Featured content

Nyahoza: Barua yetu kwa CHADEMA inasema kusimamisha chama kwa muda, sio kufuta
Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza, amesema barua waliyoiandikia CHADEMA haimaanishi kufutwa kwa chama hicho, bali ni hatua ya kuwataka wajieleze kabla ya kuchukuliwa hatua za kusimamishwa kwa muda au kutozwa faini endapo watabainika na makosa. Katika barua ya Mei 7, Msajili alinukuu kauli za John Heche na Oliver Kisaka kuhusu maandamano ya Oktoba 29, 2025. Nyahoza amesema CHADEMA imepewa nafasi ya kujieleza kabla ya hatua yoyote kuchukuliwa.
Msigwa: Wakosoaji wa nje ni miradi, Watu wanatumika kuichafua nchi
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema baadhi ya watu wanaokwenda nje ya nchi kuikosoa Tanzania hutumia vibaya uhuru wa kujieleza kwa kutoa taarifa za upotoshaji na kuzua taharuki. Amesema uhuru una mipaka yake kwa mujibu wa sheria na haupaswi kuhatarisha usalama wa nchi. Akizungumza Msigwa amesema baadhi ya wakosoaji hao hutumia mitandao ya kijamii kueneza taarifa zisizo sahihi, huku akidai wengine wamekuwa sehemu ya miradi yenye malengo ya kuichafua nchi.
Nassari: Wanavuka boda kutoka Kenya kuja kununua Vitunguu, nao wanahesabiwa ni Watalii
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, amesema takwimu zinazoonesha watalii nchini kufikia milioni 5.3 hazioneshi uhalisia, akidai kuwa baadhi ya watu wanaovuka mipaka kwa shughuli za biashara hujumuishwa kama watalii. Ametoa mfano wa wananchi wanaotoka Kenya kuingia Mwang’ola, Karatu kununua vitunguu lakini nao huhesabiwa kama watalii. Nassari ameyasema hayo Mei 15, 2026, Bungeni mjini Dodoma alipokuwa akichangia Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii,
Madonna, Shakira na BTS Kutumbuiza Fainali ya Kombe la Dunia
Mastaa wakubwa duniani Madonna, Shakira, na kundi la BTS wataongoza jukwaa siku ya fainali ya Kombe la Dunia Julai 19, 2026 huko New Jersey, Marekani. Michuano hii mikubwa inaandaliwa kwa ushirikiano wa nchi tatu ambazo ni Marekani, Canada, na Mexico.
Jaji Warioba: Naamini Vifo vya Oktoba 29 vilikuwa vingi zaidi kuliko wanavyosema
Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba, ameeleza wasiwasi wake kuhusu ripoti ya uchunguzi wa matukio ya Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu 2025, amesema anaamini vifo vilikuwa vingi zaidi kuliko ilivyoripotiwa Aidha, amehoji mapendekezo ya kuwajibishwa kwa waliotenda, walioagiza je?, huku akirejelea Uchunguzi wa tukio la Mwaka 1976 Mkoani Shinyanga ambapo baadhi ya viongozi walijiuzulu.
Tanzania yashuka nafasi 22 kwenye orodha ya Uhuru wa Vyombo Vya Habari Duniani
Tanzania imeshika nafasi ya 117 kwenye orodha ya Uhuru wa Habari Duniani ya Mwaka 2026 iliyotolewa na Reporters Without Borders (RSF), ikiwa ni anguko la nafasi 22 kutoka nafasi ya 95 ya Mwaka 2025. Upande wa Afrika Mashariki, Tanzania imeshika nafasi ya pili, nyuma ya Kenya iliyoshika nafasi ya 106, Burundi imefuatia katika nafasi ya 119, huku Democratic Republic Congo ikishika nafasi ya 130 na Uganda nafasi ya 131.
Tanzania yadaiwa kuwazuia Wabunge wa Ulaya Kufanya Ziara Nchini
Wakuu, Kuna taarifa nzito sana imetolewa na Bunge la Ulaya (European Parliament) kuhusu mahusiano yetu ya kidiplomasia na hali ya haki za binadamu hapa nchini. Kwa mujibu wa chapisho rasmi kutoka kwenye tovuti ya bunge hilo, Serikali ya Tanzania imeikatalia kamati ya Wabunge wa Ulaya kufanya ziara yao rasmi iliyokuwa imepangwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu wa Mei. Kwa ufupi, haya ndiyo yaliyo kwenye hii taarifa: Lengo la Ziara: Ujumbe huu kutoka Kamati Ndogo ya Haki za Binadamu (MEPs)...
Rais Samia: Yaliyotokea Oktoba 2025 yametia doa kwenye Taifa letu
Rais. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Dodoma, tarehe 08 Mei, 2026 amesema matukio yaliyotokea nyuma hayakuwa na manufaa kwa mtu yeyote na yalisababisha vijana wengi kuingia kwenye matatizo kwa kufuata mkumbo bila kuelewa madhara yake. "Nililolotokea nyuma halikuwa jema kwa yeyote yule. Na mtego ule anaingia aliyekuwemo na asiyekuwemo... Kumbukumbu lile lilikumba vijana wengi sana na wengi waliingia kwa kutokujua kwa mkumbo. Lakini walivyokamatwa kama mama nikasema...
Lissu aomba apelekwe Dodoma kusikiliza kesi yake dhidi ya AG na Kamishna wa Magereza
Kesi hiyo imetajwa kwa mara ya pili, Mei 5, 2026 kwa njia ya Mtandao, Lissu akishiriki kwa njia hiyo kutoka gerezani Ukonga, Lissu amedai ikiendelea hivyo atakosa haki ya kusikilizwa kikamilifu chini ya Ibara ya 13(6) (a) ya Katiba. Hata hivyo, Mwanasheria Mkuu ameibua pingamizi la awali akidai kesi hiyo ni batili inakiuka Kifungu cha 8(2) cha Sheria ya Utekelezaji wa Haki za Msingi na Wajibu (BRADEA). Mahakama imeahirisha kesi hiyo hadi Mei 21, 2026 itakapotoa uamuzi wa maombi hayo ya Lissu.
Kihongosi: Kuna watu wanatumia video za matukio ya Oktoba 29 kama mtaji wa kisiasa
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi akizungumza na waandishi wa habari kwenye Makao Makuu Dodoma Mei 4, 2026, amesema kuna baadhi ya watu wanatumia video za matukio yaliyotokea wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 kama mtaji wa kisiasa.
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo yaomba Tsh Bilioni 525.3 kwa  mwaka wa fedha 2026/2027
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, Mei 4, 2026 amewasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 ambapo ameomba Bunge kuidhinisha jumla ya Tsh. bilioni 525.3, ambapo kati ya fedha hizo Tsh. Bilioni 39.07 zimetengwa kwa ajili ya mishahara, Tsh. Bilioni 28.06 kwa ajili ya mengineyo na Tsh. Bilioni 458.19 kwa ajili ya miradi ya maendeleo
Waziri Kairuki: Matumizi ya Internet yameongezeka kwa 19.5%, watumiaji wafikia Milioni 58.9
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki, akiwasilisha taarifa ya wizara hiyo Bungeni Aprili 30, 2026, amebainisha sekta ya mawasiliano nchini imeendelea kukua kwa kasi, ambapo idadi ya watumiaji wa Intaneti imeongezeka kwa 19.5%, kutoka milioni 49.3 (Machi 2025) hadi kufikia milioni 58.9 (Machi 2026).
Mahakama yakataa Lissu kuunganishwa kwenye kesi ya mgawanyo wa mali za CHADEMA
Aprili 30, 2026, Mahakama Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imekataa ombi la Tundu Lissu la kuunganishwa katika Shauri Namba 8323/2025 lililofunguliwa na Said Issa Mohamed na wenzake dhidi ya Bodi ya Wadhamini pamoja na Katibu Mkuu inayohusu mgawanyo wa mali za CHADEMA.
AZAKI: Tume ilitumia taarifa za Polisi ambao nao wanatuhumiwa kuua waandamanaji
Mwakilishi wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Halima Sonda, wakati akiwasilisha sehemu ya tamko la asasi za kiraia (AZAKI) na watetezi wa haki za binadamu kuhusu ripoti ya matukio ya Oktoba 29, 2025 mbele ya waandishi wa habari Aprili 27, 2026, alisema kuwa Tume hiyo ilitumia vyanzo rasmi kama Polisi na vituo vya afya, ambavyo pia vinalalamikiwa kuwa wahusika wakuu wa ukiukaji wa haki, ikiwemo kuua na kutesa raia.
Jaji Juma: Baada ya Ripoti Kutoka, tumepokea simu za matusi zaidi ya 300
Tume ya kuchunguza matukio ya Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu 2025, imezungumza na vyombo vya habari Aprili 28, 2026 ikiwa ni baada ya siku tano ilipowasilisha na kukabidhi Ripoti yake kwa Rais Samia Aprili 23, 2026. Jaji Mkuu Mstaafu Ibrahim Juma, ambaye ni mmoja wa Wajumbe wa Tume hiyo amesema kwamba kuwa kuna watu hawataki maoni ya watu wengine yasikike na kwamba baada ya kutoa ripoti wamepokea simu za matusi zaidi ya 300.
Maswali 10 Muhimu Kuhusu Ripoti ya Tume ya Jaji Chande
Hatimaye Tume ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, imetoa ripoti yake baada ya kufanya uchunguzi kwa siku 153. Tume hiyo iliyoongozwa na Jaji Mkuu mstaafu, Mohamed Chande Othman, ilikuwa na wajumbe wanane ambao ni: Dkt. Stergomena Tax, Jaji Mkuu mstaafu Profesa Ibrahim Hamis Juma, Balozi Ombeni Yohana Sefue, Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu Said Ally Mwema, Balozi Paul Meela, Balozi David Kapya, Balozi George Madafa, na Balozi...
Jaji Chande: Tume imepokea ushahidi toka kwa Watu 63,603
Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025, Jaji Mohamed Chande Othman, amesema Tume hiyo imepokea ushahidi kutoka kwa Watanzania 63,603 kwa njia mbalimbali. Amesema ushahidi huo umepatikana kupitia mahojiano ya ana kwa ana na mashahidi 1,323, mashahidi wa viapo 553, na madodoso 4,891 yaliyokuwa na maswali bila majina ya wahusika.
Msigwa: Deni la Taifa linakua siyo kwa sababu tunatumia vibaya fedha
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema kuwa ongezeko la deni la taifa halitokani na matumizi mabaya ya fedha, bali ni matokeo ya uwekezaji mkubwa katika miradi ya kimkakati ya maendeleo inayolenga kuleta mapinduzi ya kiuchumi. Msigwa amefafanua kuwa fedha hizo zimeelekezwa katika ujenzi wa miundombinu ya kisasa kama reli ya mwendokasi (SGR), upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam, uimarishaji wa shirika la ndege (ATCL), pamoja na kuboresha huduma za kijamii ikiwemo kusambaza umeme vijiji
Rais Samia: Mmeshuhudia siku tatu zile, hakukuwa na harusi wala mabaa, zilikuwa siku nzito
Rais Samia Suluhu amesema amani ni hazina ya shughuli zetu za kiuchumi na kijamii akisisitiza kwamba bila amani hakuna kujenga uchumi, hakuna shughuli za kijamii. Ameongeza kuwa, mmeshuhudia siku tatu zile (Oktoba 29) ambapo hakukuwa na shughuli za burudani, harusi, kitchen party, mikusanyiko ya kijamii, wala michezo yoyote. Amesema zilikuwa siku tatu nzito.
Msanii A.Y: Niwe mkweli suala la kutengeneza Mdundo wa Taifa, haliwezekani
Msanii mkongwe wa Bongo Fleva, Ambwene Yesaya (AY), ameweka wazi msimamo wake kuhusu mjadala wa “mdundo wa taifa,” akisisitiza kuwa utambulisho wa muziki hauwezi kulazimishwa kupitia mipango ya mezani bali hujitengeneza wenyewe kadri muda unavyokwenda. Amesema muziki wa Bongo Fleva tayari una ladha yake inayotambulika kimataifa, akitoa mfano kuwa hata nchi kama Nigeria zilipitia hatua za kuiga kabla ya kufikia utambulisho wao wa sasa, hivyo wasanii wanapaswa kuthamini muziki wa nyumbani.
Back
Top Bottom