Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Mods hebu ondoeni hizi thread, zilianza hoja za Tuntemeke baada ya kuona zimezimwa Zitto anaibuka na hoja zake zisizojali ni lini na wakati gani zinapaswa kuongelewa. Binafsi naamini Chadema ina hazina ya viongozi waadilifu tena wenye upeo mkubwa sana wanaoweza kutatua migogolo inayoletwa na wasioitakia mema CDM kila kukicha. Mtakuwa mashahidi jinsi suala la Shibuda lilivoisha kimyakimya. Alijua wangeropoka ndomana alijihami. CDM wakampuuza tena bila kumuuliza chochote. Suala la Zitto litaisha kwani CDM nawaamini kwa kumaliza matatizo bila kuleta madhara kama ilivo ccm na vyama vingine. Uamuzi wowote wa CDM lazima uungwe mkono na wafuasi na wananchi kwa ujumla kwani huwa hawakurupuki. WE ARE FEDUP WITH ZITTO. Unataka 2kuongelee ww2 muda wote? Halafu una ubinafsi na hupendi wengine ndani ya CDM wapate umaarufu zaidi yako. Kwa taarifa yako ww hata ukiondoka CDM huna madhara yeyote kwa sasa. Tuna vijana ambao wamekuzidi hata ww. Ni bora 2mpe Urais hata Tundu Lissu au Mnyika muda ukifika lakini sio ww.
 
CHADEMA imejengwa na ZITTO plus SLAA wakiwa BUNGENI walisumbua sana SERIKALI ndiyo maana leo hii CDM imekuwa kambi rasmi ya UPINZANI.Sioni sababu ya kumzuia kijana ZITTO kuingia kwenye kinyang'anyiro hicho au ndiyo UDIKTETA wa MADARAKA? You should practice what you are preaching.....
 
ZITTO anafaa sana kuliko SLAA ni kijana, anafanya maamuzi bila kukurupuka. Ni mfumo gani huo wa nchi ambao SLAA anaweza kbadilisha ambao ZITTO hawezi? Nchi yetu ni ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, nchi inayofuata utawala wa Sheria, nchi yetu inaheshimu haki za binadamu na mawazo ya kila mtu bila kujali rangi, kabila, wala dini. SLAA anataka kuja na nini? Tuwepuke hao wanaokuja na hoja za mifumo mipya yasije yakatokea yale ya LIBYA, MISRI, TUNISIA na kwingineko. NARUDIA tena ZITTO ni zaidi ya mawazo mgando ya MZEE SLAA ya siasa za majungu, visasi na uchu wa madaraka.

Zito hafai wewe umetumwa tu au mpambe wake! anapenda sifa tu hafai kabisa haaminiki na msaliti ananunulika kirahisi Dr.anafaa kwa sana
 
Kwa ushauri wa bure epuka sana hizi siasa zenye mlengo wa kugawa watu.Nadhani kwa nilivyofuatilia mjadala huu na hao wanaokutuhumu kuwa wewe unashirikiana na Zitto katika hiyo mipango yenu mnaoijua wenyewe soon itafumuka na mtaabika vibaya sana.Hawa wanaojadili humu na kutokumuunga mkono Zitto sio kwamba hawamkubali ama sio wafuasi/wanachama/wapenzi wa chadema,la hasha! hawa ni watu wanajadili kwa kina athari za maamuzi ya kamanda wao kimtazamo zaidi.

Napata shaka kuwa na wewe ni mmoja wa wanasiasa ambao hawataki kukosolewa.Napenda kukushauri upitie hoja za watu wote walioonyesha kumpinga Zitto kwa hili alilotamka kisha uyachambue ,kwa kuwa ni rafiki yako wa karibu sana umpe machache kama changamoto.Wanadamu tunatofautiana na kila mmoja anamapungufu yake ,suala la msingi ni kuheshimu mawazo na mitazamo ya watu kuhusu mapungufu yako.Hii inasaidia mtu kujijenga na kuimarika kimtazamo,hata katika kuchangia na kutetea hoja.

Mimi ni mmoja kati ya watu wanapinga kauli hii ya Zitto ya sasa ,lakini si kwamba napingana na mitazamo/hoja zake zenye malengo ya kutuondoa katika dimbwi la umasikini -kwa kutuonyesha njia na mwelekeo thabiti wa kimapinduzi.

quote_icon.png
By Matola Pili Ben Saanane nimekuwa nikifuatilia mabandiko yako kwa makini sana na kuna kipindi nilidhani huwa unaonewa, kumbe nilikuwa najidanganya, humu jamvini umejipambanuwa kwamba wewe ndio unayejuwa siasa na yeyote ambaye atakuwa kinyume na mtazamo wako basi wewe utambatiza kila aina ya jina mara mnafki mara hivi mara vile, kumbe sasa nimejiridhisha ni kweli chama chako kiliposema huna maadili hakuna walipokuwa wamekosea, kwa nini unatetea Alliance ndani ya chama? narudia kukwambia tena jifunze kwa John Mnyika, yule kijana anaaminika machoni pa watu kwa sababu he is humbled,......jiulize ni kwa nini kijana mmoja Mnyika alundikiwe vyeo na nyinyi wasomi mpo? endelea na Alliance. zako.
Mwakalinga na Matola, nafikiri sasa mmeanza kuelewa kitu ambacho wengine tulikiona tangu zamani. Kadri muda unavyokwenda ndivyo mambo yanavyozidi kuwa wazi zaidi.
 
CHADEMA imejengwa na ZITTO plus SLAA wakiwa BUNGENI walisumbua sana SERIKALI ndiyo maana leo hii CDM imekuwa kambi rasmi ya UPINZANI.Sioni sababu ya kumzuia kijana ZITTO kuingia kwenye kinyang'anyiro hicho au ndiyo UDIKTETA wa MADARAKA? You should practice what you are preaching.....

Nani kamkataza Zitto kuwania nafasi hiyo???
Zitto amelalamika kuwa kakatazwa kuwania nafasi iyo???
Unaongelea kauli za viongozi wa chama au maandiko ya kwenye mitandao ya kijamii??
Unauhakika kuwa haumuamishii Zitto mawazo yako binafsi????
 
Urafiki wa Zitto Kabwe na Jack Nzoka Deputy Director wa Idara ya Usalama wa Taifa wewe unataka kutuaminisha ni wa kawaida? hivi si wewe chama chako ndio kilisema Usalama wa Taifa ndio waliokuwa wanachakachuwa kura za CHADEMA? je inaingia akilini wakati chama kiko vitani kwenye uchaguzi mkuu halafu Zitto Kabwe anakuwa na mawasiliano ya karibu sana na one of your party enemy? (TISS)

Zitto Kabwe ni rafiki yako na kama alitoa makala hii ili kumjibu huyo mwandishi sasa mfikishie na ujumbe huu, aje hapa atupe ufafanuzi wa yeye kuwa karibu na Usalama wa Taifa. nitamuhesabu Zitto Kabwe kama ni Double Agent until he proves otherwise without resonable dought.

Matola,

Nimekuambia nidhamu ni jambo muhimu sana.Tafadhali unapojenga hoja uwe na ushahidi.NAOMBA UTHIBITISHE kwamba chama changu CHADEMA kilisema kuwa mimi ni USALMA WA TAIFA.Njoo na facts hapa.

Hii tabia ya watu kuchafua watu kwa maslahi yao binafsi ndiyo iliyotufikisha hapa.Tukiendelea na tabia hii tutaacha kuwa na heshima ya kuwa watanzania.Mtu mzima akiandika kitu ambacho hana uthibitisho nacho tumuiteje? Nawaachhia wana JF na wenye akili timamu wachague jina.....!
Urafiki wangu na yeye ni kuhusu itikadi,dira na mwelekeo wa nchi,yeye ni kiongozi wangu,ni mwanachama mwenzangu.Tuna mtizamo unaofanana,ni rafiki katika mapambano ya fikra.Siwajibiki kumweleza hayo unayonituma

kwanza,Aje hapa awape ufafanuzi?wewe na nani hasa? Hili lina tija gani?mbona suala la posho hukusimamia na ku-question mahusiano yake na TISS? alipoteuliwa kuwa waziri kivuli wa fedha mbona hauku-question kuhusu uhusiano wake na TISS? Alipoteuliwa kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni mbona huku-question Uhusiano wake na TISS? anapotoa hoja ya mkonge bungeni na katika utekelezaji wake wa kazi katika kamati ya hesabu za serikali na mashirika ya umma mbona hujawahi question uhusiono wake na TISS?

Hoja ya ujana inatesa sana watu.Tuwe fair otherwise nafurahi sana Comrade Thabo Mbeki akiwa Nairobi last week alitoa kauli nzito na inayotakiwa kufanyiwa kazi.Alisema

"The youth of the African continent should prepare themselves for a rebellion against their older generation and claim their leadership role"

"To ensure that [the youth] actually exercises the leadership everybody rhetorically accepts and proclaims is its due, the youth must organise and ready itself to rebel, so to speak."
 
Mwakalinga na Matola, nafikiri sasa mmeanza kuelewa kitu ambacho wengine tulikiona tangu zamani. Kadri muda unavyokwenda ndivyo mambo yanavyozidi kuwa wazi zaidi.
Hata kama nilikuwa sijui kusoma sasa nimeletewa picha ili nione.......Kuna mahala nimewaomba wenye notebook na wandike maneno haya, halitokuwa jambo la kushangaza ukisikia Zitto Kabwe ameangushwa Ubunge na mgombea wa CCM uchaguzi wa 2015, inashangaza sana mtu ambaye hata Ubunge wa jimboni kwake ameshinda kwa mbinde kwa simple majority anakuja na ndoto za Urais in wrong timing!! interesting.
 
...haya mambo ya kila mtu kujiona kwamba anaweza kuwa raisi yamesabisha huyo baba mwanaasha.JK amefanya madudu kibao na watanzania tumeshindwa kumshikisha adabu kwahiyo kila mtu sasa anaona kumbe ata mimi naweza kuwaa raisi coz hata nkabolongo sitafanywa kitu!...
 
CHADEMA imejengwa na ZITTO plus SLAA wakiwa BUNGENI walisumbua sana SERIKALI ndiyo maana leo hii CDM imekuwa kambi rasmi ya UPINZANI.Sioni sababu ya kumzuia kijana ZITTO kuingia kwenye kinyang'anyiro hicho au ndiyo UDIKTETA wa MADARAKA? You should practice what you are preaching.....
images
 

Nani kamkataza Zitto kuwania nafasi hiyo???
Zitto amelalamika kuwa kakatazwa kuwania nafasi iyo???
Unaongelea kauli za viongozi wa chama au maandiko ya kwenye mitandao ya kijamii??
Unauhakika kuwa haumuamishii Zitto mawazo yako binafsi????

Dr.SLAA kachanganyikiwa coz anaomba dua baya kwa ZITTO atimuliwe haraka sana...subiri wapoteze Arumeru ili wamjeruhi ZITTO kama walivyofanya CUF na NCCR.
 
Matola,

Nimekuambia nidhamu ni jambo muhimu sana.Tafadhali unapojenga hoja uwe na ushahidi.NAOMBA UTHIBITISHE kwamba chama changu CHADEMA kilisema kuwa mimi ni USALMA WA TAIFA.Njoo na facts hapa.

Hii tabia ya watu kuchafua watu kwa maslahi yao binafsi ndiyo iliyotufikisha hapa.Tukiendelea na tabia hii tutaacha kuwa na heshima ya kuwa watanzania.Mtu mzima akiandika kitu ambacho hana uthibitisho nacho tumuiteje? Nawaachhia wana JF na wenye akili timamu wachague jina.....!
Urafiki wangu na yeye ni kuhusu itikadi,dira na mwelekeo wa nchi,yeye ni kiongozi wangu,ni mwanachama mwenzangu.Tuna mtizamo unaofanana,ni rafiki katika mapambano ya fikra.Siwajibiki kumweleza hayo unayonituma

kwanza,Aje hapa awape ufafanuzi?wewe na nani hasa? Hili lina tija gani?mbona suala la posho hukusimamia na ku-question mahusiano yake na TISS? alipoteuliwa kuwa waziri kivuli wa fedha mbona hauku-question kuhusu uhusiano wake na TISS? Alipoteuliwa kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni mbona huku-question Uhusiano wake na TISS? anapotoa hoja ya mkonge bungeni na katika utekelezaji wake wa kazi katika kamati ya hesabu za serikali na mashirika ya umma mbona hujawahi question uhusiono wake na TISS?

Hoja ya ujana inatesa sana watu.Tuwe fair otherwise nafurahi sana Comrade Thabo Mbeki akiwa Nairobi last week alitoa kauli nzito na inayotakiwa kufanyiwa kazi.Alisema

"The youth of the African continent should prepare themselves for a rebellion against their older generation and claim their leadership role"

"To ensure that [the youth] actually exercises the leadership everybody rhetorically accepts and proclaims is its due, the youth must organise and ready itself to rebel, so to speak."

Traitors Statement, hapa kwa wataalamu wa saikolojia hawapati shida kugunduwa kwamba Zitto hana uwezo na wala wapambe wake ukiwemo wewe Ben wa kuweza kujisafisha kwa tuhuma hii nzito ndio maana nilitahadharisha sihitaji jibu jepesi katika maswali magumu.
Mimi ni kijana kama wewe na Zitto lakini kwangu mimi umri kwangu si kigenzo katika uongozi wa nchi maana hatutafuti mashindano ya marijali.
Dhambi ya usaliti na tamaa ya madaraka haitawaacha salama note my word.
 
=BARRICK walikuwa wanamlipa $25000 kila mwez for 6 months in2009.
=Kwa kuitetea DOWANS alilipwa 80mil (TSH)
=Kuhusu post ya Mkumbo alikuwa sahihi kwa sababu hata yeye KITILA pale cdm yuko kwa ZITTO na anamfahamu vizuri ZITTO kwani ni KITILA aliyemleta Zito UDSM akitokea ZANZBAR UNIVERSITY wakati ule KITILA alikuwa RAIS wa DARUSO

hiii ingesimama Kama uzi unaojitegemea jamani
 
Dr.SLAA kachanganyikiwa coz anaomba dua baya kwa ZITTO atimuliwe haraka sana...subiri wapoteze Arumeru ili wamjeruhi ZITTO kama walivyofanya CUF na NCCR.

Kuomba dua hivi kunafanyika hadharani? au mwenzetu umejuaje? Badiriki ndugu yangu hata mimi nina maslahi binafsi na system iliyopo madarakani kwasasa lakini siwataki kabisa waendelee kuongoza nchi hii.
 
kinachonishangaza sijawahi kusikia popote Dr. Slaa kuwahi kutangaza kuwa rais wa nchi hii, yeye aliombwa agombee nafasi hiyo, mara nyingi viongozi wanaoombwa na wanachi kuwaongoza ni viongozi waadilifu pasi nashaka kuwa hatumiwi wala hakutumwa na kundi fulani,
 
Dr.SLAA kachanganyikiwa coz anaomba dua baya kwa ZITTO atimuliwe haraka sana...subiri wapoteze Arumeru ili wamjeruhi ZITTO kama walivyofanya CUF na NCCR.

Bado hujajibu swali nililokuuuliza.
Tabia ya kuhepa hoja mmeambukizwa na Mkapa.
Jibu hayo maswali kama mleta thread.

 
Waberoya unakumbuka umewahi kuandika nini kuhusu Zitto humu JF?

Hakuna kitu kibaya kama unafiki! Zitto ni mnafiki kama wewe!

Unakumbuka aliwahaidi nini wakazi wa kigoma? Eti 2015 hagombei ubunge bali Urais! Tena wakati huo Dr Slaa akigombea Urais! Huyu si ana matatizo ya akili!

Zitto kuingia Chadema akiwa na miaka 16 sio issue, Zitto kushiriki kuijenga Chadema ya leo sio issue pia kama hawezi kusimama kiitikadi na Chama; aliyewahi kuwa mwenyekiti wa CDM na mbunge wa kwanza wa upinzani Tanzania Bwana Aman K. Amerudi CCM! Sembuse Zitto!

Eti haki yake msingi! Hiyo haki hata Matonya anayo Waberoya!


ukiwa mkweli wa nafsi yako ndiyo unafiki?? au kuchukia ,wivu na kupinga chochcote ndiyo siyo unafiki??
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom