Featured content

Rais Samia kwa Rais wa Ghana: Kila kitu kipo salama Tanzania baada ya uchaguzi
Rais Samia amesema Tanzania iko katika hali ya utulivu kisiasa na mambo yote yako chini ya udhibiti baada ya uchaguzi wa Oktoba 2025 huku shughuli za kijamii na kiuchumi zikiendelea kama kawaida. Ameeleza kuwa baada ya matukio ya kisiasa yaliyojitokeza, serikali iliunda Tume ya Uchunguzi ambayo ripoti yake itasaidia kuanzisha Tume ya Maridhiano na baadaye kufanya mapitio ya Katiba Alitoa kauli hiyo Machi 2, 2026 mjini Arusha Rais Samia na kuongeza kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano
Iran yathibitisha kuwa Kiongozi Mkuu, Ayatollah ameuawa
Kiongozi Mkuu wa Iran ameuwawa katika mashambulizi ya Israel na Marekani, vyombo vya habari vya serikali ya Iran vimesema. Serikali ya Iran imetangaza siku 40 za msiba wa taifa baada ya kifo cha Kiongozi Mkuu Khamenei kilichotokea siku ya Jana katika mashambulizi ya Marekani na Israel. Source: Reuters Pia soma LIVE - Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Israel + Marekani vs Iran Ubalozi wa Iran nchini ulivyopost kuhusu hilo.
Ruvuma: Lazaro Komba wa CCM ashinda Ubunge jimbo la Peramiho
Msimamizi wa Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Peramiho Exavery Luyagaza amemtangaza Dkt. Lazaro Kiliani Komba wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa mshindi wa kiti cha Ubunge wa jimbo la Peramiho kwa kupata kura 69002 sawa na ushindi wa asilimia 87 wa kura halali zote zilizopigwa. CCM imevishinda vyama vya siasa 14 katika uchaguzi mdogo wa ubunge uliofanyika Februari 26, kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge Jenister Mhagama, aliyefariki dunia Desemba 11, 2025, jijini Dodoma.
UEFA Champions: Madrid kukutana na Man City. PSG wapangwa na Chelsea hatua ya 16 Bora
Timu vigogo barani Ulaya; Arsenal, Real Madrid na Liverpool ni miongoni mwa klabu zilizojua hatima yao baada ya droo ya hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kupangwa Ijumaa. Real Madrid watakutana tena na Manchester City katika hatua ya mtoano kwa msimu wa tano mfululizo, baada ya kupangwa kukabiliana katika hatua ya 16 bora. Wakati huohuo, mabingwa watetezi Paris Saint-Germain (PSG) watacheza na Chelsea na Arsenal kukutana na Bayer Leverkusen.
Zimbabwe yakataa Msaada wa Marekani wa Dola Milioni 367
Serikali ya Zimbabwe imekataa ufadhili wa Dola Milioni 367 (Tsh. Bilioni 937) kutoka Marekani uliolenga Sekta ya Afya, ikieleza wasiwasi kuhusu athari zake kwa uhuru wa nchi na udhibiti wa Kitaifa. Balozi wa Marekani nchini Zimbabwe, Pamela Tremont amethibitisha kuwa mazungumzo yamevunjika, akisema mamlaka za Zimbabwe zimeihakikishia Washington kuwa ziko tayari kuendelea kupambana na magonjwa kama VVU, Kifua Kikuu (TB) na Malaria bila msaada huo.
Gerson Msigwa: Meli iliyokamatwa na Cocaine El Salvador imesajiliwa Zanzibar
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, akizungumza Februari 26, 2026 na Waandishi wa Habari, amesema meli iliyokamatwa nchini El Salvador ikiwa na tani 6.6 za Cocaine ikiwa na bendera ya Tanzania ilisajiliwa Zanzibar, na kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tayari imechukua hatua ya kuifutia usajili meli hiyo. Ameongeza meli nyingi zinazosajiliwa katika nchi fulani si lazima zitoke au zifanye kazi katika nchi hiyo.
Vatican: Pope Leo XIV kufanya ziara ya kwanza barani Afrika
Papa Leo XIV anatarajiwa kufanya ziara ya siku 10 barani Afrika kuanzia Aprili 13, 2026 safari ambayo itakuwa ya kwanza kwake tangu achaguliwe kuongoza Kanisa Katoliki, na atatembelea Algeria, Cameroon, Angola na Equatorial Guinea. Pia itakuwa mara ya kwanza kwa Papa kutembelea Algeria, taifa lenye Waislamu wengi. Disemba 2025, Papa Leo alitangaza nia yake ya kufanya ziara nchini Algeria, kuzuru maeneo ambayo Mtakatifu Augustine aliishi
Wizara ya Afya: Kuna ongezeko la Mafua makali ya influenza na UVIKO 19 nchini
Wizara ya Afya Tanzania imetoa tahadhari kufuatia ongezeko la wagonjwa wa mafua makali ya Influenza na UVIKO-19 nchini, na kuwataka wananchi kuchukua hatua za kujikinga na maambukizi yanayoweza kusambaa kwa kugusa maeneo au vitu vilivyochafuliwa na majimaji kutoka kwa mgonjwa. Kwa mujibu wa wizara hiyo, takwimu za ufuatiliaji zinaonesha kuwa kila mwaka kuanzia Novemba hadi Aprili kumekuwa na ongezeko la maambukizi hayo nchini na duniani.
El Salvador: Meli yenye bendera ya Tanzania yakamatwa ikiwa na Tani 6.6 za Cocaine
Rais Nayib Bukele ametangaza kuwa Jeshi la Wanamaji limetekeleza operesheni kubwa zaidi ya kukamata kwa Dawa za Kulevya katika historia ya nchi hiyo, ni baada ya kukamata Tani 6.6 za Cocaine zilizokuwa zikisafirishwa baharini na Meli iliyokuwa ikipeperusha bendera ya Tanzania. Kufuatia operesheni hiyo, jumla ya Wanaume 10 walitiwa mbaroni. Watuhumiwa hao wanatoka katika nchi za Colombia, Nicaragua, Panama, na Ecuador, wakiashiria mtandao mpana wa kimataifa uliohusika katika usafirishaji
CHADEMA: Umoja wa Mataifa umezitaka Mamlaka kumuachia huru Lissu na kumlipa fidia
CHADEMA imetoa taarifa kuwa Kikundi Kazi cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kuhusu Uhifadhi Holela (UNWGAD) kupitia Kitengo Kazi, imezitaka mamlaka za Tanzania kumuachia huru Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, pamoja na kumlipa fidia ikidai kuna ukiukwaji mkubwa wa Haki za Binadamu kwa mujibu wa Sheria za Kimataifa tangu kukamatwa kwake Aprili 9, 2025.
Lissu: Wanataka tuzungumze mambo ya Oktoba 29, mtakuwa mmefungulia balaa
Mahakama Kuu imesikiliza hoja za upande wa Jamhuri na Tundu Lissu kuhusu notisi ya ushahidi wa ziada wa shahidi, ACP Amin Mahamba katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti huyo wa CHADEMA, aliyesisitiza kwamba jambo hilo halina msingi kisheria. Lissu ameonya kuwa, kuruhusu notisi hiyo kutafungua “Sanduku la Pandora” la matatizo yasiyoweza kudhibitiwa, hususan kuhusiana na matukio ya Oktoba 29, 2026. Upande wa Jamhuri ikiwa wanataka kurekebisha taarifa, wafuate kifungu cha 294 cha CPA.
JAB yampa onyo kali Zungu kwa kukiuka maadili maudhui ya Uchelewaji wa Ndege ya ATCL
Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imesema mwandishi Kelvin Justine Raphael (Zungu) alikiuka maadili ya uandishi wa habari kupitia maudhui aliyochapisha kuhusu ucheleweshaji wa ndege ya ATCL. Zungu alichapisha maudhui Februari 21, 2026 akilalamikia kucheleweshwa kwa safari ya ndege ya ATCL kwa abiria waliokuwa Mwanza bila taarifa, akidai alipoteza fursa ya kusaini mkataba.
Kenya: Wanaodaiwa kuwa Watanzania wakamatwa wakijaribu kumteka mwanaharakati Mshabaha Hamza
Wanaodaiwa kuwa Watanzania wakamatwa nchini Kenya wakijaribu kumteka mwanaharakati Mshabaha Mshabaha Hamza, katika tukio linalodaiwa kuwa jaribio la kumrudisha kwa nguvu nchini Tanzania. Tukio hilo lilitokea Februari 22, ambapo polisi kutoka vituo vya Lukenya na Kyumbi pamoja na maafisa wa DCI walimuokoa mwanaharakati huyo na kuwakamata washukiwa watatu waliokuwa ndani ya gari lililohusishwa na tukio hilo.
Polisi yakanusha Kikundi cha ‘TFF’ kufanya uhalifu, yaonya 'Wachochezi' wa Mtandaoni
Jeshi la Polisi limekanusha taarifa zinazosambazwa na kikundi kinachojiita Tanzania Freedom Fighters (TFF) kikidai kufanya mazoezi porini na kutenda uhalifu. Polisi imebainisha kuwa madai hayo si ya kweli na yanatolewa na watu waliopo nje ya mipaka ya nchi kwa lengo la kusababisha taharuki na kuchochea chuki miongoni mwa Watanzania. Jeshi hilo limesisitiza kuwa linaendelea kuwafuatilia na kuwatia mbaroni watu wanaotumia mitandao ya kijamii kuhamasisha vurugu na uhalifu na uhalifu wa kijinai.
Muda wa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Oktoba 29 Waongezwa Hadi Aprili 2026
Mamlaka ya Uteuzi imeongeza muda wa siku 42 kwa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani ya Uchaguzi wa 2025, ikisogeza ukomo wa kazi hiyo hadi Aprili 3, 2026. Ongezeko hilo limetokana na uhitaji wa kufanya uchambuzi wa kina wa kisayansi wa taarifa zilizokusanywa na kuziba mapengo ya kishahidi ili kuhakikisha ripoti inakamilika kwa usahihi. Awali, Tume hiyo inayoongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Chande, ilitarajiwa kukamilisha majukumu yake ndani ya siku 90, yaani Februari 2026.
TABORA: Mahakama Kuu yaupiga chini utaratibu wa “uwakili wa viti maalum”
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tabora, Februari 17, 2026 kupitia kesi ya Amina Mwaluko dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imebatilisha utaratibu wa baadhi ya Watu wakiwemo Maafisa wa Mahakama, na Maafisa Sheria wa Sekta za Umma kupewa Uwakili bila kuhitimu Astashahada katika Shule ya Sheria kwa Vitendo (Law School of Tanzania) wanaofahamika kwa jina la Mawakili wa Viti Maalum Katika Uamuzi huo Mahakama Kuu imeeleza kwamba Sheria iliyoruhusu utaratibu huo ni batili, zipo kinyume na Katiba
Bwege kuhamia CHADEMA, asema ACT Wazalendo si rafiki sahihi kwake
Mbunge wa zamani wa Kilwa Kusini, Selemani Bungara maarufu kama “Bwege”, ametangaza kujivua uanachama wa chama cha ACT Wazalendo kuanzia Februari 18, 2026. Kupitia taarifa yake, amesema uamuzi huo umeanza rasmi tangu tarehe hiyo. Bungara amesema ACT Wazalendo si rafiki sahihi kwake kama alivyodhani awali, akieleza kuwa matarajio yake yalikuwa tofauti na alivyokuta.
Afrika Kusini: Mtoto wa Robert Mugabe akamatwa kwa tuhuma za kumfyatulia mlinzi risasi
Jeshi la Polisi nchini Afrika Kusini limemkamata Bellarmine Mugabe, mtoto wa kiume wa aliyekuwa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe Jijini Johannesburg kufuatia tukio la kumpiga risasi mlinzi katika makazi yake yaliyopo Hyde Park. Mamlaka nchini humo zimeeleza kuwa uchunguzi wa kina unaendelea kufanyika, ikidaiwa majeruhi yupo katika hali mbaya, huku tukio hilo likiwa linachunguzwa kama kesi ya jaribio la mauaji.
Kesi ya Lissu: Shahidi wa Siri (P7) ajibu maelezo yake “hayapo” polisi alipoulizwa na Lissu mahakamani
Katika kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, Shahidi wa 11 wa Kificho wa Jamhuri (P7) alikiri mbele ya mahakama kuwa maelezo aliyoulizwa mahakamani hapo na Lissu “hayapo” kwenye maelezo yake ya Polisi. Shahidi alijibu mara kwa mara “hayapo” au “sijataja” baada ya Lissu kumhoji kuhusu matukio ya kuhusu CHADEMA kuzuia uchaguzi, kuhusu Tume ya Uchaguzi na uchaguzi wa mwaka 2024 na tuhuma za wizi wa kura.
TANZIA: Kardinali Pengo afariki Dunia
Pumzika kwa amani mwadhama Kardinali Pengo. Tuonane mbinguni asubuhi iliyo njema. ===== YAH: TANGAZO LA KIFO Ninayo masikitiko makubwa kuwatangazieni kwamba leo tarehe 19/02/2026 saa 04:00 usiku huu mpendwa baba yetu Mwadhama Polycarp Cardinal Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele akiwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam. Taarifa za mazishi zitawajia mara baada ya mipango kukamilika. Tumwombee...
Back
Top Bottom