Akizungumza leo Jumanne, Oktoba 7, 2025, katika Wilaya ya Sengerema, jijini Mwanza, Dkt. Samia amesema: “Tutaheshimisha nchi yetu tukiwa na amani, tukifanya uchaguzi bila matatizo, vurugu au zogo. Tutaheshimisha nchi yetu tukizingatia sheria zetu, tukitafuta haki na kila mtu akapata haki yake.”