Featured content

Tanzania yashika Namba 2 kwenye nchi ambazo Uhuru wa Raia umeshuka zaidi Duniani
Tanzania imeshika nafasi ya pili duniani kwa kuporomoka zaidi katika masuala ya haki za kisiasa na uhuru wa raia kwa mwaka 2025, kulingana na ripoti mpya ya shirika la kimataifa la Freedom House. Katika ripoti hiyo inayoitwa Freedom in the World 2026: The Growing Shadow of Autocracy, Tanzania imeshuka kwa alama saba (7) na kuzama zaidi kwenye kundi la nchi "Zisizo Huru" (Not Free) Matokeo haya yanaifanya Tanzania kuwa nchi ya pili duniani kwa kuporomoka zaidi kwa viwango vya uhuru kwa...
Rais Samia: Tume imeshirikisha Majaji kutoka Uganda, Namibia ili kutafuta waliohusika
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo Agosti 07, 2026, amezindua rasmi Tume ya Rais ya Uchunguzi wa Wahusika wa Ghasia na Ukiukwaji wa Sheria katika Matukio ya Ghasia wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Rais Samia amebainisha kuwa ameunda tume hiyo kwa kutumia mamlaka aliyopewa chini ya Sheria ya Tume za Uchunguzi (Sura ya 32). Tume hiyo inakwenda kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini waliohusika, waliotoa...
Kenya yapendekeza kufuta mfumo wa Ufadhili wa Masomo ya Vyuo Vikuu
Serikali imependekeza mageuzi makubwa katika mfumo wa ufadhili wa elimu ya juu kwa kufuta mfumo wa sasa wa ufadhili wa masomo (scholarships na grants) na kuubadilisha na mfumo ambapo wanafunzi wote watakaodahiliwa katika vyuo vikuu na taasisi za umma watapata mikopo badala ya ruzuku. Pendekezo hilo liko mbele ya Bunge kupitia mswada mpya unaolenga kurekebisha mfumo wa ufadhili wa elimu ya juu. Chini ya mfumo unaopendekezwa, wanafunzi watastahili kupata mkopo utakaogharamia ada na gharama...
Polisi: Dereva wa Pikipiki Simiyu alizuiwa kupisha Msafara wa Mwenge lakini alikaidi
Jeshi la Polisi Tanzania, lingependa kutoa ufafanuzi juu ya picha mjongeo inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikionesha Dereva wa Pikipiki akizozana na Askari Polisi huku askari hao wakijitahidi kuyaondoa barabarani magunia ya alizeti aliyokuwa amebeba dereva huyo kwenye pikipiki. Tukio hilo lilitokea Julai 30,2026 Wilaya ya Bariadi Mkoa wa Simiyu. Askari hao walikuwa wanapitisha msafara wa Mwenge wa Uhuru ndipo Dereva huyo wa pikipiki alisimamishwa kwa ajili ya usalama wake na wa watu...
EWURA yashusha bei za mafuta mwezi Agosti, hali ya nauli ikoje mtaani?
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza rasmi bei mpya kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli nchini, zikionyesha nafuu kubwa kwa wananchi kuanzia LEO Jumatano, Tarehe 05 Agosti 2026 saa 6:01 usiku. Katika mabadiliko hayo ya mwezi Agosti, bei za mafuta zimeshuka nchinzima kutokana na mwenendo wa bei katika soko la dunia: Petroli: Imeshuka kwa TZS 92 kwa kila lita. Dizeli: Imeshuka kwa TZS 204 kwa kila lita. Mafuta ya Taa: Yameshuka kwa TZS 440 kwa kila lita.
Kesi ya Ugaidi ya Mhadhiri wa UDOM yaahirishwa hadi Agosti 19, 2026
Shauri la ugaidi linalomkabili mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Dk. Melikisedeki Kaijage, limeahirishwa hadi Agosti 19, 2026 baada ya kutajwa leo, Agosti 5, 2026, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma. Shauri hilo lilitajwa mbele ya Hakimu Mfawidhi, Zabibu Mpangule, ambapo ilielezwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kulisikiliza. Badala yake, jukumu lake ni kuhakikisha taratibu za awali, ikiwemo ukamilishaji wa faili la shauri, zinakamilika kabla ya kesi kupelekwa katika mahakamani
Dkt. Koshuma: Kukaanga chapati kwa vipande vya Godoro kunaweza kuingiza kemikali kwenye chakula
Daktari mstaafu wa magonjwa ya ndani, aliyewahi kufanya kazi katika kitu cha afya kikubwa mkoani Dar es Salaam, Kituo cha Afya Sinza Dar es Salaam Dk. Phoibe Koshuma, anasema magodoro ya kisasa yanatengenezwa kwa povu la anachokitaja kwa jina ‘polyurethane’ ambayo ni aina ya plastiki laini yenye chembe nyingi za hewa ndani yake.
Tozo za Daraja la Mwalimu Nyerere (Kigamboni) zitaendelea hadi mwaka 2046
Daraja la Mwalimu Nyerere halikujengwa kwa mkopo wa kawaida wa Serikali. Lilijengwa kupitia mkataba wa aina ya DBFOT, ambapo Serikali ilichangia asilimia 40 ya gharama za mradi na NSSF asilimia 60. Serikali ilikubaliana kuirejeshea NSSF sehemu yake ya gharama, kwa kuendesha daraja la Mwalimu Nyerere na kukusanya tozo kwa miaka 30 ili kurejesha uwekezaji wake kabla ya kukabidhi daraja kwa Serikali baada ya kurejesha gharama.
Rais Samia: Misaada na Mikopo nafuu tuliyoizoea inaendelea kuondoka, tukaze Buti
Rais Samia Suluhu, amewataka Watanzania na viongozi kukaza buti na kufunga mikanda kutokana na mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa yanayoendelea duniani, amesema hayo Agosti 3, 2026 katika uzindizi wa Nyenzo za Utekelezaji wa Dira 2050 pamoja na kushiriki katika Mkutano wa Mazungumzo Maalum na Sekta Binafsi kuhusu Utekelezaji wa Dira 2050, Agosti 03, 2026 ''Misaada na mikopo tuliyo izoea inaendelea kuondoka tukaze buti "
Mnyika: Kauli ya Rais kuhusu 'Mwenzetu Kutafakari' haituhusu CHADEMA
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo John Mnyika amesema kuwa chama hicho na Mwenyekiti wake Tundu Lissu mpaka hivi sasa hakijafanya mazungumzo yoyote na serikali huku akiipinga kauli iliyotolewa na Rais Samia Julai 30, 2026. Kupitia mkutano wake na waandishi wa habari leo Agosti 3, 2026 ameeleza kauli ya Rais Samia alipokuwa akizungumza na vyama vya siasa kuwa yupo mwenzao mmoja ambaye anaendelea kutafakari masharti haikihusu CHADEMA.
Mkuu wa Polisi na Afisa wa Ulinzi wa zamani Sri Lanka wahukumiwa kifo kwa mashambulizi ya 2019
Mahakama Maalum (Permanent Trial-at-Bar) imewakuta na hatia aliyekuwa Mkuu wa Polisi nchini Sri Lanka, Pujith Jayasundara, na aliyekuwa Katibu wa Wizara ya Ulinzi, Hemasiri Fernando, na kuwahukumu adhabu ya kifo kwa kushindwa kuzuia mashambulizi ya mabomu ya Pasaka 2019 yaliyosababisha vifo vya Watu 279.
Ado: Ukifunga Mlango wa Demokrasia, unafungua mlango wa machafuko
Mbunge wa Tunduru Kaskazini, Ado Shaibu, amesema maridhiano ya kisiasa hayawezi kufanikiwa bila kuwepo kwa ukweli na uwajibikaji kuhusu matukio ya kisiasa yaliyotokea nchini. Amesema hatua ya kwanza katika mchakato wa maridhiano ni kuweka wazi ukweli kuhusu matukio yaliyojitokeza kabla, wakati na baada ya uchaguzi wa mwaka 2025 akidai kuwa kipindi hicho kilizalisha wafungwa wa kisiasa, watu waliotekwa na wengine kuuawa.
Mrindoko: Polisi wanakukamata wanasema wameagizwa, ukiuliza kosa, wanajibu "Utajulia mbele"
Joseph Mrindoko wa Wachokonozi amesema kuna changamoto katika utawala wa sheria, utendaji wa baadhi ya watumishi wa serikali na uelewa wa wananchi kuhusu haki zao za kisheria. Amesema baadhi ya Watanzania huamini kuwa mtu anapohojiwa au kushikiliwa na polisi tayari ana hatia, badala ya kutambua kuwa anaweza kuwa anachunguzwa au anatuhumiwa bila hatia kuthibitishwa.
Serikali ya Ghana yaongeza Muhula wa rais na wabunge kutoka miaka 4 hadi 5
Serikali ya Ghana imekubali pendekezo la kuongeza muda wa muhula wa urais kutoka miaka minne hadi mitano, Taarifa iliyotolewa na Waziri wa Sheria wa nchi hiyo Dr. Dominic Akuritinga Ayine Rais John Dramani Mahama aliunda kamati mwaka 2025 kupitia upya Katiba ya mwaka 1992 na kutoa mapendekezo mbalimbali, ambapo baadhi yake yamekubaliwa na serikali. Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Sheria, Dominic Ayine, amesema pia muda wa Bunge utaongezwa ili uendane na muhula mpya wa rais...
Mahakama ya Rufaa yatupilia mbali maombi ya DPP ya kuongeza ushahidi katika Kesi ya Tundu Lissu
Leo, tarehe 30 Julai 2026, Mahakama ya Rufaa ya Tanzania imetoa uamuzi muhimu katika shauri lililomhusisha Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) dhidi ya Tundu Antiphas Lissu. DPP alikuwa amewasilisha maombi ya kupitia upya uamuzi wa Mahakama Kuu uliokataa jaribio la upande wa mashtaka la kuwasilisha ushahidi mpya. Kiini cha Mzozo Upande wa mashtaka ulitaka kuwasilisha ushahidi wa ziada kupitia shahidi wao, ACP Amini Mahamba, ambaye alikuwa kiongozi wa timu ya uchunguzi wa matukio yaliyohusiana...
Rais wa TFF, Karia: Timu isipoingia ‘Dressing Room’ itakatwa Pointi Tano
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia, amesema Shirikisho hilo limepitisha maboresho makubwa ya kanuni za mpira wa miguu kuelekea msimu mpya, ikihusisha kuongeza adhabu za kifedha na makato ya pointi kwa klabu zitakazokiuka taratibu. Wallace Karia, ameeleza kuwa shirikisho hilo limeamua kununua vifaa maalumu vya kisasa vya kubaini gesi zenye madhara (harmful gases) katika vyumba vya kubadilishia nguo wachezaji (changing rooms) ili kumaliza migogoro na tuhuma za...
Hivi ndivyo mfanyabiashara alivyotapeliwa kwa stakabadhi ya kughushi. Je, unajilindaje?
Mmoja ya wafanyabiashara wanaopokea malipo kwa njia za kidigitali amepoteza takribani Tsh. Milioni 47 baada ya kuingizwa kwenye mtego wa matapeli wanaotumia Akili Mnemba (AI) pamoja na programu za kughushi risiti za malipo. Kama wewe ni mfanyabiashara unayepokea malipo kupitia Lipa Namba, benki au mtandao wa simu, kuwa makini sana usije ukapigwa.
KENYA: Mathare North gizani kwa siku kadhaa; Wakazi walalamika
Wakazi wa sehemu ya Mathare North wameendelea kulalamikia kukosekana kwa umeme tangu Ijumaa iliyopita, wakisema hali hiyo imeathiri maisha yao ya kila siku huku juhudi za kurejesha huduma zikionekana kuwa za polepole. Kwa mujibu wa wakazi, kukosekana kwa umeme kumeathiri biashara ndogo ndogo, usalama wa usiku, uhifadhi wa vyakula na uwezo wa wanafunzi kusoma nyumbani. Wanasema wamekuwa wakitoa taarifa kuhusu hitilafu hiyo lakini bado hawajaona hatua za haraka za kurejesha huduma. Wakazi...
DCP Misime: Wanaotaka mikutano watoe taarifa Polisi, hali ya usalama ni shwari
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, DCP David Misime, amesema hali ya usalama nchini kwa sasa ni shwari, hivyo Jeshi litaendelea kupokea taarifa za nia ya kufanya mikutano ya hadhara na vikao kutoka kwa vyama vya siasa na wadau wengine kwa mujibu wa sheria. Soma: Waziri Katambi apiga marufuku mikutano ya siasa kwa vyama vyote Misime amesema katika kipindi ambacho kulikuwa na viashiria vya baadhi ya watu kupanga vitendo vya kihalifu, Jeshi la Polisi lilizishauri taasisi na vyama...
Katambi: Hatuna ugaidi Tanzania, Vinaweza kuwepo viashiria
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amesema Tanzania haina ugaidi, huku akisisitiza kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria wala anayepaswa kupewa kinga kutokana na cheo, taaluma, dini au hadhi yake katika jamii. Amesema vyombo vya dola vinaendelea kuchukua hatua dhidi ya yeyote anayehusika na vitendo vinavyokiuka sheria bila ubaguzi.
Back
Top Bottom