Zitto: Tunapata maduhuli na si "gawio"

Zitto: Tunapata maduhuli na si "gawio"

Asante sana. Nilikuwa naumiza kichwa tcra wanafanya biashara gani waweze toa "gawio" bilioni 30?
1. Kwa mantiki hii hata TRA wenyewe wanapaswa kulipa hii maduhuli.
2. Kwa mashirika ambayo yanakusanya (hayazalishi) kama TRA, TCRA, EWURA, na mengine kama hayo hiyo 15% aliyosema Zitto iongezwe hadi 80% kwasababu wanatumia fedha yet vibaya kwa mambo ya anasa kwmfn majengo ya kifahari, mishahara na marupurupu kibao ambapo wafanyakazi wengine wanatoka jasho viwandani na secta kama za afya, Polisi, TAZARA nk.
3. Inakera sana kuona taasisi kama mifuko ya eti: "akiba za wafanyakazi" zinajenga magorofa badala ya kuneemesha wafanyakazi wenyewe. Halafu vyama vya wafanyakazi navyo ni kama vimepigwa pini!
 
Hayo ni mambo ya lugha tuu, kwa sisi wa Kanda ya Ziwa, ukigawiwa fedha yoyote, jina la fedha hiyo ni gawiwo!.
P.
Hapana Paskali, usipotoshe. Haya maneno yana maana zake rasmi. Gawio hapa imetumika kwa maana ya Dividend, ambayo tafsiri yake ni "a sum of money paid regularly (typically annually) by a company to its shareholders out of its profits (or reserves)". La msingi zaidi tujue ni formula gani wametumia hawa waliotoa hayo Maduhuli. Zitto anaeleza msingi wa kisheria wa utoaji wake. Na hapo ndio maana ya neno inatokea. Hiyo maana inayotumika "KANDA YA ZIWA" siyo ambayo Zitto anaiongelea, na sidhani kama hao waliotoa hiyo wametoa tu bila kufuata kanuni na sheria. Zitto ameshughulika na hayo mambo kwa undani, nadhani ni vizuri kumpa heshima katika hilo.
 
Na hayo mapato ghafi(Turnover) TANAROADS wanapata wapi?

TANROADS hawana mapato yoyote. Wanapewa fungu kutoka hazina kutokana na kodi, ufadhili au mkopo ili wajenge barabara.
 
Asante Mitandao sikuizi tukidanganywa haichukui siku tushaujua ukweli!
 
Unahisi TANROADS haina mapato ya kibiashara? Hujui TANROADS wanapokea mapato kutokana na mabango yaliyopo mabarabarani? Ni vema ukafanya utafiti wako kujua source ya hayo mapato.
Kwenye hili Zitto kakurupuka sana. Si kila kitu ni cha kupibgwa ilimradi umepinga.

According to Zitto, pesa zilizotolewa jana ni makusanyo, hivi kampuni kama TTCL ikitoa 25 ya makusanyo yake, same to NMB, TIB, TIPER, etc zitaweza jiendesha kweli????
Mambo mengine ni ya kufikiria na kuacha wanasiasa wafanya siasa zao.

Na appreciate sana siasa za Zitto, japo kwenye hili kapeleka wananchi chaka.

Soma sheria ujue tofauti ya levies, kodi n.k. Mapato hutokana na uwekezaji flani. Collection za kodi na ushuru ni makusanyo yasiyo ya biashara ndio maana hayalipiwi kodi ya mapato.
 
TAMWA? ndugu unaijua TAMWA? ile ya enzi za akina Ananilea Nkya? hii ni TANZANIA MEDIA WOMEN ASSOCIATION. Chama cha waandishi wa Habari wanawake. sasa hao watatoaje maduhuli kwa Magu?
Watajua wenyewe,
 
Zitto, you are wrong. Unawadanganya watu lea kiki za kisiasa. Kila mhasibu anajua mashirika ya umma nayo yana kitu kinaitwa Surplus kinachopatikana na simple equation: Receipts - Expenditures = Surplus.(Makusanyo toa Matumizi). Kwa lugha ya kiswahili ningesema ni FAIDA. Ni kitu hicho hicho kwa makapuni kwa lugha tofauti, yaani Revenues - Costs= Profit (Mapato toa Gharama = Faida). Huyu mtu ana lake jambo. Si bure.
 
Nimekumbuka mambo ya:-
Preference shareholders
Ordinary shareholders
Earnings Before Income Tax
Earnings After tax
Net profit/earnings
Retained earnings
Dividends
Earnings per share (EPS)
Bila kusahau kifungu 180 cha Company Act ya Tz kinacholazimu gawio kutokana na faida na si vinginevyo. Acha tu niishie hapa bila kusa
Ok ok sawa
 
Waha wako wapi wamfafanulie ZITTO maana ya GAWIO ? Anasumbua bure wakati kila kitu kiko wazi labda kiswahili cha KIMAHESABU kinamtatiza! DIVIDENDS= GAWIO !
GAWIO ni jina au sio Gawia(KUKUPATIA) ni nini tendo lenyewe.

Ebu tujaribu kutengeneza sentence kupitia GAWIA" Juma amenigawia pesa(GAWIO) yangu/langu.

Ninachokiona hapa kuchanganya kiingereza kutafsiri kwenda kiswahili kwa GAWIO=DIVIDEND wakati tafsiri ambayo haina mantiki na maana yoyote.

Kwaiyo alichosema mheshimiwa rais kipo sahihi kuliko Zitto ambaye ni mpotoshaji tu.
 
Magufuli katusaidia sana kuwafahamu wanasiasa waongo waongo
Nani aliyesema alipoingia madarakani alikuta sukari sh 5000?Nani aliyesema akitoka mapumziko chato ataweka salary slip hadharani?

Uongo ni tatizo la kitaifa,linaanzia juu kabisa kwa Mr Pr...daa!
 
Zitto, you are wrong. Unawadanganya watu lea kiki za kisiasa. Kila mhasibu anajua mashirika ya umma nayo yana kitu kinaitwa Surplus kinachopatikana na simple equation: Receipts - Expenditures = Surplus.(Makusanyo toa Matumizi). Kwa lugha ya kiswahili ningesema ni FAIDA. Ni kitu hicho hicho kwa makapuni kwa lugha tofauti, yaani Revenues - Costs= Profit (Mapato toa Gharama = Faida). Huyu mtu ana lake jambo. Si bure.
Bado unamuamini mtu ambaye haijui dunia kila kukicha anatuma watu nje kisa kimombo?
 
My cabinet November 2020

1. President: Zitto Kabwe
2. Vice P: Fatma Karume (sina uhakika kama anaweza kukubali though)
3. PM: Tundu Lissu
4. Treasury: Freeman Mbowe
5. Defence: Davis Mwamunyange (sina uhakika kama anaweza kukubali though)
6. Home Affairs: Jenerali Ulimwengu (sina uhakika kama anaweza kukubali though)
7. Information, Culture, Arts & Sports: Joseph Mbilinyi "Sugu"
8. Energy & Minerals: John Mnyika
9. Foreign Affairs: Hussein Mwinyi (mnyonge myongeni but...)
10. Constitution & Legal Affairs: Halima Mdee
11. Agriculture, Livestock & Fisheries: John Heche
12. Land & Human Settlement: William Lukuvi (mnyonge myongeni but...)
13. Works, Transport & Communication: Makame Mbarawa (mnyonge myongeni but...)
14. President's Office (TAMISEMI): Esther Bulaya
15. Health & Community Development: Anna Mgwira
16. Education, Science, Technology & Vocational Training: Joyce Ndalicho (mnyonge myongeni but...)
17. Industry, Trade & Inv: Adolf Mkenda (huyu si mwanasiasa lakini naukubali utendaji wake kupitia u-PS pale)
18. nk, nk (nadhani mnaweza kumalizia kwa kuangalia falsafa iliyoko kwenye list yangu hapo juu)

walete waletee!!!
 
wanauza leseni za masafa.......

Juzi wameuza kwenye mnada leseni za masafa kwa Azam na Vodacom zenye thamani ya USD 20m ambayo ni kama TZS 45b. Zitto anaposema maduhuli angalau yafike 80% ya makusanyo ninamuelewa sana. Tena mimi ningependa wao wawe mawakala tu kama TRA, pesa zao za matumizi ya kujikimu ziombwe kutoka serikalini,kila wanachokusanya kipelekwe moja kwa moja hazina. Huenda kama nchi tungeokoa pesa nyingi sana kwani mengi ya mashirika haya, yana matumizi ya ajabu ajabu sana kwa kuwa wanakalia pesa nyingi.
 
K
Juzi wameuza kwenye mnada leseni za masafa kwa Azam na Vodacom zenye thamani ya USD 20m ambayo ni kama TZS 45b. Zitto anaposema maduhuli angalau yafike 80% ya makusanyo ninamuelewa sana. Tena mimi ningependa wao wawe mawakala tu kama TRA, pesa zao za matumizi ya kujikimu ziombwe kutoka serikalini,kila wanachokusanya kipelekwe moja kwa moja hazina. Huenda kama nchi tungeokoa pesa nyingi sana kwani mengi ya mashirika haya, yana matumizi ya ajabu ajabu sana kwa kuwa wanakalia pesa nyingi.
Kuna mapoyoyo humu acha tu
 
Back
Top Bottom