mpenda njaa
Member
- Jan 29, 2016
- 24
- 1
kuzimu ndio nini
Mkuu,huyu sio yule analiaga machozi ya damu???..na akilia hapo alipolilia Kama ni mti unakaukaAsante sana ngoja nikamsake
Mkuu,huyu sio yule analiaga machozi ya damu???..na akilia hapo alipolilia Kama ni mti unakauka
Picha haifunguki mkuu
Daah..!Picha haifunguki mkuu
Unabisha nini hata huko kwenye bible yako vituko vya uchawi vipo huyu anasimulia kilichopo mbona unajihami hautaki tujue dunia ilivyo ili tufanye maamuzi sahihi usizuie elimu na watu watambue kuwa kuna ulimwengu zaidi ya huu.Ndo mana hatuendelei na mauaji ya vikongwe na zeruzeru hayaishi kwa ajili ya watu km nyie wenye kushindwa kuyaona yaonekanayo na kujifanya mnaujua ulimwengu wa kiroho. Mmekaa kuogofya wenzenu kwa kusingizia mnauwezo wa kuvunja nguvu za kuzimu. Hebu waseme wengine lkn hata wakristo ambao tunaamini Yesu alishuka kuzimu na kumchakaza shetan bado tunadanganyika. Hebu fungueni macho IWENI NA IMANI mwamini kwanza Kristo Yesu naye atakutendea na si kungoja eti akutendee ndo umwamini.... Mnanikera na mazingaombwe yenu basi tu....
Mkuu sijawahi kumuona huyu mdudu..kwa lugha ya kwetu anaitwa nguumaakilia anatoa chozi za damu!!
Miaka si mingi nyuma, ukiwa na kipara wewe ni dili Ziwa Tanganyika. Wenye kipara walipotea katika mazingira ya kutatanisha na miili yao ilipatikana ikiwa haina vichwa.NKwa sifa hizo za L.TGK natafuta mwenyeji wa huko awe Guide wangu nikatembee!!
Kwetu Kilimanjaro wana msimu wao wa kuja, akikaa mahali huwa wakati wa kuondoka hupiga kelele.mshana jr huyu bututu yeye ni mkubwa kuliko bundi yaan yeye anafanana na tai sema tai ni mkubw kidogo. Huyu ndege ana miguu mirefu na anarangi nyeusi na mdomo wake ni mrefu,mwekundu.
Na anaonekana mara chache sana tofauti na bundi
Mbali na migebuka umesahau kuhe au kuku wa ziwaniZiwa Tanganyika linasifika sana kwa urefu Wa kina chake, dagaa watamu wasio na mchanga, samaki aina ya migebuka, meli ya MV Lihemba na fukwe zake nzuri zenye mchanga mweupe zinazozungukwa na milima yenye uoto mbichi Wa kijani kibichi.
Mbali ya sifa hizo pia Ziwa Tanganyika linasifa nyingine tofauti kwenye ulimwengu Wa kiroho. Ziwa Tanganyika ni mlango Wa kuzimu.
Wachawi wote NGULI Wa Sumbawanga, Kigoma na Congo ambayo zamani ilijulikana kama Zaire hutoka katika ziwa hili.
Uchawi Wa Gamboshi umetokea ndani ya ziwa hili. Uchawi Wa Wamanyafu nao mizizi yake ni kwenye hili ziwa.
Ili kuweza kwenda kuzimu unahitajika kuwa na mtaalam mzoefu ambaye atakuombea kibali cha kwenda huko.
Miongoni mwa mahitaji muhimu ya safari yako ni mayai saba viza, mbuzi mweupe au mweusi asiye na doa wala baka lolote, kucha za bundi, manyoya ya shingoni ya kipanga Aziz na vitu vingine utakavyoambiwa na kiongozi wako.
Buha tunamwita gihugugu.Huyo ndege SUMBAWANGA tunamwita tutu!!
Ni adimu sana kuonekana, Lakini nilizoea kumuona na kusikia sauti yake mara moja kwa mwaka..
Duuuh !! Mkuu hatari umenitisha!!Miaka si mingi nyuma, ukiwa na kipara wewe ni dili Ziwa Tanganyika. Wenye kipara walipotea katika mazingira ya kutatanisha na miili yao ilipatikana ikiwa haina vichwa.
Umemfuga?Asante sana ngoja nikamsake