Serikali ya Sierra Leone imefuta mashtaka yote, yakiwemo ya uhaini, yaliyokuwa yakimkabili Rais wa zamani wa nchi hiyo, Ernest Bai Koroma, aliyekuwa akihusishwa na jaribio la mapinduzi ya serikali lililotokea mwaka 2023.
Koroma, mwenye umri wa miaka 72, amekuwa akikanusha kuhusika na jaribio hilo la mapinduzi la Novemba 2023. Katika tukio hilo, watu wenye silaha walivamia ghala la silaha la jeshi na magereza kadhaa, ambapo wafungwa wapatao 2,000 walitoroshwa.