Jeshi la Polisi linawashikilia Watu 6 kwa kudaiwa kumuua Askari Polisi, Roland Mollel baada ya kumshambulia, tukio lililotokea katika Mtaa wa Mlimani, Kata ya Muriet, jana Aprili 15, 2026.
Kamanda wa Polisi Mkoa, SACP Justine Masejo amesema Roland alikuwa katika shughuli zake binafsi baada ya kazi, kulitokea taharuki iliyotokana na kusambaa maneno ya kundi la Watu wakidai eneo lao kuna wezi, marehemu akapita akiwa amebebwa katika bodaboda, kundi la Watu likawashambulia huku wakiwakimbiza.