Recent content by Kinnega

  1. K

    Ikulu yanuka ukabila?

    Wafanyakazi inabidi walipwe laki 5 kama hukosei. Na kama unakosea?
  2. K

    Accidents at Kibaha: A Scientific Reason?

    Na kama kumbukumbu zako zitakuwa sio sahihi? Hata watoto ukiwasomea hadithi ukaanza na "kama sikosei" wataona bora wakacheze ukuti wa mnazi.
  3. K

    Tulipokwama kama Taifa; tutajinasua?

    Hili neno la uzima limetulia kweli kweli, isipokuwa tu haliko kwenye jamvi lake. Sijui kama taratibu zimebadilika, lakini ilikuwa unawatumia wahusika ujumbe binafsi wakuwie ruksa kubandika mawaidha yako mawili matatu kwenye jukwa husika. Sio jamvi la siasa. Enenda na amani ya Bwana, na...
  4. K

    Accidents at Kibaha: A Scientific Reason?

    Umejuaje? Lete chanzo, lete takwimu. Utapataje majibu ya "kisayansi" kwa maswali ya kisiasa?
  5. K

    GE2010 Kanuni za Uchaguzi 2010 na mgogoro wa Sheria ya Gharama

    Mheshimiwa Dr. Slaa, wewe ni kiongozi, Mbunge wetu, huwezi kututamkia "Watanzania hawaelewi issues"! Kisiasa inaonyesha hujali hata kutuonyesha unanyenyekea kwa tuliokupa taadhima ya kutuongoza, na ulivyo mwepesi kutumia lugha za kujumuisha watu jumla jumla na kuwashusha. Tafadhali Mheshimiwa...
  6. K

    World's cleverest man turns down $1million prize after solving one of mathematics' gr

    Basi kama unakubali kwamba nadharia ya “Taifa Teule” ni hekaya, na kwamba kipaji chake hakitokani na Uyahudi wake, unapoona taarifa ya Myahudi mwenye kipaji acha kujikunja kinyumenyume kuimbia sifa weledi wa taaluma wa Wayahudi wa miaka elfu tano ulela. Toa muktadha wa uhusiano wa kipaji na...
  7. K

    GE2010 Kanuni za Uchaguzi 2010 na mgogoro wa Sheria ya Gharama

    Mheshimiwa Dr. Slaa ametuambia amepitia "Kumbukumbu Rasmi za Bunge" na "Schedule of Amendments" na kuhitimisha kwamba swala hili halikupitishwa na Bunge. "Hansard" ni Kitabu cha Kumbukumbu ya Mazungumzo katika Bunge. Je pia rekodi rasmi ya kila kilichofanyika Bungeni? Vipi kama kipengele...
  8. K

    World's cleverest man turns down $1million prize after solving one of mathematics' gr

    Elimu ya vinasaba na asili ya viumbe hai inafundisha kwamba hakuna kundi lolote la binadamu au Wamakonde, au Wayahudi au Mataifa, ambalo lina kipaji cha akili kuliko kundi lingine liwalo lote. Inatakiwa nirudie, hakuna! Ulichoeleza kinasaidia kufasili ni kwa nini kuna Wayahudi wengi waliobobea...
  9. K

    GE2010 Kanuni za Uchaguzi 2010 na mgogoro wa Sheria ya Gharama

    Ningeziona hizo kanuni ndio ningeweza kumuunga mkono Mh. Dr. Slaa, au kutofautiana nae.
  10. K

    john mnyika wa CHADEMA alipata Div ngapi?

    Hizo ulizotoa ni taarifa za matokeo ya mitihani yote miwili, kidato cha nne na sita? "Kama sikosei...sina hakika...kama nakumbuka...washashi nisahihisheni" zimesheheni kujengea msingi wa hoja ya kumwombea msamaha mtahiniwa ukitetea matokeo. "Kama nakumbuka vizuri," kama unakumbuka vibaya...
  11. K

    tatizo lafoleni TZ ni udogo wa barabara

    "Endapo wakijenga," kina nani wakijenga? Usiniambie tukutanulie barabara ili siku "ukipata bahati" ya kwenda kwenu utanue. Una jukumu, sio "ukipata bahati," una wajibu wa kwenda kujenga ardhimama yako! Kipaumbele chetu cha kwanza sasa hivi sio kutanua upana wa barabara. Usiwe nje ya mguso...
  12. K

    Hata ikisainiwa kwa mbwembwe; sheria hii bado ni mbaya!

    Duu, ndugu mwandishi umetuchambulia na kututafsiria sheria na katiba kwa staili ya meza kama ilivyo, bila kutupa nukuu ya kipengele hata kimoja. Sheria inakosea, sheria inasema, sheria inakataza... Sheria inasemaje?
  13. K

    Controversial Masaki plot declared open space

    Basi wanajamvi na "harakati za komputa" wazidi kuwa na nguvu, na wapongezwe, kama ndivyo. Lakini wakati tunapima ufanisi na tija ya mchango wa JF, ingependeza tujue wana JF walifanya nini katika kuzuia majengo haya yasiendelee. Katika maandamano ya wakazi wa eneo hilo kulikuwa na bango la...
  14. K

    Jipatie Nakala yako: Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania by Nyerere

    Sio baraza la mawaziri kwa ujumla wake ndio linaamua ubinafsishaji wa shirika kama NBC? Kama mwenyekiti wa baraza la mawaziri kala hongo halafu kapigia chapuo kuuza kipande cha nchi na wajumbe wa kikao wamenyweshwa chai na chapati za Ikulu wakalala kikaoni hoja ikapita basi kosa la kuuza NBC...
  15. K

    Kulikoni ITV kutotangaza habari za Simba SC?

    Sio swala la "Wana Simba mmekereka," ni swala zaidi la kiufundi/kikazi kuhusu uandishi habari nchini: Jana habari muhimu kuliko zote nchini kimichezo ilikuwa ni kuna timu imeshinda ubingwa, haijalishi ni ipi, kuna mechi iliyoamua klabu bingwa itakayoiwakilisha Tanzania kimataifa. Utaachaje...
Back
Top Bottom