Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema ‘hajali’ kama Iran itashiriki katika michuano ya Kombe la Dunia la 2026, ambalo litaandaliwa kwa ushirikiano wa mataifa matatu; Marekani, Mexico na Canada itakayoanza Juni 11 hadi Julai 19, 2026.
Akizungumza Machi 3, 2026 na tovuti ya Politico, Trump alisema anaona Iran ni nchi iliyoshindwa vibaya. Hata hivyo, kiongozi wa shirikisho la soka la Iran, Mehdi Taj, amedokeza mashaka yake kuhusu uwezekano wa kushiriki mashindano hayo.