Featured content

Makala ya CNN kuhusu Matukio ya Uchaguzi Tanzania yapata tuzo
Mwandishi wa Habari wa Shirika la Habari ya Kimataifa CNN, Larry Madowo ameshinda Tuzo ya NABJ Salute to Excellence 2026 kufuatia Makala ya kiuchunguzi kuhusu vifo vilivyotokea nchiniTanzania wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Jaji Warioba: Watanzania wanaishi kwa uoga, wanaogopa kutekwa, kupotea na kubambikiwa Kesi za uhaini
Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, amesema Watanzania kwa sasa wanaishi katika mazingira ya hofu, tofauti na ilivyokuwa zamani. Amesema wananchi wengi wanaogopa kutekwa, kupotea na kukumbwa na madhara mengine, hali inayowafanya kushindwa kutoa maoni yao kwa uhuru. Kwa mujibu wa Jaji Warioba, hofu hiyo imeathiri ushiriki wa wananchi katika mijadala mbalimbali ya kitaifa. Amesema watu wengi sasa wanaogopa kueleza wanachofikiri, wakihofia kwamba maoni yao yanaweza kuwapelekea kukamatwa...
Katambi: Ajenda ya Katiba Mpya si ya wapinzani ni ya CCM, ilianza tangu chini Kikwete
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amesema Ajenda ya Katiba Mpya sio Ajenda ya Wapinzani bali ni ajenda ya Chama cha Mapinduzi (CCM) iliyoanza tangu Awamu ya Nne chini ya Uongozi wa Rais wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambapo Rais wa Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu akiweka wazi nia ya kuleta Katiba Mpya na ndio maana Ajenda hiyo ipo katika Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.
Msigwa: Tuhuma za Tanzania kuingilia Uchaguzi Mkuu Zambia si za kweli
Serikali ya Tanzania imekanusha tuhuma za kutuma raia wake kwenda Zambia kuingilia au kuvuruga Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo uliofanyika Agosti 13, 2026. Serikali imesema madai hayo hayana ukweli na imeanza kuyafuatilia kupitia njia za kidiplomasia. Tuhuma hizo zilitolewa na mgombea urais wa chama cha NRPUP nchini Zambia, Brian Mundubile, ambaye alidai kuwa Watanzania wamepelekwa nchini humo kwa lengo la kuingilia mchakato wa uchaguzi. Kauli hiyo imezua mjadala nchini Zambia katika kipindi cha...
Jaji Warioba: Naamini kwa ratiba iliyopo hatutakuwa na Katiba Mpya Mwaka 2028
Jaji mstaafu Joseph Warioba amesema dalili zinaonyesha kuwa serikali imekubali mapendekezo ya Tume ya Jaji Mohamed Chande Othman, ambayo kwa undani wake hatafahamu, isipokuwa kwenye hotuba yake aliyotoa huku utekelezaji wake ukiendelea. Miongoni mwa mapendekezo makubwa ni kuundwa kwa Tume ya Maridhiano na kukamilisha mchakato wa katiba mpya ifikapo mwaka 2028.
Mundubile: UNPD wameamua kutumia mbinu ya Tanzania, hawawezi kushinda uchaguzi huu
Wanapeleka wizi wa kura kwenye taifa la Kikristo, Wanatumia mbinu za Tanzania.👇 "UNPD hawawezi kushinda uchaguzi huu, hakuna muujiza. Sasa wameamua kutumia “mbinu (formula) ya Tanzania.” Zambia si Tanzania, Zambia si Tanzania… Hii ni Zambia. Wale wanaofikiri wanaweza kuingiza katika nchi hii mbinu inayofanya kazi Tanzania, hawawezi kufanikiwa kamwe. Ndugu zangu Watanzania ambao mmekodiwa, tafadhali tokeni katika nchi yetu."- Brian Mundubile. Mgombea Urais kupitia kupitia chama cha upinzani...
Polisi: Tunamhoji Peter Madeleka kwa Tuhuma za kudharau amri ya Mahakama Kuu
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limesema kuwa tarehe 14 Agosti 2026, saa 9:30 alasiri, eneo la Mikocheni B, Kinondoni, limemkamata na linamhoji Peter Madeleka kwa tuhuma za kudharau amri za Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, maarufu kama “Mahakama ya Mafisadi.” Kwa mujibu wa Jeshi hilo, amri hizo zilitolewa na Mahakama tarehe 27 Julai 2026 na tarehe 13 Agosti 2026. Soma > Malisa: Wakili Madeleka amekamatwa na watu waliojitambulisha ni polisi Jeshi la...
Zambia yasitisha zoezi la kuhesabu kura baada ya ripoti za "vurugu" katika baadhi ya maeneo
Zambia imesitisha zoezi la kuhesabu kura kote nchini leo Ijumaa kufuatia ripoti za vurugu katika baadhi ya maeneo. Afisa mkuu wa uchaguzi Brown Kasaro amesema "Ghasia hizo zinawalenga wafanyakazi wa uchaguzi, na katika baadhi ya matukio zimesababisha wizi wa karatasi za kura kwenye masanduku ya kura". Ameongeza kuwa tume hiyo itatathmini upya uamuzi wa kusitishwa zoezi hilo ndani ya saa 24. Taifa hilo lenye utajiri wa shaba kusini mwa Afrika lilipiga kura Alhamisi katika uchaguzi...
Shahidi kesi ya Lissu apata dharura, kesi yaahirishwa hadi Agosti 17, 2026
Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, imeahirishwa hadi Jumatatu, Agosti 17, 2026, baada ya upande wa Jamhuri kuomba muda zaidi kutokana na changamoto za kiafya alizopata shahidi wa 18 aliyepaswa kuanza kutoa ushahidi leo Ijumaa.
Padri Kitima: Bado hatujamsikia Rais akisema neno 'Samahani' kwa yaliyotokea
Wakuu, Padri Kitima leo kwenye mahojiano maalum amesema japo Rais alikiri kutokea kwa changamoto na kusema matukio hayo hayakuwa ya kawaida na hayatapaswa kujirudia, bado hajatamka neno "samahani" kwa niaba ya watendaji wa serikali yake. "Ni kweli Mheshimiwa Rais alisema yaliyotokea hayakupaswa kutokea na hayatatokea tena. Lakini bado hatujamsikia akisema 'samahani' kwa niaba ya watendaji wake waliokusababishia wananchi maumivu hayo," alisema kiongozi huyo wakati wa mahojiano hayo.
TBS: Tumewasilisha taarifa ili Rwanda itoe sababu ya kuzuia vinywaji vya Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti Vyakula na Dawa Rwanda (FDA) iliripotiwa kuzuia vinywaji aina 52 kwa madai ya kutokuwa na ubora ikiwemo kutoka Tanzania, Kenya na Uganda.
Artan asema kuchezesha UEFA Super Cup ilikuwa kama Kombe la Dunia kwake
Baada ya kunyimwa ruhusa ya kuingia Marekani kwa ajili ya Kombe la Dunia, Omar Artan alikuwa mwamuzi wa kwanza kutoka Afrika kuchezesha fainali ya UEFA Super Cup Agosti 12, 2026 mjini Salzburg, nchini Austria katika Uwanja wa Red Bull Arena (pia unajulikana kama Stadion Salzburg), ambapo klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Aston Villa.
Polisi: Tunawashikilia Askari Watatu kwa tuhuma za kifo cha raia katika Hifadhi ya Ngorongoro
Ufafanuzi kuhusu tukio la mtu mmoja kufariki Ngorongoro Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha lilipokea taarifa kuwa kuna watu wawili wanaume wamefikishwa katika Hospitali ya Lutheran Wilayani Karatu na kati ya hao wawili mmoja alikuwa ameshafariki dunia na mmoja yu hai anaendelea kupatiwa matibabu. Pia soma ~ Sefu Musa adaiwa kuawa na askari baada ya kutuhumiwa kuwa mjangili Ngorongoro Timu ya Askari Polisi ilifika katika Hospitali hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo...
Walioomba ruzuku, wanunua picha ya Samaki (Pomboo) kwa Tsh. Bilioni 1.8 kwa ajili ya Rais Samia
Wachimbaji madini nchini wamenunua picha moja kwa ajili ya kumpa zawadi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Samia Suluhu Hassan kwa thamani ya Shilingi Bilioni 1.8. Wachimbaji hao wamenunua picha inayowaonesha Pomboo (Dolphin) wakiwa ndani ya maji Kizimkazi. Katika hafla ya usiku wa sanaa za picha uliofanyika Kizimkazi Zanzibar, Rais Samia ameeleza kuwa picha hiyo ina historia kubwa katika maisha yake jambo ambalo limewavutia zaidi Wachimba madini nchini Tanzania kwa umoja wao na...
Nondo: Kupitia Katiba Mpya wale wanaojifanya 'Miungu Watu' katika Ofisi za Umma watatuheshimu
Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa ya Chama cha ACT-Wazalendo, Abdul Omary Nondo ameeleza hayo wakati akihutubia katika kongamano la ACT Wazalendo la Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani lililofanyika katika Ukumbi wa Mrina, Dar es Salaam, Agosti 12, 2026.
Wakili Maduhu: Vijana wa ACT jiulizeni Serikali ya CCM ina nia ya dhati ya kufanya maridhiano?
Wakili William Maduhu akizungumza leo tarehe 12 Agosti 2026 wakati Ngome ya Vijana ya ACT Wazalendo chini ya Mwenyekiti wake Abdul Nondo inapoadhimisha Siku ya Vijana Duniani kwa kufanya Kongamano katika Ukumbi wa Mrina, Dar es Salaam.
Temba: Kamati ya Kuondoa Malori Dar inaundwa na mtu mwenye 'yard', atamshauri nini RC?
"Uongezekaji wa Malori nchini umekuwa muda mrefu, tangu Mwaka 2014 tuko hapa ITV tunazungumza hili suala mpaka leo, msongamano uko mwingi tangu mzani ukiwa pale Kibaha bado kulikuwa na msongamano, niwape elimu Watanzania pale Bandarini ni Boda," Alphonce Temba - Mwakilishi wa Wananchi. Video: ITV
Mabadiliko ya Kanuni za BoT (GN No. 206, 2026): Fursa au Mtego wa Kifedha kwa Tanzania?
Wakuu, nadhani mmeona Taarifa ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupitia barua ya Agosti 6, 2026, ikizungumzia Maboresho ya Kanuni za Fedha za Kigeni kupitia Tangazo la Serikali (GN) Na. 206 la mwaka 2026 (Foreign Exchange (Amendment) Regulations, 2026). Suala hili limenivutia sana kutaka kulijua kwa undani: Uamuzi huu unamaanisha nini, una faida gani, na una hatari gani kwa uchumi wetu? Hatua hii ya BoT kuwaruhusu wawekezaji wote wa kigeni (wasio wakazi) kununua Hatifungani (Treasury Bonds)...
Heche: Kosa ambalo tumewahi kulifanya CHADEMA ni kuwaamini Watu wasioaminika
John Heche anasema anasema moja ya makosa ambayo wamewahi kuyafanya ni kuwaamini watu wasioaminika, anasema waliwaamini CCM kwenye maridhiano a Mbowe na kumbe ulikuwa ni ulaghai tu na kosa lingine ni kuwaamini CCM kwenye katiba mppya wakati ule wa mchakato bungeni na baada ya hapo CCM kupitia Rais Kikwete akawazunguka na kuongeza watu wa CCM kupita NGOs hali ambayo ikaongeza nguvu na kushindwa kuwapa watanzania katiba
Wafungua kesi wakitaka Mawakili 399 waondolewe katika orodha ya Mawakili
Je, kuwa na Shahada ya Sheria na kufanya kazi kwenye mazingira ya sheria ni sawa na kuwa na mafunzo maalumu yanayomwandaa mtu kuwa Wakili? Hili ni moja ya maswali makubwa ambayo mimi na wenzangu wengine wanne katika shauri hili tumeamua kulipeleka mbele ya Mahakama Kuu ya Tanzania. Tarehe 30 Julai 2026, tuliwasilisha shauri la kikatiba kuhusu namna kifungu cha 16(2) cha Sheria ya Mawakili kinavyotumika kutoa msamaha (exemption) kwa baadhi ya watu kutopitia mafunzo ya kitaaluma ya Law...
Back
Top Bottom