Featured content

Senegal wapokwa ubingwa wa AFCON 2025 na CAF, apewa Morocco
Morocco imetawazwa kuwa mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika la 2025 baada ya uamuzi wa CAF siku ya Jumanne kueleza kuwa ushindi wa bao 1-0 wa Senegal kwenye fainali umebatilishwa. Senegal ilishinda mechi hiyo kwa bao la Pape Gueye katika muda wa nyongeza, ushindi ulipatikana katika mazingira yenye utata baada ya wachezaji wa Senegal kutoka nje ya uwanja wakigoma wakati wa dakika 90 za kawaida za mchezo.
Mafwele, wengine 42 kutoa ushahidi kesi ya askari wanaodaiwa kughushi vibali vya silaha
Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Faustine Mafwele ni miongoni mwa Mashahidi 43 wanaotarajiwa kutoa ushahidi katika kesi ya askari wanaotuhumiwa kughushi vibali vya kumiliki silaha. Kesi hiyo inawakabili Watu tisa, wakiwemo maofisa sita wa Jeshi la Polisi, inasikilizwa na Hakimu Mwandamizi, Geofrey Mhini, na inatarajia kuanza kusikilizwa Aprili 2026.
Je, uwanja huu ulitumika Gabon kwenye AFCON 2017 na sasa umetelekezwa? Uhalisia upoje?
Wadau mbalimbali wametaka kujua uhalisia wa picha zinazosambaa mitandaoni zikionyesha hali ya viwanja vya michezo vilivyotumika katika mashindano ya AFCON nchini Gabon mwaka 2017 vikiwa katika hali mbaya ya uharibifu na kutelekezwa. Stade Omar Bongo ni moja kati ya viwanja vilivyopangwa kutumika katika AFCON 2017 lakini haukuweza kutumika kwa sababu hadi kufikia mashindano kuanza haukuwa umekamilika, hivyo haukukidhi vigezo.
Mkurugenzi DUWASA: Kama umechimba kisima tumia na familia yako usiwape wengine
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dodoma, Mhandisi Aron Joseph, amesema Watu wanaochimba visima vya maji wanapaswa kuvitumia na familia zao pekee na wasitoe huduma kwa Wananchi wengine. Kauli hiyo ameitoa Machi 16, 2026, kupitia Clouds TV kwenye kipindi cha Clouds 360 akidai sababu ya hatua hiyo ni maji ya chini ya ardhi kubadilika sifa zake kila siku, na wengi kutopima ubora wake kabla ya kuyatoa kwa wengine ambapo yanaweza kuathiri mtaa mzima.
Mahakama yatupilia mbali shauri la TLS  kupinga amri ya IGP kuzuia watu kutoka nje Oktoba 29, 2025
Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Dar, imetupilia mbali shauri la kikatiba lililofunguliwa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) dhidi ya Inspekta Jenerali wa Polisi kupinga amri ya kutotoka nje iliyotolewa Oktoba 29, 2025. Mahakama imebaini dosari za kisheria katika hati ya kiapo ya Rais wa TLS, Boniface Mwabukusi. TLS ilidai amri hiyo ilikiuka Katiba ya mwaka 1977 na haki za wananchi, na kuomba kuundwa kwa tume huru ya kuchunguza vurugu zilizosababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali
Sahara Media Group yafilisiwa na kufungwa rasmi kwa kushindwa kulipa madeni
Mahakama Kuu, Divisheni ya Biashara, imeamuru kufilisiwa na kufungwa rasmi kwa Sahara Media Group Limited baada ya kubainika kuwa kampuni hiyo imepata ukata wa fedha, kushindwa kujiendesha pamoja na kulipa madeni. Uamuzi huo umetolewa na Jaji Dkt. Mwajuma Kadilu kufuatia ombi la kampuni kutaka kufilisiwa baada ya ripoti ya Afisa Mkuu Steven Diallo kuonesha kampuni imepata hasara ya zaidi ya Tsh. Bilioni 3.9 mwaka 2023 na kuwa na deni la kodi la takribani Tsh. Milioni 97.7 kwa TRA.
TPA yasogeza hadi Julai 1, 2026 kuanza kwa Ada ya Uendelezaji wa Miundombinu ya Bandari
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imetoa wito kwa Wadau wa bandari kukamilisha masharti na marekebisho ya mikataba waliyonayo na Wateja wao wa ndani na nje ya nchi ndani ya muda uliobaki kabla ya kuanza kutumika kwa Ada ya Uendelezaji wa Miundombinu ya Bandari (PID), Julai 1, 2026 Nyongeza hiyo inalenga kuwapa nafasi wateja na Wadau ikiwemo kampuni za usafirishaji wa meli, mawakala wa forodha na usafirishaji, wasafirishaji wa mizigo, waagizaji, wauzaji nje na ndani ya nchi.
Mdau: Fao la Kujitoa limerudishwa kisheria, kwanini NSSF hamtangazi?
Mdau amehoji kuhusu utekelezaji wa mabadiliko ya Sheria ya Mfumo wa Hifadhi ya Jamii upande wa Fao la Kukosa Ajira baada ya kurejeshwa kwa Fao la Kujitoa Desemba 2025. Anasema NSSF haijaeleza taarifa ya mabadiliko hayo kwa umma, badala yake wanaendelea kupewa mafao yao kwa mfumo wa asilimia 33, jambo linaloathiri uchumi wao na kuzua maswali kuhusu uwazi wa utekelezaji wake.
Mwigulu: Muuguzi aliyemfanyia mgonjwa upasuaji  nyumbani kwake afukuzwe kazi
Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba ameagiza mamlaka husika kumfukuza kazi Muuguzi wa Mkoa wa Tabora aliyedaiwa kumfanyia mgonjwa upasuaji wa Tumbo nyumbani, kwenye Kochi kwake badala ya hospitalini. Akizungumza Machi 4, 2026, amesema mbali na kufukuzwa kazi, muuguzi huyo pia afikishwe kwenye vyombo vya sheria kwa hatua zaidi za kisheria, pamoja na kufutiwa leseni yake ya uuguzi.
Mwigulu: Wanaokaa vikao kwamba huyu tumfanyeje, niwaambie hamnifanyi kitu
Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba, amewaambia baadhi ya Watendaji wanaodaiwa kukaa vikao kupanga njama dhidi yake, kuwa hatishwi na vitisho vya aina yoyote. Amedai maisha yake yamejengwa katika mazingira ya kuhangaika tangu utotoni, akianzia kuchunga Ndama wa Baba yake, na hata kukutana na Wanyama wakali kama Simba na Chui ambao hawakumfanya chochote
Joseph Butiku: Tukubali tunaye Rais, ameunda Tume itusaidie kujua yaliyotokea
Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku Machi 4, 2026 wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Maridhiano (Maridhiano Day) yaliyofanyika Wilayani Ilemela amewataka Watanzania kukubaliana na uhalisia kwamba nchi tayari ina Rais aliye tayari kwa maridhiano. Akizungumza katika hafla hiyo, amesema kuwa tume iliyoundwa na Rais Samia imeongezewa muda hadi mwezi Aprili, na kuwataka wananchi kuwa na subira ili iwasaidie kujua yaliyotokea Oktoba 29, 2025.
Trump: Sijali kama Iran itashiriki Kombe la Dunia 2026
Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema ‘hajali’ kama Iran itashiriki katika michuano ya Kombe la Dunia la 2026, ambalo litaandaliwa kwa ushirikiano wa mataifa matatu; Marekani, Mexico na Canada itakayoanza Juni 11 hadi Julai 19, 2026. Akizungumza Machi 3, 2026 na tovuti ya Politico, Trump alisema anaona Iran ni nchi iliyoshindwa vibaya. Hata hivyo, kiongozi wa shirikisho la soka la Iran, Mehdi Taj, amedokeza mashaka yake kuhusu uwezekano wa kushiriki mashindano hayo.
Possi: Tanzania inapinga madai ya Washirika wa Kimataifa kuhusu Oktoba 29, wamefumbia macho chanzo
Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa (UN), Dkt. Abdallah Possi, katika Kikao cha 61 cha Baraza la Haki za Binadamu, amejibu kauli za Jumuiya ya Ulaya, Uingereza, Uswisi, Sweden, Ireland, Ubelgiji na Norway pamoja na Human Rights Watch na Amnesty International kuhusu matukio ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania. Akizungumza mjini Geneva Machi 2, 2026, Possi alisema Serikali imesikitishwa na kauli hizo alizodai zimechagua matukio bila kuzingatia muktadha.
SI KWELI | Yanga yamtimua kocha Pedro na mikoba yake kurithiwa na Patrick Mabedi
Kuanzia Machi 3, 2026 kumekuwa na barua/taarifa kwa Umma yenye utambulisho wa klabu ya Yanga ikieleza kuwa klabu hiyo imemtimua kocha wake Mkuu Pedro Goncalves na hivyo klabu hiyo itaongozwa kwa muda na kocha msaidizi Patrick Mabedi. Baada ya ufuatiliaji wa kina imebainika kuwa taarifa hiyo si ya kweli.
Ujumbe wa sauti wa Vijana wa Hamasa - CCM kwenye Vituo vya SGR usitishwe, unagawa abiria kiitikadi
Mdau wa JamiiForums.com ametaka wimbo wa vijana wa hamasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unaochezwa kwenye vituo vya SGR usitishwe mara moja kwa kuwa Treni hiyo inatumika na Watu wenye kiitikadi tofauti.
CHADEMA Zanzibar: Hatujamtuma Said kukishtaki chama, ni kesi yake na makundi yaliyomtuma
CHADEMA Zanzibar, kimetoa taarifa ya kukanusha madai yaliyotolewa na Said Issa Mohamed kuhusu kufungua kesi kwa niaba ya chama juu ya mgawanyo wa mali na kujitambulisha kama kiongozi wa chama hicho. Taarifa imeeleza kesi hiyo siyo ya Chama bali ni ya Said Issa Mohamed aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar pamoja na makundi yaliyomtuma, na kwamba hakijawahi kumpa mamlaka, ridhaa wala maamuzi ya kufungua kesi kwa niaba yake na kwa sasa si kiongozi wa ngazi yoyote ndani ya Chama.
JAB yampa Pascal Mayalla saa 24 kuthibitisha kauli yake dhidi ya Waziri Mkuu
Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari Tanzania (JAB), imempa muda wa masaa 24 mwandishi wa habari Mwandamizi, Paschal Mayala, kuthibitisha kauli yake aliyoitoa kwenye kipindi cha Jambo Asubuhi kinachorushwa na Jambo TV. Kauli hiyo inahusiana na matukio yaliyotokea kwenye ibada ya mazishi ya Marehemu Kadrinali Pengo, ambapo Mayala alisema kuwa Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba, alichukizwa na kitendo cha waombolezaji kuwashangilia viongozi wakuu wastaafu.
Rais Samia: Tumuombe Mungu Marekani na Iran wazungumze misukosuko iishe
Rais wa Samia Suluhu, Machi 3, 2026, amesema tumuombe Mungu, Marekani na Israel zikae Meza moja ya mazungumzo na Iran ili kurejesha utulivu wa dunia na kulinda uchumi wa nchi mbalimbali na dunia irudi katika hali ya kawaida. Kauli hiyo imekuja wakati wa Vita ya Marekani na Israel dhidi ya Iran iliyozua hofu ya kukatika kwa mnyororo wa usambazaji wa nishati duniani.
Meya Kinondoni: Wamiliki wa 'Swimming Pool' tunawatungia Sheria waanze kulipa Kodi
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Songoro Mnyonge, Machi 2, 2025, katika kikao cha Baraza la Madiwani, amependekeza wamiliki wa 'Swimming Pool' watozwe kodi. Mnyonge alisema kuwa hadi sasa Halmashauri haikuwa ikipata mapato yoyote kutokana na maeneo ya kuogelea, licha ya biashara hiyo kuwa kubwa na watu wanalipa fedha nyingi katika maeneo kama Kunduchi.
Mapingamizi dhidi ya Lissu kuunganishwa Kesi ya Mgawanyo wa Mali CHADEMA yatupiliwa mbali
Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dar es Salaam imeyatupilia mbali mapingamizi yaliyowekwa na Said Issa Mohammed na wenzake kupinga Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu kuunganishwa katika Kesi ya Mgawanyo wa Mali inayowakabili Katibu Mkuu wa Chama hicho, John Mnyika na CHADEMA kupitia Bodi ya Wadhamini. Uamuzi huo umetolewa na Jaji Hamidu Mwanga Machi 03, 2026 na msingi huu maombi ya msingi ya Lissu yatasikilizwa Ijumaa Machi 6, 2026 Saa Tatu Asubuhi mbele ya Jaji Hamidu Mwanga.
Back
Top Bottom