Katibu Mkuu wa Chama cha CHAUMMA, Salum Mwalimu, ametangaza kujiondoa kwa muda katika nafasi yake ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizowasilishwa dhidi yake mbele ya Kamati Kuu ya chama hicho.
Katika barua aliyomwandikia Mwenyekiti wa Taifa wa CHAUMMA, Hashim Rungwe, Juni 30, 2026, Mwalimu amesema uamuzi huo unalenga kutoa nafasi kwa uchunguzi huru kufuatia tuhuma zilizojadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika Juni 29, 2026, katika makao makuu ya chama hicho, Kinondoni Biafra, Dar.