KUHUSU KUANZISHWA KWA WILAYA YA TANGANYIKA
Mhe. Waziri tunakupongeza kwa kusaidia kuanzishwa kwa Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi, imekuwa msaada mkubwa sana hasa kwa sisi wakazi wa Karema,Kabungu na Mishamo ambapo umbali wa kupata huduma umepungua kutoka kilometa 160 kutafuta huduma wilayani.
Pamoja na tamko lako kwa vyombo vya habari,Mhe. tusaidie ofisi ya wilaya ya Tanganyika ianze,tuletewe watumishi na mkoa ili huduma zetu ziishie pale na anapobidi Mkuu wa Wilaya yule wa Mpanda atakuwa anatusaidia wakati serikali ikiendelea na hatua za uteuzi..Mpaka sasa tunahangaika kwani Mkoa wa Katavi haujafanya juhudi zozote za kuianzisha wilaya hiyo tangu serikali itangaze,tunajiuliza kwanini tunaendelea kuteseka kutafuta huduma wilaya ya mpanda iliyoko manispaa huku nauli ni shilingi elfu kumi na mbili mpaka kufika huko na muda mwingine unaambiwa uje kesho kuna vikao?
Mhe.Waziri Simbachawene na Katibu Mkuu tusaidieni kutoa kero hii kwani hakuna gharama kubwa kuanzisha ofisi hiyo,tunateseka na kuonewa sana,cheti cha kuzariwa ni elfu kumi,nauli kwenda na kurudi ni 24,000 bado utaambiwa uje kesho matokeo yake mpaka upate cheti au shida nyingine ni unakuta umetumia zaidi ya elfu 80 na bado kulala guest.
Naomba mliangalie kwa haraka jambo hili mtusaidie sababu mkuu wa mkoa wetu yuko kimya na hana habari licha ya kumweleza kupitia katibu wake mara nyingi
Watiifu kwa Serikali,
Wakazi wa Karema na Mishamo
Tunashukuru