Featured content

Jaji Mkuu Masaju: Nisingependa Viongozi wa Kisiasa waingilie shughuli za Kisheria, wachukulieni hatua
Jaji Mkuu wa Tanzania, George Masaju akifungua Mkutano Mkuu wa Chama cha Madalali Juni 30, 2026 amesema hatarajii kuona viongozi wa kisiasa wakiingilia utendaji wa shughuli za Mahakama kwa kigezo cha nyadhifa walizonazo katika kamati za ulinzi na usalama za mikoa au wilaya.
Rungwe: Salmu Mwalimu aliingilia majukumu ya Mwenyekiti, Halmashauri Kuu imemtengua
Mwenyekiti wa Chama CHAUMMA, Hashimu Rungwe, ametangaza maamuzi ya Halmashauri Kuu ya chama hicho iliyoketi Juni 30, 2026, jijini Dar es Salaam. Katika kikao hicho, Halmashauri Kuu imemtengua rasmi Katibu Mkuu wa chama, Salum Mwalimu Juma, kuanzia tarehe hiyo ya kikao. Maamuzi hayo yamekuja baada ya kutathmini mwenendo mzima wa uongozi ndani ya chama huku Halmashauri Kuu ya CHAUMMA ikimemteua Benson Kigaila kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho.
Kigaila: Sheria haisemi vyama viombe kibali kufanya Mikutano au Maandamano, Polisi wanapewa taarifa tu
Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Benson Kigaila amesema tabia ya serikali kushiriki kuvunja sheria inatakiwa kupingwa na kila Mtanzania anayetaka utawala wa sheria, hadharani na sirini. Haya mambo lazima yapingwe kwa nguvu zote kwani yanahatarisha misingi ya demokrasia nchini. Kigaila amefafanua kuwa Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992 haitaki vyama kuomba kibali, bali kutoa taarifa ya saa 48 kwa Jeshi la Polisi ili liandae ulinzi na sio kuzuia mikutano.
Pendekezo: Iundwe 'Yanga Law', wanaokaidi vyumba vya kubadilishia nguo wapokwe alama 3
Mdau wa soka amependekeza kuundwa kwa sheria maalumu aliyoipa jina la 'Yanga Law' kuelekea msimu wa 2026/27 wa Ligi Kuu ya NBC ili kuimarisha nidhamu, ushindani na hadhi ya ligi. Amesema kutokana na matukio yanayojirudia ya baadhi ya klabu, hususan Yanga SC, kudaiwa kukaidi taratibu za matumizi ya vyumba rasmi vya kubadilishia nguo, kuna haja ya kuweka adhabu kali zaidi ili kukomesha tabia hiyo na kuondoa vitendo vinavyoonekana kushusha hadhi ya ligi.
Kocha wa Uholanzi Koeman ajiuzulu baada ya kutupwa nje Kombe la Dunia
Ronald Koeman amejiuzulu rasmi kama kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uholanzi baada ya timu hiyo kutolewa kwenye Kombe la Dunia 2026 katika hatua ya 32 bora kufuatia kufungwa na Morocco kwa mikwaju ya penalti. Koeman ametangaza uamuzi huo siku baada ya kipigo hicho kilichokatisha safari ya Uholanzi kwenye mashindano hayo.
Salum Mwalimu ajiuzulu kwa muda CHAUMMA kupisha uchunguzi
Katibu Mkuu wa Chama cha CHAUMMA, Salum Mwalimu, ametangaza kujiondoa kwa muda katika nafasi yake ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizowasilishwa dhidi yake mbele ya Kamati Kuu ya chama hicho. Katika barua aliyomwandikia Mwenyekiti wa Taifa wa CHAUMMA, Hashim Rungwe, Juni 30, 2026, Mwalimu amesema uamuzi huo unalenga kutoa nafasi kwa uchunguzi huru kufuatia tuhuma zilizojadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika Juni 29, 2026, katika makao makuu ya chama hicho, Kinondoni Biafra, Dar.
Mpina: ACT Wazalendo tunaenda mahakamani kupinga Sheria ya Fedha 2026
Naibu Waziri Mkuu Kivuli wa ACT Wazalendo, Luhaga Mpina, amesema chama hicho kimepanga kufungua kesi mahakamani kupinga baadhi ya vipengele vya Sheria ya Fedha wa mwaka 2026, kikidai kuwa vinaongeza mzigo wa kodi kwa wananchi wa kipato cha chini huku vikitoa misamaha kwa wawekezaji wakubwa.
Heche: CHADEMA haitafanya maridhiano na CCM bila mpatanishi wa kimataifa
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche Juni 25, 2026 kwenye mahojiano na kituo cha Redio, cha VOS amesema kuwa chama hicho hakiko tayari kuingia kwenye maridhiano yoyote na Chama Cha Mapinduzi (CCM) bila uwepo wa mpatanishi wa kimataifa (mediator) asiyekuwa na upande, akitolea mfano wa mifumo ya usuluhishi iliyowahi kutumika nchini Kenya na kwingineko duniani.
Katambi: Kitambulisho cha NIDA sio taarifa binafsi, ni Public
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amesema kutoa Kitambulisho cha Taifa (NIDA) unapotembelea nyumba ya kulala wageni hakumaanishi kuanika taarifa binafsi, kwani kitambulisho hicho si taarifa binafsi. Soma Pia: Waziri Katambi: Wamiliki wa Hoteli, AirBnB, Guest Houses na Lodge nchini wasajili wageni wote kwa kutumia kitambulisho cha NIDA Akizungumza Juni 29, 2026, jijini Dodoma alipokuwa akizungumza katika mahojiano na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Katambi amesema...
Chalamila: Kuna vijana wanataka kuchoma bandari kavu, kisa foleni
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amefanya kikao na viongozi wa mkoa huo pamoja na Mkoa wa Pwani kwa lengo la kutafuta suluhu ya kudumu ya foleni katika jiji hilo. Chalamila amebainisha kuwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika maboresho ya bandari, ukuaji wa idadi ya watu, na kuimarika kwa shughuli za kiuchumi havipaswi kugeuka kuwa mwiba na kero kwa wananchi.
Madeleka: Hakuna Sheria inayolipa Jeshi la Polisi mamlaka ya kutoa vibali vya mikutano ya vyama vya siasa
Wakili Peter Madeleka amesema kuwa hakuna sheria yoyote inayolipa Jeshi la Polisi mamlaka ya kutoa au kuzuia vibali vya mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa. Akifafanua kuwa, kwa mujibu wa sheria za nchi, jukumu la vyama vya siasa vinapotaka kufanya mikutano hiyo sio kuomba kibali, bali ni kutoa taarifa tu kwa jeshi hilo ili liweze kuratibu ulinzi na usalama.
Rais wa Soka Saudia, Al-Misehal ajiuzulu baada ya timu kutolewa Kombe la Dunia
Rais wa Shirikisho la Soka la Saudi Arabia, Yasser Al Mashal ametangaza kujiuzulu baada ya taifa hilo kutolewa katika hatua ya makundi ya Kombe la Dunia. Al Mashal ameeleza kuwa Saudia kutofuzu hatua inayofuata ni matokeo yasiyoendana na matarajio ya nchi yake.
Katambi: Wamiliki wa Hoteli, Airbnb, ‘Guest Houses’ na ‘Lodge’ wasajili wageni wote kwa vitambulisho vya NIDA
Leo bungeni Waziri wa Mambo ya Ndani, Patrobas Katambi ameagiza wamiliki wa nyumba zote zinazotoa malazi kwa wananchi kuhakikisha zinasajili wageni wote wanapata huduma kwa kutumia kitambulisho cha NIDA, vinginevyo watachukuliwa hatua. Katambi amesema 'Nitumie fursa hii, wamiliki wa hoteli zote, Airbnb, guest houses na lodge nchini, kuanza kusajili kila anayeingia mle ndani kwa kutumia vitambulisho vya NIDA. Wageni wote wanaoingia kwenye majiji, miji, wajisajili. Unapoenda kwenye hoteli...
Waziri Katambi apiga marufuku mikutano ya Siasa kwa Vyama vyote
Leo bungeni Waziri wa Mambo ya Ndani, Patrobas Katamb ameagiza Jeshi la Polisi kusitisha vibali vya mikutano ya siasa kwa kipindi kisichojulikana. Moto umekuwa mkali na uwanja umeinama kwa upande wa CCM hadi kuomba tena Msaada wa jeshi la polisi , ingawa wananchi tuliwaonya CCM kuwa vita hii ya kubishana na CHADEMA mtaangukia pua lkn walibisha. Waziri wa Mambo ya ndani, akiwa bungeni amesema ''Kwa sababu ya taharuki hizi ambazo zimekuwa zikiendelea, nitatumia fursa hii pia, Mheshimiwa...
Prof. Assad: Kesi yangu ya kutenguliwa iko Mahakama ya Rufani, Mwaka wa 6 haisikilizwi
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mstaafu, Mussa Juma Assad, ameonyesha wasiwasi wake kuhusu kuchelewa kusikilizwa kwa kesi yake iliyopo katika Mahakama ya Rufani, akisema kinachomshangaza ni kesi hiyo kufikisha mwaka wa sita bila kutolewa maamuzi.
Prof. Assad: Nikipigiwa simu ya maagizo, asubuhi yake nilikuwa naandika barua ya tulichokizungumza
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mstaafu, Mussa Juma Assad, amesema katika kipindi chake cha utumishi alikuwa akipokea simu za maelekezo kutoka kwa baadhi ya watu wakimtaka asifanye maamuzi fulani, lakini mara nyingi alisimamia alichokiamini kuwa sahihi. Aliongeza kuwa ilikuwa desturi yake kila alipopokea maelekezo ya namna hiyo, asubuhi yake aliandika barua rasmi kuweka kumbukumbu ya mazungumzo hayo na msimamo wake kuhusu suala husika.
Makonda: Tanzania ndiyo Baba na Mama wa demokrasia Afrika
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amewataka watu duniani kote kutotiririsha kauli kuwa Tanzania haina demokrasia, akisisitiza kuwa nchi hiyo ndiyo "baba na mama" wa demokrasia barani Afrika. Akizungumza bungeni Juni 22, 2026, Makonda alieleza kuwa mchango wa Tanzania katika kupokea na kuwatunza wapigania uhuru wa mataifa ya kigeni ndio ulioweka misingi imara ya ukombozi na demokrasia barani Afrika.
Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer ajiuzulu
Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, ametangaza kujiuzulu nafasi yake Jumatatu hii baada ya kukabiliwa na shinikizo la miezi kadhaa, hatua inayofungua njia kwa nchi hiyo kupata Waziri Mkuu wa saba katika kipindi cha muongo mmoja uliopita. Akihutubia nje ya Ofisi ya Waziri Mkuu (10 Downing Street), Starmer ambaye amekuwa madarakani tangu Julai 2024 alikiri wazi kuwa amepoteza uungwaji mkono kutoka kwa wabunge wa chama chake cha Labour.
Katambi: Nimetenga Tsh. Milioni 100 kuwalipa watoa taarifa za uhalifu nchini
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amesema Serikali imetenga Shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuwazawadia wananchi watakaotoa taarifa sahihi zitakazosaidia kubaini na kuzuia vitendo vya uvunjifu wa amani nchini. Amesema hatua hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano kati ya wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama katika kulinda amani, usalama na utulivu wa nchi.
Prof. Tibaijuka: Lissu kuendelea kusalia Gerezani haina afya, Nchi haiwezi kutulia bila maridhiano
Mwanazuoni na Waziri wa zamani, Profesa Anna Tibaijuka, amebainisha kuwa nchi haiwezi kupata utulivu wa kweli wa kisiasa ikiwa hakuna maridhiano ya dhati, huku akisisitiza kuwa kuendelea kusalia gerezani kwa Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, hakuna afya kwa ustawi wa taifa.
Back
Top Bottom