Featured content

Dkt. Shija: Sakata la Kaijage limeshusha Morali, linaweza kusababisha Mgomo wa Wafanyakazi UDOM
Sakata la kisheria linalomkabili Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedeki Kaijage, limechukua sura mpya baada ya upande wa mashtaka kubadilisha mashtaka yake na kumfungulia rasmi kesi ya ugaidi. Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Taaluma UDOM (UDOMASA), Dkt. Gerald Enos Shija, ameeleza kuwa hatua hiyo imeshusha sana morali ya wafanyakazi na kuwatia hofu.
Dkt. Nchimbi: Watanzania pambaneni mpate Katiba Mpya yenye muafaka katika Taifa
Makamu wa Rais, Dkt. Emmanuel Nchimbi, akizungumza leo Julai 23, 2026 katika Mkutano wa Wanachama wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) unaofanyika Jijini Dar es Salaam, amesisitiza Watanzania kupambana kupata Katiba Mpya na kwamba taifa linahitaji Katiba yenye muafaka na makubaliano ya wadau wote itakayolinda haki za raia na kulipeleka taifa mbele kwa miaka ijayo.
Mhadhiri wa UDOM aliyetuhumiwa kuhamasisha maandamano akabiliwa na shitaka la ugaidi
Dk Melikisedeki Kaijage, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) aliyekuwa akishikiliwa na Jeshi la polisi mkoani Dodoma kwa madai ya kuhamasisha maandamano ya Julai 7, 2026, sasa amebadilishiwa shitaka na kuwa la ugaidi na hivyo kunyimwa dhamana. Awali, Jumanne Julai 21, Dk Kaijage alipewa dhamana na Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, baada ya kushikiliwa katika kituo cha Polisi Chang’ombe jijini humo tangu Julai 8, 2026, lakini kabla hajaachiliwa, akapewa shitaka hilo. Soma pia: Mhadhiri...
Kwa kigezo hiki, Mbappe kushinda Ballon d'Or mwaka 2026?
Waandaaji wa tuzo ya Ballon d'Or wameeleza kuwa kushinda Kombe la Dunia pekee hakutoshi kumhakikishia mchezaji kutwaa tuzo hiyo ya kifahari. Kupitia taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti rasmi ya tuzo hiyo, wamebainisha kuwa mafanikio katika Kombe la Dunia ni miongoni mwa vigezo muhimu, lakini si kigezo cha moja kwa moja cha kushinda Ballon d'Or.
Msigwa: Serikali inafanya tathmini ya Tamko la Jumuiya ya Madola, tutawapa majibu
Serikali ya Tanzania imethibitisha kupokea tamko kutoka kwa Jumuiya ya Madola linaloitaka kumwachia huru Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, ndani ya siku 30. Akijibu swali la mwandishi wa habari, Msemaji wa Serikali alieleza kuwa serikali imeliona tamko hilo na kwa sasa inafanya tathmini ya kina ya maeneo yote yaliyobainishwa kwenye barua hiyo ili kuona namna ya kulitolea maamuzi na majibu rasmi.
Heche: Hakuna mazungumzo yatakayofanyika bila Mwenyekiti kuwa nje
Kaimu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche, amesema hakutakuwa na mazungumzo na Serikali hadi Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, awe huru na vikao halali vya chama vitoe uamuzi kuhusu hatua zinazofuata. Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 22, 2026, Heche pia amesisitiza kuwa CHADEMA haitashiriki mazungumzo bila kuwepo kwa mpatanishi huru wa kusimamia mchakato huo.
Kaizer Chiefs yamtangaza Adolf Mtasingwa kutokea klabu ya Azam
Klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini imethibitisha kumsajili kiungo mkabaji wa timu ya taifa ya Tanzania, Adolf Bitegeko, kutoka Azam FC kwa ada ambayo haijawekwa wazi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kikosi kwa msimu ujao. Bitegeko, (27) na aliyekuwa nahodha wa Azam FC, anakuwa mchezaji wa kwanza kutoka Tanzania kuichezea Kaizer Chiefs. Kabla ya kujiunga na Azam Januari 2024, aliwahi kuzichezea klabu mbalimbali nchini Iceland.
Wakili Malangalila: Mahakama Kuu imeamuru Mhadhiri wa UDOM aachiwe kwa dhamana
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, imeamuru Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedeki Kaijage, aachiwe kwa dhamana kuanzia Julai 21, 2026, wakati upelelezi wa tuhuma za uchochezi zinazomkabili ukiendelea. Uamuzi huo umetolewa na Jaji Joachim Tiganga wakati wa usikilizwaji wa Shauri Na. 15653/2026. Kaijage amekuwa akishikiliwa katika Kituo cha Polisi Chang'ombe kwa tuhuma za kuhamasisha maandamano yaliyojulikana kama "Sabasaba". Upande wa Serikali ulieleza mahakamani...
Wasira: Kila siku Lissu anaweka mapingamizi, ndio maana kesi inachukua muda mrefu
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Stephen Wasira amesema; "Mahakama inaendelea vizuri. Tena yeye Tundu Lissu, rafiki yangu, anaitumia mahakama kama shule ya sheria; yeye anajitetea mwenyewe. Kila siku anaweka mapingamizi, majaji wanaahirisha kwenda kutazama hicho alichokisema—ndio maana inachukua muda mrefu. Lakini kesi hii itaisha." "Sio lazima CHADEMA wakisema tunakubali, tutakubali mambo ya CHADEMA ambayo yana make sense...kwa sababu huwezi kutulazimisha kuachia mtu ambae kesi yake...
Mechi 5 za mwanzo kwa Yanga, Simba na Azam FC Msimu wa 2026/27
Baada ya mchezo wa Ngao ya Jamii Agosti 12, 2026 wa Dabi ya Kariakoo kati ya Yanga SC na Simba SC, timu hizo mbili zitaendelea na maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC 2026/2027. Yanga SC itasafiri kuelekea Ruangwa, Lindi, ambapo Agosti 15, 2026 itacheza dhidi ya Namungo FC katika mchezo wake wa mwanzo wa ligi. Kwa upande wa Simba SC, baada ya mchezo huo wa Ngao ya Jamii, kikosi hicho kitaelekea Bukoba mkoani Kagera kwa ajili ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar FC utakaopigwa Agosti 16...
Fahamu mambo mbalimbali kuhusu gari aina ya Subaru Forester
BAADHI YA MASWALI YALIYOULIZWA NA WADAU KUHUSU GARI HII Wakuu rafiki yangu mmoja yupo interested na hizi gari aina ya Subaru Forester lakini kabla hajaingiza maamuzi mzima mzima alitaka kujua yote ya husuyo hizi aina za haya magari. Stability zake, upatikanaji wa spare na mengine yote ambayo mtu yeyote angependa kuyajua.Huyu jamaa yupo mkoani na amejaribu kuangalia aina hizo hazipo na yeye yupo interested nayo kwa kuwa ni 4DW kulingana na maeneo anayoishi anahitaji mkoko wa namna hiyo. Kwa...
Meli ya mafuta yenye bendera ya Tanzania yatekwa nyara na maharamia wa Somalia
Meli ya mafuta yenye bendera ya Tanzania, MT ASANA, imetekwa na maharamia wanaoshukiwa kutoka Somalia katika pwani ya Yemen, kwa mujibu wa vyanzo vya usalama na maafisa wa eneo hilo. Tukio hilo lilitokea baada ya meli hiyo kuondoka Mukalla, Yemen siku ya Ijumaa. Baada ya kutekwa, meli hiyo ilipelekwa katika pwani ya Caluula, eneo la Bari kaskazini mashariki mwa Somalia, ambako inaendelea kushikiliwa na watekaji, kwa mujibu wa maafisa wa eneo la Puntland.
Bobi Wine appoints Nambeshe acting NUP President
National Unity Platform (NUP) President Robert Kyagulanyi Ssentamu, popularly known as Bobi Wine, has appointed Hon. John Baptist Nambeshe as the party’s Acting President, replacing Dr. Lina Zedriga Waru, whose four-month tenure has ended.
Mapfumo defends US$1 million Chivayo deal, says his principles remain intact
Chimurenga music legend Thomas “Mukanya” Mapfumo has defended his decision to accept a US$1 million performance offer from businessman Wicknell Chivayo, saying the deal does not mean he has abandoned his values, activism or support for ordinary Zimbabweans. The 81-year-old music icon has faced criticism from some fans and social commentators who accused him of compromising his long-standing reputation as a voice for social justice and human rights.
AZAKI: Serikali ya Tanzania imeilipa kampuni ya BGR Group Tsh. Bilioni 7.886 kuisafisha taswira ya nchi
Wawakilishi wa Asasi za Kiraia (AZAKI) Tanzania, Julai 16, 2026, wamesema kumekuwa na jitihada za kutumia njia za mkato kushughulikia changamoto za kisiasa na kiutawala nchini badala ya kuzingatia misingi ya katiba na utawala wa sheria. Wamedai kuwa kumekuwa na matukio ya utekaji, mateso, kuwekwa mahabusu kwa baadhi ya watu na vifo vinavyodaiwa kuhusishwa na mazingira ya kisiasa, huku wakisema hatua hizo zinalenga kunyamazisha sauti zinazotetea amani na uwajibikaji. Soma: AZAKI: Hali ya...
Dkt. Bana: Hamuwezi kuridhiana wakati Kiongozi mmoja wa kisiasa yuko Gerezani
Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Dkt. Benson Bana, amesema mchakato wa maridhiano hauwezi kuanza au kufanikiwa ikiwa bado kuna kiongozi wa kisiasa anayekabiliwa na kesi mahakamani, huku akisisitiza kuwa pande zote lazima zijiridhishe kwanza kabla ya kukaa meza moja. Dkt. Bana amesema ni vyema kusubiri hukumu ya mahakama kwa kuwa ndiyo chombo chenye mamlaka ya kutoa haki.
Sierra Leone: Serikali yafuta Mashtaka ya Uhaini dhidi ya Rais wa zamani, Ernest Bai Koroma
Serikali ya Sierra Leone imefuta mashtaka yote, yakiwemo ya uhaini, yaliyokuwa yakimkabili Rais wa zamani wa nchi hiyo, Ernest Bai Koroma, aliyekuwa akihusishwa na jaribio la mapinduzi ya serikali lililotokea mwaka 2023. Koroma, mwenye umri wa miaka 72, amekuwa akikanusha kuhusika na jaribio hilo la mapinduzi la Novemba 2023. Katika tukio hilo, watu wenye silaha walivamia ghala la silaha la jeshi na magereza kadhaa, ambapo wafungwa wapatao 2,000 walitoroshwa.
TLS, LHRC, Dk. Slaa wamburuza Mahakamani Waziri Katambi kwa kuzuia mikutano ya Kisiasa
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kwa kushirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Dk. Willibrod Slaa, wamefungua kesi ya kikatiba katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Tabora, wakipinga kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, kuhusu zuio la mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa. Mbali na Katambi, wadaiwa wengine ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).
Morogoro: Wananchi wapinga mauaji yanayofanywa na Askari wa Hifadhi
Ndugu na jamaa wa kijiji cha Kisaki mkoani Morogoro wameandamana na kutoa malalamiko mazito dhidi ya askari wa wanyamapori (maliasili) kwa tuhuma za kuwauwa kikatili wananchi wanaoingia msituni kutafuta riziki zao, kama vile kukata mbao. Mmoja wa wananchi, ameeleza kuwa vitendo hivyo vya ukatili vimekithiri na kuacha majonzi makubwa kwa jamii, huku akiongeza kuwa msituni kuna mafuvu na miili mingi ya binadamu wenzao waliopoteza maisha kwa kupigwa risasi na askari hao
Biashara ya genge inalipa sana, kinachokwamisha watu ni kuwekeza mtaji mdogo sana
Mdau amesema biashara ya kuuza genge ni mojawapo ya biashara nzuri na yenye faida, lakini changamoto inayowafanya wengi wasifanikiwe ni kuanza na mtaji mdogo sana. Ameeleza kuwa kuwekeza mtaji wa mfano wa shilingi 80,000 pekee kunafanya iwe vigumu biashara kukua, huku akisisitiza kuwa mafanikio yanahitaji uwekezaji wa kutosha na kuondoa hofu ya kupata hasara.
Back
Top Bottom