Shauri la ugaidi linalomkabili mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Dk. Melikisedeki Kaijage, limeahirishwa hadi Agosti 19, 2026 baada ya kutajwa leo, Agosti 5, 2026, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma.
Shauri hilo lilitajwa mbele ya Hakimu Mfawidhi, Zabibu Mpangule, ambapo ilielezwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kulisikiliza. Badala yake, jukumu lake ni kuhakikisha taratibu za awali, ikiwemo ukamilishaji wa faili la shauri, zinakamilika kabla ya kesi kupelekwa katika mahakamani