Featured content

Polisi yakanusha Kikundi cha ‘TFF’ kufanya uhalifu, yaonya 'Wachochezi' wa Mtandaoni
Jeshi la Polisi limekanusha taarifa zinazosambazwa na kikundi kinachojiita Tanzania Freedom Fighters (TFF) kikidai kufanya mazoezi porini na kutenda uhalifu. Polisi imebainisha kuwa madai hayo si ya kweli na yanatolewa na watu waliopo nje ya mipaka ya nchi kwa lengo la kusababisha taharuki na kuchochea chuki miongoni mwa Watanzania. Jeshi hilo limesisitiza kuwa linaendelea kuwafuatilia na kuwatia mbaroni watu wanaotumia mitandao ya kijamii kuhamasisha vurugu na uhalifu na uhalifu wa kijinai.
Muda wa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Oktoba 29 Waongezwa Hadi Aprili 2026
Mamlaka ya Uteuzi imeongeza muda wa siku 42 kwa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani ya Uchaguzi wa 2025, ikisogeza ukomo wa kazi hiyo hadi Aprili 3, 2026. Ongezeko hilo limetokana na uhitaji wa kufanya uchambuzi wa kina wa kisayansi wa taarifa zilizokusanywa na kuziba mapengo ya kishahidi ili kuhakikisha ripoti inakamilika kwa usahihi. Awali, Tume hiyo inayoongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Chande, ilitarajiwa kukamilisha majukumu yake ndani ya siku 90, yaani Februari 2026.
TABORA: Mahakama Kuu yaupiga chini utaratibu wa “uwakili wa viti maalum”
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tabora, Februari 17, 2026 kupitia kesi ya Amina Mwaluko dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imebatilisha utaratibu wa baadhi ya Watu wakiwemo Maafisa wa Mahakama, na Maafisa Sheria wa Sekta za Umma kupewa Uwakili bila kuhitimu Astashahada katika Shule ya Sheria kwa Vitendo (Law School of Tanzania) wanaofahamika kwa jina la Mawakili wa Viti Maalum Katika Uamuzi huo Mahakama Kuu imeeleza kwamba Sheria iliyoruhusu utaratibu huo ni batili, zipo kinyume na Katiba
Bwege kuhamia CHADEMA, asema ACT Wazalendo si rafiki sahihi kwake
Mbunge wa zamani wa Kilwa Kusini, Selemani Bungara maarufu kama “Bwege”, ametangaza kujivua uanachama wa chama cha ACT Wazalendo kuanzia Februari 18, 2026. Kupitia taarifa yake, amesema uamuzi huo umeanza rasmi tangu tarehe hiyo. Bungara amesema ACT Wazalendo si rafiki sahihi kwake kama alivyodhani awali, akieleza kuwa matarajio yake yalikuwa tofauti na alivyokuta.
Afrika Kusini: Mtoto wa Robert Mugabe akamatwa kwa tuhuma za kumfyatulia mlinzi risasi
Jeshi la Polisi nchini Afrika Kusini limemkamata Bellarmine Mugabe, mtoto wa kiume wa aliyekuwa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe Jijini Johannesburg kufuatia tukio la kumpiga risasi mlinzi katika makazi yake yaliyopo Hyde Park. Mamlaka nchini humo zimeeleza kuwa uchunguzi wa kina unaendelea kufanyika, ikidaiwa majeruhi yupo katika hali mbaya, huku tukio hilo likiwa linachunguzwa kama kesi ya jaribio la mauaji.
Kesi ya Lissu: Shahidi wa Siri (P7) ajibu maelezo yake “hayapo” polisi alipoulizwa na Lissu mahakamani
Katika kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, Shahidi wa 11 wa Kificho wa Jamhuri (P7) alikiri mbele ya mahakama kuwa maelezo aliyoulizwa mahakamani hapo na Lissu “hayapo” kwenye maelezo yake ya Polisi. Shahidi alijibu mara kwa mara “hayapo” au “sijataja” baada ya Lissu kumhoji kuhusu matukio ya kuhusu CHADEMA kuzuia uchaguzi, kuhusu Tume ya Uchaguzi na uchaguzi wa mwaka 2024 na tuhuma za wizi wa kura.
TANZIA: Kardinali Pengo afariki Dunia
Pumzika kwa amani mwadhama Kardinali Pengo. Tuonane mbinguni asubuhi iliyo njema. ===== YAH: TANGAZO LA KIFO Ninayo masikitiko makubwa kuwatangazieni kwamba leo tarehe 19/02/2026 saa 04:00 usiku huu mpendwa baba yetu Mwadhama Polycarp Cardinal Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele akiwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam. Taarifa za mazishi zitawajia mara baada ya mipango kukamilika. Tumwombee...
Mahakama: Kifungu kinachoruhusu mashahidi wa kesi wa kificho ni batili na kinyume na Katiba
Mahakama Kuu Mwanza imesema Kifungu cha 194 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kinachoruhusu kuficha mashahidi ni batili na kinyume na Katiba. Serikali imepewa miezi 12 kurekebisha Sheria hiyo ili iendane na Katiba kabla ya kuondolewa au kubadilishwa rasmi. Uamuzi huo umetolewa Februari 16, 2026 katika Shauri la Kikatiba Namba 22482/2025 kati ya Godfrey Mjuni Martin Basasingohe dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Mashtaka
Rasmi: Gamondi asaini mkataba wa miaka miwili kuinoa Taifa Stars
Kocha Miguel Gamondi Februari 16, 2026 amesaini mkataba rasmi wa miaka miwili kuinoa timu ya Taifa ya soka ya Tanzania (Taifa Stars). Gamondi ataiongoza Taifa Stars kuelekea michuano ya AFCON 2027, itakayofanyika katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda, akiindeleza mafanikio aliyoyapata katika AFCON 2025, ambapo timu ya taifa ya Tanzania ilitinga hatua ya 16 bora.
AFCON 2027: CAF yathibitisha Tanzania, Uganda na Kenya kuandaa michuano hiyo
Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe amesema Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) ijayo, itafanyika Mwaka 2027 nchini Kenya, Tanzania na Uganda kama ilivyopangwa na kwamba siyo Mwaka 2028 kama baadhi tetesi zinavyodai. Akizungumza Februari 13, 2027 kwenye Kikao cha Kamati ya Utendaji ya CAF kilichofanyika jijini Dar es Salaam, Motsepe amesema “Madai kuwa ninaondoa AFCON kwa sababu nchi zetu tatu hazijawa tayari hayana msingi wowote.”
Songwe: Mwenyekiti wa Umoja wa Madereva wa Malori, Godlove Materu aachiwa kwa dhamana
Mwenyekiti wa Taasisi ya Taifa ya Taaluma ya Madereva Tanzania (TATAMATA), Godlove Materu, ameachiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kukamatwa Februari 5, 2026, kufuatia kudhaminiwa na mke wake Februari 9, 2026. Materu alidaiwa kukamatwa Februari 5, 2026 na watu wasiojulikana, na Februari 8 viongozi wa TATAMATA waliwapa Polisi siku mbili awe amepatikana, usiku huohuo Jeshi la Polisi Songwe lilikiri kumshikilia kwa tuhuma za kijinai.
Kesi ya Lissu | Tundu Lissu: Mimi sijala
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, anayekabiliwa na kesi ya uhaini, aliahirishiwa shauri lake baada ya kuiambia Mahakama kuwa 'hajala', hali iliyowafanya baadhi ya wafuasi wake kulia na wengine kupoteza fahamu. Jaji Dastan Ndunguru akaamua kuahirisha kesi hiyo.
AFCON 2027: CAF huenda ikaahirisha mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika
Gazeti la The Guardian la Uingereza limeripoti kwamba mashindano hayo yanaweza kusogezwa hadi mwaka 2028, likitoa sababu mbili kuu: nchi mwenyeji Kenya, Uganda na Tanzania bado hazijawa tayari kikamilifu kuandaa mashindano hayo makubwa na ratiba ya uchaguzi wa Kenya mwaka 2027, ambayo huenda ikaleta mazingira yasiyo tulivu kwa maandalizi na usalama wa mashindano. Kwa sasa, timu ya ukaguzi kutoka Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) iko nchini Tanzania
Zambia: Mahakama yataifisha Magari 79, mali 23 za Mtoto wa Rais wa zamani, Edgar Lungu
Mahakama ya Makosa ya Uhujumu Uchumi na Fedha nchini Zambia imetaifisha magari 79 na mali 23 zisizohamishika zinazomilikiwa na Dalitso Lungu, Mtoto wa Rais wa zamani wa Nchi hiyo, Edgar Lungu, baada ya kuamua kuwa mali hizo zilitokana na uhalifu. Uamuzi huo ulitokana na maombi yaliyowasilishwa chini ya Kifungu cha 29 cha Sheria ya Kutaifisha Mapato ya Uhalifu Na. 19 ya Mwaka 2010, yaliyolenga kutaifishwa kwa mali za Dalitso bila kuwepo hukumu ya jinai.
Gerson Msigwa: Maridhiano ni jambo la hiari sio kulazimishwa
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, akizungumza Februari 10, 2026 katika mahojiano na BBC Swahili, amesema endapo kutakuwa na wadau watakaokataa kushiriki kwenye maridhiano mara mchakato huo utakapoanza, hawatalazimishwa kwani ushiriki ni wa hiari. Ameongeza kuwa anayekataa kutambua uchaguzi anapaswa kuwa na hoja za msingi, na kwamba uchaguzi ulifanyika kwa mujibu wa sheria, kwa misingi ya uhuru na haki; walioshinda wameshinda na walioshindwa kura hazikutosha.
Tanzania yaomba msaada China kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya AFCON  2027
Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Mwaka Mpya wa Kichina yaliyofanyika Februari 6, 2026 katika Ubalozi wa China, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, James Millya aliiomba Serikali ya China kuisaidia Tanzania kujenga miundombinu ya kisasa kwa ajili ya mashindano ya AFCON yanayotarajiwa kufanyika Mwaka 2027. Tanzania inajenga viwanja vitatu kwa ajili ya maandalizi ya michuano hiyo, ikiwemo Kiwanja cha Fumba - Zanzibar, Samia Suluhu kilichopo Mkoani Arusha, pamoja na Uwanja wa Dodoma.
Nchimbi: Tumuombee Rais Samia, Mungu afunge mageti ya Ikulu dhidi ya Watu wabaya
Makamu wa Rais, Emmanuel Nchimbi, amewaomba viongozi wa dini kuendelea kumuombea Rais Samia dhidi ya watu wabaya, ili wasipate nafasi ya kumsogelea au kuingia Ikulu. Pia, kupitia maombi hayo, Rais aweze kutambua wezi, waongo, wafitini, watu wasio waaminifu, na wale wenye mawazo ya kumwaga damu au kuleta madhara. Amesema hayo Februari 6, 2026 wakati wa hafla ya Usimikaji na Uzinduzi wa Uongozi wa Awamu ya Tano wa The Council Of Pentecostal Churches Of Tanzania (CPCT) iliyofanyika Ukumbi wa Agape
Jamhuri ya Kongo: Rais Sassou (82) kugombea tena urais baada ya miaka 42 madarakani
Akiwa na miaka 82, Rais wa Jamhuri ya Kongo, Sassou N’guesso ametangaza kugombea tena urais katika uchaguzi wa Machi 15, 2026, baada ya kuwa madarakani kwa jumla ya miaka 42. Aliingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 1979 hadi 1992, kisha akarudi mwaka 1997 baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe. Tangu wakati huo, ameshinda chaguzi nne mfululizo, huku marekebisho ya katiba mwaka 2015 yakimruhusu kuendelea kugombea bila kikomo cha umri au vipindi vya urais.
Tunduma: Polisi wakiri kumkamata Dereva wa Malori. Yadaiwa alipanga kufanya uhalifu
Baada ya Chama cha Madereva wa Malori kutangaza mpango wa kufanya mgomo iwapo mwenzao asingepatikana ndani ya siku mbili, Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limetoa ufafanuzi likikanusha taarifa zinazosambazwa mitandaoni kuwa Godlove Materu hajulikani alipo baada ya kukiri kumshikilia. Polisi wamesema Materu, mkazi wa Tunduma, alikamatwa kwa tuhuma za kijinai, wakiongeza kuwa alipanga kufanya uhalifu katika maeneo mbalimbali Tunduma. Wamesema uchunguzi umekamilika na hatua za kisheria zinaendelea
Nape: Vyombo vya Dola visipojali UTU, CCM itang'oka!
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye ametahadharisha kuwa bila kusimamia utu, Chama cha Mapinduzi (CCM) inaweza kuondoka madarakani hivyo akaonya wanachama ndani ya chama hicho wasione aibu kusimamia utu. Nape aliyewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ametoa kauli hiyo bungeni leo Alhamisi Februari 5,2026 wakati akichangia Mapendekezo ya Mpango wa Serikali uliowasilishwa mwanzoni mwa wiki na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na...
Back
Top Bottom