Marius Borg Høiby, mtoto wa kwanza wa Binti Mfalme Mteule wa Norway, Mette-Marit, amehukumiwa kifungo cha miaka minne jela baada ya kupatikana na hatia ya ubakaji, kushambulia, na unyanyasaji katika mahusiano ya karibu.
Aidha, Høiby hakuhudhuria mahakamani Juni 15, 2026 kutokana na changamoto za kiafya, hivyo alifuatilia usomaji wa hukumu hiyo kwa njia ya video akiwa gerezani. Mbali na kifungo hicho, mahakama imemuamuru kuwalipa fidia waathiriwa wa vitendo vyake.