Dk Melikisedeki Kaijage, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) aliyekuwa akishikiliwa na Jeshi la polisi mkoani Dodoma kwa madai ya kuhamasisha maandamano ya Julai 7, 2026, sasa amebadilishiwa shitaka na kuwa la ugaidi na hivyo kunyimwa dhamana.
Awali, Jumanne Julai 21, Dk Kaijage alipewa dhamana na Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, baada ya kushikiliwa katika kituo cha Polisi Chang’ombe jijini humo tangu Julai 8, 2026, lakini kabla hajaachiliwa, akapewa shitaka hilo.
Soma pia: Mhadhiri...