Elections 2010 Kanuni za Uchaguzi 2010 na mgogoro wa Sheria ya Gharama

Status
Not open for further replies.
Mie nashangaa inakuwaje watu wale wale (wasio na udhu) waliotumia fedha chafu katika uchaguzi uliopita leo hii hata bila soni wanatia sahihi mkataba huo kwa mbwembwe bila hata kuwaomba wananchi radhi kwa vitendo viovu walivyofanya katika uchaguzi uliopita. Kama kweli CCM na Serikali yake wana nia njema na hiyo sheria mpya ya uchaguzi, jambo ambalo wangelipaswa kufanya ni kutamka wazi kabisa kwamba Sisi CCM tuliwakosea wananchi katika uchaguzi uliopita kwa kutumia fedha nyingi chafu na safi ili tupate uongozi. Kwa dhambi hiyo tuliyoifanya, tunaomba radhi sana na tunatarajia wananchi watatusamehe ili tuweze kuanza ukrasa mpya.

Nina uhakika wapo Watanzania waliosonya kwa hasira kuona mbwembwe zisizo za lazima katika utiaji sahihi wa sheria hiyo.
 
Mheshimiwa Dr. Slaa ametuambia amepitia "Kumbukumbu Rasmi za Bunge" na "Schedule of Amendments" na kuhitimisha kwamba swala hili halikupitishwa na Bunge.

"Hansard" ni Kitabu cha Kumbukumbu ya Mazungumzo katika Bunge. Je pia rekodi rasmi ya kila kilichofanyika Bungeni? Vipi kama kipengele ndani ya mswaada kikiwasilishwa lakini kisizungumzwe, kitakuwepo kwenya "Kitabu cha Kumbukumbu ya Mazungumzo katika Bunge"?

Na, "Schedule of Amendments" nadhani ni orodha ya vipengele vilivyopangwa au vilivyotakiwa kufanyiwa maboresho. Lakini kilichopangwa huwa ndio kinachofanyika?

Mheshimwa Dr. Slaa angetuonyesha nyaraka ambayo ni toleo rasmi la mwisho la muswada ambao umepigiwa kura na wabunge, sio kumbukumbu ya mazungumzo.

Wana JF,

...sehemu ya 7(3) ambayo haikujadiliwa kabisa Bungeni. Nimeipitia Hansard, nimepitia Schedule of Ammendment, nimepitia na Majadiliano ndani ya Bunge katika Kumbukumbu Rasmi ya Bunge yaani Hansard, iliyoandaliwa tarehe 16/2/2010...
 
Dr. Slaa please kama unauhakika na hilo, nenda mahakamani. Tuko nyuma yako, hata gharama za kesi ni(tu)tachangia, naamini tuko wengi ambo tumechoka na kufanya wajinga.
Tafadhali lifikishe kwa Spika wa bunge rasmi na tusikie msimamo wake. Mahakamani ni lazima...huu ni uhaini.
 
Mheshimiwa Dr. Slaa ametuambia amepitia "Kumbukumbu Rasmi za Bunge" na "Schedule of Amendments" na kuhitimisha kwamba swala hili halikupitishwa na Bunge.

"Hansard" ni Kitabu cha Kumbukumbu ya Mazungumzo katika Bunge. Je pia rekodi rasmi ya kila kilichofanyika Bungeni? Vipi kama kipengele ndani ya mswaada kikiwasilishwa lakini kisizungumzwe, kitakuwepo kwenya "Kitabu cha Kumbukumbu ya Mazungumzo katika Bunge"?

Na, "Schedule of Amendments" nadhani ni orodha ya vipengele vilivyopangwa au vilivyotakiwa kufanyiwa maboresho. Lakini kilichopangwa huwa ndio kinachofanyika?

Mheshimwa Dr. Slaa angetuonyesha nyaraka ambayo ni toleo rasmi la mwisho la muswada ambao umepigiwa kura na wabunge, sio kumbukumbu ya mazungumzo.

Hapo rend font mkuu hakuna uwezekano kama huo. Hata kama kisizungumzwe, kitatajwa!

Mimi ni kama nilivyosema kule kwenye thread nyingine kwamba, lengo la sheria hii ni kudhibiti vyama vingine. Rais anajidai kuonyesha kukerwa na tatizo la funding lakini mazungumzo yanaonyesha kwamba hata yeye alipita kwa mtindo kama huo. Ni munufaikaji wa mfumo huo. Asitudanganye.

Hiyo ilistahili kuwa sheria ya CCM na katiba yao
 
hivi unategemea nini unapokuwa na rais anayependa sifa sifa tu hana hata muda wa kusoma vitu na hayo ndo nadhara yake..akiambiwa anacheka cheka mnakataa....unawekaje siginecha bila kusoma vitu kwa undani?
 
Mheshimiwa Dr. Slaa ametuambia amepitia "Kumbukumbu Rasmi za Bunge" na "Schedule of Amendments" na kuhitimisha kwamba swala hili halikupitishwa na Bunge.

"Hansard" ni Kitabu cha Kumbukumbu ya Mazungumzo katika Bunge. Je pia rekodi rasmi ya kila kilichofanyika Bungeni? Vipi kama kipengele ndani ya mswaada kikiwasilishwa lakini kisizungumzwe, kitakuwepo kwenya "Kitabu cha Kumbukumbu ya Mazungumzo katika Bunge"?

Na, "Schedule of Amendments" nadhani ni orodha ya vipengele vilivyopangwa au vilivyotakiwa kufanyiwa maboresho. Lakini kilichopangwa huwa ndio kinachofanyika?

Mheshimwa Dr. Slaa angetuonyesha nyaraka ambayo ni toleo rasmi la mwisho la muswada ambao umepigiwa kura na wabunge, sio kumbukumbu ya mazungumzo.

Nadhani umemiss kitu kimoja muhimu. Kwenye muswada (bill) uliopelekwa bungeni kwa mjadala na hatimaye kupitishwa na bnge hicho kipengele hakipo. Hivyo kwa Dr Slaa kwenda kwenye 'kumbukumbu' nyingine naamini ilikuwa ni kujaribu kujiridhisha kwamba hakukuwapo na namna nyingine rasmi ambayo ilipelekea kifungu hicho kuongezwa na bunge.
 
Serikali yakiri hoja ya Dk. Slaa nzito
• Mwanasheria Mkuu ajiandaa kuomba radhi

SIKU moja baada ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, kudai Rais Jakaya Kikwete amepotoshwa kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi, serikali imesema itaomba radhi na kurejesha muswada huo bungeni.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alisema:
"Kama kweli ikithibitika, tuko tayari kuomba msamaha na kurudisha bungeni suala hili ili lifanyiwe marekebisho… namhakikishia Dk. Slaa kuwa tutarudisha bungeni ili makosa hayo yaondolewe. "Siamini na si dhani kama ni kweli, kwa sababu eneo hilo nakumbuka lilijadiliwa kwa kina mno, tena Dk. Slaa na John Cheyo (Mbunge wa Bariadi Mashariki) walitoa mchango mzuri uliozua mjadala mrefu na hatimaye tukafikia mwafaka."
 
Serikali yakiri hoja ya Dk. Slaa nzito
• Mwanasheria Mkuu ajiandaa kuomba radhi

SIKU moja baada ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, kudai Rais Jakaya Kikwete amepotoshwa kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi, serikali imesema itaomba radhi na kurejesha muswada huo bungeni.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alisema:
“Kama kweli ikithibitika, tuko tayari kuomba msamaha na kurudisha bungeni suala hili ili lifanyiwe marekebisho… namhakikishia Dk. Slaa kuwa tutarudisha bungeni ili makosa hayo yaondolewe. “Siamini na si dhani kama ni kweli, kwa sababu eneo hilo nakumbuka lilijadiliwa kwa kina mno, tena Dk. Slaa na John Cheyo (Mbunge wa Bariadi Mashariki) walitoa mchango mzuri uliozua mjadala mrefu na hatimaye tukafikia mwafaka.”
Sasa Kumekucha.Ndiyo maana nikasema kama ushahidi wa Mh. Dr Slaa Unajitosheleza hiyo sheria ni batili kwa mantiki ya kwamba kilichopitishwa na bunge kama sheria tarajiwa sicho kilichosainiwa kuwa sheria kamili kwa mantiki ya kwamba kuna kifungu kimeongezwa.Rais na wasaidizi wake wa karibu walitakiwa wawe na nakala zote mbili kilichopitishwa na bunge na anachotakiwa kukisaini ili kujiridhisha kabla kumwaga wino yaani hiyo ni aibu ukosaji wa umakini uliyokidhiri, ni vipi Rais unapotoshwa? hii inaonyesha uvivu wa kupitia mambo au kusoma.Sikumoja watakuja saini mkataba wa kuiuza nchi bure kwa watu wengine na hapo ni Irreversible action,au kwa lugha ya mtaani ikirudi pancha.Mungu Ibariki Tanzania tuipushie viongozi wa aina hii wasio kuwa makini!
 
Serikali yakiri hoja ya Dk. Slaa nzito

• Mwanasheria Mkuu ajiandaa kuomba radhi

na Kulwa Karedia

SIKU moja baada ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, kudai Rais Jakaya Kikwete amepotoshwa kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi, serikali imesema itaomba radhi na kurejesha muswada huo bungeni.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alisema:

“Kama kweli ikithibitika, tuko tayari kuomba msamaha na kurudisha bungeni suala hili ili lifanyiwe marekebisho… namhakikishia Dk. Slaa kuwa tutarudisha bungeni ili makosa hayo yaondolewe.


“Siamini na si dhani kama ni kweli, kwa sababu eneo hilo nakumbuka lilijadiliwa kwa kina mno, tena Dk. Slaa na John Cheyo (Mbunge wa Bariadi Mashariki) walitoa mchango mzuri uliozua mjadala mrefu na hatimaye tukafikia mwafaka.”

Dk. Slaa alidai Rais Kikwete amepotoshwa katika baadhi ya vipengele, kikiwamo kipengele kinachohusu uthitibishwaji wa wajumbe wanaounda timu za kampeni kwa ajili ya wagombea urais, wabunge na udiwani.

Alisema Bunge halikukubaliana kuhusu kipengele hicho, wala hakimo katika kumbukumbu za Bunge; na kwamba kiliongezwa baadaye, kabla ya Rais Kikwete kusaini muswada huo kuwa sheria.

Hata hivyo, Jaji Werema alishtushwa na kauli ya Dk. Slaa, na kudokeza kwamba inawezekana hata mwanasiasa huyo hakukielewa vema kipengele hicho.

“Nimeshutushwa na kauli ya Dk. Slaa… wasaidizi wangu wameniambia haya mambo, saa sijui tatizo liko wapi… nafikiri anapaswa kuelimishwa tu.

“Tunajua sasa zipo kampeni, hivyo kila mtu anataka kufanya au kufuatilia kwa makini sheria hii, sasa namshauri Dk. Slaa aisome kwa makini,” alisema Jaji Werema.

Alisema kumbukumbu zinaonyesha kuwa wakati wa kujadili muswada huo kila kipengele kilipitiwa kwa umakini wa hali ya juu na kuridhiwa na wabunge.

“Nakumbuka katika kumbukumbu zangu wakati tunajadili muswada huu tulipitia kipengele kwa kipengele; sasa haya mengine yatakuwa yametoka wapi?” alihoji Jaji Werema.

Alisema kama kweli kutakuwa na baadhi ya vipengele ambavyo vitakuwa vimechomekwa kwenye sheria hiyo kinyemela, sheria hiyo inaweza kurudishwa bungeni kwa ajili ya kufanyiwa marekebisho haraka.

Akizungumzia sheria hiyo, juzi Dk. Slaa alisema anashangazwa na kilichotokea Ikulu siku Rais Kikwete aliposaini sheria hiyo.

Dk. Slaa alisema atamchukulia hatua mtu aliyehusika kuongeza kipengele hicho bila idhini ya Bunge.

Katika kushangaa huko, Dk. Slaa alionyesha kitabu cha kumbukumbu za Bunge (Hansard), ambacho hakionyeshi viongozi wanaopaswa kufanya uhakiki wa timu za kampeni za wagombea.

“Katika sheria aliyosaini rais kuna kifungu cha 7 (3), ambacho hakikuwepo kabisa kwenye muswada uliojadiliwa na kupitishwa bungeni, kwa kweli nimeshangazwa sana, kwa sababu rais amedanganywa,” alisema Dk. Slaa.

Kabla ya kuzungumza na Jaji Werema, gazeti hili liliwasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salvatory Rweyemamu, ili atoe msimamo wa Ikulu. Alisema hana jibu, akamshauri mwandishi wa habari hizi kuwasiliana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, kwa kuwa ndiyo inayohusika zaidi na suala hilo.

“Sina cha kujibu katika hili, nakuomba uwatafute watu wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, hawa ndio wako kwenye nafasi ya kuzungumzia suala hili kwa kina,” alisema Rweyemamu.


NIMEAMINI: MBUNGE MMOJA WA CHADEMA NI WABUNGE 60 WA CCM
 
Kama ni kweli suala hili basi serikali imedhibitisha ni jinsi gani inavyolidharau Bunge na Rais JK anazidi kuaibishwa maana kila akifanyacho kwa Mbwembwe nyuma yake kuna usanii na wanamfedhehesha. Bado tunakumbuka ufunguzi wa hotel Arusha na kesho yake kubomolewa au ule uzinduzi wa Tamasha la malaria huku akifanywa "mradi"
 
Kama ni kweli suala hili basi serikali imedhibitisha ni jinsi gani inavyolidharau Bunge na Rais JK anazidi kuaibishwa maana kila akifanyacho kwa Mbwembwe nyuma yake kuna usanii na wanamfedhehesha. Bado tunakumbuka ufunguzi wa hotel Arusha na kesho yake kubomolewa au ule uzinduzi wa Tamasha la malaria huku akifanywa "mradi"

Unanikumbusha lille la msaada wa MCC ambapo raisi alikabidhiwa mfano wa cheki where the amount in figures differs with the amount in words.
 
Kwa mara nyingine tena huu ni upuuzi wa rais iweje adanganywe kila siku yeye jaman...cheki feki yeye na sheria za nchi tena loh!!!
 
Kwa mara nyingine tena huu ni upuuzi wa rais iweje adanganywe kila siku yeye jaman...cheki feki yeye na sheria za nchi tena loh!!!

Yako mengi sana ambayo Mkuu wa Kaya amekuwa akipelekwa kwenye njia za mbigiri; Ufunguzi wa Snow Crest Hotel Arusha ambayo siku chache baadaye TANROADS waliipiga nyundo, kuitwa Ikulu Mkurugenzi wa Ngorongoro badala ya Longido wakati wa kukabidhi gari la wagonjwa.

Nakumbuka siku za nyuma Spika alimshauri aongeze ukali kidogo lakini watu walifikiri ilikuwa dhihaka kwake ila ukweli ni kuwa Mkuu na wanaomshauri hawako makini hata kidogo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom