Featured content

Waziri Katambi apiga marufuku mikutano ya Siasa kwa Vyama vyote
Leo bungeni Waziri wa Mambo ya Ndani, Patrobas Katamb ameagiza Jeshi la Polisi kusitisha vibali vya mikutano ya siasa kwa kipindi kisichojulikana. Moto umekuwa mkali na uwanja umeinama kwa upande wa CCM hadi kuomba tena Msaada wa jeshi la polisi , ingawa wananchi tuliwaonya CCM kuwa vita hii ya kubishana na CHADEMA mtaangukia pua lkn walibisha. Waziri wa Mambo ya ndani, akiwa bungeni amesema ''Kwa sababu ya taharuki hizi ambazo zimekuwa zikiendelea, nitatumia fursa hii pia, Mheshimiwa...
Prof. Assad: Kesi yangu ya kutenguliwa iko Mahakama ya Rufani, Mwaka wa 6 haisikilizwi
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mstaafu, Mussa Juma Assad, ameonyesha wasiwasi wake kuhusu kuchelewa kusikilizwa kwa kesi yake iliyopo katika Mahakama ya Rufani, akisema kinachomshangaza ni kesi hiyo kufikisha mwaka wa sita bila kutolewa maamuzi.
Prof. Assad: Nikipigiwa simu ya maagizo, asubuhi yake nilikuwa naandika barua ya tulichokizungumza
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mstaafu, Mussa Juma Assad, amesema katika kipindi chake cha utumishi alikuwa akipokea simu za maelekezo kutoka kwa baadhi ya watu wakimtaka asifanye maamuzi fulani, lakini mara nyingi alisimamia alichokiamini kuwa sahihi. Aliongeza kuwa ilikuwa desturi yake kila alipopokea maelekezo ya namna hiyo, asubuhi yake aliandika barua rasmi kuweka kumbukumbu ya mazungumzo hayo na msimamo wake kuhusu suala husika.
Makonda: Tanzania ndiyo Baba na Mama wa demokrasia Afrika
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amewataka watu duniani kote kutotiririsha kauli kuwa Tanzania haina demokrasia, akisisitiza kuwa nchi hiyo ndiyo "baba na mama" wa demokrasia barani Afrika. Akizungumza bungeni Juni 22, 2026, Makonda alieleza kuwa mchango wa Tanzania katika kupokea na kuwatunza wapigania uhuru wa mataifa ya kigeni ndio ulioweka misingi imara ya ukombozi na demokrasia barani Afrika.
Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer ajiuzulu
Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, ametangaza kujiuzulu nafasi yake Jumatatu hii baada ya kukabiliwa na shinikizo la miezi kadhaa, hatua inayofungua njia kwa nchi hiyo kupata Waziri Mkuu wa saba katika kipindi cha muongo mmoja uliopita. Akihutubia nje ya Ofisi ya Waziri Mkuu (10 Downing Street), Starmer ambaye amekuwa madarakani tangu Julai 2024 alikiri wazi kuwa amepoteza uungwaji mkono kutoka kwa wabunge wa chama chake cha Labour.
Katambi: Nimetenga Tsh. Milioni 100 kuwalipa watoa taarifa za uhalifu nchini
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amesema Serikali imetenga Shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuwazawadia wananchi watakaotoa taarifa sahihi zitakazosaidia kubaini na kuzuia vitendo vya uvunjifu wa amani nchini. Amesema hatua hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano kati ya wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama katika kulinda amani, usalama na utulivu wa nchi.
Prof. Tibaijuka: Lissu kuendelea kusalia Gerezani haina afya, Nchi haiwezi kutulia bila maridhiano
Mwanazuoni na Waziri wa zamani, Profesa Anna Tibaijuka, amebainisha kuwa nchi haiwezi kupata utulivu wa kweli wa kisiasa ikiwa hakuna maridhiano ya dhati, huku akisisitiza kuwa kuendelea kusalia gerezani kwa Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, hakuna afya kwa ustawi wa taifa.
Prof. Tibaijuka: Watu waliopotea ni doa kubwa kwa taifa, Polisi wana wajibu wa kuwatafuta
Waziri Mstaafu na Mchumi Profesa Anna Tibaijuka amesema jukumu la kwanza la serikali si kujenga barabara au kuleta maendeleo ya kiuchumi, bali ni kulinda maisha ya wananchi na mali zao, huku akieleza masikitiko yake kuhusu ongezeko la matukio ya watu kupotea nchini ambayo ameyataja kuwa doa kubwa kwa taifa.
Mwanamfalme wa Norway ahukumiwa kifungo cha miaka 4 jela kwa ubakaji na unyanyasaji
Marius Borg Høiby, mtoto wa kwanza wa Binti Mfalme Mteule wa Norway, Mette-Marit, amehukumiwa kifungo cha miaka minne jela baada ya kupatikana na hatia ya ubakaji, kushambulia, na unyanyasaji katika mahusiano ya karibu. Aidha, Høiby hakuhudhuria mahakamani Juni 15, 2026 kutokana na changamoto za kiafya, hivyo alifuatilia usomaji wa hukumu hiyo kwa njia ya video akiwa gerezani. Mbali na kifungo hicho, mahakama imemuamuru kuwalipa fidia waathiriwa wa vitendo vyake.
Bunge la Ulaya lataka msaada wa Tsh. Bilioni 473.9 kwa Tanzania usitishwe
Bunge la Ulaya (MEPs) limeitaka Tume ya Ulaya (EU) kufuta mpango wa ufadhili wa Euro milioni 156 (sh. Bilioni 473.9) kwa Tanzania wa mwaka 2026, likidai kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa Haki za Binadamu na misingi ya Kidemokrasia baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Mwigulu: Dhahabu haijauzwa, ni mambo ya watu wenye ajenda ya kutengeneza chuki ndani ya nchi
Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba, amesema dhahabu inayohifadhiwa kama akiba ya taifa haijauzwa, akisisitiza kuwa mkakati uliopo ni kuongeza akiba hiyo na si kupunguza. Akiwasilisha majibu ya serikali mbele ya Bunge jijini Dodoma Juni 18, 2026, Mwigulu amejibu hoja na maswali mbalimbali ya Wabunge waliohoji juu ya mwenendo na usalama wa akiba ya madini hayo ya thamani nchini.
Serikali: Mchakato wa Katiba Mpya utaanza baada ya Maridhiano, Rais ataeleza muda ukifika
Serikali kupitia Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Homera, imesema mchakato wa kushughulikia Katiba Mpya utatekelezwa baada ya kukamilika kwa kazi za tume husika pamoja na mchakato wa maridhiano unaoendelea nchini. Akizungumza 17 Juni 2026 jijini Dodoma, Dkt. Homera amesema Serikali inaendelea kuweka kipaumbele katika hatua mbalimbali za kitaasisi ili kuhakikisha masuala hayo yanakamilika kabla ya kuendelea na mchakato wa Katiba Mpya.
Marekani na Iran zasaini mkataba wa awali wa kusitisha Vita
Rais Donald Trump amesaini nakala ya makubaliano kati ya Marekani na Iran katika Jumba la Kifalme la Versailles nchini Ufaransa, na kuhitimisha ziara yake ya G7. Kwa mujibu wa afisa mmoja wa Marekani, baada ya hapo Marekani iliwatumia Wairani picha ya makubaliano hayo yaliyosainiwa. Waraka huo kisha ukasainiwa na Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian. Makubaliano haya yanazitaka Marekani na Iran kufikia mkataba wa mwisho na kamili ndani ya siku 60.
Serikali ya Guinea ya Ikweta yajiuzulu baada ya kutofikia malengo
Serikali ya Guinea ya Ikweta imejiuzulu kwa kutofikia malengo yake, huku serikali mpya ikitarajiwa kuundwa hivi karibuni. Makamu wa Rais, Teodoro Nguema Obiang Mangue, amesema Waziri Mkuu, Manuel Osa Nsue Nsua, amewasilisha barua ya kujiuzulu kwa niaba ya baraza zima la mawaziri lililoteuliwa mwaka 2024 baada ya serikali kufikia chini ya asilimia 10 ya malengo yaliyowekwa, akisisitiza kuwa uwajibikaji wa umma lazima uendane na matokeo.
P Diddy apunguziwa muda wa kifungo Jela, sasa kutoka Februari 23, 2028
Msanii P Diddy anatarajiwa kuachiliwa kutoka gereza la shirikisho la Marekani mapema zaidi baada ya tarehe yake ya kuachiwa kurekebishwa tena, kulingana na taarifa mpya zilizochapishwa na Federal Bureau of Prisons. Tarehe mpya sasa imewekwa kuwa Februari 23, 2028.
Musukuma: Mawaziri wa Zanzibar chungeni kauli zenu za kibaguzi bungeni
Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma, amewaonya baadhi ya wabunge na mawaziri wa Zanzibar kuepuka kauli na mijadala inayoweza kusababisha mgawanyiko na kuhatarisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ametoa kauli hiyo bungeni wakati wa mjadala kuhusu hali ya uchumi wa taifa, mpango wa maendeleo, na bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Musukuma amemuomba Rais Dkt. Hussein Mwinyi, kuchukua hatua dhidi ya mawaziri wanaodaiwa kutoa kauli zenye viashiria vya ubaguzi bungeni.
Nigeria: Mahakama yaiagiza Tume ya Uchaguzi kukifuta chama kikuu cha upinzani kuelekea uchaguzi wa 2027
Mahakama Kuu nchini Nigeria imeiamuru Tume ya Uchaguzi (INEC) kukifuta chama kikuu cha upinzani (ADC) na vyama vingine vinne kwa kushindwa kukidhi vigezo vya kikatiba katika uchaguzi wa 2023. Uamuzi huo uliotolewa na Jaji Peter Lifu Juni 15, 2026, unatarajiwa kubadilisha kabisa uwanja wa ushindani wa kisiasa. Hatua hii inaweka kiwingu kizito kwa Makamu wa zamani wa Rais, Atiku Abubakar, ambaye alitarajiwa kugombea urais kupitia ADC ili kumkabili Rais Bola Tinubu katika uchaguzi wa Januari 2027.
Kwanini FIFA imeondoa Majina (logo) halisi za Viwanja vya Kombe la Dunia 2026?
Katika Kombe la Dunia la 2026 linalofanyika Marekani, Mexico, na Canada, viwanja kadhaa vimebadilishwa majina (chapa) yao kwa muda kutokana na sera kali ya FIFA ya "Uwanja Msafi" (Clean Stadium Policy). Mabadiliko haya yanatokana na moja ya sheria za kibiashara zinazosimamiwa na FIFA katika mashindano yake ambapo chini ya sheria hii, hakuna uwanja unaoruhusiwa kuonyesha chapa yoyote ya kibiashara ambayo si mdhamini rasmi wa FIFA.
KOMBE LA DUNIA: Kipa mkongwe Vozinha ang'ara Cape Verde ikizuia Uhispania kufunga bao
Kipa mkongwe wa Cape Verde, Vozinha (40), ameokoa michomo 7, ikiwemo 6 ya ndani ya boksi, na kuwa shujaa kwa kuisaidia timu yake kutoka sare ya 0-0 dhidi ya mabingwa wa Ulaya, Uhispania, katika mchezo wa Kundi H wa Kombe la Dunia 2026. Matokeo hayo yameifanya Cape Verde kupata pointi yake ya kwanza kabisa katika historia ya kushiriki Kombe la Dunia.
Zungu: Kwanini Makampuni ya Simu hayauzi Hisa kwa Umma?, TCRA na CMSA wahojiwe!
Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu (Mb), Juni 15, 2026, ameeleza Bungeni kuwa tangu Serikali ilipofanya marekebisho ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOKA) mwaka 2016, kampuni zote za simu zilitakiwa kuuza angalau asilimia 25 ya hisa zake kwa umma kupitia soko la hisa ndani ya kipindi kilichoishia Juni 2018. Amesema hadi sasa ni kampuni ya Vodacom pekee iliyotekeleza takwa hilo la kisheria.
Back
Top Bottom