Zitto: Tunapata maduhuli na si "gawio"

Zitto: Tunapata maduhuli na si "gawio"

Kama Rais anadanganya, lengo lake ni kumdanganya nani??
Yan kutoka November 5, 2015 hadi leo July 23, 2018 bado unajiuliza swali hili? Watz mna akili nzito sana yan, ndo maana Jiwe anawachezea tu anavyotaka

Nani mkweli katika hili, ni Zitto au Jiwe
Zitto ameuliza, kama ni gawio(dividends), TCRA, EWURA, TANROADS na SUMATRA for instance wanafanya BIASHARA gani tujue? So Jiwe is a masterful LIAR, intellectually inept!
 
Sasa kama siyo gawio bali ni maduhuli kwanini ofisi ya Rais imeruhusu hili kufanyika tena kwa mbwembwe nyingi mno? Nani mkweli katika hili, ni Zitto au Rais?

Kama Rais anadanganya, lengo lake ni kumdanganya nani?? Na kama Zitto hayuko sahihi lengo lake ni nini?? Mimi nafikiri tunahitaji ufafanuzi wa kina kuhusu hili jambo.

Cc. Pascal Mayalla
Huu ni utawala wa kujitangaza kuficha waliowengi ili waamini kuna nguvu kubwa inafanyika kumbe ni yaleyale wafichuaji wa haya wapo hatarini utawala huu mfano huyu atatafutiwa sababu tu anyamazishwe

Inamaana mashirika yaliobinafsishwa awamu ya tatu hayakutoa gawio?
 
Tcra wametoa nao, tena wamevuka malengo kwa maelezo yao. Wakala wa vipimo, TAA, TIPA, etc yaani taasisi na kampuni zote ambazo serikali ina hisa, ziwe kidogo au nyingi.
Sijawasikia UDA wakitoa gawio. Tanesco hawajatoa. Wajitathmini.
A T C haimo?
 
Mashirika yapo zaidi ya 100
Lakini yaliyotoa gawio ni mashirika 47 tu .

Swali kwa Zito hiyo 15 % huwa yanakatwa hayo 47 tu na yanayobaki hayakatwi ?

Kama hoja ya Zito ina kweli basi tungeyaona mashirika yote zaidi ya 100 yakitoa gawio leo
 
Nashauri Zitto akamatwe na kushitakiwa kwa uchochezi wa kumdhalilisha rais wa JMT.

Rais wa nchi ni kama baba kwenye familia, sio mtu, huyu ni an institution, na kwa mujibu wa katiba yetu, rais wetu hawezi kukosea ndio maana jashitakiwi. Hata kama Zitto ni mkweli na hayo ni maduhuli na sio gawio, kama rais kasema ni gawio, then ni gawio!.

Haiwezekani rais wetu aseme kitu hiki halafu atokee mtu mwingine, ambishie rais!.

P.
😀😀😀
 
Nashauri Zitto akamatwe na kushitakiwa kwa uchochezi wa kumdhalilisha rais wa JMT.

Rais wa nchi ni kama baba kwenye familia, sio mtu, huyu ni an institution, na kwa mujibu wa katiba yetu, rais wetu hawezi kukosea ndio maana jashitakiwi. Hata kama Zitto ni mkweli na hayo ni maduhuli na sio gawio, kama rais kasema ni gawio, then ni gawio!.

Haiwezekani rais wetu aseme kitu hiki halafu atokee mtu mwingine, ambishie rais!.

P.
Ha ha ha ha mkuu umejibu kisiasa sana na siyo kitaaluma kabisa, anyways mimi nimekuelewa lakini swali linabaki pale pale, kati ya Rais na Zitto nani mkweli katika hili swala la gawio na maduhuli? Ukiniambia kuwa eti Rais hawezi kusema uongo nakataa kabisa.

Wanachotaka kujua Watanzania ni UKWELI tu basi.
 
Faida vs Ushuru/Kodi. Lugha mbili tofauti. Mmoja ya kiutendaji nyingine ya Kibiashara.
Hivi Kamusi ya Biashara Tz hii hakuna?
 
Uongo jumlisha gharama zilizotumika leo ndio faida ya kuwapa nchi washamba na limbukeni. Ndio maana Wabunge na Madiwani wa upinzani hawatakiwi ili tulishwe matango pori na malaika huku vigelegele vikipigwa na Lusinde.
 
tenor (1).gif
 
Zitto ungekaa kimya pia ingependeza sanaa. Si kila jambo ulitolee tamko ni hekima na busara siku zote unapokuwa umenyamaza kuliko unapokuwa unazungumza.

Nawaombeni enyi mnaojiita wanasiasa kujitafakari wakati mwengine kwa michango yenu kama inaumuhimu wowote kwa maendeleo ya taifa au la.

Hivi mtu akiita gawiwo au mchango au pato au duhuli na akalitoa kwa mwenye hisa unapungukiwa na nini ukinyamaza kimya bila ya wewe usiye na kiasi hicho kuchangia kwa jamii?

Tuwe wastaarabu wakati mwengine badala ya kuwa washenzi na wenye kukosa adabu kwa matamko yasiyokuwa na tija kwa taifa letu.

Nimuulize zito na mnaomuunga mkono maelezo yake hapo juu yamesaidia nini kwa taifa ukilinganisha na shughuli iliyofanyika leo? Je tule maneno au fedha zilizochangiwa leo?
swala lililopo ni kuwa kwa nini atudanganye? ameshatuona sisi ni mazombi ee?
 
Kama ningekuwa rais zitto ningempa nafasi fulani asaidie kuyafanya mawazo yako mengi mazuri ktk utendaji. Zitto why are you always appear to be right? Simaanishi ktk hili tu. Mara nyingi huwa ni kama mtoa mawazo mbadala.
Je hutumiki vizuri ktk bunge na serikali? Hizi gvt organs huwa hawakutani na interest groups kupata insights zao au huwa unasubiri wakosee au unajua lazima watakosea mahali then uwakosoe?
Mtu asimaye uhongo usidhani uwa ni bahati mbaya, bali huwa amezamilia sasa ni wewe kungamua ulichoambiwa.
 
Sasa kama siyo gawio bali ni maduhuli kwanini ofisi ya Rais imeruhusu hili kufanyika tena kwa mbwembwe nyingi mno? Nani mkweli katika hili, ni Zitto au Rais?

Kama Rais anadanganya, lengo lake ni kumdanganya nani?? Na kama Zitto hayuko sahihi lengo lake ni nini?? Mimi nafikiri tunahitaji ufafanuzi wa kina kuhusu hili jambo.

Cc. Pascal Mayalla

Methinks Zitto anajua anachozungumzia. Lakini ama kwa kutojua au kwa makusudi, kuna watu wameamua kupotosha umma kuwa mashirika yote hayo yametoa gawaio. Kama tcra, ewura, na executive agencies kama hizo nao wametoa 'gawio' basi ni ishara kwamba kuna upotoshwaji kiasi fulani hapa. Inawezekana kweli kuna mashirika yamefanya biashara kweli na kupata faida kiasi cha kutoa gawio lakini yaliyo mengi yasingeweza kutoa gawio kwa kwa maana ya gawio kweli. Ila kama ni tozo ya turnover yao basi hilo linaleta sense.
 
Back
Top Bottom