Zitto usipeleke hoja Jumatatu; be strategic...

Nadhani Zitto anganza na kutafuta ushawishi wa kura za kuto kuwa na imani na spika halafu akipatikana mtu kama Sita pale kwenye kiti suala la kupiga kura za kutokuwa na imani na PM pamoja na boss wake ni kama kumsukuma mlevi na hapo ndio bunge litavunjwa kiulaini.
 
Ikumbukwe pia kuwa hoja ya kumshtaki Rais chini ya article 46 ni RAHISI zaidi kwani nayo inahitaji kura 70 kuweza kuletwa mezani na sababu za kumshtaki Rais Bungeni ni za chini kidogo - mojawapo ni kuwa amedhalilisha ofisi ya Urais! Nimesema mahali pengine kuwa kutokuwa na imani naWaziri Mkuu ni kutokuwa na imani na rais hivi viwili kwa mfumo wetu havitenganishwi. Wote ambao wameunga mkono kwa kutia sahihi kura 70+ ina maana hawana imani na rais hakuna tafsiri nyingine. Kwa vile hili ni kweli ni muhimu basi kwenda moja kwa moja for the "jugular" yaani kuleta mashtaka dhidi ya Rais katika kikao kijacho!

BIG POINT Mzee Mwanakijiji......................tunachohitaji ni kumwondoa JK na wala siyo PM.......tulimwondoa Lowassa na baadhi ya mawaziri na matatizo bado yako palepale...............sasa anayefaa kuondoka ni JK.....................ashitakiwe sasa khalafu mengineyo yatafuata................nchi hii maisha yamekuwa magumu kupita kiasi na ni yeye tu wa kushikishwa adabu........
 
....With all due respect to Mwanakijiji, nasikitika kuwa hiki ndicho nilichokiona kwenye hoja yake hii, na endapo Zitto atadanganyika kuifuata hoja ya Mwanakijiji, then mwisho wa siku ategemee matokeo yake kuwa "zero" kama ilivyotokea kwa rafiki yako, go Zitto go...

I am 99% right... don't doubt me.
 
Short-term apeleke. Long-term asipeleke.

A qstn: btn CHOICE and STRATEGIES what should come first here?
 
BIG POINT Mzee Mwanakijiji......................tunachohitaji ni kumwondoa JK na wala siyo PM.......tulimwondoa Lowassa na baadhi ya mawaziri na matatizo bado yako palepale...............sasa anayefaa kuondoka ni JK.....................ashitakiwe sasa khalafu mengineyo yatafuata................nchi hii maisha yamekuwa magumu kupita kiasi na ni yeye tu wa kushikishwa adabu........

Mkuu hiyo sababu ya kuidhalilisha ofisi ya Rais imekaa vibaya; sijui mtu atai prove vipi na kumfanya Spika akubali hoja kujadiliwa. Hiyo ndio nyepesi kulinganisha na zingine. Lakini kwa Waziri Mkuu kuna hii ya kushindwa kuisimamia serikali. Hiyo iko wazi kama mawaziri wanashutumiwa na kutuhumiwa kwa wizi si ina maana hawasimamiwi vizuri! Msimamiaji wao kashindwa na kwa mujibu wa Katiba msimamiaji ni Waziri Mkuu. Zitto ameona kitu ndio maana akataka aanze kuimong'onyoa serikali kuanzia shinani asikimbilie kwenye mzizi kwa kuwa mzizi ni mgumu kidogo kulinganisha na shina na matawi yake. Mizizi ikikosa hewa na chakula inaweza kunyong'onyea. Hiyo sababu ya kusimamia ingekuwa pia ndiyo mojawapo ya sababu za kumshtaki Rais bungeni mbona Zitto angeenda moja kwa moja tu na kutafuta saini 70 kwa ajili ya kumshtaki Rais.
 
Mi nadhani wacha tuanze na hili tumbo joto la waziri mkuu kwanza, ili watanzania waone kama haya mambo yanawezekana...unajua watanzania wanatakiwa wafumbuliwe macho kwanza
 
lakini zitto si alitoa ultimatum;? kwamba mpaka kufika J3 kama mawaziri waliotajwa na CAG hawajajiuzulu atapeleka hoja bungeni? sasa si wamejiuzulu!

Wako wapi waliojiuzulu? na kama wamejiuzulu, jee Rais aliyewateua kakubali? Tafakari, usisikie udaku wa JF ukajuwa ndio ukweli.
 
Kaka au Dada (sielewi ipi sahihi) unaejiita MzeeMwanakijiji, ngoja chama chako cha CCK ndio ukipe ushauri huo. Zitto anapeleka Jumatatu na yeye anakijuwa akifanyacho zaidi yako. Ushauri wako hauna mshiko.

Now, Kikwete akipenda just to outplay everybody atatangaza tu kuvunja baraza na akaunda baraza jipya chini ya PInda huyo huyo. Halafu itabidi ipigwe kura ya kumkubali kama waziri mkuu (namna nyingine ya kuwalazimisha watu kupiga kura ya kuwa na imani naye au la).. It is a war, na vita vinapiganwa kwa strategy! Thats all I'm saying. Hii hoja ikipelekwa j'tatu the oppossion WILL lose the argument ya change.

Mkuu Ribosme, soma vizuri hayo maelezo ya mwisho ya Mwanakijiji. Mimi naona yana uzito fulani hasa hapo kwenye red. Tafakari.
 
I am 99% right... don't doubt me.

...Ni kweli kabisa, upo sahihi sio kwa 99% bali ni kwa 100% kabisa lakini ni kwenye "ulimwengu wa ndoto" tu usiowezekana katika mazingira ya Tanzania ya sasa, naamini unaijua hii reality vizuri sana lakini unapinga tu for the sake of debating kama class mate wa Salma2015....

Mawazo Bora ndani ya mawazo Bora ni uchakachuaji

nakumbuka tulipokuwa shule, kwenye ile elimu ya sekondari kubwa ya miaka miwili, mkaka mmoja ambaye mara zote alipenda group discussion ambayo ladies wako kibao, yeye alijifanya mtaalam sana wa hesabu za minyororo, na mkipata kipande cha swali na mkakukuruka nalo kwa muda na kupata jibu, yeye huchomoka akajitenga pembeni na kukukuruka nalo zaidi ili tu apate njia nyingine mbadala wa kulifanya swali hilo hata kama njia yake ni ya kubuni ili mradi jibu analijua basi ataungaunga mpaka nae aonekane kidume flan wa mafiga hayo yaliyoitwa mase au mets au 'nyuma ya nyumba' (backhouse). Basi akishajitengenezea njia yake anavamia kwenye group ambapo nyie that time mmeshasolve mafiga kama kumi hivi..utaskia.. 'eheee nimeshapata njia nyingine ya kufanya lile swali'.. basi atawabugudhi mpaka awaonyeshee na sometimes anasahau anarudi kuundaunda jibu anakuja tena.. yaaani kero tu.. hatimae aliruka na Div Zero ukingoni mwa shule...

...Katika hoja hii, atleast approach ya Zitto inaweza kuleta matokeo chanya lakini approach yako ni kama "the bridge to NoWhere"...
 
Napenda kuwakumbusha wana bodi, tusidhani CCM nao wamelala kwenye hili! Kama kweli mawaziri wameanza kujiuzuru, hoja itapoteza mashiko!!

Nina uhakika kura 178 za kumuondoa PM hazitapatikana...wait and see.
 
Binafsi naamini kama kweli mawaziri watajiuzulu inavyosemwa itaharibu kwa kiasi hoja ya kutikuwa na imani na waziri mkuu. Think about it!

hapa kunahitajika plan B iwepo ambayo lazima ifikie lengo la awali na isije kujikuta inaishia hewani na kukosa maana halisi .. maana baada ya kujiuzuru kila mtu ataamini wanatakiwa wapewe muda kwa ajili ya kuona matokeo ya hayo mabadiliko lakini bado hao watakaochaguliwa hawatasaidia chochote kwani kwenye hizi wizara kuna makatibu wakuu n.k ... je hili watu wanalitazamaje?
 
ndugu MWANAKIJIJI kwa kiasi una hoja japokuwa unasahau kuwa kuelekea 2015 CCM ina wadau ambao hawana cha kupoteza(waadilifu wasiotaka kugombea tena) na ambao wakichekelea watapata hasara(vijana waadilifu ambao kimsingi wanakubalika kwa wapiga kura na wana nia ya kuendelea) na wapo mafisadi ambao wanajua siyo tu kuwa hawakubaliki lakini hata hatari ya kuingia jela inawakabili.CDM ikipeleka hoja ya kumtoa Pinda hatari kubwa iko kwa Pinda maana kimsingi ana dalili zote za kuwa MBABAISHAJI na kwa hiyo CDM na CCM-2015 + watampa kichapo, jumlisha na waoga, wazee waadilifu na wanamtandao waliowekwa kando na kuitwa magamba,zisipotimia za kumchinjia baharini Pinda bado zitaweka historia dhidi ya Pinda JK na wabadhirifu wote kuywa hawawezi kufanya hayo yote and get away with it!
 
Ninakubalina nawe Mwanakijiji kwa kiasi kikubwa. Lakini pia ninatofautiana nawe kwa sehemu fulani. Labda nitoe hoja zangu kwanza kisha nitaeleza ni kwa namna gani tunatofautiana, na similarities will take care themselves.

Ikumbukwe kuwa kumuwajibisha kiongozi wa nchi kidemokrasia ni kama ni tukio la kipekee. Labda hata hizo fikra hazijawahi kuwepo achilia mbali uthubutu. Hii ndio imepelekea viongozi wengi, hasa katika ngazi ya uwaziri kujifanyia mambo watakavyo, ilimradi tu wana-uswahiba na Rais. Mara kadhaa tumemsikia Pinda akisema Mamlaka yangekuwa yangu ningemuondoa huyo mtu leo. Kwamba yupo mtu juu yake ambaye ni rafiki wa mkosefu huyu na ndiye aliye muweka. Mimi sina jeuri ya kumuwajibisha.

Maana yake ni hii. Watendaji wakuu kama Makatibu wakuu kwa upande mmoja, na Mawaziri kwa upande mwingine, maadam wana-uswahiba na rais, kamwe hawatafiria kuwajibika kwa maslahi ya taifa. Watafanya kazi kwa maslahi yao binafsi au kikundi kidogo cha watu.

Hoja kama hii ya Zitto, kwa kiasi fulani inawakumbusha hawa miungu watu, ikiwa ni pamoja na Rais kuwa kuna uwezekano wa kuwaondoa kama watu watachoshwa kabisa na madudu wanayoyafanya. Hii walau italeta nidhamu na kuongeza ufanisi.

Wakati tunahitaji mabadiliko makubwa ya kimfumo (ambayo ndiyo ndugu yangu Mwanakijiji unayalenga), tunahitaji pia kuonyesha nini kinawezekana kwa sasa. Lengo letu kuu ni kuwa na taifa bora, lenye kutumia rasilimali zake kwa manufaa ya wananchi wote. Ikiwa tendo kama hili linaweza kubadilisha mwelelkeo wa watawala, na kuwa na ufanisi, hilo tunalikubali. Ikiwa hakuna mabadiliko, we go for the great change. The good thing is we have all we need for both. Immediate and planned great future change.

Kwahiyo tofauti zetu Mkuu mwanakijiji ni kuwa, kile kidogo kinachowezekana, na kifanyike sasa wakati tunajipanga kufanya makubwa zaidi. Who knows, inawezekana hata hiki kidogo kikalipa!
 
mh zitto siku zote natambua uwezo wako kifikra,kiutendaji na msimamo wako kiutendaji na wabunge wote wa chadema ninachoweza kusema ni kwamba watanzania tumeona juhudi zenu nadhani wengi watakubaliana nami kuwa wabunge mmeacha itikadi zenu ili kutetea maslahi ya watanzania hii inaleta faraja, natoa pongezi za dhati kwake filikunjombe lugola na wabunge wote wa ccm waliokuunga mkono wewe zitto,huu komaa na kura hizo kwa manufaa ya wana wa tanzania naamini viongozi wabovu na wazembe wa kufannya maamuzi mwisho wao umefika.:A S shade:
 
mh zitto siku zote natambua uwezo wako kifikra,kiutendaji na msimamo wako kiutendaji na wabunge wote wa chadema ninachoweza kusema ni kwamba watanzania tumeona juhudi zenu nadhani wengi watakubaliana nami kuwa wabunge mmeacha itikadi zenu ili kutetea maslahi ya watanzania hii inaleta faraja, natoa pongezi za dhati kwake filikunjombe lugola na wabunge wote wa ccm waliokuunga mkono wewe zitto,huu ni mwanzo mzuri komaa na kura hizo kwa manufaa ya wana wa tanzania naamini viongozi wabovu na wazembe wa kufannya maamuzi mwisho wao umefika.:A S shade:
 
Hayo yote yakifanyika na ikachaguliwa teem mpya makini,,je CDM watashika dola 2015/2020?

Sijaelewa nia ya upinzani ni nini hasa.
1.Ni kuombea Mungu chama tawala kizidi kuboronga na wao (wapinzani)kujikita kueielezea jamii madudu hayo na kuomba ridhaa?
2.Kuikosoa serikali ili iende sawa na (chamatawala) kuendelea kushika hatamu?

Namba moja ni sawa, lakini namba 2; hata kama watakatifu wote na malaika watapiga magoti kukiombea chama tawala kijikosoe - HAIWEZEKANI. CCM ni janga la kitaifa, halina dawa, hata kiungo kikishambuliwa na kansa madaktari huwa wanashauri kikatwe tu!
 
Kwa mara ya kwanza kabisa nimeshuhudia makundi makubwa sana ya watu sehemu ambazo zina tv.Makundi ambayo nimezoea kuyaona wakati wa mechi za soka.Jambo ambalo sijalijua ni sababu ya watu kufanya hivyo!Kuhusu mada hii ya MM Mwanakijiji nakubaliana nayo,tulishashuhudia kujiuzulu kwa mawaziri lakini hakukua na mpya.Tatizo ni serikali haina mpya na imeshindwa kutimiza majukumu yake kama serikali,hili liko wazi!
 
Back
Top Bottom