Featured content

Mpenzi wangu ana-chat sana na ex wake, nikimuuliza anadai ni mazoea tu!
Mdau wa JamiiForums ameomba ushauri baada ya kuwa mpenzi wake anatumia muda sana ku-chat na mpenzi wake wa zamani (ex). Anasema hali hii inampa wasiwasi huenda mpezi wake amepata mpenzi mwingine. Anauliza amuulize au akae tu kimya atabadilika?
Mizania: Mkojo wa Ngamia ni salama kutumika kama dawa kwa binadamu
Wadau wamekuwa wakihoji ikiwa kama mkojo wa Ngamia ni Dawa au lah, baada ya video mtandaoni kusambaa zikionyesha Wananchi kutoka Tanzania wakiumwa kwaajili ya kutibu. Kwa mujibu wa WHO, mkojo wa Ngamia hauna faida ya Kitabibu kwa wagonjwa wa Saratani na unaweza kusababisha maambukizi kama Brucellosis. Matumizi yake yanahusishwa zaidi na imani za kidini.
Nyaraka za Siri za Epstein: Kisiwa cha Mnemba kama 'Uchochoro' nchini Tanzania
Februari 4, 2026 DAR ES SALAAM — Kwa muda mrefu, yamekuwepo maneno ya chini kwa chini, tetesi zilizopuuzwa kama umbea wa vijiweni. Lakini sasa, swali sio tena kama Tanzania inahusika kwenye mtandao wa uhalifu wa ngono wa Jeffrey Epstein, bali ni mizizi hiyo imechimba kirefu kiasi gani. Kufuatia hatua ya Wizara ya Sheria ya Marekani (DOJ) kumwaga hadharani kurasa milioni tatu za nyaraka nzito wiki hii, "Kivuli cha Epstein" kimetua rasmi katika ardhi ya Tanzania. Tofauti na nyaraka za awali...
Matokeo ya Kidato cha Nne 2025 yatangazwa. Ufaulu wapanda
Ufaulu Umepanda. Futatilia hapa. https://www.youtube.com/live/uwbLeIIRXOc?si=m-Iyj06qeAYHlPCl Kupata Matokeo fungua link hii: https://matokeo.necta.go.tz/results/2025/csee/index.htm --- Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika kuanzia Novemba 17, 2025. Matokeo hayo yametangazwa leo Jumamosi Januari 31, 2026 na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Profesa Said Mohammed. Jumla ya wanafunzi 569,883 walifanya...
Tanzania kuuza sehemu ya Hazina yake ya Dhahabu kusaidia kufadhili miradi ya miundombinu
Tanzania inapanga kuuza sehemu ya hazina yake ya dhahabu kusaidia kufadhili miradi ya miundombinu, kufuatia kupungua kwa msaada wa wafadhili ambao kumelazimisha serikali kutafuta vyanzo vya ndani vya fedha. Rais Samia Suluhu Hassan amekubali uamuzi huu, akizingatia usimamizi wa rasilimali za ndani ili kukabiliana na mahitaji ya kifedha. Benki Kuu ya Tanzania imeripoti kuwa kuna hazina kubwa ya dhahabu, ikionyesha uwepo wa rasilimali muhimu kwa juhudi kama hizi. Marekebisho ya kiuchumi...
Wapiganaji 5 wa ISIS raia wa Tanzania wakamatwa Somalia
Serikali ya Jimbo la Puntland imetoa picha na maelezo rasmi yanayowaonyesha makumi ya wapiganaji wa kigeni wa kundi la Islamic State (ISIS-Somalia) waliokamatwa wakati wa operesheni ya kupambana na ugaidi inayoendelea katika safu ya milima ya Calmiskaad (Al-Miskad) kwenye Milima ya Golis. Kwa mujibu wa Idara ya Kupambana na Ugaidi (CT) ya Puntland, mahabusu hao walikamatwa wakati wa "operesheni endelevu za kijeshi zinazolenga maficho ya ISIS katika Milima migumu ya Al-Miskaat, ambayo...
Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei afariki Dunia
Wakuu, Heche kupitia mtandaoni ametangaza kifo cha mwasisi wa chama chao CHADEMA, Mzee Edwin Mtei baada ya familia kuthibitisha huku mipango ya mazishi ikiendelea nyumbani kwake Tengeru, Arusha. ===== Baadhi ya mambo muhimu kuhusu Ediwin Mtei ambayo pengine ulikuwa hufahamu Elimu,"Shahada ya Sanaa (Political Science, History, Geography) - Makerere (1957)" BoT, Gavana wa kwanza (1966–1974) Uwaziri, Waziri wa Fedha (1977–1979) Siasa, Muasisi na Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA (1992)...
Serikali kutumia zaidi ya Sh. Bilioni 2.7 kukodi Kampuni ya Marekani ili ‘Kurekebisha Taswira ya Nchi’
Januari 16, 2026 WASHINGTON, D.C. — Ikikabiliwa na uangalizi wa kimataifa kufuatia matukio yaliyotokea wakati wa uchaguzi mkuu wa 2025 ulioharibu sifa yake, Serikali ya Rais Samia imezindua operesheni kabambe ya kujenga ushawishi nchini Marekani. Tanzania imekodi kampuni inayoongozwa na Mbunge wa zamani wa Republican ili kurekebisha sifa yake na kujiweka kama mshirika muhimu katika mbio za kimataifa za madini adimu (rare earth minerals). Kulingana na majalada ya Sheria ya Usajili wa...
Samia: Nimeliponya Taifa kwa kuanzisha Wizara ya Vijana na ...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, amesema ili kuliponya Taifa amechukua hatua kadhaa ikiwemo kuanzisha Wizara ya Vijana iliyopo chini ya Ofisi ya Rais, kuwaachia huru watuhumiwa wa kesi ya Uhaini na kuanzisha Tume Huru ya Uchunguzi wa vurugu za Oktoba 29.
Uganda yazima Intaneti ili kupisha Uchaguzi Mkuu Januari 2026
Serikali ya Uganda, kupitia Tume ya Mawasiliano ya Uganda (UCC), imetangaza kusimamisha kwa muda huduma za intaneti kwa umma na usajili wa laini mpya za simu nchini humo, ili kuzuia usambazawaji wa taarifa potofu, vitendo vinayoweza kuchochea vurugu au kuhatarisha usalama wa taifa. Kwa mujibu wa agizo hilo, waendeshaji wote wa mitandao ya simu na watoa huduma za intaneti wametakiwa kusitisha huduma hizo kuanzia Januari 13, 2026 saa 12 jioni hadi itakapotolewa taarifa nyingine ya kurejesha...
Rais Samia: Huko Mahabusu kuna watu hawana hatia
Rais Samia Suluhu Hassan, amesema hayo leo Januari 13, 2026 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) katika viwanja vya Makao Makuu ya Mahakama (Judiciary Square), mkoani Dodoma. "Huko mahabusu huko kuna mtu anafungwa kwa kesi ya kubambikiwa tu sasa 'engineering' gani imetumika Mahakamani mpaka mtu akaenda jela kwa kesi ya kubambikiwa, akitoka anasema mimi sikuwa na kesi nilibambikiwa tu lakini nimekaa nimetoka, sasa wewe uliyepeleka ukamnyima...
Je, ulifika miaka 30 bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?
Habari ya weekend great thinkers? Maisha yananipa experience tofauti, Sikuwahi kufikiria kama ningefika third floor bila kuwa na familia wala watoto, kuna muda nahisi kupanic nahofia watoto wasije kuniita bibi badala ya mama, au kukosa kabisa sababu ya umri mkubwa🤔 Enzi hizo nilikua nashangaa mtu hasa mdada unafikaje hadi 30s huna familia, aisee kumbe ni kweli now ni mimi mwenyewe. Mlioanza familia mkiwa 30s je ni kweli au mnaona dalili za watoto wenu kuwaita bibi au babu? Vipi changamoto...
UFAFANUZI: Ugumu zoezi la urejeshaji wa nauli za SGR
Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaendelea na zoezi la urejeshaji wa nauli kwa abiria aliyeshindwa kusafiri Desemba 31, 2025 jioni na Januari 1- 2, 2025 kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu. Hata hivyo zoezi hili limekumbwa na ugumu kufuatia baadhi ya abiria kukatiwa tiketi na watu wengine hivyo mawasiliano yao (simu ama email) kutokuwamo katika mfumo wetu wa tiketi hivyo kusababisha kikwazo cha mawasiliano baina ya pande zote hususani abiria aliyelipa na kusafiri. Ndugu abiria...
FT: Morocco 1-0 Tanzania | AFCON 2025 | 16 Round
Mchezo wa Tanzania dhidi ya Morocco katika hatua ya 16 Bora ya AFCON 2025 unapigwa leo Januari 4, 2026, katika Uwanja wa Prince Moulay Abdellah, Rabat, Morocco. Huu ni mchezo wa kihistoria kwa Taifa Stars ambao kwa mara ya kwanza wamefanikiwa kufika hatua ya mtoano katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika. Morocco, wakiwa wenyeji wa mashindano, wanaingia wakiwa na rekodi bora baada ya kuongoza kundi lao bila kupoteza, hali inayowafanya kupewa nafasi kubwa ya kusonga mbele mbele ya...
Ukiukwaji wa Haki za Binadamu nchini Venezuela chini ya Nicolás Maduro
Tangu Nicolás Maduro achukue hatamu za uongozi mwaka 2013, Venezuela imepitia misukosuko mikubwa ya kisiasa na kijamii ambayo imesababisha shutuma nzito za ukiukwaji wa haki za binadamu. Mashirika ya kimataifa yamekuwa yakiandika ripoti mbalimbali zinazoonyesha mbinu za kimfumo zinazotumiwa na Serikali kudhibiti upinzani na kukandamiza uhuru wa raia. Baadhi ni kama ifuatavyo: 1. Uminywaji wa Uhuru wa Vyombo vya Habari Uhuru wa kujieleza na Vyombo vya Habari umepungua kwa kiasi kikubwa...
Mwaka 2025 umeisha, Utamkumbuka Samia kwa lipi?
Kipekee nitamkumbuka kuwa ndiye Rais wa kwanza Tanzania kujiapisha kwenye Barracks za kijeshi. Ni Rais wa kwanza Tanzania kuwekwa kwenye group linalowania tuzo ya Kiongozi Jeuri wa Mwaka, Tyrant of the Year. Ni Rais wa kwanza kumaliza siku 100 zake za kwanza akiwa amejificha. Ndiye Rais ambaye hakuwashukuru waliomchagua baada ya uchaguzi. Kalishukuru Jeshi la Wananchi, Jeshi la Polisi na Tume ya Uchaguzi kawaacha wananchi waliomchagua. Ni Rais wa kwanza Tanzania kukataliwa na...
Mahakama: BAKWATA si Chombo cha Waislam wote
Leo waislam wameshinda kesi waliofungua dhidi ya BAKWATA kujipa mamlaka ya kuwaongelea waislam na kukwamisha miradi Kwa ukiritimba ati wao ndo watoe vibali Kwa taasisi zingine za kiislam Shehe Ponda amesema mahakama katika hukumu hiyo, mahakama imeitamka kuwa BAKWATA sio taasisi inayosimamia Waislam wote Bali wale waliohiari kuwa chini ya taasisi ya BAKWATA Pia Shehe Ponda ameahidi kuandaa kongamano kutoa elimu juu ya umuhimu wa hukumu ya Leo Kwa waislam Assalam Alyekum ======= WAISLAMU...
Mwigulu: Mnasema maisha magumu? Magari namba E yamejaa Barabarani
Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba amewashangaa na kuwazodoa wanaodai Kuna maisha magumu wakati Kuna Utitiri wa magari Namba E Yamejaa Barabarani,Harusi na Bar Zinajaza na Benki Kuna Foleni ya kutoa na kuweka pesa. Mwigulu anasema Suala la ugumu wa Maisha ni hakuna siku litaisha Duniani ndio maana hata Mataji wakubwa wanajiua. --- ".... Kila kipato kinapoongezeka na matamanio nayo yanaongezeka, hiki ndicho kinachosababisha ugumu wa maisha. Nilipita hapa mjini juzi, kila baada ya gari mbili...
Samia: JWTZ ijiepushe na mashinikizo ya kisiasa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan amelitaka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuepuka mashikizo ya kisisa akieleza kuwa kuwa mshikamano kati ya uongozi wa kisiasa na uongozi wa kijeshi ni nguzo muhimu ya usalama wa Taifa, hata hivyo amesisitiza kuwa JWTZ ni jeshi la wananchi na linapaswa kubaki huru na siasa za vyama, likiwa na utii kwa Serikali halali iliyopo madarakani. Rais Samia ameyasema hayo akizungumza na Wakuu wa Kamandi, Wakuu...
Tamko kuhusu JamiiForums kuendelea kuzuiliwa kupatikana Tanzania
TAARIFA KWA UMMA Mnamo Septemba 6, 2025, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilisitisha Leseni ya Maudhui Mtandaoni ya JamiiForums na kuzuia upatikanaji wa jukwaa kwa siku 90, kwa madai ya ukiukwaji wa Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta. Pamoja na kutambua athari kwa haki ya wananchi kupata taarifa na kutoa maoni, tulitii agizo hilo hadi huduma ziliporejeshwa Desemba 06, 2025. Tangu kurejeshwa, tumepokea taarifa kutoka kwa watumiaji wetu wa Tanzania kuwa kuanzia Desemba 7...
Back
Top Bottom