chadema

CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama cha kiasiasa nchini Tanzania ambacho kilianzishwa tarehe 28 Mei 1992 na mwanasiasa mkongwe Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Waziri wa Fedha katika miaka 1997 hadi 1979.

Mwaka 2000 CHADEMA hakikuwa na mgombea wa Urais. Mwaka 2005 mgombea wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa namba tatu kati ya wagombea kumi akapata asilimia 5.88 za kura.

Mwaka 2010 CHADEMA ilipata asilimia 27.1% na mgombea Urais wa chama Wilbroad Peter Slaa na kura 4,627,923 kwa 31.75%.

Hata hivyo CHADEMA imekataa matokeo mengi kutokana na mchakato mzima kuwa mikononi mwa Tume ya Uchaguzi isiyo huru.
  1. J

    SI KWELI PreGE2025 Maria Sarungi ameandika kwenye ukurasa wake wa x kuwa Godbless Lema apokea bilioni 4 kuisambaratisha Chadema

    MARIA SARUNGI AMEANDIKA KWENYE UKURASA WAKE WA X KUWA GODBLESS LEMA APOKEA BILIONI 4 KUISAMBARATISHA CHADEMA. "🚨‼️Kaka yangu GODBLESS LEMA ametuchoma wapigania Haki.🚨‼️ Wakati tunalilia haki, tunapambana kwa ajili ya Mdude, yeye anapokea bilioni 4 kwa ajili ya kuizamisha CHADEMA polepole...
  2. S

    CHADEMA ni vilui luwi wa vyura

    Niseme ukweli ,nilikuwa nawaaminia sana CHADEMA na haswa viongozi wao ,nikiwaona na magwanda na namna wanavyosema nilijiaminisha wanaweza kuuteka umma na wao kuwa mstali wa mbele. Ila mapambano sio lelemama ,nilitegemea Mwaka huu twente faiv CHADEMA wataunga pale walipowekeza CUF kuishauri...
  3. P h a r a o h

    Hisia zangu zinavyo nituma CHADEMA wanashinda urais uchaguzi mkuu

    Nikienda mbele nikirudi nyuma, nikisimama nikikaa, nikiamka nikilala naona chadema wanashinda urais uchaguzi mkuu
  4. Erythrocyte

    Mbeya: Chadema Waingia Mochari kutafuta Maiti ya Mdude Nyagali, Waonyeshwa Maiti mpya zilizookotwa kuanzia Juzi, Wazikagua

    Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimeingia ndani ya mochwari (Friji la kuhifadhia maiti za binadamu) ili kujaribu kuutambua mwili wa Mwanachama wao aliyesemekana kutekwa na kupigwa na Polisi wa Mbeya kwa Maelekezo kutoka Juu. Soma Pia: Mdude Nyagali adaiwa kukamatwa na kupigwa na watu...
  5. W

    PreGE2025 Katibu wa CHADEMA kanda ya ziwa awataka viongozi wa dini kutoyumbishwa na wanasiasa

    Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Victoria, Zakaria Obadi amekosoa kitendo cha baadhi ya wanasiasa kukosoa viongozi wa dini kujihusisha na siasa kuwa huo ni uoga. Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake amewataka viongozi wa dini kutokuyumbishwa na maneno...
  6. W

    PreGE2025 Chadema wapeleka ushahidi waliomteka mdude

    Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wamedai kuwa wataendelea kuandamana kwenda Ofisini kwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya kwa lengo la kumpa ushahidi wa watu wanaodai ni askari wamehusika na tukio la kumteka na kumjeruhi Mpalukwa Nyagali, maarufu Mdude na kuwataka...
  7. Waufukweni

    PreGE2025 CHADEMA Kanda ya Victoria: Viongozi na wanachama waliohama ni makapi tu

    Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Kanda ya Victoria kimesema kipo imara na hakiwezi kuyumba kwani viongozi na wanachama waliohama hivi karibuni kwao ni kama makapi tu Katibu wa CHADEMA kanda ya Victoria Zacharia Obadi amesema viongozi hao walikuwa na makosa ya usaliti na kwamba...
  8. Kididimo

    Tahadhari Wana JF na great thinkers. Watoa threads nyingi humu za kuipinga Chadema na kwingineko avatars zinabandikwa majina bandia ya Kichagga . Ni

    Wanabodi na wapenda haki kote naomba tuchukue tahadhari. Kuna mkakati maalumu unaendelea wenye lengo moja, kuhakikisha Uchaguzi wa October unafanyika. Hata mimi napenda ufanyike. Chadema kama chama cha upinzani, kimevalia njuga mabadiliko kwanza ya sheria na namna ya ufanyaji uchaguzi bora na...
  9. S

    Baada ya Lissu kushitakiwa kwa uhaini, CHADEMA wafunguliwa kesi, na mojawapo ya madai ni CHADEMA isimamishwe na mahakama kufanya shughuli za kisasa

    Vita bado ni kali, ila hawatashinda. Katika kesi hiyo, walalamikaji ni baadhi ya viongozi wa bodi ya wadhamini wa chama wakiwa na jumla ya hoja 7 wanazotaka mahakama izifanyie kazi mojawapo ikiwa ni kuiomba mahakama isimamishe kwa muda CHADEMA kufanya shughuli za kisiasa. Taarifa hii...
  10. albab

    CHADEMA kuweni serious basi!

    Kwanza nianze kwa kusema kila mtu ana uhuru wa kupandisha mada yoyote humu na nasikitika wafuasi wa chadema kujiona wao ni bora, wenye elimu zaidi, wenye exposure zaidi ya mtu anaepingana nao. Hii ni dalili nyingine ya UJINGA. ...... Nachelea kusema CHADEMA mnachokifanya ni upuuzi na ni kwa...
  11. Nipe Maji

    SI KWELI PreGE2025 Zitto Kabwe asema CHADEMA imekufa kisiasa

  12. Nipe Maji

    PreGE2025 POTOSHI Jaji Warioba asema CHADEMA kususia uchaguzi ni kujifuta kwenye Ramani ya siasa

  13. Nipe Maji

    PreGE2025 POTOSHI Kibatala awataka wanachama wa CHADEMA kuiacha mahakama ifanye kazi yake bila maingiliano

  14. Lord Denning

    Ushauri kwa Chadema: Wekeni rekodi vizuri ya Matukio yote ya Utekaji, Kuuwawa, kulawitia na Kupotezwa kwa Watu wenu na Watanzania. Mtanishukuru baadae

    Dunia haijawahi kuwa sehemu nzuri sana kwa Watawala Madhalimu. Wote waliofanya vitendo vya kuua, kuteka, kuwalawiti na kupoteza raia walikuja kukutana na mkono wa Sheria. Wengine kwa Mahakama za ndani ya Nchi zao na Wengine kwa Mahakama za Nje za Kimataifa. Hali iliyopo nchini Tanzania kwa...
  15. W

    PreGE2025 Amos Makalla: CHADEMA wapo kwenye harakati za kufanya Tanzania isitawalike

    Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla amesema kuwa baada ya uchaguzi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kitageuka kuwa kama jukwaa la harakati kwa sababu wamepoteza muelekeo na malengo ya chama cha siasa ambayo lenho kuu...
  16. Z

    Chadema ndio wanapaswa kulaumiwa na wanachama wao kwa kukataa kusaini kanuni za maadili na sio kuilaumu Tume Huru ya Uchaguzi

    Nimemshangaa sana mzee wetu Warioba Kuishangaa Tume na kuzishangaa Kanuni za uchugazi badala ya kuwashangaa Viongozi wa Chadema (Katibu Mkuu) ambaye kwa Jeuri tu walisusia kusaini kanuni hizo za uchaguzi na huku wakitambua kufanya hivyo kutawazuia wao kushiriki uchaguzi Mkuu. Jambo hilo sio tu...
  17. B

    Kuna kosa gani CHADEMA kwenda mahakamani kesi ya Lissu? Mbunge Anatropia ahoji bungeni

    Kuna haha ya kuongeza neno hapa? Kwa hakika serikali ijitafakari.
  18. B

    Mbeya CHADEMA waandamana kwenda ofisi ya RPC kumsaka Mdude

    Makamanda Mbeya wamechafukwa: Wanachama na Viongozi wa CHADEMA Mkoa wa Mbeya wameamua kufanya maandamano ya amani ya kwenda katika ofisi za kamanda wa polisi mkoa Mbeya ili kufahamu nini hatima ya mwanachama wao Mdude ambaye hadi sasa hawafahamu alipo tangu kutoka taarifa juzi kuwa amechukuliwa...
  19. Masai wa Town

    PreGE2025 Mdude Nyagali adaiwa kukamatwa na kupigwa na watu waliojitambulisha Polisi

    Mwanachama wa JF na mdau mkubwa wa mitandao, Mdude_Nyagali amechukuliwa na watu waliojitambulisha kuwa ni polisi usiku huu. Walikuwa na silaha, wamevunja mlango. Mdude amepigwa sana, alikuwa amelala nyumbani kwake Mbeya. Watu hao wamevamia wakiwa na silaha, wakabomoa mlango, wakampiga sana...
  20. S

    PreGE2025 CHADEMA na Wanaharakati kwa ujumla, anzisheni michango kusaidia familia ya Mdude

    Habari! Natoa wito kwa viongozi wa CHADEMA na wanaharakati wa haki za binadamu na wadau wengine kuanzisha michango kusaidia familia ya Mdude katika kipindi hiki ambacho hatima ya Mdude bado ni kitendawili. Huyu Bwana alitoa maisha yake kupambania Taifa hili na watu wake na pia alikuwa ni...
Back
Top Bottom