chadema

CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama cha kiasiasa nchini Tanzania ambacho kilianzishwa tarehe 28 Mei 1992 na mwanasiasa mkongwe Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Waziri wa Fedha katika miaka 1997 hadi 1979.

Mwaka 2000 CHADEMA hakikuwa na mgombea wa Urais. Mwaka 2005 mgombea wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa namba tatu kati ya wagombea kumi akapata asilimia 5.88 za kura.

Mwaka 2010 CHADEMA ilipata asilimia 27.1% na mgombea Urais wa chama Wilbroad Peter Slaa na kura 4,627,923 kwa 31.75%.

Hata hivyo CHADEMA imekataa matokeo mengi kutokana na mchakato mzima kuwa mikononi mwa Tume ya Uchaguzi isiyo huru.
  1. Just Pray

    GE2025 CHADEMA yapinga ongezeko idadi ya wapiga kura

    Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kupitia kwa Mkurugenzi wake wa Oganaizesheni, Mafunzo na Uchaguzi Mwl. John Pambalu kimeipinga taarifa ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) inayoonyesha ongezeko la idadi ya wapiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge, Madiwani unaotarajiwa...
  2. Carlos The Jackal

    Huenda kilichozinduliwa Kwa ajili ya Uranium ,Nyuma yake kuna Uchimbaji wa Dhahabu !

    Kwa namna Madini ya Uranium yanavyochakatwa kuanzia Uchimbaji, Usalama wake katika Muktadha wa Usafirishaji, Usalama wa Mazingira , Usalama wa Binadamu, Usalama dhidi ya Jaribio watu wenye nia Ovu na malighafi ya Uranium . Hilo tu lilitosha Leo Kwa Rais na Walinzi wake kuvalishwa Mavazi Rasimi...
  3. Waufukweni

    GE2025 John Heche: Waliokatwa CCM wananipigia Simu, wanalalamikia mwenendo wa Chama na kuonesha matumaini kwa CHADEMA

    Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Heche, amesema baadhi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliokatwa kwenye mchakato wa uteuzi wamekuwa wakimpigia simu wakilalamikia mwenendo wa chama hicho na kueleza matumaini yao kwa CHADEMA. Akizungumza nje ya Mahakama...
  4. mr mkiki

    Mfuasi wa CHADEMA ni Aibu kubwa kujadili MAJINA ya Wagombea wakati huu wa OPARESHENI ya kudai REFORM

    1.Wafuasi na wanachama wa CHADEMA hatusambazi kazi za chama mitandaoni kwa kiwango cha kutosha. Tumejazana Facebook, Twitter, Instagram, TikTok na kwingine huko, lakini hatubebi kazi za chama. 2.Wafuasi na wanachama wa CHADEMA hatutembelei ipasavyo akaunti rasmi za chama katika mitandao ya...
  5. Idugunde

    Kwa huu mnyukano ndani ya CCM kama CHADEMA Ingeshiriki uchaguzi ingeshinda kwa kishindo kama uchaguzi wa 2010

    Uchaguzi wa 2010 CHADEMA ilipata matokeo mazuri sababu CCM ya wakati huo ilikuwa imepoteza imani kwa wananchi. Na kulikuwa na mpasuko na makundi makubwa. Mwaka huu kwa CHADEMA hii ambayo inakubalika na huu mparaganyiko ndani ya CCM CHADEMA wangeshinda kwa kishindo na kupata viti vingi zaidi ya CCM
  6. M

    GE2025 Waliokuwa wabunge wa CHADEMA (Covid 19) waliohamia CCM na kubwagwa kura za maoni Ubunge

    Nadhani wote tunawakumbuka wale wabunge 19 walioingizwa bungeni kinyemela kwa tiketi ya CHADEMA huku chama kikiwa hakitambui uwakili wao. Yaliongelewa mengi sana, kesi ikaenda mahakamani, danadana mpaka sasa, wakakingiwa kifua na Spika na mifumo mingine ya maamuzi, kumbe ilikuwa ajenga tu...
  7. H

    Utawala wa Wapalestina Wawataka Hamas Kusalimisha Silaha. Wasema Hawaungi Mkono Ugaidi

    Utawala wa Wapalestina, mjini Ramallah, umesema kuwa wao ndio mamlaka halali ya utawala wa eneo lote la Wapalestina, na kwamba Kundi la kigaidi la Hamas, lisalimishe silaha zake kwa utawala halali, na wasijihusishe na chochote kwenye utawala wa wapalestina. Waziri mkuu. Mohammad Mustafa ...
  8. Parabolic

    GE2025 CHADEMA yalia na idadi ya wapiga kura: "Hao milioni 2.6 wametoka wapi?"

    Mkurugenzi wa Oganaizesheni, Mafunzo na Uchaguzi wa CHADEMA, John Pambalu amekosoa takwimu zilizotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kuwa idadi ya wapiga kura mwaka huu inafikia zaidi ya 37.6, wakisema idadi hiyo inapingana na takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu iliyotoa idadi ya...
  9. W

    GE2025 Kwa hili CHADEMA chukueni hatua nyingine

    Habari ya Leo GT. Kwa hili CHADEMA CHUKUENI HATUA; 1: Kesi hizi zilitengenezwa ili muanze kuhangaika na muhimili wa mahakama, Je nia yao ni nini? a: Kupunguza pressure mtaani b: Kupunguza mzigo kwa CCM c: CCM na watu wao kujificha katika muhimili mwingine, ionekane ya kwamba...
  10. sameer0220

    Ukitaka kuoga matusi nenda kinyume na CHADEMA

    Tatizo huwa ni nini hasa kwa wafuasi wa CDM kwamba ukiwauliza swali ili ujifunze unapewa matusi Ukienda kinyume na maono yao unashambuliwa NB mimi sio mfuasi wa chama chochote mimi ni mtu huru😅
  11. Idugunde

    Tafiti za kisayansi zimeonyesha CHADEMA hii chini ya Lissu haiwezi kusambaratika kwa fedha na nguvu ya mahakama

    Naona mshikamano ni mkubwa sana kwa wanaChadema kwa sasa. pamoja na mizengwe ya utawala wa CCM Mimi mwenyewe nashangaa huu mshikamano unatoka wapi. Kesi za kubambikiwa na kuzuiwa kufanya shughuli za siasa kupitia matapeli wa huko Kizimkazi. Bado watu wapo imara.
  12. Doctor Mama Amon

    Naomba nakala ya hukumu ya Jaji Mwanga iliyokataza Chadema kufanya siasa

    Nimefuatilia mapambano kati ya polisi na Chadema, kwa sababu ya hukumu ndogo iliyotolewa na Jaji Hamidu Mwanga hivi karibuni. Jaji Mwanga, anasikiliza Kesi Namba 8323/2025, iliyofunguliwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar, Said Issa Mohammed, dhidi ya Bodi ya Wadhamini ya CHADEMA na...
  13. D

    Baada ya ramli zao kushindwa, Sasa chadema wa JF wamehamia kwenye kumchonganisha kidini

    Yeah, wiki iliyopita CHADEMA walikuwa wanakesha humu kushusha mamia ya mathreads ya kumchulia Mama Samia Suluhu Hassan, The Mother of Modern Tanzania. Walitoa Kila aina ya Dua mbaya kwa amiri jeshi huyu mkuu. Kila mmoja alijitahidi kutoa Yale matamanio yake yaliyojaa kifuani mwake (of course...
  14. Tlaatlaah

    CHADEMA wanafuatilia zaidi mchakato wa kura za maoni za CCM, kuliko CCM wenyewe, unadhani ni kwanini?

    Kila mdau wa JF ni shuhuda kwenye hilo, kwasababu liko wazi sana. Je, Chadema wameona kwamba, CCM ni darasa tosha la siasa na wanajifunza demokrasia kwa maneno na vitendo, au upweke unaowakumba baada ya chama chao kusambaratishwa na uropokaji wa viongozi wao wapya wakuu, umewakosesha cha...
  15. Roving Journalist

    GE2025 Wanachama 11 wa CHADEMA wakamatwa kwa kufanya mkusanyiko usio halali - Wilayani Nkasi‎

    Jeshi la Polisi mkoa wa Rukwa limewakamata wanachama 11 wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kati yao wanaume 7 na wanawake 4 wakiwemo viongozi wanne wa chama hicho kwa kufanya mkusanyiko usio halali. Viongozi hao ni Winfrida Joseph Khenani (Katibu mwenezi wa Baraza la vijana CHADEMA...
  16. mcTobby

    Sawa CHADEMA imekufa, basi CCM fanyeni hivi

    Tokea magufuli amekufa tulisikia hiki kibwagizo kwamba CHADEMA ishakufa. Hadi sasa enzi za malkia kibwagizo ni kilekile kwamba Tanzania hakuna upinzani wa CHADEMA okay Nice nakubali. Sasa kwa vile CCM ni chama kikongwe na kina ushawishi barani Afrika kifanye hivi, kingewaruhusu tu hao...
  17. Nipe Maji

    SI KWELI PreGE2025 Msajili wa vyama vya siasa akiri kupokea barua ya CHADEMA kushiriki uchaguzi mkuu 2025

  18. Lord Denning

    Mahakama kwa kulinda Integrity na Trust ya Mahakama itisheni faili ya Kesi ya CHADEMA inayosimamiwa na Jaji Hamidu mfanye mapitio

    Nakujua vizuri wewe ni msabato safi unayependa Haki pamoja na mapungufu yako kama binadamu. Sidhani kama mnajua picha mnayojenga Mhimili wa Mahakama hasa kwenye kuaminika na kutenda Haki kwa Wananchi na Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kutokana na mwenendo mliokuwa nao miaka ya hivi karibuni...
  19. Waufukweni

    GE2025 Mwenezi BAWACHA, Sigrada Mligo ajiondoa CHADEMA, ahamia CHAUMMA

    Aliyekuwa Katibu Mwenezi wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) taifa, Sigrada Mligo, ametangaza kujiondoa rasmi ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akilalamikia kile alichokiita kauli za kubeza mchango wake na mazingira ya “unyanyasaji wa ndani ya chama.” Akizungumza na...
  20. Roving Journalist

    GE2025 Kesi ya Mgawanyo wa Mali CHADEMA imeahirishwa hadi Agosti 7, 2025

    Baada ya Jaji Hamidu Mwanga kusikiliza hoja za ombi la kutaka ajitoe kwenye Kesi namba 8323/2025 ambayo imetoa zuio la muda kwa Chama cha Chadema kufanya shughuli zozote zile kiutendaji na oparesheni, uamuzi wake unatarajiwa kutolewa Julai 28, 2025. Kesi iliyofunguliwa na aliyekuwa Makamu...
Back
Top Bottom