Hatimaye sasa nimejiridhisha pasipo na shaka ni kwa nini zitto Kabwe ni swahiba mkubwa wa Deputy Director wa Usalama wa Taifa ndugu Jacky Nzoka, Zitto aje hapa kuuelezea umma wa JF ni sababu zipi za msingi zilizokuwa zinamfanya awe na mawasiliano ya mara kwa mara wakati chama chake kiko katika uchaguzi mkuu na Idara ya usalama wa Taifa ndiyo ilikuwa inaihujumu CHADEMA? hapa sitalajii jibu rahisi kwa swali gumu.
Pili Ben Saanane nimekuwa nikifuatilia mabandiko yako kwa makini sana na kuna kipindi nilidhani huwa unaonewa, kumbe nilikuwa najidanganya, humu jamvini umejipambanuwa kwamba wewe ndio unayejuwa siasa na yeyote ambaye atakuwa kinyume na mtazamo wako basi wewe utambatiza kila aina ya jina mara mnafki mara hivi mara vile, kumbe sasa nimejiridhisha ni kweli chama chako kiliposema huna maadili hakuna walipokuwa wamekosea, kwa nini unatetea Alliance ndani ya chama? narudia kukwambia tena jifunze kwa John Mnyika, yule kijana anaaminika machoni pa watu kwa sababu he is humbled,......jiulize ni kwa nini kijana mmoja Mnyika alundikiwe vyeo na nyinyi wasomi mpo? endelea na Alliance. zako.
Nikikuuliza ni wapi wazee walisema Ben Saanane huna maadili utanijibu?Do credibility a favour na uje uthibitishe hilo.Tuache upotoshaji.
Matola,
Just as everyone is entitled to their opinion then everyone should be entitled to their own actions(good or bad).
Unajua ukitaka kuheshimika ni lazima pia uwe na nidhamu.Heshima na nidhamu ni two way traffic.
Kuhusu Mnyika,sina utamaduni wa kujadili watu kama unataka kujadili watu jadili mwenyewe.Mnyika ni kiongozi wangu,ni rafiki yangu tunaheshimiana.Kuhusu suala la vyeo mimi sipo hapa kujadili hilo kuna mamlaka ya uteuzi kawaulize maswala hayo
Kuhusua Alliance ndani ya chama,ni alliance ipi niliyoitetea? Nakiri uchaguzi wa BAVICHA nilifanya Alliance.Je hilo ni tatizo? kuna political theory yoyote inayokataza aliance?chama kinakataza makundi,ofcourse makundi si healthy kwa mustakabali wa chama..Na hilo naunga mkono.hakuna uchaguzi unaofanyika bila kuwa na makundi ila cha msingi ni jinsi ambavyo kila mmoaja anakuwa tayari kuvunja makundi baada ya uchaguzi
Nilipomaliza uchaguzi wa BAVICHA nilisema nitaendelea kutetea zoezi la demokrasia ndani ya chama changu.Kama ilivyo kwa mimi kutokuwa tayari kuona Dr.Slaa anazushiwa tuhuma za uongo au Kamanda mbowe ndivyo hivyo nitakavyopambana na upotoshaji unaofanywa dhidi ya kamanda Zitto na wanachadema wengine wa CHADEMA kwa ujumla.
Mkuu mimi huwa sina mahaba na mtu; mimi huwa nina mahaba na hoja zinazopalilia demokrasia kuanzia kwenye vyama vya siasa ili kustawisha demokrasia ndani ya nchi.
Kama CCM na vibaraka wake wanampenda mimi sijui labda unisaidie hizo sababu labda ndizo zinakufanya useme hana sifa.
Ninachokipinga ni kwamba Zitto hana sifa. Mimi najua kwamba ana sifa za kikatiba (ukiachilia hiyo ya umri) ambayo yeye mwenyewe ameisema vizuri tu kwamba kama Katiba itakuwa imeruhusu. Sasa Mkuu wewe unasema hana sifa ila husemi hana sifa kwa vipi? Hapo ndipo nashindwa kukuelewa.
Comrade Kimbunga,
I had thought that with more education and analytical thinking, our people would get past these narrow highly subjective conclusions about our reality. Unadhani baadhi ya watu hawajaelewa hili suala?wengine ndiyo hivyo hawewezi kuelewa lolote,na wengine wameelewa ila ni husda zao tu.Wengine wapo kazini.lol
Ndipo hoja ya umri hapa inapopata nguvu zaidi, yaani tupo kwenye mchakato wa Katiba ya Wananchi na ni sisi Wananchi ndio tutakaosema tunataka katiba gani halafu anatakoa mtu mwenye uchu na ulevi wa madaraka na kuanzisha mijadala ambayo haina tija!...nadhani kwa mtu mzima mwenye busara za kutosha hawezi kufanya hivyo na hapa hoja ya umri inazidi kupata nguvu kwamba miaka 35 BIG NO.
Niko interested sana Zitto aje hapa kutoa maelezo ni nini kinaendelea kati yake na Deputy Director wa Idara ya Usalama wa Taifa. hapa ninajuwa ninachokisimamia na ninachoamini, na tukienda mbali zaidi nasikitika kuwajulisha mashabiki wake msishangae Zitto akikataliwa Ubunge jimboni kwake mwaka 2015 katika masanduku ya kura.
Zitto Kabwe ndiye mbunge pekee ambaye alitaka kugombea Ubunge kwenye majimbo matano tofauti kwenye uchaguzi wa 2010, na alipogombea kwao Kigoma Ushindi wake ulipungua kura alizopata kufananisha na zile za mwaka 2000.
Matola,
Kuhusu suala la kuwa Interested na zitto kuja hapa akueleze sijui nini siwezi kulijadili,atalijadili yeye mwenyewe.
Kwa hiyo suala la katiba kujadiliwa watu wanazuiwa kusema wanachoamini? Kweli hata katiba mpya itaandikwa hakuna mabadiliko yoyote kama tunafikia hatua kuchagulia watu marafiki na kitu cha kusema.
Tuna safari ndefu huko mbele.Guys,let us be matured,tatizo la hii hoja ni nini?mara wengine wanasema kuna uchaguzi Arumeru kwa hiyo timing ni mbaya.Nguvu zinazotumika ku-condemn hili kwa nini zisitumike kuelewesha watu kama unadhani hili lina athari kwenye hizi chaguzi?
Kwa ushauri wa bure epuka sana hizi siasa zenye mlengo wa kugawa watu.Nadhani kwa nilivyofuatilia mjadala huu na hao wanaokutuhumu kuwa wewe unashirikiana na Zitto katika hiyo mipango yenu mnaoijua wenyewe soon itafumuka na mtaabika vibaya sana.Hawa wanaojadili humu na kutokumuunga mkono Zitto sio kwamba hawamkubali ama sio wafuasi/wanachama/wapenzi wa chadema,la hasha! hawa ni watu wanajadili kwa kina athari za maamuzi ya kamanda wao kimtazamo zaidi.
Napata shaka kuwa na wewe ni mmoja wa wanasiasa ambao hawataki kukosolewa.Napenda kukushauri upitie hoja za watu wote walioonyesha kumpinga Zitto kwa hili alilotamka kisha uyachambue ,kwa kuwa ni rafiki yako wa karibu sana umpe machache kama changamoto.Wanadamu tunatofautiana na kila mmoja anamapungufu yake ,suala la msingi ni kuheshimu mawazo na mitazamo ya watu kuhusu mapungufu yako.Hii inasaidia mtu kujijenga na kuimarika kimtazamo,hata katika kuchangia na kutetea hoja.
Mimi ni mmoja kati ya watu wanapinga kauli hii ya Zitto ya sasa ,lakini si kwamba napingana na mitazamo/hoja zake zenye malengo ya kutuondoa katika dimbwi la umasikini -kwa kutuonyesha njia na mwelekeo thabiti wa kimapinduzi.
Mwakalinga,
Well, Apologies if i don't paint out my wishes concisely.
Nikikuuliza ulete uthibitisho wa kukigawa chama,unaweza kuleta? Wanaonituhumu ?
You are basing all your accusation on a hearsay plus you jumped into conclusion. We'll damage ourselves before we can able to fix ourselves.
Bora umenipa benefit of doubt.Mara nganpi tumekosoana na kubishana sana hapa JF tangu niwe member 5 years ago na sijawahi kumkosea heshima yeyote anayenipinga kistaarabu? Akina Mugongo Mugongo,ACID,MTM,Field Marshal,Waberoya,Kimbunga,Kasheshe,Mwanakijiji,Mkandara na wengineo wengi watakushangaa sana kwa kauli hii ya kwamba ninaweza kuwa sikubali kukosolewa.
Nitasema kile ninachoamini na nitasimamia kile ninachoamini.Upotoshaji wowote utakaofanywa kwa maslahi ya wachache siwezi kuvumilia,siogopi kuchafuliwa na siogopi matusi wala vitisho.Ninachojali ni maslahi ya watanzania kupitia dira sahihi,najali maslahi ya vijana na nitapigania kwa gharama yoyote ile.Mkuu waangu pengine haupo ground kujua kinachoendelea,vijana wanatumika kama daraja la watu kisiasa.busara za viongozi wetu waliokuwa above 40 ndizo zilizozalisha hili bomu ambalo wanafiki wanajaribu kujifanya kwamba linawaumiza.Leo hii wanapita wanasiasa waliosababisha lindi la umaskini na wengine walioshindwa kuishinikiza serikali ilifanyie kazi tataizo la ajira kwa vijana leo hii wanalia machozi ya mamba.siwezi kucheka naoa
Umeongelea kuhusu kuheshimu mawazo ya wengine,huwa ninaheshimu mawazo ya wengine sana hasa wale ambao wanaonipinga.Wnaonipinga huwa ninawasikiliza zaidi,hata katika maisha yangu ya Uongozi vyuo vikuu na Eneo langu la kazi wanajua hivyo.Anayenipinga namsikiliza zaidi
Kwa dhamira ya moyo wangu kabisa, SIAMINI KAMA ZITO ANAWEZA KUWA HATA WAZIRI MKUU ACHILIA MBALI KUWA RAIS. Namwona ni mtu anayependa sana madaraka, Umwenyekiti wa CHADEMA anataka yeye, uongozi wa kambi ya upinzani bungeni anataka yeye, kila nafasi kubwa ya kiuongozi anataka yeye. Watu wa namna hiyo ni wa kuwaogopa sana, watu wa namna hiyo wakiupata uongozi huwa ni ving'ang'anizi sana maana wakati wote hawapendi kuishi au kufanya kazi chini ya mtu mwingine. Zito anafanya mambo mengi mazuri lakini yenye msukumo wa hila wa nia ya kujijenga ili aweze kuyapata madaraka makubwa. Ninafahamu kuwa viongozi wa CHADEMA wanalijua hilo lakini ni wenye busara na wanamwacha mpaka siku ile ambapo Watanzania wengi watamjua Zito ni nani na ni mtu wa namna gani. Zito anasumbuliwa sana na fikra kuwa yeye ni mtu maarufu sana na anafahamu sana. Haiwezi kuingia akilini, mtu mwenye fikra zilizotulia anafikia kutaka kuacha jimbo lake eti akagombee ubunge jimbo la Geita au Kahama, kwa sababu gani? Na wananchi wa Kigoma walimtendea wema sana kumpa hizo kura kwa kitendo alichowafanyia, na ninaamini aliupata ushindi wa ubunge kwa vile JK alitaka ashinde, na ndiyo maana JK alienda majimbo yote ya Kigoma kupiga kampeni lakini hakwenda jimboni kwa Zito.
ZITO FOR PRESIDENCY, A BIG NO. Ana haki ya kugombea kama mtanzania mwingine yeyote lakini kupewa dhamana hiyo, siungi mkono. Ninaamini leo kama kukitokea chama chochote cha siasa, iwe CCM, CUF, TLP, PPT Maendeleo, n.k. ambacho kingeweza kumhakikishia Zito kuupata Urais, ni lazima angeenda huko. Kwake kilicho muhimu ni Urais wala siyo itikadi ya chama. Ni nia hii ya Zito ndiyo inayomfanya asitulie sana, mara yupo karibu na naibu mkurugenzi wa usalama wa Taifa, mara anafanya mikutano na akina RA, hii yote ni kwa sababu hajui ni nani na ni chama gani kitakachomhakikishia kuupata urais. WATU WA NAMNA HIYO NI WA KUWAOGOPA SANA KATIKA NAFASI KUBWA KAMA YA URAIS. Sina chuki wala ugomvi na Zito, nafurahia uwezo wake wa kujenga hoja na kufuatilia lakini sina imani na dhamira yake, na hii wakati fulani huwa ni hulka
Mkuu,kwa hiyo hata majukumu yake ya kamati ya hesabu za serikali na mashirika ya umma anayafanya kwa msukumo?suala la Posho anafanya kwa msukumo?
- Ninaamini ni haki ya Zitto kikatiba kugombea anything, msiomataka Zitto mnapwaya sana kwenye hoja wengi wenu mnajikita kwenye kujali chama kuliko Taifa, that is very sad kama hatuwezi kutenganisha Taifa na Vyama vya siasa, then hili taifa tutakwama daima. Simfahamu vizuri Zitto ila siamini kwamba hawezi kuaminika na Taifa, miswaada yake yote bungeni ni masilahi ya Taifa tu na hasa wananchi, I mean wananchi wa jimbo lake wanaiamini naye sana which is the most important ishu of all.
- Zitto, kuwa rafiki na Viongozi wa CCM siamini kwamba ni ishu ya kumfanya asiwe Rais mzuri, unless kuna something else hakisemwi hapa, kwamba ana tamaa ya madaraka labda mtuambie kiongozi gani Duniani asiye na tamaa ya madaraka zaidi ya aliyonayo, mtajeni mmoja tu!
- Kwamba ni Raifiki wa Rostam, unless kama hutumiii cell phone za bongo, wewe sio rafiki wa Rostam, ila kama unatumia any of them basi wewe automatically unashirikana na Rostam vile vile, ni hoja haina mshiko kwamba anaigawa CDM then huko CDM mtakuwa wanafiki wa Dunia, jinsi mnavyoweza kuweka smilling face to the public huku mnamchukia kama mnavyojisema hapa kwenye hii thread.
- Ninasema hivi, simjui sana Zitto on a personal level, lakini wale mnao-claim kumjua so far mnashindwa kuweka hoja nzito za kutushawishi tusimjua kwa karibu kwamba hafai kuwa Rais, mnajaribu sana kuonyesha hana royalty kwa chama, hapo ndipo mnajiharibia sana maana mnathibitisha kwamba CDM kuna unafiki Zitto is good kupiga kampeni za chama chenu Arumeru, lakini hafai kugombea urais kwa chama chenu, shame on all of you mnaomchukia bila sababu za msingi!
-Again, mimi simjui sana Zitto kwa karibu, ila nawaomba wale wote mnao-claim kumjua na kwamba hafai kuwa Rais kwa tiketi ya CDM, tupeni hoja nzito za kumchukia kwenu maana so far mnapwaya sana kwenye hoja za ku-back up chuki zenu, tunaojali Taifa kwanza tunafurihishwa na uamuzi wa Zitto kwa sababu unafungua njia kwa Vijana wote wanaotaka kugombea nafasi kubwa za taifa, otherwise tusiwe part of the problem kwa kulilia mambo ya zamani tu!
Es!
Field Marsha ES,
Bravo mkuu,Unajua tangu upotee na akina Mugongo mugongo jukwaa hili limepwaya sana .Wamebaki akina Mkandara,Mwanakijiji,na wakuu wengine wachache kutetea heshima ya JF kwa hoja.
Nashindwa kuelewa mtu anaposema fulani ana urafiki na Rostam sijui anamaanisha nini? Je,wanaofanya biashara na Rostam je? Kama una simu yenye laini ya VODA hufanyi biashara na Rostam?Mbona humfanyii Economic Embargo? Je ni Zitto pekee kwenye kambi ya upinzani mwenye urafiki na wana-CCM?
Huyo jamaa ni mbishi aliyepitiliza. Ma-radicals kama huyu hawatakiwi kupewa mamlaka makubwa sana.unaongelea maadili?huyu kama alijibizana na balozi kwenye kikao kama vile anajibizana na kimada wake mbele ya jumuiya ya watanzania atashindwa kufanya nini?kama aliweza kupotosha mdahalo chuoni na kugawa darasa profesa akagomea darasa hadi likafikia kwenye seneti ya chuo na ubalozi wa tanzania unategemea nini?kama aliweza kutembea na profesa wake unategemea awe na maadili gani aidi? kama aliweza kusababisha vurugu alipokuwa angombea chuo kikafungwa badala ya kujutia yeye akawa anawahi mahakamani kupinga amri ya chuo kumzuia kugombea unategemea nini?damu ya watu ilimwagika lakini alijifaragua tu kwenye kampeni zake kusimama dakika moja kabla ya kampeni ili kuvuta kura.Hii ndiyo aina ya akina Ghaddafi,kagame au huyu wa syria?
nilishamwambia tanzania haiko tayari kuongozwa na mujahidini au ma-ayattolaah.kama wanataka wahamie Iran kwa maradicals wenzao.waroho wakubwa wa madaraka hawa.Huu mtandao wao sasa ni mkubwa kuliko mnavyofikiria wakuu.Hili ni kundi ambalo litaleta vita kali dhidi ya wazee naona hadi vijana wa CCM akina Nape,Makamba na akina Bashe wako kundi hili.aliposimama Bashe na kuwaambia wazee ni tatizo haikuwa kwa bahati mbaya.huyu dogo Ben Saanane ana kisirani kibaya sana. ila ninachoona ni kwamba kama Zitto huko baadae atakuwa mwenyekiti wa chama chao au Rais na kwa jinsi ninavyoona anaungwa mkono na hawa vijana itakuja kutokea kama ya Zuma na Malema.
Maskini Freeman Mbowe watetezi wake wanazidiwa nguvu.kiboko ya hawa ni kutafuta wasomi nguli kuliko wao wanaojua kujenga hoja kwa umahiri ili kukabiliana nao.Nimesoma andiko la zitto nimegundua anaweza kujenga hoja na kuhamisha hata mawazo ya watu.hawa ni mabingwa wa propaganda. Saanane,ana uwezo mkubwa ni msomi aliyebobea na anajiamini isipokuwa akitumia taaluma yake vizuri na kujiamini kwake anaweza kukisaidia chama.Hizi raslimali anazoelekeza kwa kundi la Zitto zitaleta athari kwa vijana.Angesaidiana na John Heche kuisuka Bavicha naamini hali ya jumuiya hiyo ingekuwa imebadilika.Huyu dogo huwezi kumshauri hilo sana sana atakujibu kwa kukudhalilisha na watu watamuamini. Bavicha imegawanyika,makamu mwenyekiti girlfriend wa saanane yupo kundi la akina zitto.je kwa staili hii huko mbele si kuna mpasuko mkubwa?wiki mbili tu nilitabiri kama zitto atagombea uenyekiti wa chama au urais tutarajie mpasuko huko chadema kwa kuwa najua vijana alio nao kundi moja mbowe hataweza kuhimili vishindo vyao.hili ndilo linalotokea sasa
hawa wako tayari kuua ili wapate wanachotaka
Nuclear1,
Naomba ulete uthibitisho wa hayo uliyoandika.Ongeza list kabisa Willy malecela,Baraka Kange,Makongoro Nyerere,Ole Millya,Julius Mtatiro,David kafulila na wengineo! Tujadili mada iliyoko mezani achana na personal vendatta na kuchafua majina ya watu.Kwa bahati mbaya sijengi hoja au kusimamia hoja katika kufurahisha watu.Usidhani kila mtu yuko kama wewe mkuu
Remove the hatred induced politics of Tanzania and misguided priorities.Throw away your "no victor, no vanquished" mantra. It does not exist in practise. Surely, it does not exist in the minds of CHADEMA elites
The problem with most guys including you is that they are selectively hypermetropic. They see only what they want to see and blank-out others from their view. You are assertions are just inflammatory. Well you have the right to your opinion but not to your facts.
In reality you think you are doing good and giving Opposition what they want but in reality you are just hurting the Opposition camp legacy and most importantly the CHADEMA name with you silly fact fixing games.