Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma imemwachia huru Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedek Kaijage, baada ya Serikali kueleza kuwa haina nia ya kuendelea na mashtaka yaliyokuwa yakimkabili, huku mahakama ikimwekea masharti ya mwenendo.
Kaijage ameachiwa huru leo, Alhamisi, Septemba 10, 2026, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma, Denisi Mpelembwa baada ya Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Serikali, Jonathan Chuwa, kuiambia mahakama Serikali haina nia ya...