Featured content

Serikali: Mchakato wa Katiba Mpya utaanza baada ya Maridhiano, Rais ataeleza muda ukifika
Serikali kupitia Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Homera, imesema mchakato wa kushughulikia Katiba Mpya utatekelezwa baada ya kukamilika kwa kazi za tume husika pamoja na mchakato wa maridhiano unaoendelea nchini. Akizungumza 17 Juni 2026 jijini Dodoma, Dkt. Homera amesema Serikali inaendelea kuweka kipaumbele katika hatua mbalimbali za kitaasisi ili kuhakikisha masuala hayo yanakamilika kabla ya kuendelea na mchakato wa Katiba Mpya.
Marekani na Iran zasaini mkataba wa awali wa kusitisha Vita
Rais Donald Trump amesaini nakala ya makubaliano kati ya Marekani na Iran katika Jumba la Kifalme la Versailles nchini Ufaransa, na kuhitimisha ziara yake ya G7. Kwa mujibu wa afisa mmoja wa Marekani, baada ya hapo Marekani iliwatumia Wairani picha ya makubaliano hayo yaliyosainiwa. Waraka huo kisha ukasainiwa na Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian. Makubaliano haya yanazitaka Marekani na Iran kufikia mkataba wa mwisho na kamili ndani ya siku 60.
Serikali ya Guinea ya Ikweta yajiuzulu baada ya kutofikia malengo
Serikali ya Guinea ya Ikweta imejiuzulu kwa kutofikia malengo yake, huku serikali mpya ikitarajiwa kuundwa hivi karibuni. Makamu wa Rais, Teodoro Nguema Obiang Mangue, amesema Waziri Mkuu, Manuel Osa Nsue Nsua, amewasilisha barua ya kujiuzulu kwa niaba ya baraza zima la mawaziri lililoteuliwa mwaka 2024 baada ya serikali kufikia chini ya asilimia 10 ya malengo yaliyowekwa, akisisitiza kuwa uwajibikaji wa umma lazima uendane na matokeo.
P Diddy apunguziwa muda wa kifungo Jela, sasa kutoka Februari 23, 2028
Msanii P Diddy anatarajiwa kuachiliwa kutoka gereza la shirikisho la Marekani mapema zaidi baada ya tarehe yake ya kuachiwa kurekebishwa tena, kulingana na taarifa mpya zilizochapishwa na Federal Bureau of Prisons. Tarehe mpya sasa imewekwa kuwa Februari 23, 2028.
Musukuma: Mawaziri wa Zanzibar chungeni kauli zenu za kibaguzi bungeni
Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma, amewaonya baadhi ya wabunge na mawaziri wa Zanzibar kuepuka kauli na mijadala inayoweza kusababisha mgawanyiko na kuhatarisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ametoa kauli hiyo bungeni wakati wa mjadala kuhusu hali ya uchumi wa taifa, mpango wa maendeleo, na bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Musukuma amemuomba Rais Dkt. Hussein Mwinyi, kuchukua hatua dhidi ya mawaziri wanaodaiwa kutoa kauli zenye viashiria vya ubaguzi bungeni.
Nigeria: Mahakama yaiagiza Tume ya Uchaguzi kukifuta chama kikuu cha upinzani kuelekea uchaguzi wa 2027
Mahakama Kuu nchini Nigeria imeiamuru Tume ya Uchaguzi (INEC) kukifuta chama kikuu cha upinzani (ADC) na vyama vingine vinne kwa kushindwa kukidhi vigezo vya kikatiba katika uchaguzi wa 2023. Uamuzi huo uliotolewa na Jaji Peter Lifu Juni 15, 2026, unatarajiwa kubadilisha kabisa uwanja wa ushindani wa kisiasa. Hatua hii inaweka kiwingu kizito kwa Makamu wa zamani wa Rais, Atiku Abubakar, ambaye alitarajiwa kugombea urais kupitia ADC ili kumkabili Rais Bola Tinubu katika uchaguzi wa Januari 2027.
Kwanini FIFA imeondoa Majina (logo) halisi za Viwanja vya Kombe la Dunia 2026?
Katika Kombe la Dunia la 2026 linalofanyika Marekani, Mexico, na Canada, viwanja kadhaa vimebadilishwa majina (chapa) yao kwa muda kutokana na sera kali ya FIFA ya "Uwanja Msafi" (Clean Stadium Policy). Mabadiliko haya yanatokana na moja ya sheria za kibiashara zinazosimamiwa na FIFA katika mashindano yake ambapo chini ya sheria hii, hakuna uwanja unaoruhusiwa kuonyesha chapa yoyote ya kibiashara ambayo si mdhamini rasmi wa FIFA.
KOMBE LA DUNIA: Kipa mkongwe Vozinha ang'ara Cape Verde ikizuia Uhispania kufunga bao
Kipa mkongwe wa Cape Verde, Vozinha (40), ameokoa michomo 7, ikiwemo 6 ya ndani ya boksi, na kuwa shujaa kwa kuisaidia timu yake kutoka sare ya 0-0 dhidi ya mabingwa wa Ulaya, Uhispania, katika mchezo wa Kundi H wa Kombe la Dunia 2026. Matokeo hayo yameifanya Cape Verde kupata pointi yake ya kwanza kabisa katika historia ya kushiriki Kombe la Dunia.
Zungu: Kwanini Makampuni ya Simu hayauzi Hisa kwa Umma?, TCRA na CMSA wahojiwe!
Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu (Mb), Juni 15, 2026, ameeleza Bungeni kuwa tangu Serikali ilipofanya marekebisho ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOKA) mwaka 2016, kampuni zote za simu zilitakiwa kuuza angalau asilimia 25 ya hisa zake kwa umma kupitia soko la hisa ndani ya kipindi kilichoishia Juni 2018. Amesema hadi sasa ni kampuni ya Vodacom pekee iliyotekeleza takwa hilo la kisheria.
RC Chalamila: Wanatamani kuleta chokochoko, nguvu itakayotumia awamu hii kulinda amani, haijawahi kutokea
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewataka Wenyeviti na Watendaji wa Mitaa na Kata kuendelea kusimamia amani na utulivu katika maeneo yao, akieleza kuwa kuna baadhi ya watu wanaotamani kuibua chokochoko kupitia mitandao ya kijamii na njia nyingine. Chalamila alitoa kauli hiyo Juni 15, 2026, wakati akizungumza na viongozi hao, akisisitiza kuwa Serikali haitavumilia vitendo vyovyote vinavyoweza kuhatarisha amani na usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Japan waendeleza utamaduni wao wa kusafisha chumba cha kubadilishia nguo baada ya mechi
Mdau anasema moja ya mila na desturi bora zaidi katika ulimwengu wa soka, ni kitendo cha timu ya Japan kusafisha kabisa chumba chao cha kubadilishia nguo, huku mashabiki wao nao wakiokota takataka uwanjani baada ya mechi kumalizika—haijalishi matokeo ya mwisho yamekuwaje. Kwa mara nyingine wameacha chumba chao cha kubadilishia nguo kikiwa katika hali ya usafi wa hali ya juu baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Uholanzi, ikiwa ni mwendelezo baada ya kufanya hivyo kwenye Kombe la Dunia 2022
China imezika Shahada 12,200+ zilizopitwa na wakati kupisha AI. Tanzania bado tumelala?
Kuna ukweli mmoja mchungu sana kuhusu mfumo wetu wa elimu ya juu hapa nchini ambao kama tusipoujadili sasa, kwa uwazi na bila kupepesa macho, tutakuja kujuta kama taifa baada ya miaka mitano au kumi ijayo. Wakati sisi hapa Tanzania bado tunapambana kuongeza udahili wa wanafunzi kwenye kozi zilezile zilizoundwa tangu miaka ya 1990, wenzetu kule China wanafanya mapinduzi makubwa na ya kutisha (academic overhaul) ili kuendana na zama za Akili Unde, almaarufu Artificial Intelligence (AI). Bomu...
Baada ya kuwavuruga viungo wa Brazil, Bouaddi awaweka Arsenal, Liver na PSG vitani kusaka Saini yake
Kiungo Ayyoub Bouaddi, amezitikisa hisia za mashabiki wa soka ulimwenguni kufuatia kiwango bora cha kipekee alichokionesha kwenye mchezo wake wa kwanza wa Kombe la Dunia (World Cup debut) dhidi ya miamba ya soka, Brazil katika mchezo uliomalizika kwa sare ya 1–1 pale MetLife Stadium, New Jersey, Marekani.
Mwamuzi Omar Artan kulipwa posho yote ya Kombe la Dunia, licha ya kunyimwa Visa ya Marekani
Mwamuzi wa Womalia, Omar Artan, ambaye alinyimwa visa ya kuingia nchini Marekani kuchezesha Kombe la Dunia linaloendelea la 2026, atalipwa posho yake yote ya mashindano hayo. Vyanzo vya habari vimeiambia BBC Sport kwamba, ingawa Artan hatashiriki kabisa katika Kombe la Dunia, Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) imeahidi kumlipa stahiki zake alizokuwa anastahili kulipwa endapo angechezesha.
Pigo kwa timu ya England, Vifaa vyaibwa kabla ya Mechi Kombe la Dunia 2026
Timu ya taifa ya England imepata pigo kubwa kabla ya mechi yao ya kwanza ya Kombe la Dunia. Kiasi kikubwa cha vifaa vya timu kimeibwa Kansas City, Marekani, wakati vilipokuwa vinasafirishwa kutoka Florida kwenda kambi yao ya mazoezi.
Davido avaa koti lenye majina ya waliotekwa Nigeria akitumbuiza tamasha la FIFA
Msanii Davido amevutia hisia za wengi baada ya kuvaa koti lenye majina ya wanafunzi 39 na walimu saba waliotekwa nyara nchini Nigeria, wakati akitumbuiza kwenye tamasha la 'FIFA Countdown Concert' jijini Los Angeles, Marekani. Hatua hiyo imeonekana kama ishara kubwa ya kuwakumbuka waathirika na kupaza sauti kuhusu usalama wa watoto na walimu maeneo yenye migogoro.
Kumbukizi | RC Dkt. Kleruu alivyopigwa Risasi Siku ya Krismasi Isimani mwaka 1971
Mauaji ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Wilbert Andrew Kleruu, yanaendelea kukumbukwa kama moja ya matukio makubwa zaidi katika historia ya nchi. Kleruu, msomi na mtendaji mahiri wa serikali ya Mwalimu Nyerere, aliuawa kwa kupigwa risasi na mkulima Said Abdallah Mwamwindi siku ya Krismasi mwaka 1971 katika kijiji cha Mkungugu, Isimani, kufuatia mgogoro uliokuwa umeibuka kuhusu sera za vijiji vya ujamaa na umiliki wa mashamba.
Baada ya kukosa Kombe la Dunia, Mwamuzi wa Somalia Artan apewa Mechi ya UEFA Super Cup
Shirikisho la Soka Barani Ulaya (UEFA) limemteua mwamuzi wa kimataifa kutoka Somalia, Omar Abdulkadir Artan, kuchezesha fainali ya UEFA Super Cup kati ya Paris Saint-Germain (PSG) na Aston Villa, itakayofanyika Agosti 12 mjini Salzburg. Hatua hiyo inakuja siku chache baada ya Artan kuzuiwa kuingia nchini Marekani, hali iliyomfanya ashindwe kushiriki kama mwamuzi katika Kombe la Dunia 2026 licha ya kuwa miongoni mwa waamuzi waliokuwa wameteuliwa na FIFA.
Prof. Kitila: Tanzania haitakubali kupangiwa marafiki wala maadui
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo amesema ziara za Rais Samia Suluhu nje ya nchi zinalenga kutafuta washirika wa biashara na uwekezaji badala ya wafadhili, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa falsafa ya kuifungua nchi kiuchumi, kisiasa na kijamii. Akiwasilisha Bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2025 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2026/27, amesema Tanzania itaendelea kutafuta fursa za biashara na uwekezaji bila kuchagua upande.
Ufunguzi Kombe la Dunia 2026
Mexico itafungua Kombe la Dunia dhidi ya Afrika Kusini mjini Mexico City. Hii ni marudio ya mechi ya ufunguzi ya Kombe la Dunia 2010, ambapo timu hizi zilitoka sare ya 1–1 nchini Afrika Kusini. Jambo la kipekee ni kwamba Estadio Azteca maarufu "hekalu la soka" ni moja kati ya viwanja vya mpira wa miguu vyenye historia kubwa na ya kipekee zaidi duniani baada ya kuandaa mechi za Kombe la Dunia katika matoleo matatu tofauti: 1970, 1986 na sasa 2026.
Back
Top Bottom