jamii

  1. Idugunde

    Hili la Wachaga kutoajiriwa Serikalini na Taasisi za Umma awamu ya tano, Mbowe anadanganya umma?

    Namnukuu Mbowe ''Miaka mitano ya Hayati Magufuli ilikuwa ni miaka ya mateso kwa watu wa Kaskazini hususan Wachaga, ilifika wakati Magufuli akatoa maagizo ya Wachaga kutoajiriwa Serikalini na kwenye Taasisi za Umma''
  2. M

    Polisi Marekani wamejiwa juu baada ya kupiga picha na jambazi na kuposti kwenye mitandao ya jamii

    Inakuwaje wanajamvi! Wananch Marekani wamewalalamikia Polisi kwenda kinyume na miiko ya kazi kwa kupiga picha na jambazi waliomkamata na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii. Jambazi hilo lilijaribu kuiba benki likashindwa na kutokomea vichakani ambapo polisi walimfukuzia hadi kumkamata.
  3. Naantombe Mushi

    Ni kwanini jamii ya wahindi imesahaulika kwenye teuzi za kisiasa?

    Ni moja ya swali huwa linanijia kichwani kila siku. Tanzania ni moja ya nchi ambazo zimebahatika kuwa na hawa watu pamoja na nchi ya Kenya. Jamii ya wahindi wa Tanzania na Kenya, wana historia ndefu kwa hizi nchi. Na wengi mpaka babu zao wamezaliwa huku, ikimaanisha wana haki zote za uraia wao...
  4. beth

    Prof. Anangisye: Chuo Kikuu makini hakiwezi kuvumilia Wanataaluma wasiofanya Utafiti

    Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Prof. William Anangisye amesema Utafiti ni muhimu kwa maendeleo kwa Umma na ulimwengu wa ujumla akiongeza kupitia Tafiti hizo, Chuo vina wajibu wa kutatua changamoto zinazokabili jamii. Ameeleza hayo Mei 24, 2021 katika Maadhimisho ya Sita ya...
  5. T

    Hivi ni mwanasiasa gani kwa sasa mwenye mvuto na ushawishi zaidi kwa jamii ambaye anastahili kuwa alama ya siasa za Tanzania?

    Kama mada inavyojieleza hapo juu, kila nchi kwa nyakati tofauti hujaaliwa kuwa na mwanasiasa au wanasiasa wenye kujaaliwa vipaji vikubwa vya uongozi kiasi cha kugeuka kua kichocheo na hamasa kubwa kwa wanasiasa wanaoibukia na hata wasio wanasiasa. Ndipo nikajiuliza tunao wanasiasa wa namna hiyo...
  6. YONA RAPHAEL

    Nahitaji kujua lilipo soko la zao la ngwara / fiwi jamii ya maharage

    Mimi ni mfanyabiashara chipukizi, napatikana Tanga. Natafuta wanunuzi wa zao la ngwara au fiwi jamii ya maharage na choroko. Nina gunia zisizo pungua 8 store. Pia itapendeza kupata mawasiliano au kujua trend ya bei ya zao hili sokoni hususani kwa mkoa wa Arusha.
  7. Mlaleo

    Iran kaingiwa na nini Israel? Anataka ipigwe kura kutoka kwa Wayahudi, Wakrito na Waislam Israel kumaliza Mgogoro

    Vyanzo kutoka Iran, Vinasema kutatua mgogoro wa wa Karne nyingi kati ya Israel na Palestina ni kupiga kura miongoni mwa wakazi wote waishio katika maeno ya mgogoro wa kiuraia, utamaduni au udini. 'Lengo letu 'Wairani' wa utatuzi kwa Wapalestina ni kuitisha kura ya Maoni kwa kuwajumuisha jamii...
  8. comte

    Mei 15, ilikuwa siku ya familia duniani, lakini sikuona kama Tanzania tumeipa umuhimu

    Jana Mei 15, 2021 ilikuwa siku ya familia duniani. Familia ndiyo taasisi ya kwanza ambayo sote tumepita na wenye bahati tumeitengeneza au tutaitengeneza. Sasa hivi taasisi ya familia inapitia changamoto kubwa sana kuliko taasisi yoyote. Nimejaribu kupitia mabadiko yetu jana nasikitika kusema...
  9. Course Coordinator

    TAMISEMI ongezeni category ya Ustawi wa jamii ,wengi wanalia maombi yao yanakwama.

    Kwenu TAMISEMI. Waombaji wa ajira wanahangaika kuwa mfumo wa kujisajili na ajira hasa upande wa Ustawi wa jamii unawakataa kwa sababu option iliyo ni ya Health (Bachelor degre ,diploma,advanced dimploma na certificate). Kwenye NTA level mmeeka level 7 pekee wakati kuna vyuo vinatoa NTA level 8...
  10. Wakusolve

    Naomba ufafanuzi kuhusu Kozi ya Maendeleo ya Jamii

    Mwenye uelewa na hii kozi ya maendeleo ya jamii(community development) inayotolewa SUA anasaidia ni wapi utafanya kazi na je ni kozi yenye soko kwa sasa?
  11. D

    Kuliko kufunga wasiojulikana; Serikali ingefunga na wale wasanii wanaotongoza wanafunzi ili fundisho lifike kwa jamii

    Huko vijijini kuna kesi za masikini kuwarubuni watoto wa shule kingono na huamuliwa ili iwe fundisho kwa jamii. Huko vijijini kuna kesi za walimu kuwatongoza wanafunzi kwa tuhuma ya kuwakonyeza au kuchat nao tu na huamuliwa jera ili fundisho kwa jamii. Je, Serikali haioni kuwa kuna umhimu wa...
  12. The Dictator

    Unamchukuliaje mwanaume anayevaa hereni katika jamii yako?

    Hereni ni pambo linalotumiwa na wanawake tangu enzi na enzi za mababu zetu lakini kwa sasa hii imekuwa tufauti sana kwani hata wanaume siku hizi wanavaa. Je, ni sahihi kwa mwanaume kuvaa hereni kwa sehemu yoyote kwa namna yoyote ile na kwa kisingizio chochote kile?
  13. uchumi2018

    Pongezi kwenu Mdee na Bulaya kwa kuzungumzia mifuko ya Hifadhi ya Jamii Bungeni

    Habari zenu wadau. Nimeona mimi kama mfanyakazi ninayeguswa na sheria na taratibu za mifuko ya hifadhi ya jamii nitoe pongezi kwa wabunge hawa Halima Mdee na Ester Bulaya kwa hoja zao bungeni kutetea wastaafu ambao ndio wachangiaji na wanufaika wa mifuko hii. Ni mara nyingi tumesikia wabunge...
  14. B

    Madahara ya kukutana kimwili nje ya ndoa au pasipo kuwa katika ndoa

    MADAHARA YA KUKUTANA KIMWILI NJE YA NDOA AU PASIPO KUWA KATIKA NDOA Kukutana kimwili nje ya ndoa ni lango linalotumiwa na adui kuharibu vipawa vya Mungu ndani ya watu, Kwani tendo la ukutana na mtu kimwili si kujifurahisha tu kama wengi wanavyofikiri bali hiki ni kifungo cha Nafsi Na...
  15. Sky Eclat

    Mazao jamii ya maharage ni fursa nzuri ya biashara

    Mazao jamii ya maharage ni maharage, kunde, choroko, mbaazi, njugumawe nk. Kutokana na idadi ya wasio kula nyama duniani kuongezeka soko la mazao haya limeongezeka sana. Mazao haya hutumiwa na watu wa dini na race zote. Licha ya mabara mengi kuwa watumiaji wazuri wa mazao haya, Afrika ya...
  16. J

    Halima Mdee amcharukia Kimei Bungeni, kuhusu deni la Serikali kwa mifuko ya hifadhi ya Jamii

    Mbunge Halima Mdee amemcharukia Mbunge wa Vunjo Charles Kimei baada ya Halima Mdee kuchangia kuwa Serikali imekopa fedha nyingi kwenye mifuko ya hifadhi za jamii kiasi cha trilioni 10 na kufanya mifuko hiyo na kutolipa madeni hayo kumefanya mifuko hiyo kushindwa kulipa mafao ya wastaafu...
  17. Miss Zomboko

    Shonza: Maafisa wa maendeleo ya Jamii siku hizi wamekuwa Maafisa mikopo. Kumekuwa na kesi nyingi za Ubakaji na Ulawiti wa Watoto

    Mbunge wa Viti Maalum, Juliana Shonza, amesema kumekuwa na kesi nyingi za Ubakaji na Ulawiti wa Watoto katika Jamii lakini Maafisa waliopewa kazi ya kutatua changamoto hizo hawafanyi majukumu yao Amesema kumekuwa na kesi nyingi za matukio ya Unyanyasaji lakini nyingi zinaishia kwenye Jamii bila...
  18. Pain killer

    Ongezeko la vijana wadogo walinzi, hii inaleta picha gani kwenye jamii?

    Habari wakuu. Nimejikuta natafakari sana, kwenye nchi hii tajiri kama wanavotuaminisha viongozi wetu na maendeleo ya technology lakini Sikh hizi kunaongezeko la vijana wadogo wanaofanya kazi ya ulinzi. Wengi wao ni kuanzia miaka 22 wasichana na wavulana, wengine ni wahitimu Wa form four, six...
  19. Orketeemi

    Mapendekezo - Modulo ya hifadhi za jamii Igor mikopo Kwa watumishi

    Wakuu salaam. Nimeonelea nitumie ukurasa huu kutoa pendekezo ninaloona ni la manufaa sana kwa mustakabali wa taifa letu. Imekuwa ni kawaida Kwa watumishi kuhangaika kutafuta mikopo kwenye mabenki Kwa riba kubwa sana na wakati mwingine watumishi wamekuwa wakipata mikopo inayowaumiza mitaani...
  20. Idugunde

    Kwanini wanasisasa wa upinzani wamepoteza mvuto katika jamii? Ni uthibitisho kuwa jamii haiwaamini tena?

    Zamani wanasiasa wa upinzani walikuwa wakisimama kuongea ulikuwa unaona jamii nzima inazizima. Na kila mtu anaona wameongea hoja za msingi. Siku hizi hakuna anayeona kama kuna la msingi wameongea na jamii ina wapuuza huku ikiwaponda kimoyomoyo na kimaneno. Mfano ni Halima Mdee anaongea pumba...
Back
Top Bottom