Eng. Y. Bihagaze
JF-Expert Member
- Sep 8, 2011
- 1,487
- 913
Mawazo Bora ndani ya mawazo Bora ni uchakachuaji
nakumbuka tulipokuwa shule, kwenye ile elimu ya sekondari kubwa ya miaka miwili, mkaka mmoja ambaye mara zote alipenda group discussion ambayo ladies wako kibao, yeye alijifanya mtaalam sana wa hesabu za minyororo, na mkipata kipande cha swali na mkakukuruka nalo kwa muda na kupata jibu, yeye huchomoka akajitenga pembeni na kukukuruka nalo zaidi ili tu apate njia nyingine mbadala wa kulifanya swali hilo hata kama njia yake ni ya kubuni ili mradi jibu analijua basi ataungaunga mpaka nae aonekane kidume flan wa mafiga hayo yaliyoitwa mase au mets au 'nyuma ya nyumba' (backhouse). Basi akishajitengenezea njia yake anavamia kwenye group ambapo nyie that time mmeshasolve mafiga kama kumi hivi..utaskia.. 'eheee nimeshapata njia nyingine ya kufanya lile swali'.. basi atawabugudhi mpaka awaonyeshee na sometimes anasahau anarudi kuundaunda jibu anakuja tena.. yaaani kero tu.. hatimae aliruka na Div Zero ukingoni mwa shule..
samahani Mwanakijiji .. sasa nadhani jamaa yetu huyu mnaweza kuwa mnafanana fanana kimtazamo.. Wabunge leo wameweka Historia ya kuthubutu, hata kama si kweli kiranja huyu wa mawaziri atang'oka, ila hatua hii ni ukomavu wa uthubutu ambao kwa miongo mingi ya uhai wa Bunge ZOTOTO haikuwahi kufikia. Ingepongezwa hatua kama hii na kuweka imani kwamba kuna hatua zaidi hapo baadae inaweza kuchukuiwa. ukisema hatua hii ifie mkononi utakuwa na udhaifu wa kuwaza..
ungeanza na Kichwa cha habari kwamba PELEKA hoja ila kuwe na strategy baadae ya desh..........desh........ na desh........... hapo ungeeleweka ila ulipotumia neno USIPELEKE.. hapo ndipo uzi wako ulipopotokea mkuu.. si kila shambulio au si kila pambano unalenga ushindi, sometime unapima nguvu ya adui.. ukimuona adui yuko kimya unarusha bomu moja kupima upepo, ukiona linajibiwa na makombora ya kufa mtu ujue hapo usiguse tangaza hali ya amani haraka urudi ukajipange upya.. kama huamini angalia masumbwi, unamkuta mtaalam anaanza kurusha kikonde kwa mkono wa kushoto anapima mtikisiko wa adui na kufanya tathimini yakinifu kwamba akivurumsha konde la kulia itakuwaje..
Bravo wabunge.. sogezeni ukuni Jumatatu .. kisha serikali ibaki ikitarajia huruma ya wabunge wao wa CCM ambao wengine wako kikazi zaidi na ukichukulia kura ni za siri, sipati picha itakuwaje..
nakumbuka tulipokuwa shule, kwenye ile elimu ya sekondari kubwa ya miaka miwili, mkaka mmoja ambaye mara zote alipenda group discussion ambayo ladies wako kibao, yeye alijifanya mtaalam sana wa hesabu za minyororo, na mkipata kipande cha swali na mkakukuruka nalo kwa muda na kupata jibu, yeye huchomoka akajitenga pembeni na kukukuruka nalo zaidi ili tu apate njia nyingine mbadala wa kulifanya swali hilo hata kama njia yake ni ya kubuni ili mradi jibu analijua basi ataungaunga mpaka nae aonekane kidume flan wa mafiga hayo yaliyoitwa mase au mets au 'nyuma ya nyumba' (backhouse). Basi akishajitengenezea njia yake anavamia kwenye group ambapo nyie that time mmeshasolve mafiga kama kumi hivi..utaskia.. 'eheee nimeshapata njia nyingine ya kufanya lile swali'.. basi atawabugudhi mpaka awaonyeshee na sometimes anasahau anarudi kuundaunda jibu anakuja tena.. yaaani kero tu.. hatimae aliruka na Div Zero ukingoni mwa shule..
samahani Mwanakijiji .. sasa nadhani jamaa yetu huyu mnaweza kuwa mnafanana fanana kimtazamo.. Wabunge leo wameweka Historia ya kuthubutu, hata kama si kweli kiranja huyu wa mawaziri atang'oka, ila hatua hii ni ukomavu wa uthubutu ambao kwa miongo mingi ya uhai wa Bunge ZOTOTO haikuwahi kufikia. Ingepongezwa hatua kama hii na kuweka imani kwamba kuna hatua zaidi hapo baadae inaweza kuchukuiwa. ukisema hatua hii ifie mkononi utakuwa na udhaifu wa kuwaza..
ungeanza na Kichwa cha habari kwamba PELEKA hoja ila kuwe na strategy baadae ya desh..........desh........ na desh........... hapo ungeeleweka ila ulipotumia neno USIPELEKE.. hapo ndipo uzi wako ulipopotokea mkuu.. si kila shambulio au si kila pambano unalenga ushindi, sometime unapima nguvu ya adui.. ukimuona adui yuko kimya unarusha bomu moja kupima upepo, ukiona linajibiwa na makombora ya kufa mtu ujue hapo usiguse tangaza hali ya amani haraka urudi ukajipange upya.. kama huamini angalia masumbwi, unamkuta mtaalam anaanza kurusha kikonde kwa mkono wa kushoto anapima mtikisiko wa adui na kufanya tathimini yakinifu kwamba akivurumsha konde la kulia itakuwaje..
Bravo wabunge.. sogezeni ukuni Jumatatu .. kisha serikali ibaki ikitarajia huruma ya wabunge wao wa CCM ambao wengine wako kikazi zaidi na ukichukulia kura ni za siri, sipati picha itakuwaje..