Featured content

Kesi ya uhaini ya Lissu yaahirishwa hadi Septemba 18, DCI, IGP na CDF wapo nje ya nchi
Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, imeahirishwa hadi Septemba 18, 2026, baada ya Mahakama kuelezwa kuwa mashahidi watatu, akiwemo DCI Ramadhani Kingai, CDF Jenerali Jacob Mkunda na IGP Camillus Wambura, wako nje ya nchi.
DRC | Wananchi waandamana kupinga Rais Tshisekedi kuongezewa muhula wa 3
Mamia ya waandamanaji walikusanyika katika mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Kinshasa, kupinga pendekezo la serikali la kufanya marekebisho ya Katiba ambayo yanaweza kumruhusu Rais Félix Tshisekedi, aliyechaguliwa mwaka 2019 na kuchaguliwa tena mwaka 2023, kugombea muhula wa tatu endapo marekebisho hayo yatapitishwa kupitia kura ya maoni. Takriban watu 10 wamekamatwa kufuatia maandamano hayo yaliyofanyika Septemba 15, 2026 jijini Kinshasa pamoja na Lubumbashi, hata baada...
Kundi la EPP katika Bunge la Ulaya lampendekeza Lissu kuwania Tuzo ya Sakharov
Wakati sisi tukimfungulia kesi za Uhaini mataifa ya Ulaya yanathamini mchango wake. Kati ya viongozi mashuhuri Duniani waliopata tuzo hii ni pamoja na Nelson Mandela, Malala Yousafzai, Nadia Murad, Denis Mukwege, Aung San Suu Kyi, na Václav Havel. ======= Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tundu Lissu amependekezwa rasmi kuwania Tuzo ya Sakharov ya Mwaka 2026, ambayo ndiyo heshima ya juu zaidi inayotolewa na Umoja wa Ulaya (EU) kwa watetezi wa haki za binadamu na uhuru...
Padri Kitima: Waliokosewa ni wananchi sio vyama, wao ndio waongoze mchakato wa Maridhiano
Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Dkt. Charles Kitima, amesema dhana ya maridhiano nchini inapaswa kuanza kwa kukiri na kukubali ukweli kuhusu matatizo yaliyopo. Akifafanua kuhusu maana ya maridhiano, amesema neno hilo linapaswa kueleweka kwa upana, akitumia mfano wa neno la Kiingereza “reconciliation”, ambalo kwa mtazamo wa Wakristo na Waislamu linahusisha kwanza hatua ya kukiri makosa kabla ya kufikia hatua ya kupatana. Padre Kitima amesema ili kufikia...
Dkt. Kijo-Bisimba: Haukuwa Uchaguzi, siku tumeruhusiwa kutoka tulikuta maboksi mitaani
Mkurugenzi mstaafu wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na mwanaharakati mkongwe, Dkt. Hellen Kijo-Bisimba, amehoji uhalali wa uchaguzi, akisema alichokiona siku hiyo hakikidhi viwango vya uchaguzi. Akizungumza Septemba 15, 2026, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Demokrasia Duniani, Dkt. Kijo-Bisimba amesema; "Mimi hofu yangu ni kwamba sikujua kama kweli palikuwa na uchaguzi. Kwa sababu hiyo siku ya uchaguzi, bahati nzuri nilikuwepo hapa nchini, na mimi sikuwa nimejiandikisha kwa...
Lutgard Kagaruki: Marekebisho ya katiba sio suala la hiyari ya kisiasa ni hitaji la dharula
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Kudhibiti Tumbaku Tanzania (TTCF), na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Lutgard Kokulinda Kagaruki, amesema changamoto za kiutawala na vikwazo katika ushiriki wa wananchi vilivyojitokeza wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2025 vimedhihirisha kuwa mfumo mzima wa utawala nchini unahitaji kufanyiwa marekebisho ya kina. Amesema marekebisho ya Katiba si suala la hiari ya kisiasa tena, bali ni hitaji la dharura, akisisitiza kuwa utawala...
Janeth Rithe: Mimi ni sadaka kwa wengine, kama wamejifunza kuua na sisi tunatakiwa kujifunza kufa
Akizungumza katika mahojiano na M & S Podcast yaliyorushwa Septemba 9, 2026, Mwenyekiti wa Ngome ya Wanawake wa Chama cha ACT-Wazalendo, Janeth Rithe, ameeleza kuwa mazingira ya sasa ya kisiasa nchini yanahitaji viongozi wenye kujitolea kama "sadaka" kuwa tayari kufa ikiwa una dhamira ya kuwa sauti ya wananchi. "Kwa hiyo sasa hivi ukiingia kwenye siasa ni ujikane nafsi, na uwe kweli una dhamira ya kutaka kuwatetea na kuwasemea watu. Lakini kama huna dhamira hiyo huwezi. Utakuwa unajawa...
Ado Shaibu: Yuko wapi aliyekuwa Makamu wa Rais, Dkt. Emmanuel Nchimbi?
Mbunge wa Tunduru Kaskazini, Ado Shaibu Ado, ametoa wito kwa familia ya Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Emmanuel Nchimbi kujitokeza hadharani na kuwahahakishia Watanzania kuwa yuko salama. Ado ametoa wito huo Septemba 10, 2026 wakati akizungumza katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika Kata ya Bugogwa, Mtaa wa Igomba huko Ilemela, Mwanza.
Utafiti: Kunywa Chai au Kahawa ya Moto sana inaweza kusababisha Saratani ya umio
Je, huwa unaagiza kahawa ya moto sana au unapenda chai ikiwa inachemka? Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Oxford wamegundua uhusiano kati ya unywaji wa vinywaji vyenye joto kali sana na saratani ya umio, yaani mrija unaounganisha koo na tumbo. Tabia za unywaji wa karibu watu milioni moja nchini Uingereza zilifuatiliwa, na matokeo yakaonyesha kuwa watu wanaokunywa vinywaji vyenye joto kali sana walikuwa na hatari iliyoongezeka mara tatu ya kupata saratani hiyo. Pia, mara ngapi mtu anakunywa...
IGP Wambura, DCI Kingai na CDF Mkunda waitwa kutoa ushahidi kesi ya Lissu
Mahakama Kuu kupitia Jaji Dunstan Ndunguru imekataa ombi la mshtakiwa Tundu Lissu la kuwaita baadhi ya mashahidi wa utetezi katika Kesi ya Uhaini Na. 19605/2025, likieleza kuwa ushahidi wao hauna umuhimu kwa kuwa jukumu la kuthibitisha kosa ni la Jamhuri. Hata hivyo, Jaji Ndunguru ameagiza kutolewa kwa wito rasmi (summons) kwa Mkuu wa Majeshi (CDF), Mkuu wa Polisi (IGP) na DCI ili wafike Mahakamani kutoa ushahidi wa utetezi, huku kesi hiyo ikiahirishwa hadi Septemba 11, 2026.
Mhadhiri wa UDOM aliyetuhumiwa kwa Ugaidi aachiwa huru
Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma imemwachia huru Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedek Kaijage, baada ya Serikali kueleza kuwa haina nia ya kuendelea na mashtaka yaliyokuwa yakimkabili, huku mahakama ikimwekea masharti ya mwenendo. Kaijage ameachiwa huru leo, Alhamisi, Septemba 10, 2026, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma, Denisi Mpelembwa baada ya Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Serikali, Jonathan Chuwa, kuiambia mahakama Serikali haina nia ya...
Daktari Bingwa wa Mloganzila, Conrad Agonza, anayedaiwa kumshambulia Trafiki afikishwa Mahakamani
Daktari bingwa wa magonjwa ya ndani katika Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dk Conrad Agonza Kahyoza amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni Dar es Salaam, leo Septemba 10, 2026, baada ya kukamatwa na polisi kwa tuhuma za kumshambulia askari wa Usalama Barabarani katika eneo la Lugalo, Dar es Salaam. Tukio hilo lilitokea Jumanne Septemba 8, 2026 saa 1:30 asubuhi katika Barabara ya Bagamoyo, Lugalo, wakati askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, F.8886 SGT Andrew...
Heche: Nilikamatwa na Kusomewa Shtaka la Ugaidi la Kuchoma Vituo vya Mwendokasi Kimara hadi Magomeni
Baada ya jana Septemba 9, 2026 Makamu Mwenyeekiti wa CHADEMA Bara, Joun Heche kupanda Kizimbani na kuanza kutoa ushahidi wake katika Kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyeekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu na leo tena anaendelea. Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam leo Septemba 10, 2026, huenda ikatoa uamuzi kuhusu pingamizi la Serikali katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu. Pingamizi hilo linahusu ombi la Lissu la kuwaita viongozi na maafisa...
Brenda: Hatukususia uchaguzi, tulitaka marekebisho ya Sheria na Uchaguzi wa Kidemokrasia
Shahidi wa nne katika kesi ya uhaini namba 19605/2025 inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa Chama hicho, Brenda Rupia, leo Septemba 8, 2026 ataendelea kutoa ushahidi wake wa utetezi dhidi ya Tundu Lissu. Jana Septemba 7, 2026, shahidi huyo alianza kutoa utetezi wake, ambapo Lissu alianza kwa kumuongoza kujibu maswali kwamba mkutano wa tarehe 3 Aprili ulihusu nini na nani aliyeuandaa. Katika...
Maghorofa ya Samia Kawe kugeuzwa AirBnB? Hivi hawaoni Janga la Makazi linalotishia Dar? Je, mlengwa ni nani?
Habari wakuu, majuzi nikiwa naperuzi insta nilikutana na tangazo la dalali la apartment ya AirBnB. Nilikuwa tayari nimeshapita, lakini nikastuka baada ya kugundua kuwa jengo lile ni la mradi wa Samia Housing Scheme uliopo pale Kawe. Swali likanijia mara moja: Hivi hizi nyumba tunawajengea kina nani hasa? Watalii, wafanyabiashara matajiri wanaopita Dar, au maharusi wanaotafuta sehemu ya kulala usiku wa harusi yao? Tusisahau kwamba Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linajenga kwa kodi zetu...
Masoud: Alishinda Ubunge, akapewa cheti, akanyang’anywa akapewa mwingine ambaye yuko Bungeni
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othuman Masoud, amesema uchaguzi wa Zanzibar haukuwa “smooth” kama baadhi ya watu wanavyodhani, akieleza kuwa kulikuwa na matukio mbalimbali ambayo chama chake, ACT-Wazalendo, kiliwasilisha malalamiko yake kwa Tume ya Uchaguzi. Soma pia >> Othman Masoud: Hakukuwa na Uchaguzi 2025, Vyombo vya dola kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi na CCM viliamua nani awe Mshindi Othuman amesema moja ya matukio yanayoonyesha mazingira ya uchaguzi huo ni kuwepo kwa...
Jaji Warioba: Amani haikuletwa na Bunduki na hutailinda kwa Bunduki
Akizungumza leo Septemba 7, 2026, kwenye Mkutano wa wa Kitaifa wa Kutafakari Hali ya Kisiasa Nchini uliondaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Jaji Mstaafu, Joseph Sinde Warioba amesema: "Kurudi kwenye amani ya kweli, ni lazima turudi kwenye misingi ile ya zamani. Tuwe na usawa, tusiwe na ubaguzi wa aina yoyote. Tutarudi kwenye misingi ya amani. Amani hailetwi na bunduki, na hutalinda amani kwa bunduki. Lakini kwa sasa tunafikiri bunduki ndiyo inaweza kulinda amani. Inaweza kuleta...
Imetimia Miaka 9 tangu Lissu ashambuliwe kwa risasi, uchunguzi umefikia wapi?
Wakuu, Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, ajeruhiwa kwa risasi. Kwa sasa wapo hospitali ya Mkoa, mjini Dodoma. Ameshambuliwa kwa risasi wakati akishuka nyumbani kwake Area D Mjini Dodoma, alikuwa akitokea Bungeni na alienda Nyumbani kula chakula cha mchana. Lissu amepigwa risasi 5, miguuni na tumboni. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema hali ya Mbunge huyo aliye hospitalini sasa ni mbaya...
Ramani mpya ya dunia, yaonesha ukubwa halisi wa Afrika
Umoja wa Mataifa umepiga kura ya kupitisha ramani mpya rasmi ya dunia iliyobuniwa kuonyesha ukubwa halisi wa kijiografia wa bara la Afrika na maeneo mengine ya kanda ya ikweta. Mabadiliko haya yanalenga kuchukua nafasi ya "Mercator projection" (ramani ya kale ya Mercator), ambayo imekuwa ikitumika kwa muda mrefu lakini imekuwa ikikosolewa kwa kupotosha vipimo—ikionyesha maeneo ya kaskazini mwa dunia (kama vile Ulaya na Marekani ya Kaskazini) kuwa makubwa zaidi kuliko yalivyo, huku...
Rais Duma: Unapoingia madarakani inaweza kukuchanganya na kukufanya ujione Mungu mdogo
Rais wa Botswana, Duma Boko, amezungumzia hatari zinazoweza kuambatana na madaraka ya kisiasa na jinsi kushika wadhifa kunaweza kumbadilisha kiongozi mtazamo wake kuhusu yeye mwenyewe. Akihojiwa na eNCA’s CheckPoint Podcast, amesema unapoingia madarakan inaweza kukuchanganya sana na kukufanya ujione kama nusu-mungu, na viongozi wengi hutumbukia kwenye mtego huo. Amesema kuwa viongozi wanaoingia madarakani wakiahidi kuwa tofauti na waliowatangulia wanaweza baadaye kujikuta wakitekwa na...
Back
Top Bottom