Featured content

KOMBE LA DUNIA: Kipa mkongwe Vozinha ang'ara Cape Verde ikizuia Uhispania kufunga bao
Kipa mkongwe wa Cape Verde, Vozinha (40), ameokoa michomo 7, ikiwemo 6 ya ndani ya boksi, na kuwa shujaa kwa kuisaidia timu yake kutoka sare ya 0-0 dhidi ya mabingwa wa Ulaya, Uhispania, katika mchezo wa Kundi H wa Kombe la Dunia 2026. Matokeo hayo yameifanya Cape Verde kupata pointi yake ya kwanza kabisa katika historia ya kushiriki Kombe la Dunia.
Zungu: Kwanini Makampuni ya Simu hayauzi Hisa kwa Umma?, TCRA na CMSA wahojiwe!
Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu (Mb), Juni 15, 2026, ameeleza Bungeni kuwa tangu Serikali ilipofanya marekebisho ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOKA) mwaka 2016, kampuni zote za simu zilitakiwa kuuza angalau asilimia 25 ya hisa zake kwa umma kupitia soko la hisa ndani ya kipindi kilichoishia Juni 2018. Amesema hadi sasa ni kampuni ya Vodacom pekee iliyotekeleza takwa hilo la kisheria.
RC Chalamila: Wanatamani kuleta chokochoko, nguvu itakayotumia awamu hii kulinda amani, haijawahi kutokea
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewataka Wenyeviti na Watendaji wa Mitaa na Kata kuendelea kusimamia amani na utulivu katika maeneo yao, akieleza kuwa kuna baadhi ya watu wanaotamani kuibua chokochoko kupitia mitandao ya kijamii na njia nyingine. Chalamila alitoa kauli hiyo Juni 15, 2026, wakati akizungumza na viongozi hao, akisisitiza kuwa Serikali haitavumilia vitendo vyovyote vinavyoweza kuhatarisha amani na usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Japan waendeleza utamaduni wao wa kusafisha chumba cha kubadilishia nguo baada ya mechi
Mdau anasema moja ya mila na desturi bora zaidi katika ulimwengu wa soka, ni kitendo cha timu ya Japan kusafisha kabisa chumba chao cha kubadilishia nguo, huku mashabiki wao nao wakiokota takataka uwanjani baada ya mechi kumalizika—haijalishi matokeo ya mwisho yamekuwaje. Kwa mara nyingine wameacha chumba chao cha kubadilishia nguo kikiwa katika hali ya usafi wa hali ya juu baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Uholanzi, ikiwa ni mwendelezo baada ya kufanya hivyo kwenye Kombe la Dunia 2022
China imezika Shahada 12,200+ zilizopitwa na wakati kupisha AI. Tanzania bado tumelala?
Kuna ukweli mmoja mchungu sana kuhusu mfumo wetu wa elimu ya juu hapa nchini ambao kama tusipoujadili sasa, kwa uwazi na bila kupepesa macho, tutakuja kujuta kama taifa baada ya miaka mitano au kumi ijayo. Wakati sisi hapa Tanzania bado tunapambana kuongeza udahili wa wanafunzi kwenye kozi zilezile zilizoundwa tangu miaka ya 1990, wenzetu kule China wanafanya mapinduzi makubwa na ya kutisha (academic overhaul) ili kuendana na zama za Akili Unde, almaarufu Artificial Intelligence (AI). Bomu...
Baada ya kuwavuruga viungo wa Brazil, Bouaddi awaweka Arsenal, Liver na PSG vitani kusaka Saini yake
Kiungo Ayyoub Bouaddi, amezitikisa hisia za mashabiki wa soka ulimwenguni kufuatia kiwango bora cha kipekee alichokionesha kwenye mchezo wake wa kwanza wa Kombe la Dunia (World Cup debut) dhidi ya miamba ya soka, Brazil katika mchezo uliomalizika kwa sare ya 1–1 pale MetLife Stadium, New Jersey, Marekani.
Mwamuzi Omar Artan kulipwa posho yote ya Kombe la Dunia, licha ya kunyimwa Visa ya Marekani
Mwamuzi wa Womalia, Omar Artan, ambaye alinyimwa visa ya kuingia nchini Marekani kuchezesha Kombe la Dunia linaloendelea la 2026, atalipwa posho yake yote ya mashindano hayo. Vyanzo vya habari vimeiambia BBC Sport kwamba, ingawa Artan hatashiriki kabisa katika Kombe la Dunia, Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) imeahidi kumlipa stahiki zake alizokuwa anastahili kulipwa endapo angechezesha.
Pigo kwa timu ya England, Vifaa vyaibwa kabla ya Mechi Kombe la Dunia 2026
Timu ya taifa ya England imepata pigo kubwa kabla ya mechi yao ya kwanza ya Kombe la Dunia. Kiasi kikubwa cha vifaa vya timu kimeibwa Kansas City, Marekani, wakati vilipokuwa vinasafirishwa kutoka Florida kwenda kambi yao ya mazoezi.
Davido avaa koti lenye majina ya waliotekwa Nigeria akitumbuiza tamasha la FIFA
Msanii Davido amevutia hisia za wengi baada ya kuvaa koti lenye majina ya wanafunzi 39 na walimu saba waliotekwa nyara nchini Nigeria, wakati akitumbuiza kwenye tamasha la 'FIFA Countdown Concert' jijini Los Angeles, Marekani. Hatua hiyo imeonekana kama ishara kubwa ya kuwakumbuka waathirika na kupaza sauti kuhusu usalama wa watoto na walimu maeneo yenye migogoro.
Kumbukizi | RC Dkt. Kleruu alivyopigwa Risasi Siku ya Krismasi Isimani mwaka 1971
Mauaji ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Wilbert Andrew Kleruu, yanaendelea kukumbukwa kama moja ya matukio makubwa zaidi katika historia ya nchi. Kleruu, msomi na mtendaji mahiri wa serikali ya Mwalimu Nyerere, aliuawa kwa kupigwa risasi na mkulima Said Abdallah Mwamwindi siku ya Krismasi mwaka 1971 katika kijiji cha Mkungugu, Isimani, kufuatia mgogoro uliokuwa umeibuka kuhusu sera za vijiji vya ujamaa na umiliki wa mashamba.
Baada ya kukosa Kombe la Dunia, Mwamuzi wa Somalia Artan apewa Mechi ya UEFA Super Cup
Shirikisho la Soka Barani Ulaya (UEFA) limemteua mwamuzi wa kimataifa kutoka Somalia, Omar Abdulkadir Artan, kuchezesha fainali ya UEFA Super Cup kati ya Paris Saint-Germain (PSG) na Aston Villa, itakayofanyika Agosti 12 mjini Salzburg. Hatua hiyo inakuja siku chache baada ya Artan kuzuiwa kuingia nchini Marekani, hali iliyomfanya ashindwe kushiriki kama mwamuzi katika Kombe la Dunia 2026 licha ya kuwa miongoni mwa waamuzi waliokuwa wameteuliwa na FIFA.
Prof. Kitila: Tanzania haitakubali kupangiwa marafiki wala maadui
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo amesema ziara za Rais Samia Suluhu nje ya nchi zinalenga kutafuta washirika wa biashara na uwekezaji badala ya wafadhili, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa falsafa ya kuifungua nchi kiuchumi, kisiasa na kijamii. Akiwasilisha Bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2025 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2026/27, amesema Tanzania itaendelea kutafuta fursa za biashara na uwekezaji bila kuchagua upande.
Ufunguzi Kombe la Dunia 2026
Mexico itafungua Kombe la Dunia dhidi ya Afrika Kusini mjini Mexico City. Hii ni marudio ya mechi ya ufunguzi ya Kombe la Dunia 2010, ambapo timu hizi zilitoka sare ya 1–1 nchini Afrika Kusini. Jambo la kipekee ni kwamba Estadio Azteca maarufu "hekalu la soka" ni moja kati ya viwanja vya mpira wa miguu vyenye historia kubwa na ya kipekee zaidi duniani baada ya kuandaa mechi za Kombe la Dunia katika matoleo matatu tofauti: 1970, 1986 na sasa 2026.
Kesi ya Uhaini ya Lissu iliyopangwa kusikilizwa Juni 11 yaahirishwa hadi Julai 6, 2026
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa taarifa kuwa shauri la Maombi ya Jinai Na. 7440840/2026 kati ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na Mwenyekiti wa chama hcho, Tundu Lissu, ambalo lilipangwa kuendelea Juni 11, 2026, limeahirishwa. Kwa mujibu wa taarifa ya Mahakama ya Rufani ya Tanzania, shauri hilo sasa limepangwa kwa ajili ya Judgments, Rulings & Orders siku ya Jumatatu, Julai 6, 2026, saa 3:00 asubuhi.
Mwanaharakati wa Sudan Kusini adaiwa kutekwa Nairobi, Kenya
Athorbey Al-Gaddhaffy-Dit mwanaharakati wa kisiasa na mfichua maovu (whistleblower) anadaiwa kutekwa jijini Nairobi na watu wenye silaha, huku watetezi wa haki za binadamu wakihofia uwezekano wa kurudishwa nchini kwake Sudan Kusini kwa nguvu. Polisi wamemwambia mke wake kuwa Dit alitekwa na wanaume waliovaa barakoa waliokuwa wakitumia gari jeupe, alipokuwa akitoka katika Kasino moja jijini Nairobi.
Canada: Rubani ashtakiwa kwa kurusha ndege mara 900 kwa miaka 16 bila kuwa na leseni sahihi
Rubani wa zamani wa shirika la ndege la Air Canada, Geoffrey Wall mwenye umri wa miaka 59, ameshtakiwa na polisi kwa kufanya kazi kama kapteni wa ndege kwa miaka 16 bila kuwa na leseni sahihi. Inadaiwa kuwa alihudumu kama kapteni wa ndege kubwa za abiria kati ya mwaka 2009 na 2025 bila kuwa na leseni maalum inayohitajika kwa ndege hizo (Airline Transport Pilot License). Katika kipindi hicho, aliruka ndege zaidi ya mara 900 katika safari za ndani na nje ya Canada.
Kaimu Waziri wa Afya-Zanzibar: Hatuwezi Kuwatibu wasio Wazanzibari
Kaimu Waziri wa Afya Zanzibar, Saada Mkuya Salum amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haiwezi kugharamia matibabu kwa Watu wasio Wazanzibar. Saada ametoa kauli hiyo Juni 8, 2026 wakati akijibu hoja kwenye Baraza la Wawakilishi Zanzibar kupitia vikao vinavyoendelea vya kujadili bajeti mbalimbali. “Mtu ambaye sio Mzanzibar anakwenda katika hospitali zetu anaonesha matibabu kadi, pili Watu kuzuiwa nadhani nilitoa maelezo sana, sio ZHF inaanza bali inaendelea kuwasajili wengine ambao sio...
Iran yadai FIFA imefuta tiketi za mashabiki wake Kombe la Dunia Marekani
Shirikisho la Soka la Iran (FFIRI) limesema kuwa FIFA au mamlaka za Marekani zimeondoa mgao wa tiketi uliokuwa umetengwa kwa mashabiki wa Iran kwa mechi zote tatu za hatua ya makundi zitakazochezwa Marekani. FFIRI ilieleza kuwa tayari ilikuwa imeanza mchakato wa kuuza tiketi hizo kwa mashabiki wake, na baadhi yao walikuwa tayari wamepanga safari za kuhudhuria mechi hizo.
Mahakama Kuu yaamuru Gachagua kulipwa fidia ya Tsh. Bilioni 1 kwa kuondolewa Madarakani
Mahakama Kuu imeiamuru Seneti ya Kenya kumlipa aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua fidia ya kikatiba ya Ksh. 50 Milioni (zaidi ya Tsh.Bilioni 1), baada ya kubaini kuwa haki yake ya kusikilizwa kwa haki ilikiukwa wakati wa mchakato wa kumwondoa madarakani (impeachment) uliomwondoa ofisini Oktoba 2024.
Mwamuzi wa Somalia azuiwa kuingia Marekani, kuchezesha Kombe la Dunia 2026
Mwamuzi mashuhuri wa soka kutoka Somalia, Omar Artan, amezuiwa kuingia Marekani licha ya kuwa miongoni mwa waamuzi 52 walioteuliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kuchezesha mechi za Kombe la Dunia 2026 litakalofanyika nchini Marekani, Canada na Mexico. Artan, ambaye angekuwa Mwamuzi wa kwanza kutoka Somalia kuchezesha fainali za Kombe la Dunia, alizuiwa kuingia nchini humo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Miami na kurejea Istanbul, Uturuki, ambako amekuwa akiishi hivi sasa.
Back
Top Bottom