Featured content

TLS, LHRC, Dk. Slaa wamburuza Mahakamani Waziri Katambi kwa kuzuia mikutano ya Kisiasa
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kwa kushirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Dk. Willibrod Slaa, wamefungua kesi ya kikatiba katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Tabora, wakipinga kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, kuhusu zuio la mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa. Mbali na Katambi, wadaiwa wengine ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).
Morogoro: Wananchi wapinga mauaji yanayofanywa na Askari wa Hifadhi
Ndugu na jamaa wa kijiji cha Kisaki mkoani Morogoro wameandamana na kutoa malalamiko mazito dhidi ya askari wa wanyamapori (maliasili) kwa tuhuma za kuwauwa kikatili wananchi wanaoingia msituni kutafuta riziki zao, kama vile kukata mbao. Mmoja wa wananchi, ameeleza kuwa vitendo hivyo vya ukatili vimekithiri na kuacha majonzi makubwa kwa jamii, huku akiongeza kuwa msituni kuna mafuvu na miili mingi ya binadamu wenzao waliopoteza maisha kwa kupigwa risasi na askari hao
Biashara ya genge inalipa sana, kinachokwamisha watu ni kuwekeza mtaji mdogo sana
Mdau amesema biashara ya kuuza genge ni mojawapo ya biashara nzuri na yenye faida, lakini changamoto inayowafanya wengi wasifanikiwe ni kuanza na mtaji mdogo sana. Ameeleza kuwa kuwekeza mtaji wa mfano wa shilingi 80,000 pekee kunafanya iwe vigumu biashara kukua, huku akisisitiza kuwa mafanikio yanahitaji uwekezaji wa kutosha na kuondoa hofu ya kupata hasara.
Morocco kujenga uwanja mkubwa zaidi duniani kwa ajili ya Kombe la Dunia 2030
Morocco kujenga uwanja mkubwa zaidi duniani kwa ajili ya Kombe la Dunia 2030 Uwanja huo utajengwa katika eneo la El Mansouria, kilomita 38 kaskazini mwa jiji la Casablanca, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Morocco kwa ajili ya Kombe la Dunia la FIFA 2030, ambalo litaandaliwa pamoja na Hispania na Ureno. Kampuni za usanifu za Populous na Oualalou + Choi ndizo zimebuni mradi huo, unaotarajiwa kuifanya Grand Stade Hassan II kuwa uwanja mkubwa zaidi wa soka duniani.
Msigwa: Kinachomponza Lissu ni Akili, mmeamua kufungia Akili yake ndani ya Gereza
Kada wa CHADEMA, Mchungaji Peter Msigwa, amesema Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, hapaswi kulazimishwa kuomba msamaha ili aachiwe huru, akisisitiza kuwa hana kosa linalohitaji msamaha.
Prof. Tibaijuka: Rais naendelea kushauri Tundu Lissu aachiwe huru kwani kesi haikamiliki
Waziri wa zamani, Profesa Anna Tibaijuka, amemshauri Rais Samia kumwachilia huru Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, ambaye amekuwa rumande katika Gereza Kuu la Ukonga kwa zaidi ya mwaka mmoja akisikiliza kesi ya uhaini inayomkabili. Kupitia ujumbe aliouchapisha katika mtandao wa X, Tibaijuka amesema kesi hiyo imechukua muda mrefu bila kukamilika na kumtaka Rais kuongozwa na hekima na busara alizoonyesha alipotoa sera ya maridhiano ya 4Rs.
Oburu Oginga: Chama cha ODM kumuunga mkono Ruto Uchaguzi Mkuu wa 2027
Chama cha Orange Democratic Movement (ODM) kimetangaza kuwa hakitasimamisha mgombea urais katika uchaguzi mkuu wa Kenya wa mwaka 2027, badala yake kitamuunga mkono Rais William Ruto kuwania muhula wa pili madarakani. Kauli hiyo ilitolewa, Julai 12, 2026, na kiongozi mwandamizi wa ODM, Oburu Oginga, ambaye amesema uamuzi huo umetokana na mazungumzo ya kisiasa yanayoendelea kati ya chama hicho na viongozi wa serikali.
IMF yaipatia Tanzania mkopo Nafuu wa takriban Tsh. Trilioni 1.16
Wizara ya Fedha imeeleza kuwa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limeidhinisha kutolewa kwa Dola za Marekani Milioni 443.9 (takriban Tsh. Trilioni 1.16) kwa Tanzania baada ya kukamilisha tathmini za mwisho chini ya programu za ECF inayohusisha upatikanaji wa mkopo nafuu ya kuimarisha uchumi wa nchi kupitia sekta za uzalishaji na huduma za jamii na RSF ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
FIFA yafikiria uwezekano wa Kombe la Dunia kushirikisha timu 64 ifikapo 2030
Rais wa FIFA, Gianni Infantino, amesema shirikisho hilo litajadili uwezekano wa kuongeza idadi ya timu zitakazoshiriki Kombe la Dunia la mwaka 2030 kutoka timu 48 hadi 64. Amesema pendekezo hilo litajadiliwa na kamati husika baada ya kumalizika kwa Kombe la Dunia la 2026, akisisitiza kuwa mashindano hayo yanapaswa kutoa fursa kwa mataifa mengi zaidi kushiriki.
Kombe la Dunia 2026: Timu nne bora duniani zatinga nusu fainali kwa mara ya kwanza
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Kombe la Dunia la FIFA, timu nne zinazoongoza katika viwango vya ubora vya FIFA (FIFA World Rankings) zimefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali. Hatua ya nusu fainali ya Kombe la Dunia 2026 imekamilika kwa kuzikutanisha timu nne bora duniani kwa mujibu wa viwango vya FIFA: Ufaransa, Argentina, Hispania na England.
Senegal yamtimua kocha Pape Thiaw na benchi lake la ufundi
Shirikisho la Soka la Senegal limemfuta kazi kocha mkuu Pape Thiaw na benchi lake lote la ufundi baada ya kutolewa katika hatua ya 32 bora, wiki chache tu baada ya kusaini mkataba mpya kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia la FIFA. Senegal ilikuwa ikitarajiwa kuwa miongoni mwa timu zitakazowania ubingwa wa Kombe la Dunia, baada ya kuifunga Morocco katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Januari 2026.
Jumuiya ya Madola yaipa Tanzania siku 30 Kutatua suala la kushikiliwa kwa Tundu Lissu
Wakuu, Nimeona niwaletee mrejesho na uchambuzi wa waraka muhimu sana ambao umetoka leo tarehe 10 Julai 2026 kutoka kwa Kundi la Mawaziri wa Jumuiya ya Madola linaloshughulikia Demokrasia na Haki za Binadamu (CMAG - Commonwealth Ministerial Action Group). Kikao chao cha 73 kimefanyika leo kwa dharura (extraordinary session) na kutoa Tamko la Kuhitimisha (Concluding Statement) ambalo sehemu kubwa limejadili hali ya kisiasa na haki za binadamu hapa nchini kwetu Tanzania. Kwa ufupi, Tanzania...
ACT: Tunataka uchunguzi huru na wa haraka kuhusu Uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania
Chama cha ACT Wazalendo kimetaka kufanyika kwa uchunguzi huru na wa haraka kuhusu uchaguzi wa viongozi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), baada ya kuzuka kwa sintofahamu kuhusu matokeo ya Uchaguzi wa Urais, ambapo Leonard Thadeo aliyepata kura moja alitangazwa mshindi.
Sadio Mané atangaza kustaafu kuichezea Senegal, baada ya miaka 14
Baada ya Senegal kuondolewa kwa maumivu katika hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia 2026 kufuatia kufungwa mabao 3-2 na Ubelgiji, nyota wa timu hiyo, Sadio Mané, ametangaza kustaafu kuchezea timu ya taifa. Mané (34), alitangaza uamuzi huo kupitia taarifa iliyochapishwa na gazeti la Senegal la Le Quotidien, akihitimisha safari ya miaka 14 akiwa na timu ya taifa ya Senegal. "Fahamuni kwamba nilijitoa kwa kila kitu kwa ajili ya bendera hii. Nilitoa uwezo wangu wote na siku zote nilipigania...
Mnyika: Fedha za 'ToneTone' ziko salama, kwa sasa anayehusika kusaini ni Katibu Mkuu
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, amethibitisha kuwa fedha zote zinazochangwa na wananchi pamoja na wanachama, ikiwemo mifumo ya kielektroniki na zile za "tonetone" zinazokusanywa mikutanoni, ziko salama kabla na baada ya matumizi. Mnyika aliongeza kuwa, kwa mujibu wa taratibu za kifedha za kitaasisi, yeye kama Katibu Mkuu ndiye Afisa Masuhuli wa chama ambaye anasimamia uidhinishaji huo.
Taharuki za Kisiasa nchini zinaweza kuathiri fursa ya kuwa mwenyeji wa AFCON 2027?
Tanzania inatarajiwa kuandika historia kwa kuwa kati ya wenyeji wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027. Michuano hiyo inatazamiwa kufungua fursa kubwa na nyingi kutokana na kukusanya mataifa mbalimbali, hivyo kuwa kivutio kwa mashabiki Duniani. Wakati maandalizi yakishika kasi, Mdau anasema hali ya Kisiasa tangu na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 imekuwa na vipindi vya taharuki, inachangiwa na wito wa maandamano unaosambazwa mitandaoni na Wanaharakati au vikundi visivyojulikana.
Rais Samia: Maridhiano si udhaifu, bali ni ukomavu wa kisiasa unaojenga umoja wa nchi
Rais Samia Suluhu amesema maridhiano ni ishara ya ukomavu wa kisiasa unaojenga umoja na kuheshimiana, akisisitiza kuwa siasa zinapaswa kuongozwa na hekima, utu na maslahi ya taifa badala ya mivutano isiyoisha. Amesema wananchi wanahitaji amani, usalama na utulivu, akizungumza Julai 9, 2026, wakati wa kushuhudia Tamko la Pamoja la Maridhiano ya Kisiasa kati ya CCM na ACT-Wazalendo katika Viwanja vya Ikulu, Zanzibar.
NECTA yafuta matokeo ya Kidato cha 6 na Ualimu waliotumia ChatGPT kujibu mtihani
Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limefuta matokeo ya watahiniwa 58 baada ya kubainika kufanya udanganyifu kwenye mitihani. Waliofutiwa matokeo ni watahiniwa 44 wa Mtihani wa Kidato cha Sita na 14 wa Mtihani wa Stashahada ya Ualimu wa Elimu ya Msingi (DPEE), baadhi wakitajwa kutumia AI (Chatgpt).
Neymar Jr atangaza kustaafu kuichezea Timu ya Taifa ya Brazil
Neymar Jr ametangaza rasmi kustaafu kuichezea timu ya taifa baada ya Brazil kutolewa kwenye Kombe la Dunia na Norway katika hatua ya 16 Bora, ikiwa ni mara ya kwanza Brazil kushindwa kufika hatua ya robo fainali ya Kombe la Dunia tangu mwaka 1990.
JWTZ: Wasioitakia mema nchi yetu, wanahamasisha kufanya vurugu, hatutasita kuchukua hatua
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limewataka wananchi kupuuza wito wowote unaohamasisha vurugu na uvunjifu wa amani, likisisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaohusika na vitendo hivyo. Katika taarifa yake kwa umma, JWTZ imesema kuwa ina jukumu la kulinda usalama wa nchi na wananchi kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na Sheria ya Ulinzi wa Taifa Sura ya 192. Jeshi hilo limeeleza kuwa litaendelea kushirikiana...
Back
Top Bottom