Makamu wa Rais, Emmanuel Nchimbi, amewaomba viongozi wa dini kuendelea kumuombea Rais Samia dhidi ya watu wabaya, ili wasipate nafasi ya kumsogelea au kuingia Ikulu. Pia, kupitia maombi hayo, Rais aweze kutambua wezi, waongo, wafitini, watu wasio waaminifu, na wale wenye mawazo ya kumwaga damu au kuleta madhara.
Amesema hayo Februari 6, 2026 wakati wa hafla ya Usimikaji na Uzinduzi wa Uongozi wa Awamu ya Tano wa The Council Of Pentecostal Churches Of Tanzania (CPCT) iliyofanyika Ukumbi wa Agape