Featured content

Marekani na Iran zakubaliana kusitisha mapigano kwa wiki mbili
Rais wa Marekani Donald Trump amesema amekubali kusitisha mashambulizi dhidi ya Iran kwa muda wa wiki mbili, kufuatia pendekezo la wapatanishi katika mgogoro huo. Trump amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya mazungumzo na viongozi wa Pakistan, akiwemo Waziri Mkuu Shehbaz Sharif, ambao waliomba muda zaidi kwa juhudi za kidiplomasia.
Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Oktoba 29 yaongezewa Muda tena hadi Aprili 24
Mamlaka ya Uteuzi imeridhia maombi ya muda wa ziada kwa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 hivyo imeiongezea tena muda wa siku ishirini na moja (21) na kuitaka ikamilishe kazi kabla au ifikapo Aprili 24, 2026. Mamlaka hiyo imeeleza sababu za kuongeza muda huo kwa Tume ni pamoja na kuiwezesha Tume kukamilisha uchambuzi wa ushahidi, taarifa na maoni yaliyopokelewa, kutoa fursa kwa wataalamu wa uchunguzi wa kisayansi kufanyia kazi...
Naanza biashara ya kuku, wapi nipeleke kati ya Dar na Dodoma?
Habari... Nipo mkoa wa Tabora nataka kufanya biashara ya kuku na kupeleka Dar es salaam au Dodoma je wapi ni sahihi? Faida za Dodoma Bei inaweza kuwa juu kutokana na nature ya watu wanaoishi huku(Target costumer ni mostly employed) Ukaribu na Tabora kwa usafiri wa roli. Faida ya Dar es salaam, Faida za ni uhakika wa wateja. Changamoto ni safari ndefu lakini pia usafiri kuku kuibiwq nk Je nipeleke kuku wapi?
Askofu Kinyaiya: Ukistaafu nenda kwako kapumzike, Usitese watu nyuma ya mwingine
Akitoa salamu za Pasaka kawaasa wasitaafu wapumzike wasitumie viongozi waliopo madarakani kuwaumiza watu. Ujumbe umfikie.
Mwigulu: Ofisi ya Waziri Mkuu inaliomba Bunge liidhinishe Tsh. Trilioni 12.5 za matumizi
Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba ameliomba Bunge kuidhinisha jumla ya Tsh. Trilioni 12.5 kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027, wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Ofisi yake Bungeni, Aprili 1, 2026.
Zungu: Waziri wa Nishati kutana na Kamati ya Nishati kujua uhakika wa mafuta kupatikana nchini
Spika wa Bunge, Mussa Zungu amemuagiza Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi kukutana na Kamati ya Bunge ya Nishati ili kujua hatma ya hali na mwenendo wa kupanda kwa bei ya mafuta nchini. Hatua hiyo imefuatia baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kutangaza bei mpya za mafuta hapa nchini zilizoanza kutumika kuanzia Aprili 1, 2026, ambapo Petroli kwa Dar es Salaam imepanda kutoka Tsh. 2,864 hadi Tsh. 3,820 kwa Lita moja.
LATRA: Wasafirishaji msiongeze nauli bila idhini ya mamlaka kwa kusingizia mafuta kupanda
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), imewataka wadau wote wa sekta ya usafirishaji nchini, kutopandisha nauli kwa kigezo cha kupanda kwa bei za mafuta na badala yake wafuate utaratibu rasmi utakaowekwa na watakaopandisha hawatasita kuwachukulia hatua kali za kisheria. Mkurugenzi Mkuu wa LATRA, CPA Dkt. Habibu Suluo, amesema Aprili 8 kutafanyika kikao cha wadau jijini Dar es Salaam kujadili jambo hilo
Diamond: Naogopa kuongelea mambo ya Serikali, unaweza kusema ukweli ukakuletea madhara
Msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, amesema anaogopa kuzungumzia masuala yanayohusu Serikali wakati wa mahojiano katika kituo chake cha Redio, Wasafi FM, akidai kuwa kusema ukweli kunaweza kumletea madhara.
Msigwa: Gharama za Uwanja wa Arusha zimeongezeka baada ya CAF kusema tuongeze vitu
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amefafanua kuwa gharama za ujenzi wa Uwanja wa Mpira wa Arusha zimeongezeka kutoka makadirio ya Tsh. Bilioni 187 hadi Tsh. Bilioni 338 kutokana na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kusema tuongeze vitu ili kukidhi mahitaji.
CAG: Deni la Serikali ni Tsh. Trilioni 110, ndani ya Mwaka limeongezeka Tsh. Trilioni 12.7
Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, imebaini kuwa deni la serikali limefikia Tsh. Trilioni 110 kufikia Juni 30, 2025. Ongezeko hili la Tsh. Trilioni 12.7, sawa na asilimia 13 ndani ya mwaka mmoja, likijumuisha deni la ndani la Tsh. Trilioni 35.5 na deni la nje la Tsh. Trilioni 74.55. Akizungumza Machi 30, 2026, Kichere ameeleza kuwa ukuaji wa deni hilo umechangiwa zaidi na kuongezeka kwa mikopo ya nje.
Amnesty yaonya Kombe la Dunia 2026 linaweza kuwa jukwaa la ukandamizaji
Shirika la kutetea Haki za Binadamu la Amnesty International limetoa onyo kuwa Mashindano ya Kombe la Dunia 2026 yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 11 hadi Julai 19, 2026 nchini Marekani, Canada na Mexico, yanaweza kugeuka kuwa "jukwaa la ukandamizaji." Amnesty imelitaka Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) na nchi waandaaji kuchukua hatua za dharura kulinda Haki za Binadamu za Wachezaji, Mashabiki na Jamii zinazozunguka mashindano hayo.
CAG: Uwanja wa Arusha ulikadiriwa Tsh. Bilioni 187, Mkataba ukasainiwa kwa Tsh. Bilioni 338
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere akisoma ripoti ya ofisi yake ya Mwaka 2024/2025, Machi 30, 2026 amesema alibaini upungufu katika mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Mpira wa Arusha, ambapo ulikadiriwa kugharimu Tsh. Bilioni 187 lakini mkataba ukasainiwa kwa Tsh. Bilioni 338. Uwanja huo unatarajiwa kutumika katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, itakayofanyika kwa pamoja Kenya, Tanzania, na Uganda kati ya Juni 19 hadi Julai 18, 2027.
Seleman Said Bungara (Bwege) afariki dunia
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kilwa Kusini mkoani Lindi kupitia Chama cha CUF, Selemani Said Bungara maarufu Bwege, amefariki dunia, Machi 30, 2026, alipokuwa akipatiwa matibabu katika hospitali binafsi iliyopo Kigamboni, jijini Dar es Salaam. Enzi za uhai wake Bwege amewahi kutumikia vyama vya Siasa vya CUF, ACT Wazalendo na hivi karibuni ilidaiwa alikuwa mbioni kujiunga na CHADEMA, ingawa mchakato rasmi wa kukabidhiwa kadi ya chama hicho ulikuwa haujakamilika.
CAS: Uamuzi wa Rufaa ya Senegal utatoka haraka iwezekanavyo
Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) imetangaza kuwa itatoa uamuzi wa rufaa ya Senegal "haraka iwezekanavyo" kufuatia hatua ya nchi hiyo kupinga kuvuliwa taji la Mataifa ya Afrika (AFCON), uamuzi uliofanywa na Shirikisho la Soka Afrika (CAS) mnamo Machi 18, 2026. Awali, Januari 18, 2026, Senegal ilitwaa ubingwa kwa ushindi wa goli 1-0, na baada ya maamuzi ya Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika (CAF), Morocco ilipewa ushindi wa mezani wa Magoli 3-0 kwa maelezo Senegal kukiuka Kanuni za
Je, mchakato wa kuhakiki taarifa kwenye vyombo vya habari unaendana na kasi ya kuenea kwa taarifa potoshi?
Shiriki nasi katika Mjadala huu kupitia Instagram Live ya JamiiForums, utakaoongozwa na mwandishi wa habari, Imani Luvanga, wazungumzaji ni Nuzulack Dausen wa Nukta Africa pamoja na Mpoki Thompson, Mhariri Mkuu Mwananchi Communication.
UN yapitisha azimio la kutambua utumwa wa Waafrika kama Uhalifu dhidi ya Binadamu
Hatua hiyo iliidhinishwa kwa kura 123 za kuunga mkono kuwa biashara ya utumwa wa Waafrika na mfumo wa kuwafanya kuwa mali ulikuwa miongoni mwa uhalifu mkubwa zaidi dhidi ya Ubinadamu na madhara yake ambayo yanaendelea kuathiri maisha ya watu hadi leo. Hata hivyo, nchi tatu ambazo ni Argentina, Israel na Marekani zilipinga azimio hilo, huku nchi 52 zikijizuia kupiga kura.
Usimamizi wa 'Mikopo ya Dharura kupitia simu' nchini Tanzania
Utangulizi Kuwa kwa kasi kwa huduma za kifedha za kidijitali nchini Tanzania kumeleta mapinduzi makubwa katika upatikanaji wa mikopo na huduma za malipo kwa mamilioni ya wananchi. Miongoni mwa ubunifu huu ni kuibuka kwa huduma za mkopo wa dharura kupitia simu za mkononi, zinazojulikana kwa majina tofauti ya kibiashara ikiwemo Songesha. Huduma hizi huwezesha watumiaji kukamilisha miamala hata wanapokuwa na salio pungufu kwenye pochi zao za simu, hivyo kutoa mkopo wa muda mfupi papo kwa hapo...
TANZIA | Waziri William Lukuvi afariki Dunia
Mwanasiasa mkongwe William Lukuvi amefariki Dunia, asubuhi ya Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa mshtuko wa moyo. Taarifa ya msiba wa William Lukuvi, aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani, imetangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka. Lukuvi, alizaliwa Agosti 15, 1955 na amewahi kuwa Mbunge kwa vipindi saba tangu mwaka 1995.
Wakili: Bado kuna kesi za waliokamatwa kwa tuhuma za uhaini Oktoba 29
Wakili wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), William Maduhu ameeleza licha ya Rais Samia kutoa agizo kwa DPP kufuta kesi za uhaini zinazowakabili vijana kufuatia matukio ya Oktoba 29, 2025, bado kuna mashauri Mahakamani ya waliokamatwa kwa tuhuma za uhaini. Amesema hayo Machi 19, 2026 katika mahojiano na Jambo TV, akidai Dar es Salaam mpaka sasa wamebaki watu 8 katika Mahakama ya Kisutu, Arusha watuhumiwa 9, Mwanza na Dodoma wamebaki watuhumiwa 4.
Kenya hatarini kupoteza Haki ya kuandaa AFCON 2027 kwa kushindwa kulipa ada ya uandaaji
Kenya ipo hatarini kupoteza haki ya kuwa mwenyeji wa Michuano ya AFCON 2027 kutokana na kuchelewa kulipa ada ya uenyeji ya Dola Milioni 30 (takribani Tsh. Bilioni 77) kwa Shirikisho la Soka la Afrika (CAF). Katibu Mkuu wa Wizara ya Michezo, Elijah Mwangi, ametahadharisha kuwa nchi hiyo inatakiwa kukamilisha malipo hayo ifikapo Machi 30, 2026. Hali hii inatia wasiwasi kwani washirika wenza katika zabuni ya "East Africa Pamoja," yaani Uganda na Tanzania, tayari wameshalipa fedha.
Back
Top Bottom