Featured content

DCP Misime: Wanaotaka mikutano watoe taarifa Polisi, hali ya usalama ni shwari
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, DCP David Misime, amesema hali ya usalama nchini kwa sasa ni shwari, hivyo Jeshi litaendelea kupokea taarifa za nia ya kufanya mikutano ya hadhara na vikao kutoka kwa vyama vya siasa na wadau wengine kwa mujibu wa sheria. Soma: Waziri Katambi apiga marufuku mikutano ya siasa kwa vyama vyote Misime amesema katika kipindi ambacho kulikuwa na viashiria vya baadhi ya watu kupanga vitendo vya kihalifu, Jeshi la Polisi lilizishauri taasisi na vyama...
Katambi: Hatuna ugaidi Tanzania, Vinaweza kuwepo viashiria
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amesema Tanzania haina ugaidi, huku akisisitiza kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria wala anayepaswa kupewa kinga kutokana na cheo, taaluma, dini au hadhi yake katika jamii. Amesema vyombo vya dola vinaendelea kuchukua hatua dhidi ya yeyote anayehusika na vitendo vinavyokiuka sheria bila ubaguzi.
Polisi India asimamishwa kazi kwa kutumia bunduki ya kivita kuwatawanya waandamanaji
Mamlaka nchini India zimemsimamisha kazi afisa mmoja wa polisi baada ya kutumia bunduki ya kivita aina ya AK-47 kufyatua risasi hewani ili kuwatawanya wanafunzi waliokuwa wakiandamana katika jimbo la Bihar. Tukio hilo lililotokea mwishoni mwa wiki katika mji wa Siwan lilinaswa kwenye video zilizosambaa mitandaoni, zikimuonyesha polisi huyo akiwa amevalia vifaa vya kukabiliana na ghasia akielekeza bunduki hiyo kwa waandamanaji kabla ya kufyatua angalau risasi tatu hewani. Julai 6, 2026...
Zinedine Zidane apewa kibarua cha kuinoa Ufaransa hadi mwaka 2030
Shirikisho la Soka la Ufaransa (FFF) limemtangaza rasmi Zinedine Zidane kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Ufaransa, akichukua nafasi ya Didier Deschamps kwa mkataba utakaodumu hadi mwaka 2030. Zidane, ambaye aliwahi kuiongoza Real Madrid kutwaa mataji makubwa barani Ulaya, ataiongoza Ufaransa katika mashindano ya Euro 2028 pamoja na Kombe la Dunia la 2030.
Nondo: Lissu ni Mwenyekiti wa chama kikubwa cha upinzani, aachiwe, kesi yake ni ya Kisiasa
Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Julai 26, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa ya chama cha ACT-Wazalendo, Abdul Omary Nondo amewasilisha mapendekezo makuu matano yanayopaswa kutekelezwa na Serikali: Kuachia Huru Tundu Lissu: Alisisitiza kuwa kuachiwa kwa Lissu bila masharti ni hatua ya kwanza na ya lazima kabla ya mazungumzo ya maridhiano. Kufuta Kesi za Ugaidi: Alitoa wito wa kufutwa kwa kesi za ugaidi zinazowakabili wananchi, vijana, na viongozi wa...
KOREA KUSINI | Rais wa zamani akutwa na hatia ya kudanganya wakati wa Kampeni za Uchaguzi 2022
Aliyekuwa Rais wa Korea Kusini, Yoon Suk Yeol, amepatikana na hatia ya kudanganya wakati wa kampeni zake za urais. Hukumu hii mpya imekuja baada ya kuondolewa madarakani mwaka 2025 kutokana na hatua yake ya muda mfupi ya kutangaza sheria ya kijeshi. Yoon amekana mashtaka hayo, na mawakili wake wanapanga kukata rufaa wakidai kuwa hukumu hiyo imetokana na tafsiri mbaya ya ukweli wa mambo pamoja na sheria ya uchaguzi. Endapo Yoon atashindwa katika rufaa hiyo, inaweza kukisababishia pigo kubwa...
Dkt. Shija: Sakata la Kaijage limeshusha Morali, linaweza kusababisha Mgomo wa Wafanyakazi UDOM
Sakata la kisheria linalomkabili Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedeki Kaijage, limechukua sura mpya baada ya upande wa mashtaka kubadilisha mashtaka yake na kumfungulia rasmi kesi ya ugaidi. Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Taaluma UDOM (UDOMASA), Dkt. Gerald Enos Shija, ameeleza kuwa hatua hiyo imeshusha sana morali ya wafanyakazi na kuwatia hofu.
Dkt. Nchimbi: Watanzania pambaneni mpate Katiba Mpya yenye muafaka katika Taifa
Makamu wa Rais, Dkt. Emmanuel Nchimbi, akizungumza leo Julai 23, 2026 katika Mkutano wa Wanachama wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) unaofanyika Jijini Dar es Salaam, amesisitiza Watanzania kupambana kupata Katiba Mpya na kwamba taifa linahitaji Katiba yenye muafaka na makubaliano ya wadau wote itakayolinda haki za raia na kulipeleka taifa mbele kwa miaka ijayo.
Mhadhiri wa UDOM aliyetuhumiwa kuhamasisha maandamano akabiliwa na shitaka la ugaidi
Dk Melikisedeki Kaijage, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) aliyekuwa akishikiliwa na Jeshi la polisi mkoani Dodoma kwa madai ya kuhamasisha maandamano ya Julai 7, 2026, sasa amebadilishiwa shitaka na kuwa la ugaidi na hivyo kunyimwa dhamana. Awali, Jumanne Julai 21, Dk Kaijage alipewa dhamana na Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, baada ya kushikiliwa katika kituo cha Polisi Chang’ombe jijini humo tangu Julai 8, 2026, lakini kabla hajaachiliwa, akapewa shitaka hilo. Soma pia: Mhadhiri...
Kwa kigezo hiki, Mbappe kushinda Ballon d'Or mwaka 2026?
Waandaaji wa tuzo ya Ballon d'Or wameeleza kuwa kushinda Kombe la Dunia pekee hakutoshi kumhakikishia mchezaji kutwaa tuzo hiyo ya kifahari. Kupitia taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti rasmi ya tuzo hiyo, wamebainisha kuwa mafanikio katika Kombe la Dunia ni miongoni mwa vigezo muhimu, lakini si kigezo cha moja kwa moja cha kushinda Ballon d'Or.
Msigwa: Serikali inafanya tathmini ya Tamko la Jumuiya ya Madola, tutawapa majibu
Serikali ya Tanzania imethibitisha kupokea tamko kutoka kwa Jumuiya ya Madola linaloitaka kumwachia huru Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, ndani ya siku 30. Akijibu swali la mwandishi wa habari, Msemaji wa Serikali alieleza kuwa serikali imeliona tamko hilo na kwa sasa inafanya tathmini ya kina ya maeneo yote yaliyobainishwa kwenye barua hiyo ili kuona namna ya kulitolea maamuzi na majibu rasmi.
Heche: Hakuna mazungumzo yatakayofanyika bila Mwenyekiti kuwa nje
Kaimu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche, amesema hakutakuwa na mazungumzo na Serikali hadi Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, awe huru na vikao halali vya chama vitoe uamuzi kuhusu hatua zinazofuata. Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 22, 2026, Heche pia amesisitiza kuwa CHADEMA haitashiriki mazungumzo bila kuwepo kwa mpatanishi huru wa kusimamia mchakato huo.
Kaizer Chiefs yamtangaza Adolf Mtasingwa kutokea klabu ya Azam
Klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini imethibitisha kumsajili kiungo mkabaji wa timu ya taifa ya Tanzania, Adolf Bitegeko, kutoka Azam FC kwa ada ambayo haijawekwa wazi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kikosi kwa msimu ujao. Bitegeko, (27) na aliyekuwa nahodha wa Azam FC, anakuwa mchezaji wa kwanza kutoka Tanzania kuichezea Kaizer Chiefs. Kabla ya kujiunga na Azam Januari 2024, aliwahi kuzichezea klabu mbalimbali nchini Iceland.
Wakili Malangalila: Mahakama Kuu imeamuru Mhadhiri wa UDOM aachiwe kwa dhamana
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, imeamuru Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedeki Kaijage, aachiwe kwa dhamana kuanzia Julai 21, 2026, wakati upelelezi wa tuhuma za uchochezi zinazomkabili ukiendelea. Uamuzi huo umetolewa na Jaji Joachim Tiganga wakati wa usikilizwaji wa Shauri Na. 15653/2026. Kaijage amekuwa akishikiliwa katika Kituo cha Polisi Chang'ombe kwa tuhuma za kuhamasisha maandamano yaliyojulikana kama "Sabasaba". Upande wa Serikali ulieleza mahakamani...
Wasira: Kila siku Lissu anaweka mapingamizi, ndio maana kesi inachukua muda mrefu
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Stephen Wasira amesema; "Mahakama inaendelea vizuri. Tena yeye Tundu Lissu, rafiki yangu, anaitumia mahakama kama shule ya sheria; yeye anajitetea mwenyewe. Kila siku anaweka mapingamizi, majaji wanaahirisha kwenda kutazama hicho alichokisema—ndio maana inachukua muda mrefu. Lakini kesi hii itaisha." "Sio lazima CHADEMA wakisema tunakubali, tutakubali mambo ya CHADEMA ambayo yana make sense...kwa sababu huwezi kutulazimisha kuachia mtu ambae kesi yake...
Mechi 5 za mwanzo kwa Yanga, Simba na Azam FC Msimu wa 2026/27
Baada ya mchezo wa Ngao ya Jamii Agosti 12, 2026 wa Dabi ya Kariakoo kati ya Yanga SC na Simba SC, timu hizo mbili zitaendelea na maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC 2026/2027. Yanga SC itasafiri kuelekea Ruangwa, Lindi, ambapo Agosti 15, 2026 itacheza dhidi ya Namungo FC katika mchezo wake wa mwanzo wa ligi. Kwa upande wa Simba SC, baada ya mchezo huo wa Ngao ya Jamii, kikosi hicho kitaelekea Bukoba mkoani Kagera kwa ajili ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar FC utakaopigwa Agosti 16...
Fahamu mambo mbalimbali kuhusu gari aina ya Subaru Forester
BAADHI YA MASWALI YALIYOULIZWA NA WADAU KUHUSU GARI HII Wakuu rafiki yangu mmoja yupo interested na hizi gari aina ya Subaru Forester lakini kabla hajaingiza maamuzi mzima mzima alitaka kujua yote ya husuyo hizi aina za haya magari. Stability zake, upatikanaji wa spare na mengine yote ambayo mtu yeyote angependa kuyajua.Huyu jamaa yupo mkoani na amejaribu kuangalia aina hizo hazipo na yeye yupo interested nayo kwa kuwa ni 4DW kulingana na maeneo anayoishi anahitaji mkoko wa namna hiyo. Kwa...
Meli ya mafuta yenye bendera ya Tanzania yatekwa nyara na maharamia wa Somalia
Meli ya mafuta yenye bendera ya Tanzania, MT ASANA, imetekwa na maharamia wanaoshukiwa kutoka Somalia katika pwani ya Yemen, kwa mujibu wa vyanzo vya usalama na maafisa wa eneo hilo. Tukio hilo lilitokea baada ya meli hiyo kuondoka Mukalla, Yemen siku ya Ijumaa. Baada ya kutekwa, meli hiyo ilipelekwa katika pwani ya Caluula, eneo la Bari kaskazini mashariki mwa Somalia, ambako inaendelea kushikiliwa na watekaji, kwa mujibu wa maafisa wa eneo la Puntland.
Bobi Wine appoints Nambeshe acting NUP President
National Unity Platform (NUP) President Robert Kyagulanyi Ssentamu, popularly known as Bobi Wine, has appointed Hon. John Baptist Nambeshe as the party’s Acting President, replacing Dr. Lina Zedriga Waru, whose four-month tenure has ended.
Mapfumo defends US$1 million Chivayo deal, says his principles remain intact
Chimurenga music legend Thomas “Mukanya” Mapfumo has defended his decision to accept a US$1 million performance offer from businessman Wicknell Chivayo, saying the deal does not mean he has abandoned his values, activism or support for ordinary Zimbabweans. The 81-year-old music icon has faced criticism from some fans and social commentators who accused him of compromising his long-standing reputation as a voice for social justice and human rights.
Back
Top Bottom