Mzibua Vyoo
Senior Member
- Nov 8, 2023
- 159
- 355
Ahsante sana.Yeye ndiye
Bibi atafurahi sana kumwona mkata sanda alivyo. Anatusimuliaga tu yeye mwenyewe hajui alivyo. Ngoja nikamwonyeshe picha
Ahsante sana.Yeye ndiye
SwadaktaAhsante sana.
Bibi atafurahi sana kumwona mkata sanda alivyo. Anatusimuliaga tu yeye mwenyewe hajui alivyo. Ngoja nikamwonyeshe picha
Jamii forums humu kuna elimu ya kila aina, huwezi amini huyu ndege leo ndio namsikia. Ngoja nimfatilie zaidini ndege Wa porini, adimu sana kumuona, aña rangi nyeusi na midomo mikubwa myekundu. Mbeya hujulikana kwa jina LA bututu. Akilia nyumbani kwenu mtaandamwa na mikosi maisha yenu yote
Mv LIEMBA itapendeza zaidi.Ziwa Tanganyika linasifika sana kwa urefu Wa kina chake, dagaa watamu wasio na mchanga, samaki aina ya migebuka, meli ya MV Lihemba na fukwe zake nzuri zenye mchanga mweupe zinazozungukwa na milima yenye uoto mbichi Wa kijani kibichi.
Mbali ya sifa hizo pia Ziwa Tanganyika linasifa nyingine tofauti kwenye ulimwengu Wa kiroho. Ziwa Tanganyika ni mlango Wa kuzimu.
Wachawi wote NGULI Wa Sumbawanga, Kigoma na Congo ambayo zamani ilijulikana kama Zaire hutoka katika ziwa hili.
Uchawi Wa Gamboshi umetokea ndani ya ziwa hili. Uchawi Wa Wamanyafu nao mizizi yake ni kwenye hili ziwa.
Ili kuweza kwenda kuzimu unahitajika kuwa na mtaalam mzoefu ambaye atakuombea kibali cha kwenda huko.
Miongoni mwa mahitaji muhimu ya safari yako ni mayai saba viza, mbuzi mweupe au mweusi asiye na doa wala baka lolote, kucha za bundi, manyoya ya shingoni ya kipanga Aziz na vitu vingine utakavyoambiwa na kiongozi wako.