Featured content

SI KWELI | Yanga yamtimua kocha Pedro na mikoba yake kurithiwa na Patrick Mabedi
Kuanzia Machi 3, 2026 kumekuwa na barua/taarifa kwa Umma yenye utambulisho wa klabu ya Yanga ikieleza kuwa klabu hiyo imemtimua kocha wake Mkuu Pedro Goncalves na hivyo klabu hiyo itaongozwa kwa muda na kocha msaidizi Patrick Mabedi. Baada ya ufuatiliaji wa kina imebainika kuwa taarifa hiyo si ya kweli.
Ujumbe wa sauti wa Vijana wa Hamasa - CCM kwenye Vituo vya SGR usitishwe, unagawa abiria kiitikadi
Mdau wa JamiiForums.com ametaka wimbo wa vijana wa hamasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unaochezwa kwenye vituo vya SGR usitishwe mara moja kwa kuwa Treni hiyo inatumika na Watu wenye kiitikadi tofauti.
CHADEMA Zanzibar: Hatujamtuma Said kukishtaki chama, ni kesi yake na makundi yaliyomtuma
CHADEMA Zanzibar, kimetoa taarifa ya kukanusha madai yaliyotolewa na Said Issa Mohamed kuhusu kufungua kesi kwa niaba ya chama juu ya mgawanyo wa mali na kujitambulisha kama kiongozi wa chama hicho. Taarifa imeeleza kesi hiyo siyo ya Chama bali ni ya Said Issa Mohamed aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar pamoja na makundi yaliyomtuma, na kwamba hakijawahi kumpa mamlaka, ridhaa wala maamuzi ya kufungua kesi kwa niaba yake na kwa sasa si kiongozi wa ngazi yoyote ndani ya Chama.
JAB yampa Pascal Mayalla saa 24 kuthibitisha kauli yake dhidi ya Waziri Mkuu
Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari Tanzania (JAB), imempa muda wa masaa 24 mwandishi wa habari Mwandamizi, Paschal Mayala, kuthibitisha kauli yake aliyoitoa kwenye kipindi cha Jambo Asubuhi kinachorushwa na Jambo TV. Kauli hiyo inahusiana na matukio yaliyotokea kwenye ibada ya mazishi ya Marehemu Kadrinali Pengo, ambapo Mayala alisema kuwa Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba, alichukizwa na kitendo cha waombolezaji kuwashangilia viongozi wakuu wastaafu.
Rais Samia: Tumuombe Mungu Marekani na Iran wazungumze misukosuko iishe
Rais wa Samia Suluhu, Machi 3, 2026, amesema tumuombe Mungu, Marekani na Israel zikae Meza moja ya mazungumzo na Iran ili kurejesha utulivu wa dunia na kulinda uchumi wa nchi mbalimbali na dunia irudi katika hali ya kawaida. Kauli hiyo imekuja wakati wa Vita ya Marekani na Israel dhidi ya Iran iliyozua hofu ya kukatika kwa mnyororo wa usambazaji wa nishati duniani.
Meya Kinondoni: Wamiliki wa 'Swimming Pool' tunawatungia Sheria waanze kulipa Kodi
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Songoro Mnyonge, Machi 2, 2025, katika kikao cha Baraza la Madiwani, amependekeza wamiliki wa 'Swimming Pool' watozwe kodi. Mnyonge alisema kuwa hadi sasa Halmashauri haikuwa ikipata mapato yoyote kutokana na maeneo ya kuogelea, licha ya biashara hiyo kuwa kubwa na watu wanalipa fedha nyingi katika maeneo kama Kunduchi.
Mapingamizi dhidi ya Lissu kuunganishwa Kesi ya Mgawanyo wa Mali CHADEMA yatupiliwa mbali
Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dar es Salaam imeyatupilia mbali mapingamizi yaliyowekwa na Said Issa Mohammed na wenzake kupinga Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu kuunganishwa katika Kesi ya Mgawanyo wa Mali inayowakabili Katibu Mkuu wa Chama hicho, John Mnyika na CHADEMA kupitia Bodi ya Wadhamini. Uamuzi huo umetolewa na Jaji Hamidu Mwanga Machi 03, 2026 na msingi huu maombi ya msingi ya Lissu yatasikilizwa Ijumaa Machi 6, 2026 Saa Tatu Asubuhi mbele ya Jaji Hamidu Mwanga.
Rais Samia kwa Rais wa Ghana: Kila kitu kipo salama Tanzania baada ya uchaguzi
Rais Samia amesema Tanzania iko katika hali ya utulivu kisiasa na mambo yote yako chini ya udhibiti baada ya uchaguzi wa Oktoba 2025 huku shughuli za kijamii na kiuchumi zikiendelea kama kawaida. Ameeleza kuwa baada ya matukio ya kisiasa yaliyojitokeza, serikali iliunda Tume ya Uchunguzi ambayo ripoti yake itasaidia kuanzisha Tume ya Maridhiano na baadaye kufanya mapitio ya Katiba Alitoa kauli hiyo Machi 2, 2026 mjini Arusha Rais Samia na kuongeza kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano
Iran yathibitisha kuwa Kiongozi Mkuu, Ayatollah ameuawa
Kiongozi Mkuu wa Iran ameuwawa katika mashambulizi ya Israel na Marekani, vyombo vya habari vya serikali ya Iran vimesema. Serikali ya Iran imetangaza siku 40 za msiba wa taifa baada ya kifo cha Kiongozi Mkuu Khamenei kilichotokea siku ya Jana katika mashambulizi ya Marekani na Israel. Source: Reuters Pia soma LIVE - Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Israel + Marekani vs Iran Ubalozi wa Iran nchini ulivyopost kuhusu hilo.
Ruvuma: Lazaro Komba wa CCM ashinda Ubunge jimbo la Peramiho
Msimamizi wa Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Peramiho Exavery Luyagaza amemtangaza Dkt. Lazaro Kiliani Komba wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa mshindi wa kiti cha Ubunge wa jimbo la Peramiho kwa kupata kura 69002 sawa na ushindi wa asilimia 87 wa kura halali zote zilizopigwa. CCM imevishinda vyama vya siasa 14 katika uchaguzi mdogo wa ubunge uliofanyika Februari 26, kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge Jenister Mhagama, aliyefariki dunia Desemba 11, 2025, jijini Dodoma.
UEFA Champions: Madrid kukutana na Man City. PSG wapangwa na Chelsea hatua ya 16 Bora
Timu vigogo barani Ulaya; Arsenal, Real Madrid na Liverpool ni miongoni mwa klabu zilizojua hatima yao baada ya droo ya hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kupangwa Ijumaa. Real Madrid watakutana tena na Manchester City katika hatua ya mtoano kwa msimu wa tano mfululizo, baada ya kupangwa kukabiliana katika hatua ya 16 bora. Wakati huohuo, mabingwa watetezi Paris Saint-Germain (PSG) watacheza na Chelsea na Arsenal kukutana na Bayer Leverkusen.
Zimbabwe yakataa Msaada wa Marekani wa Dola Milioni 367
Serikali ya Zimbabwe imekataa ufadhili wa Dola Milioni 367 (Tsh. Bilioni 937) kutoka Marekani uliolenga Sekta ya Afya, ikieleza wasiwasi kuhusu athari zake kwa uhuru wa nchi na udhibiti wa Kitaifa. Balozi wa Marekani nchini Zimbabwe, Pamela Tremont amethibitisha kuwa mazungumzo yamevunjika, akisema mamlaka za Zimbabwe zimeihakikishia Washington kuwa ziko tayari kuendelea kupambana na magonjwa kama VVU, Kifua Kikuu (TB) na Malaria bila msaada huo.
Gerson Msigwa: Meli iliyokamatwa na Cocaine El Salvador imesajiliwa Zanzibar
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, akizungumza Februari 26, 2026 na Waandishi wa Habari, amesema meli iliyokamatwa nchini El Salvador ikiwa na tani 6.6 za Cocaine ikiwa na bendera ya Tanzania ilisajiliwa Zanzibar, na kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tayari imechukua hatua ya kuifutia usajili meli hiyo. Ameongeza meli nyingi zinazosajiliwa katika nchi fulani si lazima zitoke au zifanye kazi katika nchi hiyo.
Vatican: Pope Leo XIV kufanya ziara ya kwanza barani Afrika
Papa Leo XIV anatarajiwa kufanya ziara ya siku 10 barani Afrika kuanzia Aprili 13, 2026 safari ambayo itakuwa ya kwanza kwake tangu achaguliwe kuongoza Kanisa Katoliki, na atatembelea Algeria, Cameroon, Angola na Equatorial Guinea. Pia itakuwa mara ya kwanza kwa Papa kutembelea Algeria, taifa lenye Waislamu wengi. Disemba 2025, Papa Leo alitangaza nia yake ya kufanya ziara nchini Algeria, kuzuru maeneo ambayo Mtakatifu Augustine aliishi
Wizara ya Afya: Kuna ongezeko la Mafua makali ya influenza na UVIKO 19 nchini
Wizara ya Afya Tanzania imetoa tahadhari kufuatia ongezeko la wagonjwa wa mafua makali ya Influenza na UVIKO-19 nchini, na kuwataka wananchi kuchukua hatua za kujikinga na maambukizi yanayoweza kusambaa kwa kugusa maeneo au vitu vilivyochafuliwa na majimaji kutoka kwa mgonjwa. Kwa mujibu wa wizara hiyo, takwimu za ufuatiliaji zinaonesha kuwa kila mwaka kuanzia Novemba hadi Aprili kumekuwa na ongezeko la maambukizi hayo nchini na duniani.
El Salvador: Meli yenye bendera ya Tanzania yakamatwa ikiwa na Tani 6.6 za Cocaine
Rais Nayib Bukele ametangaza kuwa Jeshi la Wanamaji limetekeleza operesheni kubwa zaidi ya kukamata kwa Dawa za Kulevya katika historia ya nchi hiyo, ni baada ya kukamata Tani 6.6 za Cocaine zilizokuwa zikisafirishwa baharini na Meli iliyokuwa ikipeperusha bendera ya Tanzania. Kufuatia operesheni hiyo, jumla ya Wanaume 10 walitiwa mbaroni. Watuhumiwa hao wanatoka katika nchi za Colombia, Nicaragua, Panama, na Ecuador, wakiashiria mtandao mpana wa kimataifa uliohusika katika usafirishaji
CHADEMA: Umoja wa Mataifa umezitaka Mamlaka kumuachia huru Lissu na kumlipa fidia
CHADEMA imetoa taarifa kuwa Kikundi Kazi cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kuhusu Uhifadhi Holela (UNWGAD) kupitia Kitengo Kazi, imezitaka mamlaka za Tanzania kumuachia huru Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, pamoja na kumlipa fidia ikidai kuna ukiukwaji mkubwa wa Haki za Binadamu kwa mujibu wa Sheria za Kimataifa tangu kukamatwa kwake Aprili 9, 2025.
Lissu: Wanataka tuzungumze mambo ya Oktoba 29, mtakuwa mmefungulia balaa
Mahakama Kuu imesikiliza hoja za upande wa Jamhuri na Tundu Lissu kuhusu notisi ya ushahidi wa ziada wa shahidi, ACP Amin Mahamba katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti huyo wa CHADEMA, aliyesisitiza kwamba jambo hilo halina msingi kisheria. Lissu ameonya kuwa, kuruhusu notisi hiyo kutafungua “Sanduku la Pandora” la matatizo yasiyoweza kudhibitiwa, hususan kuhusiana na matukio ya Oktoba 29, 2026. Upande wa Jamhuri ikiwa wanataka kurekebisha taarifa, wafuate kifungu cha 294 cha CPA.
JAB yampa onyo kali Zungu kwa kukiuka maadili maudhui ya Uchelewaji wa Ndege ya ATCL
Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imesema mwandishi Kelvin Justine Raphael (Zungu) alikiuka maadili ya uandishi wa habari kupitia maudhui aliyochapisha kuhusu ucheleweshaji wa ndege ya ATCL. Zungu alichapisha maudhui Februari 21, 2026 akilalamikia kucheleweshwa kwa safari ya ndege ya ATCL kwa abiria waliokuwa Mwanza bila taarifa, akidai alipoteza fursa ya kusaini mkataba.
Kenya: Wanaodaiwa kuwa Watanzania wakamatwa wakijaribu kumteka mwanaharakati Mshabaha Hamza
Wanaodaiwa kuwa Watanzania wakamatwa nchini Kenya wakijaribu kumteka mwanaharakati Mshabaha Mshabaha Hamza, katika tukio linalodaiwa kuwa jaribio la kumrudisha kwa nguvu nchini Tanzania. Tukio hilo lilitokea Februari 22, ambapo polisi kutoka vituo vya Lukenya na Kyumbi pamoja na maafisa wa DCI walimuokoa mwanaharakati huyo na kuwakamata washukiwa watatu waliokuwa ndani ya gari lililohusishwa na tukio hilo.
Back
Top Bottom