Featured content

Lissu: Sina imani kabisa na Mahakama kwenye masuala ya Uchaguzi
Hatua ya maswali ya dodoso (Cross Examination) kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, yanatarajiwa kutamatishwa leo Agosti 27, 2026 na kufungua mlango kwa shahidi mwingine wa Lissu kupanda kizimbani kwaajili ya kutoa utetezi wake. Jana Agosti 26, 2026, Tundu Lissu alihitimisha kutoa ushahidi wake mbele ya jopo la majaji watatu, wakiongozwa na Jaji, Dunstan Ndunguru, ambapo ambapo baada ya hatua hiyo, upande wa Jamhuri (Washtaki) walipewa nafasi ya kuuliza maswali hayo kwa mshtakiwa...
Deogratius Ndejembi apitishwa kuchukua nafasi ya Makamu wa Rais
Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imemfutia uanachama wa Chama hicho leo Agosti 26, 2026 aliyekuwa Makamu wa Rais, Dkt. Emmannuel Nchimbi ambaye alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo na kustaafu siasa jana Agosti, 25, 2026. ============= Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imemteua Deogratius Ndejembi kushika nafasi ya Makamu wa Rais, nafasi ambayo ilibaki wazi baada ya aliyekuwepo, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kutangaza kujiuzulu 25, Agosti 2026. Tuseme watamtangaza...
Dkt. Emmannuel Nchimbi afukuzwa uanachama wa CCM
Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imemfutia uanachama wa Chama hicho leo Agosti 26, 2026 aliyekuwa Makamu wa Rais, Dkt. Emmannuel Nchimbi ambaye alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo na kustaafu siasa jana Agosti, 25, 2026. Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Chama hicho Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro leo Agosti 26, 2026 akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba. Dkt. Migiro ameeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa mara...
Lissu: Hakuna shahidi aliyesema Serikali iliogopa, wala Ikulu haikukalika kwa kauli zangu
Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu amemaliza kujitetea kama shahidi wa kwanza mbele ya jopo la Majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru katika kesi ya Uhaini Na. 19605 inayomkabili katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam.
Makamu wa Rais, Dkt. Emmanuel Nchimbi atangaza kustaafu siasa, ajiuzulu
Makamu wa Rais wa JTanzania, Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo na kustaafu siasa pamoja na utumishi wa umma. Katika taarifa yake kwa umma iliyotolewa Agosti 25, 2026, Dkt. Nchimbi amesema amemuandikia barua Rais wa Tanzania, Samia Suluhu, kumjulisha uamuzi wake wa kuachia nafasi hiyo.
Zambia yafunga Mahakama huku muda wa rufaa za uchaguzi ukikaribia kuisha
Nchini Zambia majengo yote ya Mahakama Kuu na Mahakama ya Katiba yamefungwa kwenye siku iliyokuwa ya mwisho kisheria kwa mgombea wa upinzani, Brian Mundubile, kuwasilisha pingamizi la matokeo ya uchaguzi wa urais. Nchini Zambia, maombi yote ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais lazima yawasilishwe ndani ya siku saba tangu kutangazwa kwa mshindi. Tume ya Uchaguzi ilimtangaza Rais Hakainde Hichilema kuwa mshindi wa uchaguzi huo kwa kupata kura 2,965,326 dhidi ya kura 1,856,217 alizopata...
Kesi ya Uhaini | Lissu: Sikumuomba Rais Samia nirudi nchini, Yeye ndiye aliyenitafuta
Tundu Lissu amesema hakuwahi kuomba kurejea nchini, bali Rais Samia Suluhu Hassan ndiye aliyemtafuta mwaka 2022, wakati huo Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, akiwa gerezani. Lissu amesema baada ya kupata ujumbe huo alishauriana na viongozi wenzake kabla ya kukutana na Rais Samia nchini Ubelgiji.
Tume ya Jaji Lila: Tutachunguza nguvu iliyotumika kudhibiti ghasia za Oktoba 29, 2025
Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa Matukio ya Ghasia ya Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, Jaji Shaban Ally Lila, amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa Tume hiyo inaenda kutekeleza kazi iliyoelekezwa ya kuchunguza na kubaini wahusika wa ghasia za Uchaguzi Mkuu wa 2025. Tume hiyo iliundwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuchunguza matukio ya ghasia yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, kufuatia mapendekezo ya Tume ya...
Lissu: Tume ya Uchaguzi ni ya CCM na haifai katika mfumo wa Demokrasia wa Vyama Vingi
Shauri la uhaini namba 19605/2025 dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu, kuendelea leo Agosti 24, 2026 katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar Es Salaam, ikiwa katika hatua ya uwasilishaji wa ushahidi wa mshtakiwa mbele ya jopo la Majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru Ikumbukwe Agosti 21, 2026 Tundu Lissu alikutwa na kesi ya kujibu, ambapo alipewa nafasi ya kujitetea na akatumia nafasi hiyo kuwataja mashahidi wake. Lissu...
Mahakama: Lissu ana Kesi ya kujibu kutokana na ushahidi wa Jamhuri uliotolewa
Jopo la majaji watatu, wanaoongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru wanaosikiliza Shauri la uhaini Namba 19605/2025 dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu wanatarajiwa kutoa uamuzi leo Agosti 21, 2026 kama Mwanasiasa huyo anayo kesi ya kujibu au hana katika shauri hilo. Ikumbukwe, Agosti 17, 2026, Lissu aliiomba mahakama kutamka kuwa hana hatia na itamke kuwa anatakiwa kulipwa fidia. Akitumia kifungu cha 312(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), Lissu alisema upande wa Jamhuri...
Wasonga: Mhadhiri UDOM anatuhumiwa kutaka kuchoma majengo yote ya umma na makazi ya Polisi nchini
Kesi ya Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedeki Kitunzi Kaijage, imeahirishwa hadi Agosti 27, 2026, huku upande wa utetezi ukieleza kuwa hatua inayofuata ni kuendelea na mchakato wa uchunguzi wa awali. Kaijage anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 16278 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma, ambapo anatuhumiwa kwa makosa mawili yanayohusishwa na sheria ya kuzuia ugaidi. Akizungumza Agosti 19, 2026 jijini Dodoma, Wakili wa Kaijage, Godfrey Wasonga, amesema tuhuma...
Kihongosi: Maridhiano yataendelea tu hata kama Vyama vya Siasa vitakuwepo au visiwepo!
"Maridhiano sio kwa ajili ya Vyama Vya siasa tu. John Heche, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA) anaposema maridhiano hadi awepo Tundu Lissu ni utashi wake yeye kwamba yeye anaamini hivyo! "Lakini maridhiano yanaweza kufanyika kwa sababu Tundu Lissu ana kesi mahakamani ameshtakiwa kwa mujibu wa Sheria za nchi na hakuna mtu ambaye yupo juu ya sheria. "Namshauri waje kwenye maridhiano. Na kama suala Tundu Lissu atoke mahakama itatoa hukumu kadri itakavyoona ana...
Leseni ya Gazeti la Mwanahalisi yasitishwa kwa Miezi Sita
Idara ya Huduma za Habari (MAELEZO) imesitisha kwa miezi sita leseni ya Gazeti la MwanaHALISI kuanzia Agosti 19, 2026, baada ya kubainika kuwa limekiuka masharti ya leseni kwa kuchapisha habari isiyozingatia usahihi na mizania. Uamuzi huo umehusishwa na habari yenye kichwa “Nchimbi agoma kujiuzulu” iliyochapishwa katika toleo la Agosti 6–12, 2026.
Waitara: Watanzania wanataka Katiba Mpya, wanataka kupunguza nguvu ya Dola
Mbunge Mwita Waitara amesema suala la Katiba Mpya ni jambo muhimu kwa Tanzania, akieleza kuwa kuna mambo matatu ambayo wananchi wanayataka, likiwamo kuwepo kwa Tume Huru ya Uchaguzi ili kuhakikisha uchaguzi unakuwa wa haki kwa vyama vyote bila kujali upande wa kisiasa. Waitara amesema Watanzania wanataka uchaguzi ambao kila mshiriki atatendewa haki, akisisitiza kuwa tofauti za kisiasa hazipaswi kuwafanya Watanzania kuonekana kama maadui. “Hata hao wapinzani ni Watanzania na walioko chama...
MALI | Mtangazaji, Mwanamtandao wahukumiwa Miaka 7 jela kwa kukosoa Serikali
Mahakama ya Rufaa ya Bamako nchini Mali imewahukumu kifungo cha miaka saba jela Mtangazaji wa Televisheni na Redio, Mohamed Youssouf Bathily (Ras Bath), pamoja na mwanamitandao Rokia Doumbia, kwa kosa la kuikosoa Serikali ya Kijeshi, katika hukumu iliyotolewa Agosti 17, 2026.
Kesi ya Lissu kutolewa uamuzi Agosti 21, 2026, asema "Nikija tunapeleka moto si wakawaida"
LISSU KUACHIWA AGOSTI 21? MAJAJI KUAMUWA KAMA ANA KESI YA KUJIBU AU LA SIKU YA IJUMAA Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu ameieleza Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Dar es Salaam leo Agosti 17, 2026 kuwa hana kesi ya kujibu katika shauri la uhaini linalomkabili huku akiiomba mahakama kutamka kuwa hana hatia na itamke kuwa anatakiwa kulipwa fidia. Kesi imeahirishwa hadi Agosti 21, 2026 siku ya Ijumaa ambapo Majaji watatu wataamuwa kama Tundu Lissu ana kesi ya kujibu au la. Kesi ya uhaini...
CHADEMA: Jamhuri imetangaza kufunga ushahidi kesi ya Uhaini dhidi ya Lissu
Ushahidi wa upande wa Jamhuri katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, umefungwa rasmi leo Agosti 17, 2026, katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Dar es Salaam. Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, ameiambia mahakama kuwa baada ya kupitia ushahidi uliotolewa, Jamhuri imeona mashahidi 17 waliotoa ushahidi wanatosha kuthibitisha hoja zao. Lissu ameeleza kuwa hana pingamizi na uamuzi huo, huku Jopo la Majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dunstan...
Makala ya CNN kuhusu Matukio ya Uchaguzi Tanzania yapata tuzo
Mwandishi wa Habari wa Shirika la Habari ya Kimataifa CNN, Larry Madowo ameshinda Tuzo ya NABJ Salute to Excellence 2026 kufuatia Makala ya kiuchunguzi kuhusu vifo vilivyotokea nchiniTanzania wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Jaji Warioba: Watanzania wanaishi kwa uoga, wanaogopa kutekwa, kupotea na kubambikiwa Kesi za uhaini
Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, amesema Watanzania kwa sasa wanaishi katika mazingira ya hofu, tofauti na ilivyokuwa zamani. Amesema wananchi wengi wanaogopa kutekwa, kupotea na kukumbwa na madhara mengine, hali inayowafanya kushindwa kutoa maoni yao kwa uhuru. Kwa mujibu wa Jaji Warioba, hofu hiyo imeathiri ushiriki wa wananchi katika mijadala mbalimbali ya kitaifa. Amesema watu wengi sasa wanaogopa kueleza wanachofikiri, wakihofia kwamba maoni yao yanaweza kuwapelekea kukamatwa...
Katambi: Ajenda ya Katiba Mpya si ya wapinzani ni ya CCM, ilianza tangu chini Kikwete
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amesema Ajenda ya Katiba Mpya sio Ajenda ya Wapinzani bali ni ajenda ya Chama cha Mapinduzi (CCM) iliyoanza tangu Awamu ya Nne chini ya Uongozi wa Rais wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambapo Rais wa Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu akiweka wazi nia ya kuleta Katiba Mpya na ndio maana Ajenda hiyo ipo katika Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.
Back
Top Bottom