Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kwa kushirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Dk. Willibrod Slaa, wamefungua kesi ya kikatiba katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Tabora, wakipinga kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, kuhusu zuio la mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa.
Mbali na Katambi, wadaiwa wengine ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).