Featured content

Maelekezo ya Lissu "Futeni kesi zangu na za chama, nikiwa huru ndiyo tuzungumze"
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, ameeleza utayari wake wa kushiriki mazungumzo ikiwa tu atakuwa huru baada ya kufutwa kwa kesi zote zinazomkabili yeye pamoja na chama chake. Kupitia taarifa iliyotolewa Aprili 16, 2026 na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Brenda Rupia, imeeleza kuwa Lissu amesema kesi ya Uhaini inayomkabili inatokana na msimamo wake wa No Reforms, No Election.
Arusha: Watu 6 wakamatwa wakituhumiwa kumuua Askari kwa kudhani ni Mwizi
Jeshi la Polisi linawashikilia Watu 6 kwa kudaiwa kumuua Askari Polisi, Roland Mollel baada ya kumshambulia, tukio lililotokea katika Mtaa wa Mlimani, Kata ya Muriet, jana Aprili 15, 2026. Kamanda wa Polisi Mkoa, SACP Justine Masejo amesema Roland alikuwa katika shughuli zake binafsi baada ya kazi, kulitokea taharuki iliyotokana na kusambaa maneno ya kundi la Watu wakidai eneo lao kuna wezi, marehemu akapita akiwa amebebwa katika bodaboda, kundi la Watu likawashambulia huku wakiwakimbiza.
Rais wa FIFA: Nimeonana na Iran, itashiriki Kombe la Dunia 2026 Marekani
Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Gianni Infantino amewahakikishia mashabiki wa Soka Duniani kuwa timu ya taifa ya Iran itashiriki Kombe la Dunia 2026, licha ya mashaka yaliyotanda tangu Marekani na Israel zilipoingia katika vita na Iran. Amesema Iran imefuzu kihalali kushiriki Kombe la Dunia na wachezaji wake wana haki ya kucheza na kuiwakilisha nchi yao.
Mwigulu: Elimu ya msingi ya lazima kuwa miaka 10
Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba ametangaza kuanza kwa utekelezaji wa mfumo mpya wa elimu utakaofanya elimu ya msingi kuwa ya lazima kwa kipindi cha miaka kumi, akisema ni sehemu ya mageuzi makubwa yaliyofanywa na Rais Samia Suluhu. Akihitimisha hotuba ya bajeti bungeni, ameeleza kuwa mabadiliko hayo ni makubwa zaidi tangu yale ya mwaka 1967 yaliyoongeza elimu ya lazima kufikia darasa la saba.
Afrika Kusini: Kiongozi wa Upinzani Julius Malema ahukumiwa miaka 5 jela
Kiongozi wa Chama cha Upinzani cha Economic Freedom Fighters (EFF), Julius Malema amehukumiwa kifungo cha Miaka Mitano jela na kulipa faini baada ya kupatikana na hatia ya makosa matano ikiwemo kumiliki silaha kinyume cha Sheria na kuifyatua hadharani hali iliyohatarisha maisha ya Watu. Mwanasheria wake amesema watakata rufaa dhidi ya uamuzi huo ili kuzuia kiongozi huyo kupelekwa gerezani.
Mahakama ya Rufani yairuhusu CHADEMA kuendelea na shughuli za Kisiasa nchini
Mahakama ya Rufani Kanda ya Dodoma, leo Aprili 15, 2026 imetengua maamuzi ya Mahakama Kuu yaliyokizua Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kufanya shughuli za Siasa nchini, kufuatia kesi iliyofunguliwa na Said Issa Mohamed (aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar), Maulidah Anna Komu na Ahmed Rashid Khamis dhidi ya chama hicho.
Korea Kusini: Raia kuanza kupewa Intaneti ya bure kama haki ya msingi sawa na maji na umeme
Korea Kusini imekuwa nchi ya kwanza kutekeleza mpango wa kuwapatia wananchi Intaneti bure hata baada ya vifurushi kuisha, kwa kasi ya takriban 400 Kbps. Hatua hii inalenga kuhakikisha upatikanaji wa huduma muhimu mtandaoni kama sehemu ya mkakati wa kuifanya Intaneti kuwa haki ya msingi, tofauti na nchi kama Ufilipino, Estonia na Costa Rica ambazo hutoa Wi-Fi ya bure katika maeneo ya umma.
Kakoso: Serikali iweke tozo kwenye mawasiliano ya simu kusaidia kujenga barabara
Mbunge wa Tanganyika (CCM), Selemani Kakoso, amependekeza kuongeza tozo ya shilingi 100 kwenye matumizi ya simu ili kusaidia kukarabati miundombinu. Ametoa hoja hiyo Aprili 13, 2026, Bungeni Dodoma akichangia bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Amesema iwapo litakubaliwa na wataalamu, linaweza kuingizia Serikali karibu Tsh. Trilioni 1 zitakazosaidia kutatua changamoto ya miundombinu.
Polisi: Mwanamtandao Ashlee Jenae alifia Hospitali baada ya kukutwa amejinyonga
Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Unguja Kaskazini, Benedict Mapujira amesema Mwanamtandao Ashy Robinson (Ashlee Jenae), Raia wa Marekani alifia Hospitali alikowaishwa baada ya kukutwa na Mhudumu wa Hoteli akiwa amejinyonga katika chumba chake cha hoteli. Ameongeza kuwa Mwili wa Ashlee bado upo Zanzibar kama sio jana basi leo utakuwa umefanyiwa uchunguzi
Rais wa Djibouti ashinda muhula wa sita kwa 97.8%
Rais wa Djibouti, Ismael Omar Guelleh, ameshinda tena uchaguzi kwa asilimia 97.8 ya kura, na hivyo kujihakikishia muhula wa sita madarakani unaoongeza utawala wake kufikia miaka 27. Katika uchaguzi huo uliofanyika Aprili 10, 2026, alikabiliana na mgombea mmoja wa upinzani, Mohamed Samatar, huku vyama viwili vikuu vya upinzani vikisusia uchaguzi tangu Mwaka 2016 vikidai kukosekana kwa usawa katika mamlaka za uchaguzi. Ushiriki wa wapiga kura ulikuwa 80.4%
Mwabukusi: Tunahitaji ukweli waliotekwa wako wapi? Na wa 'Mauaji ya Halaiki' ya Oktoba 29, 2025?
Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi amevitaka vyombo vya dola na taasisi za usimamizi wa uchaguzi kutoa majibu ya haraka kuhusu kile alichokiita “mauaji ya halaiki” na miili ya raia iliyopotezwa Oktoba 29, 2025, akisisitiza kuwa taifa haliwezi kupona bila ukweli na uwajibikaji.
UTAFITI: Tanzania miongoni mwa nchi zenye Uhuru mdogo zaidi wa mtandao
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Cloudwards mwaka 2026, ulioshirikisha nchi 171 na kutathmini viwango vya udhibiti wa mtandao kwa kuzingatia vigezo kama matumizi ya majukwaa ya mitandao ya kijamii, upatikanaji wa maudhui ya kisiasa na kidini, kanuni zinazohusu matumizi ya VPN pamoja na maudhui ya kiuchumi na kijamii. Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoonesha kuwepo kwa udhibiti wa majukwaa ya mitandao ya kijamii, ikiwemo X, JamiiForums.com na Clubhouse, kwa kiwango cha 28%.
TG-MSG: Tume ya Matukio ya Oktoba 29 iache danadana, Watanzania wanahitaji Uwajibikaji
Mtandao wa Asasi za Kiraia nchini (CSOs) kupitia Kikundi Elekezi cha Wadau wa Utawala Tanzania (TG-MSG) umeitaka Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 inayoongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Othman Chande kuacha kuchelewesha mchakato huo na badala yake kutoa ripoti kamili kwa umma. Tume hiyo ilisema Mamlaka ya Uteuzi imeridhia maombi yao ya muda wa ziada wa siku 21 ili kukamilisha kazi kabla au ifikapo Aprili 24, 2026.
Heche: Walitufuata na kutupa masharti ili Lissu aachiliwe, tumekataa kuwapigia magoti
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche amesema pamoja na Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu kuwa kizuizini mwaka mmoja, amekataa kuwapigia magoti ili aachiliwe huru. Heche amesema mojawapo ya masharti ilikuwa akubali kuacha siasa na kuishi nje ya nchi, lakini amekataa. Amesisitiza kuwa Lissu amechagua kubaki kizuizini kuliko kuacha kuwatetea Watanzania au kusaliti misingi ya haki na demokrasia anayoisimamia.
TABOA: Aprili 12 Basi hazipelekwi 'service', usafiri utakuwepo kama kawaida
Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (TABOA) kimesema huduma za usafiri zitaendelea kutolewa kama kawaida kufuatia mazungumzo kati yake na Serikali. Katibu Mkuu wa TABOA, Priscus John, amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kukutana na Waziri wa Uchukuzi, Makame Mbarawa, na viongozi wa chama hicho. Ikumbukwe April 8, 2026, Priscus alitoa taarifa kwa wananchi ambao hawajafanya 'booking' mpaka Aprili 12 wasifanye, kwani hawawezi kuendelea kutoa huduma baada ya bei za mafuta kupanda
LATRA: Madereva watakaogoma Aprili 12, 2026 tutawafutia leseni
Mkurugenzi wa Udhibiti Uchumi wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Abdallah Mhagama, amesema kanuni na sheria zinazosimamia utoaji wa huduma za usafiri ziko wazi, na zinaweka masharti kwa watoa huduma ikiwemo kutofanya migomo, akibainisha kuwa mgomo wowote utakaofanyika ni kinyume cha sheria utachukuliwa kuwa batili kwa mujibu wa masharti ya leseni zilizotolewa kwa watoa huduma hao. Amesema endapo dereva atashiriki mgomo, mamlaka itashughulika na kila mmoja kwa kuwafungia Leseni.
Samia: Serikali ipunguze matumizi ya mafuta, msafara wangu maafisa wote watatumia "kibasi"
Rais Samia ametangaza hatua mpya za kubana matumizi ya mafuta serikalini, akibainisha kuwa matumizi hayo yamekuwa makubwa kutokana na wingi wa magari yanayotumika katika safari za kikazi. Amesema juhudi hizo zitaanza katika ofisi yake mwenyewe. Amesema kuwa popote atakapokwenda, maafisa wote wataingia kwenye basi moja (kibasi). Msafara utabakiwa na gari la Rais (escort), magari ya polisi, na gari la akiba pekee, huku maafisa wengine wote wakisafiri kwa pamoja ili kuokoa gharama.
Jaji Chande: Tume ya Matukio ya Oktoba 29 inajitegemea kwa kila kitu, hatuna dalali
Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Vurugu za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, Jaji Mstaafu Mohamed Chande Othman, amesema tume hiyo iko huru na haiikingiliwa na mamlaka yoyote, akikanusha madai kuwa muda wa kazi yake umeongezwa ili kuruhusu kuhaririwa kwa ripoti yake. Tume hiyo iliyoundwa na Rais Samia, Novemba 20, 2025 kuchunguza matukio yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu, ingawa mpaka sasa imeongezewa muda mara mbili
Marekani na Iran zakubaliana kusitisha mapigano kwa wiki mbili
Rais wa Marekani Donald Trump amesema amekubali kusitisha mashambulizi dhidi ya Iran kwa muda wa wiki mbili, kufuatia pendekezo la wapatanishi katika mgogoro huo. Trump amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya mazungumzo na viongozi wa Pakistan, akiwemo Waziri Mkuu Shehbaz Sharif, ambao waliomba muda zaidi kwa juhudi za kidiplomasia.
Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Oktoba 29 yaongezewa Muda tena hadi Aprili 24
Mamlaka ya Uteuzi imeridhia maombi ya muda wa ziada kwa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 hivyo imeiongezea tena muda wa siku ishirini na moja (21) na kuitaka ikamilishe kazi kabla au ifikapo Aprili 24, 2026. Mamlaka hiyo imeeleza sababu za kuongeza muda huo kwa Tume ni pamoja na kuiwezesha Tume kukamilisha uchambuzi wa ushahidi, taarifa na maoni yaliyopokelewa, kutoa fursa kwa wataalamu wa uchunguzi wa kisayansi kufanyia kazi...
Back
Top Bottom