Featured content

Davido avaa koti lenye majina ya waliotekwa Nigeria akitumbuiza tamasha la FIFA
Msanii Davido amevutia hisia za wengi baada ya kuvaa koti lenye majina ya wanafunzi 39 na walimu saba waliotekwa nyara nchini Nigeria, wakati akitumbuiza kwenye tamasha la 'FIFA Countdown Concert' jijini Los Angeles, Marekani. Hatua hiyo imeonekana kama ishara kubwa ya kuwakumbuka waathirika na kupaza sauti kuhusu usalama wa watoto na walimu maeneo yenye migogoro.
Kumbukizi | RC Dkt. Kleruu alivyopigwa Risasi Siku ya Krismasi Isimani mwaka 1971
Mauaji ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Wilbert Andrew Kleruu, yanaendelea kukumbukwa kama moja ya matukio makubwa zaidi katika historia ya nchi. Kleruu, msomi na mtendaji mahiri wa serikali ya Mwalimu Nyerere, aliuawa kwa kupigwa risasi na mkulima Said Abdallah Mwamwindi siku ya Krismasi mwaka 1971 katika kijiji cha Mkungugu, Isimani, kufuatia mgogoro uliokuwa umeibuka kuhusu sera za vijiji vya ujamaa na umiliki wa mashamba.
Baada ya kukosa Kombe la Dunia, Mwamuzi wa Somalia Artan apewa Mechi ya UEFA Super Cup
Shirikisho la Soka Barani Ulaya (UEFA) limemteua mwamuzi wa kimataifa kutoka Somalia, Omar Abdulkadir Artan, kuchezesha fainali ya UEFA Super Cup kati ya Paris Saint-Germain (PSG) na Aston Villa, itakayofanyika Agosti 12 mjini Salzburg. Hatua hiyo inakuja siku chache baada ya Artan kuzuiwa kuingia nchini Marekani, hali iliyomfanya ashindwe kushiriki kama mwamuzi katika Kombe la Dunia 2026 licha ya kuwa miongoni mwa waamuzi waliokuwa wameteuliwa na FIFA.
Prof. Kitila: Tanzania haitakubali kupangiwa marafiki wala maadui
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo amesema ziara za Rais Samia Suluhu nje ya nchi zinalenga kutafuta washirika wa biashara na uwekezaji badala ya wafadhili, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa falsafa ya kuifungua nchi kiuchumi, kisiasa na kijamii. Akiwasilisha Bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2025 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2026/27, amesema Tanzania itaendelea kutafuta fursa za biashara na uwekezaji bila kuchagua upande.
Ufunguzi Kombe la Dunia 2026
Mexico itafungua Kombe la Dunia dhidi ya Afrika Kusini mjini Mexico City. Hii ni marudio ya mechi ya ufunguzi ya Kombe la Dunia 2010, ambapo timu hizi zilitoka sare ya 1–1 nchini Afrika Kusini. Jambo la kipekee ni kwamba Estadio Azteca maarufu "hekalu la soka" ni moja kati ya viwanja vya mpira wa miguu vyenye historia kubwa na ya kipekee zaidi duniani baada ya kuandaa mechi za Kombe la Dunia katika matoleo matatu tofauti: 1970, 1986 na sasa 2026.
Kesi ya Uhaini ya Lissu iliyopangwa kusikilizwa Juni 11 yaahirishwa hadi Julai 6, 2026
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa taarifa kuwa shauri la Maombi ya Jinai Na. 7440840/2026 kati ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na Mwenyekiti wa chama hcho, Tundu Lissu, ambalo lilipangwa kuendelea Juni 11, 2026, limeahirishwa. Kwa mujibu wa taarifa ya Mahakama ya Rufani ya Tanzania, shauri hilo sasa limepangwa kwa ajili ya Judgments, Rulings & Orders siku ya Jumatatu, Julai 6, 2026, saa 3:00 asubuhi.
Mwanaharakati wa Sudan Kusini adaiwa kutekwa Nairobi, Kenya
Athorbey Al-Gaddhaffy-Dit mwanaharakati wa kisiasa na mfichua maovu (whistleblower) anadaiwa kutekwa jijini Nairobi na watu wenye silaha, huku watetezi wa haki za binadamu wakihofia uwezekano wa kurudishwa nchini kwake Sudan Kusini kwa nguvu. Polisi wamemwambia mke wake kuwa Dit alitekwa na wanaume waliovaa barakoa waliokuwa wakitumia gari jeupe, alipokuwa akitoka katika Kasino moja jijini Nairobi.
Canada: Rubani ashtakiwa kwa kurusha ndege mara 900 kwa miaka 16 bila kuwa na leseni sahihi
Rubani wa zamani wa shirika la ndege la Air Canada, Geoffrey Wall mwenye umri wa miaka 59, ameshtakiwa na polisi kwa kufanya kazi kama kapteni wa ndege kwa miaka 16 bila kuwa na leseni sahihi. Inadaiwa kuwa alihudumu kama kapteni wa ndege kubwa za abiria kati ya mwaka 2009 na 2025 bila kuwa na leseni maalum inayohitajika kwa ndege hizo (Airline Transport Pilot License). Katika kipindi hicho, aliruka ndege zaidi ya mara 900 katika safari za ndani na nje ya Canada.
Kaimu Waziri wa Afya-Zanzibar: Hatuwezi Kuwatibu wasio Wazanzibari
Kaimu Waziri wa Afya Zanzibar, Saada Mkuya Salum amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haiwezi kugharamia matibabu kwa Watu wasio Wazanzibar. Saada ametoa kauli hiyo Juni 8, 2026 wakati akijibu hoja kwenye Baraza la Wawakilishi Zanzibar kupitia vikao vinavyoendelea vya kujadili bajeti mbalimbali. “Mtu ambaye sio Mzanzibar anakwenda katika hospitali zetu anaonesha matibabu kadi, pili Watu kuzuiwa nadhani nilitoa maelezo sana, sio ZHF inaanza bali inaendelea kuwasajili wengine ambao sio...
Iran yadai FIFA imefuta tiketi za mashabiki wake Kombe la Dunia Marekani
Shirikisho la Soka la Iran (FFIRI) limesema kuwa FIFA au mamlaka za Marekani zimeondoa mgao wa tiketi uliokuwa umetengwa kwa mashabiki wa Iran kwa mechi zote tatu za hatua ya makundi zitakazochezwa Marekani. FFIRI ilieleza kuwa tayari ilikuwa imeanza mchakato wa kuuza tiketi hizo kwa mashabiki wake, na baadhi yao walikuwa tayari wamepanga safari za kuhudhuria mechi hizo.
Mahakama Kuu yaamuru Gachagua kulipwa fidia ya Tsh. Bilioni 1 kwa kuondolewa Madarakani
Mahakama Kuu imeiamuru Seneti ya Kenya kumlipa aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua fidia ya kikatiba ya Ksh. 50 Milioni (zaidi ya Tsh.Bilioni 1), baada ya kubaini kuwa haki yake ya kusikilizwa kwa haki ilikiukwa wakati wa mchakato wa kumwondoa madarakani (impeachment) uliomwondoa ofisini Oktoba 2024.
Mwamuzi wa Somalia azuiwa kuingia Marekani, kuchezesha Kombe la Dunia 2026
Mwamuzi mashuhuri wa soka kutoka Somalia, Omar Artan, amezuiwa kuingia Marekani licha ya kuwa miongoni mwa waamuzi 52 walioteuliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kuchezesha mechi za Kombe la Dunia 2026 litakalofanyika nchini Marekani, Canada na Mexico. Artan, ambaye angekuwa Mwamuzi wa kwanza kutoka Somalia kuchezesha fainali za Kombe la Dunia, alizuiwa kuingia nchini humo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Miami na kurejea Istanbul, Uturuki, ambako amekuwa akiishi hivi sasa.
Said Issa: CHADEMA imekiuka Katiba kunifukuza Uanachama
Said Issa Mohammed, aliyefukuzwa uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa madai ya kukiuka katiba, kanuni na miongozo ya chama, amesema uamuzi huo ni kinyume na katiba ya chama hicho. Hatua ya kumfukuza ilipitishwa na Kamati Tendaji ya Kanda ya Pemba baada ya kuhusishwa na kufungua kesi dhidi ya bodi ya wadhamini na Katibu Mkuu wa CHADEMA, shauri ambalo baadaye lilitupiliwa mbali na Mahakama Kuu kutokana na kasoro zilizobainika.
Naibu Waziri - Hassan: Wanaofanya kazi Hoteli za Zanzibar si Wazawa, tufanye Mapinduzi
Naibu Waziri wa Vijana, Ajira na Uwezeshaji, Zanzibar Hassan Khamis Hafidh, akichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Vijana katika Baraza la Wawakilishi Juni 6, 2026, alisema licha ya kuwepo kwa hoteli 1,184 zilizosajiliwa Zanzibar, idadi kubwa ya wafanyakazi katika baadhi ya hoteli hizo si wazawa inabidi tufanye Mapinduzi.
Nigeria: Mahakama yapiga marufuku Wabunge kutumia Tsh. Bilioni 212 kununua magari na kulipana marupurupu
Jaji wa Mahakama Kuu ya Lagos, Yellim Bogoro, Mei 6, 2026 amebatilisha mpango wa Bunge la Nigeria wa kutumia Naira Bilioni 110 (Tsh. Bilioni 212) kununua magari ya kifahari na kulipana marupurupu, kufuatia kesi iliyofunguliwa na taasisi ya Socio-Economic Rights and Accountability Project (SERAP) Mwaka 2023. Jaji Bogoro alisema matumizi hayo ya fedha yalikuwa makubwa kupita kiasi na yalilenga kuwanufaisha moja kwa moja viongozi walioyaidhinisha
Bishop Kaziimba Slams Govt Over Withdrawn Medical Intern Allowances
The Archbishop of the Church of Uganda, Most Rev. Stephen Samuel Kaziimba Mugalu, has strongly criticized government over its decision to withdraw allowances for medical interns, describing the move as unfair and a risk to Uganda’s already strained health system. Speaking during a Sunday service at All Saints’ Cathedral in Kampala, Archbishop Kaziimba questioned government spending priorities, arguing that it was unreasonable to cut funding for frontline health workers while maintaining...
Atwine: Uganda is Open to Treating American Ebola Patients
Ministry of Health permanent Secretary, Dr. Diana Atwine, has revealed that Uganda would be willing to treat American Ebola patients if requested by the United States, highlighting the country's growing reputation in Ebola management and response. Speaking in an interview with NTV, Dr. Atwine disclosed that the U.S. government initially approached Uganda with a proposal to have American citizens infected with Ebola treated in the country. However, before Uganda could formally respond...
Rais Samia: Tanzania haiko kwenye Vikwazo vyovyote
Rais Samia Suluhu amesema Tanzania haiko kwenye vikwazo vya kimataifa (sanctions) na kwamba Serikali inaendelea kujipanga kuharakisha maendeleo ya nchi. Akijibu swali kuhusu madai ya kuwepo kwa vikwazo dhidi ya Tanzania, alisisitiza kuwa hakuna hatua zozote za aina hiyo zinazoikabili nchi kwa sasa. Kauli hiyo ameitoa wakati akiwa na Rais wa Urusi, Vladimir Putin, katika Kongamano la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF’26) lililofanyika St. Petersburg, Urusi, tarehe 5 Juni 2026
Nchimbi: Rais Samia amekwenda kuliwakilisha Taifa Urusi na Mamlaka ya Urais amenikabidhi
Makamu wa Rais Emmanuel Nchimbi amesema Rais Samia Suluhu amekwenda Urusi kuliwakilisha Taifa, huku mamlaka ya urais yakikabidhiwa kwake kwa mujibu wa Katiba. Kauli hiyo ameitoa Juni 5, 2026, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani jijini Dodoma. Nchimbi amesema waandaaji walitamani Rais Samia awe mgeni rasmi wa tukio hilo kutokana na umuhimu wake, lakini ratiba zake za kitaifa na kimataifa zilifanya isiwezekane kushiriki.
Ufafanuzi wa Serikali kuhusu Kura ya Kamati za Bunge la Ulaya (EU) dhidi ya Tanzania
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imesema kura iliyopigwa katika Kamati ya Mambo ya Nje na Kamati ya Maendeleo ya Bunge la Ulaya kuhusu Mpango wa Ushirikiano wa Maendeleo kati ya Umoja wa Ulaya na Tanzania bado si uamuzi wa mwisho. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Juni 3, Wizara imefafanua kuwa mchakato huo bado unaendelea na mapendekezo hayo yanapaswa kuwasilishwa kwenye kikao cha Bunge zima la Ulaya kwa ajili ya mjadala na maamuzi ya mwisho mwezi huu.
Back
Top Bottom