulia kila kibuyu, nimeenda kwa wenzangu wanaojua kuangalia kama mimi, Leo kama unataka ckukuu iwe njema wekea simba tu kwenye betting, kipigo kitakatifu atakula mwafrika kusini.
Iwe mvua iwe Jua ni mauaji tu hapa Zanzibar Leo.Dalili zote za maangamizi zimeonekana yaani ni kama
Mvua za vuli zinazoendelea Lindi usiku huu Toka mchana sio ndogo radi zinarindima sijapata kuona.
Ule mngurumo wake na sauti yake MPAka nyumba unahisi inashake ..sasa najaribu ku imagine wakazi wa Gaza ambao sio member wa hamas jinsi wanavyokumbana na mabomu ya Israel
Eeh Mungu baba tusamehe...
usinunue kipindi cha kiangazi kama unataka kiwanja tafuta msimu wa mvua eneo unaliona vizuri kama lina asili ya matope au kuna maji yanapita chini kwa chini ili kuepuka changamoto.Na bora matope kuliko ununue kiwanja sehemu ambayo ni wetland.kiangazi hutagundua .
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza Mameneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) wote nchini kuhakikisha wanakagua vipenyo vya makalvati na madaraja yote katika maeneo yao kabla na baada ya msimu wa mvua ili kujiridhisha kama vinapitisha maji kwa urahisi bila kuathiri barabara.
Majaliwa...
Ndugu katika mapambano.
Leo jumatatu nimestuka saa tisa usiku naona mvua ipo kidogo nimejilaza naamka saa 11 mapema haijapoa.
Nimeshindwa kutoka mpka naandika huu Uzi hapa na nmesogea nilipo weka mwamvuli Toka mwaka jana nmeufungua vyuma vyote vimeachia Kwa kutu.
Nyie mnanunua miamvuli gani...
Daraja la Mto Matandu likiwa limekatika tena leo, Jumatatu Aprili 7, 2025, baada ya mwaka jana kukatika kufuatia mvua za El Nino zilizoambatana na kimbunga Hidaya. Pia, daraja la Somanga Mtama limekatika na kukata mawasiliano kati ya Dar es Salaam na mikoa ya kusini.
SOURCE: Mwananchi Digital...
Hali ya Soko letu la Bombambili hapa Mkoani kwetu Songea Mjini sio nzuri hasa inapotokea mvua imenyesha, miundombinu yake inakuwa siyo rafiki.
Wafanyabiashara na wateja wote wanapata wakati mgumu kupita na kufanya shughuli zao nyingine kutokana na matope, uchafu na mvurugano uliopo...
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA) imesema kwamba katika msimu huu wa mvua za masika, kunatarajiwa ongezeko la mvua katika mwezi wa Nne mwaka huu 2025.
Akizungumza na Torchmedia ofisini kwake jijini Dar es Salaam, mchambuzi wa hali ya hewa kutoka TMA, Joyce Makwata, amesema kwamba...
Abiria wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) maarufu mwendokasi wameelezea malalamiko yao baada ya moja ya mabasi hayo kuvuja maji wakati wa mvua jijini Dar es Salaam.
Katika video iliyosambaa mitandaoni, abiria walionekana wakitumia miamvuli ndani ya basi huku wengine wakieleza kusikitishwa na hali...
Najiuliza itawezekana kweli iwe zipo tu kwa ajili ya kutuhangaisha sisi waogopa radi?!!! Kwamba inajisikia Raha tu kutuona tukikimbilia vunguni mwa vitanda Kila zinapopiga?!!
Hapana, lazima zitakuwa na sababu na uhusiano mkubwa na mvua. Elimu yenu tafadhali 🙏🙏
Kuanzia saa 11 unusu jioni hii imepita mvua kidogo tu Arumeru-Arusha umeme umekata, jamani hii miundombinu imejengwa na nini? Hii ni aibu! Kwa hiyo gizani mtindo moja
Mwanamke aliyejulikana kwa jina la Rukia Said akikadiliwa kuwa na umri wa miaka 25-30 amekutwa na umauti ndani ya basi la abiria akisafirishwa kutoka Kilwa Pande kuelekea Hospitali ya Rufaa mkoani Lindi - Sokoine kwa lengo la kupatiwa matibabu.
Katika Hali isiyo ya kawaida mwili wa marehemu...
Kuna ukame ambao unatishia maisha ya watu na mali zao.
Akina Mwamposa and Co. Ltd wamejinasibu na kufanya miujiza kurekebisha mambo kama magonjwa, bahati kuondoa mikosi , kuleta utajiri etc etc.
Najiuliza, mbona sasa hawafanyi miujiza mvua ikanyesha?
Tunao zaidi ya 400
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.