Mitando imekuwa na huduma mbovu ya Network sana, Mfano Vodacome now day inasumbua mnoo, kutuma sms, internet kuna mtu haifanyi kazi, Je, Ni kuwa imeelemewa sana wateja wameongezeka ikiwa hawajaongeza jitihada ya kuwamudu. Au tatizo liko wapi!
Na tigo ndo kabisaaaa
Hawatoi tamko lolote lile...
Mimi katika kuishi kwangu nilijua Waharifu ndo wanadukua Mitandao ya Kijamii kama Facebook, Instagram, twitter, Whatsapp nk, baada ya Mfanyabiashara maarufu wa Magari Jijini Dar Samweli Shammy kupasua jibu na kuweka wazi kinagaubaka jinsi alivyo dukuliwa nikashangaa sana.
Nimeshangaa kusikia...
Mbona kusajili mnatuma mawakala mpaka maporini huko wanafika na usajili unafanyika bila mlolongo wowote iweje kufuta namba mpaka mtu afike kwenye duka la mtandao husika?
Yaani mnaendekeza faida tu kwa upande wenu bila kujali madhara kwa mteja na jamii yake au taifa kwa ujumla! Kumbukeni baadhi...
Kwa wale watumiaji wa mtandao pendwa wa X, nadhani mtakuwa mashahidi. Kwenye misiba hii ya taifa nimemuona sana. Pia kwenye habari za kigogo ama Malkia, watu humtumia sana kwenye replies. Ni nani huyu? Ama ana uhusiano gani na matukio kama haya?
Ama wanamtumia kwenye issue za huzuni kwa sababu...
Habari Zenu wadau, natumai mnaendelea kukaza na life popote mlipo. Swali langu ni Moja tu Tangu umeanza kuijua na kuitumia mitandao ya kijamii imekusaidia vipi kuunganisha na watu waliobadili maisha yako?.
Natamani kujua waliofanikiwa kupitia mitandao ya kijamii.
Sababu watu wa kada zote na...
Wakuu wa baadhi ya makampuni makubwa ya mitandao ya kijamii duniani wamehojiwa na wanasiasa katika Seneti ya Marekani na kukaangwa vilivyo kuhusu ulinzi wa watoto mtandaoni.
Wameulaumu uongozi wa Meta, TikTok, X, Snap, na Discord kwa kutochukua hatua za kutosha kulinda watoto dhidi ya madhara...
Mkurugenzi Mtendaji wa Meta, Mark Zuckerberg ameomba msamaha kwa familia zinazosema watoto wao walidhuriwa na mitandao ya kijamii, wakati wa kikao kilichowaka moto katika Bunge la Seneti la Marekani.
Bw Zuckerberg - ambaye anaendesha Instagram na Facebook - aliwageukia na kusema "hakuna mtu...
Wakuu,
Hili jambo linawezekana kuonekana kawaida, lakini limenishangaza kidogo.
Leo nilikua napitia habari huko mitandaoni, nikapata wasaa wa kuongalia taarifa za baadhi ya jamaa tulio kuwa pamoja kipindi cha nyuma.
Kitu kilicho nishangaza ni kuona kuna account moja ya mtu tulikua tunasoma...
Salaam humu.
Kuna jamaa amekuja kwangu nimuungie kifurushi kwenye mtandao mmoja pendwa nikajifanya kama mjuaji sana na madoido yangu nikamuungia akaondoka zake.
Baada ya dakika tano karudi analalamika nimemuungia kifurushi siyo chenyewe kuja kuangalia kweli dakika zimepungua nikatoa macho...
Walipoleta utaratibu wa kusajiri kwa alama za vidole walituambia ni kwasababu ya kudhibiti matapeli, ila kadri siku zinavyoendelea ndivyo wanavyoongezeka.
Je, mfumo ulikuwa wa upigaji umeshindwa kuwadhibiti? Au TCRA wanashirikiana na hawa wapigaji? Je, kwanini wasiweke utaratibu rahisi kabisa...
Habari zenu,
Hili ni swali kwa Vijana wabishi walioamua kuoa Single Mother.
Unajisikiaje pale unapoona Single Mother uliemuoa anampost mtoto wake na kuandika maneno kama My World, My Everything halafu Baba Mtoto nayeye anakuja kucomment My family.?
Kumbuka kuwa wewe hujawahi kutamkiwa hayo...
NIMEEJIULIZA swali Nape na Mwigulu ni Wajumbe wa Halmshauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) kikao kilichompitisha Nchimbi kuwa Katibu Mkuu, Swali je kwanini Nape na Nchimbi walijitokeza tena kwenye mitandao kumpongeza hii ina maana gani?
Kwa kuenea kwa teknolojia na intaneti, watoto wengi wanakua kama watumiaji wa kidijitali na wapenzi wa mitandao ya kijamii. Ingawa kuna faida nyingi za matumizi ya mitandao ya kijamii kwa watoto, kuna hatari kadhaa kama vile kutolewa kwa maudhui yasiyofaa, uhusiano na watu wasiojulikana, na...
Habari potofu au habari za kupotosha zimekuwepo kwa muda mrefu kabla ya kuibuka kwa mitandao ya kijamii. Hata kabla ya enzi za teknolojia ya digitali, watu walikuwa wakitumia njia mbalimbali kusambaza habari potofu kwa lengo la kufikia malengo yao, iwe ni kisiasa, kiuchumi, au kijamii.
Hapo...
RIPOTI: Nchi za Tanzania, Kenya, Sudan na Ethiopia zimetajwa katika Nchi 25 ambazo zilipoteza jumla ya Tsh. Trilioni 22.6 kutokana na kuzimwa kwa Mitandao ya Kijamii na Intaneti kulikodumu kwa zaidi ya Saa 79,238 mwaka 2023.
NetBlocks imeripoti kuwa Kenya pekee ilipoteza takriban Tsh. Bilioni...
Mrembo mmoja wa Instagram ameyashika macho ya wacheza mpira wa miguu maarufu, mastaa pamoja na mabilionea, lakini yote si kama unavyoweza kudhania.
@emilypellegrini amejikusanyia followers zaidi ya laki mbili kwenye Instagram ndani ya miezi minne tu. Ingawa picha na video zake zinaonekana kuwa...
Mbunge Lugangira: Matumizi ya Mitandao Katika Uchaguzi Yaingie Katika Sheria
MBUNGE wa Viti Maalumu, Neema Lugangira ameshauri Mswada wa Sheria ya Tume Huru ya Uchaguzi uwe na Ibara inayoongelea masuala ya Matumizi ya Mitandao katika Uchaguzi ikiwemo (Akili Mnemba - AI).
Lugangira ametoa...
Kwa wafuatiliaji wa Azam tv watakumbuka miaka ya nyuma ilikuwa ni ngumu Azam tv kuipa airtime Christmas kama ambavyo ilikuwa inafanya kwenye sikukuu ya IDDI
Basi wakulungwa walimaindi sana ikiwemo kushusha nyuzi humu kuhusu Azam tv na udini..
Kwa mfano mwaka jana Azam walikuwa wanakwepa...
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres wakati akizindua ripoti maalumu iliyoundwa ili kuimarisha uadilifu wa habari kwenye majukwaa ya kidijitali.
Kengele ya hatari kuhusu tishio linaloweza kusababishwa na maendeleo yanayokuwa kwa kasi ya Akili Bandia (AI) haipaswi kuficha uharibifu...
Ni watu wanaosumbua sana,
Reality sio matapeli ila jinsi wanavyoshawishi unaona kabisa ni biashara inayoshahabiana na biashara za kitapeli.
Akianza tu mwambie naomba nikuulize swali , akikupa ruhusa muulize hivi; BIMA maana yake ni kuwekeza unufaike wakati ambao huenda utakuwa hauko vizuri...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.