Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, amesema Watanzania kwa sasa wanaishi katika mazingira ya hofu, tofauti na ilivyokuwa zamani. Amesema wananchi wengi wanaogopa kutekwa, kupotea na kukumbwa na madhara mengine, hali inayowafanya kushindwa kutoa maoni yao kwa uhuru.
Kwa mujibu wa Jaji Warioba, hofu hiyo imeathiri ushiriki wa wananchi katika mijadala mbalimbali ya kitaifa. Amesema watu wengi sasa wanaogopa kueleza wanachofikiri, wakihofia kwamba maoni yao yanaweza kuwapelekea kukamatwa...