Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Haya matamanio ya kuangushwa ubunge hayawezi kuzuilika.Vipi kama hataenda kwenye ubunge?na hata kama hatakuwa Mbunge bado wimbi hili la vijana na mtizamo kama wake wataibuka kwa wingi.Utaendeleza matamanio yako?

Ati Kwamba wewe ni kijana kama mimi,haimaanishi tunafanana.Naomba urudi kwenye mada au ujibu hayo niliyokuuliza.Pia kama wewe ni mstaarabu leta uthibitisho kwamba chama changu kiliniita Usalama wa Taifa.
Kwanza ningependa kukuweka sawa hakuna mahala ambapo wewe nimekuita ni Usalama waTaifa kwa sababu hakuna vetting yoyote makini inayoweza kukupitisha wewe kuwa Inteligence security officer hili unalifahamu wazi.
Pili unapomzungumzia vijana na hata mimi ni kijana kwahiyo usijipe mamlaka ya kudhani vijana wote wana mawazo finyu ya kupelekeshwa tu hobelahobela! unapolia Zitto alihujumiwa jimboni mwake hivi ni nani aliyekihujumu chama chake kwenye jimbo la Kafurila? hivi inakuingia akili naibu katibu mkuu wa CHADEMA awe mpiga zumari wa NCCR Mageuzi?

Ben sikufahamu na wala hunifahamu na mbaya zaidi sina hata kadi ya CHADEMA ila ningependa nikueleze haya yafuatayo:
Dhamira na hulka ya mtu huwa haijifichi ni jambo la kushangaza na kustaajabisha sana mimi sijawahi kukuona kwa sura lakini nimefanikiwa kuijuwa tabia yako kupitia mtandao, je inakuwaje kwa wale ambao mnafanya nao siasa za daily routine? Nadhani bado hujachelewa jitazame sidhani kama huo msimamo wako kama una afya yoyote ya kisiasa kwa future.
 
Najua Mh.Zitto Kabwe hauna nia wala dhati ya kuwa raisi Tanzania..! hiyo ni moja ya mkakati wako na CCM kuimaliza CHADEMA huku ukishirikana na swahiba wako January Makamba..,siujui wemekupa shs.ngapi mheshimiwa au wamekuahidi cheo gani serikalini (mkuu wa wilaya,katibu CCM)..!
Lakini Jua Nguvu ya Umma Haichezewi..,wako wapi madiwani wa Arusha (watano) waliosaliti chama..,yuko wapi Walid Kabourou,yuko wapi Tambwe Hiza..yuko wapi Agustino Lyatonga Mrema, ingawa anapata pensheni ya ubunge lakini heshima hana kama zamani..!
Zitto Kabwe Watu wamekufa,kuteseka na kufungwa kuitetea CDM..,leo hii wewe unataka kukiuza CDM kwa bei chee...kumbuka ulipotoka Zitto..,hivi ungegombea ubunge CCM mwaka 2005 ungelipata hilo jimbo la kigoma Kaskazini..,wengeshakutosa zamani kwenye kura za Maoni..,CHADEMA wakakupokea leo unakiuza chama "KWELI SHUKRANI YA PUNDA NI MATEKE'' najua ni haki yako kikatiba kugombea uraisi lakini inaonyesha nia yako ni kuimaliza CHADEMA..!
Hivi wewe ni mtu wa aina gani?hivi kusema anautaka uraisi tu imekuwa nongwa? basi hiki Chama ni noumer!!kwa hiyo si ruhusa kutoa maoni ndani ya chama midomo yote inafungwa ila midomo miwili au mitatu ndiyo inaruhusiwa kusema? kama ni hivyo kazi ipo na sijui kama kuna dhamira ya kweli.Wacheni kukandamiza demokrasia.
 
Anachokisema winnet forever hapa chini ndio na mimi ninachokijua,
Zitto hajatangaza rasmi hapa JF kama wengi wanavyojenga picha ionekane hivyo, Zitto alikuwa anajibu hoja na si kwamba alifanya timing eti kipindi hiki ndio atangaze
Kama alivyotangaza kugombea ubunge kwenye majimbo matano mwaka 2010 eheeeeh!!..........
 
CHADEMA imejengwa na ZITTO plus SLAA wakiwa BUNGENI walisumbua sana SERIKALI ndiyo maana leo hii CDM imekuwa kambi rasmi ya UPINZANI.Sioni sababu ya kumzuia kijana ZITTO kuingia kwenye kinyang'anyiro hicho au ndiyo UDIKTETA wa MADARAKA? You should practice what you are preaching.....


Igweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
zitto kabwe hana nguvu as far as Mapacha watutu wa ccm wako kando ya system

Zitto alitegemea sana support ya hawa mabwana kuleta vurumai CDM ila kwa sasa naona kilichobakia ni asogezwe kule waliko madiwani wa ARUSHA tena mapema
 
Najua Mh.Zitto Kabwe hauna nia wala dhati ya kuwa raisi Tanzania..! hiyo ni moja ya mkakati wako na CCM kuimaliza CHADEMA huku ukishirikana na swahiba wako January Makamba..,siujui wemekupa shs.ngapi mheshimiwa au wamekuahidi cheo gani serikalini (mkuu wa wilaya,katibu CCM)..!
Lakini Jua Nguvu ya Umma Haichezewi..,wako wapi madiwani wa Arusha (watano) waliosaliti chama..,yuko wapi Walid Kabourou,yuko wapi Tambwe Hiza..yuko wapi Agustino Lyatonga Mrema, ingawa anapata pensheni ya ubunge lakini heshima hana kama zamani..!
Zitto Kabwe Watu wamekufa,kuteseka na kufungwa kuitetea CDM..,leo hii wewe unataka kukiuza CDM kwa bei chee...kumbuka ulipotoka Zitto..,hivi ungegombea ubunge CCM mwaka 2005 ungelipata hilo jimbo la kigoma Kaskazini..,wengeshakutosa zamani kwenye kura za Maoni..,CHADEMA wakakupokea leo unakiuza chama "KWELI SHUKRANI YA PUNDA NI MATEKE'' najua ni haki yako kikatiba kugombea uraisi lakini inaonyesha nia yako ni kuimaliza CHADEMA..!

Yuko wapi Chacha wangwe?
 
Dr.SLAA kachanganyikiwa coz anaomba dua baya kwa ZITTO atimuliwe haraka sana...subiri wapoteze Arumeru ili wamjeruhi ZITTO kama walivyofanya CUF na NCCR.

Padre alijua amesha MONOPOLIZE u candidate; lazima achanganyikiwe.. CHURCH keshaharibu, huku CDM vijana wamekuja juu. NICE MOVE ZK
 
Umetumwa? wewe ndio Zitto Kabwe, unadhani sifahamu ninachokiuliza au unadhani wote humu viherehere vya wanasiasa? Mabere Marando alishajibu siku nyingi Mahusiano yake na TISS, hapa yanahitajika maelezo ya Zitto Kabwe na siyo maelezo ya wapambe wa Zitto Kabwe. tena ningekushauri kama unampenda kaa mbali na hili.

Acha utoto wewe. Nani kakuuliza mahusiano ya TISS na Mabere Marando? Miye nakuambia sina mahaba na mtu naona wewe una visa tu na huyo Zitto. Kwa hiyo wewe ni mpambe wa nani?

Mimi ni mtu huru na nina uhuru wa kutoa mawazo yangu na siwezi kuzuiwa na mtu yeyote.
 
zitto kabwe hana nguvu as far as Mapacha watutu wa ccm wako kando ya system

Zitto alitegemea sana support ya hawa mabwana kuleta vurumai CDM ila kwa sasa naona kilichobakia ni asogezwe kule waliko madiwani wa ARUSHA tena mapema
Ni mapema sana jamani kumshutumu ZITTO, tusubiri, tusikie na kauli za SLAA na MBOWE ndipo tumshambulie. Tukumbuke kuwa anayo haki ya kugombea yeye kama mtanzania. Sidhani kama akifuata taratibu na chama kikamteua tutakuwa na cha kusema.
 
Tatizo la zitto anafiriki anaomvuto wa kushawishi vijana amesahau watu wapo kwa ajiri ya CDM
 
Mbona watu wanatafsiri vibaya msimamo wa Zitto? hebu tusome tena hii mistari halafu mtamuelewa, tuache chuki na mitazamo hasi wadau
Hata hivyo kazi hii hata kama naitaka ni lazima wenye nchi waamue kunipa kazi hii. Ni lazima kwanza Chama changu kiseme wewe ndio mwanachama unaestahili kuifanya kazi hii. Ni lazima Watanzania wengi waseme wewe ndio mwananchi mwenzetu unayeweza kuchukua jukumu hili. Kuitaka tu haitoshi. Ni lazima wananchi wakuamini na kukupa jukumu hili.


"Sasa kama wananchi watasema huyu Zitto anapaswa kubeba jukumu hili mwaka 2015 tuache iwe. Kama watasema hapana wewe bado mpaka mwaka 2020 au hata 2025 tuache iwe hivyo. Pia Kama hawataki kabisa tuache iwe hivyo.Hata hivyo kazi hii hata kama naitaka ni lazima wenye nchi waamue kunipa kazi hii. Ni lazima kwanza Chama changu kiseme wewe ndio mwanachama unaestahili kuifanya kazi hii. Ni lazima Watanzania wengi waseme wewe ndio mwananchi mwenzetu unayeweza kuchukua jukumu hili. Kuitaka tu haitoshi. Ni lazima wananchi wakuamini na kukupa jukumu hili.


Sasa kama wananchi watasema huyu Zitto anapaswa kubeba jukumu hili mwaka 2015 tuache iwe. Kama watasema hapana wewe bado mpaka mwaka 2020 au hata 2025 tuache iwe hivyo. Pia Kama hawataki kabisa tuache iwe hivyo."

Kwanini mnasema anakivuruga chama? kwa nini mnasema kanunuliwa na CCM ndio maana mwenyewe kamaliza kwa kuuliza

"Huu woga dhidi ya Zitto unatoka wapi?"
 
Tatizo la zitto anafiriki anaomvuto wa kushawishi vijana amesahau watu wapo kwa ajiri ya CDM

Mkuu hapo sikubaliani na wewe, zama za kuwepo kwa ajili ya Chama siyo huu, ndiyo maana kuna mijadala hata ya kuwepo kwa mgombea binafsi. Ni mawazo mgando kufikiria Chama badala ya watu, japo kuna watanzania aambao bado wana mawazo kama hayo na mifano ya wazi inajidhihirisha kwa baadhi ya wabunge kuchaguliwa si kwa sababu wana uwezo bali kwa sababu tu kushabikia Chama. hakika hii ni hatari sana.
 
Zitto siyo kuwa hajakoma, ana haki na kakomaa, hebu fikilieni wanajamvi hivi mnakumbuka marais wa nchi hii, mbona wengine Zitto keshawashinda vigezo? Labda umri lakini mambo mengine yuko juu yao, Kwa hekima hebu pima kati ya Zitto na Mkapa!!

Haya mambo ya kutangaza nia mapemza ndo yanaigawa CCM na makundi mpaka sasa. Kwa kuwa hatujawa na mgombea binafsi, Chama ndo kina wajibu wa kumtafuta mpeperusha bendera wake. Hata Dr. Slaa alipendekezwa na kuombwa na chama kugombea uraisi 2010.

Namheshimu Zitto but huu haukuwa mda muafaka wa kuonyesha kuwa anauota uraisi. kitakachofata hapa ni yeye kuanza kuandaa kundi la kumsaidia kutimiza ndoto yake. At the end CHADEMA itakuwa kama CCM. Makundi kwa kwenda mbele
 
Urafiki wa Zitto Kabwe na Jack Nzoka Deputy Director wa Idara ya Usalama wa Taifa wewe unataka kutuaminisha ni wa kawaida? hivi si wewe chama chako ndio kilisema Usalama wa Taifa ndio waliokuwa wanachakachuwa kura za CHADEMA? (TISS)

Zitto Kabwe ni rafiki yako na kama alitoa makala hii ili kumjibu huyo mwandishi sasa mfikishie na ujumbe huu, aje hapa atupe ufafanuzi wa yeye kuwa karibu na Usalama wa Taifa. nitamuhesabu Zitto Kabwe kama ni Double Agent until he proves otherwise without resonable dought.

Hayo maneno hapo juu kwenye Red ni nani kayasema?Nimekwambia ulete uthibitisho kwamba chama changu kiliniita usalama.Ni wapi ambako chama kiliniita usalama wa Taifa ?


Kwanza ningependa kukuweka sawa hakuna mahala ambapo wewe nimekuita ni Usalama waTaifa kwa sababu hakuna vetting yoyote makini inayoweza kukupitisha wewe kuwa Inteligence security officer hili unalifahamu wazi.
Pili unapomzungumzia vijana na hata mimi ni kijana kwahiyo usijipe mamlaka ya kudhani vijana wote wana mawazo finyu ya kupelekeshwa tu hobelahobela! unapolia Zitto alihujumiwa jimboni mwake hivi ni nani aliyekihujumu chama chake kwenye jimbo la Kafurila? hivi inakuingia akili naibu katibu mkuu wa CHADEMA awe mpiga zumari wa NCCR Mageuzi?

Ben sikufahamu na wala hunifahamu na mbaya zaidi sina hata kadi ya CHADEMA ila ningependa nikueleze haya yafuatayo:
Dhamira na hulka ya mtu huwa haijifichi ni jambo la kushangaza na kustaajabisha sana mimi sijawahi kukuona kwa sura lakini nimefanikiwa kuijuwa tabia yako kupitia mtandao, je inakuwaje kwa wale ambao mnafanya nao siasa za daily routine? Nadhani bado hujachelewa jitazame sidhani kama huo msimamo wako kama una afya yoyote ya kisiasa kwa future.

Matola,

Kuwa mstaarabu na kwa muungwana ukikosea unaomba msamaha.

Halafu mimi sina uwezo wa kupelekesha mtu na ndiyo maana hata mimi napinga kupelekeshwa.Napenda demokrasia,uhuru wa mawazo sipendi utumwa wa fikra.Siabudu,sisujudii fikra mfu.Ningekuwa napenda hayo ningekuwa naongea lugha nyingine tofauti na hii ambayo najua nudhi watu wengi,siyo hapa JF tu.Ila sijenge hoja kwa matamanio au katika kufurahisha watu.Naangalia uhalisia na logic.Kwa hiyo kupelekesha watu huwa nina-discourage hiyo tabia.Naheshimu kila mwanadamu,naamini katika utu

Ati hunifahamu na wala sikufahamu? Kwani hili lina uhusiano gani na huu mjadala?Nimekuuliza maswali,ukashindwa kujadiliana kistaarabu na kuaanza kuita watu majina,je ningekujibu kwa stahili hiyo ingekuwaje? Tuwaache watu waamue ni nani ameenda personal au too low.....

Tuendelee na mjadala au utoe majibu ya maswali niliyokuuliza.Kuhusu ninaofanya nao kazi/siasa ni issue nyingine wanajua wao.Sihitaji unijue au nikufurahishe ndiyo niwe mwanasiasa/kiongozi au mtu mzuri kwenye jamii.

Kuhusu Zitto kumpigia kampeni mgombea wa NCCR-Mageuzi hilo ni tatizo? Kwani ni yeye tu aliyefanya hivyo?Hebu kuweni fair,tena NCCR-Mageuzi ni kambi ya Upinzani.Nikuulize swali lingine,Katika harakati za kambi ya upinzani Kijana David Kafulila aliungana na chadema kuibana CCM hadi wakatolewa nje ya ukumbi wa bunge.Je,kule Kyela ni nani aliyempigia kampeni Dr.Mwakyembe (CCM) ? Kama Zitto kufanya vile kwa NCCR-Mageuzi na ikageuka kosa je kwa aliyempigia/waliompigia kampeni Dr.Mwakyembe 9in regardless of conditionalities) hawakufanya kosa?

Je,kwenye issue yoyote/harakati za upinzani bungeni Dr.Mwakyembe ni lini aliwahi kuungana na CHADEMA kwenye movement yoyote ndani ya Bunge?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom