Ndugu,
Kuna tofauti kubwa kati ya madhuhuli na gawio. Madhuhuli hukatwa kwenye mapato ghafi kabla ya kutoa gharama yoyote ile. Gawio hutolewa baada ya kupata faida, baada ya kutoa matumizi na gharama za uendeshaji.
Shirika linapotoa sehemu ya mapato yake kabla ya kutoa gharama za uendeshaji (mishahara, kodi n.k.) na uwekezaji kuna hatari ya haya mashirika kushindwa kujiendesha na zaidi ya yote kutegemea ruzuku na mikopo zaidi. Kwa sasa hatari hii inaweza isionekane. Huko mbeleni yanaweza kufa na kubinafsishwa.
Pia, pesa zote za haya mashirika kwa sasa zipo Hazina na si benki binafsi. Mwanasiasa akizitaka ili kutimiza malengo yake ya kisiasa ni rahisi kuzichukua kwa kisingizio chochote kile (hili "gawio" ni mojawapo). Kuna mkurugenzi au mjumbe wa bodi wa kubisha? Wameambiwa watafukuzwa wasipoleta "gawio".
Tunafanya siasa kwa faida ya muda mfupi, mbeleni ni giza. Shirika linaishi kwa ruzuku leo linatoa "gawio". Vitu vingine ni aibu.
Bams JokaKuu Salary Slip