Abiria (kutoka neno la Kiarabu عبر ˁabara kwa maana ya kuabiri, kuvuka eneo la maji) ni watu wanaosafiri kwa kupanda meli, ndege, gari, basi, pikipiki au treni.
Abiria hutumia vyombo hivyo vya usafiri kama njia ni mbali, au kama hawana usafiri wa binafsi au kama wanapendelea matumizi ya usafiri wa umma kuliko usafiri wao binafsi.
Kwa kawaida wakipanda wanalipia kiasi fulani kama nauli ili mwenye chombo hicho aweze kuwalipa dereva na wahudumu wengine pamoja na gharama za chombo chenyewe na matumizi yake.
Adha ya usafiri kutoka jiji la Dar Es Salaam kwenda Mikoa mingine nchini bado imekuwa kitendawili ambacho kila Mwisho wa mwaka hasa mwezi wa 12 kinakosa kutenguliwa. Inaelezwa kuwa kwa mwezi wa 12 kwa mwaka huu 2025 Ongezeko la abiria limekuwa mara dufu na mapema sana(kuanzia Disemba 01, 2025)...
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limewakamata madereva watano wa magari ya kubebea wagonjwa kwa tuhuma za kubeba abiria kinyume cha sheria.
Kamanda wa Polisi mkoani humo, SACP Alex Mkama, amesema madereva hao waliokuwa wakisafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Kagera wamekamatwa kufuatia...
Baada ya siku 21 tangu kusitishwa kwa huduma ya mabasi yaendayo haraka katika barabara ya Mbagala kuelekea Gerezani na Kivukoni kufuatia uharibifu uliotokea wakati wa maandamano ya Oktoba 29, huduma hiyo imeanza rasmi kurejea leo kwa kubeba abiria.
Katika baadhi ya vituo vya Kilwa Road, mabasi...
Wakuu,
Serikali za kiafrika zina changamoto sana, kwamba bila kushinikizwa na vitisho haziwezi kujisimamia?
Au ni kwa sababu ya uchaguzi, kwamba ukipita wakishapata "ridhaa ya wananchi" tutarudi kukekule?
Hii inaweza kuwa danganya toto, watu wasihadaike maana hawa ccm wanajulikana kwa kuhadaa...
Hii siyo kwamba mtoto anaringishiwa nyonyo wakuu? Jana Ajira elfu 41, leo Mwendokasi Mbagala inaanza kubeba abiria kuna vimatukio flani hivi kama vya kupoza moto.
===
Ni rasmi mabasi yaendayo haraka (BRT) awamu ya pili barabara ya Mbagala (Kilwa), yameanza majaribio leo, Msemaji wa Serikali...
Kutokana na hizi changamoto ambazo zinazidi kuwa kubwa za usafirishaji wa abiria kwa njia ya mwendokasi, nimewaza ni kwa nini wenye mabasi ya coaster ya private (yale yasiyo na rangi maalumu za ruti), yasichukue hizi fursa za kusafirisha abiria hawa?
Maana yangu ni kwamba, chukulia wewe una...
Abiria ambao walikuwa kwenye usafiri wa daladala Eicher T 798 EDZ walijikuta katika taharuki baada ya gari hilo ambayo walikuwa wanasafiria kutoka Masaki kwenda Gongolamboto kuwaka moto kwa chini.
Moto huyo uligundulika na Wananchi ambao wapo nje ya gari hiyo na kusaidia gari hiyo kusimama na...
Abiria wanaotumia usafiri wa Mwendokasi wameshuka kupitia madirishani katika Kituo cha Magomeni Mwembechai, jijini Dar es Salaam, baada ya basi walilokuwa wakisafiria kusimamishwa na polisi kwa madai ya kuzidisha abiria kupita kiasi.
Tukio hilo lilitokea leo asubuhi, majira ya 08:25, ambapo...
Katika kuongeza mapato nchini na ukizingatia SGR inajaza siku 5 kabla ya safari. Inafaa sasa SGR kwa kushirikiana na TRA waaanzishe Kodi kwa abiria na Wasindikizaji wote angalau 20,000/= kila trip.
Kamanda wa Polisi Mkoa, Augustino Senga amesema Watu 5 wamefariki Dunia na wengine wanne kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria aina ya Hiace yenye Namba za usajili T476 DHL lililokuwa likitokea eneo la Chipaka lililopo Halmashauri ya Mji wa Tunduma Wilayani Momba Mkoani Songwe, kuelekea Mpemba...
Shirika la Ndege la Southwest Airlines Nchini Marekani, limetangaza sera mpya ambayo itawaathiri moja kwa moja Wasafiri wenye miili mikubwa ambao kuanzia Januari 27 2026 watalazimika kulipia siti mbili badala ya moja iwapo miili yao haitoenea vizuri ndani ya siti moja.
Kabla ya sera hii mpya...
Nauli za usafiri wa anga wa kimataifa huenda zikapanda kwa dola 45 kwa tiketi ya safari ya njia moja na dola 90 kwa safari ya kwenda na kurudi endapo ada mpya itaanza kutekelezwa kama ilivyopangwa.
Serikali inapanga kuanzisha ada ya urahisishaji wa abiria kwa wasafiri wote wa kimataifa kuanzia...
Mimi naishi Mvuti, ni mbali kidogo mpaka kufika mjini ila barabara yote ni mkeka mpaka mjini ninakofanyia kazi.
Barabarani nimeona sana damu za bodaboda na abiria wao.
Ukiona watu wamezunguka na mtu kafunikwa mtandio tayari aidha bodaboda au abiria wake hana uhai.
Siku moja niliona utumbo wa...
Mwenye uelewa na haya mambo, nakumbuka zamani haikuwa issue kubadili lori na kuwa basi la abiria kwa kuunda na kuvisha bodi.
Je hili linawezekana leo? manake unaweza kubadilisha alafu ukaambiwa haijakidhi viwango. Mwenye taarifa sahihi weka mezani. Asante
Usafiri wa gari za kutoka Jiji la Mbeya kuelekea Wilayani Kyela uliyumba kwa saa kadhaa jana Agosti 7, 2025 baada ya madereva wa magari ya abiria kugoma, wakilalamikia kero, usumbufu na faini kubwa zisizoendana na uhalisia na hali ya kipato chao kutoka kwa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.