Featured content

Mahakama: Kifungu kinachoruhusu mashahidi wa kesi wa kificho ni batili na kinyume na Katiba
Mahakama Kuu Mwanza imesema Kifungu cha 194 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kinachoruhusu kuficha mashahidi ni batili na kinyume na Katiba. Serikali imepewa miezi 12 kurekebisha Sheria hiyo ili iendane na Katiba kabla ya kuondolewa au kubadilishwa rasmi. Uamuzi huo umetolewa Februari 16, 2026 katika Shauri la Kikatiba Namba 22482/2025 kati ya Godfrey Mjuni Martin Basasingohe dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Mashtaka
Rasmi: Gamondi asaini mkataba wa miaka miwili kuinoa Taifa Stars
Kocha Miguel Gamondi Februari 16, 2026 amesaini mkataba rasmi wa miaka miwili kuinoa timu ya Taifa ya soka ya Tanzania (Taifa Stars). Gamondi ataiongoza Taifa Stars kuelekea michuano ya AFCON 2027, itakayofanyika katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda, akiindeleza mafanikio aliyoyapata katika AFCON 2025, ambapo timu ya taifa ya Tanzania ilitinga hatua ya 16 bora.
AFCON 2027: CAF yathibitisha Tanzania, Uganda na Kenya kuandaa michuano hiyo
Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe amesema Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) ijayo, itafanyika Mwaka 2027 nchini Kenya, Tanzania na Uganda kama ilivyopangwa na kwamba siyo Mwaka 2028 kama baadhi tetesi zinavyodai. Akizungumza Februari 13, 2027 kwenye Kikao cha Kamati ya Utendaji ya CAF kilichofanyika jijini Dar es Salaam, Motsepe amesema “Madai kuwa ninaondoa AFCON kwa sababu nchi zetu tatu hazijawa tayari hayana msingi wowote.”
Songwe: Mwenyekiti wa Umoja wa Madereva wa Malori, Godlove Materu aachiwa kwa dhamana
Mwenyekiti wa Taasisi ya Taifa ya Taaluma ya Madereva Tanzania (TATAMATA), Godlove Materu, ameachiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kukamatwa Februari 5, 2026, kufuatia kudhaminiwa na mke wake Februari 9, 2026. Materu alidaiwa kukamatwa Februari 5, 2026 na watu wasiojulikana, na Februari 8 viongozi wa TATAMATA waliwapa Polisi siku mbili awe amepatikana, usiku huohuo Jeshi la Polisi Songwe lilikiri kumshikilia kwa tuhuma za kijinai.
Kesi ya Lissu | Tundu Lissu: Mimi sijala
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, anayekabiliwa na kesi ya uhaini, aliahirishiwa shauri lake baada ya kuiambia Mahakama kuwa 'hajala', hali iliyowafanya baadhi ya wafuasi wake kulia na wengine kupoteza fahamu. Jaji Dastan Ndunguru akaamua kuahirisha kesi hiyo.
AFCON 2027: CAF huenda ikaahirisha mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika
Gazeti la The Guardian la Uingereza limeripoti kwamba mashindano hayo yanaweza kusogezwa hadi mwaka 2028, likitoa sababu mbili kuu: nchi mwenyeji Kenya, Uganda na Tanzania bado hazijawa tayari kikamilifu kuandaa mashindano hayo makubwa na ratiba ya uchaguzi wa Kenya mwaka 2027, ambayo huenda ikaleta mazingira yasiyo tulivu kwa maandalizi na usalama wa mashindano. Kwa sasa, timu ya ukaguzi kutoka Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) iko nchini Tanzania
Zambia: Mahakama yataifisha Magari 79, mali 23 za Mtoto wa Rais wa zamani, Edgar Lungu
Mahakama ya Makosa ya Uhujumu Uchumi na Fedha nchini Zambia imetaifisha magari 79 na mali 23 zisizohamishika zinazomilikiwa na Dalitso Lungu, Mtoto wa Rais wa zamani wa Nchi hiyo, Edgar Lungu, baada ya kuamua kuwa mali hizo zilitokana na uhalifu. Uamuzi huo ulitokana na maombi yaliyowasilishwa chini ya Kifungu cha 29 cha Sheria ya Kutaifisha Mapato ya Uhalifu Na. 19 ya Mwaka 2010, yaliyolenga kutaifishwa kwa mali za Dalitso bila kuwepo hukumu ya jinai.
Gerson Msigwa: Maridhiano ni jambo la hiari sio kulazimishwa
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, akizungumza Februari 10, 2026 katika mahojiano na BBC Swahili, amesema endapo kutakuwa na wadau watakaokataa kushiriki kwenye maridhiano mara mchakato huo utakapoanza, hawatalazimishwa kwani ushiriki ni wa hiari. Ameongeza kuwa anayekataa kutambua uchaguzi anapaswa kuwa na hoja za msingi, na kwamba uchaguzi ulifanyika kwa mujibu wa sheria, kwa misingi ya uhuru na haki; walioshinda wameshinda na walioshindwa kura hazikutosha.
Tanzania yaomba msaada China kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya AFCON  2027
Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Mwaka Mpya wa Kichina yaliyofanyika Februari 6, 2026 katika Ubalozi wa China, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, James Millya aliiomba Serikali ya China kuisaidia Tanzania kujenga miundombinu ya kisasa kwa ajili ya mashindano ya AFCON yanayotarajiwa kufanyika Mwaka 2027. Tanzania inajenga viwanja vitatu kwa ajili ya maandalizi ya michuano hiyo, ikiwemo Kiwanja cha Fumba - Zanzibar, Samia Suluhu kilichopo Mkoani Arusha, pamoja na Uwanja wa Dodoma.
Nchimbi: Tumuombee Rais Samia, Mungu afunge mageti ya Ikulu dhidi ya Watu wabaya
Makamu wa Rais, Emmanuel Nchimbi, amewaomba viongozi wa dini kuendelea kumuombea Rais Samia dhidi ya watu wabaya, ili wasipate nafasi ya kumsogelea au kuingia Ikulu. Pia, kupitia maombi hayo, Rais aweze kutambua wezi, waongo, wafitini, watu wasio waaminifu, na wale wenye mawazo ya kumwaga damu au kuleta madhara. Amesema hayo Februari 6, 2026 wakati wa hafla ya Usimikaji na Uzinduzi wa Uongozi wa Awamu ya Tano wa The Council Of Pentecostal Churches Of Tanzania (CPCT) iliyofanyika Ukumbi wa Agape
Jamhuri ya Kongo: Rais Sassou (82) kugombea tena urais baada ya miaka 42 madarakani
Akiwa na miaka 82, Rais wa Jamhuri ya Kongo, Sassou N’guesso ametangaza kugombea tena urais katika uchaguzi wa Machi 15, 2026, baada ya kuwa madarakani kwa jumla ya miaka 42. Aliingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 1979 hadi 1992, kisha akarudi mwaka 1997 baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe. Tangu wakati huo, ameshinda chaguzi nne mfululizo, huku marekebisho ya katiba mwaka 2015 yakimruhusu kuendelea kugombea bila kikomo cha umri au vipindi vya urais.
Tunduma: Polisi wakiri kumkamata Dereva wa Malori. Yadaiwa alipanga kufanya uhalifu
Baada ya Chama cha Madereva wa Malori kutangaza mpango wa kufanya mgomo iwapo mwenzao asingepatikana ndani ya siku mbili, Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limetoa ufafanuzi likikanusha taarifa zinazosambazwa mitandaoni kuwa Godlove Materu hajulikani alipo baada ya kukiri kumshikilia. Polisi wamesema Materu, mkazi wa Tunduma, alikamatwa kwa tuhuma za kijinai, wakiongeza kuwa alipanga kufanya uhalifu katika maeneo mbalimbali Tunduma. Wamesema uchunguzi umekamilika na hatua za kisheria zinaendelea
Nape: Vyombo vya Dola visipojali UTU, CCM itang'oka!
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye ametahadharisha kuwa bila kusimamia utu, Chama cha Mapinduzi (CCM) inaweza kuondoka madarakani hivyo akaonya wanachama ndani ya chama hicho wasione aibu kusimamia utu. Nape aliyewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ametoa kauli hiyo bungeni leo Alhamisi Februari 5,2026 wakati akichangia Mapendekezo ya Mpango wa Serikali uliowasilishwa mwanzoni mwa wiki na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na...
Mpenzi wangu ana-chat sana na ex wake, nikimuuliza anadai ni mazoea tu!
Mdau wa JamiiForums ameomba ushauri baada ya kuwa mpenzi wake anatumia muda sana ku-chat na mpenzi wake wa zamani (ex). Anasema hali hii inampa wasiwasi huenda mpezi wake amepata mpenzi mwingine. Anauliza amuulize au akae tu kimya atabadilika?
Mizania: Mkojo wa Ngamia ni salama kutumika kama dawa kwa binadamu
Wadau wamekuwa wakihoji ikiwa kama mkojo wa Ngamia ni Dawa au lah, baada ya video mtandaoni kusambaa zikionyesha Wananchi kutoka Tanzania wakiumwa kwaajili ya kutibu. Kwa mujibu wa WHO, mkojo wa Ngamia hauna faida ya Kitabibu kwa wagonjwa wa Saratani na unaweza kusababisha maambukizi kama Brucellosis. Matumizi yake yanahusishwa zaidi na imani za kidini.
Nyaraka za Siri za Epstein: Kisiwa cha Mnemba kama 'Uchochoro' nchini Tanzania
Februari 4, 2026 DAR ES SALAAM — Kwa muda mrefu, yamekuwepo maneno ya chini kwa chini, tetesi zilizopuuzwa kama umbea wa vijiweni. Lakini sasa, swali sio tena kama Tanzania inahusika kwenye mtandao wa uhalifu wa ngono wa Jeffrey Epstein, bali ni mizizi hiyo imechimba kirefu kiasi gani. Kufuatia hatua ya Wizara ya Sheria ya Marekani (DOJ) kumwaga hadharani kurasa milioni tatu za nyaraka nzito wiki hii, "Kivuli cha Epstein" kimetua rasmi katika ardhi ya Tanzania. Tofauti na nyaraka za awali...
Matokeo ya Kidato cha Nne 2025 yatangazwa. Ufaulu wapanda
Ufaulu Umepanda. Futatilia hapa. https://www.youtube.com/live/uwbLeIIRXOc?si=m-Iyj06qeAYHlPCl Kupata Matokeo fungua link hii: https://matokeo.necta.go.tz/results/2025/csee/index.htm --- Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika kuanzia Novemba 17, 2025. Matokeo hayo yametangazwa leo Jumamosi Januari 31, 2026 na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Profesa Said Mohammed. Jumla ya wanafunzi 569,883 walifanya...
Tanzania kuuza sehemu ya Hazina yake ya Dhahabu kusaidia kufadhili miradi ya miundombinu
Tanzania inapanga kuuza sehemu ya hazina yake ya dhahabu kusaidia kufadhili miradi ya miundombinu, kufuatia kupungua kwa msaada wa wafadhili ambao kumelazimisha serikali kutafuta vyanzo vya ndani vya fedha. Rais Samia Suluhu Hassan amekubali uamuzi huu, akizingatia usimamizi wa rasilimali za ndani ili kukabiliana na mahitaji ya kifedha. Benki Kuu ya Tanzania imeripoti kuwa kuna hazina kubwa ya dhahabu, ikionyesha uwepo wa rasilimali muhimu kwa juhudi kama hizi. Marekebisho ya kiuchumi...
Wapiganaji 5 wa ISIS raia wa Tanzania wakamatwa Somalia
Serikali ya Jimbo la Puntland imetoa picha na maelezo rasmi yanayowaonyesha makumi ya wapiganaji wa kigeni wa kundi la Islamic State (ISIS-Somalia) waliokamatwa wakati wa operesheni ya kupambana na ugaidi inayoendelea katika safu ya milima ya Calmiskaad (Al-Miskad) kwenye Milima ya Golis. Kwa mujibu wa Idara ya Kupambana na Ugaidi (CT) ya Puntland, mahabusu hao walikamatwa wakati wa "operesheni endelevu za kijeshi zinazolenga maficho ya ISIS katika Milima migumu ya Al-Miskaat, ambayo...
Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei afariki Dunia
Wakuu, Heche kupitia mtandaoni ametangaza kifo cha mwasisi wa chama chao CHADEMA, Mzee Edwin Mtei baada ya familia kuthibitisha huku mipango ya mazishi ikiendelea nyumbani kwake Tengeru, Arusha. ===== Baadhi ya mambo muhimu kuhusu Ediwin Mtei ambayo pengine ulikuwa hufahamu Elimu,"Shahada ya Sanaa (Political Science, History, Geography) - Makerere (1957)" BoT, Gavana wa kwanza (1966–1974) Uwaziri, Waziri wa Fedha (1977–1979) Siasa, Muasisi na Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA (1992)...
Back
Top Bottom