Yanapatikana kwa wingi nchini Kenya. Naamini na hapa kwetu Tz kuna watu wanaoyalima.
Sina uhakika kama nimeshayala. Lakini leo katika kupitia makala za kilimo, nimekutana na mada inayoihusu.
Nimeshangazwa kusoma kwamba hayana mbegu. Ni kweli ndivyo yalivyo? Yana uhusiano wowote na GMO...
WAkuu habari za usiku huu?
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Naomba kufahamishwa jinsi ya kutengeneza juisi aina ya milkshake, vitu vinavyowekwa humo mpaka inakamilika kwa ajili ya kunywewa.
Mbali na hilo naomba kufahamishwa mchanganyiko mzuri wa juisi inayopendwa na nzuri kwa ajili ya...
Salaam.
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Naomba mwenye kujua ofisi za hawa jamaa wanaitwa Selcom malipo mtandaoni.
Mnamo tarehe 01 November nilipita kituo cha mafuta cha Puma pale posta kuweka mafuta bahati mbaya sikuwa na cash hivyo nikaona kuna njia ya kulipia kwa simu...
Habari za maisha wakuu,
Natamani nipate andiko ambalo limeorodhesha taasisi zote za serikali na binafsi, wakala, mamlaka, NGO'S Na vyama ili nijue dhima yake Na mambo inayosimamia.
Nimechungulia kayika tovuti kuu ya serikali lakini naona inapwaya information ilizonazo hazijitoshelezi ofisi...
Ni muda sasa baada ya kusikia kuhusu vifaa hivi vya umeme (kuchaji)....Hivyo ninauhitaji navyo lakini ni bora kufahamu kuhusu vipengele hivi...
1:- Je baiskeli za umeme zipo tz na zinapatikana wapi dar au nyanda za kusini..
2:- Kama zipo kampuni gani ni bora na imara...?.
3:- Gharama zake...
Wana-Jukwaa habari ya muda huu, naomba kufundishwa jinsi ya kupata hati miliki ya nyumba, baada ya kuandikishana kwenye kitongoji husika sasa nahitaji kupata Hati Miliki
Natanguliza shukurani.
Habari za wakati huu my virtual family JF
Nikienda moja kwa moja kwenye mada nina interview hivi karibuni ya TA(Tutorial Assistant) katika institute X kwahiyo naomba kufahamishwa kuwa hizi interview zinakuwa vipi. Accounting & Finance
Hasa nazungumzia written tunayoanza nayo na oral pia...
Wadau habari zenu,
Kuna hii Biashara ya kununua na kuuza vifuu ambayo ningependa kuifahamu kuanzia
- Gharama za kununua Kama kwa kilo hununuliwa kiasi gani na kuuza kiasi gani
- Changamoto zake (japo hakuna Biashara inayokosa changamoto ila NI Bora kujua japo kwa uchache)
- Kama Kuna ubora...
Mfano mtu alioa mke akazaa watoto na mke wa kwanza na kwenye uhai wao wakapata na Mali ,then baadaye mke wa kwanza akafa ,na mume akaoa mke wa pili Kisha baadae huyu mume anafariki je kwenye mirath Ni Nani anafaidika na kilichobakia?
Nimekuwa nikijiuliza na kukosa majibu sahihi kuhusu uvaaji wa barakoa kwa kiongozi mkuu wa nchi yetu. Anapokuwa ndani na nje ya nchi.
Mara nyingi akiwa ndani ya nchi huvaa na akiwa nje havai! Pengine wapo wengi wangependa kujua.
Je, inamaanisha nini?
Habari za muda huu wanajamvi.
Naomba kufahamu zaidi kuhusu elimu tajwa hapo juu.
Mimi ni muhitimu wa kidato cha sita mwaka huu 2022,nimesoma tahasusi ya HKL.
Hivyo naomba mwenye ufahamu anipe dondoo kuhusu elimu hii.
Ahsanteni.
Mtu anayekuwa na digrii 3 au zaidi je anakuwanazo ktk fani tofauti? Na je ipi maana ya phd kwa kirefu? Na masters nini na ktk hao yupi yupo juu?
Nasubiri
Kufuatia maandalizi ya maadhimisho ya miaka 100 ya kuzaliwa kwa baba wa taifa la tz, hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere, naomba kufahamishwa kama kumewahi kuwa na desturi au utamaduni kwa jamii za kiafrika; kusherehekea siku za kuzaliwa kwa viongozi waliotangulia mbele za haki au hata kwa...
Haijanitokea kwa mtu mmoja au wawili. Ni watu wengi sana. Wengine ni watu wangu wa karibu. Unampigia simu kwa namba ngeni halafu hapokei baadaye anakwambia hapokeagi namba ngeni.
Mwingine labda ni mtu ambae hamjawahi kuwasiliana na ndiyo kwa mara ya kwanza labda umepata namba yake. Nayeye hana...
Kwa wanaofahamu machimbo ya vifaa vya ujenzi vya wizi, hasa hasa nondo. Maana si tumeamua kukomoana, wacha tutafute alternative. Pia na mabati, kama kuna anaefahamu hayo machimbo, najua yapo, maana huwa nasikiaga sikiaga watu wakinunua kwa bei ya kuokota.
Wanajamvi habari za j2!
Ninaomba kujuzwa, hivi inawezekana Kwa wenzetu walioko nje ya nchi yaan wanaoishi ughaibuni mtu akafariki ndg zake huku Tz wasijue?
Najua wapo ambao tunawaombeaga michango ya kusafirishwa lakini je wapo ambao hatuambiwagi kabisa habari zao? Kama wapo miili ama maiti zao...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.