Serikali ya Guinea ya Ikweta imejiuzulu kwa kutofikia malengo yake, huku serikali mpya ikitarajiwa kuundwa hivi karibuni.
Makamu wa Rais, Teodoro Nguema Obiang Mangue, amesema Waziri Mkuu, Manuel Osa Nsue Nsua, amewasilisha barua ya kujiuzulu kwa niaba ya baraza zima la mawaziri lililoteuliwa mwaka 2024 baada ya serikali kufikia chini ya asilimia 10 ya malengo yaliyowekwa, akisisitiza kuwa uwajibikaji wa umma lazima uendane na matokeo.